Wakati hayo
yakiendelea huko kwa wenye dhamana,..... huku gerezani, alipo profesa nako mambo yalikuwa yamebadilika, ..
Mambo yalimuendea vibaya profesa kwani kinyume na alivyotarajia, na walivyokubaliana,
profesa alijikuta akihamishwa gereza na kupelekwa gereza ambalo ni baya kuliko yote
kwenye nchi hiyo, na wengi wanaopelekwa huko ni wale walioshindikana.
‘Siku hiyo
bro, nilifanywa kushitukiziwa......’akasema mdogo mtu
‘Kwanini
uhamishiwe huko na wakati kesi yako ilikuwa bado,na hujahukumiwa?’ akauliza
kaka mtu
‘Bro, ujue
hata kufungwa kwangu, hata kushitakiwa kwenyewe, yote ni mambo ya fitina tu, hiyo kesi ni mambo ya kukomoana tu..watu
waliataka kujionyesha kuwa wao zaidi, na hawagusiki,....’akasema mdogo mtu
‘Kukomoana
wakati wewe kweli ulikuwa unajishughulisha na biashara hiyo ya milungula....au
wewe ulitaka ufanye makosa usishitakiwe?’ akaulizwa na kaka mtu
‘Biashara
hiyo sikuwa nimefanya peke yangu, wangapi wanafanya mambo hayo na
hawajakamatwa, kwanini mimi nikawa ndio mhanga, nilikuja kugundua kuwa pamoja
na ya kuwa nilikuwa na makosa lakini kulikuwa na uenevu, wakubwa na familia zao
huwa wanalindwa, kuna namna ya kulindana ....’akasema mdogo mtu
‘Mimi
sijui.....’akasema kakamtu
‘Ndio hivyo,
dunia hii wanyonge ndio wanataabika, wanyonge ndio wanabeba mateso yote ya
dunia, watu wanaiba mabilioni, unasikia kabisa wamefisidi, unasikia
wamesababisha hasara, unasikia
wamegushi, wamefanya hiki na kile na gharama yake ni mapesa mengi hawa
hawafungwi, hawa hawaoenekani wezi,wezi ni hawa wanaoiba kuku,....wanaoiba pesa
ndogo ndogo.....’akasema
‘Mimi
siyajui hayo...’akasema
‘Nikuambie
ukweli, hata sheria zikiwekwa zinawalenga wanyonge tu...kwanini wanyonge
wawaghasi wenye nacho, kwanini, hawa wasio nacho, hawaachi kuwauliza wenye
nacho wamepataje, wasitoe mauchafu yao yakaonekana...mimi nilikuwa nimewalenga
wao....’akasema mdogo mtu
‘Hahaha,
unajua mimi hata sikuelewi, uliwalenga wao, au ulikuwa unatafuta
masilahi,...lakini tuyaache hayo, unasema ulihamishwa gerezani, ikawaje, vii
hujaonana na wakili wako, ili kuandikishana mkataba wa kuuza nyumba, ilikuwaje?’
akauliza kakamtu
‘Ndio hivyo,
asubuhi na mapema tunaamuka gari likafika na mara nikaitwa jina langu,
nikaambiwa nahamishwa gereza....
Tuendelee na kisa chetu....
‘Kwanini,mbona
kesi yangu bado..?’ nikauliza
‘Wewe
hukustahiki kuwekwa hapa, hapa wanawekwa watu wa kesi za kawadia, kesi yako ni
ya mauaji, ....’akaambiwa
‘Lakini mimi
sijaua ...mumesikia hata huko mahakamani, aliyeua hajakamatwa, mimi walinishuku
tu, na siwezi kuhukumkiwa kabla mahakama haijaamua hivyo,...’nikajitetea
‘Hayo
waulize wahusika sisi tunatimiza wajibu wetu...’akasema huyo mkuu wa msafara,
hacheki, ....
‘Mimi siwezi
kuondoka hapa mpaka nionane na wakili wangu, nina haki yangu
kisheria,....’akasema profesa
‘Mimi hayo
sijui, sisi tunafuta amri kutoka kwa
wakubwa zetu, ingia ndani ya gari
tunaondoka sasa hivi, usitupotezee muda....’akasema huyo askari magereza.
‘Mimi siwezi
kuondoka hapa mpaka wakili wangu afike...’nikagoma, na wao wakaangaliana, na bila kusita, wakanijia kama vile walikuwa wanajua nitafanya hivyo, walishajua mimi nina kiburi, bro mimi sina nguvu za misuli lakini kwakiburi cha mdomoni, huniwezi....
Lakini mbele ya hao wababe, nilisalimu amri...
‘Mhh , sasa
ikawaje..?’ akauliza kaka mtu
*********
‘Profesa
aligoma kabisa kuingia kwenye gari, ikabidi watumie nguvu, na kumgonga na
virungu vyao kwenye magoti, na hatimaye profesa akasalimu amri, na kuingizwa
kwenye hilo gari la wafungwa kama gunia...
‘Unaleta
ubishi, ....sasa dawa ya ubishi wako ndio hiyo...’wakasema wakati huo profesa
alikuwa akigugumia maumivu
Profesa
alifikishwa kwenye hilo gereza ambalo sifa zake zimeenea nchi nzima, na
alipofika hapo, akajikuta anakaribishwa kama mtu fulani aliyekuwa akisubiriwa
kwa hamu, kama mwanamziki mashuhuri,au mtu fulani aliyekuwa akiongelewa na sasa
keshafika...
Akaingizwa
ndani na taratibu za kuandikishwa zikafuatwa, na hatimaye, akapelekwa kwenye
chumba chake...na kama kawaida vyumba hivyo huchangiwa watu wawili wawili, mmoja juu na mmoja chini.
‘Nilipofika kwenye
hicho chumba mwenzangu ambaye alikuwa yupo humo, hakuwepo, ilikuwa muda wa
ambao wengi walikuwa kwenye shughuli mbali mbali, na sikuambiwa kitanda changu
ni cha juu au chini.
Nikabakia
nimesimama kwa muda,nilishajua gerezani kulivyo, kuna ubabe, na sikutaka kuanza
kukosana na huyo aliyekuwa humo, lakini nilikuwa nimechoka, miguu ilikuwa
inauma, mwili hauna nguvu, nilihitajia kulala.
Nikakaa
kwenye kitanda cha hapo chini, na kwasababu ya kuchoka, na maumivu usingizi
ukawa umenichukua,....nilishituka nainuliwa juu kwa juu na kubamizwa chini
‘Wewe ni
mdudu gani unalalia kitanda changu..’sauti kama ya chura ilinguruma.
‘Samahani
sikujua, ...’nikasema nikiwa sakafuni.
‘Hukujua
eeh, sasa utajua...’akasema huku akinisindilia mateke, na kunikanyaga kama mtu
anayeua nyoka kwa mguu.
Ilipiata
dakika mbili, nikiendelea kupata hicho kipigo,mpaka alipokuja kiranja wa humo
ndani na kuuliza
‘Kuna nini
kinaendelea humu ndani...’akasema na huyu jamaa akamalizia kunikanyaga kichwani
nikahisi vinyota, na kabla sijaa sawa, akamalizia na kunipiga teke la mbavuni,
nilihisi mbavu zimeachia.
‘Damu,
zikawa zinanitoa puani, mdomoni...’akasema profesa, na ikabidi sasa yule
kiranja atoe ishara kwa askari wa gereza liyekuwepo humo, wakafika na kunikuta
nipo sakafuni sijitambua
Hilo jamaa
lilipoulizwa likasema nimekuja na kulala sehemu yake, na mimi nikaulizwa
nikasema mimi ni mgeni sijui ,sikujua kutanda changu ni kipi,
‘Karibu
gereza la kifo, hiyo ni chai chakula bado...’akasema huyo kiranja wa hapo, huku akanikagua, naona alijua kweli nimeumizwa, akaamrisha nibebwe na kupelekwa chumba cha huduma ya kwanza, mmoja wa akaniinua kama gunia akaniweka begeni kama vile mtu anaweka gunia begani na kuzidi kuniumiza mbavu, hakujali ninavyolalamika,alinibeba hadi chumba cha huduma ya kwanza na huko, nikapigwa sindano...nikaanza kuhisi mwili ukiuma uma...kuwashwa utafikiri upupu,..
Ile hali ya
kuwashwa, ilinifanya nihangaike, ...niliachwa hapo kwa muda, kwakweli, dawa
hiyo ilizidi hata hayo maumivu niliyokuwa nayo ya kupigwa, niliwashwa, unajua
kuwashwa, ni zaidi ya upupu,nilihangaika, mpaka nalia kama mtoto walipofika
walinikuta nalia kwa maumivu nahangaika, siwezi hata kukaa., wakaanza kunicheka
ninavyohangaika...
‘Sasa
umepona, kama hujapona tukuongezee nyingine....’akasema huyo dakitari, akiwa na
askari wa hapo na kiranja wa wafungwa, nikajikuta nikisema
‘Nimepona afande....nisaidieni,
nisaidieni...’ akasema profesa na wale maaskari na kiranja wa wafungwa wakawa
wanacheka, hadi kushika mbavu...na yule docta akanisogelea na kunipiga sindan
nyingine, na haikuchukua muda ile hali ikaisha, na akasema;
‘Haya kama
umepona, haya kimbia...’ akasema, na mimi kwa haraka nikaanza kukimbia kuelekea huko kwenye chumba changu.
Yaani yale
mateso ya kuwashwa, ilibidi nikimbie
sana, hadi chumba nilichopangiwa,...milango ile ukifika kwenye chumba chako,
kama unatakiwa kuingia, kinajifungua chenyewe, nikaingia, na nilimkuta yule
jamaa kalala, anakoroma utafikiri simba, nikapanda kwenye kitanda cha juu,
nikiogopa kumuamusha na kusubiri kitakachofuata baadaye.
*******
Usiku ni
kama kumekucha, mengi yaliyotokea usiku huo yalikuwa mabaya kiasi kwamba siwezi
kusimulia, ...kumbe ikifika usiku wanafanyaje milango hufunguliwa na
viranja,...nikajikuta naamushwa, nikatolewa juu ya kitanda hadi sakafuni,..
Lile jamaa
jirani wangu, akawa anatizama ninavyozalilishwa,.. niliomba roho tu itoke, na
hadi asubuhi kunapambazuka, sikuamini kuwa bado nipo hai, ...niliteseka,
nilinyanyasika, nilizalilishwa, hadi saa tisa hivi...
Ilipofika saa tisa hivi, kukatanda ukimia
fulani, kila mtu akarudi sehemu yake, kumbe wenyewe wanafahmu kuwa muda huo ni
muda wa ukaguzi, nilihisi ukimia, na
hapo ndio usingizi unataka kunichukua, kengele ikalia, na kengele ikilia
ole wako uchelewe, ole wako wako uchelewe kutoka, kwani milango inafunguliwa
kwa umeme kwa muda huo ukichelewa unafungiwa ndani na ukikutwa upo ndani na hao
viranja, mateso utakayoyapata hutaweza kuyasahau.
Tulitoka nje
ya milango yetu, ikaja kukaguliwa halafu mnaongozana kwenye uwanja ambapo hapo
mnapangiwa kazi zinaitwa za kupasha viungo moto.., kazi hizo zikiisha kwa saa
mbili hivi, sasa mnasimamishwa uwanjani kama kuna wakupelekwa mahakamani,
wanachukuliwa, kama kuna wagonjwa ....
Mara
nikasikia
‘Profesa una
wageni wako...’niliposikia hivyo nikapumua, nikajua hatimaye huenda wakili wangu
amekuja na huenda nitajua ni ni wamekifanya na nini mustakabali wangu,
Nilipofika
chumba cha wageni nilimkuta wakili na kijana wetu, nilishangaa, maana zaidi
aliyekuwa akija alikuwa ni mama mtemi,.... leo yupo kijana wetu, kiukweli
nilikuwa kwenye hali mbaya sana, nilikuwa nachechemea, lakini nilijikaza,
nisije kuonekana hali niliyo kuwa nayo, nilitamani kulia ili kijana anione ni
kama vile kijana ukimuona mzazi, japo sasa mimi ndiye mzazi, machozi
yalinitoka...japo nilijaribu kujizuia...
‘Pole sana
profesa, najua upo kwenye mateso makubwa, lakini mambo yalifanyika kwa haraka sana , hata
kuhamishwa kwako mimi sikuambiwa,....’akaanza kusema huku akitoa makaratasi
kwenye mkoba wake
‘Hutaamini
kijana wetu hakunisalimia kabisa aliniangalia kama kinyaa, kama mtu ambaye
anamuabisha, ...nilichoka, na wakili akasema;
‘Nimekuja na
kijana wako ili awe ni shahidi ,pamoja na mengine mengi yeye aliwahi kuishi
kwenye nyumba yako hiyo ambayo itachukuliwa kama dhamana, kwahiyo yeye atakuwakilisha
wewe kama mdhamini wako,...’akasema
‘Mama mtemi
anaongea na wakuu wa gereza kuona jinsi gani atakavyoweza kusaidiwa, japokuwa
gereza hili , haliingiliwi, ukifika huku, hakuna sheria hakuna mtu anayoweza
kuingilia....’akasema
‘Sasa kwanza
nimuulize kijana wako kama yupo tayari na hili zoezi maana ni zoezi muhimu
sana, kila kitu keshakisoma na tathimi ya gharama ya nyumba imeshajulikana na
tumeshaongea na watu huko kwenu wamelithibitisha hilo,...’akasema na hata
wakiongea akili yangu haikuwepo hapo, nilihisi kichwa kikinguruma sauti za
ajabi ajabu..
‘Na madalali
tayari wameshapatikana,...lakini tukaona haina haja, kuna watu wapo huku wanaotoka
nchini kwako, wapo tayari kuinunua hiyo nyumba yako,imekuwa ni rahisi kwetu,
tukaona tuwachukue hao hao...’akasema
‘Muhimu ni
kujua kuwa pesa itakayopatikana italipa madeni ya watu, kwani madeni uliyo nayo
ni mengi sana, hata sikutegemea..., mama mtemi anayo nakala ya orodha ya
madeni, hata mimi ninayo hapa...’ akasema akitoa hiyo nakala na akawa
anaikagua...
‘Na zaidi ya
hapo tutaona jinsi gani tutakavyoweza kuimaliza hii kesi haraka
iwezekanavyo...’akasema
‘Kijana wako
ameshirikiana nasi na tumeshapata wateja wazuri tu, na nyumba itanunuliwa kwa
pesa nzuri tu, na hilo la madeni ya watu utakuwa hunalo tena..utabakiwa
kupambana na maamuzi ya hakimu tu...’akasema
‘Sasa kijana
sijui una lolote la kusema kwa mzee wako huyo...’akasema akimgeukia huyo kijana
wetu, na kijana wetu akaniangalia na kusema;
‘Mimi sina
la kusema muhimu ni kuwa madeni ya watu yatalipika, maana sitaweza kuvumilia
hilo, na mimi siwezi kujiingiza kwenye hayo madeni ambayo
hayanihusu,...’akasema
‘Na
waliponiambia niwe mdhamini,nimekubali tu, kushiirikiana na hilo, ili tu kuhakikisha
hakuna kinachobaki kama madeni, ...na mengine hayanihusu, hayo umejitakia
mwenyewe acha sheria ichukue mkondowake, na hayo yanategemea mahakama
itakavyoamua....’akasema
‘Kwahiyo upo
tayari kumsimamia mzee wako, na kuhakikisha kuwa nyumba itawakilishwa kwa
mnunuaji...?’ akaulizwa
‘Nipo
tayari,..mimi sina tatizo kwa hilo, ili kusiwe na kunyosheana kidole kuwa mimi
nilikuwa naishi na mtu mwizi, muuaji,...sipendi...’akasema
‘Profesa huu
hapa ni mkataba, unaweza kuupitia, kijana wako ameshasoma na kuona kila kitu
kipo tayari, iliyobakia ni wewe tu kuweka sahihi yako na nakala moja tutampatia
mnunuaji., nyingine nitabakia nayo mimi na nyingine kijana wako kama mdhamini
wako..’akasema
‘Ni nani
mnunuaji?’ akauliza sasa profesa alipoona hana jinsi
‘Mnunuaji
anafahamiana na kijana wako, hilo halina shida, huyo mnunuzi hakuweza kuja
huku, unajua wengi hawapendi kuja sehemu hizi ....’akasema, na profesa
akaupitia ule mkataba na kuona gharama gani iliandikwa kama thamani ya hiyo
nyumba.
Kiukweli...,
ilikuwa ni pesa nzuri tu, hata profesa hakutegemea kuwa nyumba yake itauzwa kwa
kiasi chote hicho
‘Sasa hii
hapa ni orodha ya madeni ya watu...’akaambiwa na kuipokea hiyo karatasi,
alishangaa kuona ile pesa yote inaishia kwenye madeni ya watu, na yeye habakiwi
na kitu
‘Haiwezekani..kwanini
mumefanya hivi,ina maana gani kunifanyia hivi....’akasema
‘Kwanini ...wewe
ulitakaje,..kwani hayo madeni huyatambui, je unafikiri yangelipwaje bila
kufanya hivyo?’ akaulizwa.
‘Mimi sina
madeni kiasi hicho chote, hayo madeni mengine yametokea wapi....’akasema huku akijaribu kuyapitia hayo
madeni yaliyoorodheshwa hapo, na mwisho akaona gharama za kuwalipa watu mbali
mbali ili kuhakikisha kesi inakwenda vyema
‘Hizi gharama nyingine hapa analipwa nani...?’ akauliza profesa
‘Hayo ya
kuwalipia watu ili kuhakikisha kesi inakwenda vyema, sio hongo, ipo
kisheria,...kwahiyo isikutie shaka, utakuja kuona mwenyewe huko mbele, sasa hivi
huoni tunaimaliza kesi ya mauaji, ndio kazi zake hizo,....’akaambiwa.
Profesa
akapewa peni ili aweke sahihi yake, na wakati anasita mara akamuona mama mtemi
akija, na nyuma yake yupo yule jamaa aliyekuwa naye chumba kimoja, na wengine
aliwakumbuka ni miongoni mwa wale waliokuwa wakimtesa usiku, wakawa wanaongea
na mama mtemi..., halafu wale wafungwa wakaondoka,na mama mtemi akawa anakuja
pale walipokuwa wamekaa
‘Ameshaweka
sahihi maana sina muda tena hapa...’akasema mama mtemi
‘Ndio
anaweka sahihi yake...’akasema wakili
‘Nimeshaongea
na mkuu wa kituo, na nimeongea na wakuu wa humu na watemi wa humu kuwa sasa
ukitoka hapa kama umekubaliana na wazo hilo wasikusumbue, unajua wengi
nawafahamu fahamu hasa wale wa zamani....’akasema
Profesa
akawa kashikilia ule mkataba, akageuka kumuangalia kijana wake,kijana wake
alikuwa katizama chini, hamuangalii usoni, akageuka kumuangalia mama mtemi, mama
mtemi akawa anatabasamu kinafiki tu
Akilini
profesa akawa anajaribu kuwaza ina maana hii saini hapa ndio itanimaliza
kimaisha sitakuwa na nyumba tena, nyumba ambayo inanifanya nionekane mtu
nikirudi nyumbani, nyumba niliyoihangaikia maisha yote....akasita
Na wakati
huo huo kichwani akawa anahisi kelele, na milio ya ajabu, akahisi kama
kuchanganyikiwa, akajua kama anazidi kukaa jela mwaka tu, atakuwa kichaa,
alipohisi hivyo, akaishusha peni kwenye
sehemu ya kuweka sahihi,....
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment