‘Mimi kamwe sijakubaliana na hilo mnanilazimishia
tu, kwa vile mumeamua wenyewe fanyeni mtakavyo, msinishirikishe tena, lakini msije
kuja kusema mimi nimekubaliana na nyie
hapana, vunjeni sheria wenyewe,....’akasema shahidi,
‘Hutujakulazimiaha shahidi,huo ni uamuzi wako, sisi
tulichokuwa tunataka ni kukutanisha wewe na baba yako, ambaye ulikuwa
humfahamu, mfahamiane, na muafikiane, ...japokuwa kosa limefanyika, lakini
kwanza hebu fahamianeni,...ni muhimu hilo kiubinadamu...’akaambiwa na
‘So what..?’ akauliza kwa mshangao,
‘Ili iweje!...haah, tulifanya hivyo, tukijua kuwa
hilo laweza kuwa ni muhimu kwako, kuwa wewe hatimaye umemfahamu baba yako, ni
vyema mkakaa mkaongea mkajuana na makosa ni makosa yanaweza kuangaliwa upya,
ina maana wewe hujafurahi kumtambua baba yako, uliyekuwa humfahamu, ....?’
‘Ili iweje? Ndio nawauliza hivyo,..., hata kama yeye
ni baba yangu, so what,..., hawa
wababa wanajitokeza kwenye raha tu, wababa gani hao,....huyo sio baba yangu,
huyo ni muhalifu, hebu niwaulize ina maana sheria haitafanya kazi yake kwa vile
huyo ni baba yangu, ....na ni nani kawathibitishia hilo kuwa ni
kweli,...’akasema akiangalia saa yake
‘Jamani nyie watu,... hebu angalieni wenyewe, muda
mliotumia, gharama, bado mnatafuta njia ya kukwepesha haki isifannyike, kwa
vile...no siwezi kuamini hili, yeye ni nani kwenu....?’ akauliza
‘Tulijua labda kwako itakuwa ni faraja kumpata mzazi
wako, tulijua baada ya hilo, wewe utabadili nia, utapenda kwanza mkae na baba
yako mfahamiane vyema....ndio mawazo yetu, ..na kama ni baba yako kweli,
kihekima ni vyema mkakaa kwanza mkajuana,..ina maana hilo kwako sio muhimu,....?
‘ aliulizwa
Yeye alitikisa kichwa kuashiria kushangazwa
‘Ina mama kumbe wewe humtaki mzazi wako,..inashangaza kabisa kuna
nini hapa,..’akasema muendesha mashitaka akitikisa kichwa
‘Huyo sio baba yangu, huyo ni mhalifu, mbele ya
mahakama huyo ni mhalifu, nilishaongea mbele ya hakimu, hao watu ni
matapeli,..., je alichofanya ni kizuri, hajakosea,
haijalishi kamfanyia nani....’akasema huyo jamaa, huku muendesha mashitaka
akiwa haamini, kaduwaa....
Muendesha mashitaka huyo alipoona shahidi huyo
kadhamiria anachokiongea akaamua kumuuliza swali ambalo alishawahi kumuuliza
kabla
‘Nakuuliza
tena, je upo tayari.mzazi wako, baba yako afungwe, na hata baada ya kuthibitishwa
kuwa huyo ni baba yako mzazi, ?’ akamuuliza
‘Muheshimiwa, kwanza huna uhakika kuwa huyo ni baba
yangu, unao uhakika huo? ...huna,.... pili, hata kama ni baba yangu, tusema
hivyo, ila sio baba yangu, siwezi kuwa na baba kama huyo,..mfano akikosea ina maana hastahiki kushitakiwa,...?’
akauliza shahidi
‘Sijakukatalia hilo,...ila huyo ni baba yako,
ulikuwa humfahamu,....kutokana na wakili mtetezi, na tulitaka kulithibitisha hilo kisheria kwa
kupata vipimo vya kitaalamu,kama vielelezo,ambavyo vitathibistiha kuwa huyo ni
baba yako, na tulitarajia hilo linaweza kuwa furaha kwako, na ungeliweza
kubadili nia,....’akaambiwa
‘Ndivyo sheria inavyotaka hivyo,...?’ akauliza huyo
shahidi kwa mshangao
‘Kuthibitisha ndio...sheria inataka tuthibitishe
hilo, tutafanya hivyo,ili na wewe ujirizishe...’akaambiwa
‘Kuwa mhalafu akidhaniwa kuwa ni mzazi wako, wewe
mtoto uliyetendewa makosa huna haki tena,..si ndivyo mnavyotaka kufanya, sheria
ndivyo inavyosema.....?’akasema na kuuliza
‘Oh,....labda wewe hujatuelewa,...tulichotaka
kukifanya ni kuja kuondoa lawama,
....kama wewe bado unashinikiza, hata baada ya kufahamu kuwa huyo ni baba yako,
basi sisi tutafuata taratibu, lakini kuna hayo mambo lazima yafanyike, hayo ni
maagizo ya muheshimiwa,....’akaambiwa
‘Maagizo gani?’ akauliza
‘Kwanza kuthibitisha kuwa kweli huyo ni baba yako,
ushirikiano wako unahitajika, hilo tutalifanya kwa kuchukua damu yako na ya
mshitakiwa, kuhakiki hilo, na pili kuwemo na kikao cha mariziano, kama kweli ni
baba yako, ...na baada ya hapo, kesi itaendelea...tutaona .....’akaambiwa
‘Mnapoteza muda bure for nothing, am sory...’akasema na kugeuka kuanza kuondoka
‘Sikiliza kijana, wewe bado mdogo, hujui athari ya
haya yote, sisi tumefanya haya kwa nia njema kabisa, kwa ajili ya maisha yako
ya baadaye, sio kwamba tumeshindwa kutimiza wajibu wetu, lakini tusije kufanya
hivyo, baadaye yatakayotokea nije mimi
kulaumiwa,...nakuuliza tena, upo tayari kumfunga baba yako baada ya
kuthibitisha hilo?’akaulizwa shahid.....
‘Sikuelewi muheshimiwa.......
Yule shahidi, ambaye kutokana na wakili mtetezi ‘ni mtoto wa mshitakiwa’, hakutaka kuendelea
kusikiliza akaanza kutoka nje akiwa na hasira hakujali muito wa muendesha
mashitaka ambaye alikuwa hajamalizana naye,...
Na wakati huo kukatokea tukio upande wa pili, tukio
lililomteka akili muendesha mashitaka badala ya kuendelea na mtu wake, akawa
anaangalia jambo, upande huo wa pili huku akiwa kanyosha mkono wa kumuashiria
huyo shahidi asubiri....asiondoke
Lakini shahidi huyo hakusubiri...aliondoka!
Ni wakati huo huo, ....wakati shahidi huyo anaondoka
Upande ule wa pili, upande ambao sasa wakili
muendesha mashitaka alikuwa akiuangalia..., akatokea mama mmoja, aliyekuwa akionekana
kutaka kuongea na wale watu kwenye lile kundi, lakini ilionekana watu wale
hawakuwa tayari kumsikiliza,...
Lakini cha ajabu, alichoona wakili huyu, ni pale
yule mama, ghafla alipogeuka, kipindi kile kile huyu shahidi akiwa anatembea
kutaka kuondoka, na ndipo wakili muendesha mashitaka akagundua kuwa mtu wake
keshaondoka, ...na kujaribu kumsimamisha lakini alikuwa keshachelewa.
Muendesha mashitaka akawa sasa anatoa simu yake
kutaka kumpigia mlinzi kuwa asimruhudu huyo shahidi kuondoka, na alipotoa simu
yake akakuta haina chaji, imezimika, ..
*********
Yule mama akiwa
katulia, akiwa katega masikio, akasikia wakisema;
‘Mimi siwezi kukaa na huyo muhuni, labda kama yupo mzazi wake mwingine
atalifanya hilo,...’ sauti hiyo ilimuuma sana, akasimama, japokuwa aliambiwa
asije kuondoka hapo, lakini alihisi vibaya
‘Mimi kama sio baba yake na ameshasema hivyo, sitaweza kukaa na huyo muhuni, huo ndio
msimamo wangu, ....’ sauti ile ambayo anaifahamu vyema ikasema tena
Oh, wewe usiseme hivyo huyo ni mwanao....akawa
anasema kiakili, akaona anahitajika kuliongea hilo, yeye anahitajika kuchukua
hatua kabla hajachelewa,
Akaanza kutembea kuelekea hapo wanapozungumza hao
watu, haikuwa mbali ana pale alipokuwa amekaa..
‘Kama mimi nilivyosema ,.huyu ndiye baba yake, atakaa
naye watakubaliana...’sauti ikasema na huyo mama akazidi kujisikia vibaya,
kwani hajui baba mwingine zaidi ya huyo anayeongea, kwanini leo amkane
mwanae,....hapana ni lazima ni mwambie ukweli...akawa sasa anatembea
‘Kama mama yake angelikuwepo hapa, basi angejumuika
naye, kwenye hicho kikao, wakakubaliana lakini sio.....’ sauti hiyo ilisema na
yeye alishafika karibu, na ndipo akaona asizidi kunyamaza akasema;
‘Mimi mama yake nipo nitakaa naye meza moja
nitaongea naye, ....’na wote wakageuka kuangalia sauti ilipotokea, na
waliomsikia , waliokuwa karibu naye wakamuona, lakini cha ajabu wakampuuzia....
**********
Mama yule moyo ukawa unamuenda mbio, kwani kuna
hisia nyingine zilikuwa zikimuhitajia, alihitajika kufanya jambo, na akiendelea
kukaa na hao watu, atachelewa, kwa haraka akazifuata hizo hisia, akageuka kwa jinsi
hisia zilivyomtuma,....haraka, fanya haraka,...hisia zikamwambia hivyo...
Kweli kwa haraka akaanza kutembea, akahisi kuna jambo jingine muhimu zaidi ya kuongea
hapo, akatembea kuelekea huko hisia zinapomtuma,...akahisi, akamuhisi, mwili
ukaingia na kitu kama msisimuko, akahisi ile hali ya uzazi, mama na mwanae,....
akasimama, akanyosha mkono wa kutaka kumshika alijua kuwa ndio yeye....lakini aliikuta akipigwa
kikumbo, akapepesuka...lakini hakuanguka
Akaitahidi, kwani alijua asipofanikiwa hapo, ndio
basi tena.......lakini hisia, na ule msisimuko ukaanza kumuisha, ina maana
keshaondoka.....hisia zikamtuma akimbie kuelekea huko...akatembea kwa haraka
kuelekea huko, huku akisema;
‘Subiri, usiendoke....subiria wewe mtoto,
utaangamia...’ huku akitembea na mara akapigwa kikumbo na mtu mwingine, lakini
alijua kabisa huyo sio anayemtaka, akazizoa zoa, na akajihisi yupo mlangoni,
akahisi hali ya hewa ya nje, akajua yupo nje,, hata mwanga ulipenya kwenye
mboni zake, ....mwanga unamsaidia kuona,...lakini sio sana, anaweza kuona giza
akajua ni mtu kamkaribia, lakini hawezi kumtambua
Ila cha ajabu, ....aliyekuwa mumewe, ...hata akipita
nje ya nyumba atamtambua, ...hata akiwa kwenye kundi la watu atamtambua,...lakini
keshakuwa mbali naye tena, inabakia kumbukumbu za maisha yao ya upendo enzi
hizo.....
Hisia hizo za ajabu, pia zipo kwa mwanae, mtoto wake
aliyemuona kama sehemu ya mwili wake, siku alipompotea alihisi kupotewa na
sehemu ya mwili wake, na kweli aliliona hilo, kwani uafahamu wa kuona
ukaondoka, mwili ukawa hauna nguvu, na alijua kama mwanae ataweza kurejea akawa
karibu naye, huenda ufahamu huo utarudi...
Siku aliondokewa na ufahamu huo, alilia sana,
alitaabika, akawaambia ndugu zake wajitahidi wampate mtoto wake, lakini
hakupatikana, na akawa akilia usiku na mchana,..hadi akawa haoni kabisa, ikawa
imebakia hisia, na kumbukumbu wakati anamlea mtoto wake, hadi siku ile kule
kisimani alipokwenda kuchota maji,
Anakumbuka vyema, siku ile ilimjia ile...akapatwa na
kizunguzungu akaanza kuvutwa, na hali ili ikitokea fahamu humpotea na
kinachoendelea baadaye hakifahamu mpaka kupute muda, fulani, akizundukana
huambiwa tu alifanya hivi na vile
‘Hiki ni kifafa, lakini kinatokana na urithi,ila
kilikuwa hakina nguvu sana, nguvu yake ilisababishwa na msomgo wa mawazo, kama
ataweza kudhibiti mawazo yake, hili tatizo linaweza kupoa, lakini sio
kupona...’anakumbuka siku alipokwenda na mama yake akimuhangaikia, kipindi
hicho alishajifungua...na kauli hiyo ilimkatisha tamaa moja kwa moja
‘Mimi sasa kiburudisho changu ni mwanangu, huyu ndiye atanipa tumaini...nikiwa naye
sitakuwa na mawazo.....’akasema akiwa akimlea mwanae, lakini cha ajabu kipindi
hicho tatizo hilo lilimuandama sana,....na ikawa ndio sababu ya kumpoteza mtoto
wake....
Kupotea kwa mtoto wake ikawa ni pigo kubwa
sana,.....macho yakawa hayaoni, ..kuna muda kunakuwa na unafuu anaweza akaona
kwa mbali,... lakini hali hiyo haidumu kwa muda mrefu, maana mawazo ya mtoto
wake yakimjia basi hisia za kuona hufifia kabisa...
‘Sasa usichelewe, kumuona mtoto wako, huko mahakamani ndio sehemu yako yam wish ya
kumsaidia huyo mtoto wako, hakikisha unamzuia asitoke hapo mahakamani kabla
hajashikana mikono na baba yake, kabla hamjashikana mikono wewe na mtoto wako
kuashiria kukubaliana, muhimu mridhiane, ukifanikiwa kwa hilo matatizo yote
yatakwisha,....
'Nakuonya, ukichelewa huyo mtoto akitoka hapo mahakamani,
kitakachokuja kutokea huko mbele, ni hatari,...nasikitika... hutaweza kumsaidia
tena huyo mtoto wako na wewe mwenyewe...’alikumbuka ndoto hiyo iliyokatishwa
kwa yeye kuzindukana kwenye usingizi, na
aliyekuwa akimuambia hayo, alikuwa hamjui....
Na alipozindukana, akakumbuka kuwa siku hiyo ndiyo
siku ya kesi, akawaambia ndugu zake ni lazima afike huko mahakamani,.....
‘Uende kufanya nini, hujaitwa kama shahidi,
...’akaambiwa
‘Ninakwenda kusaidia, nakwenda kumuokoa mtoto wangu,
na baba yake, nisipofika nikasaidia, hakuna msaada mwingine wa kulitatua hili
tatizo ...’akasema
‘Kwa vipi, ...wewe unakwenda kuleta matatizo
huko.....’akaambiwa
‘Ni lazima niende, ni muhimu sana niwepo....’akasema
na ndugu wakashindwa kumzuia, basi akaambiwa wataondoka na mdogo wake ambaye
amekuwa msaada mkubwa kwake.
Mdogo wake huyo ndiye anayemsaidia kila anapotaka
kwenda na amekuwa sasa yeye ndiye macho yake , kumuelezea kile kinachoendelea,
na ndiye muongozaji wake kwa kila anachotaka kukifanya, kama inahitajika
kutembea au kufanya chochote, na kiukweli, ...walipendana sana.
Basi mdogo mtu alipoambiwa kuhusu hiyo safari,
alikubali mara moja akasema;
‘Mimi nitaenda naye.....’
Na wanandugu japokuwa hawakutaka hiyo safari, lakini
kwa vile huyo mdogo wake atakuwa naye, wakawa na amani kidogo, kwani yeye anamjulia
huyo mama, hasa ikitokea tatizo la kuanguka kwa matatizo hayo ya kifafa, huyo
mdogo wake alikuwa anafahamu amfanyie nini dada yake...
‘Hakikisha huachani naye, na ukienda sokoni kununua
hizo bidhaa uwe naye, usimuache....’akaambiwa, na kosa alilolifanya ndio hilo,
aliondoka akamuacha dada yake, akiendelea kusikiliza kinachoendelea mahakamani,
dada yake hakutaka kuondoka kabisa mpaka akamilishe kilichompeleka hapo, na
kukamilika kwake ni mpaka akutane na mshitakiwa na huyo shahidi aliyekuwa
kasimamishwa siku hiyo
Huyo Mama alishindwa afanye nini, akamwambia mdogo
wake:
‘Unajua mdogo wangu, ni muhimu nionane na huyo
mshitakiwa,...kama nilivyokuambia wakati tunakuja’akasema huyo mama.
‘Kwa hivi sasa itakuwa vigumu sana, alipofika tu
aliambiwa aende akakae kule mbele, nilishindwa kumuambia kuwa unataka kuongea
naye...’akasema mdogo wake
‘Sasa nitampataje, maana ni muhimu sana...’akasema
huyo mama
‘Kwahivi sasa ni vigumu sana, kwani haruhusiwi
kuongea na mtu mpaka kesi imalizike....’akasema mdogo wake,na huyo mama
akasikitika kweli, lakini hakuwa na la kufanya, baadaye ndio akaitwa huyo
shahidi huyo mama alishahidi kitu, ...na hata alipoitwa huyo shahidi hali yake
na shauku ikawa ipo juu, na akamuuliza mdogo wake;
‘Na huyo shahidi, nitampataje.....’akauliza
akimshika mdogo wake kwenye vigana vya mkono.
‘Huyo anayehojiwa sasa hivi huwezi kumuona pia,
inabidi tusubiria amalize kuongea na wakati anatoka ndio nimfuate....’akasema
mdogo wake
‘Oh, kila mtu muhimu kumuona mpaka kesi imalizike,
na ikimalizika hapo kila mtu anaondoka mbio mbio, huu kweli ni mtihani, kukosa
nguvu za haya macho sina ujanja, sijui sasa tutafanyaje maana muda wa amani
unakwisha, kitakachofuata ni hatari...’akasema dada yake, na mdogo wake
hakumuelewa, alichukulia ni maneno ya dada yake ya kila siku, akazarau.
Wakati kesi inaendelea huyo mdogo mtu akaona atumie
nafasi hiyo akanunue vitu, ili wakiondoka wasiende sokoni, kwani muda utakuwa
sio mnzuri kwenda sokoni na kurudi kituoni, akasema
‘Sasa dada sikiliza kesi bado inaendelea, mimi
nakimbia sokoni, kununua vitu, nitarudi kabla kesi haijamalizika, nikirudi
nitahakikisha hao watu wako mnaongea nao, mmoja baada ya mwingine...’akasema
‘Kweli...sijui, haya nenda haraka usichelewe,
utanikuta hapa hapa,...mimi nimeshakata tamaa,na huyu shahidi hamalizi tu,
mbona wanamtesa tu...maswali mengi...hawajui tatizo ni nini, wangeniita
mimi....’akasema huyo mama
‘Haya wewe usiondoke, ....ukae hapo hapo,
....’akasema mdogo mtu na kuondoka kwa haraka...na aliporudi, alikuta kesi
imekwisha kinachoendelea hakieleweki kila mtu kashika shavu, huyu anaongea hiki
yule anaongea kile...
Akaingia ndani ya mahakama, hakumkuta mtu, akatoka
mbio na kuanza kuulizia,
‘Jamani kuna mama mmoja nilikuwa naye humu ndani ana
matatizo ya macho mumemuona wapi...?’ akaanza kuulizia..hadi alipokutana na
Profesa akiwa na ndugu yake, na ndipo akawaelezea kuwa huyo mama alikuwa
akitaka kuongea na huyo mshitakiwa
‘Mhh...kuna tatizo limetokea....’akaanza kuongea
Profesa, kaka mtu alikuwa hawezi hata kuongea
‘Tatizo gani, dada yangu kapatwa na nini....?’
akauliza na wakati huo gari la wagonjwa lilikuwa linaondoka kuelekea
hospitalini
*********
Kwani ilikuwaje...swali aliloulizwa aliyekuwa
shahidi, na hapo kumbukumbu zikamreea wakati akiwa mahakamani wakati alipokuwa
akiongea na muendesha mashitaka, na sasa akawa mbio mbio kutoka nje.....
Ni wakati ule, akiwa anatoka mbio,..na wakati
anatoka akageuka kuangalia kundi lile, kundi lile ambalo lilimnyima raha,
lakini cha ajabu macho yake yakamuona mama mmoja, aliyekuwa akigeuka , na
kuanza kutembea muelekeo wa mlangoni....huko anapoelekea yeye, hakuwa na muda
wa kumuangalia huyo mama ni nani,
japokuwa hisia zake zilimvuta kufanya hivyo, akazizarau, nia ni kutoka mle
ndani kwa haraka, kabla muendesha mashitaka hajamzuia tena
‘Huyu muendesha mashitaka lazima nimkimbie haraka..atanichelewesha
hajali muda huyu, hanielewi....’akawa anaongea kwa sauti ndogo, huku akitembea
kwa mwendo wa haraka, hakutaka kizuizi kingine mbele,...oh, huyo mama!
Cha ajabu alichokiona ni kwa jinsi yule mama
alivyotembea kwa haraka na kuja kuweza kusimama katika ya njia, ambayo yeye
alitakiwa kupita, ili aufikie mlango na kutoka nje.
Kwa hasira , kwa kuchanganyikiwa hakutaka hata
kufahamu huyo mama ni nani, akamfikia yule mama na kumpiga kikumbo, na yule
mama akapepesuka, lakini huyo mama hakuanguka, na huyo mama hakuacha,kunyosha
mikono kama kutaka kumzuia, na wakati anampiga huyo mama kikumbo, ndio alisikia
sauti ya huyu mama akisema;
‘Mwanangu kubali, ...kubali yaishe, shikana mkono na
baba yako, usipofanya hivyo,...utapata taabu, acha ukaidi.....’sauti hiyo
aliisikia masikioni mwake,ilikuwa ya huyo mama, lakini hakusimama akawa
ameshatoka nje,
‘Mwanangu mwanangu, kila mtu ananiita hivyo,
nitakuwa na wazazi wangapi....’akasema huku akiingia kwenye gari lake..hakutaka
kugeuka nyuma, hakutaka kuongea na mtu, alikuwa akikimbizana na muda!
Akili ilikuwa kama sio yake, kwanza alishachelewa,
alitakiwa kumpeleka mkewe kwenye sherehe za akina mama, akina mama wanaotoka
huko ulaya walipokuwa wakiishi, na mkewe ni kiongozi wa hilo kundi, kwahiyo
ilikuwa ni muhimu sana kwa mkewe, na zaidi walitakiwa kwenda na waume zao!
‘Nitafika mahakamani, nikiona wananichelewesha
nitaondoka tu....’alimwambia mkewe, na mkewe akasema;
‘Sawa usiniangushe, nikifika pale bila mume, sijui
nitajisikiaje...’akasema mkewe
‘Ni lazima tutakwenda wote, sizani kama kesi hiyo
itachukua siku nzima, ushahidi wangu upo wazi....’akamuhakikishia mkewe
Na bahati mbaya, ikatokea hivyo, muda ukawa ni
kitendawili kwake, na alipoona saa zinazidi
kwenda na muendesha mashitaka anazidi kumbana, akaona hana jinsi , ndio akatoka
mbio, ....hakujali cha nani tena....alishaamua,
Aliingia kwenye gari, akawasha gari tayari kwa kuondoka,
akageuza kichwa kuangalia nyuma, akaona kweupe,.. na kwa haraka, akarudisha
gari nyuma, akaangalia kwa haraka kushoto, halafu kulia, akaona hakuna mtu, akaligeuza
gari kwa haraka,muundo wa U,....na wakati analigeuza kwa haraka, ndipo akamuona
yule mama...akitembea kwa haraka na kuliingia gari....
Alishachelewa, akajaribu kukanyaga breki, lakini
gari lilishakubali, alichoona ni yule mama akirushwa hewani, na kutupwa pembeni
mwa barabara kuu....
Gari lilishageuka kwa jinsi alivyochanganyikiwa
akakanyaga mafuta, gari likaondoka kwa mwendo wa kasi, na kuingia barabara kuu,
hakusimama wala kuangalia kushoto au kulia, kichwani alikuwa anakumbuka miadi
yake na mkewe, alishachelewa, akazidi kuongeza mwendo.... kuelekea nyumbani
kwake!.
‘Nitajibu hilo tatizo baadaye....sio kosa langu,
walioona watanisaidi...’akasema huku akiendesha gari lake kwa mwendo kasi,...na
alipofika nyumbani alimkuta mkewe mlangoni, akiwa kakasirika, alishajiandaa
kuondoka na gari lake mwenyewe,
‘Samahani mke wangu,....’akasema na mkewe hakusema
kitu, akaingia kwenye gari, kwa haraka wakaondoka kuelekea huko kwenye hiyo
shughuli!
**********
Waliporudi tu, wakakuta ujumbe, jamaa anatafutwa na
polisi, ...kabla hajakaa sawa polisi wakaingia, jamaa akakamatwa...hadi kituo
cha polisi, kwenda kujieleza!
‘Kosa lako umegonga, na baada ya kugonga ukaondoka,...japokuwa
uliyemgonga ndiye mwenye makosa, mashahidi waliona....yule mama haoni vyema, aliiingiza
mwenyewe wakati gari linapiga kona kuingia barabara kuu....
‘Kosa lako kwanini hukusimama....?’ akaulizwa
‘Ni kweli nakubali ajali hiyo ilitokea,.... lakini sio
kosa langu, na sikuweza kusimama kwasababu nilikuwa na dharaura ya muhimu sana,
nilikuwa na miadi isiyoweza kusubiria mke wangu alitakiwa kuwahi kwenye mkutano
muhimu wa wanawake wa waliowahi kuishi nchini mwao, kuna msaada wa kuwekeza
hapa nchini kwetu, kwa kupitia kwa hao akina mama, ...na mgeni rasimi ni mke wa
mkuu wa nchi, hebu angalia umuhimu wake...’akasema akitabasamu kuonyesha
alikuwa akiongea jambo la muhimu sana.
‘Lakini uligonga...na ...’afande akawa anaongea na
jamaa akamkatisha akisema;
‘Halafu afande, Mke wangu ni kiongozi wa umoja huo,
na mimi nilitakiwa niwe naye, walitakiwa kuongozana na waume zao, kwahiyo
nilikuwa na haraka,...haraka, ... na ukumbuke muda ule nilitoka mahakamani
kutoa ushahidi, nilikuwa nimechanganyikiwa...maswali yalinichosha kichwa changu!
‘Umeona afande...Ikizingatiwa muda wa kuondoka na
mke wangu ulishapita, alikuwa akinisubiria, .....’akatulia akimwangalia afande
kwa makini
‘Hata kama ulikuwa na haraka gani, inapotokea ajali,
unatakiwa usubirie...si unaelewa hilo?’ akauliza
‘Afande mimi nilifuata kanuni zote za
barabarani,niliangalia kote kulikuwa hakuna mtu, na wakati nageuza gari, ndio...., huyo mama
akaliingia gari, ni kama vile alitaka agongwe, gari lilishakuwa kwenye mwendo...kiukweli
huo ni uzembe wake mwenyewe..’akajitetea
‘Umeelewa kosa lako?,...., kwanini ulipogonga
hukusimama, kisheria na kiubinadamu, ilitakiwa usimame, uone hali ya huyo mama,
ili asaidiwe, ...baadaye ungelitoa huo udhuru wako, baada ya trafiki kufika na
kupima,... wewe uliona mkutano huo ni muhimu kuliko maisha ya huyo mama,...?’
akauliza afande
‘Hivi nikuelezeje afande,...wawezekezaji toka nje,
...hilo sio muhimu, ...., na mgeni rasmi
ni mke wa mkuu wa nchi, na mke wangu ndiye mwenyekiti wa umoja huo, sasa hebu
jiulize mgeni rasmi afike, na mwenyekiti hayupo....angeelewekaje, ....na kwa
ujumla mimi sikuwa na makosa, huyo mama ndiye mwenye makosa...’akasema
akiashiria kwa mikono
‘Unamakosa, kwanza, wewe mwenyewe umekiri kuwa ulikuwa
umechanganyikiwa ukiwa umetokea mahakamani, sawa si sawa...?’ akauliza na jamaa
akaonyesha mikono ya kuashiria anapotezewa muda
‘Sheria zinasema huwezi kuendesha gari ukiwa unahisi
umechanganyikiwa, pili ukagonga hata kama kosa sio lako lakini ulitakiwa
kusimama, ili trafiki afike kukagua,...hilo kosa, nakuandikia makosa hayo, utakwenda
kujibu mahakamani...sawa?’akaambiwa na huyo askari
‘Mahakamani, niende mahakamani wakati
nimeshakuelezea, na ushahidi upo kuwa mimi sina makosa,....haiwezekani.....hilo
sikubali na mimi naondoka afande, nimechoka, na uzembe wa nyie watu, hivi hii
nchi ina watendai gani, makosa na sheria ipo wazi, mnataka kupindisha, mnataka
nini ...’akasema akitaka kuondoka
‘Sikiliza huwezi kuondoka, unatakiwa kwanza uweke
sahihi yako hapa kuthibitisha makosa yako,nipe leseni yako ya gari kwanza...’
akaambiwa
‘Leseni yangu ya nini....?’ akauliza na huyo afande
akawa anafunua kikaratasi, akasema
‘Na pili nimekuambia, huyo mama hali yake ni mbaya
sana...anataka uende ukaonane naye anakuhitaji, huo ni ujumbe kutoka huko
hospitalini...huu hapa’akasema huyo askari akimuonyesha huyo jamaa karatasi,
jamaa hakutaka hata kuuangalia, akasema;
‘Hali yake ni mbaya ok, ,... am sory, sio kosa langu,....na kwanini atake kuniona mimi, mimi
sio dakitari,....isitoshe mimi sikumgonga kwa makusudi, kwenda nitakwenda,
lakini sio leo...kwa hivi sasa nina miadi, nina wageni muhimu nyumbani....kesho,
eeeh, kesho, naweza kwenda, ...’ akasema, na yule askari akamuangalia kwa macho
ya kushangaa.
‘Wewe ni mtu wa ajabu sana, umesema ulimgonga huyo
mama kwa bahati mbaya, au sio..? basi kiubinadamu, kiutu, ulitakiwa kufika
kumuona huyo mama, na kumuomba msamaha, angalau kutoa msaada wa
kiutu....’akasema huyo askari
‘Afande, ukisema mimi nikamuomba msamaha
unakosea,...na nahisi yule mama ana matatizo...’akasema akiashiria kichwani
‘Ndio ana matatizo ya macho haoni vyema....’akasema
askari
‘Nilijua tu....’akasema huyo jamaa
‘Ulijuaje,....unaona kumbe ulifahamu huyo mama ana
matatizo hayo, kwanini hukuchukua tahadhari, halafu ungesimama basi.....,lakini
kwanza tuyaache hayo unahitajika uende huko hospitalini....hapa utaniachia
leseni yako ya gari’akasema afande
‘Nilimuona huyo mama wakati tupo ndani, mimi
natembea akazuia njia, ...lakini sikumuona jinsi alivyotaka, .... nilishutukia
tu nimeshamgonga, ,....kwa leo afande, am
sory, siwezi kwenda huko afande...na leseni yangu siwezi kukupa’akasema
‘Taarifa imesema hivyo, kuwa leo ni muhimu uende
huko ukamuone huyo mama, ...taarifa ilikuja hapa mara mbili, wanasema hali ya
huyo mama ni mbaya, na muda mwingi amekuwa akikuhitajia wewe,....’akaambiwa
‘Ananihitajia mimi kuwa ananifahamu au kwasababu ya
hiyo ajali....?’ akauliza
‘Ndio tunajiuliza na sisi, je wewe huyo mama uliyemuona
ndani humfahamu kabla, je kabla ya siku
hiyo, hukuwahi kuonana naye, huna mahusiano naye,.....?’akaulizwa
‘Simfahamu,....afande, mimi simjui kabisa,... kama
nilivyowaambia huyo mama kumuona kwangu ni wakati nataka kutoka nikiwa ndani
mahakamani, ...na kwa jinsi nilivyomuona nahisi kama ana matatizo ya
akili.....’akasema
‘Mbona nasikia, wamesema huyo mama anasema anataka
akuone wewe ni mwanae, ametaja hivyo,kuwa wewe ni mtoto wake, ....’akaambiwa
‘Mtoto wake,! Hahaha, huyo kachanganyikiwa, ....mimi
sio mtoto wake!...mimi naondoka nasubiriwa nyumbani nina wageni muhimu....’akasema
na kwa haraka akasimama na kutoka nje akitaka kuingia kwenye gari lake....lakini
akazuiwa
‘Lete leseni, hiyo ni amri...utakuja kuvipata
mahakamani...’akaambiwa na kukatokea mzozano, lakini baadaye jamaa akakubali,
akijua ni faini tu inahitajika, na akiendelea kukaidi atazidi kuchelewa. Akaitoa
leseni na kutaka kuingia kwenye gari...
‘Gari hilo huwezi kuondoka nalo ...’afande akasema
kwa sauti, na jamaa akabaki kaduwaa
Tuishie hapa kwa leo...kwani inasikitisha, tutaona
itakavyokuwa,
WAZO
LA LEO: Vyovyote itakavyokuwa thamani ya mtu yoyote huwezi
kuilinganisha na kitu ...mali, au kuithaminisha na kitu! Utu wa mwanadamu ni
kitu pekee. Inapotokea jambo, kuchagua mtu, utu wa mtu au mali,...usiangalie
mali kwanza, wengi wapo tayari kuhatarisha maisha ya watu, hata kuua, kwa ajili
ya mali, ni nani kakuambia hiyo mali unaweza kuipata ukaitumia kabla umauti haujakushika!
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment