Docta alikuwa amekaa
kwenye sofa akiwa na mkewe, nyuso zao zilitawaliwa na furaha,..hata mimi moyoni
nijisikia furaha,…kwanza docta akambusu mkewe shavuni halafu akasimama na
kunujia, akanikumbatia kwa nguvu,..huku akinishukuru sana, halafu akasema;
‘Mkuu, hata sijui
nisemeje..ngoja nirudi ….’akasema
‘Una safari,…..au
ndio hiyo ya…..’nikasema na yeye akanikatisha na kusema;
‘Kabla sijaondoka,..hatujaondoka
….’akamgeukia mkewe.
‘Mimi ninajua nina
deni kubwa kwako…hili sio mimi,…’akatikisa kichwa na akakunja uso kama anawaza
kitu, halafu akaniangalia na kusema;
‘Haya ni maagizo niliyopewa
na niliambiwa nifanye kama ifuatavyo…, na ndivyo hivyo nilivyokuambia na-, na eeh,…., kwa jinsi nilivyoagizwa, mimi, imebakia hilo agizo moja,..baada ya hilo, hayo mengine
sijui, kama kuna watu ulikuwa hujawafikia, ukawaomba msamaha, hilo ni juu yako, ..ni hili ni agizo , mimi natimiza wajibu wangu tu..…’akasema
‘Mhh, docta,
sijakuelewa, ni agizo ..kutoka kwa nani…?’ nikamuuliza nikiwa na mashaka, maana
nakumbuka mtu wangu wa imani aliniambia maneno kama hayo, kuwa nifanye mambo
kadhaa ili nifanikiwe kwenye matatizo yangu, sasa isije ikawa ndio huyo huyo....
‘Hahaha, eti kutoka
kwa nani…unajua mkuu.., hebu kaa kwanza,....utulie…’akasema akiniashiria nikae maana nilikuwa
bado nimesimama, nikiwa na hamsa fulani, nilitaka kuyafahamu hayo maagizo
ambayo yalisubiriwa mpaka nitimize hilo la kwenda kumshawishi mkewe arudi
nyumbani,
Mimi nikasogea kwenye sofa, nikakaa..na kutulia,... kukawa na ukimia fulani halafu
docta akasema;
‘Tuna muda kidogo……’akasema docta akiangalia saa yake, halafu akamgeukia mkewe, halafu mimi,... na mimi nikasema;
‘Mhh…unajua docta mimi nimekuwa nikisoma shajara ya mke
wangu, na mengi aliyokuwa ameyaandika, nikijaribu kuyafuatilia, nafanikiwa, au kupata jambo fulani, sasa uliponiagiza niende kumfuata mkeo, nilijaribu kutafuta kwenye shajara hiyo kama kuna agizo kama hilo,mhh sijaona,..
'Sasa, kuna kitu nilikuwa nakisoma kabla sijafika hapa, aliandika hivi,…. ‘….nimemuacha mume wangu
nikiwa na huzuni, …sikuweza kutimiza kile alichokitaka, hili kwangu naliona kama deni,..sijui ni nani wa kunisaidia kulilipa,… lakini ninaomba ,..’
‘Mmh, hapo
nakumbuka aliandika… ‘ namuomba mungu,
kama inawezekana hicho anachokitaka ...kipitie kwa wapendwa wangu…..` hicho
anachokitaka …’ nahisi ninachokitaka mimi au sio, mhh, ninachokitaka mimi, hapo nimeelewa, najuata kwa hilo, maana hilo lime..oh, nisamehe sana mke wangu, sijui huko ananisikia, sijui, mungu wangu ndiye unayelijua hilo, hata sijui…?’nikawa naelezea huku
nikijaribu kukumbuka ilivyokuwa imeandikwa…
Docta akawa
anatikisa kichwa kama kukubaliana na mimi..hata sikuelewa anakubaliana na mimi
kuhusu nini hasa, hiyo kauli yangu au hayo niliyoyanukuu kutoka kwa shajara ya
mke wangu….mimi nikaendelea kusema;
‘Na, …na, najiuliza sana, hivi, mmh, hao
wapendwa wake ni akina nani hasa, na wewe, ni nani,...hata sijui….’nikamalizia hivyo na docta akatabasamu na
akaendelea kutikisa kichwa halafu akasema;
‘Umeoanaee, mkeo
alishayaona maisha yako ya kabla , kutokana na ibada ya mkeo ya muda mrefu,yeye
alijawa na hisia za mbeleni, wengine wanaita ...maono…au sio,..kutokana na kumuomba mungu
kwake…alishaweza kuonyeshwa mambo ya mbeleni…, na ndio maana siku ile
alipozidiwa, ilibidi aniambie tu, kwa mdomo, maana hiyo diary yake hakuwa nayo
siku hiyo.
‘Alisemaje…?’
nikauliza nikiwa na hamasa kuyasikia hayo aliyoongea mke wangu, japokuwa
nilikuwa na hamasa zaidi ya kujua hicho alichoniitia docta,
Docta alitulia, akabadili sura ya kuwa na huzuni na ndipo akaanz kuelekezea siku hiyo, ilivyokuwa;
*******
‘Docta najua mimi
sitapona, …naiona saa yangu ya mwisho….nateseka sana docta, maumivu
ninayoyahisi sasa..hata baada ya dawa ya maumivu lakini..ooh’ akawa anagugumia
kwa maumivu…’akasema docta akiijaribu kuigiza sauti ya mke wangu.
‘Docta , ..namuomba
mungu anaichukue roho yangu haraka…, ila kwa sasa nakuomba jambo moja, najua
mengi nimekuwa nikiyaandika kwenye `diary ’ imekuwa hulka yangu hivyo,…nina
imani mume wangu atakuja kuiona hiyo shajara, na kuyasoma yote,….kama hatayaona naomba uje
umuelekeze atafute hiyo diary, ipo kwenye kabati langu ataiona tu….’docta
akatulia.
Akaendelea kusema
docta, ….`muda huo mkeo anaongea kwa shida, …na ukumbuke muda ule hakuwa na hiyo shajara yake, yupo chumba cha wagonjwa mahututi, yupo mimi na yeye tu... mkeo
anapenda sana kuandika mambo yake kwenye `diary’…hata
mimi ilikuwa hivyo zamani, lakini nikaja kuacha,…’akasema docta, halafu
akatulia kama anawaza jambo, na mimi nikasema;
‘Docta mimi naomba
uniambie hayo maagizo,….’nikasema nikikwepa kutoa machozi maana niliona kama
ananikumbushia mambo yenye kunizidishia huzuni.
‘Nitakuambia ….maana
ni muhimu,..ila nilitaka kuanzia hapo, …’akasema docta na kutulia,..hii hali ya
kuongea na kutulia ilikuwa ikinitesa, nilitaka aongee kwa haraka haraka, lakini…
‘Sasa, unajua docta
…mmh, sijui kwanini,…. kwahiyo unataka kusema yeye, ndiye alikuambia ufanye
hivyo kabla hajafariki....sijaona lakini..kwenye shajara...hajaandika hivyo...'nikasema.
'Hajaandika kuhusu nini...?' akaniuliza
' Kuwa unitume mimi nikaonane na mke wako, halafu,…sasa, hebu unifafanulie hapo, maana mimi sijakuelewa..?’ nikamuuliza
‘Naweza kusema hivyo `ndii-ooh’…' akasema na kutabasamu
'Japokuwa hakuwa na maelezo
hayo ya moja kwa moja, lakini hata mimi nilikuja kuliona hilo kuwa kwa kupitia
wewe, hili swala langu lingelifanikiwa, maana kisa cha tatizo ni nani, ni wewe
au sio…?’ akaniuliza na kuniangalia na mimi nikaguna tu.
'Mhh...'
‘Na…wewe ulishaamua
kujitakasa,…na hilo ni moja ya mambo ulitakiwa uyafanye…au sio…uende kwa mke wangu ukutane naye…umuombe msamaha au sio, umuelekezee ukweli wote, au sio…. na
najua mungu ameshaanza kukisikia kilio chako, maombi yako..,siumeona eeh, nashukuru sana maana sasa nipo na mke
wangu….’akasema akum-mpambaja mkewe.
‘Hata mimi nimefurahi
sana kwa kweli….sikutarajia kuwa shemeji engelifika…nilimuomba sana mungu afike….usiku
sikulala, nilikesha nikiomba…’nikasema nikiwaangalia kwa macho ya wivu
‘Unajua kiukweli,
wewe sasa umefanikiwa, kiukweli wewe sasa hivi moyo wako umeshasafishika,…sasa
kila utakachoomba mungu atakutimizia kwa mapenzi yake lakini,…lakini kuna
jambo, …’akatulia akiangalia saa, nilijua anaogopa kuwa atachelewa na mimi
nikaliona hilo, kwahiyo nikasema;
‘Shemeji…’nikasema
nikimgeukia mke wa docta
‘Namu shemeji….’akaniitikia,
‘Mhh…hata
sijui…..lakini nakumbuka wakati tunaondoka mzee wako alituagiza nini, mimi na
wewe mguu kwa mguu, tumchukua huyu jamaa,…. sasa siku ya ngapi leo, mzee
atakuwa kwenye hali gani jamani, au kuna taarifa gani kutoka huko, maana
ubinafsi umetutawala zaidi…?’ nikasema na kuuliza.
‘Shemeji nakumbuka
sana hilo,..ndio maana tukakuita uje kwa haraka, maana sisi hapa tupo safarini,…na
kifupi tu, baba hajambo,…na hahaha..unajua haya mambo unaweza ukacheka, lakini
hucheki kwa raha,..unajua baba kabadilika kabisa,sio yule baba ninayemfahamu
mimi,..eti, keshatoka hospitalini na kuanza
ile kazi uliyokuwa ukiifanya wewe…’akasema
‘Kazi gani hiyo
niliyokuwa nikiifanya mimi,… acha mzaha, mimi kazi zangu za nguvu, na mzee
wako, hastahiki kuzifanya hizo kazi, au…, ni kazi gani….?’ Nikauuliza
‘Kazi ya
toba……’akasema na mimi nikatabasamu, na kusema;
‘Oh, hahaha, TOBA,
mhh, nahisi hiyo itakuwa `toba ya kweli ‘…..nimefurahi sana kusikia hivyo,
kumbe sipo peke yangu….’nikasema.
Docta akaingilia
kati na kusema;
‘Sasa kabla sisi
hatujaondoka,..nataka kutimiza ile ahadi yangu kwako…, na najua hutaniangusha
kwa hilo…kwani, …eeh, kama nilivyoambiwa,… hiyo ndio itakuwa kazi yako ya
mwisho, baada ya hapo….mmh, mungu mwenyewe anajua, nikirudi tu, nitakuhitajia
hospitali, tufanye check up….’akasema
docta.
‘Sawa, mimi hilo
sina shaka nalo, siumwi, sasa hivi najihisi mzima, yale matatizo, ile hali,
lakini bado,…nina tatizo, mmh, lakini yote namuachia mungu,…’nikasema
‘Ni kweli….najua
unataka kusema nini…’akasema docta
‘Haya..kama mnasema
mzee hajambo, basi mimi nipo tayari kukaa kusikiliza kuwasikiliza kama
sitawachelewesha mnaondoka na usafiri wenu au kwa njia ya basi….’nikauliza
‘Usafiri wetu ,
ndio maana sina shaka….’akasema
‘Maana …mimi si nipo, mkirudi tutaongea au…?’ nikasema japokuwa moyoni nilitaka niambiwe
haraka hicho alichotaka kuniambia.
‘Hilo haliwezi
kusubiria kwa sasa, inabidi nikuambia ili nikirudi nikute matokeo,…kiukweli hilo
lina haraka ...na ni muhimu sana kwako,sikutakiwa
nicheleweshe hivi, lakini pia ilitakiwa lifanyike , eeh….baada ya hili zoezi
kukamilika, niliambiwa hivyo..na nashukuru kuwa kila kitu kinakwenda sawa….,
sasa iliyobakia ni sehemu ya mwisho tu, ambayo, usipoitekeleza, basi….’akatulia
‘Mhh,
kwanini…..sijaelewa, ni nani alisema hivyo, …?’ nikauliza
‘Ni huyo
aliyeniagiza nikuambie, ..na haya yeye, alisema hivyo, `…usipolitekeleza hilo…,
basi’ hakunimalizia,….sasa sijui hiyo ` basi…’ ilikuwa na maana gani…’akasema
docta
‘Mhh, ina maana
hayo aliyasema mke wangu au kuna mtu mwingine zaidi yake...?’ nikauliza.
Docta akatikisa
kichwa, huku akitabasamu, halafu akabadili taswira ya sura yake, nakuonekana
anazama kwenye huzuni, kumbukumbu ilimtawala zaidi. Kwa kipindi hiki kifupi niliona jinsi gani
docta alivyoasirika, baada ya mke wangu kufariki, haikuweza kufichika machoni
mwake.
‘Kama nilivyosema,
mke wako alishakuwa mtu mwingine,..japokuwa hakuweza kuyazuia mauti, maana
umauti hauzuiliki, muda ukifika umefika,..na nahisi ndio maana alipotamka kuwa
anaomba kifo kimjie haraka, mungu hakumchelewesha…’akasema docta
‘Sawa…naona huko upaache,
niambie docta,..hilo unalotaka kuniambia…’nikasema
‘Hayo,…ya kwenda
huko, kufanya hili na lile, niliyokuagiza mimi, ndio aliyasema mkeo…., marehemu
mkeo…,’ akigeuka kumwangalia mke wake,
akapitisha mkono wake nyuma mgongoni kwa mkewe, na mkewe akajiegemeza begani
kwake hadi raha…nikawaonea wivu.
‘Sasa sikiliza maagizo
haya kwa makini ….’akasema docta akiangalia saa yake.
NB: Mhh..mbona
maneno yanazidi kuwa mengi…nashindwa kumalizia hapa, basi tuishie hapa kwa leo,
sehemu iliyobakia sio ndefu saana, …ngoja niwape muda wa kupumua,na kujiandaa
na ijumaa. Ijumaa kareemu
WAZO LA LEO: Kumbukumbu ni muhimu
sana katika misha yetu, kumbukumbu ni historia yenye kudumu, na inakuja
kusaidia, au kuwasaidia wengine baadaye. Kuna wengi hawalijali hili, lakini
lina umuhimu wake. Na tujenge tabia ya
kuweka kumbukumbu zenye manufaa, zenye heri, maana kumbukumbu hizo zinageuka
kuwa nyenzo, au rasilimali, kwahiyo zikiwa ni za wema, malipo kwako, wewe
uliyetengeneza kumbukumbu hizo, au yaraka hizo,.. ni makubwa, unapata Baraka na
thawabu, zikiwa kinyume chake, ni madhara pia.
Wapo wengi wetu , wamekuwa
wakiandika tu, tunaona ni kawaida tu..uzushi, fitina , mambo machafu yenye
kuathiri kizazi..nk..tunaona ni kawaida tu... Lakini hala hala mti na macho,
maandishi ni kumbukumbu na ushahidi wa kudumu, ipo siku utasimamishwa na hayo
uliyoyaandika yatatolewa kama ushahidi,…sijui utajiteteaje…
Tumuombe mola atupe
hekima ya kuyapima yale tunayoyaaandika, ili yaje kuwa neema na msaada baadaye,
na atuepushe na kuandika mambo mabaya yenye kuharibu jamiii…..Aamin
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment