Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, February 13, 2017

FUPA LILILOMSHINDA FISI 3



 Mzee Masikini akiwa kajichokea, uzee wa kuchoka kuliko umri wake, ila watu wamezoa kumuita jina hilo mzee tokea ujanani, kwasababu alianza kuota mvi mapema, na watani wake wakaongezea neno `masikini'

 `Mzee masikini…’ likalolea, hadi leo anaitwa hivyo!

 Mzee Masikini alikuwa kaamuka mapema tu, shambani hakuendeki,...utalima nini,...akwa sasa anaikagua mifigo yake ambayo ilikuwa ikilia, na kilio hicho ni cha njaa….akageukia eneo la shambani, ardhi ilikuwa kame, hakuna hata jani moja lilobakia, jua linawaka kama moto wa nyikani,…akatikisa kichwa, kuashiria kusikitika, akaangalia juu kama vile anatoa shitaka lake kwa mola wake.

‘Mwaka huu…’akasema

Alitembea hatua za pole pole, mwili ulikuwa ukimuuma kila mahali, alihisi kama anaumwa, lakini haumwi, alijua kabiosa haumwi, yeye ni mpingo, maradhi hayamfuatilii sana, alijua kabisa ni mwili tu unalalamika, mwili umekosa haki yake, kwa hatua za kujongea,…akasogea hadi kwenye mti , ili angalau apate kivuli cha mti uliojaliwa kubakiwa na majani machache.

Mzee, alipiga miayo, miayo ya njaa,…akatizama jikoni, mkewe alikuwa hayupo, alidamkia kwenda kisimani kutafuta maji…maji imekuwa ni shida…akatikisa kichwa, akawaza afanye nini, akafkiria kuingia jikoni apike chai…lakini sukari hakuna,..pesa hakuna.

Akaanza kuwaza, …maisha, maisha…hali ngumu,….mpaka lini..ina maana nitakufa na umasikini wangu…!

Akageuza mawazo yake upande wa pili na kukumbuka lile tangazo la mpiga mbiu…hakulichukulia maanani sana, kilichomjia akilini zaidi ni hizo taarifa zilizokuja baadaye kupitia kwa viongozi wa kaya, kuwa wananchi wanatakiwa kutoa taarifa …na wakitoa taarifa kuna donge nono…

‘Donge nono….’akayatamka hayo maneno kwa nguvu, na kujilamba mdomoni.

‘Wananchi mnatakiwa kutoa taarifa kama kuna mtu mnayemfahamu, au kumhisia  kuhusika na na hali hii inayowaumiza vijana wetu na hata kusababisha njaa, hali ngumu, na….kama mtu anayo taarifa atoe, na atapewa zawadi kubwa kutoka kwa mkuu wa nchi….donge nono’

‘Zawadi gani hiyo, donge nono….ni donge gani hilo..?’ akajiuliza, lakini ajuavyo mkuu wa nchi akisema zawadi , huwa hatanii, inakuwa ni zawadi kweli, hata hivyo yeye hakuijali sana hiyo zawadi…, alichojali ni hatima wa vijana wa taifa,  kuna vijana wake pia ambao….wamekuwa ni wahanga wa kuharibiwa viwili wili, hawajiwezi, ..wamelegea kama mlenda, na mmoja kapotelea ughaibuni, inasadikiwa amenyongwa, kwa vile alikuwa anafanya biashara ya ‘malegeza..’

 ‘Malegeza…’ akatamka maneno hayo akitikisa kichwa.

‘Sasa kwanini nisiwajibike…’akasema kimoyo moyo.

Akawazia maisha yake …na uhatari wa jambo lenyewe..kwani huko nyuma wengi walipotea hivi hivi tu, kisa wamewataja wanaokisiwa kuwa wanafanya shughuli hizo,…za uchawi na madawa ya kulegeza viungo, na ……hapo hakumalizia.

‘Na huyu mdudu mtu ni nani….mbona wanatuchanganya hawa watu…mdudu mtu….anachukua jasho letu, pesa zetu pato letu, anawaharibu vijana wetu mauongo yao, wanalegea lakini kwa vipi…je hali ngumu, na huu uchawi vinausiano kweli au ni lengo la kuwachanganya wanachi...’akajiuliza

‘Ni watu hatari…wanakujua hata ukiwafikiria…’alisikia jamaa yake akisema;

‘Mhh…siogopi kufa tena, kwani nikifa au nikibakia hivi kuna tofauti gani… hapa kijijini  mimi ndiye ninayesifika kwa kuchapa kazi,..lakini ninapata nini…shambani kukavu, hakuna mazao, mifugo ndio hii, itakufa hivii hivi…hasara juu y ahasara,..utamuuzia nani…?’akawa anajiuliza

‘Hii kazi nyingine ya kupiga picha haina faida tena, watu hawana pesa,…’akajisema akiangalia kamera yake aliyoitundika mlangoni,

‘Aaah,..lazima nifanye jambo, lazima….kabla sijaadhirika,…lakini jambo gani..?’ akajiuliza.

Mara akaona gari la muheshimiwa likipita kwa kasi, na kutimua vumbi,..lile vumbi lilimfuata hadi alipokuwa amekaa, akaanza kukohoa, akakunja uso, akiliangalia lile gari likizidi kwenda mbali, akatikisa kichwa;

‘Mkuu….’akasema kwa sauti, na mara akakukumbuka jambo…

***********

 ‘Mkuu….’akakumbuka jambo, jambo alilokuwa akiliwazia usiku kucha, akakumbuka lile tukio…
 Ilikuwa siku moja akiwa katika kazi zake za kupiga picha, katika mitaa ya kati, wakati anapita kutafuta wateja, mara akaliona gari , gari ambalo analifahamu ni la nani, ..akalitizama kwa macho ya kuwazia, na yeye siku moja awe ndani ya hilo gari.

Aliliangalia lile gari kwa muda, na tamaa ya kulipiga picha ikamjia, na kabla hajafanya hivyo mara wakateremka vijana wawili kutoka kwenye lile gari,wakiwa na mkoba mweusi ,…na muda ule likaja gari jingine, la kifahari..

Gari la tajiri wa jiji, tajiri anayesifika sana…ana miradi mingi,  kawekeza kwenye mashamba, ana viwanda,…na sasa kaanzisha nyumba zake za ibada, anatoa misaada kwa watu, …kajenga mashule, aligombea ujimbo, lakini bahati mbaya hakushinda, sijui kwanini watu hawakumpa kura, nasikia,….hawamuamini..lakini bado anawasaidia watu.

Kwa udadsi wake mpiga picha, akaona apate picha za kuuza kwa watu wa magazeti, maana tajiri mkuu, haishi kuandikwa magazetini, kwa sifa za kila namna,..wengine wanasema hata akienda chooni, ataandikwa, ilimradi tu …ni mtu mashuhuri..

Mpiga picha akaiweka kamera yake vizuri, na kuanza kupiga picha tukio lile..alipiga tu kwa kujifurahisha..na labda hizo picha anaweza kuziuza, ndio biashara iliyobakia, akalengesha kamera yake vyema…. Mara akaona kitu cha ajabu…!

Kumbukumbu zilizidi kumrejea mzee,..kumbukumbu za tukio lile, akakumbuka alivyoona kwenye runinga wanavyofanya,…mhh….ni vile vile, sasa kwanini wasingelikutana hotelini au….alijiuliza siku ile na siku ile hakuichukulia maanani sana, aliona ni mambo ya watu yasiyomfaa…, hakujua ni nini athari yake, leo hii kaiona…kaiona ndani ya familia yake mwenyewe…inauma, …

‘Ni lazima ndio hizo…, ni lazima ndio wao…mdudu mtu!’akasema

‘Haiwezekani,…’nafsi haikukubaliana na hilo

 Haraka haraka akatoka kwenye ule mti na kuelekea ndani, akaingia chumbani kwake, na kuinama mvunguni mwa kitanda. Akalivuta begi ambalo huhifadhi kumbukumbu zake muhimu, akaliinua na kuliweka kitandani,…akaanza kutoa picha mbali mbalimbali..halafu akaziona zile picha.

‘Huu hapa ni ushahidi kamili…sasa nangoja nini..’akasema akiziangalia zile picha.

Akumbuka siku alipozisafisha hizo picha, na kurudi nazo nyumbani aliwahi kumuonyesha mkewe na kumuelekezea kuhusu lile tukio,  na mkewe alimuonya, na kumuhimiza azichane zile picha, …asizipeleke kwa wachapishaji magazeti maana zitamletea matatizo,..lakini  hakuzichana,  akazihifadhi tu....ni siku nyingi, lakini mpaka leo analikumbuka hilo tukio.

‘Donge nono…’akayasema yale maneno, akawaza na kuwazia, baadaye akasema kwa sauti ndogo…

‘Lakini ni nani ataniami….’akasema akiwa kashika shavu

Mara akachukua kakijitabu kake kadogo ambako anakutumia kuandika mambo fulani fulani aliyowahi kuyaona, anapenda kuandika, na kama angelipata mfadhili, angeshakuwa mtunzoi mashuhuru duniani, …lakini vipi…akawa anapekua kurasa za kile kijitabu,  akarudi hadi tarehe ya siku ile, ….aliandika kila kitu

‘Mhh..huu ni ushahidi, lakini ni nani ataniamini…’akajisemea tena, akakirudisha kile kijitabu, lakini kabla hajafunga lile begi lake, akajiwa na wazo,..

‘Kwanini nisijaribu,…nitakosa nini, kwanini….hapana, lazima nifanye jambo.

Kwa haraka akazichukua zile picha na kile kijitabu, na kuanza kutoka nje, hakumuaga hata mkewe, moja kwa moja hadi ofisi ya mkuu maalumu wa usalama….

Mhh…haya tuone ilikuwaje


WAZO LA LEO: Tukiamua kufanya jambo la haki tuiangalie na haki itendwavyo, na hasa pale tunapojua kuwa hiyo haki inataka uhakika, wa ushahid…tusijekupania jambo, likaja kuiharibu haki na ushahidi wake ukapotea bure na mwisho wa siku ikaonekana hiyo haki ni porojo tu! Na porojo hizo zikageuzwa kuwa silaha ya kuiharibu haki . Japokuwa haki itaendelea kuwa haki , na ukweli wake hauwezi kufutika daima.
Ni mimi: emu-three

No comments :