‘Kwanini hukuniambia mapema kuwa kijana wangu
alikuwepo kwenye hilo jengo....?’ akauliza mkuu walipokutana tena kwenye kikao
cha muda.
‘Niliacha
hilo, kwa vile sikuona umuhimu naye..ni kijana wako na unamuamini au sio,....nilijua
lifika hapo kwa mambo yake tu...’akasema mpelelezi
‘Ndio ni
kweli namuamini sana, ndio maana nikashangaa kwanini alifika kwenye hiyo hoteli....,hiyo
hoteli nilishamwambia siimanini, lakini ndio ujana, sasa ndio tatizo limetokea,
sasa mimi nimeatoka huko kwenye kikao na wakuu, wanasisitizia kesi hii
imalizike mapema kuwe na amani kwenye eneo letu, .....mimi naelekea nyumbani,
nitaongea na kijana wangu,nijue alifika hapo hotelini kufuata nini,huyo
niachieni mimi....’akasema mkuu
‘Sawa
mkuu...lakini.’akasema mpelelezi.
‘Lakini nini
kwani kuna kitu mumegundua dhidi yake....?’ akauliza mkuu akimuangalia
mpelelezi ,halafu muendesha mashitaka
‘Mhh...’mpelelezi
akasita, akimgeukia muendesha mashitaka
‘Kwahiyo...unaposema
tukuachie wewe, utaongea naye, ina maana kazi zetu tusifanya hapo sikuelewi
mkuu?’ akauliza muendesha mashitaka akimuangalia huyo mkuu.
‘Aaah
jamani..., nieleweni, nyie endeleeni na kazi yenu kama kawaida, kwani
nimewazuia?...hapana sijawazuia, ila huyo kijana nitaongea naye kwanza ili
nijue undani wake, kama alifika hapo kwa jambo gani , siunajua mzazi lazima
wajibike kwanza au, ....?’akasema mkuu
‘Sawa mkuu,...lakini
kuna mambo tumeyagundua ambayo yanahusiana na huyo kijana....’akasema mpelelezi
akimuangalia muendesha mashitaka
‘Mambo gani,
kuhusu nini....kafanya nini...?’ akauliza akionyesha uso wa kama kukasirika
Tuendelee na
kisa chetu
******
‘Mkuu, mbinu
zinaweza kutumika,...kama nilivyosema awali, lolote laweza kufanyika ili
kuficha ukweli, yanaweza kufanyika mambo mengi kwa wakati mmoja, wakahusishwa
watu wengi kwa mambo tofauti, ili tu ukweli usijulikane...’akasema muendesha
mashitaka
‘Ndio maana tulianzia
kukuonyesha sababu za matukio yote hayo...’akasema mpelelezi .
‘Lakini kama
nilivyowaelewa,na kutoka na kesi inavyokwenda ina maana kuwa mshitakiwa tuliye naye
anaondoka kwenye kosa la mauaji, au...?’ akauliza mkuu
‘Bado
hatujalithibitisha hilo, muhimu kwasasa ilikuwa kumtafuta huyu mtu mwingine ambaye
tumeshagundua kuwa alikuwepo kabla ya mshitakiwa,..na tukimpata itakuwa rahisi
sasa kutafuta ni nani aliyefyatua hiyo risasi, iliyomuua marehemu....’akasema muendesha
mashitaka.
‘Mshitakiwa,
tumemshikilia kwasababu za alama za vidole kwenye bastola, na pia ni kwa vile
alionekana akikimbia akiwa kashikilia bastola, na huu ushahidi ni kutokana na kamera
za mitaani....au sio?’ akauliza mkuu kama vile anataka kujenag hoja
‘Ndio na pia
alionekana akiingia kuelekea eneo hilo kabla ya tukio....na kaandikisha jina
kwenye daftari la wageni,....’ akasema mpelelezi.
‘Aliandika
jina lake sahihi...?’ akauliza mkuu
‘Ndio, na
hili linatufanya tuanze kumuhisi vinginevyo, maana kama alikuwa na nia mbaya,
angeliandika jina tofauti....’akasema mpelelezi.
‘Mhh....lakini
kuandika jina tofauti yaweza kuwa na mambo mengi, wengine wanaandika wakiwa na
malengo yao, kuficha ukweli, kuwa walifika hapo, hasa wanaume uchwara....sio
lazima iwe sababu ya kufanya mauaji, au...?’ akauliza mkuu
‘Ndio
mkuu....ndio maana tukawalenga wale ambao tunahisi wanahusiana na tatizo
hilo, ndio maana tulianzia mbali
kuelekezea sababu...’akasema mpelelezi
‘Na ndio
maana mkamkamata huyo mshitakiwa au sio,kutokana na sababu hizo au sio.., huyo
na mwenzake mtaalamu mliwaweka kwenye kushukiwa, mkampata huyu jamaa, mtalaamu
hamjamuona na makosa bado....au sio?’ akauliza mkuu
‘Ndio
mkuu...’akasema mpelelezi
‘Japo
tumempata, lakini bado tunahisi sio yeye aliyefyatua risasi iliyomuua marehemu,...’akasema
‘Lakini ni
kwa vile tu yeye kapata mtu wa kumtetea, au sio..lakini pia ni kutokana na
jeraha kichwani, kuwa kuna mtu alimpiga kichwani au sio,...?’ akauliza
‘Ndio
mkuu...’akasema mpelelezi
‘Sasa hii
inaashiria kuwa huenda kulikuwa na mtu mwingine aliyefanya hivyo, na ndiye tunahisi
anaweza kuwa ndiye muuaji,au sio, ...’akasema mkuu
‘Ndio
mkuu...’akasema mpelelezi
‘Na huyu mtu
alikuwa kajificha huko juu, mapema sana...na alipita hapo mapokezi kwa jina
bandia,...au sio, ...?’ akauliza
‘Sasa kama
sio huyu mshitakiwa, ni nani mwingine, wewe unahisi ni nani mwingine anaweza
kuwa ndiye muuaji, ni mtaalamu,...eeh, ni huyu jamaa wao wa kamera, au... kwani
kutokana na maelezo yako huyu mtaalamu si walikuwa kundi moja,...kwanini yeye
hatujamkamata ...?’ akauliza mkuu
‘Hatuna
vigezo vya kumkamata Mtaalamu, kwa vile yeye hajafika eneo la tukio hilo kabisa,
kuna ushahidi wa kutosha kuwa siku hiyo yeye alikuwa ofisini kwake....’akasema
mpelelezi.
‘Basi kuna
mtu mwingine alikuwepo hapo kabla, na atakuwa anaufahamu huo mpango wote na
mimi nina wasiwasi na huyu anayeshughulika kamera za hapo kwenye jengo...mlimchunguza
nyendo zake, ...?’akasema mkuu na kuuliza
‘Ndio
tumechunguza nyendo zake, ana ushahidi
kuwa siku hiyo hakufika hapo kwenye hilo jengo,na tumefuatilia na kuona kuwa ni
kweli....’akasema muendesha mashitaka.
Muendesha
mashitaka akawa anafungua makabrasha yake akitikisa kichwa kama kukubaliana na
maelezo ya mpelelezi....halafu akasema.
‘Mkuu kuna
kazi ulitoa , ulimwambia mpelelezi atafute huyu mtu ambaye hakuandika jina lake
sahihi,naona tusikie kagundua nini...’akasema mpelelezi
‘Ehe,
tuambie , umegundua ni nani...?’ akaulizwa
mpelelezi
‘Mwanzoni,
tulijua wapo wawili, maana huyu huyu mtu mmoja aliandikisha mara ya kwanza
akatoka, na akaja mara ya pili, akitumia jina bandia ...maana ilibidi tuanzie
mbali sana kuona kama tunaweza kugundua kitu....’akasema mpelelezi
‘Kwanini
kupoteza muda kuanzia mbali, sisi tulihitajia katika hao watano, ni nani
hakuandika jina lake sahihi, haya tuambie uligundua ni nani...?’ akauliza mkuu
‘Kama
tungeangalia kwa wale watano tu tusingeligundua kitu,...lakini kwa kufanya
hivyo, ndio tukamgundua ni nani...’akasema mpelelezi
‘Sasa huenda
ambao hawajaandika majina yao watakuwa ni wengi, hivi kweli wanaweza kutusaidia
kwenye hii kesi....ok, tuambie ni nani, tusipoteze muda...?’ akauliza mkuu
akimuangalia muendesha mashitaka
‘Yawezekana,
ikasaidia, maana yeye ni mpelelezi anajua ni nini anachokifanya....’ akasema
muendesha mashitaka akiwa keshafungua makabrasha yake tayari kuanza kuandika..
‘Usianze
kundika kwanza....nataka tusikie halafu tuone kipi ni kipi cha kuandika, tusije
kujichanganya...’akasema mkuu na muendesha mashitaka akatabsamu huku akiwa
kashikilia peni yake kama anataka kundika.
‘Ok, ni nani
huyo mwingine...?’ akauliza muendesha mashitaka na mkuu akatikisa kichwa kama
kulikubali hilo swali.
‘Nilipowauliza
hawa wahudumu, au walinzi walikuwepo, iliwawia shida sana kutambua, na ndio
nikawaambia hebu kwanza tuangalia nyuma huenda inaweza kuwasaidia ...’akasema
mpelelezi
‘Ehe,
ikawaje, maana hata mimi moyo wangu unanipa hamasa kuwa huyo mtu anaweza kuwa
muhusika ...kwa namna moja au nyingine kwanini hakuandika jina, angalia
alivyofanya marehemu, aliandika jina bandia kwasababu alijua anafanya
makosa....unaona eeh...’akasema mkuu akimuangalia muendesha mashitaka.
Tuliporudi
nyuma tukiangalia ni nani na nani, wengi waliandika majina yao, na wengi
wanatambulikana, na kama hatambulikani, tulitafuta mawasilianoa na kugundua ni
nani...tulijaribu kuweka muda maalumu, vinginevyo ingechukua mud
asana....’akasema mpelelezi.
‘Ndio
tukafika kwa huyu mtu, kabla ya muda ule ya watu watano, mimi nilipoangalia mwandiko tu, nikagundua
kuwa unafanana na wale watu watano,nikamuuliza mlinzi ,na malinzi akasema huyo
aliyeandika hivyo ni nani.....’akasema
‘Akasema ni
nani...?’ akauliza
‘Mlinzi
hakupenda kusema moja kwa moja, nikambana kuwa asipomsema yeye atahusika kwenye
kosa la mauaji, na yeye akamtetea kuwa huyo mtu hawezi kuhusika, ila
aliandikahivyo kwasababu maalumu...’akasema
‘Inaruhusiwa...?’
akauliza mkuu
‘Hairuhisiwi,
ni ushikaji tu, ni kwa vile huyo mlinzi anaelewana na huyo mtu, basi akakubali
iwe hivyo tu, ni kosa..hata yeye alikubali hivyo, ila alifanya hivyo, kwa
heshima fulani, na kwa kumuamini huyo mtu....’akasema
‘Huo ni
upuuzi,..huyu hajui kazi yake...’akasema mkuu
‘Ndio
hivyo,..mimi nilipoona huo muandiko haraka nikashuka hadi wale watu
watano..ooh,nikagundua kuwa ni yule yule....’akasema
‘Na hapo
mlinzi alisema nini...?’ akauliza
‘Kwa muda
huo aliyekuwa akishughulikia kuandikisha alikuwa sio yeye, yeye alikwenda
mlangoni kukagua watu, na huyu aliyefika baadaye anasema alizongwa sana na
watu,kwahiyo hakuwa makini kuangalia ni nani aliandika jina sio lake...’akasema
‘Hilo
linakubalika kweli,....?’ akauliza mkuu akimuangalia muendesha mashitaka na
muendesha mashitaka akawa anatabasamu tu..
‘Kwa vile
nilisha mgundua ni nani kutoka kwa huyo
mlinzi wa kwanza, kazi yangu ikawa ni rahisi tu, kujua ni kwanini alifanya
hivyo....’akasema mpelelezi.
‘Na cha
ajabu huyu ndiye pia aliyevuruga utaratibu wa saa, yeye ndiye aliweka saa ambayo
sio sahihi, na kuleta mvuruganyo, ...hili hawakuligundua walinzi kwa muda
huo,kwa dhana ile ya kumuamini, na kumuheshimu kuwa hawezi kufanya kitu kama
hicho...’akasema
‘Ni nani
huyo,...?’ akauliza mkuu,sasa akionyesha kuwa na mashaka.
‘Mkuu ni Kijana
wako,ndio yeye ambaye hakuandika jina sahihi mkuu....’akasema mpelelezi,na
kumfanya mkuu atulie kimia kwa muda, na baadaye akatupa jicho kuangalia kama
muendesha mashitaka anaandika kitu.
‘Lakini sio yeye
miongoni mwa yale majina matano...tulioyahisi kuwa yana matatizo, au sio?’
akauliza mkuu huku akijikuna kichwa kwa kidole
‘Kama
nilivyosema mkuu, kama tusingelianzia mbali, tusingeligundua hilo,..ni huyo
huyo...kijana wako mkuu...’akasema mpelelezi.
‘Sio kwamba
namtetea, nataka tuwe na uhakika , nimemuhoji na nina uhakika alifika hapo na
mambo yake ya ujana...na hilo la kuandika jina sio lake sikuwa na haja ya
kumuuliza kwani sikuwa na shaka,sikutarajia kuwa anaweza kufanya hivyo...’akasema
mkuu
‘Hata
walinzi walisema hivyo,...’akasema mpelelezi, na muendesha mashitaka akawa
anaandika, hakuwa ametii ile amri kuwa asindike kwanza
‘Lakini kwa
maelezo yake alifika hapo kibiashara zaidi na mambo ya ujana, ...nimemuhoji,
nikarizika naye, hana baya alilofanya, labda huko kukiuka taratibu za
kuandikisha jina sio lake...’akasema mkuu
‘Ndio mkuu,
lakini maelezo tuliyopata hapo yanatuweka kwenye sehemu ya kuamini kuwa kijana
wako anaweza kuwa anajua kitu kutokana na tukio hilo,....’akasema muendesha
mashitaka
‘Kwa
vipi....?’ akauliza mkuu akigeuka kumuangalia muendesha mashitaka
‘Tumeongea
na kijana rafiki mwenzake, ili kuona kama walikuwa na mipango ya pamoja lakini
mwenzake alisema yeye alitumwa na mama mtemi, kumsubiria mshitakiwa, akitoka amkabili
waongee naye...’akasema
‘Kuhusu
nini...?’ akauliza mkuu
‘Kuhusu kama
alifuata pesa, na kama ni pesa,...mama mtemi anamdai pesa nyingi marehemu ,
kwahiyoo akizipata tu, mama mtemi atamfuata ili aweze kulipwa deni
lake.....’akasema mpelelezi
‘Kwanini
amtumie huyo kijana...?’ akaulizwa
‘Kijana
anampenda binti wa huyo mama, na yupo tayari kufanya lolote ili kumrizisha huyo
mama.. kwa ajili ya binti yake...’akasema muendesha mashitaka
‘Lakini
kijana huyo hakusema lolote kuhusu kijana wangu kuwa anaahamu kuwa alikuwa na
jambo lolote, zaidi ya kuja hapo kwa ujana wake,...au huyu kijana wamshitakiwa
kuna lolote aliongea ...?’ akauliza mkuu
Muendesha
mashitaka akakohoa kuashiria kuwa anataka kuongea, na wote wakamgeukia na
muendesha mashitaka akasema,;
‘Siku
tulisema tuangalie waliondika majina ya bandia ,na pili tuangalie wenye utaalamu
wa mitambo ya komputa....kijana wako ana hayo
yote mawili, kutokana na uchunguzi wa mpelelezi na mimi niliamua
tufuatane ili niweze kuwa na uhakika kamili
‘Japokuwa
sikuwepo muda wote,....niliondoka na kumuacha mpelelezi akiendelea, lakini
kijana anaonekana ana makosa......’akasema
‘Kwa vipi?’
akauliza
‘Kama
alivyosema mpelelezi,...yeye ndiye aliyeandika jina bandia,....ulitoa amri
tumtafute ni nani,.... yeye ndiye aliyeandika saa isiyo sahihi, ....swali hapo
ni kwanini afanye hivyo,...najua kwa vile alikuwa na sababu zake, anaweza
kujitetea vyovyote,..’akasema muendesha mashitaka.
‘Na
unakumbuka, tulikuwa tunamtafuta mtu aliyekuwepo hapo, ambaye ni mtaalamu wa
mitamboya kamera,....kijana wako ni mtaalamu wa mitambo ya kamera...’akasema
muendesha mashitaka,hapo mkuu akanywea, akakunja uso kama anawaza jambo fulani.
‘Ok, .....Lakini
haiwezi ikawa ni sababu ya msingi ya kumshuku yeye, au sio, ukitizama sababu
zenu mlizokwisha kuzitaja huko nyuma...simtetezi, mnielewe hivyo,..’ akasema mkuu
‘Ndio mkuu,
na sisi tulichofanya ni kutelekeza yale uliyoagiza, na katika kufanya hayo ndio
tukaligundua hilo.....’akasema mpelelezi
‘Kiukweli mlivyofanya
ni sahihi kabisa, siwalaumu,...ila , ninachotaka mimi ni ili tuwe na
ushahidi..mimi nimeongea naye,...nilikaa naye nikaanza kumuhoji, nikiwa naongea
sio kama baba, kama mtu wa usalama anayetimiza wajibu wake, ...amekiri kufanya
makosa....’akasema
‘Makosa gani
mkuu,....?’ akauliza mpelelezi
‘Hayo ya
kuandika jina lisilo lake....’akasema mkuu
‘Hilo
tu....’akasema muendesha mashitaka
‘Mengine ni
utoto hayana maana na wala hayahusiani na kesi yetu....’akasema mkuu, lakini ni
vyema mukaongea naye tu, siwazuii, mnaweza kufanya kazi yenu, ila nina uhakika
na maelezo yake, hana zaidi kuhusiana nah ii kesi...’akasema mkuu.
‘Hebu mpelelezi
aeleze zaidi aliyoyagundua kabla na mimi ijayaelezea ya kwangu...’akasema muendesha mashitaka
‘Kijana wa
mshitakiwa alipofika alikutana na kijana wako, wakasalamiana, na baadaye kijana
wako aliaga kuwa anatoka kuna kitu anafuatilia,..’akasema mpelelezi
‘Alisema ni
kitu gani, kupitia kwa kijana wa mhitakiwa...?’ akauliza muendesha mashitaka
‘Alisema ana
dili anafuatilia, ....kijana wa mshitakiwa anasema hakuwa na zaidi ya kuongea
naye kwani yeye alifika hapo na mambo yake...basi kijana wa mkuu, akapandisha
kuelekea juu,.. ‘akasema mpelelezi
‘Na
nilipowahoji walinzi, huko juu ilikuwa ni mara ya pili kwenda kwa siku hiyo, alipanda
mara ya kwanza akakaa kidogo huko juu , baadaye akarudi na aliporudi ndio akaja
kukutana na huyo kijana wa mshitakiwa,...’akasema mpelelezi
‘Ok,
endelea...’akasema muendesha mashitaka, alitaka kuuliza kitu lakini akaona
haina haja kuuliza kwa muda huo.
‘Na hii mara
ya pili ndio akamwambia kijana wa mshitakiwa kuwa kuna kitu anafuatilia huko
juu, alimwambia kuna dili,...ni dili gani, au huko juu alimfuata nani, tutasema
ndio huo ujana, labda alikuwa na miadi ya binti au sio, huyo binti ni
nani,...’akasema muendesha mashitaka
‘Lakini mimi
kwa kauli yake alianiambia kuwa, kuna msichana muhudumu wa humo, mara nyingi huyo
msichana anafanyia sehemu ya juu ya hilo jengo,...na kwa kuhakiki, niliwapigia
simu hao utawala, sikutaka kuongea na huyo binti, na wao wakaniambia ni kweli
msichana huyo yupo...’akasema mkuu
‘Ndio msichana
huyo yupo, lakini hana urafiki wa akribu na huyo kijana wako, ...tuliongea na
huyo msichana akasema ni kweli alimuona huyo kijana akipita akampungia mkono,
lakini hawakukaa kuongea, yeye alikuwa na kazi nyingi hakuwa na muda wa kukaa
kuongea na mtu...’akasema mpelelezi
‘Ndio hivyo,
kijana kaniambia alitaka siku hiyo aongee naye, lakini akamkuta huyo binti ana
kazi nyingi, kwahiyo akazuga,..kama alivyosema na kurudi kuondoka
zake,...’akasema mkuu
‘Ok, sasa
kitu kingine tumechunguza alama za vidole zilizopatikana humo ndani, hatukuweza
kupata alama ya mtu mwingine....’akasema mpelelezi
‘Ndani
wapi...?’ akauliza mkuu
‘Chumba cha
mitambo hiyo ya kamera la hilo jengo, tulitaka kuona kama tunaweza kuona ni
nani mwingine aliweza kuingia humo..’akasema mpelelezi
‘Sasa
tukaona tuangalize zaidi, tukawa tunatafuta kila mahali kama tunaweza kupata
alama za mikono, zilizoachwa, alama mpya kuacha za watendaji wa humo, na kwenye
kitasa cha mlango, tukagundua kitu...kwenye
mlango wa kuingilia, tulipata alama ya dole gumba jipya ...’akasema muendesha
mashitaka
‘La
nani...?’ akauliza mkuu kwa shauku
‘La kijana
wako mkuu, unajua watu hujitahidi sana kuwa waangalifu, lakini kuna kosa dogo,
hutokea....’akasema muendesha mashitaka
‘Ndio
aliniambia kuwa alipofika hapo alitaka kuongea na mtaalamu wa hapo, kuna mambo
waliongea kuhusu kazi zao,...hawa wataalamu huwa wanashirikiana sana na alifika
hapo kumsalimia na kuongea mawili matatu, ...nahisi hapo ndio aligusa mlango,
na kuona umefungwa...’akasema mkuu
‘Kwa dole
gumba tu!? Kwanini isiwe kiganja cha mkono, kama alinyonga kitasa kufungua...?’
akauliza muendesha mashitaka.
‘Yawezekana....si
unagusa hivi kujaribu kitasa...kwanini unauliza hivyo, ...kuna shaka yoyote
dhidi yake....?’ akauliza mkuu
‘Na kwenye
chumba alichokuwa marehemu tulitambua alama hiyo hiyo ya dole gumba...’akasema
mpelelezi na mkuu, akatoa macho ya kushangaa.
‘What!..’akasema hivyo tu
‘Na,kwenye
mlango na mezani ndani ya hicho chumba alichokuwa marehemu... nahisi soksi
aliyokuwa amevaa au kitambaa alichokuwa akitumia kuzuia mikono yake haikuweza
kusitiri dole gumba....’akasema mpelelezi na mkuu akaduwaa
‘Una
uhakika....?’ akauliza mkuu na muendesha mashitaka akatoa makabrasha yake na
kuonyesha hiyo alama ya dole gumba na wapi ilipatikana..
‘Nimethibitisha
hilo mkuu, na kiukweli kijana wako anatambua jambo,...na huenda anahusika kwa
namna moja au nyingine...au walikutana na marehemu wakaongea, kama waajuana, au
.....lolote jingine!’akasema muendesha mashitaka, na mkuu akakunja uso akigeuka
kumuangalia mpelelezi. Mpelelezi akawa anamuangalia muendesha mashitaka.
‘Huenda alikuwa
akimtafuta huyo jamaa wa kamera, akaingia hadi huko, huenda alikutana na
marehemu wanajuana wakawa wanaongea, kama ingekuwa hivyo, akakuelezea hivyo,
tungerizika, .... lakini tulikuja kugundua kitu kingine zaidi..’akasema
muendesha mashitaka
‘Mpelelezi
alipogundua hilo akanipigia simu, nikafika na tukachunguza sasa kwapamoja
kujirizisha,...kiukweli ugunduzi huu sasa ulitutia mashaka mpaka tufikie kuamini
kuwa huyu kijana anahusika kwa namna moja au nyingine.....’akasema muendesha
mashitaka
‘Kitu
gani...?’ akauliza mkuu sasa akitoa sauti kavu
‘Mkuu..,
unakumbuka kwenye ile silaha,... tulikuwa tumegundua alama ya dole gumba, tukawa
hatujagundua ni alama ya nani, ....’akasema kama anauliza.
‘Unataka
kusema nini..!?, Kuwa hiyo alama ya dole gumba ni ya kijana wangu, haiwezekani?
...yule kijana hawezi....namfahamu sana....hapo kuna makosa, lazima kuna makosa
....’ akasema mkuu sasa akigeuza kichwa huku na kule.
‘Alama ya
dole gumba hilo ni ya kijana wako mkuu...hilo tumethibitisha na pia imeonekana
kwenye ule mfuko tuliokuta umetupwa kwenye ngazi za kupandia...’akasema
mpelelezi
‘Kwenye
mfuko ambao tunasadiki ndio ulikuwa na pesa....’akasema muendesha mashitaka
‘Unasema......oooh,
....yawezekana wakati anapita aliuona hu mfuko akaugusa, lakini mna uhakika
kwenye hiyo bastola....kuna alama yake?’mkuu akashika kichwa akionyesha hasira
‘Kwenye hiyo
bastola, ...kuna alama ya dole gumba ya kijana wako mkuu....’akasema mpelelezi
‘Inanipa
shida kuamini, nimeongea naye, na hakuonyesha wasiwasi wowote, maana namfahamu
akiwa na makosa anakuwa na wasiwasi, na mimi kama mzazi ningelitambua hilo,..sina
uhakika kama anaweza kuhusika,...kuna kitu kinaendelea kwenye hii kesi...!’ akasema
mkuu sasa akishindwa kuzuia hisia zake.
‘Ni kweli
mkuu, hata sisi tunahisi kuna kitu...kwani kila tunavyozidi kuchunguza mengi zaidi
yanaanza kujitokeza, hata wale tusiowategemea wanahusika....’akasema mpelelezi
‘Nani
mwingine zaidi.....?’ akauliza mkuu
‘Kiukweli
mkuu, hatukutegemea kukuta alama za kijana wako kwenye hiyo bastola iliyotumika
kumuua marehemu! Na hili linatupa fundisho kuwa kwenye kosa usimwamini kila
mtu,...’akasema mpelelezi
‘Lakini kwa
kijana wangu,...aaa hata sijui, nitamueleza nini mama yae anielewe, lakini
ngoja , niongee naye, nahisi kuna kitu...’akawa anatikisa kichwa kuonyesha
uchungu fulani.
‘Mkuu
hakukuambia hilo ulivyomuhoji, kuwa anahusika, kuwa alifanya lolote,
tunashindwa kujua, hiyo bastola ilifikaje mkononi mwake,je ndio yeye aliua, au
kulitokea nini zaidi....?’ akauliza mpelelezi, na kabla mkuu hajajibu,muendesha
mashitaka akasema
‘Na kwahiyo
tulikuwa tunaomba tuongee na huyo kijana,ili tuweze kumuhoji vizuri sisi
wenyewe bila ya wewe kuwepo, tutaweza kugundua mengi, kuliko wewe ukiwepo....’akasema
muendesha mashitaka.
‘Kiukweli,
niliongea naye, namjulia, ni kijana wangu, najua wapi akiongea vipi ananificha
kitu, lakini safari hii ilikuwa tofauti, anajiamini,...kiukweli, hata, nahisi
kuna kitu, kuna makosa, ....aah,....’Na mara simu ya mkuu ikaita, na mkuu
akaiangalia na kusema;
‘Tena ndio
huyu hapa ananipigia, ....ngoja niongee naye...’akasema akisimama kuondoka hapo
mezani ,kuashiria kuwa hakutaka wenzake wasikie anaongea nini na kijana wake,
na wawili hawa wakaangalia bila kusema kitu.
WAZO LA LEO: Unapopewa dhamana ya kutenda kazi
fulani kwa mujibu wa sheria, timiza wajibu wako bila kujali ni nani
unayemkabili, timiza wajibu wako kwa misingi na sheria na kanuni zinazokulinda,
usiangalie kuwa unayekabiliana naye ni bosi wako, au fulani, hata kama ni bosi
wako kakiuka sheria, au jamaa zake, usione hofu kutimiza kumkabili ukisimamia
kwenye haki. Haki na ukweli ndio utakaokulinda..
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment