Wakili mtetezi
akiwa anaendelea kuyawaza hayo, akawa ameshafika sehemu ambayo alitakiwa kukaa
na watu wake ili, kuliwaelezea kile walichoongea na hakimu na nini kimeamuliwa
mpaka ikafikia kuahirishwa kwa hiyo kesi,....
Akawa
anakumbuka jinsi hakimu alivyokuwa akiongea;
‘Wakili
mtetezi, nimeshutushwa sana na kauli yako uliposema huyo shahidi ambaye
alisimamishwa na muendesha mashitaka....ambaye alitakiwa kuthibitisha hayo
aliyotendewa, ni mtoto wa mshitakiwa na hawafahamiani.....’hakimu alisema
‘Kufahamiana
au kutokufahamiana, hakuzuii sheria isifanye kazi yake,....lakini kutokana na
maelezo yako na maombi yako, kunanifanya niwe na mashaka kidogo....’akasema
hakimu
‘Kutokana na
kesi yenyewe ilivyo, na maelezo ya mshitakiwa na jinsi ilivyo somwa awali na
mshitakiwa kukubali kuwa kafanya kosa ilikuwa sio rahisi kukubaliana na ombi
lako.kuwa kesi hii iwe ya madai...’akaendelea kusema hakimu
‘Lakini sasa
unasema shahidi huyo ni mtoto wa mshitakiwa, nikuulize kwanza una ushahidi gani
wa kulithibitisha hilo?’ akauliza hakimu
‘Muheshimiwa
hakimu ushahidi upo, ukihitajika nitautoa wakati wa kutoa ushahidi wangu na
mashahidi,..’akasema wakili , na hakimu aligeuka upande wa muendesha mashitaka
‘Muendesha
mashitaka umesema mshitakiwa ana makosa kutokana na ushahidi ulio nao, ..sitaki
kuingilia sana undani wa madai yako kwa
hivi sasa, ila nataka kwanza lifanyike jambo moja,...’akawaangalia mawakili hao
wawili, na hakimu aliamua kuingilia kati baada ya malumbano ya kisheria, kila
mmoja akitetea hoja yake.
‘Mimi hakimu,
baada kusikia maelezo ya wakili mtetezi, ambayo yamenishitua sana,..kuwa huyo
kijana kakutwa na yote hayo, kayafanya yote hayo akiwa hafahamu kuwa huyo ni
mzazi wake, na halikadhalika mzazi naye hafahamu kuwa huyo ni kijana
wake....’akasema na kugeuka kumuangalia wakili mtetezi.
‘Mimi sitaki
kwa hivi sasa kujua undani wa kwanini hali hiyo ilifikia hapo..., kabla
hatujaendelea na hii kesi nataka mlitatue hili jambo kwanza, ...hili mlifanye
kama wazazi, mjaribu kuweka hisia zenu kuwa nyie ni wazazi na huyo ni mtoto
wenu....’akasema hakimu
‘Kosa ni kosa
mzazi anaweza kumkosea mwanae na sheria ikachukua mkondo wake na kinyume chake
vilevile....lakini kwa jinsi alivyoelezea wakili mtetezi, tukiamua tuendelee na
kesi jinsi ilivyo, madhara yake mbeleni yanaweza kuwa makubwa....’akasema
hakimu
‘Hebu kwanza
hawa watu wajuane, na kila mmoja afahamu kosa lake, na mimi kama hakimu, nataka
nipate muda wa kulifikiria hili ombi la watetezi kama linawezekana,....’akasema
hakimu
Muendesha mashitaka akataka kulipinga hilo,
lakini hakimu hakumpa muda, hakimu akaendelea kuongea;
‘Mimi nimeona
mliangalieni hilo kwa mtizamo huo, kwahiyo kila mmoja afanye juhudi zake, wewe
wakili muendesha mashitaka, hakikisha huyo kijana anakubali kukutana na baba
yake, kwani sijui nyoyoni mwake anajisikiaje baada ya kusikia huyo ni baba yake
na hayo yalitokea...ni kazi yako kulisawazisha hilo..’akasema
‘Huyu sasa
ni mbaba na familia yake, kwahiyo
anaweza kujielewa hawa watu wakutanishwe
wakae waongee, kesi nyingine kama hizi, tutumie hekima kuzimaliza ....’akasema
akitikisa kichwa
‘Ninachotaka
mimi ni kupata taarifa ya matokeo yake, je hawa watu wamefikia wapi, na kama ni
kesi ya madai au kesi yenyewe iendelee kama ilivyo, tutajua baada ya
kukamilisha hjilo zoezi...’akasema hakimu
‘Na wewe
wakili mtetezi, huyo mzee, ...ni mshitakiwa, unayemtetea, ongea naye, sijui
moyoni mwake kalichukuliaje hilo, baada ya tafrani hiyo, najua atakuwa na
hasira sana, kama mzazi kufanyiwa hivyo na mtoto wake.mwenyewe,...sasa nataka
wewe utumie hekima zako, mzee huyo ashuke na akubali kukaa na mtoto wake
waongee....’akasema hakimu
‘Na kwa vile
wewe ndiye uliyetoa hilo ombi, najua utajua jinsi gani ya kulifanya hilo,...’akasema
na akimwangalia wakili huyo
‘Mimi nisingelipenda kusikia kuwa mzee huyo
hajakubali...natarajia changamoto, lakini mwisho wa siku zilete matunda mema,,
ila ninachotaka hili zoezi lifanyika kwa haraka iwezekanavyo., ikibidi muanze
leo hii, na isizidi wiki tuwe tumeimaliza hii kesi..;’akasema hakimu.
Tuendelee na
kisa chetu
**********
Watu hawa walisogea
upande mwingine wa mahakama, uzuri wa
mahakama hii ilikuwa kubwa, kwahiyo waliweza kuchagua sehemu nyingine na kukaa ili
waweze kuongelea swala hilo bila wenzao upande wa pili kusikia nini
wanachokiongea.
Waliokuwepo ni
mshitakiwa mwenyewe pamoja na ndugu yake, Profesa, pia walikuwepo wazee wawili kutoka
kijijini, na mwingine alikuwa msaidizi wa wakili mtetezi, wote sasa walikaa
kimia wakisubiria ni nini wakili mtetezi atakiongea..
‘Ndugu
zanguni, hakimu alituita, na kutuita huko kunatokana na hali iliyojitokeza kuwa
mtoto.kamshitakia mzazi wake, ...na wawili hao hawajuani..’akasema akimuangalia
mshitakiwa
‘Hii ilikuwa
ni hoja ya kushitukizia, wenzetu wangsema ni ‘surprise issue...’akasema akimuangalia mshitakiwa
‘Kiukweli, hii
ajenda sikuwa nimejipanga nayo, mnielewe
hivyo wazee wangu, na ni hoja ambayo niliipata muda mfupi, na sikuwa
nimejipanga ni kwa namna gani nitaongea na wewe mshitakiwa , kwani ulikuwa na
haki ya kulifahamu hilo mapema....’akasema akimuangalia mshitakiwa
‘Kama
tulivyoongea na Profesa, hili jambo lilikuwa ni la kifamilia zaidi, na haikuwa
vyema kuliweka hadharani,...’akatulia akiwaangalia wote kama anasubiria huo
utangulizi uzame kwenye ubongo wa kila mmojawapo.
‘Kutokana na
muelekeo wa kesi ikabidi nifanye hivyo, kama mlivyoona shahidi huyo,
aliyetendewa hilo kosa, alishaweka wazi kuwa kweli alihujumiwa, akafanyiwa fujo
kwenye makazi yake, mlinzi wake akaumizwa.....unafikiri hapo hata kama hakimu
ataangalia baadhi ya uwongo wa shahidi, lakini bado mshitakiwa utaoenekana una
makosa.
Kiujumla kesi
kama hizi, matokeo yake huwa ni mabaya kwa mshitakiwa, hata kama kwa mfano
ingelifanywa hii kesi iwe ni ya madai, ikaja kutajwa kiwango cha fidia, kwa
hali zetu, bado hali ingeliweza kuwa mbaya kwetu,...ndio maana nikaona niitumbukize hiyo hoja kwa madhumuni
mawili....’ akatulia
‘Kwanza ili
kuweza kushinikiza ombi letu kuwa kesi hii ibadilike iwe ya madai zaidi,ikiwezekana
iwe ya kifamilia,irejeshwe nyumbani,..kwani kwa muelekeo wa kesi ulivyokuwa
awali, hilo lilishakataliwa. Kama ombi hilo lilikataliwa, tungefanyaje, mimi
kama wakili natakiwa niende na muelekeo wa kesi inavyokwenda, ndio maana
ikabidi niitumie hiyo hoja, .sijui kama mnanielewa hapo...?’akasema na kuwa
kama anauliza.
Aliwaangalia
wajumbe, wazee walitikisa kichwa kukubali, na msaidizi wake, lakini mshitakiwa
alikuwa kainama akiwa kimia, na Profesa alibenua mdomo kama kutaka kusema neno,
lakini hakusema neno.
‘Mimi haya
yote sikuwa nayafahamu awali, Profesa alikuja
kunisimulia nikiwa nimeshajiandaa na mpangilio mwingine,...aliponisimulia hilo,
mmmh, nilishangaa, ina maana mimi ni wakili, namtetea baba aliyeshitakiwa na
mwanae, na wawili hawa hawafahamiani...na je lolote likitokea mimi
nitaelewekaje,... niliingiwa na mawazo mengi sana, nikijaribu kujiweka mimi
kama mzazi, na mtoto wangu ndio kapotea kihivyo, ilinipa shida sana....’akatulia
‘Na baya
zaidi , sikuwa na muda wa kufanya lolote, labda ningekutana na huyo shahidi, yaani
mtoto wenu, ili niongee naye nimfahamishe, nikijua kwa vyovote atakuja
kusimamishwa kulithibitisha hilo kuwa yote hayo yalitendeka, yeye angeliweza kuongea
maneno ya kupoozesha na kesi isiwe na nguvu, ..
‘Lakini hata
hivyo nisingeliweza kuongea naye bila kukutana na muendesha mashitaka...napo
kungekuwa na changamoto zake,...Nikawa nimebanwa na muda , huenda kama
ningeyafahamu mapema yangeliwezekana kwa namna nyingine yoyote...’akasema
‘Lakini hata
kama ungefahamu mapema una uhakika yangeliweza kubadili hii kesi,....?’
akauliza mzee mmoja
‘Tungeweza
kwenda na madai yetu hayo kwa hakimu mapema kabla kesi haijasikilizwa, na yeye
angelitumia busara yake kuwa kesi hiyo iahirishwe mpaka pande mbili hizi
zikutane...na kwahiyo swala hili la baba na mtogto kutokujuana, lingetatuliwa
mapema, na hatuwezi kujua, huenda kesi ingelikuwa ni nyingine.....’akasema
‘Kama
mlivyoona kwenye kesi....kijana alishinikiza kuwa mshitakiwa alidhamiria
kutenda aliyotenda, na nilipoitoa hiyo hoja kuwa huyo ni mzazi wako, mnaona
alichokifanya, akakana kuwa sio kweli, kuwa mshitakiwa ni baba yake, inaonyesha
haamini...na kutokuamini kwake , kama kesi ingeendelea ingebidi nimsimamishe Profesa...kama
haamini, hakubali, kuwa huyo ni mzazi wake, hakimu akaingiwa na shaka, .....’akasema
akimuangalia Profesa
‘Sasa ....ulivyoingia
Profesa , niliona mabadiliko ya huyo
shahidi usoni mwake,...nashukuru kuwa wewei uliingia wakati muafaka...nikiwa
naishinikiza hiyo hoja, athari za kukuona wewe, mshituko alioupata, ulisaidia
sana kwangu .....’akatulia na kumuangalia Profesa
‘Kwangu
ilikuwa ni msaada mkubwa wa kuweza kumgaragaza huyo shahidi,hadi hakimu
kushawishika, na hekima zikamuingia akaliona hilo, ‘akatulia
‘Kiukweli.....tatizo
ilikuwa kwa muendesha mashitaka, lakini na yeye hoja hiyo ilimjia bila
kutarajia, hakuwa analifahamu hilo, wakati anatafakari awezeje kulikataa hilo,
au kuweka hoja ya pingamizi, lakini akawa anasita akiwa hana uhakika je kweli
ai si kweli kuwa huyo ni mtoto wa mshitakiwa
‘Kwa hali
hiyo ya muendesha mashitaka kuchelewa kuweka pingamizi, na kutokana hoja
yenyewe kuwa na utata, ..., hakimu ikamgusa....’akatulia na taratibu akageuka
kumuangalia mshitakiwa.
‘Kwa hali
hiyo, mzee, ...’akamgeukia mshitakiwa, halafu akawaangalia wengine akisema;
‘Ndugu
zanguni, hatutakiwi kumuangusha hakimu kwa kujitolea kutumia hekima
zake...’akawa anawangalia wote na sasa akawa kamkazia macho mshitakiwa
‘Ndugu mzee
wetu, usijali nikitumia jina ‘mshitakiwa’ maana ndani ya mahakama hii ndivyo
unavyotambulikana, ....’akamwangalia huyo mzee, mzee akionekana kuchoka, na
mwingi wa mawazo, na kwa muda huo alikuwa kainamisha kichwa chini kama vile
anaona aibu watu kumuangalia, au akiwa kazama kwenye mawazo mazito.
‘Najua hali
uliyo nayo kwasasa ikizingatiwa kuwa hili jambo limekuja kwako kwa
kukushitukizia, ...ilibidi iwe hivyo,....na kiujumla sikuwa nimepanga moja kwa
moja kulifanya hili na hata Profesa hakujua kuwa nita;lifanya hilii,...kabla
ya wewe kupewa taarifa’akasema
‘Profesa
alikuwa kapanga jinsi gani ya kuja kukuambia huo ukweli, kuwa huyo kijana, ambaye
alisimamishwa leo kuwa shahidi wa kuthibitisha hayoo yaliyotokea, ni mtot o wako....’akasema
‘Lakini
imekuwa hivyo mzee wangu, mimi katika mapambano ya mahakama ikawa sina jinsi
ikabidi niiweke hiyo hoja kushinikiza ....’akasema akimuangalia mshitakiwa
Mshitakiwa
akatikisa kichwa kuashiria kusikitika, ....akahema kwa guvu, halafu akasema;
‘Hata
siwaelewi nyie watu, yaani nyie mnanifanyia hivi, mimi naheshimika na mila na
desturi etu kamwe hazichezewi, mtoto kunyanyua mkono kumpiga baba yake,
hakujawahi kutokea katika maisha yangu, hivi nyie mataka niuweke wapi uso wagu, wazee wenzangu watanielewaje.,
hamjui jinsi gani mlivyonizalilisha, ...’akasema
‘Naelewa
mzee...’akasema wakili
‘Hii ni
bahati mbaya mzee mwenzetu, ....’wazee wenzake waliokuwepo wakasema lakini
alitikisa kichwa kukataa, huku akisema;
‘Ni bahati
mbaya!!! Nyie wenyewe manielewa, hili, lini...na nini kinatakiwa kifanyike...Unajua
sasa hivi najiona kama nimevuliwa nguo mbele za watu, ...hata, sizani kama
nitawasamehe nyie watu, yaani mdogo wangu mwenyewe, badala ya kushauriana na
mimi kwanza unafaya mambo kienyeji, umazizarau...’akasema mshitakiwa
akimwangalia ndugu yake kwa jicho la pembeni
‘Lakini mzee,
kwa hali kama hiyo hatukuwa na jinsi,...labda usubirie nielezee hadi mwisho
ndio utaona kwanini ikafanyika hivyo..nitakufafanulia hatua kwa hatua ili
unielewe, hakitaharibika kitu.’akasema wakili mtetezi, lakini mshaitakiwa
akaendelea kutikisa kichwa kuonyesha hataki hata kusikiliza, na mara
akasimama....
Je itakuwaje?
WAZO LA LEO: Usikubali ukatawaliwa na hasira,
kwani hasira ikikutawala unaweza kufanya jambo kwa hasira ukaja kujijutia,
mbele ya hasira kuna majuto. Pindi ukihisi una hasira jaribu kuwa mbali na
tukio lililokufanya ufikie hapo, na muombe Mungu akuepushia na mtihani huo.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment