Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, March 20, 2017

KITANDA HAKIZAI HARAMU-22



Dereva akiwa kabadilika, alimuendea mama yake na kusema;

'Hasa wewe…nakutafuta sana..lazima nikufundishe adabu, unadiriki kusema uongo, kuwa mimi sio damu ya huyu hawara wako…..mzandiki mkubwa wewe, mara ngapi mumekuwa naye,..mimi nawaona tu…mimi sitaki uchafu huo nimechoka..sasa nakumaliza wewe kwanza…’akawa sasa anamsogelea mama yake.

‘Nisamehe mwanangu nitasema kila kitu…usinitese, usiniue mimi ni mama yako…’akasema sasa akipiga magoti huku anatetemeka.

‘Umeniuzi,…ni lazima nikufundishe adabu….wewe na mwenzako, ni kwanini mnasema mimi sio damu halali ya ….bwana wako..kwanini….’akasema sasa akiwa keshamshika mama yake na kumuinua juu, na anataka kumbamiza chini…mama huyu ana matatizo ya presha na kama hali hiyo itazidi anaweza kuathirika vibaya, sana..na kama atarushwa kama walivyorushwa wengine sizani kama anaweza kuhimili

Baba wa Soldier akaliona hili , akajua asipofanya jambo, …mke wa marehemu watamsahau, akajitutumua na kukaa vyema , akasema kwa sauti.

‘Nitasema kila kitu mwanangu…nitaitoa siri yote ya baba yako…nitasema kila kitu muachie mama yako utamuua, huyo ni mama yako…..na mimi nitasema kila kitu,…tafadhali…’akasema mzee.

‘Haya waambie ukweli, simuachiii huyu mtu, mpaka usema ukweli wote…kuwa mimi ni damu yako, kuwa wewe na mama ni wapenzi, kuwa…. Mimi ni haki sawa na familia, hii, ongea kila kitu…

‘Haya subiria, niongee…….’akasema mzee

Tuendelee na kisa chetu….

***********

 Ukumbuke haya yote yanasimuliwa na baba yake Soldier, na kwa jinsi mzee alivyozidi kuongea, ilifika mahali dereva akawa anabadilika kidogo kidogo, kwani kwa muda wote huo, alikuwa bado kamuinua mama yake hewani akitaka kumbamiza chini, lakini kila muda ulivyozidi kwenda dereva naye akawa kama anaanza kuishiwa nguvu…

Ikafika muda, dereva…, akachuchumaa,...mzee anaendelea kuongea, huku mama yake dereva kainuliwa juu, ikafikia muda dereva akakaa mkao wa kukaa,...mzee alikuwa bado anaongea

 Na baadae akamshusha mama yake na kumshikilia kama anataka kumtia kabari…na mzee anaongea, na wengi walikuwa wakimsikiliza mzee, hawakuwa na mawazo y ahuy mtu tena.

Na ilipofika sehemu hiyo tuliyoishia sehemu iliyopita, ghafla dereva akaporomoka chini…,na mama yake naye akamfuatia, na wote wakawa wamelala sakafuni, kimiaah..

Kitendo kile kiliwafanya wote waliokuwemo humo ndani kusimama kwa uwoga, na wengi waliangalia usawa wa mlango, tayari kukimbia.

Dereva na mama yake sasa walikuwa wamelala sakafuni, mama kalala, kichwa kaweka kufuani kwa mwanae. Wapo kimia kabisa…

‘ Hebu waangalieni hao watu kama wapo sawa...’ akasema yule mzee mualikwa akiwa karibu na mlango, alikuwa tayari anataka kukimbilia nje.

Na ni nani angewasogelea, kila mmoja alitoa jicho la uwoga, na aliyeweza kusogea pale baada ya kupita dakika chache, ni docta docta, kwa tahadhari akawasogelea, na kuanza kuwakagua, na alipoona kuna usalama, akaanza kuwapima mapigo ya moyo, na baadae akasema:

‘Wapo sawa..naona walipoteza fahamu kidogo, lakini naona wameshazindukana,…wapo sawa…’akasema docta.

'Docta una uhakika, maana hayo sio mambo ya hospitali, yana wenyewe hayo....'akasema mzee.

 Na mara dereva akafungua macho yake na kwa haraka akakurupuka, na kumsukuma mama yake ambaye alikuwa bado hajazindukana vyema, na kwa haraka akasimama, alikuwa kama mtu aliyeshtuliwa kwenye usingizi na ndoto mbaya, akawa sasa anaangalia huku na kule.

Kwa kitendo kile, cha kuzimama kwa haraka, wengine walishafika mlangoni, wakikimbia, kutaka kutoka nje, ambaye hakuweza kusimama na kusogea pale alipo alikuwa baba yake Soldier.

Dereva, akili ikamtulia akaangaza macho, na kushangaa kuona watu wanamkodolea macho, akatikisa kichwa na kusema:

'Kumetokea nini jamani?’ akauliza.

Hakuna aliyemjibu, watu walikuwa na wasiwasi , huenda jamaa anaweza akaanza makashi kashi mengina wakaishia kuvunjwa viuno na mbavu,..na Dereva alipoona watu wapo kimia, wanamuangalia tu, naye akaanza kuingiwa na wasi wasi, na katika kuangaza huku na kule macho yakatua kwa mama yake, alipomuona mama yake kalala sakafuni, akamsogelea kwa haraka na kusema:

'Mama nini tena, kumetokea nini jamani, mama kafanya nini….na mama umekuja-unafanya…sasa akaanza kukumbuka, na kushika kichwa, halafu akasema
‘Sasa mama, kwanini ulikuja huku,… nilikuambia haya uniachie mimi..?'akasema na kwa muda huo mama yake akawa naye akaangaza macho huku na kule na akili ilipokaa sasa, akazizoa zoa na kusimama, akawa anataka kuondoka.

‘Mama tulia kwanza haujawa sawa, unaona unavyo yumba yumba….’akasema Dereve.

'Tuondoke, twende zetu nyumbani...'akasema mama yake akimshika mwanae mkono, na watu walipoona kuna amani, ikawa sasa kuangaliana,..na hapo ikaonekana hali ya baba yake Dereva haipo sawa.

'Docta hali ya mzee sio nzuri, tufanyaje?'ilikuwa kauli ya Soldier, na docta akamsogelea baba yake Soldier na kuanza huduma ya kwanza.

Mzee akawa analalamika maumivu, na docta akasema:

'Huyu inabidi afikishwe hospitalini kwa haraka, yawezekana kuna athari ndani kwa ndani..'akasema docta.

'Sawa mimi nitamchukua kwenye gari langu...'akasema dereva.

'Wewe mimi sikuamini, ukija kutusweka kwenye makorongo..hapana, tutatafuta usafiri mwingine...'akasema Soldier.

'Kwanini niwasweke kwenye makorongo, mimi ni dereva, nina leseni?"akasema dereva akionyesha uso wa kushangaa.

‘Hakuna muda wa kubishana hapa, muhimu mgonjwa afikishwe hospitalini…’akasema docta.

Hatimaye mzee akabebwa na kuingizwa kwenye gari, haraka akafikishwa hosp, na ikawa mwisho wa kikao hicho kwa siku hiyo.

************
Zikapita siku mbili, hali ya mzee ikawa inaendelea kuwa mbaya, na siku ya tatu, taarifa zikaja, baba anataka kuongea na Soldier na dereva 

Na wote wawili wakafika harala mbele ya mzee, akiwa kalala kitandani….akasema;

'Wanangu, nimewaiteni,najua kuumwa sio kufa, lakini pia kuumwa ni dalili ya kuwa huenda umauti umekaribia, mengine ni majaliwa ya mungu..’akaanza kuongea.

‘Mzee usiwe na shaja, utapona, haina haja ya kupoteza matumaini,…’akasema Dereva.

'Nimewaiteni kwa jambo moja, siku ile kila jambo liliwekwa hadharani, hakuna utata tena na yaliyopita naomba yapite,…mjua sasa nyie ni ndugu, hakuna mjadala, kama rafiki yangu angelikuwepo hai, hili lisingelikuwepo, lakini kwa hayupo nimebakia mimi…mimi ndiye baba yenu wote, naombe mlielewe hivyo.

‘Hamna shida …’akasema dereva, na Soldier akatikisa kichwa tu.

'Sasa nawaombeni jambo moja, kwanza kuhakikisha familia ipo kitu kimoja, ondoeni tofauti zenu, jueni kuwa nyie ni damu ya baba mmoja, ndio yaliyotokea yalitokea isivyo stahiki lakini mkumbuke, mambo mengine yanaweza yakawafanya watu wakapokea mapokea ambayo kwa wengine yanaweza kuwa ni mshangao…hamjui ni jinsi gani hayo yalitokea, lakini..tumuombe mungu atusamehe tu…’akasema

‘Mzee , mimi nakuomba utulize kichwa chako….uangalia afya yako….haya mengine hayana msingi…’akasema Soldier.

‘Ni kweli kabisa mzee….’akasema dereva.

‘Pili, fanyeni jitihada mama zenu warejee ile hali yao ya zamani, mnajua akina mama zenu kipindi cha awali walikuwa kama mapacha , wanaume hali kadhalika, sasa nyie fanyeni hivyo hivyo, muishi kama mapacha, nawaombeni sana, msahauni yaliyopita….’akasema

‘Baba hayo yaache kwanza…’akasema Soldier

‘Usijali mzee, muhimu ni afya yako …’akasema dereva

 ‘’Na jingine, naona ni la tatu eeh, Soldier fanya mpango mkeo arudi, najua kaondoka kwa hasira lakini nimefurahi kuwa mtoto hakutaka kumucha, kampenda mtoto kuonyesha kuwa ni wake, nilijua atamkataa..'akatulia.

'Sasa atamkataa wakati ni mtoto wake…’akasema Dereva.

‘Una uhakika gani kuwa ni mtoto wake…?’ akauliza Soldier

‘Uhakika upi tena, kama sio mtoto wake ni wa nani,…unaona anavyofanana na wewe …lakini mimi sijui, kinachonikwanza, ni jinsi gani mke awe na roho ya namna hiyo,…kutupa mtoto…hivi nyie mnalionaje hilo, yawezekana kweli…’akatulia. Soldier akaonekana kukunja uso, lakini hakusema jambo.

‘Hayo tuyaacheni vijana wangu, …mkitaka kuchokonoa chokonoa mtafikia mahali hamtaelewana na lengo langu ni nyie wote muelewane, najua kuna sintofahamu nyingi, lakini …’akasema baba, na dereva akamkatiza kwa kusema;

‘Sawa baba tumekuelewa, lakini ni muhimu kujua huyo mtoto ni wa nani,… haya, tusema mama ni ..mke wa bro hapa,..lakini baba yake ni nani….?’ Akasema Dereva.

‘Kwa maelezo ya baba, wewe ulisema baba yake ni mzee, au…usitake kupindisha pindisha maneno, wewe subiria mzee apone, …utaniambia ukweli wote, na kama umezua jambo, utaishai jela, nakuhakikishia hilo..sitajali udugu hapa, umenisikia?’ akasema Soldier akimkazia macho dereva, na dereva akatabasamu akibenua mdomokwa dharau...

‘Bro, usiwe na shaka na hilo…ila kwa hilo ndivyo nilivyoambiwa,…lakini hata hivyo, ni nani kakuambia kuwa nilisema hivyo…?’akasema dereva akionyesha kushangaa na kugeuka kumuangalia baba yake.

‘Na nani…hahaha,ulifanya hivyo kumkomoa baba si ndio…, ili upate urithi au…sasa utapambana na mimi…umenisikia vyema..?’ akasema Soldier. Na Dereva akamuangalia baba yao pale kitandani, halafu akasema;

‘Tumuache mzee kwanza apone, najua yeye ana majibu rahisi , lakini mimi ..sikumbuki kuongea kitu kama hicho…mbele yako,…’akasema

‘Uliongea na mzee, ukimshinikiza ili akupatie urithi, na kukuandikia hati ya urithi,..hayo uliyafanya kwa siri, lakini landa pale alipokuwa anaongea baba , wewe hukuwa wewe, nasikia ikiwa hali kama hiyo hujielewi, lakini kwangu utanielewa,……’akataka kuendelea kuongea, lakini baba akawa anamzuia kwa mkono kuwa asiendelee kuongea.

‘Bro…hebu kwanza hayo tuyaache…yatafikia muda wake, tatizo hunijui…utakuja kunijua kuwa mimi sio mtu wa kutishiwa, nyau…lakini hayo tuyaache, ….’akasema

‘Tutaona…’akasema Soldier.

‘Vijana,..watoto mbona mnanikatisha tamaa, kabisa….mumenielewa nilichowaitia, wasiwasi wangu ni kuwa nikiondoka huku nyuma mnaweza kuanzisha vurugu, hilo ndio sitaki mimi, …mnanisikia hebu kwanza yafanyieni kazi hayo niliyowamambia yakikaa sawa, muone maajabu yake, hayo mengine yatajileta yenyewe…na mniombeee mungu nipone, nitawaambia kila kitu,…kuna mambo mengi hayajaka sawa, lakini hata mimi sijaweza kuwa na uhakika nayo….sasa nawaombeni mnisaidie kwa hayo niliyowaambia, ili moyo wangu uwe na amani…’akatulia.

‘Sawa mzee…’wakasema kwa pamoja.

‘Mzee, mungu akujalie upone, maana tunakuhitajia sana…’akasema dereva.

‘Hilo ni sawa…ili upate mtetezi wako..’akasema Soldier

‘Sio hivyo bro, wewe hutaki mzee apone…?’ akauliza

‘Mimi sitaki au wewe ndiye chanzo cha yote haya, hebu jiulize isingelikua wewe, baba angekuwa hapo kitandani…’akasema Soldier

‘Kwani mimi nimemfanya nini mzee…kwani mimi ndiye niliyemuumiza…mimi mpaka sasa sijajua chanzo cha mzee kuumua hivi…’akasema dereva.

‘Basi utajua tu…nimeshafungua kesi, RB, yako ninayo hapa….’akasema Soldier, na mara mlangoni akaonekana mama akija na chakula cha mgonjwa, na wote wakatulia kimia, hadi pale mama aliposogea karibu yako,

Kwa nje kulikuwa na watu wengine wanasubiria waingie,..lakini yaonekana walikuwa wakiogopa kuingia.

‘Ni nani hao wapo huko nje, si mumekuja nao, mbona hawataki kuingia ndani…?’ akauliza mzee

‘Kuna ugeni ….’akasema mama akionyesha uso usio na furaha,.., na wote mle ndani wakageukia mlangoni kuuona huo ugeni, isipokuwa mama , ambaye alikuwa akimuandalia mgonjwa chakula.

NB: Ni akina nani hao..


WAZO LA LEO: Inapofikia swala la ugonjwa, inabidi mambo mengine yashaulike, hata kama kulikuwa na ugomvi, hata kama kulikuwa na uadui..inabidi wote waangalia matatizo ya ugonjwa, kwani mgonjwa anahitajia faraja, anahitajia, huduma, na kukiendelea na sintofahamu inaweza ikawa sababu ya kumuongezea mgonjwa , ugonjwa, au kuzua magonjwa mengine. Tuweni na moyo wa huruma kwa wagonjwa wetu, hata kama ni maadui zetu.
Ni mimi: emu-three

No comments :