Sehemu iliyopita
mnakumbuka nilianza kuisoma ile shajara ya mke wangu, na humo niligundua mambo
mengi, mojawapo nililogundua ni kuhusu mahusiano yake na docta,…japokuwa
nilishaanza kubadilika, hasira zile mbaya mbaya zilishapungua, lakini kwa jinsi
shajara ile ilivyokuwa ikimtaka docta,..nikashindwa kuvumilia, na hapo nikaamua
kwenda kukabiliana na huyo docta, je kulitokea nini…
Tuendelee na kisa
chetu, nikiwa naongea na docta
**************
‘Docta kwanini mlinifanyia
hivyo..?’ nikamuuliza nikiwa nimesimama nikimuangalia kwa hasira…
‘Kwani kuna nini
tena, si tullishamalizana mimi na wewe…tumeshasameheana au sio….’akasema
‘Mke wangu alikuwa
na tatizo kubwa, mkawa mumeligundua wewe na yeye kwanini hukuniambia..?’ nikamuuliza
‘Oh,..oh, ni nani
kakuambia..najua umegundua shajara yake nini…..mmh, najua sana….lakini ni vyema
kuwa umeligundua hilo mwenyewe, kiukweli ni kuwa ni yeye mwenyewe alitaka iwe
hivyo,….mimi ningefanya nini..nilimshauri sana akuhusishe na wewe, lakini
alikataa kata kata…’akasema
‘Kwa vile wewe
ulikuwa ni hawara wake au sio….’nikasema
‘Sikiliza nikuambie
ukweli…..’akasema akiniashiria nikae kwenye sofa, sikupinga nikasogea kwenye
sofa na kumsubiria aniambie ukweli.
Na ndipo
akanihadithia jinsi waivyohangaika yeye na mke wangu kutafuta tiba, na hatimaye
ndio mke wangu akaja na wazo la kubeba mimba ili azae tu, huku akijua kwa
kufanya hivyo kungeliweza kumuharakishia maisha yake….
‘Ni hatari, kwani
mimba ingelimu-maliza mapema,..lakini hakukubali ushauri wangu, …’akasema
‘Kinachoniuma ni kwanini
….hukuniambia huo ukweli..hayo hayo yamepita,…sasa ili tuelewane,…niambie
ukweli,…ulifanyaje kwasababu ulisema kizazi chake kilikuwa kimeharibika…?’ nikamuuliza
‘Mke wako ni rafiki
yangu mkubwa toka hata kabla hujamuoa wewe, ilitakiwa mimi ndiye nimuoe, lakini
ndio ukashinda wewe, …yote hayo ni
mapenzi ya mungu,...na nimekuwa msiri wake mkubwa…na alipolipanga hilo mimi
sikuwa na kipingamizi, lakini tatizo lilikuwa ni jinsi gani ya kuibeba hiyo
mimba , bila ya kukutenda, na bila ya kuisaliti ndoa yake.’akasema
‘Ndio mkapanga
kuzini wewe na mke wangu au sio…sema ukweli tu?’ nikamuuliza nikikunja uso kwa
hasira
‘Mke wako alikuwa
muadilifu sana, pamoja na yote hayo uliyomtendea wewe,…wewe hujui tu, yeye
hakutaka kabisa kukusaliti…lakini alihitajia mtoto kama ulivyomtaka wewe…,
alitaka kabla hajafa akupatie wewe mtoto…hilo lilimtesa sana, na ndio siku moja
akaja na hilo wazo…’akatulia
‘La wewe nay eye
mzini au sio, wewe si kidume mbegu….’nikasema
‘Subiri nikuambie
ukweli… hata yeye hakulipenda hilo…lakini alifanya hivyo kwa vile anakupenda
wewe..alikuwa tayari…, afe kwa ajili yako….’akasema
‘Basi, …mimi nikamshauri
sana,..akasema nifanye lile nitakalo liweza ili tu yeye apate mtoto, na kwa
vile alishaona ..nimewafanyia wengine, akaona kwanini nisimfanyie na yeye…mimi
ni dakitari wa mambo hayo, nikaanza harakati za kukiweka sawa hicho kizazi
chake, upasuaji …nk…,..ni hatari, lakini…kwa uwezo wamungu, kizazi chake kilikuja
kukaa sawa….achilia mbali huo ugonjwa wake!..’akatulia kidogo.
‘Kwahiyo ndio
ilikuwa kazi yako..ujanja ujanja tu..mbona hakupona sasa, mbona hakumpata huyo
mtoto…?’ nikamuuliza nikiwa bado nimekunja uso kwa hasira
‘Wewe hujui
mitihani ninayokumbana nayo kwenye hii fani yangu,..wewe hujui watu
wanavyohangaika pale wanapokosa mtoto, hasa mwanamke…sipendi,lakini wakati
mwingine huruma hunijia, na ….ndio..mengine ni siri yangu…., hayo ninakutana
nayo ni siri yangu,…lakini kwa mke wako yeye ilikuwa tofauti…’akasema
‘Kuzini ni kuzini
tu, hakuna utofauti…’nikasema huku nikitikisa kichwa kuonyesha hisia zangu.
‘Mimi nimekuwa
nikifanya uchunguzi, ..kuona jinsi gani ninaweza kumwekea mwanamke mbegu kwenye
kizazi kilichoharibika….kwa njia ya kupandikiza mbegu…ili aweze
kuzaa..unakumbuka kuna kipindi nilikuambia unipatie mbegu zako za uzazi ili
tukazifanyie uchunguzi,ili tuone kama kuna tatizo…?’ akaniuliza
‘Lakini ile
…..’nikatulia nikikumbuka, ni kweli nilifanya hivyo, kipindi hicho tunahangaika
angalau nipate mtoto, lakini nilijua ni kazi bure. Na nilikuja kukata tama
nikijua huyu docta hawezi kitu.
‘Ndio…ilikuwa ni
namna niliyoitaka nione kama ninaweza kufanikisha uchunguzi wangu, sikukuambia
nilichokuwa nataka kukifanya…niliziweka hizo mbegu kwenye kizazi cha mkeo…na
hata siku ile anakuja kwangu kutaka tutende tendo ili apate uzazi, kwa vile
kwako imeshidikana..nilikuwa nimeshazipandikiza hizo mbegu kwenye uzazi wake..nilikuwa
nasubiria matokeo sikutaka kumwambia…
‘Kwahiyo kumbe ni
kweli,..mlizini..’nikasema nikimkazia macho.
‘Nisikilize
kwanza…..’akasema
‘Docta, docta,
docta…ni nini ulifanya…., kama sio kuzini na mke wangu….’nikasema na hutaamini…siku
hiyo ilikuwa tofauti, pamoja na hasira …lakini haikuwa kama ile hasira yangu ya
awali..nilishabadilika, lakini docta alikuwa akiniangalia kwa mashaka akijua
nimekuja kwa shari.
‘Kiukweli siwezi
kukuambia undani wake nilivyofanya….ila siku ile alikuja kwa vile
nilishamwambia kizazi chake kipo sawa kinaweza kubeba mimba, ila mume wake,
yaani wewe…inaweza mimba isishike, kwahiyo ndio akaja kwangu, … hakulipenda hilo….’akatulia
‘Mke wako alikuonea
sana wewe huruma…na, angelifanya nini na wewe ulikuwa unataka mtoto…,siku ile
mimi nikamuhadaa tu ili ahisi nimefanya
hivyo,na sikutaka kumwambia kuwa tayari nimeshapandikiza mbegi kwenye kizazi
chake.. ,nika….na akajua labda..na hilo nililifanya ..huwezi amini…lakini
sikufanya na yeye tenddo…’akawa hamalizii maneno yake.
‘Niambie ukweli docta,
wewe ulizini na mke wangu, huo ndio ukweli, tunalijua hilo, yeye alikuwa mpenzi wako wa siri, kwanini hukubali
ukweli ukatubu kama …yaishe tu, …?’ nikamuuliza na kusema
‘Sikuzini na mke
wako, niamini hilo….’akasema
‘Kama hukuzini na
yeye, kwanini aliamua kuitoa hiyo mimba…?’ nikamuuliza
‘Mimi nilikuwa kwenye
uchunguzi wangu…bado naendelea hatua kwa
hatua…, na sikutaka hata yeye alifahamu hilo kwanza,…na kwa vile alishafikia
hatua hiyo, nikamvunga kinamna,....sikufanya naye tendo hilo abadani,…’akasema
‘Mimi sikuelewi,
kwa vipi, hahaha, nyie watu …’nikasema nikitikisa kichwa nikawa kama nacheka
kwa dharau.
‘Niamini,…… mke
wako nilikuwa namuheshimu sana, baada ya wewe kuoana na yeye, tuliapa kuwa
urafiki wetu uwe kama wa kaka na dada....ila kwa siku ile hata yeye alijua
nimefanya hivyo, lakini kiukweli sikufanya tendo hilo,..najua ni kitu gani
nilifanya, hiyo ni siri yangu…., ila ninaomba uniamini hivyo…,ukweli ndio huo
sikuwahi kuzini na mkeo….’akasema
‘Hivi unafahamu ni
nini maana ya kuzini…..?’ nikamuuliza
‘Naelewa sana…’akasema
‘Sasa ilikuwaje
hahaha…utafikiri nacheka,…. najua unaniogopa tu…, kiukweli siwezi kukufanya
lolote kwa hivi sasa, sina nguvu hiyo tena…, ila mimi ninachotaka ni ukweli tu,
je ulizini naye sema ukweli, moyo wangu utulie..basi ukiniambia ukweli ….basi
nitafanya nini tena,…je ulizini na mke wangu..?’ nikauliza nikitaka kuujua
ukweli.
‘Mkeo alikupenda
sana..na yote yaliyotokea ni kwa ajili yako…alikuwa akikuhurumia sana, ..ndio
maana , japokuwa alijua kuwa unatembea na wanawake wengine nje…, lakini
hakutaka kukuambia,..alijua yote hayo….kiubinadamu aliumia tu ndani kwa ndani…aliniambia
yote hayo, kuhusu wanawake zako, ukafiki hata kutembea na ndugu zake,..na kila
mara alikuwa akikuombea upate mtoto hata wa nje,..lakini haikutokea…kwasababu
una madhaifu kwenye …..’ hapo hakumalizia akatulia .
‘Unataka kusema
nini, kuwa mimi siwezi kuzaa,…. ndivyo ulimdanganya mke wangu hivyo….docta
usiniharibie sifa yangu, mimi ni mwanaume,…sitaki kulisikia hilo, nimeambiwa na-na
yule …..ok, ok, …oh, nimejisahau, nisamehe…..haya sema ukweli sasa ikawaje..?’
nikamuuliza docta
‘Kwa vile saratani
hiyo ilishakwenda mbali..haikuweza kusaidia kitu, japokuwa mbegu zile ziliweza
kukaa vyema kwenye sehemu ya uzazi, lakini, nilijua ni hatari, ila nilimuomba
mungu sana, oh..ilikuwa na mateso sana kwa mkeo…alipata shida sana, maumivu
makali..
‘Oh…inanipa shida
sana kuliongelea hili….ilifikia hatua mimi nikamshauri mkeo ni bora tu aitoe
hiyo mimba..lakini yeye hakusikia, …akazidi kuvumilia..mkeo aliteseka sana,
fikiria miezi mingapi ya mateso,..na
hata siku alipoamua kuitoa hiyo mimba, mimi sikuwepo,….’akasema.
‘Ungeniambia
mapema, ningeliweza kulizuia hilo…..’nikasema nikitikisa kichwa.
‘Sizani…nakuja,
kama anavyokujua mke wako….ngoja niendelee….mke alikuja kuniambia tu kuwa
kashindwa, aliniambia akilia kwa uchungu kuwa hatimaye kashindwa kukupatia kile
ulichokitaka na sasa atakufa ukiwa huna amani, alilia sana, basi mimi moyoni
nikashukuru sana…na niliipomchunguza, nikajua sasa basi, …sizani kama ataweza kuendelea kuishi zaidi ya
miezi kadhaa.., maana hali ya kizazi likuwa mbaya sana..nikajitahidi kadri ya
uwezo wangu, …na kuna dawa hizo ambazo nilitakiwa kila mara niwe ninampatia,
kwa muda maalumu,…’akatulia akiangalia
saa yake…na simu yake ikawa inaita, akaangalia, akaikata,…
‘Hizo dawa ni aghali
sana..unakumbuka siku ile nilipofika kwako..nikakuambia nataka kumpa mkeo
dawa…ukanipiga na kuniumiza…, ilikuwa namletea mkeo hizo dawa…sawa nashukuru maana nilishaahidi
kuubeba huo mzigo..’akasema
‘Mhh…lakini mimi sikujua
hayo…’nikajitetea
‘Kwa ufupi ndio
hivyo, jirani yangu…kinachokuponza wewe ni hasira,na tamaa.. kama wote
tungeichukulia hivyo, nahisi dunia isingelikalika …sijui kama leo hii..hata kwa
hayo uliyonitendea..mmh, nahisi leo tusingeliweza
kuongea hivi, ingelikuwa ni uhasama, ndio maana nilikuambia tatizo letu
wanadamu ni `uoni’..jinsi gani ukomo wa uoni wetu ulipofikia, sikuwa na maana
ya kukudharau…kwa neno hilo uoni, wengi hatuwezi kujijua..’akatulia
‘Sawa…..’nikasema
‘Kwani kuna watu
wanaamini vitu vya ajabu, kuwa ni miungu nk…na huwezi kuwaambia kitu, ..uoni
wao umefikia hapo..tukubali hilo kuwa uwezo wa kufikiria una ukomo kwa kila mtu
hasa inapofikia kwenye imani….umenielewa hapo….?’ Akasema
‘Mhhh….’nikaguna
tu.
‘Na kwa ujumla… ,
hatupo sawa , hata ukiona maumbile yetu…,na hivyo hivyo, hata kwenye kuwaza… hatupo sawa kabisa….kila
mtu awaza lake, kwa jinsi aonavyo yeye na nafsi yake…, muhimu kwa sasa ni kuvumiliana…na
tuzidi kuwaombea wenzetu waliotangulia mbele za haki, hasa mke wako…huwezi
kujua jinsi gani alivyoteseka kwa ajili yako,inaniumiza sana, sana,…mimi kama
docta nilijua ni nini hatima yeke, lakini ilibid inifanye yale…niliyoona huenda
yatakusaidia….ili mkeo awe na amani….na bado nilikuwa namuomba mungu alete heri
zake,…kuna muda nikiliwazia hilo ninalia sana…’akatulia
‘Oh..lakini mimi
sikujua hilo….’nikasema
‘Najua,…. ndio
maana nikakuambia `uoni’…haupo sawa, wewe uoni wako uliishia hapo, …’akasema
akiangalia simu yake, kuliingia ujumbe wa maneno.
‘Sasa ni hivi, cha
muhimu timiza yale yote aliyokuwa akiyataka marehemu mke wako..,na yale yote aliyokuagizia
wewe uyafanye naomba uyatekeleze kwa kadri uwezavyo…, maana hayo ndiyo
yatamfanya mkeo huko alipo astarehe,….’akasema
‘Sawa, lakini yapi
hayo mbona sikumbuki,..si-si kumbuki mke wangu kuniagiza kitu, au una maana gani kusema
hivyo.….’nikasema.
‘Kwa leo..sina muda…
nawahi hospitalini.., kuna ujumbe umeingia kwenye simu yangu kuna mgonjwa
mahututi..nikirudi uje tuongee zaidi,..kuna mengi ambayo nahisi unataka
kuyafahamu na kuna maagizo yako
nitakuambia nikirudi….’akasema na kuanza kujiandaa kuondoka, na mimi ikabidi
niage niondoke..hata hivyo pale nilikuwa navumilia tu, moyo ulikuwa unaniuma
sana nikajikuta ninalia…
‘Hata nikilia
itasaidia nini..keshaondoka, oh…inaniuma sana….’
Nikarejea nyumbani
kwangu nikiwaza ni kitu gani hicho ambacho mke wangu alimuagiza docta, na mimi
hakuwahi kuniambia, maswali yakazidi kunijaa kichwani na kichwa kikawa kinauma
sana…, nilipofika nyumbani nikaichukua ile shajara na kuendelea kuisoma,
kuanzia pale nilipoachia ….
NB: Tuishie hapa
kwa leo, sehemu ijayo ndiyo itafichua ukweli wote na siri kubwa ya toba…toba ya
ukweli ilivyokuja kufanya kazi….na mengi ambayo yatakuwa ni heri kwetu kutokana
na hiki kisa….na huenda ikawa ndio mwisho wa kisa hiki.
WAZO LA LEO: Kuna mengi tunayapanga hapa duniani, na mambo mengi ya heri
yanakuwa na lugha `nikijaliwa..’ yanakuwa hayamaliziki kama mambo ya kidunia tu
ambayo hayana heri kwetu….
Basi tukiwa na marafiki, tukiwa ni wanandoa,
tunafahamiana sana, na bahati mwenzako akikutangulia mbele ya haki, jaribu
kukumbuka mema yake, jaribu kuyatekeleza yale ambayo alijitahidi kuyafanya na
bahati mbaya hakuweza kuyamaliza, ili kuendeleza hayo mema, na huku ukimuomba mola kuwa haya nayafanya kwa
ajili ya…rafiki yangu huyo, mwenza wangu huyo nk, mzazi wangu huyu nk,..na mola
ni mwingi wa rehema, anaweza kuyapokea kama malipo yake kwani yeye ndiye
anayetufahamu zaidi.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment