Profesa alikataa kata kata kuongozana
na wazee kwenda mjini, ili kuonana na watu waliomshitakia kaka yake, ili
ikiwezekana keso ifutwe na mambo yaongelewe nje,....
Wazee kuona hivyo wakaamua kwenda huko
mjini wenyewe ili kuona jinsi gani wanaweza kusaidia hili tatizo kihekima
zaidi, je itawezekana
Tuendelee na
kisa chetu.....
Wazee wakasafiri kuelekea huko mjini......
Na moja kwa
moja walikwenda kwenye hiyo nyumba kama walivyoelekezwa, na kama ilivyotarajiwa,
hawakukaribishwa moja kwa moja, walikataliwa kuingia ndani na mlinzi, kwa
maelezo kuwa wao hawaruhisiwi kuingia ndani kutokana na yaliyotokea huko nyuma.
‘Lakini sisi
tumekuja kuonana na hao watu kwa nia njema kabisa...’wakasema
‘Wenyewe
wametoa agizo kuwa tusiruhusu mtu yoyote kuingia, hususani anayetoka huko
kijijini kwa hao watu waliokuja hapa na kuleta vurugu,....’akasema mlinzi
‘Lakini
wenyewe si wapo ndani?’ akaulizwa mzee akijaribu kuchungulia ndani kwa kuitia
mlangoni na mlinzi akasogea kati kati ya mlango kama vile anazuia huyo mzee
asione huko ndani
‘Nimeshawaambia
hivyo wazee, inatosha nafikiri nimeleweka wazee wangu.....’akasema mlinzi
Wazee
hawakukata tamaa, wakamsihi mlinzi, hatimaye mlinzi akaona isiwe shida japo
alishaagizwa hivyo, akaona aingie aonane tena na bosi wa nyumba, na bahati
nzuri siku hiyo walikuwepo wenyewe.....
‘Nilikuambia
hao watu wakija waambie sitaki kuonana nao, hukunielewa...’ akaambiwa
‘Wamesema ni kuhusu, kesi iliyopo mahakamani...na wamefunga safari
ya mbali kutoka huko kijijini hadi hapa lengo ni wao kuonana na nyie...’akasema
mlinzi
‘Kama ni
kuhusu hiyo kesi, waambie mimi siwezi kuizungumzia lolote maana hiyo kesi ipo
mahakamani.....wewe si unaelewa hilo, ....’akaambiwa mlinzi, hatimaye mlinzi
akarudi kwa wazee na kutoa taarifa hiyo kwa hao wazee, wazee wakazidi kusihi
kuwa ni muhimu kuonana na mwenye nyumba.
‘Unajua sisi
tumetoka kijijini tumefunga safari hadi hapa, hivi kweli hamuoni kuwa ina muhimu
sana kuonana na hao watu, mwambie hata kama ni hivyo, aje tuonane naye tuongee
kidogo, asikie ombi letu...’akasema mzee mmojawapo, na mlinzi alishindwa kurudi
tena kwenda kumuona bosi wake akakaa kimia, wazee wakasubiria hapo wakizidi
kusihi...lakini hakuna kilichofanyika...
Ilipita muda mara
mama mwenye nyumba, huyo mama wa kizungu akawa anataka kutoka nje na gari lake,
ndio akawaona hao wazee, ikabidi asimame kuwaulizia wanachotaka ni nini....
‘Kwani nyie
ni nani na mnataka nini ?’ akauliza huyo mama akiwa ndani ya gari lake akiongea
kwa kuchungulia kwenye dirisha la gari
‘Sisi
tumetokea kijijini, tumefunga safari hadi kufika hapa nia ni kuonana na
anayemiliki hii nyumba, ambaye alishitakia kuwa kafanyiwa fujo. Na jamaa yetu
.tafadahali tunahitaji, tuongee na wewe au mwenye nyumba....maana mwenzetu
anaumwa, ...’akasema mzee
‘Lakini hiyo
kesi ipo mahakamani, ipo mikononi mwa mahakama, sisi hatuna la kufanya, si
mnajua sheria ilivyo, ...’akasema huyo mwanadada wa kizungu
‘Hebu niambie
mna shida gani?’ akauliza huyo mama mwenye nyumba akiwa ndani ya gari lake
akiongea kwa kupitia dirishani kwenye gari lake.
‘Wewe ndiye eeh
mwenye hii nyumba, wewe na mume wako, ambao ndio mliyemshitaki mzee mmoja
aliyefika hapa na akawaleta fujo?’ akaulizwa
‘Ndio......’akasema
huyo mwanadada wa kizungu
‘Tunafahamu sana kuwa kesi io mahakamani,...,
ndio maana tumefike tuongee, tuone jinsi gani tutasaidiana, kiubinadamu, unajua
haya yanaweza kuwatokea hata nyie, ni makosa yamefanyika, tunakubali hilo, nia yetu pia ni kuwaomba msamaha kwa hayo
yaliyotokea....’akasema mzee mmojawapo.
‘Msamaha
hakuna shida...muhimuu ni huko mahakamani watakavyoamua...lakini anyway...’akasema huyo mama wa kizungu
Yule mama wa
kizungu akageuza gari na kurudisha ndani, akamwambia mlinzi awafungulie hao wazee
waingie ndani, yeye akatangulia kuingia ndani kuanza kuongea na mume wake, ..
‘Kwanini umewaruhusu
hao watu waingie,....kwanini umefanya hivyo, tulielewana nini, na umefanya
nini, unawafahamu hao watu walivyo, itakuwa ndio mwanzo wa usumbufu, kila
wakiwa na shida watakwa wakija hapa, mimi nawafahamu sana hao watu.....’mumewe
akaja juu kweli, lakini mbele ya mkewe ikabidi baadaye akubali, na wakati huo wazee
walishaingia ndani.
Wazee wale
wakaingia na kukaribishwa kukaa kwenye viti....
Ikawa sasa ni
kikao cha hao wazee na yeye mwenye
wakati huo mkewe alikuwa kasimama kama msikilizaji tu, alikuwa na haraka ya
kuondoka.
‘Nyie ndio
wenye hii nyumba?’ wazee walianza kuuliza swali hilo mapema kabisa.
‘Ni nini
lengo lenu wazee...., sioni umuhimu wa kujibu swali lenu hilo, labda kama nyie
ni watu wa serikali mnataka uhakiki wa kuhusu anayemiliki hii nyumba, je nyie
na maofisa ardhi..?’akauliza
‘Hapana sisi
sio maofisa ardhi, sisi ni wazee tumetokea huko kijijini...’wakasema
‘Sasa kama
nyie sio watu wanaohusika na umiliki wa majengo, au kama hamuhusiani na hayo mambo ya umiliki wa
nyumba, mimi siwezi kuwajibu hili swali kwa sasa, je mna shida gani..?’ akuliza
huyo mwanaume
‘Kwasababu
walioshitaki ni wamiliki wa hii nyumba,...tumeambiwa mahakamani hivyo, kwahiyo
lengo letu ni kuonana na hao wamiliki...’wakasema
‘Sisi ndio
tuliowafanyiwa fujo, mlinzi wetu akajeruhiwa, mimi mwenyewe nikapigwa, ikabidi
tujitetee, na kwa vile tuliona tumevamiwa tukawaita polisi, na polisi wakafika wakafanya
kazi yao, je sisi tuna kosa gani...’akasema huyo jamaa
‘Poleni sana,
na tunawaomba sana msamaha kwa hilo, ....ni kweli mwenzetu alikosea alikuwa
kachanganyikiwa kwa vile alikuwa akihangaika kumtafuta ndugu yake, ambaye
aliambiwa alifika kwenye nyumba hii...na tungelikuja naye, lakini anaumwa, ....’
wakasema
‘Huyo mzee
aliyeleta fujo hakuwa amechanganyikiwa, kabisa, kama aliwadanganya hivyo, alikuwa
akiongea vyema, na akili yake timamu,...’akasema
‘Nilipofika
nilimkuta mlinzi wangu akivuja damu, mlinzi aliniambia, yeye alimsihi huyo mzee
asiingie ndani maana sisi hatukuwepo kwa muda huo na mzee akasihi kuwa ni
lazima atuone sisi, na mlinzi alipojaribuu kumuelewesha ndio akavamiwa kwa
nyuma...., akidai kwanini ndugu yake alipoteza fahamu humu ndani, anataka kujua
hilo, ...kwahiyo kwa kifupi ni kusema kuwa huyo mzee alileta vurugu, akamjeruhi
mlinzi pale alipomzuia asiingie ndani....’akasema
‘Ndio tunasema
alichanyikiwa,...kwani siku mbili kabla
amekuwa akihangaika huku na kule, kumtafuta ndugu yake...na alijua huenda kazuiliwa
humu ndani,.. na asingeliondoka mpaka ajua ni kitu gani kilimsibuu ndugu
yake..ndio maana alitaka kuonana na nyie.....’wakasema
‘Mlinzi
alimwambia sisi hatupo, na alimwambia ndugu yake kalazwa hositalini ila yeye
aling’ang’ania kuwa ni lazima aingie ndani kuongea na sisi.....’akasema
‘Ndio maana
tumekuja kuwaomba msamaha, maana kwa hivi sasa mzee huyo anaumwa, alikuwa
kalazwa hospitalini,...hali yake sio nzuri, na kiujumla kama ataendelea na
usumbufu wa hii kesi itamuathiri sana, kiubinadamu tunaomba mlione hili,
....’akasema mzee mmojawapo
‘Kwahiyo sisi
mnataka tufanye nini,..mkumbuke kaleta fuko, kavamia nyumba ya watu, kamjeruhii
mlinzi wetu akiwa kazini, mlinzi kashonwa
nyuzi sita kichwani,...’akasema jamaa
‘Poleni
sana.....’wakasema wazee
‘Mimi
mwenyewe nilipofika, nilijarabu kumsihi, akaanza kunivamia na mimi, akaniumiza
na mimi, unaona hapa...’akanyosha mkono na mguu kuonyesha mchubuko,....
‘Sasa mtu
kama huyu asiyejua sheria mlitaka sisi tukae kimia tu, yeye ni nani, acheni sheria
ichukue mkondo wake...ili ajifunze.’akasema
‘Tunakukubalia
kuwa kafanya makosa, ...ndio maana tumekuja kuwaomba msamaha, ....na tupo
tayari kuwapigia magoti kwa niaba...’akasema mzee mmoja akielekea kupiga magoti
‘Aaah,
mzee... usifanye hivyo mzee, maana haitasaidia kitu, ..kama mnaweza nendeni
mkawapigie magoti watu wa usalama, polisi na mahakama, maana kesi hiyo kwasasa ipo
mahakamani....sisi hatuna la kufanya, hata ukitupigia magoti haitasaidia
lolote,...’akasema jamaa
‘Mnaweza
kusaidia sana, na mnalifahamu hilo, ni kiasi cha kuonana na muendesha mashitaka
kuwa nyie mumesamehe, na kwa vile yule ni mzee, nyie mna uwezo kidogo,
msaidieni kesi ifutwe, mtapata baraka...hata kama ni mahamani msema kuwa mumeshamsamehe
mzee wetu huyo, na mpo tayari tuyaongee hayo nje ya mahakama...’akaambiwa
‘Unajua kuna
watu hawana busara, wanakuja kwenye majumba za watu bila hata taarifa huyo
mwenzake anayesema anamtafuta allikuja hivyo hivyo, ....akajifanya yeye ni
Profesa, mimi nilijua labda ni profesa wa chuo kikuu ninayemfahamu mimi....’akasema
‘Kwa vile
nilitarajia kuonana na huyo Profesa wa chuo kikuu rafiki yangu, alipokuja
mlinzi na kutoa taarifa hiyo nikawaambie wamruhusu,, kumbe ni huyo muhuni
fulani tu, mgonjwa mgonjwa,...kaja humu ndani ghafla kadondoka na kuoteza
fahamu,sisi, tukaingia gharama ya kumtibia, kwa gharama zetu.....’akasema na
kugeuka kumuangalia mke wake akasema
‘My wife wewe unaweza kuondoka, hawa
tumemalizana nao waondoke tu...’akasema akimuambia mkewe, na mkewe akawa
anasita kuondoka.
‘Huyo alikuwa
ni mdogo wake huyo mzee akiwa anamtafuta ndugu yake , aliyepotea siku mbili,
ndio maana akafika hapa kumtafuta...aliambiwa alikuja humu ndani na alipofika
humu hakuonekana tena akitoka.nje kutokana na maelezo ya majirani...’akaambiwa
‘Hakuonekana akitoka
wakati sisi tulimchukua na kumpeleka hospitalini, sema tulipokuwa tunatoka
hakuna aliyeona,..tulitokea mlango huu wa nyuma, tukamuingiza kwenye gari, kwahiyo
hata walinzi hawakumuona kuwa yupo ndani ya gari wakati tunatoka,..viyoo vya
gari havionyeshi ndani, kwa hali aliyokuwa nayo, sisi tulijua
keshakufa...’akasema huyo jamaa
‘Huyo mzee
sio muhuni, ni mtu na heshima zake, alikuja kama tulivyokuambia kumtafuta huyo
ndugu yake, sasa inategemea alipata majibu gani kutoka kwa mlinzi, huo ndio
wasiwasi kwa kujitetea...hatujui, na hayo tumeona yapite tu,...kosa
limeshafanyika, muhimu ni hili,
tusaidiane kulimaliza,.....tafadhali tupo chini ya miguu yako...’akasema mzee
‘Kama nilivyowaambia, ..hayo mambo sasa hivi
yapo mikononi mwa mahakama, na mimi siwezi kupoteza muda kwa kwenda mahakamani,
au kwenda sijui kwanani, muda huo sina kabisa, mke wangu ndio kabisa, sisi
tukitoka hapa ni ofisini, na huko ofisini hatuna muda wa kutoka toka, kazi zetu
hazituruhusu...’akasema
‘Kwahiyo kwa
kifupi, mimi siwezi kabisa kufuatilia hilo jambo, yeye amejitakia mwenyewe,
nyie kama mna nafasi hiyo nendeni mkafuatilie wenyewe, huko mahakamani....’akasema
na kuongezea
‘Hata hao
watu wa mahakamani niliwaambia mimi sina muda wa kufika huko mahakamani, wao
waisimamie wenyewe, wao wafanye wajuavyo wenyewe....’akasema
‘Hapo bado hujatusaidia
kwa hilo....nyie ndio mlifanyiwa fujo, nyie ndio mliwaita askari, na nyie ndio
mnaweza kwenda kuwaambia hilo swala limekwisha, mumeona tulimalize nje ya
mahakama, hiyo inawezekana na kesi ikafutwa....’akasema mzee
‘Hivi wazee
hamunielewi, muda huo sina kabisa...nyie nendeni mkaongee na hao wahusika wenyewe, waambieni mimi
nimeshasamehe, basi inatosha ....’akasema
‘Bila nyie
kuwepo, hawawezi kuamini...’wakasema wazee
‘Waamini
wasiamini sisi halituhusu tena, mimi sitainua mguu wangu kwenda kuonana na
na...eeh, sijui na nani....wao wametimiza wajibu wao, ...mlinzi wangu
ameshatibiwa nimemwambia aachane na mambo ya mahakama, walimuita sijui kutoa
ushahidi, mnataka bado mimi nihangaike eti kufuta kesi, hivi sisi tutaonekanaje
...kwanza muda huo sina
.’akasema sasa akiangalia saa yake
‘Unajua
tumetoka kijijini, mbali, kuja kuwaona,...kutokana na hili mchukulie huyo kama
mzee wao, mzazi wako....’akasema mzee mmoja, na jamaa akasimama
‘Jamani
kwaherini, mke wangu alikuwa na kikao mumemkatisha na mimi nahitajika
ofisini,....kwaherini, huko mahakamani sitakuja au na siwezi kwenda kuonana na
huyo anayesimamia hiyo kesi, hilo mnielewe hapa....sina muda huo, leo
mumenikuta nyumbani kwa dharura tu....na mtu kama huyo hawezi kuwa kama mzee au
mzazi wangu...abadani..’akasema huku akiwa ananyosha mkono wa kuwaelekeza hao
wazee watoke nje.
‘Tafadhali
kwa hisani yako....’akazidi kusihi mzee lakini jamaa akawa anazidi kuonyesha
mkono kuwaashiria watoke.
Wazee,
wakaona hawana la kufanya wakasimama na kuanza kuondoka, na walipofika getini
yule mlinzi aliyeumizwa alikuwa kafika, wakajitambulisha kwake na kujaribu
kuongea naye kama anaweza kusaidia lolote na yeye akawaambia
‘Mimi sina
tatizo, nimeshangea na muendesha mashitaka kuwa nimeshamehe tu, najua ilikuwa
ni hasira, na watu wa namna hiyo wapo, lakini wamesema hiyo ni kesi ya
kujeruhi, ni lazima isikilizwe hadi mwisho....’akasema huyo mlinzi
Wazee wale
hawakuishia hapo, walikwenda moja kwa moja kwenye mahakama inayosimamia hiyo
kesi, na majibu waliyoyapata ni yale yale, kuwa hata kama hao waliotendewa
hivyo wamesamehe, lakini kesi hiyo imeshafika mahakamani ni lazima isikilizwe
na hakimu ndiye ataamua vinginevyo....
‘Muhimu hao
waliotendewa wafike mahakamani waseme wenyewe kuwa wamesamehe...inaweza
kusaidia kupunguza adhabu....’wakaambiwa
Ikabidi wazee
warejee kijijini wakiwa wamekata tamaa,
Profesa
alipoambiwa hivyo, akahisi mwili ukimchemka kwa hasira, akikumbuka mambo ya
gerezani, akikumbuka kaka yake kapatwa na matatizo hayo kwa ajili yake, akasema
‘Nitaenda
mjini kuonana na wakili mmoja, najua atasaidia kulimaliza hili tatizo ..huyo
jamaa hajui wapi katokea,siku akijua ataumbuka ....lakini kwa hivi sasa sitaki
kuonana na yeye kwanza..’akasema
‘Utakwenda kwa
huyo wakili peke yako?’ akaulizwa
‘Haina haja
ya kwenda watu wengi nitaonana na huyo wakili peke yangu na yeye atashauri tufanyeje...’akasema
Na wakati
wanaongea kaka mtu alikuwa ndani,na mara Profesa akaitwa na huyo kaka yake...
‘Bro
unasemaje...’akasema
‘Nimekuambia
usiende huko mjini, haina haja....mimi nitaongea mwenyewe mbele ya mahakama,
nitajitetea mwenyewe...kama ni hukumu acheni itolewe,......’akasema
‘Bro wewe
hujui kesi hiyo ni mbaya, umevamia nyumba ya watu, umeumiza,...hilo ni kosa
kubwa sana...’akasema Profesa
‘Wewe
ungelisikia kashfa alizokuwa akizitoa huyo mlinzi usingelikaa kimia...nilitaka
kumfunza adabu yule mlinzi ili ajue jinsi gani ya kuongea na wageni...wakubwa
waliomzidi umri...’akasema
‘Haya umepata
faida gani....?’ akauliza
‘Ndio maana
sitaki msumbuke...halafu hebu njoo kuna kitu nataka kukuulizia,...’akaambiwa,
na yeye baada ya hao wazee kuondoka akaingia ndani kuongea na kaka yake
‘Unajua
nimeota ndoto....sikumbuki vizuri, ila ile sura ya huyo mwenye nyumba, sijui
ndio mwenye nyumba au mpangaji, kama sio ngeni kwangu....imenijia kwenye
ndoto....aah, ile ndoto sijui ilitaka kunielezea nini.....’akasema kaka mtu.
‘Mhh,...mimi
sijui, yawezekana unamfahamu ..., ndio maana nataka nikaogee na wakili,
ikishindikana itabidi mimi na wewe tuongezane mguu kwa mguu kwa hao watu , lakini
hilo ni baada ya mimi kuongea na huyo wakili, tuone atatushauri nini...’akasema
profesa
‘Mhh...hiyo
sura....nikikumbuka hiyo ndoto nitakuambia....lakini.....’akasema kaka mtu na
Profesa akawa anakuna kichwa akiwaza akamsogelea kaka yake akitaka kumuambia
jambo...
NB: Tuishie
hapa kwa leo
WAZO LA LEO:Kiongozi mwema anayewajali raia wake,
hayupo tayari kuona raia wake wanatesea, au wanaumia... ni bora yeye mwenyewe
kama kiongozi aumie kuliko raia wake, hata mmoja tu kuumua, ilivyo kiongozi
anatakiwa awaone raia zake kama sehemu ya familia yake, je baba au mama yupo
tayari kuona watoto wake wanateseke?, ..Kama haweze kuliona hilo kwa familia
yake basi kwa raia zake iwe ni hivyo hivyo,!
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment