‘Chukua chakula na uenda kwenye nyumba ya ibada utamkuta mja
wangu anafanya ibada,mja wangu huyo ana njaa, kampe hicho chakula..’ ilikuwa
maagizo kwenye ndoto kwa mchamungu mmoja. Mchamungu huyo alikuwa akiota ndoto
zake hutokea kuwa ni kweli, na hufanya kwa jinsi alivyoagizwa.
Basi mchamungu huyo alikwenda hadi kwenye hiyo nyumba ya
ibada na kweli akamkuta mja wa mungu akifanya ibada, alisubiri pale mpaka yule mtu
alipomaliza ibada yake ndio akampa hicho chakula na yule mja wa mungu
akashukuru na kumshukuru mola wake, na kuendelea kufanya ibada.
Mchamungu huyu huyu akamuambia yule mja mwema,` ndugu yangu
mja mwema.., ukiwa na shida , ukiwa na njaa karibu nyumbani kwangu, upate
chakula…’ akamuelekeza hivyo, akizidi kumuelekeza nyumbani kwake ni wapi.
‘Mimi siwezi kuja kwako, kwani wewe sio mtoa riziki, mimi
namtegemea, na kumuomba yule aliyekujalia wewe kuipata hiyo riziki na yeye
ndiye anajua na kufahamu fungu langu ni lipi…’ mchu mungu huyu akaelewa na
kugeuka kuondoka zake, hakuwa na la kusema.
*******
Hawa ni wacha mungu wa kweli, waliojaa imani thabiti…wanafikia
kuota ndoto na inakuwa ni kweli, na wanatekeleza hayo maagizo, lakini pia kuna waja
wema wa kweli…wanatii na kumnyenyekea mola wao..na kutumiza yale waliyoagizwa
na mole wao, wana imani thabiti, wanakuwa na shida, lkn bado hawasumbuki kumuomba
mtu au kumtegemea mtu, au kulalamika kwa mtu, wanajua ukweli kuwa riziki yao
wataipata tu
Wapo watu sasa hivi wanafikia kuwatukuza matajiri,
waajiri..utafikiri hao watu ni miungu wadogo.. hawajui kuwa utajiri huo kwa hao
watu umetoka kwa yule yule mola wa wote…
Lakini leo hii ni tarehe tatu ya mwezi..kuna wafanyakazi
hawajapata mishara! Hebu jiulizeni, hawa watu watakula wapi, wataishije… Sawa
huenda kuna waajiri wengine wamefanya hivyo kwa sababu za msingi, ya kuwa labda
hawana pesa, au kuna matatizo ya kibenki, basi wawaambie wafanyakazi wao, na
ikiwezekana wasema hivyo mapema iwezekanavyo kwa wafanyakazi wao, ili hao
wafanyakazi wajua jinsi ya kujipanga…. lakini wengine wanachelewesha makusudi
kwa visingizio mbali mbali, hawajli.. na
ni roho mbaya tu, kuwatesa wafanyakazi wao.
Tukumbuke kuwa, kiimani na ucha mungu…waajiri wameamurishwa
kuwa wawalipe wafanyakazi wao ujira wao kabla jasho la wafanyakazi hao
halijakauka… “Mpeni muajiriwa ujira wake kabla jasho halijakauka”. Kuna hekima
ndani yake kwa wenye kuelewa… , hatujui umri wa mwanadamu, je kama ikatokea
huyu mfanyakazi akafariki, na wakati
alikuwa na haki ya kula jasho la mshahara wake…wewe umemuhini, kwa kuchelewesha
kumlipa stahiki yake…wewe utakuja kusema nini mbele ya mungu au utasema
ilipangwa iwe hivyo,…
Lakini pia kuna mipangilio ya mtu, kila mtu ana bajeti yake
ya mwezi, wengine wamekopa, wengine wanataka kulipa ada za watoto wao,
walishaahidi kwa walimu..wengine wana madeni, wengine wanauguliwa, wanataka
kujitibia au kutibia …wewe umezuia na kumfanya huyu mfanyakazi ataabike, au
umefanya mtu huyu asiaminike tena huko
alipoahidi…, au akose huduma fulani, utakuja kusema nini mbele ya mungu. Au
hatuna imani sahihi ya mwenyezimungu?
Nawaombeni nyie mnaomiliki wafanyakazi kwenye nyanja mbali
mbali, tujitahidi kila ikifikia muda wa mtu kulipwa ujira wake tuwalipe watu
hao ujira wao,..hilo ni jasho lao,..mshahara wenyewe mnawapunja, na bado
mnauchelewesha ujira wao…kihekima tukiwalipa hicho kidogo tulichowapangaia
kuwalipa, tunajenga mahusiano mema kati ya mwajiri na muajiriwa…, na pia tunajiongezea
Baraka, juhudi za kazi nk…Baraka nyingine hujengwa kwa kutimiza hizo haki za
msingi...watu hawalalamiki!
Tumuombe mwenyezi mungu atusaidie tuweze kukumbuka jambo hili
la msingi, na tumuombe atusaidie tusiweze kujisahau kwani wakati mwingine kwa
madhaifu yetu ya kibinadamu tunafanya hivyo tukitarajia kuzungusha zaidi …
Tunakuomba ewe mola wetu utupe riziki za halali, kutokana na
jasho letu,na wala tusighilibike kwa kutafuta riziki zisiso za halali…Yote ni kwa mapenzi yako na wala sio kwa
ujanja wetu…Aaamin!
Ni mimi:
emu-three
1 comment :
MBONA UPO ADIMU
Post a Comment