‘Bro,... sitakuelezea ilivyokuwa kwa
mashidi wengine ambao waliitwa kuonyesha kuwa Profesa ndiye muuji, ....mimi
sasa nitaenda moja kwa moja kwa muhusika wetu...’akaendelea kusimulia mdogo
mtu.
‘Muhusika wetu?’ akauliza kaka mtu
‘Siunajua kesi kama hiyo, wanaanzia
mbali, ...na wanawaita watu mbali mbali, waliitwa walinzi na wahudumu wa jengo
hilo, maaskari waliokuja badaye, dakitari...na ujue jengo hilo ni kubwa na lina
shughuli mbali mbali, kwahiyo walitafuta kila mtu aliyeniona,...
Kwa ushahidi uliotolea, kila mtu
aliamini kuwa profesa ndiye aliyefanya hayo mauaji, ...
‘Bro, nilikiona kitanzi hicho....na
moyoni nikawa naomba angalau aje shahidi ambaye atatoa ushahidi wa kuniokoa, ,
....maana wote waliopita walikuwa wakinikandamiza mimi , japokuwa wakili
mtetezi alijitahidi sana kunitetea, lakini ilionekana wazi mimi ni
muuaji...’akasema mdogo mtu akiendelea kumsimulia kaka yake.
‘Nikuulize kwanza mdogo wangu je
kweli wewe uliua..?’ kaka mtu akauliza swali na mdogo mtu akatabasamu, na
kusema...
‘Bro....tuendelee na kisa
chetu,....utaona mwenyewe.....’akasema
‘Sasa ilikuwaje kwa kijana wetu
hakuitwa tena kutoa ushahidi..?’ akaulizwa
‘Aliitwa, ndio maana nasema
tutakwenda moja kwa moja kwa muhusika wetu, kuliko nikianza kuelezea kila
alichoongea shahidi, mashahidi walikuwa ni wengi, na waliongea mengi sana....’akasema
‘Nimekuelewa, ....endelea....’akasema
kaka mtu
‘Wengi, ....walitarajia,...labda, kijana wetu , kwa vile nilimlea mimi
angeonyesha utu wa kunitetea, angalau kidogo, ikionekana kuwa mimi nakabaliwa
na kosa la mauaji, ...kiubinadamu angelitakiwa kuonyesha angalau huruma fulani.
‘Lakini kama uliua, ni nani
angekuhurumia,...usimlaumu bure.....’akasema kaka mtu, nay eye hakujali kauli
hiyo akaendelea kuongea
‘Na hata mimi moyoni niliomba hivyo,.....aonyeshe
moyo wa huruma, angalau aonyeshe msaada fulani,.... japokuwa alikuwa upande wa
mashahidi wa wanaoshitaki....
Na wakati nawaza hayo mara
nikasikia.....
‘Tunamuita tena shahidi wetu, kijana
yule aliyewahi kuishi na mshitakiwa, .....’nikasikia akiitwa kijana wetu,
nikiwa nimezama kwenye dimbwi la mawazo....
Tuendelee na
kisa chetu........
*************
Kijana wetu
alikuja na safari hii hakuonekana na zile mbwe mbwe zake za awali za kunata na
madharau, safari hii alionekana mtaratibu na adabu kidogo...
Alifuata
taratibu zote za mahakamani, na akaanza
kuhojiwa na muendesha mashitaka kama ilivyo ada..., na hakutaka hata kunitupia
jicho, kwani pale nilipo nilikuwa namuangalia kwa jicho la kutia huruma.
‘Wakati
unaishi wewe na huyo mlezi wako, uliwahi kumuona mlezi wako huyo, akiwa na
bastola...?’ akaulizwa swali, swali lililonifanya nihisi kitu kama kichoma
ndani ya moyo.
Ukumbuke nilishawaambia watu wa usalama walionihoji kuwa mimi
sijui kutumia silaha, hasa bastola.
‘Ndio,
...niliwahi kumuona akiwa nayo,....’akasema shahidi moyoni nikasema sasa
nimekwisha.
‘Alikuambia
bastola ni ya nini.....? akaulizwa, nilitamani shahidi aniangalia ili
nimuonyesha ishara ya kuwa asiseme lolote.
‘Alisema bastola
hiyo ni ya kikazi, na wakati mwingine huazima kutoka kwa jamaa zake,.....anasema
wakati mwingine bastola hiyo anaitumia kuwatishia wale wanaokataa kutoa pesa
yake, .....’akasema na watu wakaguna.
‘Kwahiyo
aliwahi kukuambia kuwa anaweza kuitumia hiyo silaha...?’ akaulizwa
‘Ndio alisema
anaweza kuitumia, na mimi nilimuomba anifundishe, akawa ananionyeshea kuwa
ukitaka kufyatua risasi unavuta hiki unalenga hivi....akanionyeshea lakini
hakuwahi kunionyesha kwa vitendo.....’akasema
‘Ukisema kwa
vitendo una maana gani...?’ akaulizwa
‘Yaani
kuifyatua hiyo bastola na kutoa risasi.....’akasema
‘Aliwahi
kukuonyesha risasi zake,...?’ akaulizwa
‘Ndio
alinionyesha hata jinsi ya kuziingiza hizo risasi kwenye hiyo
bastola...’akasema
‘Kwahiyo
yeye, alikuambia bastola ya kikazi anapewa na wahusika, au wakati mwingine
anaazima, je akiazima huwa anaazima kwa nani...?’ akaulizwa
‘Alisema
huwa anaazima kutoka kwa marafiki zake, anaojuana nao, hasa wale anaofanya nao kazi, ...’akasema
‘Anaofanya nao kazi ni akina nani hao, ....!? Alikuambia kazi gani?’ akaulizwa
‘Aliniambia
yeye wakati mwingine anafanyakazi ya ulinzi na watu wengine....kwahiyo anapewa silaha kwa ajili
ya kufanikisha ulinzi huo, na wakati mwingine anakuwa hana kazi, lakini inatokea anahitaji
silaha na hayupo kazini, basi hapo huwa anaazima kutoka kwa marafiki zake,
ambao kwa muda huo, wanakuwa na silaha....’akasema
‘Hakukuambia
ni kwanini ahitajie silaha wakati hayupo kazini, au kwanini alihitajia hiyo
silaha?’ akaulizwa
‘Ni wakati
akikusanya pesa zake kwa watu anaowadai, huwa anasema ni muhimu kwenda na silaha.....’akasema
‘Ina maana huwa anakusanya pesa nyingi sana mpaka ahitajie silaha,..? Ni pesa zake
kutokana na biashara ya madawa au kutokana na nini...?’ akaulizwa
‘Aliniambia
kuwa yeye huwa na wateja wake, anaowadai kwa shughuli mbali mbali, kama vile
walichukua madawa kwake na shughuli mbali mbali, lakini mimi nilijua tu ni hao
anaowadai kwa mlungula, japokuwa hakuweza kuniambia hivyo moja kwa moja...’akasema
na watu wakacheka.
‘Alikuambia
hivyo...au wewe mwenyewe ulifikiria hivyo?’ akaulizwa
‘Alitumia
kauli ya wadeni wake anaowawajibisha kwa uchafu wao, sasa I nani kama sio hao....’akasema,
na muendesha mashitaka akasimama na kwenda sehemu yenye vidhibiti vya ushahidi
akachukua bastola.
‘Hebu
angalia hii silaha,ni silaha gani hii..?’ akaulizwa, shahidi akaiangalia na
kusema.
‘Ni
bastola.....’akasema
‘Uliwahi
kuiona kabla...?’ akaulizwa
‘Ndio, ila sina
uhakika kama ndio yenyewe..., lakini zote zinafanana hivyo, aliwahi kunionyesha
kama hiyo lakini sina uhakika kuwa kweli ndio hiyo.....’akasema
‘Kwahiyo
uliposikia kuwa mlezi wako huyo wa hadaa kaua hukuona ni bahati mbaya, kwa
jinsi alivyokuambia, na ulivyoona kuwa alikuwa na silaha kaam hiyo, na
angeliweza kuazima kwa marafiki zake, na angeliweza kuitumia, kama mtu
angelikataa kumlipa pesa yake...?’ akaulizwa japo swali liliwekewa pingamizi,
lakini baadaye ilitakiwa lijibiwe, shahidi akasema
‘Kwakweli
mimi sikuona ni ajabu maana aliwahi kuniambia yeye mbele ya pesa yake, haogopi
kuivuta hiyo trigger, hasiti kuua,..kama
mtu anamdai pesa yake akakataa, atamtishia akileta ubishi, phaaah...’akasema
akionyeshea kwa mkono ishara ya bastola.
‘Inatosha
kwa hivi sasa, muheshimiwa hakimu kama wakili mtetezi ana maswali kwa shahidi
aendelee....
Hakimu
akawauliza watetezi kama wana maswali ya kumuuliza huyo shahidi, na wakili mtetezi
akasimama, na kumsogelea huyo shahidi;
‘Unakumbuka
kuna siku mlezi wako aliitwa shuleni, ukiwa umekosea, ulipokuwa na makundi ya
vijana wa mitaani,....’akawa anaelezewa
‘Umeanza
yale yale ya utotoni,...’akalalamika shahidi
‘Unakumbuka siku mlipokamatwa hadi kufikishwa polisi,
unakumbuka mlionekana na kitu gani...?’ akaulizwa na huyo shahidi akashituka,
na kusema;
‘Muheshimiwa...
nilishakuambia kuwa kipindi kile ulikuwa ni utoto...sikuwa na akili za kuelewa
kitu, na hayo hayana maana kwangu kwasasa,wewe nai mwanasheria, unajua umri
kama ule hauna maana yoyote kisheria....’akasema shahidi
‘Usinifundihe
sheria, najua ni kwanini nakuuliza hivyo, wewe jibu swali je siku mlipokamatwa mlikutwa
na vitu gani......’akaulizwa
‘Na ...na
sigara, si sijui na kitu gani.....’akatulia
‘Kila kitu
kipo kwenye maandishi hapa unatakiwa kujibu ukweli mtupu, sema ulikutwa na vitu
gani...?’ akaulizwa
‘Bangi,
sigara na na ba-ba-stola....lakini ilikuwa ni bastola bandia....’akasema na
watu wakacheka
‘Ina maana
polisi hawajui kuwa ni bastola bandia,waliandika uwongo, au? Ujue mahakamani, au uniambie kama walichokiandika kwenye hizo
nyaraka zao ilikuwa ni uwongo, walikusingizia...?’akauliza
‘Lakini
nimekuambia kipindi kile nilikuwa sijatulia,..kwahiyo sikuwa na akili za
kutambua kuwa ni bastola halisi au ni bastola bandia...na siku zilivyokwenda
nikaja kujitambua, nikaachana na tabia hiyo, nikawa nasoma,hata walimu walikuja
kunishangaa nilivyokuja kubadilika...’akasema
‘Najua kuwa
ulikuja kubadilika, baada ya juhudi kubwa za mlezi wako huyo, ila swali langu
ni hili,..je kwa umri huo, unaouita wa utoto, ulikuwa huweze kutambua bastola
halisi na bandia au sio?’ akaulizwa
‘Ndi-o...’akajibu
kwa kusita
‘Je ulijuaje
kuwa bastola aliyokuwa nayo mshitakiwa ilikuwa bastola halisi na sio bandia...au walikuambia hao
waliokufundisha kusema hivyo?’ akaulizwa
‘Yeye mwenyewe
mshitakiwa ndiye aliniambia kuwa hiyo bastola ni bastola halisi ni hatari, ndio
maana hakutaka mimi mwenyewe niishike...’akasema
‘Hebu
utkumbushe tena, ni nani aliyekusaidia wewe kubadilia, na kutulia kwenye masomo
yako,... mpaka ukawa mtoto mwema, na ukaweza kufuatilia masomo yako, ukaacha
utundu, na mambo ya kuiga, kama hayo ya kuvuta bangi, kujiunga na makundi ya
kihuni,..na hata akili za masomo
zikaongezeka, ...?’ akaulizwa na akawa kainama chini.
‘Unatakiwa
ukinijubu uniangalie, kwanini sasa unainama chini, hujiamini tena, haya, sema ukweli wako,na ni vyema ukasema
ukweli ukumbuke umeapa kuwa hapa utasema ukweli ,ukweli mtupu, ...?’ akaulizwa
na hapo akageuka kumuangalia mshitakiwa
‘Ni yeye...mbona
nilishajibu hilo swali kabla, ni kweli sio kwamba muda wote alikuwa mtu mbaya,....kuna
siku kama hajalewa, anakuwa akinielekeza mambo mema, niishi vipi, nisome, na
vitu kama hivyo...’akasema sasa akamwangalia mshitakiwa.
‘Wakati
unafanya utundu, ukiwa na makundi mabaya, hamukuwa mnafundishana jinsi ya
kuitumia silaha, bastola,....mpaka ikafikia mmoja wenu akajeruhiwa....?’
akaulizwa na akashituka
‘Hayo ni
mambo ya kitoto,...ndio mmoja aliumia, ....ndio maana hata tukaja kukamatwa na
polisi, ni mambo mengi ya utoto, mengine siyakumbuki...hata wewe mambo kama hayo uliwahi kupitia...’akasema
‘Tulipitia
lakini sio ya kihuni, hadi kuwa na bastola za moto....’akasema wakili halafu
akauliza swali
‘Wewe
uliwahi kuwashinda wenzako kwa shabaha, umesahau...?’ akaulizwa na hapo
akatabasamu, na kusema;
‘Ndio,
lakini yalikuwa mambo ya utoto, ni mambo
ya kupita tu, ya kuiga, na kiukweli nilipojifahamu nikawa sitaki tena mambo
hayo....’akasema
‘Kwahiyo kumbe
ulikuwa unafahamu kutumia bastola,... sio kweli kwamba wewe ulifundishwa na
mshitakiwa, na huenda hata kwa mlezi wako huyo, hukuwahi kumuona na
bastola,..labda alikuwa na bastola bandia tu, ila umeambiwa useme hivyo, kwa vile
unataka mshitakiwa aonekane ana hatia,au sio....?’ akaulizwa na akakaa kimia
‘Seme ukweli
hutalaumiwa na yoyote ukiongea ukweli, ni kweli ulifundishwa kusema hivyo au
sio,?...’akasema wakili
‘Sijaambiwa
nisema hivyo, muulizeni mwenyewe mshitakiwa kama hakuwahi kunionyesha
bastola...’akasema kwa sauti ya ukali.
‘Lakini
alikuambia ni ya kikazi au sio,....na yeye aliwahi kufanya kazi za ulinzi...au
sio...., na aliruhusiwa kuwa na bastola, au sio?’ akaulizwa
‘Ndio
aliniambia hivyo...’akasema
‘Ila hayo
mengine kuwa angeliweza kuitumia, kwa wadai wake, uliambiwa useme hivyo au
sio...?, ‘ akaulizwa na kukaa kimia
‘Mimi sio
mtoto mdogo wa kuambiwa nisema hivi au vile, mimi ni msomi naweza kujua ni kiti
gani niseme..’akasema kwa sauti ya ukali
‘Sasa kwanini
nikikuuliza swali unakaa kimia...?’ akaumuuliza
‘Maswali
yako yanakera,..ni ya kujirudia rudia kunitega,...’akasema
‘Lakini ni
kweli kuwa kuna mambo umefundishwa kusema, ndio maana unakaa kimia, ukitafakari
au sio, hebu tuambie ni nani alikufundisha hivyo, ..?’ akauliza na wakili muendesha
mashitaka akaingilia kati kuwa wakili mtetezi anamlazimisha shahidi kuongea
anachotaka yeye, na hayo anayoyauliza hayana msingi na kesi yenyewe..
‘Sina zaidi
kwa shahidi huyo, ...’akasema wakili na shahidi akaambiwa na muendesha
mashitaka kuwa ushahidi wake umekamilika akihitajika tena anaweza kuitwa...
Shahidi huyo
alitoka pale sasa akiwa kainama chini hakutaka hata kuwaangalia watu, akatembea
hadi mlango wa kutokea halafu akageuza kichwa kuangalia kule alipokaa
mshitakiwa, akatikisa kichwa... na kuondoka kuelekea chumba cha mashahidi.
‘Shahidi
mwingine....’hakimu akasema akiangalia saa yake.
‘Siku hiyo bro, kila mmoja alijua mimi siwezi
kukwepa kitanzi, na hadi siku hiyo, sio kwamba kesi iliendeshwa kwa siki moja,
ilikuwa inaendelea kwa siku kadhaa, lakini walitaka iishe haraka, ili kama
walivyodai, eneo lao liwe na amani, na siku walikuwa wamebakiwa mashahidi wachache tu
‘Na kwa
ujumla hao waliokuwa wamebakia, ilikuwa ni kama kuhitimisha tu,....kwakweli
hadi hapo nikajikuta sasa nikijua mimi ni wa kifungo cha maisha kama sio
kunyongwa, nilitamani kulia, ...kidume
mie....’akasema
‘Kwanini utamani
kulia, na wakati wewe mwenyewe ndiye ulijitakia kwa uroho wako,....?’
akamuuliza kaka yake
‘Bro sio
uroho, ni kutafuta maisha,...’akasema
‘Haya bro,
ngoja nipumzike, tukija kukutana nitakusimulia ili uone ushahidi uliofuta kwa
jinsi ulivyokuja kubadili mambo,..’akasema
‘Na kijana
wetu hakuitwa tena,...?’ akauliza kaka mtu
‘Utakuja
kuona huko mbele, uone mwanao alivyo na roho mbaya,....sijui karithi kutoka
wapi...’akasema kwa sauti ya hasira
‘Hahaha...umeona
eeh,...na umesahau kuwa yeye ndiye aliyekuwa akikulisha kwa miaka sijui
mingapi, ukawa unatumia pesa ya wafadhili kwa mgongo wake,vya bure hulemeza, na
ukivikosa unaweza kulalamika kama vile ni halali yako....’akasema kaka mtu
‘Sasa huyo
wakili mtetezi alikuwa akimlipa nani, ....maana ulisema huna pesa, au ndio hizo
pesa ulizochukua za mlungula....?’ akaulizwa
‘Bro,...utakuja
kuuona, na hutaamini ukija kuwasikia
mashahidi hawa waliokuja kuitwa baadaye , na hasa pale walipokuwa wakihojiwa na
wakili mtetezi....’akasema
‘Haya
endelea...’
‘Tutaendelea
lakini sio leo nimechoka,acha nipumzike, si unajua mimi ni mgonjwa...’akasema
msimuliaji
NB:
Tutaendelea sehemu ijayo
WAZO LA LEO: Katika maswala la mlinganyo,...kutafuta
haki, yenye kuamua mambo ya pande mbili,
ili kupata ukweli, na kutoa maamuzi yenye busara, ni vyema, ukawa huegemei
upande wowote, hata kama mmojawapo ni rafiki yako, mwenzetu, au hata kama ni
upande wako, au hata kama ni ndugu yako, kwa nia njema, unachotakiwa ni
kusikiliza sehemu zote mbili bila kujali upande wowote. Halafu ndio utoe maamuzi kwa uadilifu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment