Mara kukasikika
kelele za watu wakisema ......
‘Amegonga,
kaua, kaua....’, na kelele zilipozidi zikafanya vikao vilivyokuwa ndani ya mahakama kukatishwa na watu wakatoka nje kwa
haraka, kila mmoja akitaka kuangalia ni nini kilichotokea. Na kwa ujumla, kwa
muda ule ndani ya mahakama kulikuwa hakuna shughuli zozote za kesi zaidi ya
hivyo vikao viwili ambavyo vilikuwa vinamaliza maliza kile walichokuwa
wakiongea.
Watu wale waliokuwa
mahakamani walitoka na kukimbilia nje,
na kukuta kundi la watu wakiwa wamejikusanya pembeni mwa bara bara , ni sehemu
magari yanayotoka kwenye mahakama yanapopitia ili kuingia kwenye barabara kuu.
‘Kumetokea
nini jamani....’Profesa akauliza, na swali hilo likaulizwa na karibu kila mtu
aliyekuwa katokea ndani, na hata wale waliokuwa nje, walikuwa wameshaanza kundoka, kuelekea kwenye shughuli zao, kwahiyo hao wachache waliokuwepo wakitembea kutoka eneo la mahakama hakuna
aliyeweza kuona hilo tukio zaidi ya kuhisi tu, kwani ni tukio lililotokea kwa
haraka sana.
Ni kweli wegi
hawakuliona hilo tukio, japokuwa walikuwepo hapo nje, sana sana walikimbilia
pale barabarani kuangalia nini kimetokea na ndipo wakamkuta huyo mama kalala
pembezoi mwa barabara.... ,
Ni mtu mmoja
tu, naye alikuwa akitoka mlangoni mwa mahakama, huyu alikuwa mmoja wa wazee wa
mahakama, anayeaminika, ndiye aliyebahatika kuliona hilo tukio na ilikuwa ni
kwa bahati tu, kwani wakati tukio hilo linatokea mtu huyo alikuwa anatoka
kwenye mlango wa mahakama, na wakati anatoka ndio akaliona hilo tukio.
‘Wakati
natoka tu, macho yangu yakaona ...nilihisi mwili ukiniisha nguvu, nilishindwa
hata kupiga kelele kumwambia dereva, hata hivyo gari lilikuwa kwenye mwendo ule
wa kasi wa kuzunguka,, ....’akaanza kusema.
‘Huwezi
kumlaumu dereva kabisa,....kwani huyu mama ni kama alijipeleka...ila dereva,
sijui kwanini, hakusimama, mimi sikupoteza muda nikawapigia hospitali, kijana
wangu anaendesha gari la wagonjwa......’akasema huyo mzee
Kwa muda huo,
wengi walikuwa wakihangaika kupata nafasi ya kuangalia ni nini, na japokuwa
walishahisi kuwa ni ajali, lakini wengi walitaka kuhakikisha ni nani aliyegongwa,...
Hawa walitoka
ndani ya mahakama walichelewa, kwani gari la wagonjwa lilishafika,... na
wahudumu wakawa wameshaanza kumuhudumia huyo mhanga, na maaskari wakaanza kazi
ya kuwaondoa watu wasogee mbali na eneo hilo
‘Kwahiyo ni
ajali ni mtu kagongwa....’akasema Profesa sasa akimsogelea yule mzee aliyeona
kilichotokea, na kwa muda huo alikuwa akitoa maelezo kwa maaskari usalama
‘Ndio ni
ajali mama mmoja kagongwa.....’akasema huyo mzee akimjibu Profesa
‘Kagongwa
vipi ...hapa ni sehemu ya kumgonga mtu, huyu mtu alilewa?’ ni swali jingine kwa
mtu mwingine
‘Ni ajali
kiukweli,...ila kinachonishangaza ni huyo dereva, baada ya tukio , sijui kwanini
hakusimama,....’akasema huyo mzee
‘Ilikuwaje
kwanini, ikawa ni maswali mengi na sasa waliokuwa wakielezea ni watu wengine
waliomsikia huyo mzee akisimulia...?’ akaulizwa na kwa muda ule gari la
wagonjwa lilishaanza kuondoka na huyo mhanga wa hiyo ajali.
‘Ni mama gani
huyo aliyegongwa?’ swali likauliza na huyo mzee akawa anashindwa amjibu nani,
amuache nani, ikabidi aanze kuelezea tu
‘Ni mama
mmoja hivi....’akasema huyo mzee
**********
‘Mama
mmoja,..mama yupi huyo....’aliyeuliza sasa alikuwa mshitakiwa , huku akiangalia
huku na kule kama anamtafuta mtu anayemfahamu.
Profesa naye
akawa anaangalia huku na kule na wazee wengine wakawa wanafanya hivyo hivyo,
ikionyesha kila mtu alikuwa akiliwaza hilo
‘Yule mama
aliyetuacha pale kwenye kikao yupo wapi...?’ akauliza jamaa mmoja
‘Kweli, na si
ana matatizo ya kuona, yule binti anayemsaidia na yeye yupo wapi?’ akauliza
Profesa
‘Mzee huyo
mama aliyegongwa yupoje....?’ akauliza mshitakiwa
‘Mimi
simfahamu vyema, ila wakati natoka ndio nikaona hilo tukio ..niliona lile gari
likirudi kwa nyuma, na.jinsi lilivyojigeuza kwa haraka ili kuelekea barabarani,
na wakati linaigeuza kwa haraka ndio huyo mama akatokea na kujipeleka, alikuwa
anakimbia ....’akatulia
‘Likamkanyaga..?’
akauliza
‘Halikumkanyaga,
lilimgonga, na kumrusha juu, akaenda kudondokea bara bara kuu....Lilimkosa
kosa,....’akasema
‘Akadondokea
kwenye lami? ‘akauliza mtu mwingine
‘Kichwa
kiligongwa kwenye lami, hilo nimeliona kabisa, yaani ni hatari....’akasema huyo
mzee
‘Kwahiyo
kupona ni bahati...?’akauliza mwingine
‘Ya mungu
mengi, maana nilimuona akitikisika mara mbili kama mtu anakata roho akatulia
huyo mzee akionyesha masikitiko
‘Mungu
wangu.....’aliyesema hivyo alikuwa mshitakiwa
Mara akatokea
binti mmoja akiwa kabeba kikapu akioyesha kuwa alitokea kununua vitu sokoni,
alipoona watu wapo nje wanaongea kuhusu ajali, akasimama akiwa kaduwaa, na
aliyemshitua alikuwa Profesa...
‘Wewe yule
mama yupo wapi?’ akaulizwa
‘Nilimuacha
ndani ya mahakama, nilimuambia asitoke mpaka nirudi, kwani nilitumwa kununua
hizi bidha, ili muda wa kuondoka tuondoke nazo, atakuwa yupo ndani...’akasema
huyo binti akitaka kuingia mahakamani
‘Mungu
wangu....’ilikuwa sauti ya mshitakiwa aliyekuwa kashikilia kichwa
‘Huyo mama
aliyegongwa yupoje..?’ akaulizwa mzee aliyeona hilo tukio. Na yule binti alirudi
kutoka ndani akiwa sasa kachanganyikiwa, akawa anaanza kulia...
‘Oh, dada
yangu,......oh dada yangu....’akawa anahangaika na watu wakafanya kazi ya
kumtuliza, na ikaonekana hakuna zaidi ila kuelekea huko hospitalini
***********
Hospitali
yenyewe hakikuwa mbali nimwendo wa kutembea tu, ila wale wenye usafiri,
wakasaidia kutoa msaada wa gari, na aliyeweza kusaidiwa alikuwa mshitakiwa
akiwa na
Profesa na yule binti anayetembea na huyo mama na wazee wengine
‘Mpaka sasa
tunahisi tu kuwa ndio yeye, maana watu wengi wa huku hawamafahamu huyo mama, na
.....’akasema mzee mmoja
‘Atakuwa ni
yeye.....’akasema mshitakiwa
‘Kwanini
unasema hivyo, wewe ulikuwa ndani kama sisi.....’akaambiwa
‘Hiyo ajali
niliiona kwenye ndoto....nilishaawaambia kuna mambo yatatokea...mimi nikiota
jambo fulani ujue kuna jambo litatokea,....na sijui....’akasema na watu
wakamuangalia kwa mashaka
‘Ndoto,...ndoto
inatokea ukiwaza, ...bro achana na imani yako hiyo kwani hiyo ndoto ilikuwaje,,,?’
Profesa akasema na baadaye akauliza
‘Ndoto kama
hiyo, inaashiria mikosi tu,...tumuombe mungu ...’akasema kaka mtu akiwa kama
vile yupo kwenye njozi
Na kwa muda
huo wakawa wameshafika hositalini, na haraka haraka wakaelekea chumba cha
wagonjwa mahututi, na madakitari ndio walikuwa wametoka kuhangaikia wagonjwa
waliofika muda huo
‘Samahani
dakitari kuna mama mmoja aligongwa na gari,.....’akaanza kusema Profesa
‘Nyie ndio
jamaa zake....?’ akauliza huyo dakitari akiwa na haraka za kuondoka
‘Ndio,
tulikuwa mahakamani ajali hiyo ikatokea....’akasema Profesa
‘Huyo mama
bado, hajaweza kuzindukana,....’akasema docta akiwa kasimama sasa
‘Oh, tunaweza
kumuona mara moja maana hatuna uhakika kama ni huyo tunayemuulizia...’akasema
Profesa na huyo dakitari akaonyesha uso wa kushangaa
‘Hamna uhakika...?’
akauliza
‘Ndio wakati
ajali hiyo inatokea sisi tulikuwa ndani ya mahakama, na tulipotoka
alishachukuliwa, ndio maana tunataka kuhakikisha tu kama ndio yeye huyo mama
jamaa yetu....’akasema mshitakiwa
‘Sawa
nimewaelewa, twendeni huku...’docta akasema na wote wakamfuata nyuma, na
alipoona hivyo, akasema
‘Sio wote
jamani, wawili au watatu wanatosha...’akasema na Profesa , kaka mtu na yule
binti naye akataka kwenda kuthibitisha, na mzee mwingine akajichomeka
Walifika
kwenye chumba, wakaambiwa, watamuona kwa kupitia kwenye dirisha kuna kiyoo
kinaonyesha kwa ndani, lakini hawaruhusiwa kuingia ndani, kweli alikuwa ndio
yeye, na kilio cha yule binti anayemsaidia kikatanda ikawa ni kazi ya kumliwaza
tena
‘Nitasema
nini mimi nyumbani....niliambiwa nisiachane naye hata mara moja..sasa
nimemuacha na haya yametokea,....’akasema kwa uchungu huku akilia!
‘Lakini ni
bahati mbaya....’akaambiwa na wakati huo huyo dakitari alikuwa kaingia kule
ndani, na muda baadaye akaja kuwaona....
‘Hali ya huyo
mama bado haijawa vyema , kwani kwa vipimo vya haraka aliumia kichwa na sasa
hivi tunafanya uharaka wa kupata picha.....tuone kama dawa imeingia ndani,
tutamchukua kwenye vipimo vya cit-scan,
ili tuone kuna athari gani, baada ya hapo ndio tutajua utaratibu mwingine...’akasema
docta na kuondoka
Na baada ya muda
huyo mama akachukuliwa kupelekwa chumba cha vipimo hivyo, na jamaa zake hawa
wakawa wamesimama pale pale wakisubiria, na wakati wanasubiria ndio sauti
ikatoka...
‘Masikini
....mtalaka wangu.....sasa najilaumu sana, sikutakiwa kumfanyia hivyo, huenda
haya yote yasingelitokea,.....mmh ’ilikuwa sauti ya mshitakiwa, akiwa
kajiinamia alionekana kabisa analia, na Profesa alimuangalia ndugu yake huku na
yeye moyoni akawa anajilaumu, hakusema kwa sauti, lakini akilini alisema
‘Yote haya
kosa ni langu....nisingefanya niliyoyafanya, labda haya yasingelitokea...ujanja
ujanja wangu ndio huu,...nilijua nitapata , nilijua nitamtumia nipate nay eye
apate na familia yake ipate, lakini kumbe haikuwa njia muafaka...nafahamu
kabisa hakuna atakaye lielewa hilo kila mtu atakayefahamu yote yaliyotokea
ataishia kunilaumu mimi....’akawa anawaza huku akitikisa kichwa
‘Lakini hata
hivyo, kosa sio langu....huenda mambo yangeenda vyema,..., kosa ni la hawa
watu, mama mtemi na watu wake,....wamemrubuni huyu kijana wakamuharibu, ..na
huyu kijana wangu, hata hataki kufikiria wapi alipotokea, kaamua kunisaliti,.....sitamsamehe
kwa hili, nitapambana naye....’akawa anazidi kuwaza
Haikuchukua
muda docta akaja, na hakuongea na wahusika alipitiliza kwanza, na aliporudi
akaingia tena kwenye hicho chumba na alipotoka, sasa akawajia na kusema
‘Nyie ni
ndugu zake huyo mama wa karibu au sio..?’ akauliza
‘Ndio.....’wakasema
‘Kipimo
kinaonyesha damu imepenya kwenye ubongo, kidogo....lakini kiutalamu, damu
ikigusa ubongo, kuna athari zake...., na bado tunahangaika, tuone zaidi, ila kwa
hali aliyo nayo, inabidi kuhamishiwa hospitali kubwa zaidi...’akasema ni kama
hakutaka kuulizwa maswali zaidi akaondoka
‘Sasa
docta.....’alikuwa Profesa lakini docta alishaondoka na baadaye akarudi na
kusema
‘Nilikuwa
nataka kuongea na ndugu yake wa karibu
sana....’akasema na aliyejitokeza ni Profesa na kaka mtu naye akafuata nyuma
‘Bro, wewe
pumzika, naona kwa hali yako hutakiwi , niache mimi nikaongee na docta
...’akasema Profesa, lakini kaka mtu hakutaka kuitikia wazo hilo akaelekea huko
kwa dakitari
Dakitari
hakutaka kupoteza muda, akasema
‘Ndugu
zanguni, kutokana na vipimo, yanekana damu imeingia na kugusa ubongo, mmmh, kwa
hivi sasa siwezi kusema kuwa kuna athari zozote, tunajitahidi kadri ya uwezo
wetu kupunguza hilo, na tunachoshukuru ni kuwa mgonjwa kazindukana, japokuwa akili haijawa
sawa ...’akasema
‘Oh, kwahiyo
anaweza kungea....?’ akauliza mshitakiwa
‘Mhh, hapana,bado
..ila, ni kawaida, hutokea hivyo,
mgonjwa kama huyo akizindukana huwa wengine hawawezi kusema kabisa, wengine
mwili mnzima unakuwa haufanyi kazi,....na tungesema upasuaji, lakini hapa kwetu
hatuna utaalamu huo...’akasema
‘Kwahiyo kama
damu imegusa ubongo, itakuwaje...tunaweza kutumia tiba mbadala, zipo dawa
zinasaidia...’akasema Profesa
‘Hizo dawa haziwezi
kusaidia,...tumekaa na wenzangu tukaona ni bora mtu huyu asafisrishwe kupelekwa
Muhimbili...’akasema docta
‘Muhimbili...hatafika,
mnapoteza muda bure...’alikuwa mshitakiwa akitikisa kichwa, na docta
akamwangalia halafu akayazarau manen yake akasema;
‘Sasa
tulikuwa tunahitajia msaada wenu,..gari lipo...lakini...gharama za mafuta....hata
hivyo, nilikuwa nawaambia tu, muanza kukusanya kusanya, ili tuweze kuona ....kwa
hivi sasa bad tunajitahidi ,tutakuja kuwaambia cha kufanya,...’akasema docta
‘Umesema
keshazindukana, naweza kuongea naye....?’ akauliza Mshitakiwa
‘Ndio, ...na
hilo limetupa faraja, na kuna muda aliweza kuongea na alichoweza kusema ni
maneno machache...’mtoto wangu namtaka haraka..mtoto wangu, ....’ lakini
hatuwezi kuruhusu mtu kuongea naye kwa sasa,...’akasema
‘Na huyo
mtoto wake ataongeaje naye...?’ akauliza Profesa
‘Kwani huyu mtoto
wake yupo hapa, ndio huyu binti mliyekuwa naye?’ akauliza doctor
‘Hapana huyo
binti ni mdogo wake sio mtoto wake....’akasema Profesa
‘Ni vyema
mkamuita huyo mtoto wake, inaweza kusaidia sana....’akasema docta na Profesa
akamuangalia ndugu yake aliyekuwa kainama chini, akiashiria kuwa kwenye mawazo
manzito, na alionekana kama hayupo kwenye hali nzuri
‘Vipi bro,
upo sawa.....’akauliza na kaka yake akasimama, na alionekana kama sio yeye,
akawa anaangalia hewani, halafu akasema ;
‘Mungu wangu,
nilijua tu...ile ndoto...nilijua tu...’.na ghafla mara akatikisa kichwa,
akainua mikono na kushika kichwa akiashiria maumivu, na docta akasimama haraka,
lakini alikuwa kachelewa, mzee akadondoka chini, ....
Tuishie hapo
kwa leo, tunamalizia malizia msichoke, tuzidi kuombeana heri,....
WAZO LA LEO: Jinsi umri unavyokuwa mkubwa, na
ndivyo uhimili wa matatizo unavyopungua, Ukiangalia maisha yetu ya Kiafrika,
kuhangaika hakuwiani na kipato, kiasi kwamba mtu anafikia utu uzima hata
kujiwekeza anakuwa bado, na zile zinazitwa akiba ya uzeeni zinakuwa hazina
thamani sawa na uhalisia wa maisha kutokana na kushuka kwa thamani ya pesa,..
na utakuta muda unavyozidi kwenda ndio
matatizo yanakuwa mengi, kwa uoni wangu, labda sasa pensin iangaliwe upya
thamani wakati inapochangwa iwe sawa na kipindi inapolipwa kama mafao
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment