Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, September 1, 2016

KISA CHA BINTI YATIMA-UTANGULIZI


Kilio cha mtoto kilinifanya nisimame,..kwangu mimi mtoto akilia, nahisi moyo ukiumia, maana najua mtoto mdogo kama huyo akilia anataka kutoa ujumbe wake umfikie mtu..hawezi kuongea kwa umri huo, kilio chake ndio ishara yake ya maongezi.

Kwa haraka nikamgeukia Yule mama, aliyekuwa kambeba huyo mtoto…Alikuwa ni hawa akina mama wanaouza mihogo mibichi barabarani, na kwa muda ule alikuwa na sinia lilipangwa mihogo mibichi, kichwani mwake, na mkono mwingine kashika muhogo ulibakia nusu, na mwingine kashikilia kisu. Ni hawa wajasiriamali wa barabarani, ukitaka muhogo mbichi anakukatia kipande kutegemeana na pesa yako. Anapata riziki yake halali…

Nilisogea hadi kwa Yule mama, kwa muda huo alikuwa akihangaika kuulizia wateja, abiria waliokuwa kwenye daladala, kama kuna mtu anayetaka muhogo, mimi nikawa sasa nipo nyuma yake karibu sana na yeye,  nikawa najaribu kumchekesha Yule mtoto ili aache kulia…

‘Toto nyamazaee…’nikasema na sauti hiyo ikamfanya huyo mama ageuke, na kuniangalia

‘Nikukatie wa shilingi ngapi…?’ akaniuliza

‘Mtoto analia…na kwa jinsi ulivyombeba , na nguo ulizomvalisha na kwa hali hii ya hewa utamuathiri kiafya…’nikasema..ni kweli mtoto alibebwa kwa kitenge kilichochanika na kama kafungwa mgongoni, na asilimia kubwa ya mtoto yupo uchi.

‘Nikukatia wa shilingi ngapi…?’ akaniuliza sasa akiwa anataka kuanza kukata kipande.

‘Mia mbili…’nikasema na kwa haraka aka-kata kipande kidogo, kiukweli  sikuwa na haja ya muhogo, huruma yangu ilikuwa kwa Yule mtoto. Alipomaliza kukata kile  kipande akaanza kukimenya.

‘Mtoto analia sana, muonee huruma…’nikasema , yeye wakati huo anasubiria nimkabidhi pesa.

‘Nikimuonea huruma atakula nini….acha alie akichoka atanyamaza, kwani kulia kaanza leo… au wewe unajua maisha ya huyu mtoto….kwani wengine wanaumwa huko wananitegemea…’akasema huku akiniangalia kwa macho yaliyojaa chuki. Uso umeumbwa kwa aina yake, uso unaweza ukaelezea kile kichomo moyoni mwa mtu.

‘Kwanini unaonekana una chuki hivyo, mimi ni mteja wako watakiwa uninyenyekee au sio..?’ nikasema

‘Kwasababu nawachukua sana wanaume…’akasema hapo hata wale wanaume waliokuwepo pembeni waligeuka kumuangalia, na mmoja akasema

‘Ukiwachukia wanaume ujue unamchukua hata baba yako mzazi…’wakasema

‘Kauli yangu ni hiyo hiyo, nawachukia sana wanaume, habari ndio hiyo, wewe nipe pesa yangu…’akasema na mimi nikatoa noti ya elifu moja nikampa, akanitupia jicho kama kutaka kusema , kwanini nanunua kipande kidogo, kumsumbua kutafuta chenji.

‘Usijali hiyo chenji ni ya mtoto…’nikasema , hapo akanitupia jicho tena, na mmoja wa watu akasema,;

‘Haya huyo ni mwanaume …kataa hiyo pesa anyokupatia…’sauti ikasema

‘Siwezi kukataa maana haya madhila yote ninayoyapata kisa ni wanaume..unamuona huyu mtoto, baba yake alimkataa, wakati yeye ndiye aliyeni…..’akasita, halafu akaendelea kusema

‘Anadai kuwa huyu mtoto sio wa kwake, wakati anafanana na huyo mwanaume kwa kila kitu, na mimi sikuwahi kumjua mwanaume mwingine zaidi yake,…yeye ndiye aliyenifanya nifukuzwe shule…akiniahidi atanioa….’akawa anabadili sauti kama anataka kulia.

‘Sasa hilo utamlaumu nani, kwanini ulikubali , si kwa ujinga wako, kwani alikubaka, wewe si uliona ni peremende, …kwanza wewe yaonekana ulikuwa mapepe, mtoto wa shule unatembea na wanaume wakubwa….’mmoja wa wauza vitu barabarani akasema.

‘Nilikuwa mapepe mimi hebu uliza..huyo mwanaume alikuwa mwalimu wangu…, hebu fikiria mwalimu wa shule… na mimi nilikuwa mwanafunzi wake, msitake niongee ambayo sikutaka kuyaongea. …’akasema, na kuanza kuondoka.

Mimi niliingiwa na hamu sana ya kutaka kujua ni masahibu gani yaliyompata huyo mdada, nikaahidi kumtafuta.

Hutaamini jioni wakati narudi toka kwenye mishughuliko yangu, nikakutana na huyo mdada kwenye treni, bila ajizi nikajitambulisha kwake na kumuuliza, maisha yake ya nyuma, …mdada Yule alikuwa katulia,..niliona kama macho yamevimba..alikuwa analia, na nilipomuuliza kulikoni, ikawa kama nimejichongea, akaanza kulia kwa kwikwi, nikabakia nimeshangaa.

‘Mbona unalia..?’ nikamuuliza

‘Bibi yangu amefariki..bibi ambaye ndiye alikuwa baba na mama yangu, na juhudi zote za kuuza mihogo, ni kuhakikisha napata pesa ya kwenda kumtibia, sasa amekufa…….siwezi kuamini, ..kwanini dunia hii inanieleleza, sasa sina baba, sina mama, sina hata mlezi,….nitaishi na nani…nitakwendaje kumzika bibi yangu, wakati hata pesa kidogo niliyokusanya leo wameniibia…’akasema akilia

‘Wamekuibiaje…?’ mmoja akauliza

‘Nilijua tu…kuna tatizo, ..’akasema akitikisa kichwa
Haya jamani sijui bado mnahitajia visa vyangu, hiki kingina kinaitwa kisa cha ….
‘Kisa cha binti yatima….’


  Hiki ni moja ya kisa cha haraka nilichokipata jana, na sikupenda kukilaza, nikakiingiza kwenye shajara yangu, japokuwa kwakweli kinasikitisha,…nilijaribu kukiandika kwenye simu, lakini sikuweza kuendelea, simu iliisha mfuta, chaji , sikukata tamaa!Lakini huo ndio utangulizi wake, na tukijaliwa tutakiendeleza

Ni mimi: emu-three

No comments :