Keleee…vifijo…hoi hoi…shangwe nderemo…vikatanda, pale Soldier
alipoingiza mguu wake ndani…’
‘Shujaa, shujaa, shujaa, shujaa…..’
Soldier hakuamini,..alishikwa na butwaa, akabakia kasimama pale
mlangoni, ..hakuamini kuwa ndivyo ilivyopangwa hivyo, hakuamini kuwa sifa zake
zimefika hadi huku kijijini..kiukweli alikuwa shujaa huko alipokuwa alifanya
mambo mengo ya ushujaa…
Kwa kitendo hicho akili ya mawazo yake ya sintofahamu,
yakatulia, sasa yakaendana na tukio hilo…sasa, faraja, upendo..vikatawala
kwenye ubongo wake, kumbe wanandugu,wanafamilia, jamii kwa ujumla inampenda kihivyo,
hakuamini…akabakia kutikisa kichwa tu, na tabasamu,..akazuia machozi yaliyoanza
kumtoka,…akageuza kichwa huku na huku kuwatizama waliokuwepo,..
Wapo baba na mama wa pande zote,…yaani ukweni na kwake,… wapo pia
wadogo zake, shemeji zake,…wapo majirani..wapo pia maaskari wenzake, ambao alikuwa
nao huko kwenye misheni ya kimataifa ya kulinda amani…alishangaa kumbe na wao
walialikwa hapo,…oh, akafarijika sana,…
Akainua mguu wa pili kuingia ndani, …na wa kwanza kuja
kumkumbatia kwa bashasha alikuwa baba yake mzazi…,huyu ndiye aliyemlanda,wanasema
nyoka huzaa nyoka, basi hapo ilitokea kweli, baba mtu aliwahi kuwa askari na
mtoto naye sasa ni askari…, tabia na miendendo ni ile ile ya baba na mtoto,
labda imetofautiona kidogo kutegemeana na nyakati….
Baba alimkumbatia mwanae akimpiga piga mgongoni, halafu
akamshika mwanae mkono, wakaangaliana usoni, huku wote wakitabasamu, na baba
mtu akamnongoneza kitu sikioni mwanae,..kwa kusema hivi:
‘Sasa umekuwa mwanangu, sasa nahisi faraja, …ila kabla ya yote
uwe na subira…usije kuchukulia mambo kwa pupa…nitakuja kukuambia mwenyewe ni
nini kinachoendelea, ..najua, na hata ingelikuwa mimi, ningechukua hatua kali
sana, lakini …usije kumvunja mama yako moyo, yote hayo ni kwasababu ya mama
yako…na hataki kuniambia ukweli, sasa..tuwe na subira….’halafu kwa haraka
akamshika mkono na kuanza kumtambulisha kwa wageni.
‘Wanandugu,mimi ni baba yake, mimi ndiye mlezi wake, nikiwa humu
mimi ndiye mwenye mamlaka,…nachukua nafasi hii kuwakaribisha wote, japokuwa
tulishakaribishana..ila kwasasa nahisi watarajiwa wote wamefika…hasa wale
waliokuwa pamoja na mwanangu huko walipokuwa..ni vita, ya kuwasaidia wenzetu,…kwahiyo
kazi waliyokuwa wakiifanya ni ya kujitolea…
‘Huyu mwanangu pia na wenzake waliokuwa huko mstari wa mbele
pamoja, tunashukuru sana kuwa wote wamerudi salama,..…sisi kama wanakijiji tuliona
tulifanye hili kama familia ya kijiji..Nashukuru kama kiongozi wenu wa kijiji
mliitikia hili tukashirikiana pamoja, na tumelifanikisha, hongereni sana na
ahsanteni sana…’akawa anaongea na watu wakamshangilia.
Soldier pale akili yake ilikuwa mbali, akawa kila mara
anatafakari maneno ya baba yake, hasa pale alipoambiwa;
‘..Najua,
na hata ingelikuwa mimi, ningechukua hatua kali sana, lakini …usije kumvunja
mama yako moyo, yote hayo ni kwasababu ya mama yako..’
‘Ina mama anahusika na hili….haiwezekani, mama yangu mwenyewe…’
akawa anatikisa kichwa cha kutokukubaliana na hilo, na hapo akageuza kichwa
upande ule walipokaa akina mama na akamuona mama yake akiwa amekaa mstari wa
mbele na dada zake,..huku kashika shavu, mama yake hakuonekana mwenye raha kama
walivyokuwa wengine. Anamfahamu sana mama yake,ni mpole,..na wakati mwingi sio
mcheshi wa kuruka ruka, kuongea sana, japokuwa ni mkarimu sana, ataongea maneno
machache tu…basi kamaliza
Soldier anampenda sana mama yake, anakumbuka kuna kipindi
aliwahi kupigana na baba yake kwasababa baba yake huyo alikuwa akimpiga mama
yake..na, kitendo hicho anakikumbuka hadi leo kwani kilimfanya yeye na baba
yake wakae karibu wiki nzima hawaongei lakini baadaye yeye mweneywe akajua
kafanya kosa akaenda kumpigi baba yake magoti.
Baba yake alipoona mwanae anafanya hivyo, akatikisa kichwa, …akamzuia
mwanae asimama na kusema;
‘Haina haja ya kunipigia magoti…najua mimi ndiye niliyekosea,
lakini wakati mwingine inabidi tufanye hivi,..sio kwamba napenda,..hulijui
hili, ila ipo siku utalijua… hawa akina mama, hawa…..wanawake, wengine inafikia
wanafanya mambo kama watoto, inatokea, hata sisi wanaume tunaweza kufanya mambo
ya kitoto, inatokea,…sijui kwanini…lakini mwanangu utakuja kuoa, haya utakuja
kuyaona,..ni kawaida, sio kosa lao,..sio kosa letu, ni ubinadamu, na akina
mama, wengi wanapenda kudekezwa…’akaambiwa.
‘Lakini baba mungeyaongea tu ndani…, sio kumpiga,..mama mwenyewe
mpole..nasikitikka sana kufikia hali hii…’akasema
‘Najua sana,..mimi ninamfahamu sana mama yako, kuliko
unavyofikiria wewe, na kama isingelikuwa ukali wangu, mamaa yako angelikuwa
hata sijui nisemeje, ana huruma kupitiliza, ni mpole kupitiliza, na yupo tayari
vitu viharibiwe, hapana mimi siwezi….anaonewa tu…inabidi nimkomaze,… niseme
hivyo, upole umemzidi….ila unielewe kitu kimoja,…’akatulia
Mimi ni najua ni nini ninachokifanya, usipende kuniingilia pale
ninapotimiza wajibu wangu, kama mume, … tutakosana, hii ni ndoa yangu na wewe
utakuja kuwa na ndoa yako… hujui ni nini mama yako alichokifanya, na ameniomba
msamaha sana..sina tatizo na yeye yaliyopita yamepita,..ila nakuonya sana
mwanangu, uwe makini sana..hasa ukioa ..najua wewe una tabia kama yangu,…
chunga sana mkono wako, usije ukawa kama mkono wangu…’baba yake alimuambia
hivyo..
Alipokumbuka maneno hayo akageuza kichwa kumuangalia mama yake,
na macho yao yakakutana, na mama akawa anamuangalia tu, bila kushusha macho
yake, yeye, akashusha ya kakwe,..hakutaka waangaliane sana,…hataweza kuvumilia,…
na sasa akageuza kichwa kuangalia walipokaa wakwe zake…baba mkwe, mzee Simba,
jabari kuliko majabari, simba wa nyikani aliyewahi kupigana na simba na kumuua
kwa mkono wake mwenyewe…ni simba ni kweli..mungu kamjalia minguvu,… akakumbuka
kauli yake wakati anamposa binti yake;
‘Kijana nikuonavyo wewe ni sawa na baba yako,…baba yako ana
hasira, hajui kuhimili, ila nampenda sana, anajua kuhudumia familia,..ndio
maana akanishinda kwenye chaguzi za uongozi wa kijiji,.. yeye ni mfano hapa
kijijini, kaunganisha wanakijiji, kwenye shida na njaa, baba yako alipoacha
uanajeshi alikuja moja kwa moja hapa kijijini,..tukaungana naye pamoja…sasa
umezidisha ujirani wetu na umoja wetu, kwani umekuja kumuoa binti yangu..ila
nakuonya sana…’akakumbuka maneno hayo aliyoambiwa.
‘Mwanamke hapigwi kwa fimbo, mingumi,….kama unapigana na
mwanaume mwenzako,..mwanamke hupigwa kwa kauli nzuri tu, mimi na miguvu yangu
yote sijawahi kumpiga mke wangu, ananiogopa sana,…wanasema mwanamke hapigwi kwa
fimbo anapigwa kwa nini vile, …upande wa khanga..sio hivyo…., kuna namna ya
kumnyosha mke wako, maana yeye sio mtoto mdogo, ana akili timamu,..amelelewa na
wazazi wake..ana heshima zake, sasa itunze ile heshma yake kwa maneno ya hekima…unanielewa…’aliambiwa.
‘Ole wako,..nikisikia umempiga mwanangu..najua yapo matatizo
yatatokea kama familia, hilo lipo wazi,.., najua..kuna kukwaruzana, sasa sitaki
nisikie umempiga mwanangu…kupiga, kwanza kwanini umpige kwa mingumi ,
fimbo..huyo sio mtoto mdogo…inawezakana ikatokea, akamzaba kibao kimoja..viwili
ok.., hata yeye anaweza kufanya hivyo kwako....inatokea, lakini sio kumpiga
unanielewa….kumpiga..unanielewa…’akaambiwa.
‘Narudia tena ole wako…nawafahamu sana tabia zenu,..huyo binti
yangu mpendwa, ninayempenda sana…amamranda sana mama yake, nikimuona yeye
namuona mama yake….sasa uharibu kiyoo changu uone niakavyokufanya, mimi ni simba
simba wa nyika uliza watu watakuambia…..’halafu akampiga kwa ngumi begani ngumi
yenye nguvu inauma,..jamaa anasema maumivi yake anayakumbuka mpaka leo. Baba mkwe
alipoona mkewe anamuangalia akmuonyeshea ishara ya dole…kileo dole tupu!
Pembeni ya huyo yupo kaka mtu, ….huyo ni adui yake tokea
utotoni, walikuwa kila siku wanapigana, mpaka walipofikia utu uzima ndio wakawa
kidogo wanaheshimiana, anakumbuka kaka mtu huyo hakupenda yeye amuoe dada yake,
kwani siku zote alimuona yeye kama adui yake..lakini wazee waliingilia kati
ndio wakaja kufunga ndoa hata hivyo kaka mtu huyo hakuhudhuria hiyo harusi yao,..leo
yupo kwenye shughuli, …
Soldier, aliwaangalia wengi wenye sifa hizi na zile, lakini
baadaye uso wake ukarudi kwa mama yake, mama yake alikuwa bado amemtizama,
mpaka soldier akaingiwa na mashaka…anamfahamu sana mama yake akiwa na jambo
anataka kukuambia, inachukua sana muda kukuambia, huwa anliwazia sana, na
hataki kukurupuka tu,, na jinsi alivyomuona akimuangalia,akahisi kuna
jambo..akatamani atoke pale amuendee mama yake ,amuambie watoke nje, wakaongee,
lakini hapo kuna utaratibu hauwezi kuuvunja…kwani mpaka muda huo alikuwa
hajapewa nafasi ya kusamiliana na wengine akiwemo mama yake.
‘Sasa ndugu zanguni, najua wengi mna hamu ya kumsikia shujaa,
awasalimie kidogo, leo ni kusalimiana kidogo tu,…najua mna hamu ya kusalimiana
naye mkono kwa mkono, lakini kwasasa siwezi kumruhusu, mila zetu zinazingatiwa,
atawasalimia kwa ujumla kwanza ataanza yeye kama mwenyeji wa nyumba hii, halafu
atawaita wenzake mmoja mmoja..tunataka kusikia mikakati yao ya kuendeleza hiki
kijiji, ndio maana ya kusoma, ndio maana ya kuwa kwenye nyadhif, kukumbuka
kwenu na kujua ni vipi utaendeleza jamii ya kwenu …
‘Mke wake yupo..?’ akauliza na alipotaja hivyo Soldier alihisi
damu ikimchemka,…na mara mkewe akatokea kwa nyuma akiwa amembaba mtoto..amakabidhi
mtoto yaya wake na kuelekea pale mbele waliposimama baba mkwe wake na mumewe…
‘Njoo hapa maana wewe unadhima kubwa leo,…kuhakikisha mwanangu
anapoteza mawazo yote ya kwenye vita, awe furaha zaidi ya ile ya fungate…’watu
wakashangilia
‘Eeeh, mnielewe neongea kiutu uzima hapa..sio lugha za sasa hivi
za kukera….au sio ..vinginevyo..eeh’akacheka akigeuka kumuangalia baba wa
mkwewe.
‘Najua baba yako yupo hapo, simuogopi mimi, tumekuwa hivi, ngumi
ngumi utotoni, hadi leo tunapambana kwenye uwanja wa siasa,..lakini ukweli ni
ukweli tu....lazima watoto wetu walelewe kwenye maadili mema, ikibidi nguvu
..haya,…japokuwa siku hizi hizi weeeh, …’akasema na watu wakacheka.
‘Unajua mimi na mwenzangu pale tulikuwa kama simba na yanga…hata
hivyo mwisho wa siku tunakula na kucheka, ndivyo maisha yalivyo, ni ajabu watu
mnakuwa madui kwenye ushabiki hadi kwenye misha ya kila siku , huo ni
ulimbukeni,…malizeni ushabiki , mnarudi mnanunuliana zawadi mshindi kashinda
mpe haki yake,,..sasa mama mkwe ni hivi, kiutaratibu wetu, wewe unakwenda kwa
mumeo unamshika mkono, msogee pamoja pale mbele, hicho ni kimila chetu....halafu
kwa unyenyekevu unamkaribisha mumeo nyumbani, …ukimaliza hapo, yeye, ataomba
kibali kwangu, ili aongee..jamani si ndio hivyo…eeh, sisi tunawaheshimu sana
wanawake,..wanawake mbele..’akasema na akina mama wakaitikia mbelee, na
vigelegele..
‘Bila wanawake sisi sio kitu, mwanamke ni shujaa, anajua
kuihudumia familia yake, watoto na mumewe, anamfanya mwanaume aitwe mwanaume,
bila mke mwanaume sio mwanaume, au sio..wanawake mbeleeee…’ akasema na wanawake
wakashangilia na kucheka, kukachangamka kweli, vigelegele na wakati huo mke mtu
akawa anafanya kama alivyoagizwa. na
kabla hajaendelea zaidi mtoto akawa analia..kilio kikubwa,..
Mtoto wao…. Mke mtu akageukia kule kilio kinapotoka, mumewe hali
kadhalika,….
‘Mlete huyo mtoto huku mbele anataka kumuona baba yake…’akasema
baba mkwe, na Yaya akawa anakuja na yule mtoto kuelekea pale waliposimama
Soldier na mkewe,…
Na wakati huo huo… na kule mlangoni akawa anaingia yule
dereva,..Soldier akamuona, na kugeuza kichwa kuelekea kule mlangoni, kitendo
hicho kiliwafanya hata watu wengi wageukie kule mlangoni…
NB: Jamani simu haitaki niendelee..
WAZO
LA LEO: Mke hapigwi kwa ngumi na fimbo..mke hupigwa kwa upande wa
khanga, ni maneno yenye hekima sana,..nayapenda sana, na nawashangaa wale
wanaopiga wake zao kama watoto wadogo..nasikia kuna wanawake pia wanawapiga
waume zao! Halafu haya hufanyika mbele ya watoto au mbele ya watu wengine. Hayo
ni makosa, tuchunge maadili ya ndoa zetu,..tukumbuke mke ni mzazi mwenzako, ni
ubavu wako, ana heshima zake…unavyomtendea hivyo unawafunza watoto nini hapo,
na wao waje kufanya hivyo hivyo au! Ukumbuke huyo ni mtu mnzima tendo kama hilo
linamtesa..linamnyong’onyesha, unamuumiza mwenzako kisaikolojia,..njia njema,
muite mwenzako chumbani, muongee, mpeane maadili mema, ya hekima, na hata kama
kutakuwa na kusigishana, ikabidi,..maana binadamu wote sio sawa,muyamalize huko
huko chumbani.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment