‘Nimesema huyo sio baba yangu, huyo
sio baba aliyenizaa mimi, msiwasikilize hawa watu ni matapeli, ni waongo muheshimiwa hakimu .....’ilikuwa
sauti ya shahidi wakati hakimu alipowataka mawakili atete nao.
Na kwa muda huo hakimu hakimtilia
maanani kwani alishawaita mawakili na kwa muda ule walikuwa wakielekea mbele kukutana na hakimu, hata wakili
muendesha mashitaka hakutaka kumtuliza shahidi wake, akafuata amri ya hakimu.
Na mawakili walipofika mbele ya hakimu
wakaanza kuongea,...maongezi yao yaliichukua muda kidogo tofauti na
ilivyotarajiwa kuwa ni maongezi mafupi
ya hakimu kuonya au kutoa maelekezo fulani au kupata ufafanuzi fulani, ikawa ni
mabishano ya pande mbili, lakin hatimaye wakamaliza maongezi hayo,
Baadaye mawakili hao walirejea kwenye
nafasi zao, na hakimu akasema;
‘Nimeongea na mawakili wa pande zote
mbili na kutokana na unyeti tukio hili kwenye hii kesi ...kesi hii inaiharisha hadi siku
nyingine itakayopangwa....’akasema hakimu na kugonga kirungu chake, na kesi
hiyo ikaahirishwa,
Tuendelee na
kisa chetu
**************
Kesi
iliahirishwa, watu wakaanza kutoka kila mtu akiongea lake, mawakili wakawa
wamesimama kwenye nafasi zao, na kila mmoja akiwaambia watu wake wasiondoke
kwanza.
Wakili
mtetezi akasogea pale alipokuwa mshitakiwa kabla hajasimama kuondoka,
akamnong’oneza sikioni, na mshitakiwa akasimama na kutembea kumfuata wakili huyo , na wengine wakafanya hivyo hivyo hivyo.
Kundi hili
likawa limesogea mbali kabisa na kundi la muendesha mashitaka ambaye naye
alikuwa na watu wake , wakionekana kuongea mambo yao.
Na ilionekana
kuna ujumbe mnzito kutoka kwa hakimu , ujumbe ambao ulitakiwa ufanyiwe kazi na
mawakili hao kila mmoja na watu wake, na kutokana na umuhimu wake, mawakili hao walikuwa wakihakikisha watu muhimu hawaondoki, wakawa wanamsogelea kila mmoja aliyeoneka kutakiwa kwenye ja,mbo hilo
Na kwa muda ule shahidi, aliyekuwa akitoa ushahidi wake muda mchache uliopita, alionekana kuwa na haraka ya kuondoka na kwa jinsi alivyoonekana ni kama hakutaka kuongea
na mtu, usoni alionekana kukasirika, kinyume na walivyotarajia watu wengine ..
Wengi walitarajia kuona tabasamu au namna ya kutahayari kwa kile kilichotokea, kwani mtu huyo alikuwa kamgundua mzazi wake ambaye alikuwa hamfahamu labda
ingeonekana dalili ya yeye kujikurubisha kwa baba yake, na hata kuomba msamaha,
lakini dalili hiyo haikuonekana kabisa!
Shahidi huyu
hakutaka hata kumuangalia mshitakiwa, akatoka ile sehemu ya mashahidi na kuanza
kutembea akielekea mlangoni, lakini kabla hajakatisha sehemu walipokuwepo
muendesha mashitaka na kundi lake, akasimamishwa na muendesha mashitaka..
‘Usiondoke
kwanza kuna mambo muhimu ya kuongea na wewe...’akaambiwa na muendesha mashitaka,
akamwangalia muendesha mashitaka kwa uso uliojaa hasira, akasema;
‘Mambo gani ya
kuongea, ....kama ni kuhusu huyo mzee, sitaki kusikia lolote, na hata hii kesi naiona
haina maana tena, badala ya kunisimamia ukamshinikiza mshitakiwa naona
umemuacha wakili wao kunisakama tu, ....mimi sitaki tena , amueni mnavyotaka,
sitaki kabisa ,, .....’akasema akitaka kuondoka
‘Nataka
niwaambie alichoongea muheshimiwa hakimu, ni muhimu sana, na huwezi kuondoka
mpaka usikie maagizo hayo.....’akasema muendesha mashitaka
‘Kwanini,
kwani ni lazima, .....?’ akauliza na alipoona muendesha mashitaka kakaa kimia
akasema
‘Sawa,.... haya
sema ni mambo gani, hakimu kasema nini....?’ akauliza na muendesha mashitaka
akaendelea kukaa kimia, kama vile anatafakari
jambo
‘Muheshimiwa,
msimamo wangu ni huo huo, kama
ningelifahamu mapema kuwa ni hawa watu, sijui kama ningefika hapa, lakini
nimetii amri ya mahakama tu....’akasema akilalamika
‘Hawa watu ni
watu wakorofi, mimi nawafahamu sana, na
nijuavyo huyo anayeitwa Profesa alishafariki, nashangaa kusikia kuwa bado yupo
hai,....nahisi hawa watu ni mapacha, nina uhakika yule Profesa ninayemfahamu
mimi ni marehemu, kuna mchezo unachezwa hapa, sielewi...huu ni ubabaishaji
,...’akasema na muendesha mashitaka akawa anatoa ishara wengine wa upande wake
wasogee pale waliposimama.
‘Huyo profesa
ndio huyo huyo hakuna mwingine...’akasema wakili huyo
‘Una uhakika
gani, mimi namfahamu maana niliishi naye, na alirejeshwa huku nchini akiwa
mahututi hajiwezi, na ....aliambiwa hatamaliza wiki, na watu waliomleta
walirudi wakisema walimuacha akiwa anakata roho......’akasema
‘Na zaidi
ikaletwa taarifa kuwa ameshafariki...niliambiwa na watu wenye uhakika mpaka
watu wakawa wakionana na mimi wananipa pole
ya msiba...’akasema
‘Ni taarifa
zisizo na ukweli, kwanini hukuaniambia kabla,..nikaweza kulifuatilia kwa undani....’akasema
wakili huyo
‘Nikuambie
kitu, sikujua kuwa ni hiyo familia, sasa nimejua kama kweli ndio wao wenyewe,
muheshimiwa unatakiwa uwe makini hao watu ni matapeli, waongo,...’akasema
akimuangalia huyo wakili.
‘Ndio maana
nataka tuongee, nijue chanzo cha haya yote, ilikuwaje, ....na mwisho tuje tukubaliane na kuna mambo zaidi niweze kujua la
kufanya kabla hatujaedelea zaidi...ila kwanza ni muhimu tuhakikishe
tunalimaliza hili...’akasema
‘Mimi sioni
kama kuna zaidi.....kesi iendelee hao watu wawajibike...ili mimi niishi kwa
amani....hili lililojitokeza halina msingi kwangu kabisa...’akasema
‘Halina
msingi kwako,...? akauliza wakili kwa mshangao
‘Ndio,....’akasema
kwa kujiamini
‘Aaah, ngoja
kwanza, unajua alipotuita muheshimiwa hakimu, alilichukulia kuwa wewe kwako
itakuwa kama mshituko kama kweli ulikuwa huwafahamu hao watu kuwa ni familia yako,
kwahiyo ni vyema tukakaa tukalimaliza hili, na huenda hilo likaleta faraja, na
haya mengina yakawa hayaa maana tena, ila kuna sababu ya kutoa adhabu kwa
mkosaji, lakini hilo lije baadaye,..kwahiyo mimi nataka nikusikie wewe
unasemaje.....’akasema.
‘Mimi naona
hakimu,...simuelewi.....’akataka kuongea jambo lakini akakatisha.
‘Hakimu
kachukulia hekima zaidi, ...hili jambo limemgusa yeye kama mzazi, ....mwanzoni
kama muendesha mashitaka nilijitahidi kulipinga nikisimamia kwenye kosa
lenyewe, kwani nilikuwa na vigezo vyangu, lakini ilifika sehemu nikaona kweli kuna
haja ya kuliangalia hili jambo kwa macho mawili.....’akasema akimuangalia huyo
shahidi
‘Jambo
gani...? wakati msingi wa kesi hii ni vurugu, kujeruhi, je hayo hayakufanyika,
ushahidi haupo?, kuna jambo gani zaidi ya hilo...muheshimiwa mnataka nini zaidi?’
akauliza akionyesha kushangaa
‘Ndio kuna
kesi hii ipo mikononi mwangu, lakini bado nina hisia zaidi ya hii kesi, wakati
mwingine kunatokea jambo kati kati ya kesi, na kuleta maulizo mengi, na hapo unatakiwa
utumie hekima zaidi,....’akasema
‘Hekima! .....una
maana gani kusema hekima itumike, ? ina maana hekima ni zaidi ya sheria au...?’
akauliza shahidi huyo
‘Kwenye kesi
hii lilipojitokeza hili jambo, wengi tulishikwa na mshangao, unajua
hukuaniambia hili kabla...sasa alipoliongelea muheshimiwa hakimu nikana kuwa
haja kweli ya kupata uhakika,...kutoka kwako....’akasema
‘Uhakika....!
uhakika upi?’ akauliza kwa mshangao,
‘Ndio ni
lazima kwanza nipata uhakika kutoka kwako, jinsi gani ulivyolipokea hili, ikizingatiwa
kuwa huyo ni mzazi wako, na inaonyesha wewe ulikuwa humjui,,....limekuja kama
jambo la kushitukizia, kiukweli, mimi limenigusa kama mzazi, hata hakimu imekwa
hivyo hivyo, japokuwa hajaongea moja kwa moja,...’akasema na shahidi akabakia
kimia
‘Ndio maana imenibidi niwasikilize , sio kwamba nimekubaliana na
upande wa utetezi, hapana, ila hili kwanza liwekwe sawa, ili tufanye yaliyo
sahihi,...kisheria kwa upande mmoja lakini pia kiubinadamu kwa upande mwingine...’akasema
muendesha mashitaka na shahidi huyo akawa kama katahayari, akasema;
‘Kwahiyo unataka
kusema nini muheshimiwa...., ina maana na wewe unakubali kuwa aliyoyafanya huyo
mzee ni sahihi, kuja kuleta vurugu, kuumiza watu, kwa vile tu ni .....ni mtu
mzima, kwa vile tu imekuja hiyo hoja, huoni kuwa wamekutega, huoni kuwa lengo
lao ni kupoteza muda, ,..?’ akauliza
‘Sijasema
kuwa alichokifanya ni sahihi, hili kisheria lipo pale pale mtenda kosa hata awe
nani, sheria itafuata mkondo wake, ...’akasema
‘Sasa ni
kwanini...ni kwa vile imesemwa kuwa yeye huenda akawa ni baba yangu, ....huo ni
uzushi tu, haina ukweli, ni utapeli tu,, kwanza mimi sijakubaliana na hilo kuwa
yeye ni baba yangu.... je ndio hilo unalotaka kuliongelea au?’ akauliza kwa
mshangao
‘Kwanza
unielewe, sijasema kuwa hakuna kosa, alichofanya mshitakiwa ni kosa, ikihukumiwa
hivyo mbele ya mahakama, na ndio maana baada ya kujirizisha kuwa mshitakiwa
atakuwa katenda kosa nikaamua kuisimamia hii kesi, ...’akasema
‘Si ndio
hivyo, basi kwanini mnagwaya kuchukua hatamu, kwanini hakimu anaipiga hii kesi
kalenda, kama kashindwa tunaweza kuomba hakimu mwingine mimi sina muda wakuja
kupoteza hapa, nina kazi zangu, nina mambo mengi kweli kweli,ya kufanya......’akasema
‘Nikuulize
swali,....wewe umejisikiaje ulipoambiwa huyo ni baba yako?’ akaulizwa
‘Vibaya sana,
nimejiskia vibaya sana...nikuambie ukweli, nilitamani nitoke pale kizimbani
nikimbie,...sikufahamu kuwa hili jinamizi linazidi kuniandama...’akasema
‘Kwanini...?’
akaulizwa wakili huo akishangaa
‘Kwasababu....ni
hadithi ndefu...siwei kukuambia ila hayo ya nyuma achana nayo tugange haya ya
sasa hivi....huyo mzee aah...’akasita kidogo na muendesha mashitaka akasema;
‘Ndio maana
sisi kama mawakili, tumeliona hili kwa namna nyingine kuwa pamoja nah iii kesi
kuna mambo yamejificha ambayo tusipoyatatua kwanza tukakimbilia kushindana
kisheria na kimahakama tunaweza kuleta mtafaruku mkubwa huko mbele, ....’akasema
‘Kwa vipi, na
wakati kesi ipo wazi..’akasema
‘Limejitokeza
hili swala, katikati ya kesi, na sisi kama wazazi,limtugusa, tukaona ni swala
linahitajika kusawazishwa kwanza, kwa mustakabali wa mahusiano mema kati ya
mzazi na mtoto..’akasema.
‘Mimi
sikuelewi hapo, hilo la .... linahusiana vipi na uvunjifu wa sheria,....?’
akauliza
‘Wewe ulikuwa
humfahamu mzazi wako sio...?’ akauliza wakili
‘Hahaha, hivi
nyie watu vipi, ina maana mnafumbia macho shera kwa vile umeambiwa huyo ni
mzazi wangu, na hata hujalithibitisha hilo, hivi wewe muheshimiwa hilo ndilo
liharibu kesi ya msingi, hapana, mimi siwaelewi, kwanini,......?’ akauliza
‘Ndio maana
nataka kusikia kutoka kwako, ukweli wote ulionao wewe....usilichukulie hili
jambo kwa mzaha, hili ni jambo nyeti sana, pamoja na ya kuwa kuna uvunjifu wa
sheria, lakini....’kabla hajamaliza shahidi huyo akadakia na kusema;
‘Unaona eeh,
mimi nahisi umeongea na hao watu wamekuweka sawa useme,wanavyotaka wao, au
sijui umewaogopa hao wazee, unaogopa kulogwa, au.na hakimu mbona simuelewi,
hawa watu vipi,....mimi nataka haki yangu...na nilitaka hili jambo limalizike
kwa amani, lakini kwa hali hii, ...ndio maana sikutaka kuja hapa, ‘akasema
‘Kwahiyo wewe
unatakaje....?’ akauliza wakili
‘Ninatakaje...!?...unaniuliza
hilo swali mim tena,..hohoho....!’ akaliza kwa mshanga
‘Ndio,
....nakuuliza hivyo nikiwa na maana, ...nilijua utabdili mawazo baada ya
kusikia hivyo, na nilijua utafurahia sasa hili swala tulimalize hivi
kimazungumzo zaidi ,yaani wewe mje mkae
na baba yako, muelewane, yaishe yaliyopita, huoni ni furaha kwako, umemuona
baba yako ambaye ulikuwa humfahamu..’akasema wakili
‘Kweli wewe
unazungumza hivyo, wewe mwenyewe uliniambia hii ni kesi ya jinai,sio kesi ya
madai, mkosaji katenda kosa bay asana...leo hii unaongea mengine, ...kuna kitu
gani kinaendelea...?’ akauliza kwa mshangao
‘Unielewe
kijana....’akasema wakili na shahidi huyo akamkatisha na kusema
‘Unasikia
muheshmiwa, mimi sitakubali, .....nataka huyo mzee awajibishwe,afungwe...kwa
kosa alilofanya,.....iwe fundisho kwa wazee kama hao....’akasema
‘Oh, siamini,
kuna nini kati yako na huyo mzee,...kwani ulikuwa unamfahamu kabla, ina maana
haata kama ni baba yako...mzazi, upo tayari afungwe?’ akaulizwa
‘Nani kasema huyo
ni baba yangu...sio baba yangu huyo, hao ni waongo kabisa..na kwani hakufanya
kosa...’akasema
‘Nahisi hapa
hujakubali kuwa ni baba yako mzazi au sio, Je ikidhihiri kitaalamu kuwa huyo ni
baba yako mzazi utasemaje...?’ akaulizwa
‘Utaalamu kwa
vipi...muheshimiwa mimi sikuelewi,....?’ akaulizwa
‘Kuna vipimo
vya kulithibitisha hilo..kuthibitisha kuwa huyo kweli ni baba yako mzazi.’akaambiwa
‘Unasikia
mimi sitakia kabisa kupimwa, maana moyoni najua huyo ni baba yangu, ..hata kama
mtapima, mpime ili iweje,..kinachotakiwa ni nini, vipimo au moyoni mwangu.
Najisikiaje kuhusu hao watu, niwaambie ukweli, vyovyote mtakavyofanya mnajisumbua,..’akasema
‘Nikuulize
kwanini hutaki, kwanini humtaki baba yako,..niambie ukweli, ili nijua cha
kufanya, maana mimi ni muendesha mashitaki, ni haki yako kudai fidia, ni haki
yako kama umetendewa kinyume na sheria, sheria ichukue mkondo wake, kuna nini
hujaniambia....?’ akauliza
‘Kila kitu
nimeshakuambia,..hawa watu ni wakorofi, sasa hivi wananitishia amani,
wanadiriki kusema kama nisipoondoka kwenye hiyo nyumba nitapata
mabaya.....nikajua kumbe lengo lao lao sasa ni nyumba!, ...sasa unaona ilivyo,
kwahiyo nikilogwa tu nikakubali tu kuwa hao ni wazazi wangu, watakuja na ajenda
nyingine ya kudai nyumba,mimi naona mbali ....’akasema
‘Nakuuliza
tena hili swali, je upo tayari kumuhukumu baba yako aende jela,...hata kama
umethibitisha kuwa kweli huyo ni baba yako mzazi?’ akaulizwa
‘Kama kafanya
kosa sheria ichukue mkondo wake, sheria haingalii baba au mtoto, au sio,
nimekosea hapo,...? Ukitenda kosa uwe baba au mtoto utahukumiwa ipasavyo, wewe
ni wakili unalifahamu hilo, au sio.?...sasa kwanini mnataka kupindisha
sheria...’akasema
‘Unajua
kwanini sisi tumefikia hatua hiyo, ni kuwa wewe ulikuwa huwafahamu wazazi wako,
na mzazi wako alikuwa hakufahamu,...limetokea hili ambalo linaweza kuleta
uhasama mkubwa, kwa mzazi wako kuja kujenga chuki dhidi yako,...sasa tukaona
tuking’ang’ania sheria, haya tusema huyo mzee afungwe, unafikiri ni nini
kitafuata baadaye, si chuki, visasi, na wewe hutakuwa na maisha mema, hili
nakuambia kiukweli,....’akaambiwa
‘Hahaha...wewe
ni mtu wa ajabu sana, siamini, hivi sheria zina makengeza....hapana
siamini,....mimi nadai haki yangu, nimetendewa makosa halafu nimefuata sheria,
tena mimi nije kusha maisha yasiyo mema, mlitaka nichukue sheria mikononi
mwangu au....’akasema akitikisa kichwa kwa kushangaa
‘Ni kweli
sheria ipo, na ni kweli sikutakiwa kuangalia hilo,...kuwa ni nani kafanya
kosa,... ila hili tunaweza kulisawazisha kwanza, kuhakikisha kuwa wewe
unamtambua baba yako,...halafu baadaye tutaangalia sheria inasemaje,....’akasema
‘So what....’
akauliza.
‘Ili kuondoa
chuki kwenye familia, ili wewe na
familia msije kuwa maadui wakubwa...wewe ni mtoto, huoni ni jambo la ajabu sana
kugombana wewe na mzazi wako, halafu uje umfunge, hii ni hatari, sio vizuri, unaweza ukapata
matatizo makubwa sana....’akaambiwa
‘Matatizo
makubwa kama yapi, kwani mimi nimekwenda kuleta fujo nyumbani kwake...? mimi
nina kosa gani, niambie, kwani mimi nimekwenda kudai kuwa niwe mrithi wa mali
yake, , ..sijafikia au kufikiria hivyo,...’ akasema
‘Sio hivyo
unavyofikiria wewe....’akasema wakili
‘Sio hivyo,
sasa wanataka nini kwangu,,..nikuambie kitu, nimehangaika mwenyewe na maisha
yangu hadi hatua hii unayoiona ninayo,...nimefika ulaya kama chokoraa, sina
baba wala mama, wasamaria wakanilea,....wakanisomesha, .. sikumuona baba wala mama,leo hii kwa
vile....muheshimiwa, mimi nawastahi sana, lakini anyway....’akasema akitaka kuondoka
‘Sikiliza
wewe ni sawa na mtoto wangu, nikuase hili,..nafahamu wewe hujui mazara ya haya
yote, ni bora ukubali kwa hivi sasa, hata kama moyoni mwako haujaridhika kuliko
kukataa moja kwa moja,...nikuambie ukweli utayaona maisha ni magumu na
utawatafuta hao wazee usiwaone utakuja kujuta wakati umeshachelewa.....’akaambiwa
‘Watafanya
nini, wataniloga,...kwani hawajavuna sheria muheshimiwa,hata Mungu halioni
hilo,... hebu acha imani potofu hizo wewe ni mwanasheria hukumu kutokana na
vipengele vya sheria mambo mengine niachie mimi mwenyewe, ..kama maisha magumu
kwani itakuwa mara ya kwanza, nimelelewa na nani....’akasema
‘Sikiliza
nahisi wewe hujaamini kuwa huyo ni baba yako, tunahitaji tulithibitishe hilo
kitaalamu....unasemaje..?’akaambiwa
‘Kwa vipi?’
akauliza
‘Tutachukua
damu yako tupime na huyo mzee, tuone kuwa kweli ni baba yako na kama sio baba
yako hapo tutajua kweli familia hiyo ni ya matapeli...watafungwa wote....unasemaje
kuhusu hilo....?’akaambiwa
‘Mchuke damu
yangu, hahaha.....hilo halipo na sitaki kabisa...na ili iweje kwenye sheria za
makosa kama hayo kuna kipengele kama hicho, kuwa ikitokea mtoto kamshitakia
mzazi, kwanza ithibitishwe ...kuwa kweli ni mzazi wake, ipo hiyo....’ akawa
kama anauliza.
‘Ndiyo ili
tuweze kulithibitisha hilo, huoni na wewe litakusaidia ili uwe na maamuzi yenye
kujirizisha, ni kweli siku hizi watu wanaweza kutunga uwongo tu kwa masilahii
....nakubaliana na wewe,sasa ili sote tujirizishe ngoja tufanya
hivyo....’akasema huyo muendesha mashitaka
‘Nafikiri
hujanielewa, na naona hamtanielewa, ninachoona ni mimi kuondoka zangu,....nina
mambo mengi ya kufanya siwezi kukaa hapa tukipoteza muda tu, ni nini tutakipata
hapa baada ya haya yote hapa, ...’akaonyesha
mikono kama kukata tamaa
‘Hataupotezi
muda kabisa ni jambo jema na hili tunalifanya kwa nia njema kabisa....’akasema
‘Tunapoteza
muda kabisa hapa,....hebu nambieni, kuna faida gani hapa, kama nyie watu wa
sheria hamtaki kutimiza wajibu wenu,.... ndio maana tunazidi kuwa na watu
wakorifi, magaidi kwa vile nyie watendaji mnawalea tu...., kuongea kuongea,,
...inanisikitisha sana, ..’akasema akigeuka huku na kule kama kutaka mtu wa
kumuunga mkono
‘Nielewe
kwanza....’akataka kuongea huyo wakili
‘Kosa
limefanyika lipo wazi, ...hamtaki kuchukua hatua,...we are wasting our time for nothing, men, am faded up....mimi sasa naondoka
zangu.....’akasema na kuanza kuondoka
‘Subiri, hii
ni amri ya mahakama, ni muhimu unatakiwa kutii amri hiyo, tuna mambo ya kukamilisha kabla hujaondoka, ni
lazima tuhakikishe tumekubaliana hili jambo, ili tuwesze kumwambia muheshimiwa
hakimu tumafikia wapi,.....’akasema wakili
‘Mambo gani
hayo,ya kukubaliana wakati nyie mnanilazimisha, mimi sijakubaliana na nyie, na
sitakubali kwa hilo, kama mnataka iwe hivyo mtakavyo nyie, kupotezea hilo kosa,
na haki yangu ipotee hivi hivi, mimi sipo na nyie kabisa, mkitaka kuamua nyie
kwa ubabe wenu, fanyeni, lakini sio kusema mimi nimekubaliana na nyie hapana....’akasema
‘Kijana,
....mimi siwezi kukulazimisha kuwa ukubaliane na mawazo yetu, sisi tuliona
labda tufanye hivyo, ili kuwaunganisha kwa nia njema, wewe na baba yako ambaye
ulikuwa humfahamu,..kumbe hutaki.’akasema muendesha mashitaka
‘So what.....?’ akauliza
‘Tulijua labda
kwako itakuwa ni faraja kumpata mzazi wako,..kumbe wewe hutaki, hutamki mzazi
wako,..inashangaza sana,..’akasema wakili akitikisa kichwa
‘Nakuuliza
ili iweje, ..kama sheria imevunjwa na ni kosa kwanini tufumbie macho, ..hivi
ina maana gani ya kupoteza siku zote hizo mhakamani, gharama muda, ...hilo
mbona hamliangalii, ningelikuwa na uwezo, ningewaondoa tuweke watu wenye kujua
wajibu wao..’akasema
‘Sikiliza
kijana kama wewe hutakubaliana na wazo
letu hilo basi, sisi tutatimiza wajibu wetu, na mwamuzi ni hakimu, kama mzazi
wako atapatikana na hatia, basi atafungwa,na halikadhalika kama itakuwa kinyume
chake, sheria itafuata mkondo wake,na wewe utawajibika vile vile, ...’akasema
‘Sikuelewi
muheshimiwa ina maana sasa wewe unageuka kuwa mtetezi wa huyo mshitakiwa
au...niambie ili nijue ...kama itakuwa kinyume chake kwa vipi, kwani hakufanya
fujo, hawakumjeruhi mtu, kwanini unazungumza hivyo, kunitishia au....’akasema
‘Nakuuliza
tena, je upo tayari.mzazi wako afungwe....maana sitapenda baadaye yatakayotokea
niwe wa kulaumiwa,...?’akaambiwa
‘You know, sizani kama tutaelewana hapa, ..am sory, mimi naondoka.....’akasema huyo
shahidi na kuanza kuondoka, na wakili huyu muendesha mashitaka akawa anatizama
upande wa pili alipomuona mama mmoja akiongea na wakili mtetezi, akawa
anakumbuka mama mmoja aliyeonekana na matatizo ya macho akiwa kaongozana na
binti mmoja, akaikumbuka ile sauti yake ikisema.....
‘Muokoeni
mwanangu....ifuteni hiyo kesi kwani inaweza kuleta matatizo makubwa ....;
kipindi hicho alikuwa na haraka na kesi nyingine hakuweza kumsikiliza zaidi,
leo anamuona pale akiongea na wakili mtetezi
‘Huyu anaweza
pia kuwa ni mama yako mzazi, je mama yako mzazi naye humfahamu,...’ akauliza
kumbe alikuwa akiongea peke yake, kwani shahidi yule alishaondoka
‘Wewe...rudi
hatujamalizana.....’ alikuwa keshachelewa
************
Wakati hayo
yakiendelea upande huo, huku kwa upande wa mshitakiwa na wakili wake napo
kulikuwa na maongezi kama hayo yakiendelea, wakili mtetezi alikuwa akielezea
kile walichoongea na hakimu; na sasa alikuwa akiongea na mshitakiwa, ambaye
sasa tumegundua kuwa ni mzazi wa shahidi.....
‘Je mzazi
huyu atasemaje baada ya yote hayo yaliyotokea.....
Tuishie hapa,
tutakuja kuona upande huo kulitokea nini, na je mama atasaidia nini...,
WAZO LA LEO: Hekima inaweza kuwa msaada mkubwa
kwenye majanga mengi ya mifarakano inayotokea hivi sasa duniani, kuliko vita na
kumwaga damu...na mara nyingi imeonekana kuwa kiini cha matatizo mengi kakipewi
kipaumbele, kinachoangaliwa zaidi ni tatizo lenyewe, ubabe, na masilahi.
Na wakati mwingine matatizo hutengenezwa ili
ubabe uchukue nafasi yake kwa masilahi ya wenye hisa! Tunasahau kuwa Hekima na busara ni silaha njema kwa muafaka wa
kudumu kwenye matatizo yoyote, kuliko kutumia ubabe na minguvu ambayo hujenga
chuki na visasi visivyoisha.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment