Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, February 22, 2016

SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA-10




 Mimi nilikuwa nimeshaamua kumuelezea huyo mzee ukweli wote ninaoufahamu mimi, ukweli ambao ilikuwa siri iliyofungamana na kiapo, Na sikupenda hata mimi kuuelezea mambo hayo maana yalikuwa yakinizalilisha mimi, na kuniweka uchi, ...kinyume na hali halisi.....sijui hata nielezeje...

Na hata tulipokubaliana na mchumba wangu kuwa iwe siri, niliona ni vyema iwe hivyo, ikawakati yetu,,,siri kati yangu na aliyekuwa mpenzi wangu  kwa sababu alizojua yeye mchumba wangu…lakini kwanini ilitokea vile kiukweli mimi sina ufahamu huo...

Baada ya kuligundua hilo, na baada ya tukio jingine lililokuja kutokea baadaye, ...niliumia sana, sikuwaamini kuwa hayo yalitendeka kwa mtu niliyemuamini kiasi hicho,,,,na sijui ni kwanini ikaja kutokea hivyo,nilijiuliza sana , mpaka leo naendelea kujiuliza, na sijui kama nitaweza kupata jibu kama sitaweza kumpata mmoja ya hao wanaume wanne akanifafanulia. Iliniuma sana ....na inazidi kuniuma sana, kwani matokea yake ni aibu hii kubwa. Aibu ambayo ilikuja kuniharibia maisha yangu yote....na kuonekana mwanamke wa ajabu sana.....

 Lakini hadi kesho nitang'ang'ania kuwa aliyenipa hiyo mimba ni huyo mchumba wangu,...mimi sijui mwingine, kwani yeye ndiye mwanaume nineyemfahamu, yeye ndiye aliyenionyesha hayo, na yeye kama ilikuwa hivyo ni yeye aliyesababisha hayo yote kutokea....

 Pamoja na hayo mimi sikuwa na ufahamu zaidi, sasa mzee angetaka nimuambie nini zaidi, ...kweli hawanikubaka, lakini sijui ilitokeaje...kiukweli hata mimi nahitaji maelezo, nahitaji kukutana na hawa watu waliosababisha haya yote,....ama kwa hii siri aliyotaka mume wangu,.....hata yeye nahitajika kukutana naye tena, kwanini alitaka iwe siri, kwanini hakutaka twende polisi....

Ndio maana hata mzee alipotaka nimpe jibu nilishindwa kutamaka wazi wazi.....hata hivyo niliwahi kuona huo ushahidi.....haikuwa kubakwa,...haikuwa kubakwa,....sasa ilitokeaje...ooh mungu wangu, kwanini hivi....nikabakia kulia....na hatimaye nilijua sina jinsi, natakiwa kusema, natakiwa kujibu swali la mzee;

‘Mzee wangu, mimi sikutaka kukujibu kwa haraka kutokana na swali uliloniuliza, nilitaka kwanza unielewe, na uelewe hali yangu. Najua jinsi gani ulivyojitolea kwangu, najua dhamana uliyoibeba kwa ajili yangu, na najua heshima yako, lakini kwa huruma zako uliamua kuubeba mzigo huu, na mimi  sina budi kukushukuru sana, lakini hata hivyo mimi nasita sana kukuambia ukweli, kwani hata mimi sina uhakika sana nao…’nikatulia

‘Sijakuelewa vyema, una maana gani ya kusema huna uhakika sana nao,…si umenielewa lakini, mimi ninachotaka ni jibu kuwa je hao wanaume ulitembea nao au wanakusingizia tu…?’ akauliza mzee sasa nikiona kama kakasirika, nahisi alishaanza kunihisi vibaya !

‘Mzee nitakujibu hilo swali lako, ila na mimi nataka ahadi kwako kuwa na wewe  hutazidi kuniweka uchi, nikazidi kuteseka, …haya ninayopambana nayo ni dhaidi ya uwezo wangu…mzee mimi nimechoka, siwezi tena kubeba adhabu hii, hapa nilipo najisikia vibaya sana…’nikasema na mzee akaniangalia kwa jicho la mashaka, akasema

‘Unajua sikuelewi,…wewe uliposema hao wanaume ni wanafiki,baada ya kusikia  kauli yao kuwa walitembea nawe na hadi kukupa ujazito, niliingiwa na chembe la furaha moyoni mwangu… unakumbuka ulitamka hilo neno awali, wanafiki wakubwa hao, sasa vipi tena…?’ akaniuliza na mimi nikakaa kimia, yeye akaendelea kusema

‘Ulipotamka maneno hayo, mimi niliingiwa na furaha, nikijua kumbe kweli wamekusingizia, na ndio maana nikatabasamu kuwa ndoto yangu ni ya kweli, kuwa wewe sivyo hivyo wanavyofikiria watu, wanakusingizia tu, na mimi nitaweza kuendelea na msimamo wangu wa kukusaidia…’akasema mzee.

Mzee aliposema hivyo, niliingiwa na mashaka, nikajua huenda nikimwambia mzee ukweli wote basi yeye ataingiwa na ghadhabu na hatimaye kushindwa kunitetea, lakini sasa nifanyeje, unajua kwa hali niliyokuwa nayo, sina ndugu, wazazi au rafiki wa kunisaidia, ….ilishafikia hatua kumuona huyo mzee kama msaidizi wangu,…na kweli yeye ndiye alikuwa tegemezi langu…

‘Mzee….naogopa sana kukuambia ukweli  unaotoka wewe..naogopa ya kuwa hutanielewa…..’nikasema

‘Unasikia ….binti usinipotezee muda…’akasema mzee

‘Haya mzee, ngoja kwanza nikujibu swali lako la moja kwa moja, naona unashindwa kunivumilia…unashindwa kunielewa, ..na mzee usiponielewa wewe….basi tena ….., najua utakuwa kama hao wengine…’nikasema

‘Lakini nikuulize kwani inakuwa vigumu gani kutamka, kuwa ni kweli ulitembea nao au sio kweli wamekusingizia, kuna ugumu gani hapo…mbona unanitia mashaka?’ akauliza mzee sasa akiniangalia kwa makini.

‘Mzee, bila kunielewa, hata kama nitakujibu utakavyo, haitasaidia kitu, unaweza kuchukua maamuzi ambayo sio sahihi, na …..hutanielewa, kwani ….yote hayo yamefungamana na siri,…na nashangaa kwanini wenzangu wameivunja hiyo sirii…’nikasema

‘Ni Siri gani hiyo inayoambatana na dhambi…hivi wewe huoni kuwa unaniweka kwenye wakati mgumu, kama kuna jambo mlifanya, la dhambi, mkawekeana ahadi ya kutokulisema, na likaja kugundulikana kuwa na mimi niliwasaidia, huoni kuwa nitakuwa na wakati mgumu….’akasema

‘Mzee nimekuelewa,…., lakini nachelea kutoa  jibu la swali lako kwani haliwezi kukidhi hali halisi,….ni jibu la mkato lenye mambo mengi ndani yake, ..ndio maana nilianza kukuelewesha,..’akasema

‘Umetembea nao au hujatembea nao….?’ Akauliza mzee kwa sauti ya ukali sasa

‘Mzee ama kwa vile unataka jibu la mkato, sina budi kukujibu na wewe utaamua mwenyewe…kwani hata mimi mpaka leo sina uhakika vyema ilivyokuwa,….ila viashiria na ushahidi niliokuja kuuona ulionyesha hivyo…’nikasema

‘Nijibu tu swali langu….sasa imetosha,naona una lengo la kupoteza muda, mpaka unanitia mashaka,  kama kuna mengine yatafuata baadaye…’akasema mzee

‘Swali lako mzee ulitaka kujua kuwa je hao wanaume wanne niliwahi kutembea nao,…jibu ni NDIO, niliwahi kutembea nao…’kabla sijamaliza mzee akasimama, akawa anacheza ile ya kimuhe muhe akaniangalia kwa macho yaliyobadilika ghafla,…chuki, hasira…

‘Unasema nini,….ina maana kumbe ni kweli, ina maana kukuaminia kote, kuweka dhamana yangu kwa watu kuwa sio kweli,kuwa  wewe umesingiziwa, kumbe nilikuwa nabeba mavi kwenye kapu, …nikiambiwa ni dhahabu…mungu wangu, unajua ulichokifanya, mimi sasa nitakuwa siaminiki tena…sijui nitawaambia vipi wajumbe….’akasema mzee na sasa akawa anataka kuondoka.

‘Sasa Mzee mbona unaondoka,…. wewe ndiye  baba yangu nikiondoka hapa nitakwenda kwa nani na hii hali,…hatua niliyofikia nisipopata msaada nitakuwa kwenye wakati mgumu, nahitajika vipimo, nahitajika….’nikasema na mzee akawa hataki hata kunisikiliza tena.

‘Mzee tafadhali nielewe,…mzeee halafu wewe ni kiongozi wa waumini, ina maana mtu akikosea mnamtenga, mnamkimbia…hujanisikiliza, sijakuambia huo ukweli, hiyo siri niliyotaka kukufichulia….ina maana gani sasa ukiondoka, na  niende wapi mzee wangu, watanifukuza hapa, nitakwenda wapi?’ nikauliza

‘Unajua binti, sasa naanza kukushuku vibaya,…maana hata katika kuongea kwako kote yaonyesha hujutii, ni kama vile unaona umeonewa,ndio tatizo lako…dhambi kama hizo ulitakiwa utubie uionyeshe jamii kuwa umekosea, na muhimu ulitakiwa ukawapigie wazazi wako magoti,…

'Yaanim .aaah, wanaume wanne, angalau wangekuwa wawili, wanne… umenikatisha tamaa kabia hata ya kuendelea kukutetea…kumbe ndio maana…unajua nilihisi mke wa mwenye nyumba analalamika kwa ajili ya wivu tu…lakini ile picha inaonyesha ukweli ulidhamiria kutenda dhambi na mume wa mtu..ile picha kwa yoyote akiiona…ni ushahidi tosha,… au nayo kaitengeneza huyo mke wa mtu, sio kweli…?’ akauliza/

‘Mzee ndio maana sikutaka kukupatia hilo jibu ulilotaka wewe, …..na hiyo picha inadhirisha ukweli kuwa mambo mengine yanaweza kuchukuliwa juu , juu  yakatenegenezewa fitina, ..lakini ukweli halisi sio huo….nakuomba mzee wangu nielewe…’nikasema

‘Mimi naanza kukutilia mashaka, siamini tena ndoto yangu,nahisi ilikuwa ndoto ya shetani,…kama kweli ulitembea na hao wanaume wanne,..sio mmoja, wanne, utasema walikubaka….hapana…..nambie ukweli walikubaka….?’ Akauliza na mimi nikawa nalia , kwikwi,….na sauti ikawa kama haitaki kutoka.

‘Kwa ushahidi na kauli zao, ulitembea kwa ridhaa yako mwenyewe,..huo si umalaya,….na sasa unataka kuendeleza tabia hiyo kwa mume wa mtu…je walikubaka?’ akauliza kwa hasira na mimi nikabakia kimia, siwezi hata kuongea kuna hali ilinishika sauti ikawa haitoki , maumivi ya tumbo, mgongo….nikawa nagugumia ndani kwa ndani huku  machozi yakinitoka.

Mzee akawa kageuka kuelekea nje, naona alikuwa anasita kuondoka,na hatimaye sauti ikanijia na kusema;

‘Mzee ndio maana niliogopa kukuelezea ukweli…jibu la swali lako kwani ulivyotaka nikujibu ulivyotaka wewe ni wazi itaonekana mimi nina makosa, ni vyema ungenipa nafasi nikaelezea ni kwanini hayo yalifanyika, naomba  unisikilize mzee…’nikatulia.

‘Niambie kwanza, je walikubaka…?’ akauliza

‘Sio kihivyo mzee, ,hawakunibaka…’nikasema

‘Kwahiyo ina maana ulitembea nao kwa mapenzi kwa ridhaa yako mwenyewe....’akasema
‘Sio kihivyo mzee, …..ngoja nikuambie…..’nikasema

‘Kama hawakukubaka, …mimi siwezi kusikiliza zaidi,….sitakuelewa…..’akasema na mzee akaanza kuondoka. Hakutaka hata kugeuka nyuma kunisikiliza, ….alipofika nje akasema

‘Sitaki hata kuongea na wewe na tena…’mzee akasema na kuondoka nikabakia mwenyewe , ….nikajua sasa ndio mwisho wangu….sasa nisubirie ni nini watakisema wenye nyumba….na wakati nawaza hilo mara mlango ukafunguliwa..

Bado tupo kwa majaribio, Kisa hiki kipoFace book,...ingie kwenye page yangu ya Diary yangu utakisoma kwa mapana yake...Tupo pamoja

No comments :