'Baba umepona...umeweza….ku-ku-inu.-' akawa anaongea huku anashindwa kumalizia maneno yake, macho yakiwa yamemwangalia baba, na kidigo akamwangalia mama yake ambaye naye alikuwa kwenye huo mshangao..na kwa haraka akarejesha macho kumuangalia baba yake kama vile hataki kuikosa sekunde moja ya kumuangalia baba yake…
Mama yake naye alikuwa ameshikwa na butwaa, na sasa yeye alikuwa akinua mikono juu kushukuru, kumshukuru mungu, na kwa sauti akasema….
Dereva yeye alikuwa kama baba yake alikuwa kaelekeza uso wake kule baba yake alipokuwa akitizama alikuwa naye kashikwa na mshangao wa aina yake, haamini hicho anachokiona, na hakutaka ageuke ili aweze kuona vyema, lakini mke wa Soldier alikuwa usawa unaomzuia kuhakikisha hicho alichokiona,
Soldier sasa aliamua kusogea kabisa hadi pale kitandani alipolala baba yake, akiwa na furaha usoni, akaenda kukaa karibu na baba yake, kuhakikisha kuwa anachokiona kipo sahihi, akawa anamkagua baba yake mwilini, maana kuinuka huko kulimfanya sehemy ya kifuani kuwa wazi, alikuwa kavuliwa shati, soldier akarudia tena yake maneno,;
'Hatimaye sasa baba umepona..'akasema, na baba hakujibu kitu, bado macho yake yalionyesha kuangalia jambo, ambalo lilimfanya naye awe kwenye mshangao, mshangao uliompa kitu kama mshtuka na kumfanya aweze kuinua mwili uliokuwa hauwezi kuinuka na kujikuta amekaa mkao wa kawaida pale kitandani.
Kutokana na ile hali, ya baba yake kuangalia huko mbele, kwa wale wageni, soldier naye akavutika kuangalia huko, kuona hicho baba yake alikuwa akitazama, na kitendo hicho kikafanywa pia na mama yake…
'What..'ilikuwa sauti ya Soldier, lkn alikuwa kachelewa, hakuweza kuhakiki hicho kitu, na kwahiyo ubongo wake haukuweza kunasa lolote la msingi zaidi ya kuingiwa na kiwingu kidogo cha mawazo , lakini kwa vile hakuweza kwa haraka kufahamu ni kwanini moyo na akili yake ilishtuka kidogo, akapotezea, na kumgeukia baba yake..
Kwa muda ule, huyo baba yake alikuwa katizama chini, kama anawaza jambo lakini baadae akainua uso wake kutizama huko mbele, sasa hakukiona kile alichokuwa akikitizama, …mke wake alikuwa keshajua mume wake alikuwa akitizama wapi, lakini hakuelewa ni kwanini mume wake apate mshituko wa namna hiyo mshituko ulioleta neema.
'Ndio yeye..'ilikuwa sauti iliyotokea kitandani, na sauti nyingine miongoni mwa watu waliokuja kumuona mgonjwa ikatamka maneno kama hayo ila yeye alisema:
'Ndio wewe..lakini umefuata nini huku, hujui hairuhusiwi…'huyu alikuwa dereva
'Umefuata nini huku..?'huyu alikuwa dereva alikuwa akiuliza akiwa kawageukia wale wadada wawili, haikueleweka, anamuulizia nani kati ya wale wadada wawili.
Kukapita ukimia fulani, hakuna aliyesema neno, na aliyeuvunja huo ukimia alikuwa yaya, alisema:
'Jamani huyu ni dada yangu pacha, japokuwa hatufanani sana, alikuja kunitembelea, na tumekutana naye kituoni akinitafuta, hakujua tunaishi wapi . .ana kibali rasmi..'akasema.
'Ninajua ni kwanini unafanya hivyo, ulifikiri sitakuona tena, kwanini ulinitoroka?' alisema kaka yake mke wa Soldier, sasa akimsogelea na yule msichana akawa kainama chini.
'Mlikutana naye wapi, haishi huku huyu, baada ya kupatwa na matatizo ndio alikuja kujiunga na sisi pale kambi ya wakimbizi..'akasema Yaya akiwa kama anamkinga dada yake kutoka kwa kaka wa mke wa Soldier.
'Ninafahamu, namfahamu sana huyu ndugo yako muulize mimi ni nani kwake…hakuwahi kukuambia mtu gani alimsaidia,…na anajua nilivyomwambia, kuwa nipo tayari kumsaidia zaidi,..lakini nilishangaa kutoroka, kule alipokuwa akiishia…na..na..’ kabla hajamaliza, yule yaya akasema;
Kitu kingine kilichomshangaza Soldier ni tabia ya huyo Yaya, kumbe ni muongeaji hivyo, mbona awali alikuwa anaongea,kwa mashaka, sasa akawa anamuangalia makini, ni kama aliwahi kumuona mahali, lakini hakuweza kukumbuka ni wapi…halafu akageuza uso wake kumuangalia mkewe, macho yao yakakutana, kumbe mkewe naye alikuwa akimuangalia, na kwa haraka kila mmoja akaangakia kwingine. Aliyeona hicho kitanda alikuwa mama yake Soldier, na kitendo hicho kilimfanya mama huyu atabasamu
'Hata mimi namfahamu huyo binti,..ningelifurahi kama ungeacha uso wako wazi, unaogopa nini,…kama ni wewe yule…sioni kwanini ujifiche, na kama una kibali kuwa huru,,,lakini hebu ondoa hayo mawani uache uso wazo ili nihakikishe, nahisi ndio maana ulikuwa unaogopa kuingia...'akasema dereva.
'Wewe… na tabia yako kila mtu unamfahamu,...’akasema Soldier, na Dereva akacheka kwa kama mzaha fulani, na Soldier hakutaka kuongea zaidi na huyo ndugu yake badala yake akamgeukia baba yake na kusema;
'Hata siamini, dunia hii, hapana, na sijui kwanini nilipoiona sura yake nilishikwa na mshituko wa namna hiyo,…unajua, hata sielewi ni kwanini,…hebu binti, samahani hebu sogea huku nikuone vyema, wewe ni nani hasai,...?'akauliza mzee.
'Mume wangu, hebu kaa vizuri, naona macho yako yamekuwa hayabanduki kwa huyo binti....umeshaambiwa ni ndugu yake Yaya, wewe unazidi kumtamani, huchoki, mtu bado unaumwa, ..bado ..?'akasema mkewe.
'Mke wangu bwana, wivu…utakupoza, hujui ni kwanini nasema hivyo, wewe hujiulize ni kwanini mpaka nikapatwa nah u mshtuko, hadi nikaweza kujiinua,..unajua, nilihisi kitu kinakata kwenye kiuono, nilipojilazimisha kuinuka, na sasa…ooh, nimeweza….’akasema.
'Kuhusu nini mzee..?'akauliza Soldier, sasa naye akimuangalia huyo binti kwa makini, lakini kn usingeliweza kumuona sura yake, alishajifunika, na sasa likuwa amegeukia upande mwingine.
Soldier, hakupata bahati ya kumuona vyema usoni, kwani wakati anamuangalia ndio wakati binti huyo anajifunika, inaonekana kuna kitu alikuwa akimuonyesha mke wa Soldier wakati wanaongea,... na alipogundua watu wanamuangalia akajifunika kwa haraka.
'Huyu binti ndiye yule aliyekuja na mtoto akamtelekeza kwenye mlango wa chumba cha hoteli niliyokuwa nakaa nikiwa huko nchi ya jirani, kiukweli niliapa siku ya kuonana naye namsweka ndani, maana kanisababishia majanga...'akasema mzee.
'Ndio yeye mzee, sijahakikisha lakini nilivyomuona alipojifunua hapo, nikajua ndio yeye,..hata hivyo mzee, mimi ndiye niliyemtuma afanye hivyo, nikiwa na maana muhimu sana....'akasema dereva.
'Sawa kabisa, nilijua tu haya yote wewe ndiye muhusika, haya dereva tuambie ukweli, ulivyo, kumbe wewe ndiye umempachika mtoto wa watu mimba..halafu unamsingizia mzee….'akasema Soldier akimuangalia Dereva..
WAZO LA LEO: Muumba wetu anafahamu ni lini , na kwa namna gani atupatie haja zetu, wengi wetu hufikia sehemu ya kukata tamaa, na hata kulalamika kwanini mimi…naomba sipati, kwanini mimi nakuwa mtu wa shida, kwanini mimi…na hali hii inafikia mtu kupungukiwa na imani zetu za dini, na kujiingiza kwenye shiriki. Ni kweli matatizo, shida, nk, yanafikia ukomo wa akili zetu, ukomo wa kuvumilia, lakini yote hayo tumkabidhi mola wetu , yeye ndiye anajua zaidi,..kamwe tusikate tamaa na kukufuru, tutashindwa mitihani hii ya maisha.
Ni mimi: emu-three
No comments :
Post a Comment