Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, December 18, 2015

RADHI YA WAZAZI-61



Huku kwa mshitakiwa , ...

baba wa mzazi wa kijana,

Mzee huyu hali yake iliendelea kuwa mbaya, na alikataa kabisa kupelekwa hospitalini, akawa anaugulia njumbani.

‘Br hii hali yako inanipa mashaka,....kwanini tusiende hosp?’ Profesa akamuuliza kaka yake

‘Mimi nimezoea miti shamba, kama haifanyi kazi ujue hakuna dawa nyingine ya kunitibu, na hata tukienda huko ni kujiangaisha tu....kama mwenzangu katangulia najua na mimi nitafuatia...’akasema

‘Mwenzako yupi?’ akamuuliza

‘Hahaha...bwana mdogo wewe hufahamu, ...mimi nafahamu mengi sana, wewe uliporudi jana na kuniambia hali ya mgonjwa,....ulisema mgonjwa anaonekana na nguvu ya ajabu, nikajua tu....’akasema

‘Sikuelewi bro,....mgonjwa akiwa na nguvu ya ajabu ndio anapona au ndio ....’akakatiza

‘Yategemea, ....tatizoo la mwenzangu ni tatizo kubwa, na huko kuchelewesha madakitari kusema llte ina maana yake,...nilishajua,...wewe subiria tu, utasikia,...’akasema

‘Mhh, bro, hizo hisia zako sio nzuri....’akasema, na lengo lake la kutaka kumshawishi waende hospitalini, lilikatishwa tamaa hasa pale kaka yake aliposema;

‘Mwenzangu keshatangulia,...najua hilo, na mimi nipo njiani......’akasema na Profesa akamuangalia kaka yake kwa mshangao, akihisi labda kaka yake keshachanganyikiwa

‘Bro leo mimi sikuwa na mpango wa kwenda hospitalini, maana jana, mimi niliondoka akiwa anaongea vizuri kabisa, na aliongea na mwisho alimuulizia mtoto wake kama kawaida yake...;akasema

‘Mtoto wake yupi...hebu aachane naye, na huyo ndiyo chanzo cha umauti wetu, mtoto unamzaa ukiwa na furaha, kuwa umepata tunda la familia, na huyo anaweza akawa chanzo cha kukuondoa hapa duniani...’akasema

‘Mhh....’profesa akataka kusema neno

‘Sasa huyo mtoto alifika?’ akauliza

‘Alifika muda ambao huyo mama alikuwa hajiwezi, na, cha ajabu mtoto wake alipondoka muda mfupi tu, mama huyo alizindukana,...tukajaribu kumpigia simu, na simu iliita wee, baadaye ikakata, na ilipopigwa tena ikawa haipatikani..

‘Hayo yameshaandikwa, huyo alishawakana wazazi wake kwa kauli na vitendo....na sijui kama kuna jambo la kumsaidia,..’akasema

‘Lakini.....’akataka kusema kitu profesa

‘Achana naye, ...hebu nambie kwanza kuhusu kesi , kwani nataka niondoke nikiwa sina kesi ya kujibu, ya dunia yabakie ya kujibu mbele ya mola wangu...’akasema

‘Bro, kesi, imesogezwa mbele, kutokana na hali yako...hakimu kaliona hilo, lakini pia, ukumbuke kulikuwa kunasubiriwa makubaliano yenu kuwa wewe na mtoto wako mfahamiane mkubaliane,lakini wewe umekataa hilo...’akaambiwa

‘Hahaha...hivi nikuulize, hivi kweli kuna mzazi anaweza kumkataa mtoto wake hivi hivi tu, ...’akasema kaka mtu akionyesha uchungu usoni

‘Sijui...kwakweli bro, mimi sijui,,..ndio maana watu wanawashangaa sana...’akasema

‘Mimi sijamkataa huyo mtoto, ila mimi natimiza wajibu wangu, kama mzazi, yeye kama mtoto ni wajibu wake kujirudi na kunyenyekea kwa mzazi wake, lakini sio mimi mzazi kwenda kwa mtoto kumpigia magoti, hilo halipo...’akasema

‘Tatizo nililoliona hapa ni kuwa nyote mna kasumba moja, tabia na hulka zenu zinafanana, baba kama mtoto,,,;akasema na kaka mtu akainua kichwa kumuangalia mdogo wake,

‘Samahani kulisema hilo, wote mna mihasira,.... sasa sisi tufanyeje..... yeye kasema hawezi kuja kukuomba msamaha kwa vile wewe  ndiye uliyekwenda kumfanyia fujo nyumbani kwake,..haijalishi kuwa wewe ni nani kwake....’akasema

‘Sawa..hayo tuyaache,...’ akasema kaka mtu akitaka kukwena kuliongea hilo zaidi

‘Aaah, bro ni vyema hilo tukaliweka wazi, ili tulimalize kabisa...’akasema Profesa

‘Nikuambie kitu, ipo siku utajaliwa utapata watoto wako, na wewe utaliona hilo, mimi najua huyo mtoto atajirudi, kwani na yeye sasa ana familia, lakini wasiwasi wangu ni kuwa itatokea akiwa keshachelewa, simuombei mabaya, lakini ukumbuke jambo, haya anayoyafanya kwangu, atakuja kufanyiwa,..;akasema kaka mtu

‘Usiseme hilo bro...’akasema Profesa

‘Mimi  simuombei mabaya, mimi kama mzazi namtakia maisha mema tu,....najua sitakuwepo mbeleni, ila wewe labda utakuwepo enzi hizo, utayaona,.....,mimi  sijui wewe utamsaidiaje, usije kumtumpa, ....kwani wewe ndiye uliyemuharibu, ...nakuambia hilo unielewe, kiujumla inanitia huzuni sana.....’akasema kwa sauti ya huzuni.i

‘Lakini bro kwanza unatakiwa umsamehe....huyo ni mwanao,...vijana wetu wa siku hizi wanachangamto nyingi, maisha yenu sio sawa na haya maisha yao ya sasa, unaona mitaani wanavyotukanana, mtu anamtukana mwenzake anakimbilia kutoa tusi linalomleanga mama, ni jambo la ajabu kabisa ..., ‘akasema

‘Ndio hivyo,...’akasma kaka mtu

‘Unajua bro, mengi yatasemwa kunihudu mimi, lakini mimi nilijaribu kumlea huyu kijana kadri niwezavyo, ukumbuke na mazingira nayo huchangia, wapi alipokulia,.....huyu kijana wako kuna muda alikuwa na lugha kama hizo, za mitaani, za kihuni ., nilimuasa sana...’akasema

‘Nimeshakuambia,...na unielewe hilo, hakuna mzazi anayemkataa mtoto wake, ..tunafanya mengine kwa nia ya kumrekebisha mtoto ili ajielewe, ili ajirudi,yeye ni mtoto kwasasa lakini atakuja kuwa baba wa kesho, tusipofanya hivyo, yeye atajenga msingi gani kwa kizazi chake....’akasema

‘Nimekuelewa bro...’akasema Profesa

‘Kijana ni muhimu alielewe hili, mimi kama baba, najawa na hasira, lakini moyoni bado naumia, kwani ule msingi ninaotaka kuuweka kwake, hauelewi,....yeye anafikiri elimu ya darasani inaweza kufanya kila kitu, hapana, kuna elimu ya mazingira, ya jamii, ya mahusiano, ya kuishi na watu, na hiyo huanzia ndani ya nyumba,.... hili ni kwa manufaa yake na kizazi kijacho...’ akasema

‘Bro, nimekuelewa, lakini .....;akasema Profesa

‘Hakuna cha lakini hapa,kama umenielewa, sitaki lakini, ....  muhimu hapa ni mtoto atimize wajibu wake..kama mtoto, umenisikia,.Hata kama kwasasa yeye ni baba na watoto wake, lakini akumbuke kuwa ana wazazi,...mimi nimemaliza, nataka kupumzika....’akasema kaka mtu huku akiwa kainamisha kichwa chini...

‘Ndio bro, lakini ni muhimu mkutane naye, ujaribu kumuambia hayo mwenyewe, unalionaje hilo...’akasema Profesa.

Na ndipo mlango ukagongwa, aliyefika alikuwa jirani yao, akasalimia, baadaye akamuita Profesa nje

‘Profesa vipi tuongee kidogo nje, maana wewe ni mtaalamu.....’akasema huyo jirani yao, na Profesa akatoka nje akijua kuwa jamaa huyo jirani wake huenda anahitajia dawa zake, wakatoka na kumuacha kaka yake, akiwa kajiinamia.

Huko nje ndio akapata taarifa hiyo ya msiba

‘Sasa mambo yameharibika....kama kijana hakuwahi kukutana na mama yake...oh,...’alisema Profesa akiwa kashika kichwa

*****************

Taarifa ilipofika kwa Profesa, ilikuwa kama rungu jingine kichwani mwake, moyoni alihisi kuwa sasa na mzigo mkubwa ambao hawezi hata kuubeba, je atamuelezaje kaka yake,

‘Haina jinsi lazima nimfiche.....japo kwa muda..’akasema

‘Na akishazikwa huyo mama, ndio nitakuja kumwambia kaka kihekima zaidi,....nikimwambia hivi sasa nitamuua kaka yangu....hapana, ni lazima nimfiche...’akazidi kusema kimoyo moyo....'

Wakati anayawaza haya yeye hakufahamu kuwa kaka yake alishahidi hiyo hali, alishafahamu kuna jambo, na alishahisi kuna msiba,hata kama wangetumia mbinu gani za kumficha.

Na kweli Profesa akajitahidi kumkwepa kaka yake, hakurudi kuongea naye, nia ni kuhakikisha kaka anatulia, hapati hizo taarifa, na alishawaambia majirani zake, wasije kumwambia kaka yake kuhusu msiba huo....

Ilikuwa siku ya mazishi, kesho yake, kwani msiba huo hakucheleweshwa, mazishi yalipangwa yafayike haraka, na Profesa akiwa kajiandaa kuelekea msibani, mara  alishangaa kaka yake akija kwake kwa kujikongoja, japokuwa alionekana mwenye nguvu, hata hivyo, haikuwa ile hali ya kaka yake anayoifahamu....

‘Kaka unakwenda wapi?’ Profesa akauliza

‘Lazima nikamsindikize mwenzangu nafahamu na mimi nitamfuata hivi karibuni....’akasema na hakuna aliyeweza kumzuia, ikabidi watafute usafiri, na wote wakaelekea huko kwenye msiba
Kweli walifika wakamzika na baadaye wakarejea nyumbani,..lakini kaka mtu aliporejea nyumbani , ilikuwa kama nguvu ya soda akawa hana nguvu kabisa, ikafika muda hata kuongea hawezi...

Profesa akaona atampoteza kaka yake bure, akaongea na wazee nia hasa wampeleke hospitalini, na pia ikibidi waweze kumshawishi kijana aje aonane na baba yake,....na kikao cha wazee wanandugu kikakutana.

Profesa akawaelezea ajenda hiyo, na wazee , wanandugu kwanza walilipinga hilo, kutokana na msimamo wa ndugu yao, kuwa wao wamechoka kumshawishi, kwahiyo hilo swala liachwe kama lilivyo

‘Lakini huyu mtu anaumwa, na kazidiwa, na nina imani moja ya jambo linalomuumiza bro ni kuhusu mtoto wake...’akasema Profesa

‘Sasa tufanye nini....?’ akaulizwa

‘Ndio maana nataka hekima zenu, mimi nafahamu kwenye wazee hakuharibiki neno, ....’akasema Profesa

‘Na kuna jingine linalomuumiza kaka hadi sasa...’akasema

‘Ni jambo gani tena, kwanza tulimalize hili ......wewe una wazo gani ?’ akaulizwa

‘Hili jingine litaweza kuwakutanisha,...’akasema

‘Jambo gani hilo?’ akaulizwa

‘Bro anasema hataki kesi hii iendelee kuwepo, anataka hukumu ipitishe, kama yeye anakosa sawa, kanisisitizia sana kuwa anahitajia hiyo kesi imalizike haraka iwezekanavyo, ....na mtu anayeweza kusaidia kesi hiyo imalizike ni huyo kijana wake...’akasema

‘Sasa tufanye nini...?’ akaulizwa

‘Mimi nitakwenda kuongea na huyo kijana, lakini nawaomba na nyie mnisaidia kuongea na kaka yangu...’akasema

‘Je una uhakika kuwa unaweza kumshawishi huyo kijana, peke yako?’ akaulizwa

‘Nitamshawishi, na kama itashindikana.....kwa ajili ya kaka.nitatumia karata yangu ya mwisho,....’akasema Profesa


*****************

WAZO LA LEO:Katika maisha haya ya dunia, kuna mambo muhimu tunayadharau, na kumbe tukiyafanya yanatusaidia sana. Ni muhimu tukakumbushana tu, mimi na wewe, kila mtu kwa nafasi yake  au kiongozi mwenye  dhamana ndugu kwa ndugu, au majirani kwa majirani nk..ni muhimu sana , swala hili la kuelekezana mema, na kukatazanana mabaya...

Kila mtu akichukua dhima hii akaifanya kwa moyo safi, jamii yetu itakuwa kwenye uadilifu mkubwa, tusichukie tukikanywa na kukosolewa, kwa mabaya tuliyoyafanya, na tufurahi sana, tukielekezwa kwenye mema, ...hata kama anayefanya hivyo kwako unamuona hana thamani, lakini angalia thamani ya kile anachokuelekeza au kukuonya.


Twatakiwa tuyafanye haya kila mtu kwa nafsi yake, tukikumbuka kuwa.maisha ya mwanadamu ni mafupi sana lakini mambo hayo yana faida endelevu..., sio kwa hapa duniani tu, ambapo maisha ya mtu ni ya muda mfupi tu,  lakini faidia ya mambo hayo kwa mwanadamu ni ya kudumu, yana tija hadi huko kwenye makazi yake ya kudumu.... 

Ni mimi: emu-three

No comments :