Hatari....!
Kichaa kaona silaha, tena silaha
kali.Panga, na moja ya jambo ambalo mzee huyo alikuwa akijaribu kulifanya, ni
kuhakikisha kunakuwa hakuna silaha karibu, siku hiyo ikawa kasahau kuliondoa
hilo panga, ambalo jamaa alizoea kutembea nalo, na akibadilika anaanza
kucharanga watu...
‘Panga hilo ni moja ya vitu vyake
alivyokuja navyo toka ulaya, alipewa zawadi alipokwenda ukweni kwa wanapotoka
mama mtemi..’alisema mzee,
‘Kwahiyo alikuwa akilipenda sana hilo
panga,....sasa baada ya kuharibikiwa likawa ni silaha yake, anatembea nalo,
yule anayemsemesha, anamkata nalo, watu wengi waliumizwa sana na hilo panga,
...
Mzee alihakkisha hilo panga analificha
mbali kabisa, sehemu ambapo huyo jamaa hawezi kuliona...
‘Sijui ni kwanini,...nililitoa hili
panga wakati wanafanya usafi, nikawa na nia ya kulitoa humu ndani
kabisa,....sasa mlipokuja nyie mkanisahaulisha....’akasema.
‘Sasa mzee kabla hatujaendelea naona
ulifiche, uliondoe hapo au...?’ akasema mwenzangu
‘Sawa nitalitoa, kuna jamaa kasema
anataka kulinunua, ndiye namsubiri, kama hatalichukua basi nitakwenda kuliweka
sehemu nyingine, hivi sasa kalala, hawezi kufanya lolote...’yalikuwa maongezi
ya awali, na katika kuongea wakajikuta
wamesahau kabisa kuhusu hilo panga.
Sasa ndio hapo kaliona....
Panga likaonekana, ....Jamaa akaliona
hilo panga!
Wote macho yalitutoka pima kwa uwoga, tukajua
sasa ni zamu yetu kucharangwa mapanga,..akilini kila mmoja alikuwa na wazo moja
tu, ....kujiokoa,....
Kukimbia...nafsi yangu ikaniambia
Mimi nilishaanza kujiinua, japo sio kwa
kusimama kabisa, lakini zile hisia za kufanya hivyo, tayari zilishajijenda mwilini,
mwili ulishajiandaa....kukimbia nikawa nimeshajiweka tayari, kama wanavyofanya wanariadha
wanavyojiweka tayari kwa kuanza kukimbia....
‘Kwenye mstari wako,...kaa tayari...’
iliyobakia ni sauti ya `goooo’ au filimbi, hapo haikutakiwa kusubiria hiyo
`gooo’
Na wakati hayo yakiendelea kichwani
mwangu, kumbe hata mwenzangu alikuwa
kafanya hivyo hivyo, alkuja kuniambia hivyo,
Mimi kwa kujifanya siogoi, nikasogeza
mkono kumshika mwenzangu kama kumpa matumaini, lakini nilishangaa mkono wangu
ukisukumwa pembeni, ..hakuna aliyemuangalia mwenzake.
Tukimbie ....hizo ni nafsi zetu japo
hazikutoa tamko
*************
‘Hatari...’
Hata kwa mzee mwenyewe...
Hata kwa mzee mwenyewe ilionekana
hivyo, kwani yeye alishapewa dhamana ya kuhakikisha huyo jamaa haumizi watu, na
alishawathibitishia hilo, na mara kwa mara ikitokea jamaa kachanganyikiwa watu
hukimbia kuja kumpa taarifa na yeye kwa haraka huenda kumuwahi!
Hii sasa ni hatari.....’ alisema mzee
akiangalia upande kulipokuweo kabati
Ilikuwa neno la mzee, na kauli hiyo,
ilitufanya sasa tuone kumbe kutaka kukimbia kwetu ni halali...nikainua mguu na
mwenzangu akawa keshaanza kuvuta hatua, ni ile hali ya mtu kutaka kukimbia
ukiwa bado umekaa...
‘Kwahiyo...’nikauliza na.....
Niliona kitu cha ajabu....
Yule mzee kuona vile, akasimama kwa
haraka, akasogea kwenye kabati,, akatoa kitu kama kichupa kidogo, akamimina
kitu mkononi, na kwa haraka akamuendea jamaa ambaye kwa muda huo, alikuwa
keshalikamata panga, akiwa kalishikilia barabara mkononi, kama vile hataki
limtoke,...
‘Yess....here
is my weapon....sasa mtaniambia....’akasema kwa sauti
Ni wakati sasa anageuka, mzee,
akarusha kitu kama unga usoni kwa huyo jamaa, na ule unga ilimuingia barabara huyu
jamaa usoni, tuliona akihangaika kujifuta na kupepesa macho....
‘Shiiit.....’akasema
Yule jamaa ule unga, ulimkuta kama
kushitukiza,.....alishitukia kitu kinamwagiwa usoni, na wakati anataka kujifuta
na macho yakimuwasha,.. na kabla hajaamua kufanya alichokuwa amepanga kukifanya
mara akaanza kuyumba, mara mbili na ya tatu akadondoka chini,
Na haikuchukua muda mara akanza kukoroma...
Ikawa ndio salama yetu
‘Oh, mzee hii ilikuwa ni
balaa,....’nikasema
‘Hatari....’akasema akiwa kalishikilia
lile panga mkononi..
‘Sasa mzee lifiche hilo panga mbali
kabisa...’alikuwa rafiki yangu tuliyeongezana naye
Tuendelee na
kisa chetu
*************
‘Haya ndio
maisha niliyo nayo kwasasa, akiwa hapa nyumbani nakuwa na ahueni maana naweza
kumdhibiti kihivyo, hanipi shida...., nina silaha nyingi za kumuweza, na zote
ni dawa za kienyeji...’akasema huyo mzee
‘Dawa za
kienyeji, umetengeneza mwenyewe...kwanini asipelekwe hospitalini ?’ akauliza
mwenzangu.
‘Huyu jamaa kweli
alitakiwa kuwekwa hospitali maalumu ya watu kama yeye, wenye matatizo ya akili,
lakini mimi nikaenda kumtoa,ili niwe naye karibu, .....’akasema mzee
‘Kwanini sasa
mzee, huoni hii sasa ni hatari, akishika hilo panga anaweza kuuumiza hata
kuua..?’ tukauliza
‘Unajua kama
umefuatilia kisa hiki vyema huna haja ya kuniuliza hilo swali....kwanini
nikaamua kumchukua niwe naye karibu...’akasema na akawa kama anawaza jambo kwa
makini....
‘Mimi
nilimchukua huyu mgonjwa nikijua nitaweza kumdhibiti,...lakini pia nilitaka
kujua asili ya tatizo huenda nikalimaliza mimi mwenyewe maana ninazo dawa za
matatizo ya akili, ila unatakiwa uwe karibu na mgonjwa, umfahamu muda tatizo
linapoanza....na je ni la kimaumbile au kuna sababu nyingine...’akasema
‘Kwahiyo
kumbe ni mgonjwa wako, yupo kwenye uchunguzi na uangalizi wako, ...’tukasema
‘Wakati
nataka kumchukua kule hospitalini, walinikatalia kabisa, nikawaambia mimi
namfahamu sana huyu mgonjwa, na nafahamu aina ya tiba yake, kwa muda huo
nilijua ni tatizo dogo tu, nitakuja kulimaliza,....mmh, hata,...sivyo kama
nilivyofikiria....’akasema
‘Sasa kwanini
hujamrudisha, maana kwa hali kama hii mzee mimi naona utakuja kukatwa
mapanga....’tukasema
‘Mimi hilo
siliogopi sana, hasa nikiwa naye haa karibu, na dawa zangu zikiwepo,
ninachoogoa ni wakati yupo mitaani....nimekuwa nikimfuatilia kila anapokwenda,
lakini sasa nimechoka,...watu wanaomfahamu wakiona kachanganyikiwa wanakuja
haraka kuniambia....’akasema
‘Mimi wakati
namchukua hospitalini walitaka niwahakikishie kuwa kweli nitaweza kumdhibiti,
akianza vurugu utafanyaje...’akasema
‘Basi mimi
nikawaonyesha majaribio mbele yao, kipindi hicho alishachachamaa kuwa anataka
kwenda nyumbani kwake, hashikiki,...nikamtuliza kwa dawa zangu, na kweli kila
mara, hali ya jamaa ikibadilika, na kuanza kuleta matatizo, huwa namtuliza kihivyo, ....’akasema
‘Unajua hata Profesa
alikuwa na vipaji vya madawa ya magonjwa mbali mbali, lakini kwa tatizo kama
hilo alinyosha mkono, hakuweza kabisa kumsaidia huyu mtu...’akaendelea kusema
‘Profesa??’
nikauliza na mzee akatabasamu na kutikisa kichwa halafu akasema
‘Unajua
nimemchunguza sana,..nimeona..sizani kama huu ugonjwa wake una dawa...’akasema huyo
mzee
‘Kwahiyo katika
uchunguzi wako na kukaa naye umeshafahamu huyu mtu ana ugonjwa gani...?’
nikamuuliza
‘Hahaha..vijana
sikilizeni, msije mkajidanganya kwa vyovyote iwavyo, ..’akatulia
‘Mhh,katika
maandiko, tunaambiwa, kwanza muabudu mungu wako na pili waheshimu wazazi wako,
au sio, ina maana baada ya mungu wa pili ni nani ni mzazi wako, au sio..’akasema
‘Ndio
mzee....’tukasema kwa pamoja na rafiki yangu
‘Swali
niwaulize, ni nani kasema hivyo....?’akatulia
‘Kusema
vipi?’ akauliza mwenzangu
‘Muabudu
mungu wako halafu watii wazazi wako wawili....’akasema
‘Ni mwenyezimungu
mwenyewe...’nikasema
‘Umeonaeeh....sasa
kama mwenyewe aliyetuumba baada ya kusema
tumuabudu yeye, akaja kusema tuwatii , tuwaheshimu wazazi wawili, inakuwaje mtoto,
....wewe uliyezaliwa na wazazi wawili, unakuja kumuhini, mzazi wako, ....’akasema
‘Lakini
mzee....’nikataka kusema
‘Hakuna
lakini, hakuna sababu,...kwa vyovyote iwavyo, mzazi ni mzazi tu, hutakiwi
kumkana, ...kwa vyovyote vile labda huyo mzazi atake wewe usimtii aliyeweka
hiyo amri ya kuwa baada ya yeye wanaofuatia ni wazazi wawili..kama atakuambia
usimuabudu mungu, usifaye ibada, basi huyo naye ana lake jambo....una haki ya
kutokumtii...maana atakupeleka kubaya....’akasema
‘Sasa mzee,
maana naona kama hujamaliza kisa chetu hutajaona hiyo sehemu, kwa vipi huyu
jamaa aliwakana wazazi wake, ina maana huyu ndiye yule kijana...au?’ nikauliza
na mwenzangu ambaye alikuwa akimuangalia yule jamaa akiwa kalala chini
akikoroma, akauliza
‘Ina maana tatizo
la huyu jamaa, kama tulivyoona kwenye simulizi za nyuma basi linatokana na
laana....?’ akauliza na mzee akatabasamu na kusema
‘Sio laana,
hiyo sio laana....huyo hajalaaniwa.....’akasema mzee akitikisa kichwa kukataa
‘Sasa tatizo ni
nini...kalogwa, au ilikuwaje?’ mwenzangu akauliza
‘Hahaha mimi
naona ni vyema tuendee na kisa chetu...’akasema
********
‘Hebu turudi
nyuma kidogo...;’ akaanza mzee kuendelea na kisa chetu
Profesa
alipofika pale ilipokuwa nyumba yake..., nia ni kuonana na huyo mumiliki mpya
wa hiyo nyumba....’akasema mzee akiendelea na simulizi
‘Unajua kitu
kilikuwa chako kikachukuliwa na kitu chenyewe kikiwa ni nyumba, kitu ambacho hakiondosheki,
kila ukipita unakiona,..na ukiangalia mazingira ya kuchukuliwa kwake ni kama
kunyang’anywa tu, inauma kweli....kwa wengine ni rahisi kusahau, lakini sio
watu kama Profesa!
Profesa
alikuwa na hamu sana ya kuonana na hao wanaosadikiwa kuwa ni wamiliki halali wa
hiyo nyumba, ....yeye wakati anatoka huko ulaya, alijua mumiliki halali atakuwa
huko ulaya, akiitumia nyumba hiyo kama kitega uchumi tu labda kwa kukodisha, au
kama alikuwa Mtanzania, basi atakuwa kaamua kurejea nchini,...sasa ni nani!
‘Nyumba hiyo
siku hizi wanaishi wenyewe...’aliambiwa na jamaa mmoja
Ni siku
alipofika mara ya kwanza, na kauli hiyo ilimfanya ajiulize sana, ni akina nani
hao,..wamekuja lini, kwahiyo ikamjia hamasa ya kutaka kuwafahamu hao watu
kwanza.
‘Huyu
mumilikini nani..’alijiuliza sana swali hilo, na kwa vile alikuwa hajakata
tamaa, japo kisheria ndivyo ilivyo,ya kuwa nyumba hiyo sio nyumba yake tena,
maana alishakubali nyumba iuzwe ili madeni ya watu yawezwe kulipwa, ..tena
mbele ya mwanasheria wake.
‘Na hata kama
waliuza, pesa yote isingeliishia kwenye hayo madeni, ...hebu bro, fikiria ile
nyumba yangu, ingeuzwa shilingi ngapi, eti pesa yote hiyo, iliishia kwenye
kulipa madeni, sikupata hata senti moja...’akasema kwa uchungu
‘Wao walichofaya
kwa roho mbaya zao, walinibambikia madeni mengine yasiyokuwa yangu, na wakati
ule sikuwa na uwezo wa kuyakataa,...ningekataaje wakati nilikuwa kwenye wakati
mgumu, na wao walijua nitafia huko...’akasema
‘Sasa bro, nipo
nje nataka kulifuatilia hili swala, hatua kwa hatua....’akamwambia kaka yake
wakati wanasimuliana
‘Unapoteza
muda wako bure, kama uliwahi kuweka sahihi yako, tena mbele ya mwanasheria wako
mwenyewe, wewe ulitegemea nini,..hao ndugu yangu umeshaliwa, ....’kaka yake alimwambia
‘Sio kirahisi
hivyo, bro, unajua haki nyingine ukinyamaza wajanja, wenye roho mbaya
wanazifisidi, mimi sikubali kirahisi, nitadai hadi naingizwa kaburini...wao si
wanajua nimeshakufa, sasa mzuka wa Profesa utawaandama,...Wewe subiria utaona
vumbi langu....’akasema
‘Haya bwana,
lakini usije kuniletea matatizo, haya niliyo nayo ni manzito,....yananishinda,
...’akasema kaka mtu
‘Wewe wala
usijali,...mimi nitapambana na huyo aliyeinunua.....’akasema
‘Mama mtemi
au nani?’ akaulizwa
‘Huyo
aliyenunua hiyo nyumba, si anajifanya ana pesa, sasa atajuta kwanini aliinunua hiyo
nyumba....’akasema
‘Utafanya
nini wewe wakati umejiishia,....?’ kaka yake alimuliza kwa dharau
‘Wewe subiria
tu, sitajali yeye ni nani, nitapambana
naye...kwa udi na uvumba..., nyumba hiyo nitaigeuza jinamizi, kila
atakayeichukua ashindwe kuishia, labda awe mwendawazimu....!’akasema
‘Samani mzee,
nikurudishe nyuma kidogo, ulisema kuonana na hao wanaosaidikiwa una maana gani....?’
akauliza mwenzangu
‘Maana
Profesa wakati anafika hapo hakuwa na uhakika, wa kikamilifu kuwa wanaoishi
hapo ndio wamiliki halali wa hiyi nyumba, yeye alijua watu wanaongea tu,kama ilivyo watu
wengine kuongea jambo bila ya uhakika,..
Yeye kwa vile
anafahamu ukweli halisi, aliwasikiliza tu , lakini moyoni alikuwa akifahami
undani wa hiyo nyumba, na hakutaka kuwaelezea kuwa yeye ndiye aliyeiuza hiyo
nyumba kwa kulipia madeni,
‘Profesa
alikuwa anafahamu kuwa wamiliki halali anaishi ulaya,kutokana na maelezo
aliyokuwa kayapata kutoka kwa wakili wake...’akasema mzee
‘Walionunua
walikuwa ni Watanzania, su sio, kwahiyo...huenda walikuwa wamerejea...au
sio..?’ akasema jamaa yangu
‘Mhhh....huenda,
ngoja tuone....’akaguna mzee
*********
‘Kwani kuna tatizo gani....’ Hii ndio
sauti iliyomvunja kabisa nguvu profesa, ni sauti anayoifahamu sana, ni sauti
ambayo hata akiwa usingizini angeliweza ni nani kaitamka..
Japokuwa alishamuona huyo mwanadada wa
kizungu, na jaokuwa hadi anaondoka huko, alikuwa hajawa na uhakika kama wawili
hao walishakubaliwa kuoana,....
‘Ni kiindi kilipita, na ukumbuke
kipindi kingi, wakati kijana wao ana urafiki na huyo mwanadada, ndicho kipindi
walikuwa hawaivani, na hakuwa anafahamu maendelea yao, alikuwa akisikia kwa
watu tu.
Kwahiyo aliomuona huyo mwanadada wa
kizungu, ndio kwa akili ya haraka ingeliweza kusema watakuwa na kijana wake,
lakini yeye akili yake haikumtuma hivyo, alijua huyo mdada alikuwa kaja kwa
matembezi tu,...
Huenda huyo mwanadada alifika kwenye
likizo, akaja kwa wamiliki wa nyumba hiyo nyumba labda wanafahamiana, na kwa
vile wanafahamiana hakuona ubaya kuja kuishi nao mpaka likizo yake iishe,
huenda walikodisha, huenda....
Sasa ilipotokea hiyo sauti mlangoni,
ikawa kama kitu kimemgonga kichwani, kimechuma kisu kwenye moyo wake, na hao
akili haikutaka kuendelea na hizo huenda, ikajikuta ikiishiwa nguvu, na ....akahisi
kichwa kikiuma, akahisi mwili ukiisha nguvu na mara giza likatanda usoni
akazama kwenye giza.,,,
*************
‘Who is this man...., a ghost!’ ni sauti
aliyoisikia kama ndoto, kabla ya kuzama kabisa kwenye giza, hadi alipozindukana
na kujikuta kalala kwenye kitanda, na akili ilipotulia zaidi na pua kuakisi
harufu, akajua kumbe yupo hospitalini.
‘Nimefikaje
hapa?’ akajiuliza na mara akahisi watu wakiwa karibu yake
‘Kazindukana...’sauti
ikasema
‘Ndio...’sauti
nyingine ikasema
‘Tunaweza
kuongea naye..?’ sauti nyingine ikauliza
‘Kwahivi sasa
haiwezekani,..ngojeni apumzike, huyu mtu ana shinikizo la damu,, na hali hiyo
imemjia baada ya kupata au kuona kitu cha kumshtua...’akasema docta
‘Lakini
sizani kama kaona kitu kama hicho, maana mimi ananifahamu, kama ndio yeye, na
mume wangu anamfahamu sana..kama huyu mtu ndiye huyo tunayemfahamu sis...’sauti
ya kike ikasema
‘Kama nyie
mnasema mlipomuona mlishituka sana, huenda hata yeye ilikuwa hivyo
hivyo..’sauti ikasema ambayo profesa alikuja kufahamu kuwa sauti hiyo ilikuwa
ni ya dakitari
‘Unajua docta
kama huyu mtu ndio yeye ambaye tunamfahamu sisi, ....basi atakuwa kafufuka,
maana huyo mtu tuliambiwa alishafariki,...kwa hali aliyotoka nayo huko, ilikuwa
sio ya kuishi tena...’akasema
‘Kwanini,
kwani alikuwa akiumwa nini...?’ sauti ikauliza
‘Magonjwa
ambayo asingeliweza kupona...’sauti ikasema
‘Na
alishafikia kipindi hajiwezi...’sauti nyingine ikaendeleza
‘Labda alipofika
huku alipata matibabu muafaka, ndio maana hali yake ikarejea vyema, kuumwa sio
kufa...’sauti ikasema
‘Docta,
unazungumzia ulaya,...unafahamu kabisa huko ulaya matibabu yake nii ya uhakika,
na huko ndipo walisema uhai wake hautazidi hata mwezi, ...na sio mwezi tu,
waliomleta huku walisema siku walipomfikisha hapa nchini, alikuwa hajiwezi
kutokana na maradhi aliyokuwa nayo, na alipofikishwa hoaitalini, alishafikia
hatua ya kukata roho...’sauti ikasema.
‘Kwahiyo
hawakuwa na uhakika kuwa alikufa...alikata roho,....?’ sauti ikauliza
‘Kwa hali
aliyokuwa nayo docta, ....asingeliweza kuishi, na wanasema walipiga simu huku
kuwa na uhakika wakaambiwa keshafariki....’sauti ikasema
‘Ila kiukweli
mpaka sasa hatuna uhakika kuwa mtu mwenyewe ndio huyu, huenda wanafanana
tu...’sauti nyingine ikasema
‘Kwa jinsi
ninavyomfahamu huyo mtu, ....labda kama alikuwa na pacha wake, ndio huyu huyu....’sauti
ikasema
‘Ndio yeye...una
uhakika mume wangu..?’sauti nyingine ikasema
‘Ndio maana
nasema labda kama alikuwa na pacha wake....maana kila kitu ni yule
yule....’sauti ikasema
‘Hapa
ingeliwezekana , . kama ungelikuwa na mahusiano mazuri na jamaa zake ingelifaa
uwapigie simu, ili wajue kama jamaa yao yupo hapa....’ilikuwa sauti ya kike
‘Hili
tulilolifanya linatosha, kama hawana shukurani shauri lao, hivi nani angjitolea
kiasi hiki cha pesa, kwa watu ambao hawamuhusu, gharama yote hii tuliyolipa....docta
kama hakuna zaidi sisi tunaweza kuondoka,...’sauti ya kiume ikasema
‘Sawa, ni
uamuzi wenu tu, kwa vile mumeshalipia kila kitu, na hakuna zaidi ya hapa,
gharama za kitanda mumeshalipia, labda kama atazidiwa tena....’akasema docta
‘Basi
utanipigia simu, kadi yangu hii hapa..’sauti ya kiume ikasema
‘Mume wangu,lakini
kama ni yule jamaa yako, haifai kuondoka
mapema hivi, ni bora tukasubiria kidogo, ili tuwe na uhakika na kwanini alikuja
nyumbani....’sauti ya kike
‘Ya nini
kusubiria, huenda alikuja hapo kwa shari,hawa watu sio wazuri, unajua
niliwauliza walinzi,wakati tunamtoa huyu mgonjwa nje,wanasema huyu mtu alipofika
aliulizia mumiliki wa nyumba, na kuna kauli alitoa kuwa..nyumba ilikuwa ni
yake.....sasa vitu kama hivyo vinanipa mashaka,....’sauti ikasema
‘Nyumba yake
kwa vipi,...basi ni tapeli, ....’akasema mke mtu
‘Kwani nyumba
mnayoishi ilikuwa sio yenu awali?’ sauti ikauliza
‘Docta hawa
watu ni matepeli,....achana naye,....hata kama ilikuwa sio yetu awali, lakini
tulinunua kihalali...na kama .huyu mtu ilikuwa ni yake, kwanini aliuza,
alitarajia nini, ....mimi nimeshaanza kumuhisi vibaya, simtaki kabisa akanyage tena
pale nyumbani..tumemsaidia tu kiubinadamu,..’sauti ikasema
Na wakati
wanaendelea kuongea docta yeye akaondoka, na maongezi yao yakawa yanaleta sauti
za kutokukubaliana, na mara ......
‘Haya jamani
hapa ni hospitalini kama mna maongezi zaidi mkaongelee nje sio humu
ndani..’sauti nyingine ikasema
‘Samahani
nesi, sisi tunaondoka...tumeshaongea na docta, kama kuna zaidi tutawasiliana
kwenye simu....’wakasema na mara kukawa kimia
Profesa
alipoona kupo kimia ndipo akajiinua ....japo kichwa kilikuwa kizito, lakini
aliweza kuinuka, akajiinua kitandani na kukaa, ...alitulia kwa muda akijipima
kama you bara bara, wakati huo mpira wa maji aliowekewa ulikuwa
umeshatolewa,....
Akaangaza
huku na kule , akaona hakuna watu zaidi ya mgonjwa mwingine ambaye alikuwa
kalala,...akaangalia pembeni ya kitanda, akaona ule mkoba wake wa dawa, kumbe
waliamua kuuleta na huo mkoba wake na kuuweka hapo..
‘Afadhali
wamenirudishia dawa zangu, wangelijua kuwa dawa hizi sina thamani kubwa
wasingeziitelekeza hapa, lakini baado kama , kama ni yeye, hahaha, labda mimi
sio
Profesa...’akasema akiupekua huo mkoba
wake, na alipoona kila kitu kipo sawa akageuka kushoto na kulia, akaona hakuna
mtu akasogelea mlango, akaufungua, na alipoona nje hakuna dalili ya mtu
anayemtizama akaanza kutembea kuelekea mlango wa geti la kutokea...
‘Wewe
unakwenda wapi....’alisikia sauti nyumba yake, lakini hakugeuka!
WAZO LA LEO:Ubinadamu na utu wema ni, kusaidiana bila
kuangalia huyu ni nani, kama umeona mtu anastahiki kusaidiwa na wewe una uwezo
wa kufanya hivyo, toa msaada huo kwa moyo mmoja maana hicho utoacho ndicho
chako, hiyo ni moja ya akiba yako siku ya malipo. ...
Wengi wetu
wenye mamlaka au uwezo, hutoa msaada kwa ria, kwa kujionyesha, au kwa kutarajia
kupata badala, ...na wengine hawatoi mpaka wajitangaze kwa watu, hii inaonyesha
kuwa nia yao ni kujionyesha, kuwa wanacho,kuwa wamesaidia...je huoni kuwa kwa
yule unayemsaidia inaweza kumuumiza moyo, kuwa yeye hana, yeye ni wa kusaidiwa
tu...moyoni atajisikia vibaya, Tukumbuke kutoa, kusaidia, kwenye shida, ni
moyo,na sio utajiri ,...
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment