Soldier alizindukana
kutoka kwenye usingizi baada ya kusikia kilio, kilikuwa kilia cha mtoto, kwa
haraka akainuka kitandani, na pembeni yake akamuona mtoto kalazwa karibu yake,
akajua huyo ni mkewe kafanya hivyo, akamsogelea mtoto na kumweka vyema, alikuwa
kajisaidia kwa hiyo alihitajika kubadlishwa nepi…, akawa anataka kumbadili
lakini nguo za kumbadili zilikuwa hazipo, akataka kumuita mkewe kwa sauti,
lakini akaona amchukue mtoto atoke naye nje.
Akambeba vyema huku
anamkagua,..anamuangalia usoni,… mtoto alikuwa kanyamaza kimia,..alikuwa mtoto
mnzuri mwenye afya tele tu.., na kila akimuangalia usoni, anaiona sura ya
dereva,…na …ndio yawezekana kuwa anafanana na baba yake, hapana…ndio…akawa
anajiuliza huku anatembea na kila akijiuliza anahisii mwili unamchemka…damu
insisimuka, hasira…, kwa haraka akafungua mlango kutoka nje ya chumba cha
kulala, na mara akamuona mtu kasimama mlangoni, alikuwa ni yule binti Yaya,
akiwa amesimama, hapo malngoni kama anasubiria…
‘Oh, kumbe upo hapa,
mtoto analia na mama yake hayupo, kaenda wapi,..?’ akauliza na yule Yaya,
akaonyeshea kwa kidole, kuelekea jikoni.
‘Kwani wewe huwezi
kuongea?’ akamuliza huyo binti, kwa mshangao, na huyo binti hakusema kitu akawa
anataka kumchukua mtoto, huku kainamisha kichwa chini, na Soldier akamkabidhi
huyo yaya mtoto na huyo yaya kwa haraka akaondoka, na muda wote alikuwa
anatizama chini.
‘Huyu binti vipi,
sijui hawezi kuongea na ana aibu kupitiliza,…’ akasema sasa akitembea kuelekea
mlango wa kutokea nje, alitaka akapate upepo wa nje kidogo na ikibidi achukue
na mazoezi, …alipofika nje, akaona gari likiingia hapo eneo la nyumba…, alikuwa
ni yule dereva.
Moyoni akasema, sasa
nitaongea na huyu jamaa nipate ukweli fulani,…akawa analisogelea gari na kwa
muda huo dereva naye alikuwa akifungua mlango wa gari na kutoka nje..
‘Za asubuhi mkuu,
naona kidogo umelala, hivi huko kweli mlikuwa mnapata muda wa kulala..?’
akauliza
‘Kuna muda unapata ,
kuna muda unalala kwa kimang’amu ng’amu..ndio hivyo..vipi umefika asubuhi hii
kuna abiria hapa anatoka..?’ akauliza
‘Aaah,…nimeitikia wito
wa baba yako, alinipigia simu kuwa leo niwepo hapa nyumbani ana mazungumzo na
mimi….na alitaka nije na mama, lakini mama kasema hajisikii vyema….kwahiyo,
nimetii wito, nitamuwakilisha na mama, sijui kuna nini la zaidi…’akasema.
‘Ok..karibu,…lakini
bado naona kama hawajaandaa vyema huko ndani, tunaweza kuongea kidogo..?’
akasema.
‘Bila shaka,..’dereva
akasema na wakasogea kwenye benchi lililopo chini ya miti, wakakaa, na
aliyeanza kuongea alikuwa ni dereva.
‘Unajua kazi zangu
hizi ni za kuitwa itwa…sasa sijui mzee kaniitia nini, na muda huu natakiwa
kuwachukua wanafunzi fulani, si unajua tena kazi zangu hizi,…au labda anataka
kutoka, lakini alisema ana mazungumzo na mimi,…..’akasema.
‘Ok, mtaongea tu,
hamna shida, ila mimi kitu nataka kukuuliza… kidogo, hebu niambie…wewe na baba
yangu, mpoje, maana nimesikia watu wakiongea, hili na lile…. hata kwenye
kikao..nilisiki amzeee akiligusia japokuwa hakuweza kusema ukweli…, kuna ukweli
wowote kuwa labda wewe na mimi ni ndugu moja..?’ akauliza.
‘Mhh…mtu wa kukujibu
hilo ni baba yako,..ila labda, nikuambie jambo,…hivi hujawahi kuona watu
wanafanana lakini hawana hata damu ya udugu…?’akauliza.
‘Wapo, lakini usikwepe
ukweli, kama upo ukweli huo..na mimi nastahiki kufahamu au sio, kuna leo na
kesho, baba yupo ..na…unajua tena…sasa kama upo niambie tu, hakuna shida, au
sio..?’ akauliza.
‘Sijui lolote
kwakweli,..na ….unajua nikuambie kitu, kuna mengi yanasemwa,..hata kuhusu mtoto
wako, …wengine wanasem nafanana na yeye, haya …hilo la mimi kufanana na baba
yako ndio limeenea sana, lakini ….mimi siwezi kusema lolote kuhus hilo, ili
hali msemajei yupo…. muulize baba yako…’akasema.
‘Kwanini wewe hutaki
kuniambia ukweli?’ akauliza.
‘Kwasababu baba yako
…na hata mama yako wamesema hivyo…’akasema.
‘Kuwa usiniambie
ukweli..kwanini?’ akauliza akimuangalia dereva na dereva akawa anatabasamu tu,
halafu akasema;
‘Sikiliza Soldier,
…kwani kwa mfano…mimi nikiwa,… nasemea kwa mfano tu maana …atakuambia baba yako
yote, kwa mfano,…, mimi nikiwa ni ndugu yako kuna ubaya..?’ akauliza.
‘Swali langu
hujalijibu,..je wewe ni ndugu yangu, kama watu wanavyosema au la…?’ akauliza,
sasa kwa ukali, na kabla dereva hajasema kitu, mara sauti ya kuitwa ndani
ikasikika,..
‘Mnaitwa ndani, mzee
anawasubiria…’ilikuwa suti ya ndugu yao na mazungumzo yakakatizwa..
‘Ngoja niwahi maana
hapa nitachelewa..’dereva akasimama na kuanza kuondoka kwa haraka, na Soldier
akamfuatia kwa kwa nyuma akiongea…
‘Nitaongea na wewe
baadae, kwani sio swali hilo tu, nina maswali mengine muhimu dhidi yako…,
nataka unijibu wewe kwa kinywa chako, maana nafahamu unaufahamu ukweli
ulivyo,…nitamuuliza baba, lakini kauli yako itanifanya niwe na amani zaidi, na
umesema wewe mwenyewe kwa kauli yako, kuwa unafanana na mtoto, iweje ufanane na
mtoto wangu..., sasa nataka ukweli kutoka kwako, la sivyo…sitaogopa kunyongwa
unielewe, sitanii…?’akasema Soldiera wakitembea kwenda ndani.
‘Usijali…hilo…hahaha,
ina maana na wewe unaamini hayo,…acha hizo bro,….ngoja, naona mzee huyo,
......’akasema na mara baba wa Soldier akatokea na kumuita Dereva waongee
pembeni, na Soldier yeye akaingia ndani.
********
Chumba
cha maongezi kilikuwa kimeshachangamka,…Soldier alipitisha macho kwa haraka,
…yupo mama, anakunywa chai akiwa kimia, yupo mke wake, anacheza na mtoto wapo
ndugu zake wengine wa familia,..na alikuwepo mzee mwingine, ambaye ni
mwanafamilia pia, na ….yupo mgeni , anamfahamu ni docta. Baba alikuwa bado nje
akiongea na dereva.
Soldier,
alisalimiana na wengine akamsogelea mama yake wakasalimiana na akamuuliza vipi
khli yake, mama yake akamuambia leo hajambo, hana shida..na akasogea kwenye
kiti na kukaa, alikaa karibu na docta, akawa anaongea naye;
‘Ulikuja
kwa ajili ya mama..?’ akamuuliza
‘Hapana
mzee wako aliniita tu,..kasema kuna jambo anataka nimsaidie... na kwa vile
nimefika hapa, nikasikia mama yako anaumwa, kwahiyo nikajaribu kumsikiliza ili
nijue tatizo nini hasa,….na..mama haumwi kihivyo..ila mawazo,..unajua mawazo
yanaweza kukufanya ukawa mgonjwa, nimemwambia ajaribu kulikwepa hilo, kwani
athari zake zinaweza kuwa kubwa zaidi..’akasema.
‘Docta
nikuambie ukweli, mimi sijui kabisa kinacheondelea hapa nyumbani.., lakini kwa
vile nimefika…, nina imani tutayamaliza tu, ..na…’kabla hajaendelea baba yake
akaingia…dereva hakuonekana, na Soldier akawa na wasiwasi kuwa huyo jamaa
anaweza kuondoka. Akataka kusimama ili akamzuie lakini baba yake akaanza
kuongea…
‘Jamani
tuna maongezi kidogo..tulia bwana mdogo unataka kwenda wapi…..’akasema akimnyoshea
mkono Soldier.
‘Mimi
nimeona…, ni muhimu sana tuyaongee haya kama familia,..mtaona kuna watu wengine
wasio kuwa wanafamilia kwa ukaribu wake…, lakini wana udugu fulani …mnamuona
docta hapo, huyo ni mtoto wa wajomba, anatokea familia ya mke wangu, kwahiyo ni
ndugu kwa namna fulani, ila yeye nimemuita hapa kwa jambo moja muhimu
sana…’akatulia.
‘Kuna
tatizo lipo hapa nyumbani,…lilikuwa tatizo dogo tu, la mimi na ..mke wangu,
lakini sasa naona limekwenda mbali, eeh, ni sawa, lakini kwanini iwe hivyo,..’akatulia
akiinama kidogo.
‘Sitaki
kumlaumu mtu,..na ..sio kwamba nashitaki, mimi siwezi kushitakia jambo kama
hili kwa watoto,..ila nataka niweke wazi, atakayeumia aumie..., mimi ni askari
nimepambana na matatizo makubwa sana tu,…ila mimi ni mtu mnzima na ufahamu
wangu na umri wangu unanifanya nijishushe,..na najua nifanye nini ili kuyaweka
haya mambo sawa kwa wakati muafaka!’
‘Mama
yako Soldier, sasa hivi anaumwa, hajijui tu,..na tatizo lake kubwa
kutokuniamni…sijui kwanini haniamini na umri huu…mimi sio kijana tena, haya
anasema nilikuw amsiri amekuja kugundua mwenyewe madhambi niliyoyafanya huko
nyuma,…lakini madhambi gani..hana ushahidi, anahisi tu,…sasa mimi sitaki haya
mambo yazidi kukua, maana mwisho wa siku nitakuja kulaumiwa mimi….nataka
niliweke hili wazo mbele yenu wote...’akatulia
‘Soldier,
wewe ni mtoto wa kiume, mambo kama haya yapo na yaweza kutokea kwenye familia
yako, nataka ujue kuwa,…mwanaume sio kuvaa suruwali tu,mwanaume ni kupambana na
mambo kama haya,..najua wewe umeiva na sina shaka na wewe..ila ulivyofika
kutoka huko …naona ulitaka kuingia kichwa kichwa,..tulia...bwana mdogo,
nilkuambia mapema kila kitu nitakiweka sawa, huniamini mimi baba yako..?’ akawa
anauliza ,na alipoona mwanae anataka kuongea.
‘Baba
sijasema sikuamini…ila....’akajitetea.
‘Ninajua
ni kwanini…mama ni mama tu,..kila mtoto atamuonea mama yake huruma…si unajua
tena, hapo baba anaonekana hana maana,..lakini mnashindwa kufahamu dhima ya
baba, baba wa kweli ni yule anayeangalia mambo, bila kujali maneno ya
watu,..muhimu kwake ni kuhakikisha haki inatendeka, msimamo wa familia yake
unakuwa hauyumbi, ushirikiane wake na majirani pia nao una umuhimu wake,
ubinadamu nk...sasa niwaambie ukweli, maana mimi siwezi kudekeza mtu hata siku
moja hiyo ndio silka yangu…’akakunja uso.
Kuna
tatizo lilianza zamani kidogo,…kabla baba yake dereva hajafariki, baba yake
dereva alikuwa rafiki yangu mkubwa sana…na urafiki wetu ulifikia mbali,
kusaidiana kifamilia…ilikuwa mimi nikisafiri au yeye, mmoja anachukua jukumu la
kulea familia ya mwenzake..kweli si kweli..?’ akauliza akimgeukia mkewe.
‘Ongea
tatizo…’akasema mkewe
‘Ndio
nalifichua hivyo,..lazima wanafamalia wafahamu chanzo ni nini, choko choko, ya
kutoakuaminiana imetokea wapi…
'Sawa
ongea na mimi uje unipe nafasi hiyo nieleze ni kwanini sikuamini...'akasema
mkewe.
'Sijamaliza
lakini kuongea, na wala sijakupa nafasi ya kuongea...'akasema baba
'Samahani
endelea..'akasema mkewe
'Mambo
yalianza kuharibika pale rafiki yangu alipofarikia,…hebu niwaulize kwa hali
kama hiyo mimi kama rafiki yake marehemu ningefanya nini…nimuache yule mjane
ateseke tu, hebu fikrieni hata ingelitokea jwangu angemuacha mke wangu ateseke
tu, asiwe karibu naye, sis tulishakuwa ndugu, wa shida na raha...kwahiyo
ilikuwa ni wajibu wangu kumsaidia yule mama, kwa kumliwaza, kumfanya ajione
bado yupo na sisi, sasa mwenzangu hilo halitaki, kwanini nakuwa karibu sana na
mke wa marehemu, kwanini..ikazaa menginena kusahau ukweli halisi,…’ akasema
‘Hujasema
tatizo bado hapo, …’akasema mkewe.
‘Tatizo
kwako eti ni kwa vile dereva anafanana na mimi, au sio, na kwa vile mimi
nilikuwa karibu na mke wa marehemu kwahiyo huenda nilitembea naye au sio,
kwahiyo kuzaliwa mtoto anayefanana na mimi ndio ushahidi wako kuwa mimi nina
madhambi, ni msaliti wa ndoa yangu, au sio..ushahidi wako ni huyo mtoto, au
sio....?' akauliza
'Elezea
bayana, usizunguke ...maana utapoteza muda na ukweli...'akasema mama
'Si
ndio hivyo naelezea,..kuwa ni kwanini nimekuwa karibu na mke wa marehemu,.na
unakumbuka kabisa mimi na marehemu tulikuwa tunafanana sana,...kama
mapacha..sasa kuzaa mtoto anayefanana na mimi sio ajabu…’akasema.
‘Kwahiyo
unapinga kuwa dereva sio mtoto wako uliyezaa na huyo mjane...unaikataa damu
yako, mimi nilishakuambia ukubali ukweli, na umtambulishe huyo mtoto kwa
familia kuwa huyu ni damu yako, basi...lakini hutaki, ...kwanini, ...?'
akauliza mkewe
'Huko
tutafika...usiwe na shaka...'akasema mkewe
'Nijibu
kwanza hilo swali langu je dereva sio mwanao wa nje ya ndoa...?' akauliza mkewe
'Kwanini
unishuku hivyo, ..huniamini mimi, haya hata kama huniamini mimi je humuamini
mke wa marehemu...mke wa marehemu alikuambia nini...?' akauliza baba,
'Ndio
sikuamini,..kama sikuamini wewe, hata yeye nitamuaminije,...wakati nina
ushahidi kamili kuwa hauaminiki ukiwa na yeye, lenu ni moja...'akasema mama.
'Kwa
vipi?' akauliza baba
'Kwasbabu
niliwahi kuwafumania ..wewe na mjane, au unataka niongee kila kitu mbele
ya watoto…?’ akauliza mkewe, na Soldier aliposikia hivyo akatoa macho
kumuangalia baba yae, akauliza
‘Ni
kweli baba kuwa uliwahi kufumania na mke wa marehemu…?’ akauliza Soldier, na
baba yake akaashiria kwa mkono kumwambia mwanae atulie..
NB:
Tutaendelea…
WAZO
LA LEO: Uongozi mnzuri huanzia ndani ya familia yako. Kama ilivyo jamii,
jamii nzuri huanzia ndani ya familia, jinsi familia zitakavyojengwa na kulelewa
vyema ndivyo jamii itakavyoweza kuwa na masikilizano mema na maendeleo mazuri.
Ndio maana ni muhimu sana kuangalia familia kwanza ili kuweza kuwa na jamii
njema , na familia njema huanzia kwa baba na mama, kama wana ndoa hawa
hawatakuwa wema, wenye maadili mema,..muelekeo wake ni kujenga familia mbovu
ambayo itaunda jamii mbovu na hata uongozi wake utakuwa mbovu…ni hayo kwa
leo.Ni mimi: emu-three
No comments :
Post a Comment