Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, August 28, 2015

RADHI YA WAZAZI-35



‘DNA, sio ushahidi sahihi.....?’ akauliza wakili mtetezi, akimuangalia wakili muendesha mashitaka aliyekuwa akiikagua ile karatasi, na wakili muendesha mashitaka akasema.

‘Kila kitu chawezekana mbele ya wanadamu .....’

‘Lakini sio kwa vipimo kama hivyo, hiyo ni DNA, na imesainiwa na dakitari bingwa anayefahamika,.. ‘akasema

‘Kama unaitoa kama ushahidi fuata utaratibu,.... lakini kwa hivi sasa siwezi kuikubalia karatasi kama hii kuwa ni ushahidi...haina vigezo stahiki....’akasema muendesha mashitaka huku akiwa kaishikilia ile karatasi, akawa anatembea kuelekea sehemu yake ya kukaa, na wakili mtetezi akasema

‘Sijaikabidhi hiyo nyaraka kama ushahidi muheshimiwa ....’akasema wakili mtetezi na muendesha mashitaka akawa bado kaishikilia ile karatasi  akiikagua, wakati huo wakili mtetezi alikuwa kamkarabia, na kunyosha mkono kutaka kuichukua ile karatasi,

Hakimu alipoona ile hali akasema;

‘Taratibu zifuatwe mawakili....kama ni ushahidi ukabidhiwe kiutaratibu, sitaki kuwafundisha kazi najua mnaelewa ni nini kifanyike kwa taratibu za kimahakama.....’

‘Muheshimiwa hakimu natambua kabisa bado muda wangu wa kutoa ushahidi , niliitoa tu kumuweka sawa huyu shahidi ili atambue kuwa hapa ni mahakamani, na anachotakiwa ni kusema ukweli, na ajue kuwa hapa kuna mawakili wanasheria, wanaotambua kazi yao vyema....’akasema wakili huyo akimuangalia huyo shahidi na huyo shahidi akawa kainama chini.

‘Wakili mtetezi endelea na maswali yako kwa shahidi...’akasema hakimu
Wakati huo wakili mtetezi alikuwa keshaichukua ile karatasi akawa nayo mkononi, huku akimsogelea  shahidi, na shahidi  alikuwa kainama chini, kama anawaza jambo,....

Tuendelee na kisa chetu....

**************

‘Upo tayari tuendelee na maswali yangu....’wakili mtetezi akauliza huku akimwangalia shahidi na tabasamu mdomoni, na shahidi akainua kichwa kumuangalia wakili huyo akasema;

‘Nipo tayari muheshimiwa...’ na alipotamka maneno hayo wakili mtetezi akasema

Good, safi kabisa,..Sasa unaanza kuelewa, na kuheshimu mahakama, hapa hatutaki kiburi na dharau, kijana anaanza kuelewa..’akasema wakili mtetezi akimgeukia wakili muendesha mashitaka na wakili muendesha mashitaka alikuwa akibonyeza bonyeza simu yake yaonekana alikuwa akiwasiliana na mtu kwa njia ya ujumbe wa maneno.

‘Kama mlivyoona shahidi huyo alikuwa akidanganya, na inasikitisha kuwa amefikia hatua  hata anawakana wazazi wake, hii ni hatari kabisa....’akasema wakili mtetezi.

‘Kwanini unawakana wazazi wako shahidi....’akasema wakili akimuangalia huyo shahidi usoni.

‘Mimi sijawakana wazazi wangu,...ila ninachosema muheshimiwa ni kuwa hao watu sio wazazi wangu ....hao watu ni waongo, mimi nawafahamu, nimeishi na huyomshitakwia nyumba moja namfahamu tabia yake, nimekutana na haowatu wanaoitwa ni wazazi wangu, nimewaona, ....sio wazazi wangu, kwahiyo mimi sipo tayari kuwakubali hata kwa siku moja...’akasema shahidi huyo.

‘Kwasababu gani huwezi kuwakubali na wakati ushahidi nimeshakuonyesha, hukubaliana na hivyo vipimo,...?’ akaulizwa

‘Siwezi kukubaliana navyo, kwasababu sio kweli,,...kama ungekuwa ni ushaidi sahihi ungeliutoa kama ushahidi, lakini kwa vile unatambua sio sahihi ndio maana unanionyesha kwa hivi, na hata, hao wazazi wangu kabisa kabisa, siwezi kuwakubali kwa vyovyote vile...’akasema

‘Je kama ushahidi huo upo kwenye ushahidi wangu, na vipimo hivyo  ni vya kweli, bado utaendelea kuwakana hao wazazi kuwa sio wazazi wako...?’ akaulizwa

‘Nimeshakuambia hao sio wazazi wangu,  nina uhakika huo ushahidi sio halali...na kamwe sitaweza kuwakubali watu kama hao, hilo nakuhakikishia, watafute mtoto mwingine sio mimi, ....’akasema akitikisa kichwa.

‘Nakuuliza tena hata kama kipimo hicho ni sahihi...hutaweza kuwakubali hao wazazi kuwa ni wazazi wako, na kwasababu gani...?’ akauliza na wakili muendesha mashitaka akaingilia kati akasema hayo maswali hayana msingii na hayana uhusiano na kesi.

‘Yana uhusiano na kesi, kwasababu ya kupima uhakika wa majibu ya shahidi, na tunataka kuhakikisha kuwa mshitakiwa ni baba mdogo wa huyu shahidi, kitu ambacho huyu shahidi ana kipiga, na ni vyema tukaisaidia jamii, huyu ni mtoto ana wazazi wake, iakuwaje asiwakubali, .....’akasema wakili mtetezi.

‘Wakili endelea na maswali mengine, hilo limeeleweka.....’akasema hakimu baada ya kutulia akiwaza jambo. Na wakili mtetezi akamwangalia wakili muendesha mashitaka,halafu akamgeukia shahidi, akatabasamu,.

Shahidi alikuwa kakunja uso ,kuonyesha kakasirika, na kama isingelikuwa ni mahakama, huenda, angeliondoka, zake, ..akamuangalia wakili mtetezi, safari kwa macho yasiyo yakujiamini,na wakili akauliza swali jingine.

‘Wewe unasema kuwa mlezi wako, uliyekuwa ukiishi naye alikuwa akifanya biashara ya mlungula, sawa si sawa.....?’ akaulizwa

‘Nilishaelezea hilo,....muheshimiwa,....ndio alikuwa akifanya biashara ya mlungula...muheshimiwa..’akasema

‘Kipindi hicho ulikuwa mdogo, ulijuaje kuwa alikuwa akifanya biashara ya mlungula...?’ akaulizwa

‘Kipindi hicho, sikuwa makini na hilo, japokuwa nilijua kuwa anafanya vitendo hivyo, lakini jinsi nilivyozidi kukua, nimekuja kugundua na kutambua vyema kuwa alikuwa akifanya biashara ya mlungula....’akasema

‘Kwahiyo kwa kipindi hicho hukuwa unafahamu hivyo,umekuja kufahamu sasa hivi ulipoongea na wakili muendesha mashitaka?’ akaulizwa

‘Nilijua hivyo kipindi hicho nilishakuwa mkubwa wa kutambua,...., ila sikuwa makini,...nilijua hivyo, hata kabla ya kuongea na wakili muendesha mashitaka....muheshimiwa’akasema

‘Kama ni hivyo, ...kuwa ulikuwa unajua kuwa baba yako mdogo alikuwa anaendesha biashara ya mlungula,...ina maana na wewe ulikuwa muhusika wa biashara hizo za mlungula au sio...?’ akaulizwa.

‘Kwa vipi niwe muhusika,...,maana mimi nilikuwa mdogo tu, na ...sikuwa nafuatilia mambo yake, mimi nilikuwa nasoma, nay eye alikuwa na kazi zake, na mimi sikuwa na muda wakufuatilia ni nini anachokifanya, ila nilikuwa naona,nasikia anavyoongea na simu, naona matendo yake...’akasema kwa hamaki

‘Kwa vile ulikuwa hufuatilii mambo yake, ...hukuwa na uhakika kama kweli alikuwa akifanya biashara hizo au la....umejua hivyo baada ya kuongea na muendesha mashitaka au sio...?’

‘Nimeshakuambia,...muheshimiwa,  nilikuwa naona, na pia nasikia,akiwasiliana na watu,..’akasema kwa hamaki.

‘Kwahiyo shughuli hizo zakuwasiliana na watu, akifuatilia milungula alikuwa akizifanyia humo ndani,  unasikia, unaona akiongea na wagusika, au sio....?’ akaulizwa

Shahidi akakaa kimia...

‘Huna uhakika na hilo, ....au nikuulize tena swali langu...?’ akaulizwa

‘Mara nyingi mawasiliana ya biashara hizo hakuwa akizifanyia ndani, alishaniambia kuwa vitu kama hivyo, huwa anatakiwa kuchukua tahadhari, kwahiyo mara nyingi alikuwa haongelei hapo ndani....’akasema.

‘Kwahiyo humo ndani alikuwa akiwasiliana kuhusu mambo mengine ya kikazi na mambo yake binafsi..?’ akaulizwa

‘Ndio....muheshimiwa’akasema kwa sauti ndogo

‘Kwahiyo huna uhakika kuwa hata huko nje alikuwa akiwasiliana kuhusu biashara hiyo ya mlungula, huenda ni mambo hay ohayo ya kikazi, au sio....?’ akauliza na shahidi akakaa kimia, halafu akasema;

‘Ndio sina uhakika....lakini ...alishaniambia kuwa akiwa anafanya mambo hayo anachukua tahadhari,..huenda huko alikuwa akifanya hivyo...’akasema

‘Huenda , ina maana huna uhaika.....’akasema na kabla shahidi huyo hajajibu wakili akauliza swali jingine.

‘Katika nyumba mliyokuwa mkiishi wewe ulikuwa na chumba chako au mlikuwa mnachangia chumba kimoja na baba yako mdogo....?’ akaulizwa

‘Nilikuwa na chumba changu,....na yeye  alikuwa na chumba chake muheshimiwa, na halafu kwanini unamuita baba yangu mdogo? ’akasema na kuuliza

‘Kwani mdogo wa baba huwa anatwaje...?’ akaulizwa

‘Lakini huyo sio mdogo wa baba yangu, na hata wafadhili wanafahamu hilo, hata sheria za hapa zinafahau hivyo, ndio maana nilitafutia wafadhili, hilo lipo wazi, usitake kulazimiha,...hao sio wazazi wangu nielewe hivyo, na haitakuwa hivyo kamwe...’akasema

‘Swali langu jingine ni hili je huyo baba yako mdogo,...ulisema alikuwa akija na wanawake,..humo ndani mnapoishi au sio?’ akaulizwa

‘Ndio....huyo `m-shi-ta-ki-wa’ alikuwa akija na wanawake wengine...muheshimiwa.’akasema akimuangalia wakili huyo kwa makini.

‘Na akija na wanawake hao,  wewe unakuwa chumbani kwako, na yeye anaingia chumbani kwako, .....au sio...?’akaambiwa

‘Hapana alikuwa akiingia chumbani kwake,kwanini aingie chumbani kwangu...?.’akasema na kuuliza

‘Na wewe wakati huo upo wapi, wakati anaingia na hao wanawake?’ akaulizwa

‘Chumbani kwangu,..nasoma...au nimelala....’akasema

‘Sasa uliwaonaje wakifanya huo uchafu,maana kwa kauli yako ya mwanzo ulisema alikuwa akija na wanawake na kufanya uchafu wao mbele yako,..au sikukusikia vyema? ‘akauliza na kabla hajajibu wakili akauliza

‘Au usema ukweli,.... wewe ulikuwa na tabia ya kwenda kuwachungulia chumbani kwao...’watu wakacheka

‘Mimi siwezi kufanya hivyo,...sikuwahi kwenda kuwachungulia, mimi sia tabia hizo chafu,... mimi nilikuwa nasoma chumbani kwangu, sikuwahi hata siku moja kufanya mambo kama hayo.....’akasema kwa hamaki na alipotambua kuwa kaongea kwa hamaki akasema;

‘Muheshimiwa...’.

‘Kwahiyo hiyo kauli uliyosema mwanzoni kuwa alikuwa kifanya uchafu mbele yako, ulikuwa umejitungia, wewe mwenyewe, au uliambiwa useme hivyo,....?’akaambiwa na kabla hajasema neno akaulizwa swali jingine.

‘Hebu nikuulize swali, ni nani wanavaa hereni, na kusuka nywele, kwa kawaida ni nani wanafanya hivyo...?’ akaulizwa na akaonyesha uso wa kutahayari, na kugeuka kwa muendesha mashitaka ili amtetee kwa swali hilo.

‘Swali hilo linahusiana nini na kesi hii......’akasema akionyesha mikono ya kutahayari, na huku akiendelea kumuangalia muendesha mashitaka.

‘Hiyo sio kazi yako, kazi yako ni kujibu swali ninalokuuliza...’akaambiwa

‘Ni wanawake.....’akasema na alipogundua hilo swali ni la mtego, akasema

‘Hata wanaume , wasanii, wacheza mziki, ...wanafanya hivyo...’akasema

‘Kwanini wewe umetoboa masikio, unasuka nywele, eeeh, kwani wewe ni msanii, mwanamziki au....kwanini unawaiga wanawake,  hujiamini ?’ akaulizwa,na akajishika masikio, na kusema

‘Ni uamuzi wangu binafsi,..sizani kama inakuhusu...na ni mitindo tu’akasema

‘Je mzazi wako alifurahia hicho kitendo...?’ akaulizwa

‘Kitendo gani....?’ akauliza

‘Cha wewe kutoba masikio na kusuka nywele....?’ akaambiwa

‘Hapana hakupenda, ...alinikemea...alinikataza....’akasema

‘Wewe ulipokemewa ulisema nini...?’ akaulizwa

‘Nilimwambia ...ni usasa zaidi, wengi wanafanya hivyo, ...sioni ubaya wake, ...akaniambia inaleta picha mbaya hasa ....,na akasema hao anaowaita wazazi wangu hawatapenda wakiniona hivyo,na kipindi hicho nilikuwa sijakutaa na hao anaowaita wazazi wangu...’akasema

‘Wewe unavuta sigara, ...?’ akaulizwa

‘Mwanzoni nilijaribu nikaacha,siunajua tena utoto, ujana, muheshimiwa....’akasema

‘Kwanini uliacha...?’ akaulizwa

‘Niliona haina maana yoyote kwangu...nilikuja kujitambua...’akasema

‘Hukuacha baada ya kukatazwa na mlezi wako...?’ akaulizwa

‘Ndio....alinkataza...’akasema

‘Uliwahi kuvuta bhangi...?’ akaulizwa na hapo akakaa kimia bila kujibu hilo swali.

‘Kwanini hutaki kujibu hilo swali....?’ akaulizwa

‘Kwasababu ni mambo ya utotoni, ujanani, wengi hupitia, na baadaye huacha, ni kama kuuliza kama niliwahi kula mchanga, au...kuchezea uchafu nikiwa mdogo....hayo wengi wanayapitia na baadaye huachana nayo..’akasema

‘Huachana nayo wakipata mtu wa kuyakemea hayo mambo au sio...?’ akaulizwa

‘Ndio....’akajibu huku akibenua mdomo kama anaona kero, na alipojitambua akasema

‘Ndio muheshimiwa, wakipata mtu wa kuwakemea, na wengie huacha wenyewe wakijitambua...’akasema

‘Kuna kipindi wewe ulibobea kwenye mziki, ukawa unapigisha mziki nyumbani, na ukawa husomi,....unakumbuka...?’ akaulizwa

‘Ndio lakini ni kipindi nikiwa mdogo, sielewi kitu, nilipokuwa mkubwa nikabadilika....’akasema

‘Ni nani alikukataza kufanya hivyo....?’ akaulizwa

‘Kufanya nini....?’ akaulizwa

‘Kuvuta bhangi, kupiga mziki,....ili usome ....?’ akaulizwa

‘Ni yeye....’akasema

‘Ni yeye nani...?’ akaulizwa

‘Mshitakiwa...’akasema akionyesha kidole pale alipokaa mshitakiwa

‘Je kipindi unavuta sigara, ukajaribu hata bhangi, ukawa unapigisha miziki , ukawa hata kusoma hupendi ilikuwa kipindi gani, ukiwa shuleni bweni au uliporudi nyumbani kukaa na baba yako mdogo...?’ akaulizwa

‘Ni kipindi nikiwa bweni, nilikuwa natoroka shule, kwenda nje, na wenzangu, walikuwa wakinihadaa tu, lakini niliporudi kukaa na .....huyo mshitakiwa nikaanza kubadilika,nilishajitambua,....’akasema

‘Ulibadilika kwa vile alikuonya, akawa anakuelekeza lipi jema na lipi baya, akawa anakukataza kuvuta sigara, kupiga miziki,....ili usome ,ili uwe na elimu ambay o sasa unayo....kweli si kweli....?’ akaulizwa

‘Lakini pia na mimi niliona havina faida kwangu, ....ndio nikaacha...’akasema

‘Je kama ungeliendelea kukaa bweni, ungebadilika, sema kwa ukweli wako...?’ akaulizwa

‘Ningebadilika ndio....wengi wanabadilika, ni swala la uamuzi...na umri unachangia....’akasema

‘Je baba yako huyo mdogo hakuchangia kubadilika kwako,hakukukataza kuvuta bangi, kuvuta sigara, kucheza mziko, hakukuelekeza kusoma, akawa anakuasa uwe mtoto mwema...?’ akaulizwa

‘Alinikataza ndio...sijakataa hilo...ila pia na mimi mwenyewe nilihajitambua nikaona hayo hayana umuhimu ,muheshimiwa..’akasema

‘Halafu unasema ni mlezi mbaya, unasahahu yote hayo, kuwa aliwahi kukuanya, kukuelekeza,...hebu jiulize kama angeacha ukawa unapiga mziki, husomi, ....ukawa unavuta bangi, ungefika hapo ulipo...yote hayo umeyasahau....sina zaidi muheshimiwa, ....’akasema mtetezi na muendesha mashitaka akasema

******

‘Tunaingia sehemu ya pili, shahidi unaweza kuondoka, tutakuita tena kwenye sehemu ya pili, ...’akasema muendesha mashitaka na shahidi akawa anatoka sehemu ile ya kutolea ushahidi akiwa kainama chini,tofauti na alivyoingia kwa mbwembwe...

‘Unajua ukweli huwa unauma wazazi wengi hawapendi kuambiwa hawajui kulea,au kazi wanaofanya ya kuingiza pesa sio halali, hata kama kweli wamekosea, au kazi wanayofanya sio sahihi, ...sio halali watasema kwani, kwani wewe unakula nini....’akaongea na watu wakacheka.

‘Wapo, tunawaona...’akazidi kusisitizia

‘Kijana usijali upo sahihi kabisa, umezungumza ukweli wako...’akasema na wakati huo huyo shahidi alikuwa anatembea kumpita huyo wakili muendesha mashitaka.

‘Sasa tunaingia kipengele muhimu sana, kipengele cha kuonyesha jinsi mshitakiwa alivyotenda kosa  la kumiga risasi marehemu na kusababisha kifo chake.....’akasema

NB: Naona tuishie hapa....

WAZO LA LEO: Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo, na watoto wengi huiga matendo yetu wazazi , au matendo ya walezi wao, au hao wanaishi karibu nao..., matendo huigwa haraka sana,....sasa ni jukumu letu wazazi, hasa wale wanaokuwa nje ya kazi kwa muda mwingi, na kazi ya kulea watoto ikawa mikononi mwa wafanyakazi wan je, tujitahidi kuwaelekeza hao wafanyakazi tabia ambazo zitakuwa kiyoo kwa watoto wetu,vinginevyo, tutakuja kujilaumu wakati tumeshachelewa

Ni mimi: emu-three

No comments :