‘What the hell,... Who is this man..?’
Mwanadada wa kizungu aliyekuwa kashikilia gilasi ya maji ilidondoka mkononi, akawa katoa
macho ya uwoga, akiwa haamini anachokiona mbele yake....
Profesa akiwa kaduwaa baada ya kumuona
huyo mwanadada wa kizungu vyema usoni, akiwa haamini kuwa ni kweli kwa
aliyemuona, maana sura za wazungu nyingine ni kama zinafanana kama hujawazoea
vyema, lakini kwa profesa aliyeishi huko, anawafahamu vyema, lakini pia kwa
akili za kibinadamu kama hujawekea jambo maanani kichwani, unaweza usiwe makini
nalo...
Profesa hakutarajia kabisa kuwa mwenye
nyumba hiyo anaweza kuwa ni mtu anayemfahamu, hakutarajia kabisa na haikuwa
kichwani mwake, ndio maana alipomuona huyo mwanadada mwanzoni, japo kuna kitu
kama hisia ilimjia akihisi ni kama vile aliwahi kuiona hiyo sura
mahali,...lakini akili haikukubali kwa haraka,....sasa kamuona kwa usawa wake,
wameangaliana, mshituko ...
Profesa alitulia, akipumua taratibu
akiogopa kupandisha shinikizo la damu japo kwa hatua hiyo tayari athari
zilishajitokeza....ukiwa na shinikizo la damu kitu kidogo tu kinaleta kimuhe
muhe kwenye mzunguko wa damu...
Na kabla hajatulia vyema, maana
huenda,...huyo mwanadada alialikwa tu na wenye nyumba, au huenda alikuja
likizo, akaja kukaa hapo kwa wenye nyumba kwa vile wanafahamiana au kwa vile
...akiwa a hizo huenda nyingi, akijipa matumaini,....mara akasikia sauti,
ikisema;;
‘Kwani kuna tatizo gani....’
Ni sauti hii ndiyo iliyomvunja nguvu,
ni sauti hii iliyomfanya hata zile juhudi zake za kujipa moyo zikashindwa
kuhimili,....akahisi kichwa kikiuma, akahisi mwili ukiisha nguvu na mara giza
likatanda usoni akazama kwenye giza....
Tuendelee na
kisa chetu
***********
‘Ina maana
mpaka unafika hapo hukuwa umesikia au kufahamu wamiliki wa hiyo nyumba,
iliyokuwa nyumba yako ni akina nani....?’ nikamuuliza kabla hajaendelea.
‘Kiukweli
sikuwa na ufahamu huo, hata kaka yangu alikuwa hajui hilo japokuwa alikuwa
akifika huku mjini mara kwa mara,...na alikuwa akikutana na watu waliokuwa
wakipita kariu na hiyo nyumba,... lakini kwa vile hakuna aliyefikiria hilo,.....hakuna
aliyejali
‘Profesa
alikuwa mgonjwa kwa muda mrefu, na maswala ya nyumba hayakuwa na maana, maana
ugonjwa huo wengi walitarajia kuwa ni wa kumuondoa profesa duniani, hauana
dawa.....’akaendelea kusema huyo mzee
‘Kwahiyo
hakuna aliyekuwa akijali maswala ya nyumba, nyumba ya nini, ...nyumba ingekuja
kuulizwa baadaye watu wakitafuta urithi......’akasema.
‘Lakini mpaka
hapo ulikuwa hujawa na uhakika kuwa hao uliowakuta ndio wamiliki au huenda
walikodisha, ...?’ akaulizwa
‘Nyie
subirini niendee msiwe na kiherehere...na mkumbuke tunamuongelea Profesa...sio
mimi, ...mkumbue sana....’akasema akijinyoha kidogo,...
Na wakati
mzee anajinyosha, mara yule jamaa aliyekuwa kalala akasimama, ....yule jamaa
tuliyemkuta barabarani, akiwa kachanganyikiwa,....
Yule jamaa
aliposimama, aligeuka huku na kule kama vile anatafuta kitu,...sisi
tulimuangalia mzee kama ataweza kumsaidia huyo jamaa labda ana njaa...lakini
mzee alikaa kimia tu, akiwa na yeye anamuangalia
Baadaye huyo
jamaa akatulia, akageuza kichwa taratibu hadi pale walipokaa hao wageni,
akawaangalia kwa makini halafu akasema;
‘Unajua dunia
niwaambie kitu....’akasogea karibu na walipokaa hao watu
‘Hii dunia
hii....’akawa anaonyesha kama kuzungusha duara
‘Hii dunia ni
mviringo sio...huku mwanzo unakwenda huku mwisho... ni kama nyumba tu, huku
ukuta na huku ukuta ni mfano, tunachukulia hivyo, si tunapenda kila kitu kwa
mfani ili tuelewe...
‘Wewe na
mimi kama mwanadamu unatoka ukuta huu
kwenda upande mwingine wa nyumba, hujui kabisa kuwa upande huo unaokwenda una
mwisho,... utafika sehemu utagota, hakuna kuendelea na mbaya zaidi huwezi
kurudi ulipotoka, yaani kila unapokwenda nyuma kunazibwa. .....’akatabasamu
‘Nyie watu,
mnamjua mungu...?’ akauliza na kutulia, na huyo mzee ndiye aliyetusaidia
hakujibu swali ila alisema;
‘Hawa ni
wageni, msomi, unatakiwa uwasabahi. Kwanza, ukawafahamu ni akina nani, hawa ni
wageni wako....’akaambiwa
‘Wageni...haaaa,
nani asiye mgeni.....’akashika kidevu
kama anashangaa au kutafakari
‘Kila mtu ni
mgeni katika hii dunia..na hakuna aliye mwenyeji katika hii dunia, ..sisi sote
ni wageni na wasafiri,tulipotoka hatupajui, au nani anayejua katoka wapi,..?’
akasema na kuuliza
‘Kwa kujipa
tumaini, tutasema tumetoka ndani ya tumbo la mama...sasa na huko kwenye tumbo
la mama ulifikaje, utasema ni kutokana na makutano ya mbegu ya mume na yai la
mama, ...tunajipa matumaini hayo....’akawa kama anatafakari kama kutuacha
tuelewe anachokiongea
‘Sasa
niwaulize,....na hizo mbegu na yai zilitoka wapi......utafika sehemu utajua
kuwa hata ulipotoka hupajui.....’akatulia,
‘Kweli si
kweli....?’ akawa natuangalia akitarajia labda tumjibu, lakini sisi tulikaa
kimia
‘Kwahiyo basi
sote hatujui tumetoka wapi, huo ndio
ukweli....
‘ukweli ni
kuwa sisi tumejikuta tupo duniani, hahahaha,
‘Tupo duniani
bwana, ....hapa kila mtu anajifanya mjanja, anajiona kafika, ...wengine
wanamiliki majumba, wanajenga magorofa makubwa,...wanaendesha magari ya
kifahari.....wanatawala, wanajiona wao ni .....hahaha
‘Ni maraisii
watarajiwa, si mnawaoa wakimwaga sera, mimi nikichaguliwa,
nitakuwa....nitafanya...wewe....unajua kesho ilivyo wewe...hakuna hata mmoja
anayesema, mimi mungu akijalia...hakuna,..kwanini,...kiburi....
‘Unajua
niwaambie kitu..., jana nilifika ofisi fulai..., eti naambiwa kumuona bosi
mpaka niwe na miadi naye, niandike kwenye dafutari, ili nipangiwe siku ya kumuona...huyu
naye kawa adimu, hajui...hajui kabisa kuwa yeye ni kama mimi tu...
‘Huyo
bosi,....hajuii kabisa siku itafika...sio mimi wala yeye, ataondoka
tu....anajiona yeye ni tofauti..anadharau wenzake, anatuona tunanuka, ananiona
mimi ni punguani.....hajijui tu, kuwa yeye ndio kapungukiwa na ufahamu, huyo
angelijua, angeliwanyenyekea wanadamu wenzake...
‘Kwahiyo,
hakuna anayejua wapi alipotoka, ...na hapa tulipo sote ni wageni, na
tungelijua,....nawaambia hili, tungelijua, tungelikuwa na ufahamu,angalai kidogo
tu ....hahaha, tusingehangaika saana,tungelilambana miguuu kutafuta fadhila
....lakini wapii,,.....hahahah...unaniona mimi, eti watu wananiita kichaa,
....’akageuka kumuangalia huyo mzee
‘Eti mzee,
mimi ni kichaa....?’ akauliza halafu akawa anajikuna kichwa kama kinawasha na
yule mzee akasema
‘Wewe sio
kichaa tu, bali wewe ni kichaa msomi....’akasema
huyo mzee
‘Msomi
eeh,...msomi...mimi ni msomi eeh...tena kichaa, kichaa ni nini....kichaa!
.....’akatulia akiwaza
‘Kichaa eeh,
punguani, hahaha, unajua mzee sisi sote ni vichaa na punguani,....nikuambie
kwanini...angalia tunavyoangaika na dunia,...matendo yetu,...yapime kama sisi
sisi sote sio vichaa, punguani.....’akatulia
‘Hivi
niwaulize, haya yote ya dunia tunayohangaikia mwisho wake ni nini, umesoma, umeata
kazi, ...utajiri, mwisho wake ni nini, utaishia wapi,...utakwenda wapi....?’
akatuangalia kwa makini kama anahitajia jibu kutoka kwetu...
‘Hebu
nambieni, utakwenda wapi, hivi mtu mwenye akili atahangaika wee, akijua mwisho
wa siku, vyote alivyovihangaika hatavifaidi,....una kazi nzuri una nyumba
nzuri,....lakini utakwenda navyo...utaviacha, hivi wewe una akili...?’ akawa
kama anauliza
‘Halafu
unaniita mimi kichaa, kichaa ni nyie...mama sasa nakula , nalala, popote nakula
...popote nalala...nina shida gani, sihangaiki tena.....halafu unaniita
kichaa....hahaha...’akacheka wee hadi anataka kuanguka.
‘Mimi
nawachukia sana hao wanajoiita mabosi,....wanajifanya wamefika, eti wanaongea
lugha ya wageni, bosi, unawadharau wenzako bosi, ...hata mtu akija kwako, unajisikia,
I am a bos, I am a director, ...whatever
...na wakati mwingine wengine wanaona hata kinyaa kujiwa na wageni kama
mimi,...hahaha, hahahaha.....’akatembea hatua mbili mbele kama wanavyofanya
mwalimu darasani
‘Sasa umepata
kazi una maisha mazuri, ....utataka nini tena,...eeh, utaoa, au utaoelewa,...au
sio, ndio maisha hayo, lazima ukamilike,..baadaye nini tena...utazaa watoto, au
sio..baadaye nini tena,...utakuwa mtu mzima, au sio..utakuja kuitwa baba,
halafu ...hahahah, unaitwa mzee kama wewe, ...wanakuita mzee.au sio......ni
lazima, kama umejaliwa, ....hahahaha,
usiogope, mimi na wewe, ni lazima tufikia huko....kuitwa nani....wazee...
‘Wapendeni
wazee wenu...msije kuwa kama mimi...’hapa akatulia akiwa kama anatafakari kitu
‘Ukishafikia
uzee, na wengine hawafikii huko, unakwenda wapi,...nawauliza nyie watu,
unakwenda wapi...tusiogoe kusema maana ni lazima, .....’akatulia kama anawaza
jambo
‘Kumbuka
nilipoanza nilisema dunia ni nini, ni kama nyumba, sasa sisi tutafika mwisho wa
nyumba,....huko kuna nini, kuna ukuta hujui nyuma ya ukuta ulipotoka kupoje,
kumeshaziba wewe hujui tu, na huku nyuma huwezi kurudi tena,... na mbele umefika
mwisho wa ukuta, hujui pa kwenda, hapo sasa unamkuta yule
aliyetumwa.....hahahahaha wanaogoa hao....’akacheka huku anaruka ruka.
‘Unamfahamu
huyo,utakayemkuta hapo, mwisho wa ukuta
yeye muda wote you anakusubiria,...anajua lazima utamfikia...mimi
simtaji, maana hata mimi namuogopa....kweli namuogoa ndio maana nikifika
barabarani naangalia kushoto na kulia...’akasema na kutulia
‘Watu
wanaogopa...hahahaha, msiogope, maana huyo ni lazima ukutane naye, uwe kijana
au mzee, kama safari yako imefika, utamkuta..yupo, anakusubiria, hana wasiwasi,
anajua ipo siku utafika tu, utafika kwenye anga zake, mwisho wa ukuta,, na hapo
hapotezi muda,...hahahahahaha...’hapo alicheka sana, mpaka akaanguka chini
akatulia muda mrefu kweli,
Kwa muda
alitulia,sisi tulijua kalala,....na tulitaka mzee aendelee na story
yake,kumbe...mara akatikisika kama anataka kuamuka, halafu akarudi kukaa
kimia...
Yule mzee
akatikisa kichwa, akasema;
‘Ndio
hivyo,....akianza kuongea hapo, ni bora mumsikilize tu, ole wako umjibu, ole
wake ubishane naye...dawa ni kukaa kimia, maana akiongea sauti za watu zinakuwa
kama zinamkera,...na usipomsikiliza ukamdharau na kuondoka ...unakuwa ni adui
wake..hugeuka kuwa mbogo,....’akasema mzee
‘Sasa mzee
kwa hali hii mnaishije naye....?’ nikamuuliza
‘Hivyo hivyo,
leo naona kimecharuka, kuna kipindi anakuwa mtu safi kabisa, lakini hali
ikibadilika,....mmh,n hapo ndio kaanza na bora tuwe kimia tumsikilize hadi hapo
atakapomaliza ...’akasema huyo mzee
‘Tusubiria,
ataamuka muda sio mrefu, ....ataongea wee, atafikia kutukana, na hata kupiga
wakati mwingine....., kwahiyo tunaomfahamu akianza kuongea hivyo, tunamsikiliza
wee, hatusemi neno maka achoke,.....’akasema huyo mzee
Na ghafla
huyu jamaa akasimama kwa haraka, kama vile kapewa amri, akasimama na kuangalia
mbele kwa muda , halafu akasema;
‘Tuliishia
wapi vile....kwanza niliwaambia dunia ni
nini,...?’ akauliza na kabla hatujasema kitu akasema
‘Dunia ni
duara, lakini mimi nimeitolea mfano, kuwa dunia tuione kama nyumba,..au sio,
sisi ni wageni tumefika kwenye hiyo nyumba tukaingia ndani, ....ni wageni
tu....tulipotoka hatupajui, na muda wa kuishi kwenye hiyo nyumba hatujui,
tumekaribishwa tu,.na nani hatujui...lakini ni lazima tuondoke, .tutaondoka
tu..., tupende tusipende....mimi na wewe na yule, yoyote hata awe nani atandoka
tu, utabakia hao kwani kwako, ...kwani wenzako hawataki kuja kukaa hapo,
utasema umewahi hahaha, hujawahi, utaondoka tu....’akatulia
‘Sasa ndugu
zanguni, swali ni hili,....kama tunajua kuwa sisi ni wasafiri, ...akumbuka ule
wimbo mmoja, unasemaje mzee....wewe wa siku nyingi bwana, unaujua, unaimbaje
vile...?’ akawa kama anamuuliza huyo mzee, na mzee akawa kimia tu..
‘Hawa wazee
bwana......’akawa kama anafikiria halafu akaanza kuimba;
‘Mimi ni
msafiri bado nipo njiani, sijui lini nitafikaaaeeh...ninajiuliza wapi
ninapokwenda ,najua bado ni mbali......hahaha,....’ akarudia tena kuimba hivyo,
halafu akasema
‘Wewe, mimi,
yule na wao, sote ni nani.....wasafiri...na kilamtu anahisi, kuwa tuendao bado
ni mbali, lakini hujui, hatujui...unahisi na unajipa moyo tu...bado bado...hivi
kweli bado, jana yule kaondoka, leo huyu..kesho naweza kuwa mimi.....hahaha,
halafu mnaniita kichaa, kichaa ni nyie....
‘Hebu
naambieni, mtoto anazaliwa leo anakufa...si
mnajua kufa ni uzee, ni kuumwa, hebu niulize mtoto, hajaumwa, hajazeeka,
kazaliwa, kakaa siku , mwezi, kaondoka,.... kijana anakufa, alijua ni
badooo...mtu mnzima anakufa, alijua bado, tunajipa moyo kuwa mzee ndiye wa kufa
, eti mzee, kweli si kweli....sijui lini
nitafikaeee,...’akatulia alipoimba maneno hayo ya mwisho
‘Jiulize huko
unapokwenda unakwenda wapi....maana mwisho wa yote haya ni kaburi..hakuna
anayelipinga hilo,...ufanye ufanyalo, uringe uringavyo...utape
utapapo...udhulumu, uwe mtenda haki, lakini mwisho wa yote ni
kifoooo....’akatulia
‘Nani
hatakufa? Eeh, nani hatakufa?, ..hakuna, jana, juzi, tumezika, au sio,
unafikiri wao walikuwa hawapendi kuishi...walitarajia kuishi....kuishi hadi
kufikia ndoto yao..lakini wapi....nawasikitikia hao mabosi waliopo maofisini,
kila siku kuwahadaa wafanyakazi wao,.wadhulumaji wakubwa hao.....eti ukienda
mpaka upitie getini, uwe na miadi ya kumuona bosi,..wewe bosi wewe,...’akawa
ananyosha kidole
‘Eti bosi,
huna lolote wewe...., wewe ni maiti mtarajiwa tu...hahahha....tutaona, kama
kweli wewe ni bosi,...kuwa wewe utaishi milele....’hapo akatulia
‘Mimi
nilikuwa bosi...nimeishi ulaya,....si sawa mzee...?’ akageuka kumuangalia mzee
‘Mimi nimesomea
ulaya, nikafanyakazi ulaya, nilipata kazi ulaya,muulizeni huyo mzee...mimi ni
msomi,....’akatulia
‘Nina kila
sababu ya kujiita msomi,... maana hapa kwenu, ukijua kiiingereza kama mimi
..sio huko ulaya, hapana, ....ni hapa kweny, huku mnamuoa ni msomi, ni yule
anayejua kiingereza, kama hujui kiingereza basi wewe sio msomi, kweli si
kweli?.....
‘Hata kama
wewe fundi, uajua saana, au uwe nani ...uwe nani, kama kiingereza hakipandi,
hujawa msomi, ....mimi hapa najua kiingereza kweli kweli,....najua hesabu kweli
kweli, ....najua najua komputa hakuna anayenishinda,....sasa nipo wapi....’hapo
akatulia,...
‘Sasa nipo
wapi wajamani......sasa nipo wapi, kipo wapi...mmh, nipo wapi jamini, sijijui,
sijui..nisaidieni, niambieni nipo wapi.....’akaanza kulia, na hata kufuta
machozi...
Alikuwa
analia kiukweli,..hadi machozi yanamtoka, na sisi hatukujua kabisa tufanye
nini, tulitajia mzee atafanya jambo, lakini mzee alikuwa kajiinamia, na sis
tukaona bora tukae kimia...
‘Sasa nipo
wapi....nipo wapi, kipo wapi.....yote, hayo yapo wapi....’akachuchumaa na
kuendelea kulia, halafu akainuka na kumuendea mzee, akamuangalia huku
akiendelea kulia
‘Mzee, wewe
...unajua eeh,...nyumba hii hapa...si unaitaka,...eeh, nzuri eeh, sasa niambie
kitu kimoja, nisaidie kuniambia,...mimi nipo wapi....halafu ...eeh, nyumba yote
hii yako...dunia hii yako...si mnataka kuishi milele.....eeh, subutu,....nani
ataishi milele, lakini mnisaidie kitu...mimi ...nipo wapi....’akasema
akimuangalia mzee
Mzee akawa
kainama chini tu, katulia,...jamaa kuona hivyo akaanza kumsuta suta mzee
akimshika mebagani...
‘Mzee, mzee,
nauliza mimi.....sasa nipo wapi, ....nipo wapi?’ akamshika mzee mabegani akitulia
kumsukuma sukuma, akawa sasa kamuinamia na mzee akatikisa kichwa kama kukataa,
hakusema neno huku, kajiinamia, na yule jamaa alipoona hivyo akatugeukia sisi
na kutuangalia, akasema
‘Mzee
hajui..lakini nyie najua mnafahamu,...si nawaoana tu, mwajifanya mwajua kila
kitu au sio, wajanja wa mjini....wajua dili...au sio, sasa mtaniambia mimi nipo
wapi...’akawa anatuangalia kwa macho makali.
‘Jamani nipo
wapi...mimi nipo wapi...?’ akawa anatusogelea
‘Hamjui.....eeh...’
akashika kichwa na huku analia
‘Jamani nipo
wapi,nimepotea, au nipo kati kati ya msitu, kuna majoka, kuna kila aina ya
wanyama,au...mbona sijijui...jamani nipo wapi....hakuna anayejua,.....baba, ...’hapoa
aktulia kama kakumbuka kitu
‘Yes, father, where is my dady.....labda
baba anajua,....’akasema na sasa akageuka kumuangalia yule mzee
‘Mzee labda
baba anajua eeh, ndio...baba ,....anajua, sasa baba yupo wapi....baba, jamani
baba ...baba yupo wapi anisaidie kuniambia nipo wapi, mzee baba yupo
wapi...’akawa anamuangalia huyo mzee na mzee akawa kimia tu
‘Mzee
....kweli nimekumbuka, mama, where is my
momy.... yupo wapi, mama,...mama, hivi kweli mama, mama yangu ni nani,
yupoje,... mzee mama yupo wapi....mama,....my momy, usiniache,...don’t leave me....’akageuka huku na kule
kama anatafuta kitu
‘Mama upo
wapi,...najua mama atajua mimi nipo wapi ....mama, mzee mama.. yupo wapi,, mzee
...mzee,...mama, mama yangu yupo wapi....hapana, yupo yupo tu, mzee mama you wapi..?’
akauliza akimuangalia huyo mzee..
Mzee
alitikisa kichwa akionyesha masikitiko, lakini hakusema neno...
‘Ina maana
hakuna anayejua,eeh,...hakuna...hakuna....shiiiiiit....’akawa
sasa anafoka, akaanza kuangalia huku na kule kama anatafuta kitu,
‘Mimi nauliza
mumekaa kimia,...hahahaha, mwaniona mimi nimechanganyikiwa, mimi ni kichaa au
sio, punguani....sasa mtaniambia ....’akageuka huku na kule, kama anaendelea
kutafuta kitu
‘Wajinga
wakubwa nyie, wapuuzi, ....’akawa sasa anatoa matusi makubwa makubwa.....halafu
akatulia na akaangalia juu akatulia, halafu akasema;
‘Hakuna eeh, ....haiwezekani,...hakuna
anayejua kuwa mimi nipo wapi....niliwaambia toka awali, dunia ni kama nyumba au
sio....mumeoanaeeh...lakini mbona mimi .....oh....’akatikisa kichwa
‘Mimi nipo
wapi, nyie si mnajifanya mumefika..mnajua wapi mlipo,...mabosi,.... sasa na
mimi niambieni nipo wapi.....nyie wapuuzi, nawauliza tena mimi nipo wapi,
wewe....’akaninyoshea kidole mimi, nikajikuta nashtuka, maana
alinishitukizia...
‘Wewe, niambie
mimi nipo wapi, ...’mimi nikawa kimia, akaniangalia kwa muda kama anasubiria
jibu, halafu akamgeukia mwenzangu naye akamuuliza swali kama hilo
‘Na
wewe...niambieni mimi nipo wapi....’ na mwenzangu naye akawa kimia, halafu sasa
akawa kakasirika kabisa
‘Mnaninyamazia,
mnaniona mimi mjinga au sio...ngoja, nahisi hamnielewi, nawauliza halafu mnakaa
kimia....’akasema na kugeuka akiangalia huku na kule kama anatafuta kitu
‘Mwenzangu
akanibonyeza na akawa akaninong’oneza
akisema
‘Hapa sasa
hakuna usalama, tukimbie....’akaniambia na mimi nikageuka kumuangalia yule
mzee,na yule mzee alionekana kuwa na wasiwasi, ...nahisi hata yeye alishahisi
kuwa kinachofuata sasa ni hatari, lakini akawa anaogopa kutuambia, na wakati
huo jamaa akawa anajikuna kuna kichwa
‘Mzee....tukimbie...?’
mwenzangu akauliza na huyo jamaa akawa anahangaika akijikuna kichwa utafikiri
kuna kitu kinamghasi, na mzee akatuonyesha ishara ya kunyamaza.
‘Mkimbie,...hahaha,
mkimbie....hatoki mtu hapa,...kwanza kitu gani hicho mnaniingizia kichwani....’akasema
na akawa kama anazuia huku na huku ili mtu asipite
‘Ni nani
anasema mkimbie..hatoki mtu hapa.mpaka mniambia mimi nipo wapi....’akasema,
mimi nilitamani kumwambia you duniani...lakini nikakumbuka kuwa huyo mzee
alisema ukiongea sauti zinamkera...
‘Hata baba...yupo
wapi,...,au mama,...hawa watu wapo wapi, na wao hamtaki kuniambia wapo wapi....?’
akatuagalia kila mmoja kwa hatua
‘Kwanza mimi
siwajui,...hahaha wakafie mbali.huko, who
the hell are they......lakini nyie mnaojifanya mnajua ,....nyie,
nyie..mnajiona mumefika, mumefika eeh hahaha, mnajidanganya,...kama mumefika,
basi niambienii mimi nipo wapi ...?’ akatukodolea macho, na sisi tukawa kimia
‘You.....mtaniambia,...mimii nipo wai, la sivyo, ...eeh, ....kitaeleweka....’akawa
anageuka huku na kule kutafuta kitu, akaangaza na ghafla akatuliza kichwa
alikuwa kaona kitu...
Mimi nikatupa
macho kuona hicho alichokiona, na macho yaliotua kwenye kona ya nyumba,
nikahisi damuu ikinienda mbio,...mungu wangu, lilikuwa ni panga lipo kwenye kona ya
nyumba,...
Jamaa akaliona
na macho yake yakaonekana ya kimeta meta na dalili ya ukatili ikaonekana....
Na Wenzangu
wakaliona lile panga.. na mzee naye akaliona nilimuona akishtuka kama kutaka
kusimama, ..., na mwenzangu naye alionekana kama kaona kitu cha kutisha, kwani
macho yalikuwa yamemtoka pima kwa uwoga,, .........hatari...!
Hatari....
kila mmoja hapo akawa anawaza lake, kwa jicho moja nikaangalia usawa wa
mlangoni,....nikijua hao hakuna kuulizana tena, najua hata mwenzangu alikuwa na wazo hilo hilo....
‘Eheee,...sasa
mtaniambia ....mimi nipo wapi,...who the
hell are you anyway, who the hell are you...’akasema
‘After all, mumefuata nini hapa nyumbani kwangu...
mna msaada gani kwangu.....sina baba, sina mama, sina ndugu....who the hell.are they...ni nani wao kwanza, ..siwajui, ...siwajui...who the hell, ....kwanza mimi nani,....
hakuna anayejua, nipo wapi, hakuna anayejua...hahaha,.....’akawa sasa
analikaribia lile panga
‘Yes, ...yes,
...hii kitu itamaliza shida....mzee umekuwa ukiificha,hili, leo nimeliata, leo, leo... nimelipata....’hapo akaanza
kujikuna kichwa, mfulilizo....huku anainama kulichukua hilo panga...
Hatari....
NB: Naishia
hapa, maana inatisha....
WAZO LA LEO: Chuma uchumacho, ringa uringavyo,
fanya ufanyacho, lakini siku itafika, uliyempenda, utamuacha, au atakuacha, ulichochuma
utakiacha, ubosi, utajiri, majumba ya kifahari, watoto, utaviacha,....ni nini
utakwenda nacho kaburini.....sanda, kabari la kifahari....??, kila mmoja
ajiulize kwa wakati wake..’haya yote ya dunia nini...hata maandiko yanasema .ni
ya kupita tu au sio,? Au ni uupuuzi mtupu tu, au sio??
Ndugu
zanguni, tupendane, tusaidianeni.....tusichukiane, eti kwasababu ya siasa, eti
kwasababu ya mali, eti kwasababu ya ubosi, uraisi, ubunge nk.....maana haya
yote hayana maana kwetu, mwisho utafika vyote hivyo tutaviacha,...walikuwepo,
wakawa na sasa hawapo, na wewe utakuwepo, utakuja kuondoka na
kusahaulika,..muhimu ni kujiuliza huko unaokwenda, utakwenda na nini,.
Ni wazi
kabisa, huko, kinachohitajika ni MATENDO YAKO MEMA,... Sasa kama ni matendo
mema, mbona maisha yako yote yamejaa matendo mabaya, uovu, ufisadi...
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment