'Wakati polisi wanakuja nikuulize swali wewe mdada;...'akasema Soldier
‘Uliza tu…’akasema huyo mdada aliyekuwa kajifunika usoni, kwa sauti ya kinyonge…
‘Ina maana kweli kwa muda wote huo ulikuwa ukiwauguza wagonjwa mbali mbali akiwemo huyo mtu...ina maana kweli hukuwahi kumuona huyo mtu usoni, ukaifahamu sura yake…?’akaulizwa
‘Hutaamini, wanaume wote humo walikuwa wamefunikuwa uso na
walikuwa na sehemu yao tofauti na sehemu ya wanawake, na hakuna ruhusa wanawake
au wanaume kufika sehemu za wengine..kuna ulinzi mkali sana, wanawake kazi yao
kubwa kupika, kufua,..na kazi za kutafuta kuni.
Mimi nilikuwa nakwenda sehemu waliyoitenga kama hospitali,
na huko pia wagonjwa wanaume wamefunika usoni……'akasema
'Haiwezekani, ndio hapo naona hadithi yako ni y akutunga tu...'akasema Soldier
'Haiwezekani,...hata kidogo tu...kumuona, au hakuna aliyewahi kuumua usoni,...'akasema Soldier.
'Kiukweli wapo, na huyo mtu niliwahi kumuona
sura kidogo tu…..’akasema
‘Kama ulimuona kidogo tu, ni nani sasa kati ya hawa wawili, ni Soldier au Dereva…?’akaulizwa,
na kabla hajasema kitu polisi wakafika.
Tuendelee na kisa chetu.....
*****************
Kabla hajasema kitu
polisi wakaingia, na walijua ni nani wanayemtafuta, kwani walipoingia tu
mmojawapo akamsogelea shemeji wa Soldier, na kumwambia;
‘Upo chini ya ulinzi….’aliongeza maneno mengine na shemeji
bila wasiwasi akanyosha mikono na kuweka pingu, halafy akasogea aliposimama
dada yake na kumnong’oneza kitu, halafu akatembea kama kutangulia kutoka nje,
na kama vile kasahau kitu akamgeukia Soldier na kusema;
‘Umeharibu,…na utajuata kwa hili…amini usiamini, umeharibu
ndoa yako, na hata kama itakuwepo, lakini kwangu mimi sikutambui kama shemeji
yangu..wewe ni aadui yangu..amini hivyo…’akasema na bila kujali akaanza
kutembea kutoka nje, lakini polisi mmoja akamzuia, asitoke kwanza.
‘Jamani ni vyema kuwafahamisha hili, kwasabababu huenda
tukitoka hapa kunaweza kuwa na maneno mengi,…’kabla hajamaliza dada mtu
akauliza;
‘Tunataka kujua kwanini mumemkamata ndugu yangu kwa kosa
gani…?’ akauliza na polisi akamgeukia jamaa na kumuuliza
‘Unakubali tuyataje makosa yako…?’ akaulizwa
‘Makosa gani, sina makosa yoyote, mnahisia tu…’akasema
kijeuri.
‘Huyu jamaa anajishughulisha na biashara haramu, anajishughulisha
kama wakala wa kuwauzia waasi silaha, waasi ambao wanasumbana na serikali ya
majirani zetu…huyu jamaa pia anajishughuliza na kuuza madawa ya kulevya,
bangi…na madawa yanayotumiwa na waasi kutezea watu…pamoja na hayo ana biashara
zake, huko,…magari na hajalipa kodi…’akasema huyo askari.
‘Mna ushahidi gani kwa hayo..?’ akauliza dada
‘Ndio maana tumekuja kumshika, na akifika huko kituon
atahojiwa kwa mujibu wa sheria, na haki zake zote zitalindwa…’akasema huyo
askari
Na wakati huo wale waliovalia kijeshi wakawa wanaongea jambo
na Soldier, waliongea kwa muda, ikawa wao ndio wanasubiria, na baadaye Soldier
akageukia akamuangalia mdada, yule aliyejifunika uso…
‘Samahani dada yetu, ..kuna mambo tunatakiwa twende pamoja
tukayathibitishe huko kituoni, kwa usalama hatuwezi kuyaongea hapa hadharani,…’akasema
na Yaya akadakia na kusema;
‘Dada yangu hawezi kwenda huko ana mtoto mdogo…’akasema
‘Lakini mtoto mdogo huyo aliweza kukaa na wewe na mke wangu
kwa muda bila ya yeye kuwepo, na hatuendi kushinda huko tutarudi naye…’akasema
Soldier.
‘Kila la heri mwanangu tupo pamoja…’akasema baba mtu akiwa
kitandani na haoo… wakaondoka, na wakati wanatoka nje, mke wa Soldier akawa
anawafuatilia kwa nyuma huku machozi yakimtoka, na alipofika huko nje, akasema
kwa sauti;
‘Unamfunga kaka yangu eeh, …kwa kosa la kusingiziwa,
umeharibu kila kitu,..mimi na wewe basi tena, naondoka zangu, kwanza
ulishavunja miiko ya ndoa, halafu sasa unazidi kuiharibu familia yangu,
sitakusamehe kamwe…’akasema na kurudi ndani kwa hasira.
******************
Kutokana na tukio hilo zikapita siku mbili,
mke wa Soldier akawa kaondoka na mtoto na wale wageni wawili, na dereva bado
alikuwa akisumbuana na polisi, lakini kesi yake haikuwa na nguvu sana, baadaye
kulipotulia, baba, akaitisha kikao cha wanafamilia, mke wa Soldier na wageni
wake wakaitwa waje,…na kweli walifika, na walifika na ndugu yao mmoja, ni baba
mkubwa wa mke wa Soldier.
Koramu ikatimia, baba
na mama, Soldier na mkewe, ingawaje walikuwa hawana mawasiliano kila mtu kakaa
kivyake,alikuwepo mdada na mdogo wake, pia mama wa dereva, na dereva mwenyewe,
na wazee wawili ndugu zake baba yake Soldier….na yule dakitari upande wa mke wa
Soldier naye alialikwa, haikujulikana safari ameitwa kwa jambo gani.
‘Jamani mimi sio mkaaji sana, nimeshukuru kuwa pamoja na
hayo sisi bado ni ndugu moja, mumeoa kwetu , na pamoja na tatizo hili bado
tunatambua kuwa ndoa ipo sijui wenyewe watatuambia nini….’akasema huyo mgeni
baba mkubwa.
‘Ama kwa jamaa yetu huyo aliyekamatwa, kwa kushukiwa na
makosa mbali mbali, tumeshafanikiwa kumuwekea dhamana, na ana wakili wake
mnzuri, kwahiyo tuna imani kesi hiyo itakwisha , maana mambo ya vita huko
yamekwisha na kuna maridhiano fulani yanaendelea.
Najua kwa namna fulani jamaa yetu, huyo ana makosa yake,
lakini kama alivyosema ni katika kutafuta biashara, na alijiunga na wenzake kufanya
biashara ya silaha kama biashara nyingine hakujua kuwa hao ni waasi na kufanya
hivyo ni makosa, kwahiyo yeye akachukuliwa kama kusaidia polisi,…unajua tena,
wakili kasema kesi hiyo haina nguvu, ataona jinsi gani ya kulisaidia hilo…’akasema
‘Lakini sio kwa njia hiyo aliyotumia yeye, nakubali alikuwa
mfanyabishara lakini biashara nyingine hazikubaliki, sasa sijui kama wakili
ataweza kulitetea hilo, tunaombea iwe hivyo na ajirudi, na aache tabia yake ya
visasi…’akasema Soldier
‘Hilo tunalijua sana,..niliwahi kumkanya sana mtoto wangu
huyo kipindi cha nyuma mpaka tukakosana naye, unajua alivyokuwa m-mbishi,
lakini sasa kajifunza, aliyoyapata huko, anakiri kuwa hatarudia tena, ila
katuma ujumbe kwako kuwa, hamjamalizana yeye na wewe, mimi sijui ana maana gani..
‘Aaah, huyo nimeshamzoea, najua ipo siku tutakaa pamoja tu,
maana hakuna lenye mwanzo na lisikose mwisho wake,…mimi sina kinyongo naye, na
akiwa tayari tusameheane mimi sina tatizo, na kwanini niwe na kinyongo naye,
sioni umhimu wake…’akasema
‘Na kwa hili baba mkwe, naombeni sana, tuayamalize haya
tugange yajayo..kuna mambo mengi yametokea, na sisi ni wanadamu kukosea kupo
tu, lakini mbora wa wote ni yule anayekubali kukaa, na kuongea na kutafuta
suluhu watu wakasamehena…naomba sana, mke wangu alikubali hili, na tuyamalize
haya kwa amani,…’akasema Soldier.
‘Nimefurahi kusikia hivyo…na ndicho kilichonileta mimi,
kuona jinsi gani mtarekebisha matatizo ya ndoa yenu, …nimemuhoji mke wako,…naona
bado ana duku duku, kwanza anasema kwa nini unamficha ukweli, na hata baada ya
kujulikana ukweli bado hutaki kukiri kosa,…hasa kuhusu huyo mtoto…na pili
kuhusu kaka yake…hilo la kaka yake halina nguvu tena..ila hilo la mtoto…’akasema
huyo baba.
‘Mzee, sioni kwanini turudie huko nyuma, nafikiri yeye
ameweza kukaa na dada hapo, na kama ingelikuwa ni uwongo, angeshaambiwa, ..mimi
simjui huyo mdada, zaidi ya kukutana naye hapa, na kama tulikutana naye huko,
sikuwa n aufahamu huo…nafikiri docta anaweza kuliongelea hili kitaalamu kama ni
lazima…’akasema.
‘Haina haja…nimeshaongea na dada, na nimeelewa, lakini kama
alivyosema baba, mimi ninachotaka ni wewe kukiri kosa, na kumkubali huyo mtoto
kuwa ni wa kwako, basi…’akasema mkewe.
‘Mimi sina kipingamizi cha kukiri kosa, ila nasema hayo
yalifanyika nikiwa sina uwezo wa kutambua, na mpaka sasa sikumbuki,…kama ni
mtoto wangu hewala, namkubali, lakini bado tunahitajia uhakika wa kisayansi,…na
ndio maana mimi nikakubali damu yangu na mtoto vikapimwe, na leo yupo yule
docta ndugu yenu, atuthibitishie hilo..na mlienda wote hospitali, mimi
sikuwepo,..sijui mumekuja na majibu gani…’akasema Soldier.
*************
‘Niweni radhi kwa kikao chenu cha kwanza, najua hivi vipimo
vya sasa vya DNA, havitakuwa vya uwongo kama vile vya dereva, hivi ni halali, maana
mimi mwenyewe nimevisimamia, nia sasa ni kutengua kitendawili cha mtoto je baba
halali ni nani,…Dereva anasema yeye sio baba halali, halikadhalika, Soldier, na
hatuna jinsi nyingine ya kulitatua hilo bila kutumia vipimo hivyo, au
sio…’akasema docta
‘Mimi namkabidhi baba wa familia hii aifungue hiyo bahasha,
hakuna anayefahamu,..hata mimi nimekabidhiwa na wataalamu wa vipimo, na
nikawaambia siangalii mpka tufike huko kwa wanafamilia wenyewe…unajue tena…’akasema
docta.
‘Ila mzee kabla hujaifungua hiyo bahasha, ningelipenda
kusema neno ..unajua haya maisha yalivyo huwezi kujihakikishia kuwa unaweza
kufanya kila kitu sawa sawa,..kuna madhaifu mengi ya kibinasamu, mimi nina
yangu, dereva, na kila mtu ana yake,...na hili nataka Dereva ulielewe, mimi
kama kaka yako kama ningeliamua kufutilia kesi yako sasa hivi ungefungwa…’akasema
Soldier.
‘Kwa kosa gani…?’ akauliza Soldier akionyesha mshangao.
‘Utapeli….kugushi, kudanganya, …blackmail….hayo ni baadhi
tu, wakati huo huo umepewa dhamana ya kusaidia watu, wakimbizi, na ulikuwa
ukitoroka na kwenda nchi ya jirani, hilo ulifikiri hujulikani, na ndio maana
nilijua fika kuwa wewe unaweza kuwa baba wa huyu binti..’akasema
‘Bro, hayo tuyaache kwanza..ukweli utajielezea kwa vipimo
hivyo, mimi naviamini sana..’akasema
‘Ndio nakubali hilo, ila kama kaka yako lazima nikuonye,
sitajali kuwa wewe ni ndugu yangu, ikifikia kwenye sheria mimi nitaosha mikono
yangu, wewe uliaminika, na waajiri wako, hebu jiulize kama waajiri wako wakisikia
hivyo watakuamini tena…’akasema Soldier
‘Ok bro..nimekubali kosa.., hayo yamekwisha bro…mimi
sirudiii tena hayo makosa, nakuhakikishia hilo, sasa hivi nina furaha kubwa mke
wangu ana mimba….hahaha, raha sana, pili yale matatizo ya mama yamekwisha, sasa
mama yupo safi, tutaishi naye nitamlea na kuhakikisha hapati matatizo….’akasema
‘Sawa, tutaona hayo…muhimu tulimalize hili….’akasema soldier.
Halafu akamgeukia mdada na kusema;
‘Nilichotaka kusema ni kuwa, mdada, kwanza niombe radhi, kwa
hayo yaliyotokea nasema ukweli kutoka moyoni mwangu sikumbuki lolote kuhusu
hayo uliyosema, nakumbuka kuteswa, lakini yaliyofuata huko baadaye
sikumbuki….na sijui ilikuwaje, naomba kama hali hiyo ilikuwepo hivyo,..nisamehe
sana,…na namuomba mungu kumbukumbu hiyo isije kurejea akilini mwangu…’akasema
‘Mhh..bora iwe hivyo…’akasema huyo mdada.
‘Kiukweli sitaki nije kukumbuka hayo kama yalikuwa hivyo, …ila
hao watu walikuja kupata kipigo, na kusambaratika kabisa, na sikujua kuna watu
wa huku kwetu wanahusika,…ok, nashukuru kwa msaada wako , sijui nitakulipa
nini, kama ulivyoelezea, unanidai kwa hilo…’akasema.
‘Umlipe sasa..ikibidi mchukue awe mke wako, itakuwa bora
zaidi,…’akasema mkewe kwa sauti ya huzuni.
‘Nini…dada unazungumza nini tena…tulishaongea mimi siji
kuvunja ndoa yenu, nimekuja ili tuwekane sawa,…’akasema na Soldier naye
akasema;
‘Hapana usiseme hivyo mke wangu…ila hebu fikiria hiyo hali
na mtu alijitolea kufa kwa ajili yangu,.. mimi sijui niliponaje..kama nilikuwa
hivyo. Ndio maana wakati mwingine nahisi kama ni hadithi tu, wasingethibitisha
hili hao askari, mpaka kesho nisingelikubaliana na hilo….’akatulia
‘Wamekuambia eeh, sasa hakuna shaka tena, au sio…?’akasema
huyo mdada akiwa kambeba mtoto wake.
‘Lakini bado sijaamini..kuwa huyo ni mtoto wangu, nimegundua
kuwa dereva mlikuwa majuana naye kabla, kweli si kweli…?’ akauliza Soldier.
‘Ni kweli, aliwahi kufika hospitalini, …nakumbuka..lakini
sio kujuana kimapenzi, …’akasema huyo
mdada
‘Sasa hapo utaniambia nini…nikubali tu kirahisi hivyo…’akasema
Soldier, na wakati huo baba alikuwa kaishikilia ile bahasha juu.
‘Kwahiyo basi kwa lolote lile, napenda kutamka, kuwa huyo
mtoto atakuwa sehemu ya familia yetu, kama mke wangu yupo radhi, …mke wangu
kampenda sana huyo mtoto, na tumuombe mungu akitujalia watoto wengine, mimi na
mke wangu, basi mtoto huyo kama ni wangu kweli, atakuwa ni kaka yao wa
kwanza…’akasema
‘Hongeraaah…unaona bro, sasa tupo pamoja, kwa kauli hiyo,
nakuheshimu kaka yangu, mimi nisingeliweza kumkataa huyo mtoto kama angelikuwa
ni wangu…’akasema Dereva, akipiga makofi.
‘Lakini hatujasikia vipimo vya DNA, vipoje,…’akasema Yaya,
na dada yake akasema;
‘Sina shaka na hilo, …sasa hivi naanza kuhisi baba wa mtoto huyo ni
nani, nasikitika sana kwa hayo yaliyotokea.., sijui kama nitaweza kuyasahau,
kwangu mimi itaendelea kuwa ni ndoto ya majinamizi,… namuomba mungu hayo yote
yaweze kuisha kichwani .…’akasema huyo mdada, sasa akionyesha kama anataka
kulia.
‘Usijali, dada, hayo hayana maana tena, hakuna aliyependa
hilo litokee, …usihuzunike, na jamaii haiwezi kukuchukulia vibaya, nina imani
utaweza kumpata mume mwema ambaye ataweza kukusahaulisha machungu yote hayo….na
sina shaka, mke wangu atanisamehe,…’akasema Soldier akimgeukia mke wake.
Mke wake alikuwa kimia, na alipoinu auso wake kulionekana
kuwa na machozi, alikuwa akilengwa lengwa na machozi, sijui alikuwa akitaka
kulia kwa lipi hapo, na huyo mdada alipoona kuwa mke wa Soldier analia, akamsogelea
na kumshika begani huku akisema;
‘Mpendwa dada yangu, wewe sasa ni ndugu yangu, nakuomba
usiingiwe na huzuni,au chuki dhidi ya mumeo, …naomba ndoa yenu iwe ya amani na
furaha, …dada yangu mshukuru sana mungu wako, kwani kwa hali ilivyokuwa ,
usingeliweza kuwa na mume tena, ungelikuwa unaitwa mjane, japokuwa
wangelikupamba kwa maneno matamu ya kisiasa eti mke wa shujaa…kiukweli huyu
mume wako ni shujaaa,..mateso aliyoyapitia hakuna mwanadamu angeliweza
kuhimili..
‘Mimi mwenyewe nilishudia kwa macho yangu mumeo akipitia
mateso makali, kama ndio yeye alikuwa huko, maana sijui..ila nahisi ndio yeye,
vinginevyo, siwezi kujua,,..nilimuona akiteswa…mpaka
anapoteza fahamu, hawachoki kumtesa, mateso yalizidi mpaka anapoteza
kumbukumbu..na aikuwa kama punguani, sikujua kuwa leo ninaweza kukutana naye
akiwa katika hiyo hali…siamini kuwa ni yeye, nahisi ndio yeye, mimi sijui, …mpende
sana mume wako, na mshukuru sana mungu wako…’ akasema na kumgeukia tena
Soldier.
‘Sikupenda nishike hii mimba haraka hivyo, wazazi wangu
wananihitajia sana,..lakini ya mungu mengi, na kama nilivyosikia huyu dereva
akiimba ‘kitanda hakizai haramu ..sio lazima tendo la kupata mimba litokee
kitandani, ila hata porini… sipendi kusiki watu wakisema huyo mtoto ni wa haramu,
uharammu wake ni nini, narudia tena huyu
mtoto sio mtoto haramu kwani ametokea kwenye mazingira magumu..na akikua ana
hitajia kusikia historia yake , wapi alipotokea.
‘Sikujua kama nitaweza kujifungua salama, sikujua kama mtoto
huyu atapona, nilizaa kwenye uchungu mkali, kwahiyo ombi langu la mwisho, nawaombeni
jamani niondoke na huyu mtoto wangu, na mungu akipenda tutakuwa tunatembeleana,
maana ni lazima nirudi kwetu, nikawaone wazazi wangu..’ akasema
**********
Ikaja muda wa kuifungua ile bahasha kila mtu macho yakiwa
pale, wenye viroho hafifu ikawa ni shida kwako, na hatimaye barua ikafungulia,
na baba alipoona kilichoandikwa akamkabidhi mke wa Soldier, akamwambia soma
hapo chini kumeandikwa nini, na mke wa Soldier akasema;
‘POSITIVE…’
‘Sema tena…’akasema Dereva
`POSITIVE…’ akasema mke wa soldier sasa akimuonyeshea mama mkwe
wake.
‘Sema tena…’akasema mama
‘Positive….’akasema mke wa Soldier na kumkabidhi hiyo barua,
yule mdada, ambaye ni nesi akaikagua kwa makini na hatimaye akasema;
‘Ahsante mungu, yametimia, sasa sina shaka tena kuhusu baba
halali wa mtoto…’akasema huyo mdada akitoa machozi…na jina la utani, nitamuita
huyu mtoto komandoo…’ akasema sasa akijariibu kutabasamu, na taratbu mke wa
Soldier akawa anamuanglai amume wake,…macho yakakutana, na kilichofuata hapo ni
kilio…
Mke wa Soldier alipomaliza kulia, taratibu akamsogelea mume
wake…na bila kusema nini, akamvaa mume wake, tofauti na walivyofikiria watu,
akamkumbatiana mumewe, na mikono ya mumewe ikawa inasita kujibisha lile kumbatio,
baadae naye akafanya hivyo, huku mkewe machozi yakimtoka na alimshikili amumewe
kwa nguvu na baadae akasema;
‘Nisamehe sana mume wangu..najua hujakosea, najua hayo yote
ni mapenzi ya mungu, na tumuombe mungu ndoa yetu iendelee kudumu, nisamahe kwa
kauli zangu chafu…nasamehe kwa yote…nakupenda sana mume wangu…’akasema na
Soldier alikuwa hasemi kitu, ni kama kashikwa na butwaa fulani. Baadae akasema;
‘Nakupenda sana mke wangu…’
**************
MWISHO.
WAZO LA LEO:
Binadamu kukoseana ni jambo lisiloepukika,..kwani mawazo, hulka tabia na imani
zinatofautiana, hatuwezi tukafanana au kukubaliana kwa kila kitu, muhimu ni
kuhimiliana,kuwa na subira, kusameheana, kuvumiliana, na kuweka mbele upendo na
amani tukijua sisi sote ni watoto wa Adamu na Hawa, na tukijua kuwa hapa
duniani ni mapito tu ispo siku sote tutarejea kwa mola wetu.
‘ndio maana nasema nimechanganyikiwa maana wote
wanafanana..na kama nilivyosema sikuwahi kupata muda wa kumchunguza, maana muda
wote ni mteso, na ukiwatiba ni haraka haraka umesimamiwa na wao…kiukweli
nilipogundua nina mimba, nikawa na hamu sana ya kumfahamu huyu mtu…lakini
sikuwahi kumuona sura yake kamili kiasi cha kumtambua…’akasema
NB: Nawashukuruni sana kuwa nami kwenye kisa hiki,… natumai
mumejifunza pamoja nami, na tuzidi kuombeana heri, ili tuweze kuja na kisa
kingine kizuri zaidi, NIMEKUWA nikiandika kwa shida, kwa kukosa vitendea kazi,
lakini ipo siku mambo yakuwa vizuri,
Kama kuna maoni, hoja, mawazo msisite kunitumia kwa email,(miram3.com@gmail.com)
au hapa hapa kwa facebook(inbox)
TUPO PAMOJA
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment