Bro...Kesi iliendelea kama ulivyoona,
kiukweli wakili mtetezi alijitahidi sana kunitetea lakini ilipofika siku ile,
ambapo ndio alitakiwa na yeye sasa atoe ushahdii wake na mashahidi, ili
ionekane, kuwa mimi sijaua, wakili akaniambia yeye anataka kujitoa,kisa ni
nini, ni kwa vile hajalipwa pesa yake kutokana na makubaliano.
‘Kwani mlikubaliana nini,mtalipana
vipi..?’ akauliza kaka mtu.
‘Wakili huyo kwa kiasi kikubwa
aliongea na mama mtemi, na mimi nilikuja kukubali tu, kuwa nipo tayari anisimamie, undani wa
makubaliano sikuweza kuusoma,nililitewa huomkataba nikaweka saini yangu,
nikakubali yote yaliyyokuwa yameandikwa humo...’akasema
‘Bila kusoma....wewe si msomi, yaani
ukubali kitu, hukijui undani wake,unanishangaza kweli,haya ....sasa ikawaje...?’
akauliza kakamtu
‘Bro, siku hiyo nilikuwa
nimechanganyikiwa, kesi ya kuua,...upo rumande, bado unaambiwa unapelekwa
magereza mabaya,.....nilijikuta nakubali tu, nikafungua fungua yale makaratasi
nikaweka sahihi yangu,....basi, ..’akasema
‘Hata hujui utamlipaje....na hapo
napo ulitaka kufanya ujanja au...na huyo wakili sio wa bei mbaya, au ni hao wa
mitaani tu?’
‘Ni wakili kweli,...na wengi walijua
wakili huyo atakuwa kalipwa mapesa mengi sana, maana kazi anayoifanya sio
mchezo....’akasema
‘Sasa alilipwa kiasi gani na kwa
ujumla alitakiwa kulipwa shilling ngapi?’
akaulizwa
‘Bro,...,hata sijui mama mtemi
aliongea naye nini mpaka akakubali, huyo wakili sio mchezo, ...moyoni nikawa na
mashaka kuwa huenda mama mtemi alishazipata hizo pesa,....’akasema
‘Kwani hizo pesa zilipotoeaje,
hujatueleza siku ile ilikuwaje....?’ akaulizwa
‘Mhh, hata sijui hizo pesa zilikwenda
kwa nani, ...nilisjua kabisa huyo mama mpaka anamtafuta huyo wakili atakuwa
keshazipata hizo pesa, lakini cha ajabu nilipokutana naye tena akaniulizia tena
kuhusu hizo pesa, na alizidi kunisisitizia kuwa anahitajia hizo pesa,ili aweze
kuwalipa watu mbali mbali...’akasema.
‘Sasa....unajua sikuelewi, haya hebu
endelea kutusimulia,ukatoka siku hiyo hapo mahakamani, ulirudishwa gerezani, ni
gereza lipi hilo, au ulirudiswa kule rumande, sijui..’akasema kaka mtu
Nilirudishwa gerezani, kule
nilitolewa, nikafanyiwa mpango kupelekwa kwenye gereza lenye unafuu, lakini huo
unafuu sikuuona,....’akasema
‘Lakini siulishawahi kufungwa kabla,
kwahiyo unafahamu mazingira ya jela yalivyo au...?’ akaulizwa
‘Niliwahi kufugwa, lakini kipindi
kile sikuwa na maadui kiaisi hicho,..safari hii, nilikutana na watemi, maadui
zangu, niliwahi kuwafanyia ubaya, na kwa ujanja, nikawashinda,
wakafungwa,....walifungwa kwa makosa yao, lakini mimi pia niliwahi kutoa
ushahidi kuwa ni wakosaji,....’akasema
‘Gereza hilo nililopelekwa, wanasema
lina unafuu, lakini niliyoyakuta humo bro, ni mateso,humo ndani nilikuta pia kuna
ubaguzi,...kuna ubaguzi wa rangi, watu weusi walibagulizwa,na kunyanyasika
kweli...na pia kulikuwa na makundi ya ubabe ubabe tu....kuna utemi wa hapa na
pale...
‘Humo ndani kulikuwa na watu
walishajiona wamefika,..wanatumia miili yao,ubabe wao miguvu yao kuwanyanyasa wanyonge
kama mimi, kama unavyoniona mwili wangu, mdhaifu tu, mimi ni maneno tu, lakini
ikifika kwenye nguvu za misuli sina kitu....
Ndio, pale kulikuwa na sheria,..hata
kuna maonyo, kuwa ukiona unateswa utoa taarifa kwa wahusika, walinzi, kuna
viranja wa humo ndani,...., lakini kweli
utaweza kufanya hivyo, ..vitisho vyao hao watendaji, vilitufanya tufunge mdomo,
hata ukitendewa ubaya....
Nikuambie bro, ile siku nafikishwa
hapo utafikiri walifahamu kabla kuwa nitafika humo,...ile nafika tu, nikakutana
na mijamaa ikaanza kunikwida na kuniambia;
‘Umekuja eeh...sasa utatulipa pesa
zetu...’mmoja wa hao watu aliniambia
‘Lakini sikumbuki kama wewe unanidai,
unanidai mimi,..?.’akasema profesa akiwa kakunjwa shati
‘Hukumbuki eeh,, basi
tutakukumbusha...’akasema huyo jamaa,na kwenda zake, muda akaja na kundi la
watemi, nikawekwa pembeni, nikapewa kibano, hadi mwili wote ukaishiwa nguvu,
nilipoteza fahamu, nilipozindukana nikawa nipo chini ya walinzi.
‘keshazindukana huyo mpeleke chumba
chake...’amri ikatolewa, nikapelekwa chumbani kwangu, nafika godoro limelowa
maji, nasigiziwa eti mimi nimekojolea....
Nilitoa taarifa kwa utawala, na ikawa
nimejichongea, siku moja wakati nataka kwenda kuoga, nikanaswa huko na wababe
wawili, wakinipiga mpaka nikapoteza fahamu tena,nilipozindukana najikuta nipo
chooni, uchi.....na nimetundikwa na suruali yangu kama vile nataka kujiua....mguu
mmoja umekanyaga lile sinki la chooni, ilitakiwa niteleze ile nguo inikabe
ionekane nimejiua,..
Walinzi wakaja wakanitoa, nikapelekwa
mbele ya watawala, maaskari wa magereza, kuhojiwa kwanini nataka kujiua, nikawaelezea,
ilivyokuwa lakini hawakuniamini..
‘Kwanini unajiua wakati kesi yako
yenyewe unahitajika wewe kunyongwa, ..si umeua wewe,na hukumu yake na wewe uuliwe,
haina haja ya kujiua, subiria muda utafika utawekwa kitanzi,...si unataka kufa,
kama ulivyoua wenzako,...’akaambiwa
‘Lakini mimi sijajiua, ...walinipiga
na kunitundika hapo,...’akajitetea profesa.
‘Acha ujanja ujanja, hapa umefika,
subiria hukumu yako,....na tunakuonya, ukirudia tena, utakwenda kulala chumba
cha maji,....’akaambiwa.
Bro, hapo nimeambiwa ni gereza lenya afadhali,
..hapo nipo kwenye mateso ambayo sijawahi kuyapata bado naambiwa gereza hilo ni
gereza ambao watu wanaombewa wafungwe hapo, kwani kuna unafuu, je hilo gereza
la kifi lipoje.
‘Hilo gereza la kifo lipoje,ni kama
haya ya huku kwetu huku bongo....?’ akauliza
kaka mtu
‘Hahaha, ...bro, huko kuna watemi,
kuna watu wanakula nyama za watu, ulishasikia hilo kwenye magereza yetu,
...humo ndani kuna mijitu imeshindikana hata wakuu wa gereza wenyewe
wanawafahamu, lakini ni mijitu yenye pesa...’akasema
‘Kama ina pesa na ina uwezo huo
kwanini wakafungwa?’ akaulizwa
‘Sheria ni kitu kingine bro,
wamefungwa kutokana na sheria, lakini humo ndani ya gereza ni nani atajua ni
nini kinachoendelea, ni nani atasema, na hata kama wanafahamu, pesa
inatenda,...kwanza ukisema unakatwa kidole, unakatwa mkono,..na anayekufanya
hivyo, unaweza hata usiomuone..utamshitakia nani....’akasema
‘Kwa vipi...?’ akauliza kakamtu
‘Bro, tuendelee na kisa chetu,
tukifika huko nitakusimulia uone watu walivyokuwa wababe, watu wanakata nyama
yako na kuitafuna mbele yako...watu wanaua wanaotoa utumbo wa mtu huku anajiona.....watu
ni wanga, wachawi, lakini uchawi wao ni wa mchana,kweupe......’akasema
‘Haya endelea maana unaongezea chumvi
tu hapa,....sikuelewi....’akaambiwa na kaka mtu
‘Utanielewa tu,....ila sasa
nakurejesha gerezani nipo nasubiria kesi yangu,na nikiwa nimepumzika nikiwa na
mawazo,mara nikasikia ninaitwa kuwa nina mgeni....
Tuendelee na
kisa chetu
****************
Nilipofika
sehemu ya kukutana na wageni, nikamkuta mama mtemi, alifika na ajenda ile ile
ya...anataka kujua pesa ipo wapi, ili amlipe wakili ili awalipe watu mbali
mbali ambao yeye kajidhamini kwao, akijua pesa ipo,...
‘Na humu
watakutoa,...kwani wewe hustahiki kuwekwa humu, ukumbuke umewekwa humu kwa
mbinu tu....sasa waliokuweka humu, wanataka upelekwe kwenye gereza
linalokustahiki....’akasema mama mtemi
‘Natakiwa kupelekwa wapi....na wakati kesi
bado, sijahukumiwa?’ akauliza profesa.
‘Hukumu ni
kitu kingine, hata kama hujahukumiwa bado ulistahiki kukaa humo, kama
wanavyofanyiwa wenzako wenye kesi kama yako, kesi yako ni ya mauji,hukustahiki
kukaa humu...’akasema mama mtemi.
‘Lakini
sijaua, hata ushahidi unaonyesha hivyo....’akasema profesa
‘Ushaidi huo
kautengeneza nani,...kazi yote hiyo kaifanya nani, hadi hapo ilipofikia...?’
akauliza mama mtemi
‘Ni huyo
wakili, namshukuru sana....’akasema profesa
‘Unamshukuru
eeh, unafikiri anatangaza dini pale,...yule anahitaji pesa yake, sasa wewe umedanganya,
ukanifanya nijidhamini kwa watu mashuhuri, na nilitarajia kijana wako akija
kwako ungemuelekeza wapi pesa zilipo, lakini ukawa unampiga tarehe, hii ina
maana gani.....?’ akauliza mama mtemii.
‘Lakini mimi
sijui pesa zilipo,...pale nilipohisi zipo ndio hapo nilipomuelekeza huyo kijana
na isje mumezichukua halafu mnanizunguka, nikasema , nikiwa hata mimi sina
uhakika kuwa kweli zipo hapo au ndio mjanja kaziwahi.
‘Kwakweli
umaniabisha sana, hata sijui uso wangu nitauweka wapi, maana hao wakuu
waliokusimama hadi usipelekwe gereza la kifo, wanafikiria mimi
nimewatapeli...’akasema
‘Sasa mimi
nitafanyaje....ningelikuwa huru, ningejaribu kutafuta mwenyewe....’akasema
profesa
‘Hapa sasa
mimi unanichanganya, hawa watu nitawalipa nini, kwa hali ilipofikia, mimi nakuachia
kesi yako mwenyewe, ...wakili kakasirika, nilimlipa mimi kiasi kidogo cha
kuanzia, ikijua pesa ipo,....’akasema akionyesha kukasirika kweli.
‘Kwa hali
lipofikia, siwezi kuendelea kumlipa tena,
siwezi kuoteza pesa yangu, na hata hivyo, nitapatia wapi pesa, ...hapa nilipo
nimechanganyikiwa, hata sijui nifenye nini,...kwanza sina uhakika wa marejesho
ya pesa zangu, ukifungwa maisha je....’akasema
‘Lakini,..siwezi
kufungwa maisha, mimi sina kosa, sijaua...’akasema profesa
‘Kama huyo
wakili ataendelea na hii kesi, uhakika wa wewe kushinda ni mkubwa, lakini
kutokana na kukosekana kwa hizo pesa, mimi sina pesa za kumlipa tena, nab ado atakuwa
anadai, hata sijui nitafanya nini....’akasema akikunja ngumi kuashiria hasira
‘Ndio maana
nilitaka kuongea na kijana wangu anaweza kunisaidia kunilipia,....’akasema
profesa.
‘Kijana wako!!
Yule mpuuzi, nimeongea naye mengine anakwenda kuongea mengine, mpuuzi mkubwa,
kwanza hana pesa kabisa...mwenyewe ana madeni kibao,... ‘ akasema
‘Madeni
kutoka wapi...?’ akauliza profesa
‘Mpuuzi yule
....yeye alijua akimpata binti yangu ndio shida zake zitakwisha, halafu
anajiunga na hao wajinga, anafikiri wale watamlipa nini,...kaniambia shida zake
nyingi, sizani kama nitakubaliana naye amuoe binti yangu, sikubali kabisa,
ataniletea shida tu....’akasema
‘Lakini
amekubali kukutumikia wewe, naona hata kwenye kesi amesimamia kunikandamiza ili
kukurizisha wewe, sio kwamba mumepanga iwe hivyo....?.’akasema profesa
‘Wewe huna
akili kweli,... ina maana mimi nimlipe wakili na bado nimtumie yeye
kukukandamiza wewe, mimi ninachofanya ni kuangalia masilahi yangu basi..., kama
hakuna masilahi siwezi kupoteza muda wangu, nikusaidie wewe kwani wewe ni ndugu
yangu, kiukweli wewe ni adui yangu, lakini kama kuna masilahi, uadui nauweka
pembeni....’akasema
‘Kwahiyo tufanyeje
maana wakili aliniambia anataka kujitoa,... tafadhali mama mtemi nipo chini ya
miguu yako, nakuhakikishia akinitetea, nitajitahidi kuzipata hizo pesa ...’akasema
profesa akitaka kupiga magoti, lakini moyoni hakujua wai atazipatia hizo pesa
na ikizingatia yupo gerezani
‘Mimi siwezi
kudanganyika tena,.... labda useme pesa
hizo zipo wapi, nikiwa na uhakika, mimi nitajua jinsi gani ya kumweka sawa,
ujue nay eye yupo kazini, hawezi kufanya kazi isiyo na malipo, yeye ni wakili
binafsi, na kazi hiyo ndiyo inayomweka mjini...’akasema mama mtemi
‘Mimi sijui
wapi hizo pesa zipo, nilipotoka pale ule mfuko wenye pesa niliurushia sehemu
hiyo, niliyomuelekezea huy kijana, kama hazipo hapo mimi siwezi kujua zaidi....huenda
huyo aliyenigonga kichwani alizichukua, akaniachia mfuko mtupu, akawa kaweka
vitu vingine nikahisi ni pesa...’akasema
‘Ashindwe
kuzichukua muda huo, aje kuzichukua baadaye, huyo naye bwege,....’akasema
‘Unaongea
kama vile unamfahamu...’akasema profesa
‘Ningemfahamu
si ningeenda kwake,...nisingemuachia aondoke na pesa hizo,...sijui atakuwa ni
nani...mmh,mbona katajirika, lakini sitatulia mpaka nimtambue,....ila huyo mtu
hana akili kabisa....’akasema akisimama kuondoka
‘Sasa
utanisaidiaje,....?’ nikamuuliza
‘Mimi sijui,
kukusaidia kwangu ni mpaka niwe na uhakika wa pesa, kama una njia nyingine za
kupata pesa niambie,...’akasema
‘Mhh,
kiukweli,...kama ningelikuwa sipo kifungoni, ningekuwa nyumbani , labda ningeliweka dhamana
ya nyumba yangu...’nikajikuta nimesema hivyo
‘Nyumba eeh,
kweli...umesema jambo la msingi,...nyumba eeh, Kweli hapo umeongea kitu....’
akaruka na kukaa
‘Nilisikia
kuwa nyumba yako ina thamani kubwa, waliofika huko wamethibitisha hilo,... sasa
tufanye hivi, mimi niongee na huyo wakili, ili aweke mkataba, wa dhamana ya
hiyo nyumba, unasemaje ...’akasema
‘Hapana ngoja
nifikirie kwanza,....’akasema profesa
‘Hamna muda
wa kufikiria hapo, .....kesho wakili atakuja mtaandikishana, kesi ikiisha,
...hata kama utafungwa kidogo, lakini tuwe na uhakika kuwa kutapatikana pesa,....sasa
wewe utatoa muda ambao utaweza kuitafuta hiyo pesa,muda ukipita nyumba inapigwa mnada, ili pesa za watu
zipatikane na mimi hapo hapo nitapata pesa ya madeni yangu...hilo wazo zuri
sana,...sasa akili imetulia..’akasema akichukua simu yake
‘Nipe muda
wa kufikiria kwanza usiharakishie hilo wazo, maana sijajua ni nini
kinachoendelea huko nyumbani, na ujue naweka dhamana tu, nikitoka nitatafuta
hizo pesa, siwezi kuuza nyumba yangu....’profesa akasema
‘Hakuna cha
muda hapa,...wewe unadaiwa pesa nyingi sana, nyumba hiyo ndio itakuwa mkombozi,
....unafikiri, wewe utapatia wapi pesa,....huna jinsi inabidi hiyo nyumba
ipigwe mnada, ili hawa watu waliokudhamini wapate pesa zao....’akasema na
kupiga namba, na mara akawa anaongea na wakili
Waliongea
kwa muda, na baadaye akakata simu na kusema
‘Wakili
analifuatilia hilo , ili kuhakikisha kuwa kweli hiyo nyumba yako inaweza kulipa
madeni ya watu ikiwemo dharama zake....hapo anaongeza gharama zake za
kufuatilia hilo jambo..., nina imani hiyo nyumba italipa, kwahiyo kuanzia sasa
ujue wazi nyumba itapigwa mnada, na kama tutapata mteja mnzuri, basi
itasaidia.....’akasema
‘Hapana mimi
nimesema nyumba ni dhamana tu, mwenyewe nikitoka nitatafuta pesa yenu,.......’akasema
profesa
‘Wewe, acha
upuuzi, utatoka lini, na ukitoka pesa utapatia wapi, ...mimi nakwambia maana
nina uzoefu wa jela,ukitoka jela unakuwa kama bwege fulani, akili hata haifanyi
kazi tena....’akawa anashika kichwa kama anapiga mahesabu.
‘Nyumba
ndiye muokozi wako...angalau kesi ya mauaji itapata mtetezi,...wewe hebu
fikiria, ni lipi jema, ukafungwe maisha, au uuze nyumba hiyo, angalau hata
ukifungwa muda mfupi, sio mbaya,...maana kiukweli, una makosa, hata kama sio
makosa ya mauaji, lakini kuna makosa mengine.....’akaambiwa
‘Hamjui
mateso gani ninayoyapata huko jela, watu wamenikamia, .....na wengine wanataka hata
kuniua, nimewadanganya kuwa nikitoka nitahakikisha nawapatia pesa yao, kwahiyo
hayo ni madeni mengine...’akasema profesa
‘Hahaha,
nikuambie kitu, jela hiyo haina shida,..ngoja ufike jela ya kifo, gereza la
kifo, ile kupokelewa tu, ni lazima upoteza fahamu, wanakujaribu, ..hahaha, huko
jela ya kifo, ..ni kifo kweli...’akasema
‘Nakuonea
huruma sana...lakini ni lazima uonje shida yake, ili ujifunze, nina imani kama
utafika huko, ukatoka salama, huwezi tena kurudia tabia hiyo, kamakweli utatoka
salama...’akasema
‘Ina maana
ni lazima nifungwe, mimi nilijua wakili atanitetea, kesi nishinde, ina maana
gani sasa kuuza nyumba yangu....’akasema profesa
‘Wakili
atafanya kila liwezekanavyo, kwanza ni kupigania hilo shitaka la mauaji, hilo
ndilo muhimu sana....ukishinda hapo ina maana umeokoka na kitanzi, au kifungo
cha maisha, haya makosa mengine ni miaka mitano, au sita,....chini sana ni
miaka mitatu, ni afdhali kuliko kifungo cha maisha....’akasema
‘Miaka
mitatu....sita..mitano.....unatania...siwezi, nitakufa, sasa hivi unaona
nilivyokwisha, hata miezi mitatu bado.....’akasema profesa
‘Hahaha...ndugu,..ndugu,
ulifikiria nini wakati unafanya hayo madhambi, zawadi ya
madhambi ni
nini....ukijiingiza kwenye madhambi hayo, ujue kuna kufungwa, ujue kuna kufa,
ujue kuna kuumia.....huwezi kuwadhulumu watu ukategemea kuishi kwa amani, hata
siku moja, ni lazima siku moja utalipa, na malipo yake ndio hayo...’akasema
mama mtemi
‘Hata sijui,
....na tatizo nyie watu hamuaminiki...na kama ni hivyo, kwanini huyo wakili
asitafute mbinu, nikatoka kabisa, kesi hii ikafutwa kabisa, maana yote hii
najua ni fitina, ni wangapi wanafanya haya madhambi na bado wapo mitaani,
hawajafungwa kwanini mimi...’akalalama profesa
‘Kwanini
wewe....hahaha, hilo swali unalo jibu lake, na nikuambie kitu, huu sio muda wa
kulalama, maana unajua kosa lako ni nini, haya yote umejitakia wewe mwenyewe,.....nilikuonya,
unakumbuka,...uliza, ukiingia anga za mama mtemi, utajua, lakini sasa..sio muda
wa kuyawaza hayo,...au unataka kusema nini?’ akasema mama mtemi.
‘Lakini.....’akataka
kusema kitu profesa na mama mtemi akamkatiza na kusema
‘Lakini...nini,
unataka kusema nini, ,...huuu sasa sio muda wa kulaumiana, hatujui hakimu
atakufunga muda gani, wakili atajaribu kadri awezavyo kukutetea, muhimu kwanza
ni kuhakikisha shitaka la mauaji linaondoka, hicho ndicho kipaumbele chetu,...nitaongea
naye nitamuweka sawa, .. .’akasema akiangalia saa.
‘Unajua mimi
sasa nina imani...kwa vile sasa kuna uhakika wa pesa, kazi iliyobakia ni
kupanga mashambulizi kwenye ulingo wa mahakama,... huyo wakili atasaidia wewe
mwenyewe si-umeona kazi anayoifanya...tuombe
mungu hiyo, kesi ya mauaji iondoke, yabakie hayo makosa mengine,,...’akasema
mama mtemi.
‘Vyovyote
iwavyo, ...nimechoka ...kama mwaka utaisha nikiwa jela, sijui kama nitakuwa
hai...’akasema profesa
‘Hahaha....bado.....lakini
kwanza hebu nikuulize wewe huwezi hata kukisia ni nani mwingine anaweza kuwa
kazichukua hizo pesa,maana pesa ingekuwepo,....aah,sijui, pesa
inaongea.....’akasema
‘Mhh, hata
sijui...sijui nani kazichukua hizo pesa, kwani huyo kijana wangu kasema nini ,
kwanini hamkuja naye, ananitia mashaka
sana, nilitaka niongee naye nijua alivyofanya, katafuta wapii na wapi, kwanini
hataki kuja kuniona...?’profesa akasema kama anauliza
‘Yule achana
naye, si umeona ni shahidi wa hao watu, hawezi kukusaidia kitu kwa hivi sasa,
na huwezi kumlaumu kwa hilo, unachotakiwa kufanya ni wewe kuwa muwazi kwangu..na
ili ufanikiwe, ili wakili aweze kushinda, muelezee kila kitu , jinsi ilivyo
kuwa...’akasema
‘Nilishamuelezea
kila kitu,...hakuna nilichomficha...’akasema profesa
‘Ulimuelezea
hata huko ulipoficha hizo pesa, wewe ni bwege kweli...’akasema huyo mama
‘Sina cha
kumuelezea kuhusu pesa maana sijui wapi zilipo, ....niamini hilo, kilichotokea
pale siwezi kutambua vyema, niliamuka nikiwa sijitambui, nilipoangalia chini ya
meza nikauona huo mfuko, nikajua ndio mfuko wa pesa, nikauchukua na kutoka
nao...’akasema
‘Hukutizama
kuwa una pesa...?’ akauliza
‘Sikutizama,
....niliubeba tu, nikakimbia nao, nikipitia ngazi za nyuma, sikupitia kwenye
lifti, nilipofika eneo lenye uwazi, nikaudosha huo mfuko, sehemu ambayo sio
rahisi kuuona, ....’akasema
‘Eneo gani
hilo la uwazi, maana pale yapo maeneo mengi, ni kwenye gorofa ya ngapi...?’
akauliza
‘Sikumbuki,
nilikuwa nimechanganyikia,....na sikuwa na uhakika kama ulikuwa na pesa, au
kulikuwa na kitu gani kingine ni hapo hapo nilipomuelekeza huyo
kijana....’akasema
‘Wapi,
...nielekeze wapi nikajaribu kutafuta mimi mwenyewe.....’akasema huyo mama
mtemi
‘Nilimuelekeza
kijana, najua atakuwa amekuambia ni wapi,lakini sina uhakika ni gorofa ya
ngapi, maana nilikuwa nateremka chini kwa kupitia ngazi za watembea kwa miguu....’akasema
‘Nikuambie
kitu,.....haya sasa ni mimi na wewe, huyo kijana achana naye,.. ukimueleza kitu
ujue kitafika kwa watu wa usalama,...lakini tuyaache hayo,maana hata kama
uliweka wapi, huwezi kuukuta tena....watu wengi wamekuwa wakiutafuta,...labda
kama kuna sehemu nyingine umeficha...’akasema
‘Sijaficha
kitu,.....niamini kwa hilo...’akasema profesa akijaribu kukumbuka
‘Ok,....tuyaache
hayo, ....muhimu kwa sasa ni hilo, akija wakili kesho anakuja na huo mkataba,
kuwa umekubali hiyo nyumba iuzwe, ili uweze kulipia madeni na gharama za hii kesi,
kuanzia sasa mimi sitaki kusikia vinginevyo..tumeelewana kwa hilo...’akasema
mama mtemi
‘Nitasema
nini tena hapo, najua unachowazia wewe hapo ni pesa tu, hujali mustakabali wa
maisha yangu,... hujali afya yangu, mimi siwezi kuishi jela, nitakufa,na sasa
unataka kunimaliza kabisa nisiwe na hata na nyumba ....’akasema profesa
‘Hilo ni shauri
lako,sema wapi pesa ipo, tuachane na hiyo nyumba....ujue wewe mtu, ukileta ubishi, ujue kweli unafungwa, na ujue
huko jela utakwenda kukutana na maadui zako...kwa hivi sasa huna ujanja...,na kama
utabadili huu msimamo, ujue kuwa unakwenda kufa,...usije kunilaumu kwa
hilo...’akasema
‘Tatizo hili
wazo limekuja kwa haraka sana ....nahitajia muda wa kulifikiria...’akasema
‘Wewe
umeshalisikia gereza la kifo lilivyo,...si ulishaambiwa, ....huko, kama
uulivyosikia ukiingia huko, uage kabisa, na tatizo la huko, unakufa taratibu
huku unajiona, kwa mateso makali, ni aheri ungelinyongwa ikjulikana moja..kwahiyo
kesho fanya maamuzi ya busara, nimeshaongea na wakili, na kesho anakuja na huo
mkataba...’akasema
‘Nitafikiria
na kesho akija huyo wakili nitakuwa na jibu tayari....’profesa akasema na mama
mtemi akainuka kwenye kile kiti na kuanza kuondoka hata bila kusema neno
zaidi....na profesa akasema;
‘Jitahidi
kijana aje tuonane hiyo kesho....’akasema na mama mtemi hakusema neno akawa
ameshaondoka.
Bro, mimi sikuwa
na la kufanya, na ningekuwa na mawazo angalau ningewapigia simu huku, ili muone
jinsi gani ya kunisaidia, si mungeuza hata ngombe, .....lakini hapo akili
ilikuwa inawaza jinsi gani ya kuokoka na hicho kifungo.....akilini niliwaza
kufungwa zaidi kuliko hiyo nyumba.....usiku ukaingia na asubuhi ikafika...
WAZO LA LEO: ni toba ya kweli:
Tukumbuke
dhambi ya kumtendea mwanadamu mwenzako, ukamfanyia ubaya mwenzako, ukamdulumu
haki yake, ukajiona wewe ni mjanja, ukapata ukatajirika, msamaha wake ni wewe mwenye
kwanza kutubu kwa kukiri moyoni kuwa umekosa, halafu pili umuendee yule uliyemtendea
huo ubaya umuombe msamaha, akubali, na akubali kutoka moyoni kiukweli, kuwa
amekusamehe, kitu ambacho sio rahisi .... Basi tuache kutendeana ubaya tuache
dhuluma, ili tuwe na dunia yenye amani na mbele ya mungu tupate makazi mema.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment