Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, January 18, 2017

Sikuomba iwe hivyo



 Ni siku ya naikumbuka sana, ni siku ambayo niliteguka nyonga, si unajua tena hii shida yetu ya usafiri, na ilitokea usiku wakati narudi kazini. Usiku sikulala, nilitamani kupambazuke haraka niwahi hospitali. Lakini tatizo la ofisi yetu ili utibiwe ni mpaka upate sick sheet, na ni lazima ufike kwanza ofisini uandike kuwa umefika, usipofanya hivyo siku hiyo inakatwa, na unakatwa kwenye mshahara.

Basi kulipopambuka tu, saa kumi nikadamka, hata kutembea shida, nanyata kama kinyonga, taratibu nikawahi kituo cha reli, maana nilijua nikipanda dala dala nitaumia zaidi, japokuwa mbeleni nitahitajika kupanda hiyo daladala, uwezo wa taxi au bajaji upo wapi!

Uzuri wa treni hainaga foleni nikafika Buguruni saa kumi na mbili, kuna mwendo wa kutembea kutoka Tazara hadi buguruni sokoni , nilijikongoja hivyo hivyo, hadi nikafika kituoni,..Nilipofika hapo kituoni, niligwaya kwani umati wa watu waliokuwepo hapo…, utafikiri magari yamegoma. Nami natakiwa kwenda ofisi moja ipo kwenye jengo moja lipo njia panda ya kwenda Kawe.

Magari ya Kawe buguruni au Kawe masaki ni kama enzi zile za magari ya kwenda mbagala, ni magari ya kugombea, watu wanarukia kwenye madirisha, ukizubaa huwezi kupanda. Na mimi siwezi hata kusimama kwa muda mrefu.

‘Jamaa yangu nakuomba unisaidie naumwa,…ugombee upate siti ili unipatie nikae…?’ nikamwambia jamaa mmoja aliyekuwa akielekea njia hiyo.

‘Mimi mwenyewe sijui kama nitapata gari, hapa nilipo najisikia vibaya…’jamaa akaniambia hivyo.
Kukuru kakara ikaja gari, ikasimama pale pale nilipokuwa nimekaa, haraka nikajitahidi nikadondokea mlangoni, watu hawakujali, wakaniparamia na kuanza kunikanyaga, hakuna aliyejali, hata nilipoweza kusimama, nilikuwa nimechafuliwa nguo. Sikujali, nikasimama na kuingia ndani ya gari.

Uzuri kondakita alikuwa kakaa kwenye kiti karibu na mlangoni, akanipisha nami nikaweza kukaka kwenye kiti! Hapo nilikuwa na maumivu makali sana, ..nijiuma meno….gari likaanza kuondoka, kwa mbele ulikuwa ni mnyororo, foleni, gari halitembei. Mpaka tunafika Karume njia panda, dakika arubaini na tano zimepita,..hapo natamani hata kulia,ni maumivu makali sana!

Nikamuomba mungu, angalau nipate usingizi, na duwa zangu zikakubaliwa, nilipitiwa na kausingizi na nilipoamuka nikakuta tupo njia panda ya magomeni, kumbe tulitumia saa moja kwenye hiyo foleni, ..hadi tunafika Moroco, ni masaa mawili na nusu yamepita. Sasa kutoka hapo Moroco kuelekea huko Kawe, hapo ilikuwa kazi, mpaka abiria wanadondoka na kuzimia, trafiki hana habari na upande wetu.

Tukaondoka hapo saa jingine limepita,..tukafika sehemu wanaita kwa Warioba, hapo kuna historia, bila nusu saa au saa nzima hamuwezi kuruhusiwa kupita,..hapo abiria wengine waliamua kushuka na kutembea kwa miguu, na wale wenye uwezo wakachukua pikipiki. Sijui kuna nini sehemu hiyo!

Nilifika ofisini saa tatu na nusu, na daftari la mahudhuria limeshachukuliwa, sikujali, mimi umuhimu ni sick sheet tu..Bosi aliposikia ninaumwa, akanijia na kuanza kunibwatukia;

‘Wewe kila siku inaumwa,..veye hutaki kazi,..sasa nenda tibiwa na baki huko huko mpaka ponaeeh, ..’akasema bosi huyo.

‘Sawa bosi lakini sikuomba iwe hivi…’nikalamika.

‘Itajua mwenyewe….’akasema kwa dharau. Na kauli yake ni moja,..ningefanya nini,..nikaondoka hapo ofisini nikiwa na mawazo mengi, nitaishije. Basi nikajikongoja hadi kwenye kituo cha dala dala..nilichokikumbuka ni kuwa nilikuwa nasimama, kwani nilikaa kwenye gogo lilikuwa limewekwa hapo kituoni.

Wakati nasimama, nikahisi maumivu makali sana,…lakini nikajitahidi hivyo hivyo….nikainua mguu , hautaki, nikajitahidi, nikaweza, nikavuta hadi mlango mwa gari, unajua tena magari ya dala dala hayana kuremba,..sijainua mguu likaanza kuondoka, nilihisi nikirushwa na kudondoka chini, na kichwa kilikoswa koswa na gurudumu, na giza likatanda usoni.


Nilizindukana na kujikuta nipo hospitalini na bandeji kichwani…

Ni mimi: emu-three

No comments :