Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, November 20, 2015

RADHI YA WAZAZI-55



Wakati hayo yakiendelea upande wa muendesha mashitaka na watu wake, huku kwa mshitakiwa na wakili wake nako kulikuwa na kikao kikiendelea, kikao cha wakili mtetezi na watu wake, naye akijaribu kuelezea kile walichoambiwa na hakimu.

Wakili huyu, akiwa karizika na juhudi zake, walipokuwa mbele ya hakimu,kuwa angalau hatua muhimu imekubaliwa na kilichobakia ni kutimiza masharti ya hakimu, ambaye alitaka kuhakikishiwa kuwa kweli, watu hao wamekutanishwa, na hakuwa anafahamu ni nini kinachoendelea ndani kwa ndani kwa watu hawa.

Wakili aliondoka kwa hakimu akiwa hana uhakika kuwa alichokifanya mbele ya hakimu kweli kinaweza kuungwa mkono na mshitakiwa, tatizo kubwa ni mshitakiwa ...alifahamu kuwa ama kwa jamaa zake wataunga mkono, kumuacha Profesa ambaye anaweza kuwa ndumila kuwili, kutokana na mambo yake,

Wakati anawaza hilo ndipo akakumbuka pale Profesa alipomjia kwa dakika za mwisho na kuanza kumuelezea hilo swala, ...alianza kusema kuwa ana jambo muhimu sana ambalo kaona ni muhimu yeye kama wakili wa hiyo kesi alifahamu, ...

‘Je linahusiana na hii kesi, na je litaweza kusaidia, ....?’ wakili akamuuliza

‘Ngoja nikusimulie ilivyokuwa, kwa ufupi tu, ...na wewe utaona jinsi utakavyofanya,...kwani nimeona nikikaa kimia na hukumu ikatolewa halafu nikaja kuongea baadaye sijui kama nitaeleweka....’akasema

‘Ni jamboo gani hilo, niambie kwa haraka maana nakimbizana na muda, kuna maswala  hapa ya kufuatilia, nilikuwa napambana ili kuitoa kesi hii kutoka kesi ya jinai iwe kesi ya madai, sasa wewe wataka kuniambia nini ....’akasema wakili akiangalia saa yake, 

Na Profesa akaanza kuelezea ....

Tuendelee na kisa chetu

                                       **************

‘Ni kwanini sasa ulipogundua hivyo kuwa huyo ni yule kijana wake, mtoto wake, kijana uliyemlea huko ulaya, ni kwanini hukutaka kumwambia kaka yako?’ akamuuliza

‘Umuenielewa nilivyokuelezea awali....?’ akauliza

‘Nimekuelewa, lakini sioni sababu ya kumtokumuelezea.....’akasema na Profesa akakuna kichwa kwani hakutaka kuliweka lengo hadharani kwa hivi sasa, na wakili akaona anapotezewa muda, akasema;

‘Kama uliweza kumsimulia kaka yako maisha yako yote ya huko Ulaya, na kwahiyo kaka yako anafahamu kuwa mtoto wake ulikuwa ukiishi naye na akakugeuka na kukufanyia aliyokufanyia,.....ulitakiwa umwambie ukweli tu,....’akasema wakili huyo

‘Nilihitajia muda wa kulifikiria hilo zaidi, maana hadi hapo mimi na huyo kijana tulishakuwa maadui, hatuelewani,leo mpaka kesho ....’akasema

‘Sasa kwa hali ilivyo kwenye hii kesi, wewe huoni kuwa  usipomwambia kaka yako na kunaweza kutokea jambo baya ukawa wewe ni sababu?’ akamuuliza

‘Jambo baya kama lipi?’ akauliza

‘Kama hili kwa hivi sasa, umeona ilivyotokea mungu anawaonya kwa namna nyingine kuwa mnahitajika kulisawazisha hili mapema, ....mtoto na baba yake wamafikia kuumizana japokuwa ilikuwa siri yako, ...na sasa imeenda hadi mahakamani, hatujui kesi itakuwaje...’akaambiwa

‘Lakini hata mimi nilikuwa sifahamu, kuwa hawa watu wamerudi, ...na baya zaidi kuwa wao ndio wanamiliki nyumba yangu,...sasa kaka akafika huko na kukatokea hivyo, na kwa hali kaka aliyo nayo kama ningelimuambia, mihasira ingemzidi na huenda presha ingempanda...humjui kaka alivyo, mimi namfahamu sana,....’akasema na kutulia kidogo.

‘Kiukweli, nilikuwa natafuta namna ya kuanzia, namna ambayo haitakuja kuleta ubishani zaidi hata kaka akijua, lakini sasa limetokea hili, nikawa ansita kabisa kumwambia, kwani ...’akasita kuendelea na wakili akasema

‘Sasa kwa hali kama hiyo unataka mimi nifanye nini...?’ akauliza wakili

‘Mimi nimekwambia tu...kama inaweza kusaidia kwenye hii kesi, basi fanya ufanyavyo, ila hala hala usije kuniweka kama shahidi au kutumbukiza madai yangu , ikaonekana kuna vita inakuja , ionekane kuwa sisi tulifanya hivyo kwa nia hiyo...natumai hapo umenielewa...’akasema

‘Sijakuelewa,....’akasema wakili akiwaza jambo,..halafu akasema;
‘Nikuulize kitu, baada ya wewe kumsimulia kaka yako yote yaliyotokea huko, je hakuna siku alikugusia kuwa anatamani kukutana na huyo mtoto wake, wayamalize...?’ akaulizwa

‘Haikuwahi kutokea, tunaweza kukumbukia yaliyotokea tukaongea hili na lile lakini hajawahi kusema anatamani akutane na huyo mtoto, au hata kuulizia vipi tunaweza kuwasiliaa na huko ulaya kuona kama anaendeleaje, yeye nahisi kwake ni kama.. hayupo..tatizo kubwa ni huko kwa mama yake....’akasema

‘Kwa mama yake, ina maana mama yake anamfahamu?’ akauliza

‘Anamfahamu, ...ni kipindi hicho hicho ...nilipowakutanisha, lakini kijana aliwakana,...na huyo mama nasikia kila siku ni kumtaja huyo mtoto, na nasiki siku za karibu, amekuwa akisema yeye keshahidi kuwa mtoto wake yupo mjini,...sijui alifahamu vipi.....’akasema

‘Mhh....unahisi kuna mtu alimwambia huyo, mama, kabla wewe hujafahamu kuwa huyo mtoto wenu kesharudi hapa Tanzania..?’ akaulizwa

‘Hapana, huyo mama anahisia za ajabu, yeye haoni vyema, lakini kwa mtoto wake anamuona, hata akiwepo kwenye kundi la watu, atasema huyu hapa ni mtoto wangu hakosei, sijui anafahamu vipi...’akasema

‘Hilo kwa mama tuliache kwa sasa twende kwa huyu kaka yako, je nay eye vipi kuhusu mtoto wake, maana huyu ndiye muhusika kwenye kesi,...’akasema

‘Kaka, si unajua wanaume tena, huenda moyoni lipo, lakini hajawahi kuhangaika kwa huyo mtoto, na kama lisingelikuwa hili tatizo, sijui kama angekutana naye,.....’akasema

‘Ina maana na wewe hukujaribu kufanya juhudi zozote kuona kama mnaweza kufanya nini ili kaka yako aje kumpokea mwanae, yaishe yaliyopita..maana ni lazima angerudi Tanzania, sizani kama angeliweza kuchukua uraia wa huko,....?’ akaulizwa

‘Hivi kwa hayo niliyofanyiwa huko Ulaya, hata kama ingelikuwa ni wewe ungefanya juhudi hizo...au mkuki kwa nguruwe?’  akauliza na wakili akakaa kimia, halafu Profesa akasema;

‘Huo ndio ukweli ulivyo, na kwa vile mimi niliondoka huko kwa mabaya, tukiwa hatuelewani kabisa na huyo kijana na washirika wake, sikuwa na huruma ya kuliongelea hilo, zaidi ya chuki na kisasi, kwahiyo,.sikuwahi kumuuliza kaka zaidi kama yeye ana mtizamo gani na mwanae, nahisi hata yeye alishamsahau,, sijui lakini, siwezi kuusema moyoo wake...’akasema

‘Na ulivyoongea na baba yake unahisi akija kuambiwa kuwa huyo ni kijana wake,  je kuna muelekeo wowote kuwa yupo tayari kumpokea mwanae akijirudi, akamsamehe?’ akaulizwa

‘Hilo kwakweli sielewi, ...kama nilivyokuambia, na hata kama itatokea hivyo, yeye akamsamehe, lakini  sio kwangu mimi...kwangu mimi kwa walichonifanyia, kutaka kuniua, sizani kama ninaweza kukaa meza moja na huyo kijana vinginevyo....sijui ...labda aje kukubaliana na masharti yangu....’akasema

‘Masharti gani hayo....?’ akaulizwa

‘Masharti,!....Hayo kwa hivi sasa sitaki kuyaweka wazi, ....’akasema na kukaa kimia

‘Kwahiyo kwa upande wako hutaki kumsamehe huyo kijana kwa hayo aliyokufanyia, sasa tutawezaje kulisawazisha hili, na mimi nilitarajia kuwa wewe ndiye utakuwa msaada wangu mkubwa kwa ajili ya kulisawazisha hili jambo...’akasema wakilli

‘Unajua hawa watu walijua kuwa mimi ni marehemu, na ndilo lilikuwa lengo lao, kwahiyo hadi wananileta huku walishajiamini wameshinda, maana marehemu atasema nini....na , nina uhakika watakuwa wamewasiliana na wenzao huko Ulaya, sijui wamekubaliana nini...’akasema

‘Sizani kama litawasumbua sana kwa vile wewe ulikubali mbele ya wakili wako....’akaambiwa

‘Wakili wangu au wakili wao, walimuweka ili kuweza kufanikisha mambo yao, ...mimi najua kabisa kama wakipata taarifa kuwa mimi bado nipo hai,  huko walipo matumbo yao yapo joto, hasa huyo mama Mtemi ambaye ni mama wa huyo mke wa huyo shahidi...unaona ilivyo...’akasema

‘Lakini hayo ya kwako na madai yako, tuyaweke pembeni, kwa hivi sasa jifanye kabisa kuwa umekubaliana na yaliyotokea huko, ...’akaambiwa

‘Ndio maana nikasema ya kwangu yaacheni kando kwanza, kwani nikayachanganya na hayo ya kaka, kama atakubali kuwa kitu kimoja na mtoto wake, mwisho wa siku tutakosana naye, tutageuka maaduni,nikianza vita vyangu.....’akasema

‘Je utasaidiaje hili la kaka yako, kama ikibidi,...maana huenda tunaweza kulitumia hili kama karata yetu ya mwisho mahakamani, vipi unaweza kusaidia kwa kumshawishi huyo kijana ili akubali kuacha hayo madai yake kwa namna nyingine.....?’ akaulizwa

‘Ndio maana sikutaka kwenda kuongea na huyo kijana kwanza, maana hatutaelewana naye kabisa,na humu mahakamani angesema hayo yamefanyika kwa sababu yangu mimi, kwa hivi sasa atakuwa hajaamini kuwa mimi nipo hai,...’akasema

‘Mimi sioni kuwa kuna tatizo kwa ajili ya kulisawazisha hilo, muhimu kwa hivi sasa uwe kitu kimoja na kaka yako, kwa nia ya kumweka sawa huyo kijana na unaweza kusema madai yako unasamehe,kwa ajili ya kesi ya kaka yako ifutwe...au?’ akaulizwa

‘Madai yangu,....niyasamehe...hahaha....,labda niwe marehemu...hilo halipo, hiyo ni nyumba yangu, waliipata kwa ulaghai walionitungia, yeye  ataiacha na nitakwenda kuishi kwenye hiyo nyumba, wewe utaona tu...’akasema na wakili alitaka kumuuliza swali lakini akatulia kwanza

‘Huyo kijana kwangu hana ujanja kule walikuwa wakimtegeme mama Mtemi, hapa bongo hawaniwezi, ..na kiukweli niliwazia hilo kuwa nitumie mbinu za hadaa kuwa , mimi niende nimshawishi kuwa yeye akubaliane kuachana na kesi ya baba yake, na mimi niachane na madai yangu, lakini kwanini nidanganye,’ akasema kama anauliza

 ‘Kwahiyo sasa wewe hapo unatakaje...?’ akaulizwa

‘Ndio maana nimekuwa kimia kuhusu maswala yangu, ....sikutaka kulichanganya hili na kesi ya 

Bro....na ndio maana  nilipogundua kuwa huyu kijana ni kijana wake, sikutaka kumwambia kaka hili mapema, ili kesi yake imalizike kwanza....’akasema

‘Je kaka yako anafahamu kuwa ulikuwa na lengo la kutafuta haki zako , kwa mfano kuhangaikia hiyo nyumba yako?’ akaulizwa

‘Hilo anafahamu, lakini hakuwa anafahamu kuwa wenye nyumba ni kijana wake, hata mimi nilikuwa sifahamu hilo, kama nilivyokuambia awali...’akasema

‘Kwa hali ilivyo, na jinsi kesi ilivyo,...mhhh, ngoja tusubirie mapambano ndani ya mahakama, ila nawaza jambo, kama itatokea kaka yako akahukumiwa kufungwa, au faini, au vyote, huoni kuwa itakuwa na uhasama mkubwa sana baadaye, hasa akija kufahamu kuwa huyo ni mtoto wake,.na wewe ulikuwa unafahamu...?’akaulizwa

‘Ndio maana nimeona nikuambie hili ili na wewe uone jinsi ganii ya kupambana, lakini kama kutakuwa hakuna shida, na kesi ikaenda vyema mimi bado nataka hili liwe siri, na nije kutafuta njia ya kulitatua huko baadaye mimi na kaka yangu, wakati huo nimesharudisha haki zangu zote....’akasema

‘Unajua kwa hivi sasa umenipa mtihani mkubwa....’akasema wakili akikuna kuna kichwa chake

‘Najua...’akasema Profesa

‘Nasema hivyo kwa maana hii, kesi hii imekaa vibaya, hii kesi ilikuwa ya jinai, na nilikuwa mbioni kutafuta njia ya kuifanya iwe ya madai  ya kawaida, na nilikuwa nawaza je hata kama ikakubalika, ikija kudaiwa mapesa mengi mtakuwa nayo..., kwahiyo hadi leo kabla hujaniambia hilo, nilikuwa na muelekeo huo,sasa umekuja na hili jambo .....’akasema wakili

‘Kama unaona hili litasaidia, mtoto kujua huyo ni baba yake,  na huyo mtoto atakuwa tayari kusamehe hiyo kesi, naona tumia hiyo ajenda mahakamani, kwa namna ambayo sitahusika, ...vinginevyo, kama hakuna ulazima liache kama lilivyo, nitajua jinsi gani ya kuliwasha huko ,mbele kwa mbele muda muafaka ukifika,...’akasema

‘Kwani kwa malengo yako, maana ni ngumu, kama ulikubali hilo mbele ya wakili wako mkasainishana, sijui...sijajua undani wake zaidi, maana sijui wewe ulipangaje, na una suhaidi au vielelezo gani vya kuja kukusaidia, ...hebu niambie wewe umepanga kufanya nini, ....?’ akaulizwa.

‘Unajua hilo tuliache kwanza,...nataka watu waje kufahamu kuwa mimi sio profesa wa bure bure,... nitakuja tuongee muda huo ukifika, kama utakubali kuwa wakili wangu, lakini sio kwa hivi sasa, ila kiukweli, mimi sina amani na huyo kijana,....keshanitoka, huyo ni adui yangu,kabisa.. yaani natamani muda ufike tu , ni hii kesi ya kaka tu, inaniwekea kiwingu, ikiisha tu, napuliza filimbi ya vita,  nitapambana na hao watu mpaka dunia ifahamu kuwa mimi ni nani....’akasema Profesa

‘Nikuulize kitu, kama itafaa, mtoto huyo wenu akaja kukubali kuwa kakosa na yupo tayari kumkubalia baba yake, utaendelea na madai yako hayo....?’ akaulizwa

‘Hahaha unauliza jibu,...nimeshakuambia msimamo wangu, lakini wewe kwa jinsi utakavyoona, ni sahihi umalizane na hii kesi, mimi na huyo kijana tutakutana mbele kwa mbele, muda ukifika, tuombeane uzima tu, na nikuambie kitu, kuna vitu nafuatilia, na hata siku hiyo ya kesi naweza nisiwepo au nikachelewa kufika. Kwahiyo usiponiona, usije kushangaa, nilishaongea na Bro.......’ akasema

‘Ina maana hutakuwepo kwenye kesi ya kaka yako, ukasikiliza nini kitakachendelea, ujue wewe ni muhusika muhimu kwake, hasa kwa haya yaliyotokea........?’ akaulizwa

‘Nitakuwepo kimawazo, nalifahamu sana hilo, lakini vitu hivyo ni muhimu sana kwangu, usijali, nitajitahidi kadri niwezavyo, nifike, japokuwa nitachelewa. Kwani wewe utanihitajia kama mmoja wa mashahidi wako, siku hiyo, sizani na naomba usifanye hivyo....?’ akauliza

‘Sijajua bado,.....’akasema wakili

‘Jitahidi isiwe hivyo, nisingelipenda kuwa shahidi....’akasema

Na hiyo kesi ilikuwa hivyo, je kaka mtu atalipokeaje hilo ombi, na nini hatima ya kijana wao , je nay eye atakuwa tayari kukaa kiti kimoja na baba yake wayamalize....


Tukutane sehemu ijayo,


WAZO LA LEO: Chuki, visasi haviwezi kulimaliza jambo,kama nafsi hazitariziana... hasa mali na madaraka vinapofanywa ndivyo kipaumbele , ugomvi wa mali, uchu wa madaraka, ubinafsi, huondoa kabisa utu na ubinadamu. Hii inatokea pale nafsi ya tamaa, na ubifasi, inapokua ndiyo inamtawala mwanadamu, inapofikia hatua hii usitaraji amani, usitaraji upendo, 

Inapofikia hatua hii basi ndugu kwa ndugu wanakosana, wanauana kwasababu ya mali na madaraka,  jamii hazitapendana, nchi kwa nchi zinaingia kwenye vita kwasababu ya mali na madaraka.  Ili kupambana na haya yote, tukumbuke jambo moja, je ukiyapata hayo yote utaishi milele, ...!

Je wewe ni wa kwanza, ..je wangapi waliondoka na mali na madaraka yao,hakuna, sasa kama ni hakuna wewe unataka nini.....?

Tukumbuke mwanadamu kaja hapa duniani na kila mmoja ataondoka hata iweje, hata uwe nani, na  kwanini basi usifikirie huko tunapokwenda tutakuwaje....utaenda kukutana na nini, na hii mali uliyoichuma hapa duniani, au madaraka uliyokuwa nayo hapa duniani, ?... 

Au wewe ni wale wasiamini hilo kuwa kuna maisha mengine baada ya haya...wewe unaamini kuwa ukifa ni basi tu....kama huamini kuwa kuna maisha mengine baada ya haya, basi wewe huamini kuwa mungu yupo, na hiyo ni hatari, ,... tuweni makini , tujirudi kwani muda tunao

Ni mimi: emu-three

1 comment :

Anonymous said...

Great website you have here but I was wondering if you knew of any user discussion forums that cover the same topics talked about here?

I'd really love to be a part of community where I can get advice from other knowledgeable people that share the
same interest. If you have any suggestions, please let
me know. Thanks!