…Nilijua labda anaumwa, lkn kumbe sio ,… nilijua labda ana
tatizo la kufiwa au… lkn sivyo kama nilivyodhania, kajiinamia, kalia mpaka
machozi yamekauka, ..nilimuonea huruma sana,lkn utafanyaje, hukumu imeshapita
na iliyobakia kusonga mbele.
‘Vijana mbona upo hivi…..’ nikamuuliza kijana huyo, Swali
langu lilikuwa kama limeamusha moto uliokuwa umefunikwa na majivu, na uliwekwa
mafuta ukawa umezimika kwa upepo tu….
‘Wamenionea, mtihani wa darasa la pili nilipata division one
tena ya uhakika, darasani nilikuwa naongoza, nimesoma kwa shida, wazazi wangu masikini na nilijua huenda ikawa nafasi ya kuwaokoa wazazi wangu,...nimesoma huku naumwa, lakini sikukata tamaa...…sasa ….’akaanza kulia
‘Kwani umepata divisiona ngapi?’ nikamuuliza
‘Eti three,..inayokaribia na four…mimi..hapana haiwezekani,
yaani wamenipita hata wale niliokuwa nikiwafundisha, uso, wangu nitauweka wapi,
..natamani hata …ardhi ipasuke nizame…nisionekane tena hapa duniani, nawaonea huruma wazazi wangu wamepoteza pesa nyingi kile kidogo walichokuwa nacho walijinyima ili nisome, sasa nitawaambia nini....siwezi,siwezi kuwaona wazazi wangu wakihuzinika tena, kwanini sisi...kwanini...…’yalikuwa
maneno yaliyonifanya nihuzunika na niogope!
‘Sikiliza kijana…., unajua hata kwenye mahakama, unaweza
kuhukumiwa ukawa hujaridhika, na ndio maana wanatoa nafasi ya kuapili…unanielewa,…wanaosahihisha
hiyo mitihani ni wanadamu tu…ndio maana, hata kwenye hii mitihani kuna nafasi
hiyo ya kuapili…si unajua kuna kukata rufaa kwa ajili ya kusahihishiwa tena,
wewe kama unajiamini ulifanya vyema, nenda kajaze fomu , watakusahihishia
mitihani yako tena.
‘Sasa kwanini wafanye hivyo,…ukate rufaa ndio waone makosa
yao,..na hata hivyo mimi nitapata wapi hizo pesa,..wazazi wangu ni masikini…niambie
sasa?’ akaniuliza, hapo nami nikabakia kimia.
Matakeo ya mitihani yameshatoka, wapo wanaofurahia, na wapo
wanaohuzunika, wapo ambao wanajuta kwa hasara walizopata maana kusomesha sio
mchezo, lakn mimi najiuliza upimaji huu wa mitihani hivi kweli unaleta taswira
halali ya uwezo wa wanafunzi wetu…, au ndio mazoea tu.
Inawezekana kweli wengi wa waliofaulu walikuwa wakifanya
vizuri darasani,..lakini je tulirejea kuangalia matokea yao ya kidato cha pili,…ufaulu
wao na wa sasa, ili kuone labda kuna makosa kwenye usahihishaji, au kuna sababu
nyingine… na ukiangalia wengi wa waliofaulu wametokea shule zenye uwezo, walimu wazuri,
mandhari, vitendea kazi nk…je hili kama serikali tunaliangaliaje,…hatuoni kama
tunawagawa wananchi…
Kiukweli kufaulu mitihani ni moja ya nafasi kubwa sana ya kuwapima na kuwaendeleza vijana
wetu..lkn mimi bado nina mashaka katika upimaji huu wa Nani zaidi…HEBU
TULIANGALIE HILI KWA JICHO LA UFAHAMU WA PILI ILI TUTENDE HAKI!.
Wasiwasi wangu ni kwa hawa vijana ambao wamechanganyikiwa na
matokeo haya ya mitihani, na wasipopata wazazi wazuri wa kuwanasihi vijana wetu,
watoto hawa wanaweza kubadilika na kuwa wengine kabisa,…hawataona umuhimu wa
elimu tena, na huenda wengine wakafikia kufanya vitendo vibaya. Tulishuhudia kipindi
fulani wengine walifikia hadi kutaka kujiua.
Mimi nina imani kuwa huenda wengine wangeliweza kufanya
vyema zaidi ya hayo waliofanya vyema kama wengelikuwa kwenye nafasi za hao
waliofanya vyema, lakini watawezaje kukaa huko..yote maisha…hawa sasa, watarudi
nyumbani, na kujiunga na makundi haramu…au ndio kwaheri tena na elimu ya shule! watafanya nini tena...Yote maisha!
Mimi naona kuna haja
ya kutafuta awamu nyingine ya kuwapima hawa ambao wanaambiwa wamefeli, labda
paitwe,..elimu ya nafasi ya pili, wapimwe, kama kweli wana uwezo waweze
kuendelea mbele, au wajiunge na vyuo fulani maalumu kutokana na vipaji vyao…hawa
ni watoto wetu sote!
Pia, hawa wanafunzi pamoja na mitihani hii ya mwisho, lakini
kuwe na maksi za mitihani ya nyuma, asilimia fulani, ihusu matokea ya nyuma ,
kama wanavyofanya vyuoni, na mtihani wa mwisho uwe na maksi zake, ili
zijumlishwe pamoja na kuona je kweli hawa vijana wetu wameiva, huku nyuma walikuwa wanafanyaje…tuwapime hata vipaji
vyao nk…. Hii ni hatua nyingine ya kuwapa vijana wetu elimu stahiki, ili mwisho wa
siku tuwe na wakufunzi wazuri na pia vipaji visje kupotea bure.
Ni maoni tu kutoka kwa mzee wa busara…
Ni mimi:
emu-three
1 comment :
Ni kweli baba ila tatizo ya mfumo wetu hatuna pakuyasemea hayo na hata ukisema hayasikilizwi
Post a Comment