Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, February 22, 2017

NI VITA AU KUNG'ARISHA NYOTA


Ni sinema au ni MOVIE…(FUPA LILIMSHINDA FISI)

Wakati tunasubiria sehemu nyingine ya kisa chetu cha FISI LILILOMSHINDA FISI NIKAONA TUANGALIE PICHA…SINEMA…TASWIRA YA PICHA…..

***************************

Ndio picha imeanza…..inaonyesha taaswira mbili, vitani na uraiani!

‘Mara anaonekana kamanda wa vita yupo msitari wa mbele kupambana na maadui..akiwaekeleza wapiganaji wake cha kufanya…na milio ya mizinga inasikika huku na kule….

Mara tunapelekwa ofisini, kwa mpokea taarifa,…kuna taarifa imekuja na mjumbe!

`Kamanda anahitajika nyumbani , ana kesi ya kujibu,…’

‘Kesi ya kujibu,..kesi gani, na nani kasema …?’msemaji wa kamanda akauliza

‘Ni kesi ya jamii, sheria inamuhitajia…’akaambiwa….

‘Hawezi kurudi nyuma..yupo mstari wa mbele akigeuka nyuma, maadui watajua kasalimu amri, na itakuwa ni nafasi ya maadui kuendeleza mapambano…’akasema mleta taarifa.

‘Lakini anatakiwa na sheria, na sheria ni msumeno, na yeye ni mmoja wa watu wanaotakiwa kuitekeleza sheria kwa vitendo…’akasema mletaji wa taarifa.

‘Kwenye vita, sheria za ndani zinasubiria kwanza…’akasema msemaji.

Na mara tunaonyeshwa upande wa pili , uraiani…kuna zogo la zomea zomea, mara watu wakasikika wakisema na kupaza sauti; `alatwe aletwe….’

Kwa namna nyingine wapiganaji wanawasiliana na uraiani wanapata taarifa za nyumbani kuwa kuna vurugu,…. Wapiganaji wakapeana taarifa, nyumbani kuna vurugu, wakahisi huenda maadui wamepenya kuja kuwavamia kwa nyuma,…kunatokea sintofahmu…

Mmoja wa wapiganaji anamuendea kamanda na kumuuliza;

‘Kuna nini huko…?’ sasa badala ya kutuliza akili kumkabili adui wapiganaji wanapata changamoto nyingine, wanahitajia majibu haraka ili kutuliza akili zao…kuna nini huko nyumbani!
Wakati huo huo tunaonyeshwa mjumbe anabishana na mzungumzaji wa kamanda…

‘Ni sheria gani ilisema sheria za ndani zinasubiria…?’ akauliza mjumbe aliyetumwa..na kwa namna fulani,…sauti yake ikawa inasikika uraiani!!,…. watu wakasikia, na kuanza kushangilia….kelele zinaongezeka, ….

Na kwa namna nyingine…kelele zinawafikia hata wapiganaji, wapiganaji sasa wanageuza vichwa nyuma…

‘Kuna nini huko…..’.  wakati wanageuza vichwa sinema ikaganda!

 Swali, hawa wanaoshangilia, ni nani na wanataka nini…!!! Tukajiuliza sisi watazamaji wa ‘movie, na mara movie ikaisha hapo na kusema;  

                                   ‘Angalia sehemu ya pili….’

Tuache movie iendelee…lkn,…

Mimi nikabakia na maulizo  akilini, najiuliza maswali mengi kichwani,

‘Hivi hiyo vita ni ya nani, ilikuwa ya nchi au ya kung’arisha nyota,…je hili linalofanyika lina faida au halina faida kwetu, hasa kwa kizazi chetu, hasa kwa taifa letu..,…tusije kugeuza vita ikawa ‘vutia’ hapana...hapana...

Ninasema hivi huku nikiangalia kwa uoni wangu,…kama sio mtoto wako, kuna jamaa yako, 
kaathirika na hili janga la ‘malegeza’ mimi nayaita haya madawa ya kulevya ‘malegeza’. Hii ni vita kubwa, duniani….haijaanzia hapa…!

‘Vita hii ni kubwa ina kila aina ya mbinu…sio vita ya kung’arisha nyota hii, tuweni makini sana’
Haya ngoja tuje kuiona sehemu ya pili ya picha,..


 NB: Soma kisa kipya cha ‘Fupa lililomshinda fisi…’ utayagundua haya….!

Ni mimi: emu-three

No comments :