Mdocta waliniuliza maswali ya afya yangu, ninavyojisikia,
nilianza lini kuumwa, …na wakawa wanaandika kwenye kumbu kumbu zao,….wakawa
wanaangalia ile kadi yakungu kubwa iliyokuwa imeandikwa maelezo yangu, halafu
wakamuita nesi , na nesi akapewa maagizo ya dawa, halafu wakataka kuondoka , na
mimi hapo hapo nikaanza kuwabana kwa maswali
‘Docta, hivyo vipimo vya mtoto kukaa vibaya mtanifanyia
lini..au ndio tayari?’ nikauliza na docta wakaangaliana, halafu mmoja akasema
‘Ni nani kakuambia kuwa mtoto kakaa vibaya…?’ akaniuliza
Yule docta, na mmoja, akaniambia nilale , akaanza kunikagua tumboni, akipitisha
mkono wake tumboni mwangu, halafu akatikisa kichwa kama kukataa
‘Mtoto hajakaa vibaya…una matatizo mengine ambayo ndiyo
tunayafanyia kazi ila kama una hisi hali ambayo inafanana na hivyo,
tutakuchunguza, tutakupima kipimo cha kuangalia ndani moja kwa moja, lakini
hakuna dalili yoyote ya mtoto kukaa vibaya, ni nani alikuambia hivyo…?’akasema
docta
‘Huko nilipotoka walisema mtoto kakaa vibaya na nisipowahiwa
naweza nisijifungue salama…na ilitakiwa nije kupelekwa muhimbili kwa ajili
hiyo, walisema hilo ni tatizo kubwa na nahitajika kufanyiwa vipimo haraka
iwezekanavyo…’nikasema
‘Una vyeti vyoyote …ambavyo walikupima, au waliandika
maelezo yake?’ akauliza mwingine
‘Sina…’nikasema
‘Kiukweli kama ungekuwa na tatizo hilo tungelikugundua
mapema tu….lakini tutalifuatilai hilo, tutakupima vipimo vyote usiwe na shaka…’akasema na mwingine akaongeza
kusema
‘Muhimu utuamini sisi,…. Kwa vipimo vyetu vya awali huna
tatizo kama hilo…mtoto kakaa vyema kabisa…matatizo mengine tunayafuatilia,
utapewa dawa na maagizo mbali mbali…baadaye akija Yule mwenyeji wako mtaongea,
zaidi, yeye ni mtaalamu pia, utamuelezea yote unavyohisi, na ataweza kukushauri
zaidi….’akasema na nikaona haina haja kuuliza zaidi na docta akaita kwa sauti
‘Nesi,…..’ alimuita nesi, na nesi akaja kwa haraka
‘Huyu nesi atakupa
dawa zako na kama una tatizo jingine lolote usisite kutuambia, ..’wakasema na nikawaambia sina tatizo jingine kwa hivi sasa
na wao wakaondoka. Nesi akanipa dawa nilzotakiwa kutumia siku hiyo,na
alipomaliza akatoka.
Nilibakia nikiwa na mawazo nikijiuliza maswali mengi, ina maana hawa madakitari hawataki
kulifuatilia hilo tatizo langu, la mtoto kukaa vibaya ni kwanini, … mimi nina
uhakika, mtoto hayupo sawa, na niliambiwa na madakitari bingwa wa kule
kijijini, kwanini wao wanadharau, ngoja, akija huyo mwenyeji wangu nitamwambia
awasisitizie wanipime, kama hawawezi ni
bora niende huko Muhimbili…
Siku ikaenda kwa haraka maana walikuwa wakija watu mbali
mbali, mara wa dini mara wa kutoa misaada….wanatuhoji, na maswali yao
yalinifanya nizidi kuwa na mshaka sana…na mwenyeji wangu hakuweza kuonekana
tofauti na nilivyotarajia, kwani alisema atakuja mapema lakini mpaka muda huo
alikuwa hajafika.
Mchana ukaingia na mara wakaja kundi la watu, walipofika walisalimia wagonjwa na baadaye
mmoja mmoja akaanza kuongea maswala ya matumaini ,…walisema wazi wazi kuwa wao
wameshapima na wamejulikana kuwa wameathirika….wana ugonjwa wa ukimwi, na sasa
wanaishi kwa matumaini, na wamejitolea kuwapitia wengine
kuwaelimisha,…waliongea mambo mengi na baadaye wakakaribisha maswali….
Mimi nikaingiwa na mawazo, na sijui kwanini nilishindwa
kuvumilia, nikauliza.
‘Kwanini mnatuhubiria hayo, kwani sisi
tumeathirika…?’nikajikuta nimeuliza hilo swali
‘Kila mmoja anaweza kuathirika, na kama hujaathirika wewe na
huu ugonjwa, unaweza ukawa na jamaa yako au ndugu, au jirani, anahitajia
ushauri nasaha, kazi yetu nikuwapitishia huu ujumbe kila mtu…awe ameathirika au
hajaathirika…’akasema mmojawapo.
Waliongea na baadaye wakamaliza, na sasa ndio wakataka kuondoka,
nikagundua mtu mmoja kati yao ni kama namfahamu, yeye alikuwa akigawa
vijarida kwa wagonjwa na jamaa waliokuwepo humo ndani waliokuja kusalimia
wagonjwa wao….
‘Huyu mtu ni kama namfahamu,…atakuwa anatokea kijijini
kwetu,….’nikasema kimoyo moyo nikawa na hamu ya kuonana naye, na wakati anafika
kwangu kunigawia hiyo kijarida, nikaamua kumuuliza...
‘Mimi kama nakufahamu vile…wewe hutokei kijijini kimoja
kinaitwa…….’nikasema na yeye akaniangalia kwa makini, halafu akasema
‘Yawezekana unanifahamu, ni kweli natokea huko, lakini
sikuwa mkaaji sana, nilikuwa nafika na kuondoka…labda nikumbushe wewe ni
nani….?’ Akaniuliza na alipoongea nikaweza kumtambua vyema, sauti yake ilikuwa
sawa sawa na ndugu yake
‘Wewe sio ndugu yake……yule aliyekuwa na studio ya kupigisha
mziki na picha kule kijijini…?’ nikamuuliza, na yeye kwanza akatabasamu halafu
akatikisa kichwa , akaangalia huku na kule kama vile anawa wasi wasi na jambo,
halafu akasema;
‘Ndio ni kweli, wengi wanamfahamu sana yeye kuliko mimi,…lakini nchi ya jirani
nilikuwa nafahamika mimi zaidi kuliko yeye, na mara nyingi shughuli zetu
tulikuwa tunafanyia huko zaidi kuliko hapa nchini kwetu kutokana na sheria za
nchi yetu,…japokuwa kwasasa hawafuatulii sana, ndio maana kaka yangu akaweza
kufungua studio yake na kuanza kufanya shughuli hizo…japo kwa siri …’akasema
akigeuka huku na kule.
‘Mimi nimeshaachana na shughuli hizo….lakini
nisingelipenda kuongelea shughuli hizo,
…si unawafahamu wale watu ….mwanzoni walitutushia amani…na walikuwa tayari
kuua, ….kwahiyo ilikuwa kazi sana, ….hata hivyo polisi wanachunguza….’akasema
‘Kwahiyo na wewe ni mwenyeji kule, au unafika mara moja moja
kama mimi….?’’ akaniuliza
‘Mimi ni mwenyeji wa
huko , na nimekulia kule, hapa nimefika tu kwa ajili ya kutibiwa….’nikasema
na aliniangalia kwa mashaka, sasa akaja na kukaa karibu nami,akiwa anajiamini
kidogo.
‘Oh…pole sana, …ni vyema umekuja huku….huku watu
wanajitambua na kuelewa zaidi ya huko kijijini…kijijini ukiumwa wanakuchukulia
kama wewe ni wa kufa tu…’akasema na mimi nilitaka kumwambia kuwa mimi siumwi
huo ugonjwa,lakini nikamuacha aendelee kuongea
‘Unajua , mimi nilijiunga na kundi hili katika kuhamasisha na
kuwazindua watu wajielewe, waondokane na fikira hizo potovu, wabadili tabia
zao…mtu akiumwa ajaribu kuwa mwangalifu asiendelee kuwaambukiza
wenzake…’akatulia naona ni kama yeye hakutaka kuongea zaidi , ni kama anaficha
jambo, nikahisi anaogopa.
‘Kwa mfano wewe sasa ni mjamzito, ina maana unaweza
kujifungua mtoto naye kaathirika, au hajaathirika,…lakini kama umefuatilia
vyema taratibu na masharti yao unaweza kabisa ukazaa mtoto akakwepa kuathirika zaidi…wapo wamezaa watoto
hawana huo ugonjwa kabisa kwa vile walifuatilia masharti, huwezi amini,
….’akatulia
‘Unajue mimi, niligundua kuwa nimeathirika nikiwa hata
sikutegemea kabisa, nilishajiamini sina na siwezi kuwa nao,…ilikuwa kazi ngumu
kukubali hiyo hali, lakini sasa kama unavyoniona huwezi hata kufahamu, nina
afya yangu njema kabisa zaidi ya Yule ambaye hajaathirika…’akasema akijiangalia
angalia.
Ni kweli alionekana mwenye afya njema mwili wake ulikuwa
umejengeja vyema kimazoezi, huwezi kumfikiria kabisa kama ana tatizo kama hilo.
‘Kwa hali hiyo, …lilipotokea kundi kama hili, na mimi
nikaingiwa na hamasa, ya kutaka
kuwaelimisha wenzangu…..maana kwa hivi sasa huwezi kuwatambua wenye matatizo
kama hayo, na nia yetu nikutafuta njia ya kuukomesha huu ugonjwa usisambae
zaidi, na ikiwezekana uishe kabisa,…. tumetembea sana, hadi nchi za jirani kwa
kazi hii, tunaigiza Michezo ya sinema na, tunaelimisha kwa njia hii ya kuongea
kusambaza vijarida nk, ….na wengi wameanza kutuelewa..’akasema
‘Kwahiyo hata kaka yako amejiunga na kundi hili si nimesikia
kuwa naye kaathirika….?’nikamuuliza na
nilimuona akibadilika sura, na nilihisi kama machozi yakimlenga lenga, baadaye
akajitahidi na kusema;
‘Ndio kaka alikuwa nao, lakini hakutaka kuelewa,,..yeye
alijijua mapema…., lakini akaficha, na bila kujali akawa anatembea na wasichana
huko alipotoka na zaidi akaenda kijijini pale….oh, akawa anatembea na mabinti
wa pale mimi nilikuwa bado huko ncho ya jirani, na sijijui kuwa na mimi
nimeshaambkizwa
‘Ilitokea tu ikaja harakati za kupimwa bure nikaona name
nikapime,….oh, nikaonekana ninao. Unajua
ujana tena, mimi japokuwa nilikuwa mwangalifu sana, maana nimesoma , nafahamu
ugonjwa ulivyo, lakini kutokana na kazi tuliyokuwa tunejiunga nayo, sikuweza kuukwepa…’akatulia
‘Lakini nimeahidi kutokana na hiyo kazi, niweze kuitumia
kuelimisha watu, …’akatulia
‘Kumbe kaka alishapima, na …hakuwahi kuniambia, mimi
nilipogundulikana hivyo,…nikawa mnyonge sana,..nikawa sitaki hata kuifanya hiyo
kazi, siku moja kaka alikuja kuleta biashara zake, akanipa nizifanyie kazi,
nikakataa..akashangaa,
‘Kwanini unakataa biashara,….hii ni biashara kali wakiiona
jamaa itauzika kama njugu…’akaniambia
‘Mimi nimeamua kuachana na bisahara hii,maana najua siku
yoyote nitaondoka na huko kwampla nitasema nini….’nikamwambia
‘Hivi wewe
umepungukiwa na akili, hii ndio biashara inatufanya tuonekane hapa mjini,
tumejitarika kwa kupitia hii biashara, tuna magari , nyumba..sasa wewe wataka
tuiharibu…’akasema
‘Utajiri, ..mali na maisha haya ni ya kupita tu….mimi
naogopa mzigo wa madhambi tulioubeba, je una uhakika utapata muda wa kutubia
kablsa hujakata roho….na mimi nimegundulikana kuwa nimeathirika…’nikasema na
kuanza kulia,
Kaka yangu alikaa kimia kwa muda, hakutajia hilo, akaniambia
‘Kwanini hukuchukua tahadhari, nilikuambia…sasa ina maana
sote tunao…’akasema akitiisa kichwa, halafu akaanza kunipa moyo na kuniambia
kuwa naa yeye anao, lakini hajali kwani ni ajali kwnye mapambano.
‘Hii ni ajali kazini, lakini bao tunatakiwa kuishi, kutafuta,
wewe usijali kabisa endelea na kazi siki ikifika imefika…’akaniambia, lakini
mimi sikuweza kuendelea na hiyo kazi tena, akaifanya yeye mwenyewe, …nilianza
kuishi kwa maisha ya mashaka nikakonda, nikaanza kuumwa, na nikalazwa, …nikiwa
hospitalii nikakutana na wagonjwa wengine kama mimi wakanishauri kuwa kuna
kundi la kutiana hamasana na matumaini.
‘Ndio nikaanza kuingia na matumaini kuwa wapo wengi, na wanaimani
kuwa kuumwa kwa huu ugonnjwa sio mwisho wa maisha…nikaingiwa na hamasa kweli,
nikaanza kujielezea
Kaka yangu akapata hiyo taarifa, akanijia na kunikanya kuwa
nikimtangaza kuwa kaathirika, ataniua, na zaidi nisije kuitangaza kazi yake,
..’aliposema hapoo akageuka kuangalia huku na kule.
‘Mpaka sasa naogopa kuelezea kazi za kaka yangu, unajua zina usiri mkubwa, na nilimuahidi kaka kuwa
sitaweza kuzitangaza…japokuwa keshatangulia mbele ya haki, lakini bado nahisi
kama namuona, ….kaka alikuwa mnyama kwenye kazi zake hataki mchezo…mungu
amsaheme..’akatulia
‘Kitu ninacholaumu hadi leo ni kuwa yeye alijua kaathirika….na bado aliendelea
kutembea na mabinti wa watu, anawaambukiza, …., na mbaya zaidi akapuuzia masharti ya huu ugonjwa,..huu
ugonjwa ukifuatilia masharti yake unakuwa huna shaka,….unaishi nyema
kabisa….ndio hivyo labda siku zake zilipangiwa ziwe hivyo, na bahati, siku zake zimefika keshatangulia
mbele ya haki….’akasema
‘Oh….una maana….’nikasema
‘Ndio ameshafariki kaka yangu, nilimpenda sana..ni mtu wangu
alikuwa karibu sana nami lakini ndio hivyo mungu kampenda zaidi….’akasema
akianza kububujikwa na machozi…na mimi pale
nilipo hali yangu ikawa imebadilika ghafla, nilianza kuhisi vibaya, mwili
ukaniisha nguvu, nikanywea, nikataka kutapika….sijui kwanini nilijihisi vile
ghafla baada ya kusikia taarifa ile.
Kwa ujumla kaka yake alijulikana sana hapo kijijini, na
kutokana na kazi yake wengi walimzoa sana alikuwa mcheshi sana na kwenye
shughuli akiitwa anaipendezesha vizuri sana….alikuwa msanii wa shughuli. Na
kutokana na kipaji chake hicho, kila mtu alitaka kumuita kwenye shughuli yake
kama mwendesha shughuli. Alikuwa mtanashati anayejipenda, na alikuwa na sura
nzuri yenye mvuto na kwa hali hiyo wasichana wengi walimpenda sana. Kumbe…oooh
‘Oh, ina maana Msanii amekufa,….oh, hata sikuwa kuambiwa,
alikufa lini? Hapana sio kweli mbona mimi sijui…’ nikasema huku nikijaribu kutafuta namna ya kujizuia, ila
pale nilikuwa sijisikii vizuri kabisa.
‘Ndio, ameshafariki, na alifariki akiwa na hali mbaya sana,
aliishiwa ghafla, kuhara , kutapika…ni magonjwa hayo yaliharakisha kummaliza,
akatokwa na madonda, aah, inatisha …akapoteza wajihi wake kabisaka maana
maradhi yote yalimuandama….hakutaka kufuata masharti….hajafariki muda mrefu, hata
mwezi haujaisha,..ubishi wake bwana, halafu alifanya mambo ambayo hayastahiki,
na zaidi alijua kuwa ana tatizo la ziada ….’akasema akitikisa kichwa kwa uchungu
‘Tatzi gani la ziada…?’ nikaweza kumuuliza
‘Tabia yake hiyo ya kujitambua kuwa anao huo ugonjwa , na ya
kuwa ana hilo tatizo na bado akaendelea kutembea na mabinti mbali mbali,hata bila kuwafahamisha,
wakachukua tahadhari…kiukweli kama mtu unajijua una huo ugonjwa ni muhimu
amuelezee mwenza wake,…kwanini utembee na watu wengine ukijua utawaambukiza
mimi inaniuma sana,..sio vizuri, na pale kijijini alitembea na mabinti wengi
sana, wengi walimpenda, kwa vile alikuwa msanii mnzuri hadi kwenye mambo hayo,
ooh,….’ Akasema
‘Alikuwa na tatizo gani la ziada…..?’ nikauliza
‘Mhh…aliwahi kuoa , lakini kila akizaa mtoto hafikishi
mwaka. na ikafikia hatua wakaachana,
yeye
aliambiwa damu yake ina athari na kabla hajaoa inabidi
mchumba wake apimwe kwanza ili ijulikane kama anaweza kuzaa bila mtoto
kuambukizwa, ….
‘Ndio huo ugonjwa wa ukimwi…?’ nikauliza
‘Hapana hilo ni tatizo jingine kablsa,…mtoto anakuwa na
upungufu wa damu…mara kwa mara, na haishi kwa muda mrefu, ….yeye analijua hilo
kwani walihangaika sana na mkewe na ilifikia muda wakaachana, na akapewa hiyo
tahadhari kuwa asije kuoa, au kuzaa bila huyo mwenza kupimwa….. analijua hilo,
lakini hakujali,…’akasema
‘Mhhh mimi hata sielewi….;nikasema
‘Yeye anaelewa sana…lakini zaidi wanachojua watu kwa hivi
sasa ni huo ugonjwa wa ukimwi….’akasema
‘Oh….’nikaguna na yeye akasema
‘Kwahiyo kama ikatokea kampa mtu mimba,….inabidi awe makini
kweli, kama inatokea anapungukiwa
na damu, hiyo ni dalili mojawapo, lakini mara nyingi matatizo
hayo hutokea kwa mtoto….na hali inazidi kuwa mbaya kama akiwa na huu ugonjwa wa
kupunguza kinga, …’akasema akitikisa kichwa.
‘Oh mungu wangu….’nikasema
‘Hili lilikuja kujulikana pale kijijini, wakati kaka
amezidiwa,..yeye mwenyewe ilibidi aanza kusema, kukiri, kuwa kaathirika,
akajitahidi kutubu, na watu waliposikia hivyo, wengi wakawa wanaishi kwa
mashaka, hata wale waliopo kwenye ndoa…’akasema
‘Kwanini …?’ nikauliza
‘Kwanini…unauliza kwanini,…. huwezi jua, baba katembea na
binti wa ndani,…binti wa ndani alihadaiwa na kaka akatembea naye…..sasa huyu
baba wa ndani akikutana na mkewe itakuwaje, ni mnyororo ambao unamfuata hata na
asiyekuwepo…kwahiyo hali hiyo iliposikika, hakuna aliyekuwa na amani…na
tuliwasaidia sisi tulipofika hapo kijijini tukawahamsisha kuwa wakapime,….’akatulia
‘Kupima, ….pale kijijini ni kazi….wengi walikuwa wanapinga
kupima…’nikasema
‘Mwanzoni wengi waliogopa kujitokeza…kidogo kidogo wakaanza
kuja vituoni, na walioanza ni wavulana, wasichana kidogo ,nguvu kazi ya kijiji,
na baadaye kidogo kidogo wakaanza kujitokeza, na ambao hawakuwa na jinsi ni
akina mama wajawazito ni lazima wapime, …ni baada ya kazi kubwa ya
kuwaelimisha, kuigiza michezo mbali mbali ya hamasa….ndio wakaanza kujitokeza
kwa wingi…..na wengi wakagundulikana wameathirika…’akasema
‘Oh balaa gani hilo…na yote hayo ni sababu ya nini,
umasikini….maana vijana walijiunga huko ili kutafuta ajira, ….na ina maana basi
aliyeambukiza watu ni huyo kaka yako aui?’ nikauliza nikiwa na wasiwasi
‘Ni yeye na kundi lake…..wengi walihadaiwa walipofika hapo
kwenye mazoezi ya michezo, na….ndio hivyo…, na najua alipofika kitu cha kwanza
aliwatafuta, vijana mashababi, wasichana warembo ili wajiunge kwenye michezo ya kuigiza, michezo ya sinema na kutengenza kanda za video
si ndio ilikuwa hivyo,…lakini ndani kwa ndani wakaingizwa kwenye kuigiza
mapicha mabaya, …’akasema na kugeuka huku na kule.
‘Mapicha mabaya….?’ Nikauliza nikionyesha mshangaoo akili
yangu ikaenda mbali zaidi.
‘Ndio michezo ya kutengeneza picha za ngono, video hizo
zilienda kutengenezwa vyema nchi ya jirani kwani huko kuna mitambo mizuri, tulikuwa nayo huko na
tulikuwa wakala wa kimataifa……mimi mwenyewe nilikuwa nairatibu….’akasema na
hapo nikakumbuka zile kanda za video nilizowahi kuziona kwenye kabati la mchumba
wangu,..kumbe!
Mimi pale akili yangu ilianza kuwanga, nikijiuliza ilikuwaje
nikaingizwa kwenye mpango huo bila ya mimi kujijua, …bila ya mimi kujitambua,
nikataka kumuuliza swali lakini yeye akaendelea kuongea
‘Hii ilikuwa siri ya kundi….wazazi walikuwa hawajui, vijana
wanasema wanakwenda mazoezini huko kinachofanyika hawakijui, ni tatizo kubwa
sana, sijui serikali watafanyaje kumaliza huu uchafu, …ni kutu inayokula chuma
taratibu, hili na tatizo la madawa ya kulevya….kwani makundi kama haya yanazidi
kuongezeka na sasa wameingia hadi huko viijijini,…’akasema
‘Sasa kwanini hawakuchukuliwa hatua…’nikasema
‘Nyie mliowahi kuona mlitakwia mseme, lakini mkiuliza
mnaogopa, …kwani mlilishwa kiapo cha siri,mkiahidiwa mapesa mengi, si ndivyo
hivyo….kaka alishachukuliwa hatua, sema kwa vile alishaanza kuumwa, lakini
wazazi na serikali ya kijiji, ilishaanza kuchukua hatua za kumshitaki na
ilikuwa karibu afikishwe mahakamani, …’akasema
‘Masikini Msanii,…..ina maana hata mimi nitakuwa nao basi…lakini
ilikuwaje na mimi nikakubali kirahisi hivyo, mimi sielewi….’nikajikuta nimesema
‘Kwani na wewe uliwahi kutembea naye…oh, …wao walikuwa na
mbinu nyingi sana, kama wanakuhitajia kwenye kundi…..watakupata tu…..je wewe
uliingia kwa hiari au ?’ akaniuliza na mimi nikabakia kimia nikianza kuwazia jinsi gani niliweza kuingizwa kwenye mtego
wao. Sikujua…mchumba wangu….yeye ndiye ..oh, kichwa kilianza kuniuma.
‘Kwanza ukihitajika humo kama una sura nzuri kwa msichana
wanaweza kumtumia mchumba wako, au ikishindikana wanatumia mbinu nyingine ya
kukulewesha madawa ….’akasema
‘Kuna madawa wakikiwekea, kwenye kinywaji unakuwa kama
zezeta, utaweza kufanya yale ambayo ukiwa katika hali yako ya kawaida huwezi
kuyafanya…’akaendelea kuongea lakini mimi kwa wakati huo akili haikuwa yangu sikuwepo kabisa , nilikuwa nimezama kwenye
lindi la mawazo..
Nilianz kuwazia kuwa na mimi sasa nina huo ugonjwa,
nikawazia nipo kwenye hali mbaya, nimeisha , nina madonda mwili mnzima….,nikiwakumbukia
wale waliowahi kuumwa walivyoisha, kuna watu niliowahi kuwaona wakiteseka na huo
ugonjwa nikajihisi na mimi nitakuwa hivyo pia,….nilianza kuwanza jinsi gani
nitaweza kujifungua mtoto naye akiwa kaathirika, na huenda hataishi muda mrefu,
kisa ni mimi…niliwaza mengi, mengi sana…nikaanza kulia, ..nikaanza kuwakumbuka
wazazi wangu,….
‘Usijali…wewe umeshajitambua, kama umeshajitambua, ishi kwa
matumaini, fuata masharti utapona kabisa..hunioni mimi…nimeshapona,…japo kuwa
nimeathirika…’akasema
‘Mhh..hata sijui…kiukweli naanza kujijutia, wazazi wangu
walinikanya sana,….walinielimisha, na hata kunichapa, lakini nilikuwa mkaidi,nilimsikiliza
mpenzi wangu zaidi,…yote niliyoambiwa hayakuweza kuingia akilini mwangu, sasa
..ooh, lakini hata hivyo mimi kiukweli sijui,..kama kweli ninao au la…sijawahi
kupima, au kuambiwa…’nikasema
‘Kama hujapima usiwe na mashaka, …na ni vyema uingiwe na
moyo, wa kupima,ujenge ujasiri, uone kama unapima ugonjwa kama ugonjwa
mwingine, na uwe tayari kupokea matokea yake, ukiweza kuweka ujasiri huo, hata
ikipima utakuwa kama unatimiza wajibu tu,….hutaumia, utaweza kupona kwa haraka…’akasema
‘Kupona kwa haraka…hahaha…! Ugonjwa huu hauna dawa,
utaponaje, nitaponaje, na wakati umeshasema kuna tatizo hilo jingine la ziada,
mtoto akizaliwa, …ooh, kwanini mimi, kwanini …...Mimi namlaumu sana mchumba
wangu ndiye alisababisha yote haya…alinirubuni, ….sikujua, ..’nikaanza kuongea
kama mtu aliyepagawa, na yeye akawa na wasiwasi akiangalia huku na kule
akaongea kwa sauti ya kunong’ona
‘Kwani mchumba wako ni nani…mbona wasema kaka halafu …..?’
akaniuliza
‘Ni …handsome boy…’nikamtaja kwa jina lake la utani wanavyomuita
hapo kijijini na aliposikia hivyo akaniangalia kwa macho yenye wasiwasi.
‘Una maana Yule...mwenye gereji pale kijijini...yule alikuwa
rafiki mkubwa wa kaka yangu, …yeye alikuwa mmoja wa kundi la biashara hizo
haramu,…kwa siri alikuwa akienda nchi ya jirani kufuata vipuri vya magari na
humo aliweza kuficha hizo biashara…si ndio yule mwenye gereji kubwa…?’ akauliza
‘Ndio huyo…..’nikasema
‘Oh, unajua huyo mke wake aliyemuoa, alikuwa mpenzi wa kaka
yangu, kumbe kila akija huko nchi ya jirani, walikuwa kwa siri wana mahusiano,
kaka akaja kuyagundua hayo,….na hilo ndilo lilifanya yeye na kaka wakosane
baadaye…yaani kulitokea ugomvi siku moja, …we acha tu…’akasema.
‘Eti nini, ina maana handsome na huyo binti walikuwa
wanajuana muda, na muda huo kaka yako alikuwa keshatembea naye na anajijua anao…kwanini
lakini…ina maana,….’nikashindwa kuendelea nikishika kichwa!
‘Walikuwa wapenzi wa siri siku nyingi, si walijuana toka
huku, kaka naye hakuwa na wasiwasi aliwaamini, kumbe …wanazungukana wenyewe kwa
wenyewe…hebu nikuulize swali Je uliwahi
kuwasiliana na huyo aliyekuwa mchumba wako hivi karibuni…?’ akaniuliza
akiniangalia kwa macho yenye masikitikio.
‘Hapana nina muda kama miezi eeh…., niliondoka hapo kijijini
miezi miwili sasa….’nikasema.
‘Oh,..huyo jamaa yupo
hivi sasa ana hali mbaya sana na mkewe wake ameshamkimbia,…mimi nilijua tu wataachana,namfahamu Yule mwanamke
hakaagi na mume….., ana tabia chafu, na watu kama hao wana roho ya paka, kazi
yao ndio hiyo kuambukiza tu. Mimi niliwahi kumshauri huyo jamaa akaona mimi
naingilia mambo yao na nafanya hivyo kwa kumsaidia kaka yangu….’akasema.
‘Ina maana na yeye kwa hivi sasa anaumwa ….? Au yupo na hali
mbaya kwa vipi….?’ Nikauliza kwa mashaka.
‘Huyo aliyekuwa mchumba wako sio….? Tatizo lake alikuwa kama
kaka yangu,..hakutaka kusikia, hakutaka kukubali ukweli, yeye na kundi lao ndio
waliokiharibu hicho kijiji…nawalaumu sana kwa hilo…na hiyo nahisi ni adhabu
kwao kwa makosa waliyofanya japo kuwa sasa wanaadhibiwa na wasiostahiki…mungu
mwenyewe anafahamu ni kwanini, watu wanakanywa hawasikii, imekuwa ni sikio la
kufa,…’akataja msemo huo ulionigusa sana moyoni.
‘Nakuuliza na yeye anaumwa…au …?’ nikauliza hilo swali tena
‘Ndio anaumwa, hali
yake ni mbaya,…na hutaamini, alianza ghfla, na kwa muda mfupi tu akawa hajiwezi,
niliondoka akiwa kalazwa, na japo kuwa kakubali ukweli, lakini naona kama keshachelewa
sana, kiujumla nimemuacha akiwa kwenye hali mbaya ukimuona utamuhurumia….’aliposema
hivyo mwili wote ukanyong’onyea, nilishindwa kuvumilia, nikahisi vibaya …..
Pale nilivyo kaa, nilianza kuona giza likitanda machoni, na
kwa mbali nilimuona Yule mwenyeji wangu akija, lakini sikujua kilichotokea baadaye, kwani nilikuwa
tayari nimeshapoteza fahamu.
NB: Inabidi niishie hapa ili tuweze kuyatafakari hayo…mengi
yametokwa kwa muda mfupi, lakini tupo pamoja.
WAZO LA LEO: Tunaposhauriwa
kuhusu magonjwa ya kuambukiza tuwe makini na kufuata ushauri wa wataalamu, ni
vyema tukapima kabla ya kujiingiza kwenye mahusiano, kuna magonjwa tunaweza
kuyakwepa, kuna maambukizi tunaweza kuyakwepa, kuna matatizo ambayo tunaweza
kuyakwepesha kwenye familai zetu na vizazi vyetu,..haya kwa wazee wetu
waliyafanya mtu akitaka kuoa, au kuolewa wazee wetu walifanya uchunguza kwa familia
husika kama familia hiyo haina magonjwa ya kurithi, nia ni kukwepa matatizo
hayo kwenye familia, siku hizi kuna vipimo, je hatuwezi kuanza kuyafuatilia
haya. Tunapuuzia, na matokea yake inakuwa sikio la kufa…
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment