'Mimi ndio mgeni wako...' sauti ikasema,
‘Tcha tcha..tcha, siamini, wamekukamata Mpendwa, hahaha,...siamini eeh... natumai ulikuwa unanisubiri kwa
hamu kukutana na yoyote, au sio,nilkuambia mpendwa ipo siku...’akasikia suti ikipenya akilini, ikimtesa moyo wake.
‘Hahaha......
nimeshafika profesa, usiwe na shaka...hahaha, geuka unikaribishe mpendwa, umeona
eeh,....’akawa anaongea kwa sauti kama vile alitaka kila mtu asikie.
‘Mhh,
...nikuambie kitu, huu ni mwanzo tu,
...na natumai sasa unatakiwa uanze kuhesabu siku zako....hahaha,..’
akaendelea kuongea kwa sauti na profesa alisimama vile vile, hakutaka hata
kugeuka kumuagalia huyo mgeni.
‘Hebu geuka kwanza,
unatakiwa unipokee mgeni wako, hapa nimekuletea chakula kidogo,matunda kidogo,
na maji kidogo ili uikumbuke dunia kuwa
kuna watu wenye upendo na huruma, sio nyie mashetani mkianza kudai pesa hata
mtu akilia vipi, hamjali, hamuwaonei wenzeu huruma, ....’akazidi kuambiwa
‘Shetani
kama nyie hamstahili kuishi kwenye jamii ya wastaarabu, huko kwenye gereza la
kifo ndio mahali penu,....’akasema
‘Sasa
nimekuja mimi ninayelijua hilo gereza ambalo watu kama nyie ndio mnastahiki
kwenda, na nikuambie ukweli mimi ndiye mtu peke yake aliyewahi kuingia na
kutoka salama.....hahaha....’akatulia
‘Na usalama
wagu ndio huo...unajuza zaidi,...au nikuambie tu, maana hata nikikuambia
itasaidia nini, ...maana wewe ulifikia hatua ya kupekenyua maisha yangu na
kugundua kidogo, ....nakupa tu kama angalizo, kuwa hata kizazi changu kilipotea
huko huko.....unasikia sana....hahaha, sasa uongeze hilo kwenye mambo yako ya
kuni-blacmail....
‘Kuna watu
walinisulubu hadi kunitoa kizazi huku naona....damu zinanitoka, na
walihakikisha hakuna kilichobakia ndani, nikapoteza fahamu kwa siku saba,
nikijulikana kuwa nimeshakufa,...unasikia wewe sheteni......’akasema
‘Sasa hayo
yalikuwa yanatokea huko kwa upande wa wanawake, huko kwa wanaume...ni zaidi
mara kumi ya hayo ya wanawake, kama hujawahi kupata hata mtoto wa kusingiziwa
basi ujue ukitoka huko, wewe sio mwanaume tena, unakwenda kuwa sio
riziki...hahaha....
‘Huku kuna
kila aina ya unyama na mwingine hujawahi kuusikia duniani,....kuna mijitu
mikatili haijawahi kutokea,...mijitu hiyo haijui maisha ya duniani yapoje, ina
tikteti za kifungo cha maisha.....hahaha
‘Huko watu
hao, wanaamini kuwa, damu ya mfungwa mpya inaongeza umri, wa kuishi, kwahiyo ukifika
tu, damu yako inakuwa kinywaji chayo, sasa wataipata vipi utajulia huko huko
gerezani....hahaha.....nilikuambia sasa unaona eeh, hahaha...’akacheka saana.
‘Siwezi
kukuambia yote maana mengine ni siri ya huko, siruhusiwi kutoa siri za huko
maana ni siri za jandoni, ukifika utajionea mwenyewe.....’sauti ikazidi ,
profesa alihisi mwili ukimuishia nguvu.
‘Sasa
sikiliza nimekuja kukuona....najua kuwa wewe ni mwanaume, na mjanja, najua una
akili ya kuwaza mambo, ndio maana ukaitwa profesa, sasa kama uliitwa kiutai,
basi utakuja kuumbuka,...unasikia....mimi nataka kukusaidia....’maneno hayo
aliona ni kama utani.
‘Mimi nataka
uongee kiume, kama upo tayari mimi
naweza kukusaidia, kwani najua hatari unayokwenda kuikuta, na zaidi mimi
nafahamu wapi ni wapi utakapoponea....’maneno hayo yalimfanya profesa aingiwe
na uhai, akaweza kutikisa kichwa, lakini hakugeuka, akihisi ni utani, au ni
mtego.
‘Najua
utahisi nakutania, lakini ukumbuke kuwa mimi nakudai, sasa ukifungwa maisha
nitapatia wapi pesa zangu, ndio nikaona nije nikusaidie, ili niweze kupata deni
langu, umenielewa hapo...’akasema na hapo profesa akajua kuwa hilo linawezekana
huenda ni kweli.
‘Kwahiyo
mimi nimeongea na mkuu wa gereza, akasema yote inategemeana na wewe, lakini kwa
kiasi kikubwa inategemeana na hao
waliokushitakia, lakini kuna mambo ambayo yeye yapo ndani ya uwezo wake, ...na
hayo ndio anayoweza kukusaidia, unielewe hapo.....’akasema
‘Sasa hayo
yaliyopo ndani ya uwezo wake anaweza kukusaidia, hasa ikitegemeana na wewe....’akatulia
‘Lakini
...japo hajasema, na hawezi kusema akiwa humu, si unajua tena,...
tu,..kunahitajika pesa,...’akatulia
‘Najua kwako
pesa sio tatizo,...pesa unazo nyingi tu....na pesa ni nini, ukilinganisha na
maisha yako, hebu fikiria hiyo taabu ya huko gerezani, na hao kesi
haijatajwa,na hujui utasubiria muda gani, ....pesa ipo utatafuta nyingine
lakini uhai wako huwezi kuupata tena ukifa umekufa, ukiumizwa umeumizwa,
ukiambukizwa maradhi ndio basi tena....’akaambiwa
‘Kwahiyo
mimi nikamuelewa, nikaona nije nikusaidie kwa hilo, na kusaidia kwa vile bad
nakudai, lakini vinginevyo, wewe hustahili kukaa kwenye jamii ya
wastaarabu,...nikuambie ukweli mimi niliwahi kupitia huko, lakini ...naapa
siwezi kurejea tena huko...siwezi ,ni bora kufa....’akasema
‘Sasa najua
bad hujaamini hatari iliyopo mbele yako, ...unasubiri, kwanza uonje adhabu ya
huko, na watu hawaamini mpaka wafike, na hutaamini mpaka siku hakimu anagonga
rungu kuwa umehukumiwa kifungo cha maisha ya kuua....’akasema
‘Mimi
sijaua....’akasema profesa
‘Mimi sijui
hujaua,au umeua, tatizo ni kuwa wewe huaminiki, ..nikuulize wewe hufanyi
biashara ya mlungula, hujaniblackmail mimi...si ulikana mpaka ushahidi
ukapatikana, ..na unajau kuwa kwenye kazi kama hizo kifo kipo nje nje,...
‘Na ukumbuke
watu wakiona pesa, au yule aliyefanyiwa hivyo akiona hakuna njia nyingine
unafikiri atafanya nini, na ni nani aliyesababisha hayo kama sio wewe.....umeua,
sasa ni kuua kwa namna gani....
‘Mimi
sijaua, nilifika na kukuta huyo jamaa keshapigwa risasi....’akasema profesa
‘Hahaha,
hayo wanaongea sana, na usipoteze muda wako kuniambia mimi ilivyokuwa ,mimi sio
wakili wako,subiria aje wakili wako, na hilo ni jambo jingine nataka
kukushauri, kuwa unahitajia wakili, na wakili awe kweli wakili...’akasema
‘Nitampataje
na mimi nipo hapa ndani...?’ akauliza
‘Nilijua
wewe ni mjanja, ina maana mpaka sasa hujatafuta wakili, hahaha, wewe ni profesa
gani, kesi kama hii unahitajika kuwa na wakili, na tena wakili kweli....’akasema
‘Nitampataje,
na mimi nipo hapa,....sina mtu wa kunisaidia,..nilikuwa naumwa sana, nimepona
tu nimeletwa na hapa,na...na...’profesa akajikuta analia
‘Hahaha,
...unalia,....unalia profesa simaini...’akasema huyo mama sasa akimsogelea
profesa akamshika mgongoni kama anambembeleza
‘Mhh, pole
sana...lakini sasa unaona uchungu wake au sio, hujui ni kiasi gani nilivyolia mimi,
kiasi gani ulivyowatesa watu pale ulipowapigia simu na kuwaambia kuwa una au
kuna mapicha mabaya, una siri mbaya au vyovyote ulivyosema...unakumbuka hayo
‘Mtu
akisikia hivyo, na huenda alifanya huenda ana tatizo kama hilo, kwanza anapata
shinikizo la damu, wewe hapo unatishiakuwa kuwa unataz hizo siri, na ukizitoa, huyo mtu
ataumbuka, hebu fikiria jinsi gani mtu huyo anavyoshituka, anavyoumia moyo wake
....
‘Na
isitoshe, unamzidishia kwa kudai mapesa mengi,..mtu anaumia, hajui afanyeje,
....analia anateseka akijua kuwa hayo yaliyotokea labda sio hiari yake....humuonei
hata lepe la huruma unachotaka wewe ni pesa tu...’akasema
‘Wewe
unazidishia chumvi....watu kama hao wana pesa, na huwa ni kweli wamefanya hayo
machafu, kwanini walifanya hayo machafu
kwa namna nyingine ilikuwa njia ya kuwapiga vita kwa mabaya yao....achana na
mimi , kama umekuja kunikoga ....unaweza kuondoka tu...’profesa akasema
‘Kuwapiga
vita kwa machafu,...mimi nilikuwa na machafu gani...hahaha unajifanya unalia,...siamini, wewe ulie,...au ndio huko
kuigiza kwako...sasa unalia wakati, hujaenda huko kwenyewe, hahaha, ...siamini...’akawa
anajaribu kumchungulia profesa lakini profesa hakukubali kugeuka kuangaliana na
huyo mama
‘Profesa,
profesa....kumbe ujanja wa bure, sasa nikuambie ukweli, ndugu yagu, hujalia,..utalia
sana, utalia hadi chozi la damu litakutoka, ...kwa hali ilivyo, hakuna
atakayekuonea huruma.....’akasema kwa sauti ya chini kidogo
‘Unajua
jinsi gani watu walivyoumia,....wanaumia,hawana raha...wewe hukuwahi kuwaonea
huruma, ...roho mbaya iliwatawala, ....wewe ulijali tumbo lako, ulijali masilahi
yako, ukaona kuwa unachofanya ni kutetea masilahi yako,....wajiona wewe mjanja,
hukujali wengine..hukujali familia
zao,.....sasa ni zamu yako, na hiyo bye bye....hilo nakuhakikishia...’akasema
‘Sijaua na
haki ipo najua haki ipo,....’akasema profesa
‘Haki ipo,
kwani ni uwongo, kwani hujafanya hiyobiashara ya mlungula, na sasa umeua...haki
kwako wewe tu, wengine hawana haki, mlijiona wajanja hamtakamatwa....mwenzako
naye nasikia keshakamatwa....’akasema
‘Mwenzangu
nani...?’ akauliza
‘Unamfahamu
sana,....yeye anajifanya mjanja wa mitandao....za mwizi ni arubaini, sasa ujue
upo kivyako, kila mtu anajitetea kivyake, hapo hakua ujanja....’akasema
‘Wamemkamta
...mta...a....’akasema profesa akishindwa kuamini.
‘Hili zoezi
lilishapagiliwa na wenyewe....usicheze na polisi,...ndugu yangu, kila jambo baya
lia mwisho wake, ...karne ya ujanja wenu imeshapita,...na mwisho wa ubaya ni
nini....’akawa kama anauliza na profesa akawa katuliatu
‘Sasa ndugu
yangu, mimi nataka kukusaidia, na msaada wangu ni huo,...nipo tayari kukusaidia
ilimradi kuna uhakika wa pesa,... mambo mengi ya kufanya yanahitaji pesa, na
sio pesa ndogo,...pesa nyingi...’akasema
‘Pesa
nitaipata wapi na mimi nipo hapa jela...?’ akauliza
‘Hiyo pesa
mliyochukua kwa huyo jamaa kutoka India ipo wapi, ...hiyo ndiyo itakusaidia,
vinginevyo, acha uumie, acha ufe na hiyo pesa itapatikana na wewe muda huo
utakuwa wapi kama sio kaburini....’akaambiwa
‘Pesa ipi
hiyo ,.... mbona haipo, mbona sikuwahi kuichukua, sikuupata kabisa huo mzigo,...aah,
unazidi kunichanganya.....’akasema profesa akishika kichwa.
‘Wewe ndiye
unayejua wapi hiyo pesa ilipo...hilo linajulikana wazi, huwezi kunidanganya
mimi...’akasema huyo mama.
‘Najua
huniamini mimi, lakini wewe ndiye
utakayesemani nani akaichukue hiyo pesa,kwangu sio shida,...ila ni kwa vile
pesa inahitajika, ...nakudai sana....lakini kwanza muhimu kuna haya mambo
yanayohitajia pesa kwa ajili yako....’akasema
‘Hujanielewa,
na sijui kwanini watu hamunielewi, sikuwahi kuuchukua huo mzigo...sijui hiyo
pesa ilipo....’akasema
‘Wewe
uliingia, na hakuna mtu aliyewahi kuingia humo kabla yako, kamera
zinaonyesha...umetoka ukiwa umeshikilia mzigo, ukiyumba yumba kama mlevi, sijui
ulikuwa unaigiza ili uonekane umelewa, umeonekana kabisa...’akasema huyo mama
na profesa akaguna
‘Mhh,
kamera...nani kasema....?’ akauliza
‘Sasa hilo
la kamerahalijafika kwa polisi, ni siri tu nakudokezea, ...na hilo linaweza
kukusaidia, kama kweli hukutenda...kitu ambacho,...naamini ....japo sijaiona
hiyo kamera,....kiukweli umeua, ..hao jamaa wanasema kweli umeua, ila wao
wanaweza kusaidia maana polisi walivyo, watakuja kuipata hiyo kamera....’akasema
‘Kwenye lile
jengo hakuna kamera, mimi nina uhakika huo.....’akasema profesa
‘Hahaha
umeona eeh, kumbe ulikuwa unadhania kuwa hakuna kamera,....wenzako walikutegea,
waliwahi kuweka hiyo kamera....hahaha, pesa kama hiyo kila mtu alikuwa na mbinu
zake...ndugu yangu upo matatani...umeua, wanasema inaonyesha wazi...’akasema
huyo mama
‘Ni nani
hao,waongo, mimi sijaua....walete hiyo kamera tuone, ....kama ipo ndio
itasaidia kuonyesha ukweli ulivyokuwa..’akasema profesa
‘Sasa
sikiliza tusipoteza muda...unaye wakili, unazo pesa za kumlipa....?’ akaulizwa
‘Sina wakili
wala sina pesa....’akasema
‘Sasa hizo
pesa ndio zitumike, najua wewe huwezi kuruhusiwa kutoka, wewe huwezi kutaja
wapi pesa zilipo,...hata kama ingelikuwa mimi nisingelitaja, maana huo ndio
mtaji wako wa baadaye, lakini kunahitajika pesa....’akasema
‘Unajua
....hutanielewa....’akasema profesa
‘Nitakuelewa
tu, niamini mimi...kesi hii ni mbaya, utaenda kufia jela, ...., mimi sihitaji
kuichukua mimi hizo pesa, una watu unaowaamini, sema ni akina nani, ili waje
wakuone uwaelekeze, ili pesa hiyo itumike, uweze kuokoka kwenda hilo gereza la
kifo, hicho ndicho muhimu kwa sasa ....gerezani ni lazima uende, huwezi kukaa
hapa kwa kesi ya mauaji,....hilo halina ujanja, sasa ni gereza jipi, ndio hapa
nataka kukusaidia.....’akasema
‘Lakini mimi
sijaua mtu,...hilo unielewe, wewe mwenyewe unajua fika mimi sijafanya hivyo,
hilo mumefanya mbinu ili nifungwe, ...’akasema
‘Aaah,
usinihusishe kabisa ....nifanye mbinu ili iweje, mimi nakudai pesa nyingi,
ukifungwa nitazipata wapi,....hebu fikiria hapo, mimi sihusiki kabisa kwa hilo,
ila nilijua kabisa kwa kazi kama hiyo ipo siku itafikia haya, watu
wanakuchukia, watu wamejenga uadui na wewe......’akasema.
‘Watu gani
zaidi yako wewe....’akasema
‘Mimi najua
jinsi gai ya kukubana, sihitajii kukufanyia hivi....mimi nimeshabadilika,
siwezi kujiingiza kwenye mambo haya, ila nilikuwa tayari kuwasaidia watu ili
watu kama wewe wasiendelee na matendo haya machafu, lakini sio kwa mtindo huu,
wa kuua, mtu asiye na hatia, hapana ,hapa sasa mumevuka mpaka....’akasema
‘Mimi mnanionea
bure, mnajua kabisa mimi siwezi kuua mtu, hiyo sio fani yangu kabisa
....’akasema profesa kwa sauti ya huruma.
‘Mhh, sijui,
maana kama walivyonambia, wameshakamilisha ushahidi wote,.... nimeulizia,
nimefuatilia, nikitaka kujaribu kukusaidia, lakini kwa jinsi ilivyo, huna
ujanja...wewe umeua, sasa sijui ilikuwaje,...ni kwanini uliua, yule jamaa wa
watu ana kosa gani, alikataa kukupa hizo pesa au ilikuwaje....’akawa kama
anauliza
‘Mimi
sijaua,...na wala sijui aliuliwaje, na nani alifanya hivyo....’akasema profesa.
‘Najua
labda, ...ulikuwa unajitetea,...au ulitaka kuzichukua hizo pesa peke yako,...au
ilikuwaje, ...mmmh, ni kesi mbaya sana kwako, hata kama ni kwa kujitetea au kwa
vipi hilo utaongea na wakili wako, ....mimi nilichokuja kukuambia ni
hicho....’akasema
‘Muda
umekwisha...’sauti ya askari ikasema kutoka mlangoni.
‘Nambie wapi
hiyo pesa ilipo,....au ni nani unamuamini ili aje umuelekeze mahali hiyo pesa
ilipo, ili hiyo pesa ikafanye kazi ,..kesi hii iahitajia wakili mahiri,...wapo
mawakili nawfahamu, au, kama yupo unayemfahamu niambie ni nani, si unaliona hilo, sasa ....sema haraka
mimi naondoka zangu....’akasema
‘Mwambie
kijana wangu aje....’akasema
‘Kwahiyo
niongee na mkuu wa hapa ili afanye mipango au sio hilo tumekubaliana ...ujue
mimi nachukua dhamana hapa,.....hapa hakuna longo longo, ukidanganya unajua
utakalofanywa, mimi nitakuwa nimeosha mikono yangu....’akasema huyo mama sasa
alikuwa haongei kwa sauti kubwa, kama ilivyo kawaida yake.
‘Mwambie
kijana wangu aje asubuhi sana...’akasema kwa sauti ya kinyonge
‘Sawa,...nitafanya
hivyo, nikijua kuwa utamwambia wapi hizo pesa zilipo, ili huyo kijana akitoka
hapa akazichukue hizo pesa, nitaongea na huyu mkuu atafute mbinu za
kukuchelewesha usilepekwe huko gerezani,...
‘Lakini pia
hizo pesa zisaidie kumlipa huyo wakili wako,
na pia tuweze kuwalipa wahusika mbali mbali...ujue hili halipangwi na
mtu mmoja, kuna wahusika wengi,..natumai umenielewa.....’akasema huyo kwa sauti
ya chini kama ananong’ona.
‘Ni jambo
gumu sana....lakini nitajua jinsi gai ya kumshawishi... huyu mkuu hapa ili
aweze kutafuta mbinu za kila namna ili hata kama..... wewe uweze kubadilishwa
gereza, na ujue hilo ni la haraka, na yote yanahitajia pesa, ...’akasema huyo
mama sasa akiongea kwa lugha ya chini sana.
‘Sawa....’Profesa
akatamka hivyo, huku kichwani akiwaza jinsi gani ya kumuambia huyo kijana,
maana kiuhakika alikuwa hajui kabisa hizo pesa zipo wapi, kinyume na inavyoeleweka
kuwa yeye anajua pesa hizo zilipo, yeye ndiye alizichukua,....
‘Hivi hizi
pesa alizichukua nani,.....’akawa anajiuliza wakati akirudishwa kwenye chumba
chake, akiisubiria hiyo kesho....
WAZO
LA LEO Toka lini aliyezoea dhuluma akatosheka, na kila siku ataona alicho nacho hakimtoshi, hata kidogo alicho nacho mwenzake atataka awe nacho. Lakini tukumbuke za mwizi ni arubaini, na huwezi kuwahadaa wengine kila siku, ipo siku uwgo wago utadhihiri tu, na ndipo utakapokuja kuumbuka, jirekebishe wewe mwenye tabia hiyo maana dunia hii ni mapito tu
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment