Siku ikafika
na kesi ikabidi ifanyike, baada ya juhudi ya kutaka kesi hiyo ifanyike nje ya
mahakama kushindikana, baada ya juhudi ya kuwakutanisha wahasimu hawa wawili mshitakiwa
na mlalamikaji kushindikana, na wakili ambaye alijitahidi sana kuona jambo hilo
linamalizwa kwa amani ikafika mahali akasema kashindwa ,iliyobakia mahakama
ndiyo itaamua, ...
‘Ndugu yangu
wewe ni rafiki yangu, nakumbuka ulinisaidia sana dawa kipindi kile naumwa sana
pumu, na ugonjwa huo nimeshausahau,...nakumbuka ulinisaidia mengi enzi zile,
ndio maana nikihakikisha nafuatilia hili swala lenu nione kama litaweza
kumalizwa kwa amani, lakini naona imeshindikana....’alisema wakili akiwa kashikilia
barua mkononi
‘Lakini
hujaongea na hakimi ukamuelezea hali halisi,unaona kaka yangu
anaumwa.....’akasema Profesa
‘Sasa hivi
nimetoka mahakamani na nimepewa barua hii, kuwa kesho kutwa ni siku ya
kusikiliza kesi yenu....’akasema
‘Na
nilijaribu kuongea na waendesha mashitaka , wao ndio kabisa hawataki mazungumzo
yoyote kwani wao wanadai kuwa wana ushahidi kuwa tendo lililofanyika lilikuwa
la kudhamiria, na pia kumekuwa na vitisho kwa wenye nyumba, ambao ndio
walalamikaji ....’akasema
‘Lakini hivyo
vitisho ni nani amevifanya mbona sisi hatujawahi kufikiria kufanya kitu kama
hicho...?’ akauliza profesa
‘Wao wanasema
wana ushahidi kuwa nyie ndio mnaofanya hivyo,...mumetuma watu kuwatishia amani,
na sasa hivi wanaishi kwa hofu,.... ndio maana wanataka kesi hii ifanyie hukumu
itolewe ili iwe fundisho kwa watu wasiotii sheria....’akasema wakili
‘Hakuna namna
nyingine ya kusaidia hii kesi, maana kama kesi ni kesho kutwa, na barua
imeshotoka, unafikiria sisi tutafanya nini...je tutawezaje kushinda....’akasema
Profesa akionyesha kukata tamaa.
‘Yote sasa
inategemea mashahidi wao wa mwisho ambao watahitajika kufika kuthibitisha hilo
tukio, kwani siku za kesi zilizopita walifika walinzi tu, sasa wenye nyumba
wanahitajika kufika kuthibitisha hilo kuwa hivi sasa wanaishi kwa hofu kwa
kutishiwa amani...’akasema
‘Kwahiyo
tufanyeje...kwa hivi sasa na hali ya kaka kuna siku inakuwa mbaya,...siku
nyingine nzuri, haeleweki nahisi ni kutokana na hii kesi?’ akauliza profesa
‘La kufanya
hakuna kwa hivi sasa....labda nikusikilize wewe, ulisema kuna jambo ulitaka
kuniambia ...ni jambo gani hilo....?’akasema wakili na kuuliza
‘Mhh...ni
kweli kuna jambo ninalotaka kukuambia, sijui kama litasaidia, ni jamboo ambalo
sikupenda lijulikane kwa hivi sasa, kwani linaweza kuendeleza chuki badala ya
kusaidia lakini kwa hali ilivyo sasa ni bora nikuambie ili uone kama linaweza
kusaidia kwenye hii kesi, japokuwa kwa jinsi ninavyomfahamu huyo jamaa sizani
kama ataweza kulichukulia maanani...’akasema Profesa
‘Ni jambo
gani....lolote laweza kusaidia lakini mpaka nisikie ni jambo gani?’ akauliza
wakili, na
Profesa akaanza kumuelezea jambo hilo kwa kirefu
Tuendelee na
kisa chetu
******************
Kesi ilianza
kwa taratibu zake na waendesha mashitaka wakatakiwa kutoa mashahidi wao ambao
walihitajika siku hiyo, na ndipo akaitwa shahidi ambaye alijitambulisha jina na
baada ya taratibu za kimahakama kufuatwa, na baada ya kutaja jina lake akaanza
kuulizwa maswali...
‘Haya tuambie
wewe siku ile ya tukio ilikuwaje...?’ akaulizwa
‘Mimi
nilitokea kazini na nilipofika getini, nikapiga honi kama kawaida na wakati
geti linafunguliwa mara akatokea mtu mbele ya gari langu akiashiria nisimame,
na baadaye mtu huyo akasogea kwenye kiyoo cha gari na kuanza kugonga kwa
nguvu....’akasema
‘Alikuwa
akigonga na nini....?’ akaulizwa
‘Ni jiwe
alilokuwa nalo mkononi...’akasema
‘Alikuwa akigonga
kiyoo na jiwe...?’ akaulizwa
‘Ndio, ndio
maana nikafungua mlango kwa hasira,...na nilipotoka kwanza niliangalia mlinzi
yupo wapi,...., maana nilishaingiwa na wasiwasi, na muda ule mlinzi alikuwa kwa
ndani akifungua geti, likawa wazi, na mlinzi alipomuona huyo mtu kasimama
pembeni ya gari langu, akaja , na kwa muda huo na mimi nikawa nimeshatoka nje
ya gari.....’akasema
‘Ukisema huyo
mtu una maana gani...?’ akaulizwa
‘Mshitakiwa
huyo hapo...’akasema akimnyoshea mkono mshitakiwa
‘Ikawaje?’
akaulizwa
‘Nilishikwa
na butwaa pale nilipomuona mlinzi wangu akivuja damu.....’akasema
‘Akivuja damu
sehemu gani...?’ akaulizwa
‘Kichwani,....’akasema
‘Ukafanyaje...?’
akaulizwa
‘Kiukweli
nikahisi kuna jambo la hatari, nikamuuliza mlinzi kulikoni maana alihitajika kupata
huduma ya kwanza, kwa jinsi alivyokuwa na damu,... lakini huyo mshitakiwa
hakunipa muda huo akaniandama kwa madai yake , ..’akasema
‘Madai gani
hayo....?’ akaulizwa
‘Anasema
alikuwa akitaka kuongea na mwenye nyumba kwani kuna ndugu yake kaambiwa aliwahi
kuingia humo ndani, na kuhusu mlinzi kwanini anavuja damu akasema ni kwasababu alimfundisha
adabu kwa vile hakuwa na majibu mazuri kwa wageni........’akasema
‘Ni kweli
kuwa kulikuwa na ndugu yake humo ndani?’ akaulizwa
‘Kulikuwa
hakuna mtu yoyote humo ndani kwa siku hiyo, ...’akasema
‘Sasa kwanini
akasema hivyo?’ akaulizwa
‘Kwa maelezo
yake nikakumbuka kuwa kuna jamaa mmoja alifika siku tatu kabla ya tukio hilo,
jamaa huyo alifika akijifanya yeye ni profesa, na kwa vile mimi nilikuwa
nimetarajia kutembelewa na rafiki yangu wa chuo kikuu ambaye ni profesa nikajua
ndio yeye, kwahiyo mlinzi aliposema kuna mgeni wangu profesa sikusita kumwambia
amruhusu, na mara akatokea jamaa mmoja ambaye kwa maelezo niliyoyapata baadaye
ndiye aliyekuwa akitafutwa na huyu mshitakiwa....’akasema
‘Huyo jamaa
alikuwaje?’ akaulizwa
‘Huyo jamaa
alikuwa mgonjwa kwa jinsi alivyoonekana, mimi sikuweza hata kuongea naye, kwani
nilikuwa nje siku hiyo, nilipoingia kwa ndanii ili niweza kuongea naye, mara
ghafla al
akadondoka na
kupoteza fahamu ikawa ni kazi ya kumpeleka hospitalini, tukamtibia kwa gharama
zetu japokuwa hatumfahamu...’akasema
‘Kwahiyo
shahidi kwa jinsi ulivyosikia alisema alikuja kumuona huyo jamaa yake mgonjwa?’
akaulizwa
‘Hayo sasa
tulikuja kuambiwa baadaye, ...’akasema
‘Kwanini
alitumia nguvu badala ya kuulizia yaliyotokea kwa huyo ndugu yake, ..?’
akaulizwa
‘Mlinzi
alisema jamaa huyo hakutaka kuhojiwa, yeye aliofika alielekezwa wapi ndugu yake
you hositalini kama tulivyoacha maagizo, lakini mshitakiwa yeye alidai
anachotaka ni kuingia ndani na kuonana na wenye nyumba, na katika heka heka za
kumwelewesha huyo mshitakiwa yeye kwa
ghadhabu zake akakimbilia kumiga mlinzi, ......’akasema
‘Ni kwanini
ampige mlinzi ...?.’akasema
‘Ndio hapo
mlinzi alishikwa na butwa kwani mlinzi wakati anarudi kwenye lindo lake ,
mshitakiwa ndiye alimvamia kwa nyuma,....
‘Je unahisi
labda jamaa huyo alifanya hivyo kwasababu ya kuchanganyikiwa kuwa labda ndugiu
yake kashikiliwa humo ndani?’ akaulizwa
‘Hapana
ilionekana kabisa jamaa alifika hapo kwa shari,...kwani alielekezwa wapi ndugu
yake yupo kama angekuwa akimjali ndugu yake angekimbilia hospitalini
kumuangalia, lakini yeye alitaka kuingia ndani wakati sisi wenye nyumba hatukuwepo,
na kwanini alishikilia jiwe, ....’akasema
‘Je kuna
mambo gani mengine yalikuja kutokea baadaye kuonyesha kuwa jamaa hakuwa na nia
njema ...’akasema
‘Baada ya
hilo tukio, walifika askari, na walimkuta akiwa anapambana na mlinzi wangu, na
mimi nikiwa najaribu kumtuliza, hakusikia akaendelea kumpiga mlinzi, maaskari waliokuja
siku hiyo wanaweza kulithibitisha hilo...’akasema
‘Wakati
anafanya fujo alitamka maneno gani labda?’ akauliza
‘Alisema na bado
nitahakikisha mnahama kwenye hii nyumba,.....’akasema
‘Unahisi
kwanini alisema hivyo?’ akaulizwa
‘Kiukweli
sijui, maana hata huyo ambaye anadai ni ndugu yake wakati anaongea na walinzi,
walinzi waliniambia alizungumzia maswala ya nyumba, sasa sijui walikuwa na lengo gani na nyumba....’akasema
‘’Kwani wewe hiyo
nyumba ni yako?’ akaulizwa
‘Ndio hiyo
nyumba ni nyumba yangu, niliinunua nikiwa ulaya kwa pesa zangu, kwani nilijua
nikirudi huku nyumbani, nahitajika kuwa na nyumba yangu mwenyewe, nina hati
zote za umiliki ....’akasema
‘Ulinunua
kama ilivyokuwa au ulinunua kiwanja?’ akaulizwa
‘Nilinunua
ikiwa na nyumba ndogo tu, nikaijenga upya kama ilivyo sasa, .....’akasema
Baadaye akaja
wakili mtetezi, na kuanza kumuhoji huyo shahidi
‘Unasema
ulipofika getini kwako ulishangaa kuona mtu kasimama mbele ya gari lako na
kugonga kiyoo kwa jiwe,...’unaweza kuonyesha jinsi alivyogonga kwa jiwe
‘Nipeni jiwe
nionyeshe alivyogonga.....’akasema na watu wakacheka
‘Unamuona
yule pale mshitakiwa ni mzee wa miaka zaidi ya sitini, anaweza kweli kufanya
jambo kama hilo?’ akaulizwa
‘Swala sio
umri, mtu anaweza kuwa na umri mkubwa akafanya mambo ya kitoto....’akasema
‘Unasema
ulimuona mlinzi akivuja damu , alikuwa akivuja damu sehemu gani?’ akaulizwa
‘Kichwani....’akasema
‘Sehemu gani
ya kichwa, mbele au nyuma?’ akaulizwa
‘Nyuma....’akasema
‘Tusema mimi
nimesimama hivi nakuangalia wewe hivi kwelii unaweza kuona damu zikivuja kutoka
nyuma?’ akaulizwa
‘Alikuwa
kashikilia kichwa, na mkononi kulikuwa na damu...’akasema
‘Kwahiyo damu
uliziona mkononi sio kichwani....?’ akaulizwa
‘Mkono ulikuwa
na damu zilizotoka kichwani...’akasema
‘Unasema
mlinzi alikuja pale alipokuwa kasimama mshitakiwa,....na wewe ulikuwa
umeshatoka nje ya gari,...wakati huo mshitakiwa bado alikuwa na jiwe
mkononi...?’ akaulizwa
‘Ndi....ndi....sikumbuki,...ninachkumbuka
ni kuwa yeye alianza kumpiga mlinzi....’akasema
‘Ina maana
mlinzi alipofika tu, yeye mshitakiwa akaanza kumpiga huyo mlinzi au kulitokea
mazungumzo yaliyofikia mtafaruku huo?’ akaulizwa
‘Wakati
namuuliza mlinzi kulikoni,...ndio kukatokea mtafaruku huo, ....’akasema
‘Kwahiyo sio
kuwa mshitakiwa alianza kumpiga mlinzi kama ulivyosema awali, ..?’ akaulizwa
‘Mlinzi
alipofika wakati nauliza kulitokea nini ndio mshitakiwa akamkabili mlinzi na
kuanza
kumpiga...’akasema
‘Kwa jiwe?’
akaulizwa
‘Ha....hapana,
walishikana...’akasema
‘Kwahiyo
hakuwa na jiwe mkononi...?’ akaulizwa
‘Kwa hali
kama ile sikumbuki vyema...maana mimi niliingilia kuwaamua...’akasema
‘Mlinzi
alikuwa na nini mkononi?’ akaulizwa
‘Na fimbo
yake anayokuwa nayo akiwa lindoni ni kama rungu hivi ...’akasema
‘Je yeye
wakati kunatokea vurugu hizo fimbo alikuwa nayo mkononi
‘Ndio....’akasema
‘Lakini
hukumbuki kuwa mshitakiwa alikuwa na jiwe mkononi...?’ akaulizwa
‘Sikumbuki....sikuchukulia
maanani kukumbuka hilo....’akasema
‘Yule ni
mzee, ni baba yako, hivi kweli kwa mtizamo wako mtu kama huyo anaweza kufika
kwenye makazi ya mtu bila sababu maalumu, aanze kuleta vurugu kama
ulivyodai...?’ akaulizwa
‘Kwanza ondoa
hiyo kauli yako....’akasema
‘Kauli
gani...?’ akauliza wakili akionyesha kama kushangaa
‘Hiyo kauli
kuwa mzee huyo ni baba yangu, huyo mzee sio
baba yangu...na siwezi kuwa na baba mkorofi kama huyo....’akasema
‘Huyu mzee
sio baba yako...?’ akauliza wakili
‘Ndio huyo
mzee sio baba yangu, na siwezi kuwa na baba kama huyo hunielewi...’akasema kwa
hasira
‘Unasema
huwezi kuwa na baba kama huyo kwasababu ni mkorofi, au kwa sababu sio baba yako
wa kukuzaa...?’ akaulizwa
‘Kwa yote
mawili , kwanza sio baba yangu wa kunizaa na pili sio baba yangu kwa tabia
zake, nashukuru kwa hilo, wenye baba kama huyo wana shida ...’akasema na watu
wakacheka
‘Je kwa
kutaka kuthibitisha kauli yako hiyo, nikuulize baba yako yupoje?’ akaulizwa,
wakili muendesha mashitaka akalipinga swali hilo, na wakili mtetezi akasema
‘Swali hili
limetokana na kauli yake hiyo kuwa hawezi kuwa na baba kama huyo mimi nataka
kutambua vyema baba yake yupoje kiasi kwamba awe tofauti na huyo mshitakiwa...’akasema
‘Je hiyo
inahusiana vipi na kesi hii.....?’ akauliza wakili muendesha mashitaka
‘Nataka
kuthibitisha kauli, kuwa ina ukweli ,....’akasema
‘Ili iweje
kwenye kesi hii...?’ akauliza na hakimu akaingilia kati, na kwa mshangao hakimu
akataka swali hilo lijibiwe
‘Baba yangu
ni muungwana, aliyesoma, na hawezi kuwa na tabia kama hiyo...’akasema
‘Baba yako
amesoma,ni muungwana, alishawahi kukutembea hapo nyumbani kwako...?’ akaulizwa
‘Hapana.....’akasema
‘Kwanini?’
akaulizwa
‘Kwasababu
hayupo....’akasema
‘Kaenda
wapi?’ akaulizwa
‘Hayupo
duniani....’akasema
‘Pole sana,
ina maana keshafariki ..si ndio...?’ akaulizwa
‘Ndi-o, aah,Sijui
yawezekana....’akasema
‘Ndio halafu
hujui, kipi ni sahihi hapo.....umesema baba yako ni muungwana, msomi kuonyesha
kuwa unamfahamu , kuwa enzi za uhai wake alikuwa hivyo....au sio?’ akaulizwa
‘Nimesema
sijui, sikuwahi kumuona, na simjui....enzi za uhai wake alikuwaje.....maana sikuwahi
kuishi nao,......’akasema na watu wakacheka
‘Unasema
humjui, na hukuwahi kumuona,je ulifahamu vipi tabia zake?’ akaulizwa na wakili
akaweka pingamizi, na wakili huyu akajitetea na kuelezea kwanini kauliza swali
hilo
‘Huyu shahidi kapinga kuwa huyo hawezi kuwa ni baba
yake na baba yake ni msomi, muungwana, lakini baadaye anasema baba yake hamjui,hakuwahi
kuishi nao....kuonyesha kuwa huyu shahdi ni muongo,...’akasema wakili
‘Mimi sio
muongo, ila maswali yako hayana msingi wa hii kesi , unanichanganya tu akili
yangu.....’akasema shahidi akimuangalia muendesha mashitaka kama kuomba msaada,
na muendesha mashitaka akaweka pingamizi
kuwa maswali ya wakili hayaendani na kesi
‘
‘Yana msingi
, kwa vile nataka kulithibitisha hilo, kuonyesha kuwa huyo shahidi ni muongo, hana
heshima kwa wazee, na kuonyesha kuwa kauli zake chafu ndizo zilimfanya mzee,
mshitkiwa kupandwa na hasira....’akasema
‘Mimi
sikuwepo wakati wanaongea na mlinzi....’akasema shahidi
‘Hukuwepo ila
ulifika baadaye na wewe na mlinzi wako mkaanza kumpiga huyo mzee hadi kumvunja
mbavu,....kuonyesha jinsi gani unavyowachukia wazee, wazee ambao ni wazazi
wako.....’akaambiwa
‘Sio mzazi
wangu huyo mzee....’akasema
‘Kwahiyo
ulifanya hivyo, kwa vile sio mzazai wako?’ akaulizwa
‘Nilifanya
nini....mimi nilipoona huyo mzee analeta vurugu, kwanza alimuumiza mlinzi na bado
alitaka kunipiga na mimi, tukawa tunamzuia kwa pamoja....’akasema
‘Ndio
mumupige mzee, ambaye ni sawa na mzazi wako hadi kumvunja mbavu...?’ akaulizwa
‘Sikumvunja
mbavu mimi,...sikumpiga, na yeye sio sawa na mzazi wangu, .....’akasema
‘Wewe ili awe
sawa na mzazi wako ulitaka aweje....?’ akaulizwa
‘Awe muungwana,
asifike kwenye nyumba za watu na kuanza kuleta vurugu...’akasema
‘Kwahiyo wewe
na mlinzi mlimpiga huyo mzee kwa vile tu, hafanani na jinsi utakavyo wewe?’
akaulizwa na muendesha mashtaka akaweka ingamizi kuwa wakili anamlazimishia
shahidi kauli ambayo hajaitamka.
‘Shahidi
anasema ili amkubali mzee kuwa ni mzazi wake anataka awe vile anavyotaka yeye,
hajui kuwa uzee, na uchakavu,au uduni wa maisha umetokana na wazee hao kuhangaika ili wao wapate, ili wao
wasome, na kuhangaika kwao ndiko kumewafanya wazee hao wafikie hapo walipo, waonekane
wamechoka, ...’akasema wakili
‘Je wewe
hutazeeka...?’ akaulizwa
Watu wakaguna
, wengine wakacheka na hakimu akagonga rungu kutuliza watu, na akasema
‘Shahidi jibu
swali..lakini wakili hakikisha kuwa maswali yako yanalenga kwenye kesi, sitaki
nikufundishe wajibu wako....’akasema hakimu
‘Swali gani, muheshimiwa
hakimu....?’ akauliza hakimu akimuangalia wakili mtetezi kwa mashaka
‘Wewe unasema
humjui baba yako na ya kuwa hujui kama baba
yako yupo hai au la nauliza tena
kama ni hivyo unawezaje kusema baba yako hana tabia kama ya huyo mshitakiwa vipi
ulijua tabia ya baba yako,....?’ akaulizwa
‘Mimi simjui baba
yangu maana sikuwahi kumuona....hata hivyo, baba yangu hata kama ningemuona
hawezi kuwa na tabia kama za mshitakiwa .....’akasema
‘Kwahiyo
kauli ya kusema kuwa baba yako kafariki sio sahihi huenda yupo hai, ila
hujawahi kuonana naye...?’ akaulizwa
‘Kwani hayo ya
baba yangu kuwa hai, yahusiana gani na hilo tukio, mtu aje kwangu, hata kama ni
baba yangu afike kwenye nyumba ya mtu na kuleta vurugu, haikubaliki tabia kama
hiyo, na isitoshe huyo hawezi kuwa baba yangu, nimeshasema hilo...’ akasema
shahidi.
‘Kwasababu
nataka kukuonyesha kuwa huyo mshitakiwa hakuyafanya hayo kwa makusudi, mzee
kama yeye alikerwa na kauli zenu chafu, akakasirka na nyie kwa kuonyesha ujana
wenu mkaanza kumpiga...’akasema wakili
‘Hiyo sio
kweli....yeye ndiye aliyeleta vurugu,...usibadilishe mada.....usimtetee kwa
kitu ambacho hakikuwa hivyo....yeye kashtakiwa kwa kuleta vurugu,.....’akasema
‘Yeye sasa
hivi ni mgonjwa kavunjika mbavu, kategeuka miguu, ni kutokana na nini...?’
akaulizwa
‘Kutokana na
uzee wake.....’akasema na watu wakacheka
‘Kwahiyo mtu
akiwa mzee anavunjika mbavu anategeuka miguu....?’ akaulizwa
‘Sio lazima
iwe hivyo, ila kama mzee ni mkorofi, hajitulizi nyumbani kwake, kazi yake ni
kupita kwenye majumba ya watu na kuleta vurugu, matokeo yake ndio hayo, ataumia
miguu, na hata kuvunjka mbavu, maana anaweza kudondoka, akaumia.....’akasema
‘Hizo mbavu
zitavunjikaje kama sio kupigwa mateke, ....wewe na mlinzi hamkumpiga huyo mzee
mateke....mkamchangia kwa pamoja, mkampiga kama mwizi, wakati mzee huyo alifika
akimtafuta ndugu yake....’akauliza wakili
‘Mimi sijui
aliumiaje hizo mb\vu, huenda alifika hapo akiwa na matatizo yake akatafuta
kisingizio tu......’akasema na watu wakacheka
‘Wewe unasema
humjui baba yako, hujawahi kuonana na baba yako, au sio? lakini huyo aliyefika
hapo siku hiyo anaweza kuwa ni baba yako mzazi na alifika hapo akimtafuta ndugu
yake ambaye pia anaweza kuwa ni baba yako mdogo...’akasema wakili huyo kwa
haraka kabla wakili muendesha mashitaka hajaweka pingamizi.
‘Anaweza kuwa
hahaha,..... anaweza kuwa kwa wengine, lakini sio kwangu mimi,....na wazazi
wangu hawawezi kufanya hivyo .... hata hivyo, hayo ya kumtafuta ndugu yake
ilikuwa ni sababu tu....muheshimiwa kwanini unakwepesha kesi ya msingi ya wao
kuleta vurugu.....’akasema
‘Hujajibu
swali langu, anaweza kuwa au hawezi kuwa mzazi wako, ....?’ akauliza wakili
‘Mbona
nimeshakupa jibu tayari, nimesema hawezi kuwa mzazai wangu huyo, hata siku moja.....’akasema
kwa dharau
‘Kwanini
hawezi kuwa mzazi wako....?’ akaulizwa swali na aliona kama anakerwa kwa kurudiwa
maswali yale yale.....
‘Kwasababu
ningewajua na kuwatambia, kwa kifui mimi nimekulia hadi hapa nilipo simjui baba
wala mama nimeishi kivyangu, hata mlezi..sikuwahi kuwa naye....na....’akasita na
kutulia kuongea kwani mlangoni aliingia mtu akitembea taratibu kuelekea kiti
cha mbele walipokuwa watu wamekaa kiti cha mbele
Ile hali ya
kunyamaza kwa ghafla, iliwafanya watu wageuke kumuangalia huyo mtu aliyeingia,
na hakimu naye akaangalia kuelekea kwa huyo mtu,..na hapo wakili mtetezi
akasema...
‘Hebu nikuulize
huko ulaya ulifikaje...na ulikuwa ukiishi na nani ulipokuwa mdogo?’ akaulizwa
na wakili muendesha mashitaka akaweka ingamizi kuwa swali hilo halina msingi ,
halihusiani na kesi na wakili mtetezi akasema yeye anataka kuonyesha wazi kuwa
mshitakiwa alifika hapo kwenye nyumba kwa lengo gani, na hayo yaliyotokea ni
utomvu wa nidhamu, kwa vijana kwa kutowaheshimu wazazi wao,kwa kutoa lugha
chafu na dharau....’akasema wakili
‘Unasema wewe
humjui baba wala mama, huyo aliyekulea ukiwa huko ulaya alikuwa ni nani,,,,sio
baba yako mdogo,...?’ akaulizwa
‘Sio baba
yangu mdogo ni msamaria mwema tu,.....’akasema
‘Hata kama ni
msamaria mwema, wewe wakatii unaishi naye hukumuheshimu kama mzazi wako na je
sasa, huyo unayemuita msamaria mwema yupo wapi ?
‘Yeye alishakufa,...’akasema
‘Alishakufa,!
unahakika kuwa alishakufa au ulimuua
wewe.....?’ akauliza wakili , na watu wakacheka na wengine wakawa wanaongea kwa
kunong’ona, na minong’ono ya wengi huleta kishindo
‘Taratibu
zifuatwe....’Hakimu akasema akigonga rungu lake ..halafu akasema
‘Alkufa
mwenyewe kwa maradhi yake......’akasema na wakili akageuka kwa yule mtu
aliyeingia na kusema;
‘Basi huyo
uliyemuona akiingia ndiye mlezi wako, uliyekuwa ukiishi naye Ulaya......’akasema
wakili, huku akinyosha mkono kuelekea pale alipokaa huyo mtu.
‘Sio kweli
huyo aliyekuwa nami huko ulaya alishafariki dunia....hawezi akawa huyo
wanafanana tu......’akasema
‘Mlikuwa
mkiishi naye kwa vipi.....huko Ulaya?’ akaulizwa
‘Kama
msamaria mwema tu......’akasema
‘Hakuwahi
kukuambia kuwa yeye ni mzazi wako...?’ akaulizwa
‘Hayo
hayahusiani na hii kesi....hata kama aliniambia...’akasema
‘Ni kazi yako
kujibu swali, kama hayahusiani na hii kesi wakili wako angesema hivyo, jibu
swalii langu, je huyo uliyekuwa ukiishii naye huko ulaya hakuwahi kukuambia kuwa
yeye ni baba yako mdogo....?’ akaulizwa
‘Baba yangu
mdogo kwa vipi....?’ akauliza shahidi kwa mshangao
‘Unajifanya
hujui,....eeh...hujiu baba mdogo anakuwa vipi au hujui Kiswahili vizuri kwa
vile ulaya baba mdogo mnamuita Uncle,
au....?’akasema wakili na kuuliza na watu wakacheka
‘Ndio
sijui.......huyo hakuwa baba yangu mdogo....’akasema akimtupia jicho yule mtu
aliyeinga halafu akamkazia macho wakili
‘Hakuwahi
kukuambia kuwa wewe una wazazi wako, mkaja naye kutoka Ulaya akakutambulisha
kwa wazazi wako, bado ukawakana.....?’ akaulizwa
‘Haya
yanahusiana vipi na hii kesi....?’ akauliza akimuangalia muendesha mashitaka
ambaye alikaa kimia, alikuwa akiandika kitu kwenye makabrasha yake.
‘Jibu swali
langu , je haikuwah kutokea hivyo...yeye kukuleta huku Tanzania akakutambulisha
kwa wazazi wako, kwa baba na mama yako ukawakana....?’ akaulizwa
‘Hata kama
ilitokea hivyo, lakini sio kweli, hao hawakuwa ni wazazi wangu, na huyo hakuwa
ni baba yangu mdogo, alitumia mbinu tu ili kujipatia alichokitaka, yeye maisha
yake yalikuwa hivyo, aliwahi hata kufungwa kwa utapeli....’akasema na watu
wakacheka
‘Basi kwa
taarifa yako huyo ni baba yako mdogo halisi, muangalia vizuri ....’akasema
akinyosha mkono kwa yule mtu, halafu akaendelea kusema
‘Na ndiye
aliyekuwa akitafutwa na kaka yake,kaka yake ambaya alikuja kwako, mkampiga wewe
na mlinzi kama mnapiga mwizi, ...kaka yake ambaye ni baba yako mzazi haswa,
ambaye leo mumemfanywa awe mshitakiwa....’akasema wakili akimuonyeshea sasa
mshitakiwa na watu wakaguna
‘Sio
kweli.....huo ni uzushi,...huyo hawezi kuwa ni mzazi wangu, nilishasema na
nitasema tena....achen uzushi, ....familia hiyo naifahamu vyema mimi, ni ya
wazushi, mtu anajiita Profesa hata kusoma hajasoma,...watu wanakuja kwenye
majumba ya watu na kuleta vurugu kutafuta visingizio....’akasema kwa hasira na
watu wakawa wakacheka kidogo halafu kukawa kimia, na kukatokea kitambo cha
ukimia halafu hakimu akasema...
‘Wakili una
uhakika na unachokisema, ?’ akauliza hakimu na kabla wakili hajijibu hakimu
akasema; `Wakili mtetezi,huyo mshitakiwa ni kweli kuwa ni baba mzazi wa
shahidi?’ akauliza hakimu na kabla wakilii hajajibu shahidi akasema;
‘Huyo sio
baba yangu mzazi muheshimiwa hakimu, huyu wakili, anajaribu kunichanganya
kiakili, anajua kabisa kuwa huyo sio baba yangu mzazi, hebu angalieni,
hatufanani kabisa, asipoteze ukweli wa hii kesi...’akasema shahidi, na wakili
akasema;
‘Muheshimiwa
hakimu, nina uhakika na ninachokisema, huyo mshitakiwa ni baba mzazi wa huyu
shahidi...., lakini kutokana na tabia mbaya za vijana wetu wanafikia hatua ya
kuwakana wazazi wao kwa vile tu wanauwezo.....mzee huyo alifika.nyumbani kwa
huyo kijana akimtafuta mdogo wake, na ...’wakili muendesha mashitaka akaingilia
akisema wakili mtetezi anajaribu kukwepa kesi ya msingi na kuleta hoja
nyingine..ili kupoteza muda
Hakimu kwanza
alimuangalia wakili muendesha mashitaka halafu akamuangalia wakili mtetezi, akasema.
‘Natoa mapuziko mafupi, na wakati huo
nawahitajia mawakili wote hapa mbele nataka kuteta na nyie kidogo....’akasema
‘Huyo sio
baba yangu mzazi hawa watu ni waongo, na Profesa alishafarki zamani hawa tu ni
matapeli....’akasikia shahidi akisema kwa sauti
WAZO LA LEO: Hata jani la mgomba lililokauka lilikuwa
kikonyo, ...na wewe kijana ipo siku utakuwa mzee, usidharau wazee wako kwa vile
sasa weweuna umbo nzuri , waheshimu wazee huku ukimuoma mungu na wewe ufikie
hapo kwenye uzee ukiwa salama na afya kwani uzee hauombwi
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment