‘Bro, siku ninasomewa
mashitaka yangu sikuamini...., ‘ akaendelea kuhadhia jamaa akimuhadithia kaka
yake,
‘Mashitaka
gani....?’ akauliza kaka mtu
‘Ya
kuua.....’akasema
‘Ina maana
uliua...?’ kaka mtu akauliza kwa mshangao.
‘Si...nilikuambia
niliwahi kufungwa kwa kesi ya mauaji,....’akasema
‘Sawa,
uliniambia ulikuwa na kesi , ukafungwa, ...sasa ninachokuuliza je ni kweli
uliwahi kuua, na ulimuaa nani....ndio swali langu?’
Wewe
tuendelee na simulizi la maisha yangu ya Ulaya, na kijana wetu, utakuja
kufahamu yaliyonikuta, sio mchezo kaka, usinione nipo hivi,....nusu mfu ,
ukafikiria ni madawa ya kulevya, sio kweli....sio kweli....sikiliza kisa uelewe
mwenyewe
‘Na kijana
naye .....hakuwahi kujiingiza kwenye hayo maisha mabaya....mimi sitakuelewa kwa
hilo....?’ akauliza
‘Kijana wako
sio mtu....sijui kachukua damu na tabia ya nani.....alichonifanyia huko
ulaya,sitaki hata kukutana naye tena, hanijui, hanitambui, .....’akasema
‘Kwaini,.....ilikuwaje
akabadilika hivyo, hata wewe asikutambue, wewe dad wake,....hahaha, hebu endelea na kisa chako,maana yote
umeyataka wewe,nataka kujua maisha yake yalikuwaje, na je atarudi lini huku
nyumbani....’akasema
Tuendelee na
kisa chetu
********
Bro, siku
nafikishwa mahakamani kusomewa shitaka la kuua, nilibakia kama mtu zezeta, mtu
aliyechanganyikiwa, sikuamini.....’ akaanza kuongea akimuangalia kaka yake ,
kaka yake akitaka kuongea lakini hakumpa nafasi akaendelea kuongea
‘Nilishitakiwa
kwa kosa la kuua,.....kosa la kuwa kiongozi wa biashara ya mlungula,....kosa la
kuendesha biashara ya mdawa haramu, kosa.....,yakatajwa makosa mengi na mwisho,
kosa la kuishi kwenye nchi hiyo kinyume cha sheria...’akatulia
‘Bro....ukitajiwa
kesi ya mauji hata kama hujaua, unakuwa unakioa kitanzi shingoni
mwako....unajua siku yoyote utanyongwa, utafungwa kifungo cha maisha,
au...ukikoswa koswa,kifungo cha miaka mingi jela.....,’ akaendelea kusimulia
‘Kwahiyo
mimi nikasimamishwa mbele ya hakimu, kwa mara nyingine, na safari hii, ukipatikana
ushahidi wa kumrizisha hakimu, basi....,mimi ni mtu wa kunyongwa,
.....’akatulia akishika shavu
‘Bro,na
ujanja wangu wote, nililia....hahaha,
unaamini hilo bro, ilifikia muda nilitoa machozi na sio mara moja, kwa
kesi hiyo...nilijuta, nikaomba, na kumkumbuka mama......’akatulia
‘Mambo
yakikufika shingoni, hata kama ulikuwaje, utamkumbuka mama yako....hahaha,
unajua bro, nimeishi ulaya siku zote napambana na maisha ya shida, ...lakini
sikuwahi kuwakumbuka wazazi wangu, .....maana ukiwakumbuka na maisha niliyokuwa
naishi, utaogopa, ...ni maisha yasiyofaa, sasa wazazi hapo
utawakumbukaje....’akatulia
‘Bro,
lakini siku nasubiria, siku
nasubiria.....kuwa napelekwa jela ,....kwanza ile nasubiria kupelekwa gereza
baya kuliko yote huko....nilimkumbuka mama, nikalia,....’akatulia
‘Profesa Mti
dawa,...., unahaki ya kutafuta wakili,...na kesi yako itasikilizwa
tarehe.....’yaliyokuwa yakiongelewa siku hiyo skuweza kuyasikia kabisa, ni neno
moja moja,....nilisikia tu pale nilipoamurishwa nisimame, ili kurudishwa rumande....
‘Simama,
twende huku....’
Nikasimama
nikipepesuka,...mwili hauna nguvu, njaa, ...na mawazo, unajua ilikuwa siku ya
tatu, siwezi hata kula, chakula hakimezeki....maana nlikamatwa ijumaa usiku,
jumamosi, ...ilikuwa siku ya kuhojiwa, ...nilihojiwa siku nzima, mapaka akili
ikawa hafanyi kazi,na jumapili, nikawa nimelala tu,...lakini usingizi upo wapi,
mawazo tu
‘Na
Jumatatu, ndio nikafikishwa mahakamani,....kwahiyo sikuwa na nguvu kabisa, na
pale nilipoambiwa, twende huku,...nilikuwa nakokotwa tu... na ghafla kitu
kikatanda usoni, nikajikuta nikizama kwenye giza,....nilipozindukana nilijikuta
nipo kitandani, hospitali na pingu mkononi.....
‘Lakini
hujasema ilikuwaje,....uliuaje, au ilitokeaje mpaka ushitakiwe kwa
mauaji,..uliua kweli, au...?’ akauliza kaka mtu.
********
'Bro, ....sikumbuki ku-ua....' akasema mdogo mtu
'Sasa ilikuwaje....?' akaulizwa
'Bro wewe endelea
kusikiliza utanielewa tu....'akasema
Basi profesa alizindukana, kutoka kwenye kupotewa na fahamu na alijkuta yupo kitandani na pingu mkononi....askari wakimlinda asije
kutoroka.
Profesa alishaonekana ni mtu hatari, ni kiongozi wa kundi hatari, lililokuwa likitafutwa na polisi kwa muda mrefu, kwa biashara ya mlungula, huko wanaita blackmail.
'Bro,niliandikwa
kwenye magazeti yote kuwa hatimaye yule mtu hatari wa biashara ya mlungula,
amekamatwa, na nimekamatwa nikiwa nimeua mtu mwingine...usikie magazeti yalivyo
wachohezi, eti, nikiwa nimeua mtu mwingine....’akatulia.
‘Niliua
lini bro, hivi mimi naweza kuua mtu,...na tena waliandika kuwa huyo aliyeuwawa ni wa pili, lakini ili kunogesha biashara yao ya magezeti,ili
nionekane mtu mbaya,.....wakaandika hivyo, na ukisoma ndani huoni hayo mauaji
mengine nilivyoyafanya na mimi, na inasemekana...’akatulia.
‘Basi
nilipofikishwa hospitalini, unajua hakuna dawa zaidi, ilikuwa driu ya maji ya
glucose,sijui kama kuna zaidi, ikanirejesha kwenye uhai, nikawa mtu
tena,..ilikuwa na njaa, na zaidi ni mawazo...siwezi kusema nilipigwa, niliwahi
kuzabwa vibao viwili vitatu, wakati nahojiwa siku ile ya jumamosi lakini
havikuniathiri...
‘Unajua
wenzetu wapo makini sana na watuhumiwa, kuna haki za kumlinda mshitakiwa,
wanakuwa makini sana, wasije kulaumiwa kwa hilo, kwahiyo sikuteswa,
sikushinikizwakwa vitisho, wao wana mbinu zao nyingine, za kisomi,na utajikuta unasema
tu....’akatulia.
Basi nikiwa
pale hospitalini, nikiombea kama yawezekana niendelee kukaa hapo, lakini huna
ujanja, ....siku ya pili nikaambiwa hali yangu ipo shwari naweza kurudishwa
rumande...hapo moyo pwaaah, unajaribu kuzuia ubongo, iwe ni ndoto, iwe sio
kweli....
‘Basi bro..,
nikatolewa hapo hospitalini hadi rumande, nilipokuwa nimeshikiliwa,na huko
nikaambiwa siku inayofuata nitapelekwa gerezani, kwani hapo hawakai watu
wauwaji kama mimi....
‘Endelea na
kisa chako...’kaka mtu kwanza alitaka kuuliza swali, lakini akaona atavuruga
utaratibu wa mdogo wake,
******
‘Nimeua...mimi
sijaua....’nikasema kwa mara ya kwanza baada ay kutoka hospitalini na
kufikishwa rumande na sasa naambiwa kuwa nahitajika kupelekwa gerezani, na
gereza lenyewe nililotajiwa, ni gereza baya sana.....
‘Wengi walio-ua huwa wanasema hivyo hivyo...kwahiyo
kwako mimi sioni ajabu.’akasema askari mmoja wa hapo ani askari mdogo,tu,
lakini naye alikuwa na na kazi ya kunihoji ili kuweka kumbukumbu zao, na yeye
anasema alikuwepo kwenye harakati za kunikamata na kwa muda huo, alifika kuweka
mambo yake sawa, kabla sijaondolewa hapo.
‘Afande mimi
sijaua,....mungu ndiye shahidi,....nilifika nikakuta huyo mtu ameshauliwa,
nimeeleza na kuelezea tena, sijui mnataka niseme nini,....huo ndio ukweli ulivyo....’nikasema
kujitetea.
‘Hayo tutayaona
mbele ya hakimu, ila nilitaka tushirikiane vizuri, tusipoteze muda, ukiri kosa,
na nione jinsi gani ya kukusaidia, sasa huko mbele utakutana na wanaohusika
mimi nitafika kama mtoa ushahidi tu....’akasema huyo ofisa usalama, na pemeni
yake alikuwepo mkuu wa kituo hicho.
‘Mnaona hali
yangu ilivyo,naumwa,....sasamimi nawaomba munisaidie nisipelekwe gerezani, huko
kwa afya yangu wataniua hao watu wa huko,...mimi sijaua, hizo ni mbinu
zimefanywa ili nikauliwe huko.....huo ndio ukweli,mtafuteni muaji halisi,
....mtampata tu, lakini sio mimi...mnapoteza kwa mtu asiye na hatia...’akasema
profesa
‘Kama ulijua
usingejiingiza kwenye tabia hiyo chafu, watu kama nyie hata mimi
siwapendi,..japokuwa haki za binadamu zipo lakini nyie watu hamstahili kukaa na
jamii....wewe ni kiongozi wa mlungula, na nakumbuka sio mara ya kwanza
kushitakiwa kwa makosa kama hayo...’akasema mkuu wa hicho kituo
‘Yote ni
makosa ya kusingiziwa, wewe mwenyewe si ulioana kwenye kesi iliyopita, mbona
baadaye nilikuja kuachiwa, walipofanya uchunguzi nikaonekana sina hatia ni
uonevu tu, sisi waafrika mnatuonea sana,ni kwanini mnatuchukia...?’ akauliza
profesa
‘Hamna cha
Uafrika hapo, hakuna cha ukabila hapa, kinachotafutwa ni haki, ...huwezi
kufanya kosa ukajivika uhali yako, wengi wanatumia uhali zao,ukabila udini,
kufichia makosa yao, wanafikiria wakijivika kilemba hich hawatapatikana
kirahisi....’akasema ofisa mpelelezi
‘Hebu
fikiria ni hali gani mnayomsababishia mtu mliyemuingiza kwenye hiyo
biashara...., unajua watu wengine hufikia hata kutaka kujiua, ....’akasema mkuu
huyo.
‘Sio kutaka,
wengine wanajiua kweli....na kosa ni la hawa watu, wanachofanya ni kutoa vitisho
baada ya kutengeneza uchafu wao, mambo ambayo hayakutakiwa kuonekana kwa jamii,
mnatishia kuyatangaza, mnadai pesa,kama mtu hana pesa mnafikii atafanyaje....anaona
ni bora afe tu kuliko kuadhirika.....’akasema huyo mpelelezi.
‘Lakini mimi
sijawahi kufanya hivyo, ....mimi nimekuwa raia mwema, ...mengine wanaisingizia
tu afande....’akasema profesa
‘Ushahidi
tunao,...nimefika hapa kukuona tu, kuhakikisha kuwa kila kitu kipo kama
inavyotakiwa, na kesho nitakuja kuhakikisha umefika gerezani, ...’akasema
‘Ina maana
hamtaki kunisaidia ,mimi naumwa, kwanini mnampeleka mgonjwa gerezani, hiyo sio
haki, zingatieni haki za binadamu.....’akasema
‘Leo wewe
unaona una haki, je hao raia uliokuwa ukiwasumbua hawana haki,...wana haki ya
kuishi kwa usalama, lakini nyie watu wacheche mnakuja kuwasumbua, mumeharibu
amani ya eneo letu, kwa tamaa zenu za utajiri wa haraka haraka na sasa mnafikia
kuua, yule jamaa wa watu ana kosa gani....’akasema
‘Afande,
nimeshakuambia mimi sijaua..mimi sio muuaji,nieleweni jamani.’akasema
‘Mhh, najua
utakana sana, hakuna muuaji anayekubali kosa...lakini ushahdi wote umeshapatikana
kuwa wewe umeua...’akasema
‘Ushahidi
gani huo, najua utatengenezwa tu, kwani hilo ni gumu, ....’akasema profesa
‘Bastola
uliyotumia kumuua huyo jamaa, ina alama zako za mikononi....mashahidi
wanaokujua kwa tabia zako chafu wameshapatikana, na jinsi ulivyopanga huo
mchezo mchafu imeshajulikana, kila kitu kipo wazi,.....sasa utabisha
nini....’akasema
‘Kwa hali
hiyo,nahitaji wakili afande, naona nikiongea na nyie hamtanisaidia kitu,
nimeshawaambia ukweli wote humuamini,...najua bila wakili mtamfunga mtu asiye
na hatia nyie watu mna chuki sana na ngozi nyeusi....nawajua sana nyie watu...,
’akasema profesa akijua akisema hivyo itasaidia.
‘Wakili
utampata hiyo ni haki yako, kama unahitajia wakili wa kujitegemea ni pesa yako,
kama unahitajia wakili wa serikali atakuja mtaongea naye....sasa ni wakati wako
kujipanga, najua unazo pesa nyingi sana kwa tabia hiyo chafu....’akasema mkuu
wa hicho kituo akimuangalia askari mpelelezi aliyekuwa akiandika kumbukumbu
zake.
‘Nimechukua
pesa gani mnanizulia bure, mim sikujua
kuna pesa, sikujua kuwa huo mzigo ni pesa, kama ni pesa basi mumeziona nyie,....’akasema
‘Unajua
kabisa kuwa mzigo huo ni pesa, unajua kabisa kwasababu wewe ni kiongozi
uliyekuwa ukiongozo hilo kundi la mlungula, na unajua kabisa pesa hizo zipo
wapi....’akaambiwa
‘Sijui
niwaambie nini ili muweze kunielewa, mimi ni kama tarishi tu, kuwa ...nikachukue
mzigo sehemu fulani, kama nilivyowaelezea awali, mara nyingi huwa nachukua ile
sehemu ya hotelini hapo kunajulikana, lakini safari hii nilielekezwa kwenye
hilo jengo, kwenye hiyo hoteli,....na niliambiwa ni mzigo,sio pesa,...’akatulia
‘Uliambiwa
utakutaje huo mzigo....?’ akaulizwa
‘Niliambiwa
nikifika hapo nitakutana na mtu na huyo mtu atanikabidhi huo mzigo...’akasema
‘Sasa
mkisema ni pesa, mimi siwaelewi,...na nilipofika hapo, ndio nikamkuta huyo mtu
kalala sakafuni, ....’akasema
‘Je huo
mzigo uliukuta...’akaulizwa
‘Nimewaambia
sikuweza hata kuhangaika na huo mzigo..., nilimuona huyo jamaa akiwa kalala
sakafuni akitokwa na damu , kwenye dimbwi la damu,na hali kama hiyo hata kama
mzigo ungekuwepo nisingeliweza kuuchukua.....’akasema
‘Ukafanya
nini sasa ....?’ akaulizwa
‘Nikataharuki,
nikatoka mbio, nikiwa na lengo la kutafuta kibanda cha simu ili niwapigie simu
polisi, ndio natoka kwenye hicho chumba, nikapigwa na kitu kisogoni, nikapoteza
fahamu....’akasema
‘Hukumuona
aliyekupiga hicho kitu kichwani.....?’ akaulizwa
‘Sikumuona
kabisa...’akasema
‘Ikawaje...?’
akaulizwa
‘Nilipoteza
fahamu, nilipoamuka,...nikawa najaribu kukumbuka,....kwa vile nilizimia, na
sikuelewa, na kichwa kikawa kinaniuma sana, nikaanza kutanga tanga, huku
najaribu kukumbuka, na kutanga tanga huko, nikajikuta nipo nje, nikasikia mlio
wa king’ora cha polisi, nikahisi kuogopa nikakimbia....’akasema
‘Ukakimbilia
wapi?’ akaulizwa
‘Sehemu ya
jirani tu, nikatafuta sehemu nikalala kidogo, kichwa kilikuwa kinaniuma sana,
nikatafuta dawa ya maumivi,nikameza.....’akasema
‘Dawa
ulizipatia wapi...?’ akaulizwa
‘Nilinunua
dukani,.....’akasema
‘Nilipomeza
nikatulia, nikitafakari la kufanya,....na hapo ndio nikajaribu kukumbuka jinsi
ilivyotokea, nikaona sasa ni bora niwafahamishe polisi, na wakati natoka ndio
nikakamatwa...’akasema
‘Wewe
unasema ulitumwa kuchukua mzigo ni na nani hao waliokutuma....?’ akaulizwa
‘Nimeshakuambia
kuwa hao watu siwajui tuliwasiliana nao kwenye simu tu,....’akasema na
mpelelezi akatikisa kichwa kuonyesha kupoteza muda wake. Na mkuu wa hicho kituo
akauliza
‘Sasa
ukichukua huo mzigo unaupeleka wapi...kama waliokutuma huwajui na unaowapelekea
huwajui?’ akaulizwa
‘Waliniambia
nikikabidhiwa huo mzigo niwaambie tayari, halafu wao watanielekeza wapi sehemu
ya kuupeleka huo mzigo,...’akasema
‘Watu
waliokutuma huo mzigo huwafahamu,....wakakuambia ukiupata wanakueleza wapi pa
kuupeleka, wewe unawaamini vipi, je yakiwa ni madawa ya kulevya, ....?’ akaulizwa
‘Ukiwa
katika hali yangu, huna uhakika wa ajira kazi yoyote unaweza kuifanya, ili
mradi mwisho wa siku unapata ujira wako....’akasema
‘Kazi yoyote
unaweza kuifanya, au sio....?’ akaulizwa
‘Ndio,
ilimradi naiweza, na ni sahihi .....na kazi zenyewe ni hizo za kutumwa mizigo,
mara nyingi ndio kazi zangu, kutumwa, kufanya usafi,..na vitu kama hivyo, kazi
zisizo na taabu au ubaya wowote....’akasema
‘Unapochukua
mzigo kama huo, mara nyingi huko unapopeleka, unakutana na mtu mwenyewe, au
unafikisha wapi....?’ akaulizwa
‘Nilishawaambia
mimi nafuata maelekezo ya anayenituma, niufikishe kwa mtu, au niufikishe mahali
fulani,....’akasema
‘Kwa mzigo
huo uliambiwaje,....?’ akaulizwa
‘Niliambiwa
nikifika hapo nitamkuta huyo mtu, atanipa huo mzigo nikishaupewa, nitapewa
maagizo mengine.....’akasema
‘Na gharama
zako utalipwaje,maana sizani kama unaifanya hiyo kazi bure tu.....’akaulizwa na
huyo mkuu
‘Wananielekeza
wapi pa kuchukua gharama zangu, gharama sio tatizo, napata ushuru wangu, bila
wasiwasi, sijawahi kudhulumiwa.....’akasema
‘Kwahiyo
hiyo ndio kazi yako ya kutumwa, kupeleka mizigo,...na kulipwa ushuru...,naje
unawasilianaje na hao wanaokupa hiyo mizigo au hao unaowapelekea hiyo mizigo...?’
akaulizwa
‘Nimeshawaambia
,mimi nawasiliana na hao wanaonituma tu, kila kitu wananielekeza wao, sijui
jingine lolote,...’akasema
‘Na kwa kazi
hiyo, nilipigiwa simu kuwa niende hapo nitakuatana na huyo mtu, atanipa huo
mzigo, ...siwajui ni akina nani,mimi niliwaamini najua nikiufikisha nitalipwa
pesa yangu, wakati mwingine unaweza kuwafahamu, lakini kama hawa wa sasa hivi,
sikuweza kuwafahamu kabisa...’akasema
‘Hayo
maelezo yako hayana ukweli na hayaingii akilini...kabisa,hakuna kazi kama hiyo wewe
uelekezwe kwa simu, na watu usiowafahamu, ...hata hivyo kila kazi ya kipato,
inakibali, je kazi yako hiyo umepatia wapi hicho kibali..?’ akaulizwa
‘Kazi hiyo
haina kibali, maana ni kazi ya muda , sio kwamba, ndiyo kazi naishi nayo hiyo
tu,inatokea tu,....kwa mtu kuniamini kuwa naweza kuuchukua huo mzigo na
kuufikisha sehemu husika..’akasema
‘Unafikiri
ni kwanini hao watu hawafanyi hiyo kazi peke yao, mpaka wakutume wewe....?’
akaulizwa
‘Mimi
sijui.....’akasema
‘Umeshawahi
kutumwa mara ngapi kwa kazi kama hiyo...?’ akaulizwa
‘Mhh,sikumbuki,
...yawezekana mara tano,au zaidi..sikumbuki, ni kwa vile naaminika na
watu....’akasema
‘Kabla ya
kazi hiyo unakumbuka ulitumwa lini kuchukua mzigo kama huo kuupeleka sehemu
fulani, ukalipwa....?’ akaulizwa
‘Mhh....hata
sikumbuki, ni muda kidogo,unajua kazi kama hizo ni za muda tu,..inatokea tu,
sasa sikumbuki ..sikumbuki,.....’akatulia
‘Nikuambia
kitu, maelezo yako hayana ukweli, na unaposema hukumbuki, inaonyesha kuwa wewe
ni muongo...’akaambiwa
‘Sasa
mnataka nisemeje...niambieni mnavyotaka nyie...’akasema
‘Unajua,wewe
utakumbuka tu, ukifika gerezani,huko utasema kila kitu, maana huko kuna watu
wakorofi, wauwaji, walioshindikana,watu ambao huwezi kuamini kuwa walizaliwa na
wazazi,hawana utu....’akaambiwa
‘Yaani
mnataka nipelekwe huko kwa vile sijawaambia mnayotaka nyie, au...?’ akauliza
‘Wewe
umekamatwa kwa kosa la kuua,...wewe jamii inakutambua kama mkorofi, jamii
imekuchoka, hilo gereza linakufaa wewe,....’akaambiwa
‘Ina maana
napelekwa kwa gereza la ....’akashindwa hata kumalizia mara akasikia kuwa ana
mgeni na haraka akasimama akiwa na mawazo huenda akawa ni mtaalamuu au mtu
yoyote anayemfahamu kaja kujaribu kumwekea dhamana.
‘Nasikia una
mgeni wako huko, sisi tumemalizana na wewe, nitakutana nawe huko gerezani
kuhakikisha umefikishwa huko, na zaidi ya hapo ni kuwa ujiandae, umtafute
wakili wako, la sivyo, useme tukutafutie wakili wa serikali....’akaambiwa
‘Mimi kwa
hivi sasa nawaomba, ....msinipeleke huko gerezani, na ...’akasema
‘Kuna mgeni
wake huyu mtu afande, ...’huyo aliyetumwa akasisitiza
‘Sawa
...tumemalizana naye,....’wakasema na kuondoka, na profesa akabakia na askari
mlinzi, ambaye atampeleka kwa huyo mgeni.
Alitembea pamoja
na huyo askari mlinzi hadi sehemu ya wanapokuwa wageni, akaambiwa
asubiri,..haikupita muda akaambiwa;
‘Yaonekana
mgeni wako bado anaongea na mkuu, subiri kidogo
‘Nimeambiwa
nina mgeni yupo huku ananisubiri, halafu tena, mnasema nisubiri kwanza huyo
mgeni ni nani....’akajitetea
‘Mgeni wako
anaongea na mkuu wa mkuu wa kituo....’akaambiwa
‘Kwahiyo
nifanyeje, maana nimechoka kuongea na watu, kama ni askari, mwambieni
nimechoka, sitaki kuulizwa maswali tena...’akasema
‘Huwezi
kutupangia kazi,kwanza ujue umecheleweshwa kupelekwa gerezani, wenzako
mliofungwa nao siku hiyo wote wameshapelekwa gerezani, sema wewe umesubirishwa hapa kwa vile ulikuwa unaumwa....’akaambiwa
‘Sasa ni nani
huyo mgeni wangu......?’ akauliza
‘Ni
mimi....’sauti iliyomshitua, na kumfanya atetemeke mwili mnzima, na muda huo
ulikuwa muda wake wa mwisho wa kuonana na mtu wa kumsaidia....,aliombea na
kutarajia mgeni atakaye kuja awe mtu wa msaada, lakini sauti aliyoisikia,
ilimuashiria kuwa sasa yupo matatani, sasa hana msaada tena, na...kesho asubuhi
na mapema ni safari ya kwenda gerezani
Akaogopa
hata kugeuka, akabakia akiwa amesimama, akiwazia mengi, akiwazia, jinsi gani
atakavyopokelewa na wabaya wake, watu ambao alishawahi kukosana nao, watu ambao
aliwahi hata yeye mwenyewe kuwarubuni, na hata kutoa ushahidi ili watu hao
wafungwe kwa ajili ya kuingiza pesa, kwake kupata pesa ilikuwa jambo
lolote,....sasa atakwenda kukutana nao huko gerezani...
‘Ipo siku na
wewe utafungwa, na nipo tayari kusubiria hadi siku hiyo, ili tukatane huko gerezani,
na ukija utakuwa hawara yangu.....’akakumbuka siku alipokwenda kutoa ushahidi
wa jamaa mmoja aliyeshitakiwa kwa madawa ya kulevya, na yeye akathibitisha kuwa
kweli aliwahi kumuoana akiuza madawa hayo.
‘Huko jela kuna watu wangu, ....ukifika huko
ujue ndio mwisho wako....’akakumbuka hiyo sauti kutoka kwa mama mtemi.
Na leo yupo
rumande anasubiria kupelekwa huko, huko kwenye gereza lililoshindikana, gereza
ambalo waliwahi kufika huko wakaweza kumaliza kifungo, wakitoka, utawaonea
huruma, kwani ni lazima watatoka na tatizo fulani mwilini na wengine hawamalizi
mwezi, wanapoteza maisha.....
‘Gereza
hilo,...liliwahi kufungwa kwa vituko vyake,....kipindi hicho lilitambulikana
kama gereza la kifo, wale wanaojulikana
kuwa ni wauwaji, ...wakorofi wa jamii, ambao wanatakiwa kufia huko ndio
wanapelekwa huko...kuna visa vibaya hata havielezeki,....’aliwahi kuambiwa siku
moja
‘Mtu
ukipangiwa kwenda huko ni bora ujiue tu....’akaambiwa
‘Hata kama
hujahukumiwa unaweza kupelekwa huko?’ akauliza
‘Hata kama
hujahukumiwa!, kama kesi yako ni mauji, na wewe waonekana mkorof wa jamii,
...unapelekwa ukisubiria kesi yako huko,....na hasa kama una jambo hutaki
kulisema, ...na usiposema litaleta madhara,......wanakutupia huko, ukionja joto
yake utasema kila kitu....’akaambiwa
‘Mhh...’siku
hiyo aliogopa kabisa kwenda jela....
Leo hii anaambiwa kesho anapelekwa huko, na
ili asipelekwe huko, labda kungelitokea wakili akaongea na wakuu wa hapo au wa
huko, huenda wangelimtetea,...huenda angelipelekwa gereza jingine, akisubiria
kesi yake,....
‘Lakini mimi
sijaua, kwanini hawanielewi,.....’alijikuta akisema peke yake.
‘Mimi
sikubali kwenda huko, ni bora nijue....’akasema kwa sauti, akiwa anasubiria huyo
mgeni wake, aliombea huyo mgeni awe mtu atakayeweza kumsaidia, awe ni jamaa
yake, na jamaa yake ni nani, labda kijana wake, labda mtaalamu, ....labda
Sasa sauti
anayoisikia sasa,.....aliombea vinginevyo, ....akajua sasa kaisha, sasa
alichokuwa akiambiwa ndio hicho anakwenda kupambaa nacho, na njia peke yake
sasa ni kujiua tu....
‘Huyo hapo
ndiye mgeni wako,....’akaambiwa na mlinzi, na akabakia akiwa ameduwaa
‘Mnapewa
nusu saa tu ya kuongea maana muda umekwisha wa kuonana na wageni...’akaambiwa,
‘Na hata ruhusa
hiyo ilipotolewa, profesa hakutamani kugeuka kuonana na huyo mgeni wake,
akabakia amesimama, akiwa kampa mgongo huyo mgeni wake, alikuwa hatamani
kugeuka kuonana na huyo mgeni wake...
NB: Tuishie
hapa kwa leo
WAZO LA LEO: Kujua maumivu, au ubaya wa jambo, ni mpaka likupate na wewe, ukiambiwa tu, au ukiona
mwenzako, anahangaika ,au analalamika, utaona ni jambo la kawaida tu, na
utaweza kumpa ushauri mwenzako kuwa avumilia ndio maisha, au utalichukulia ni
la kawaida tu, lakini siku likikukuta, ..hapo ndio unaweza kusimulia,
kwani...aisifuye mvua imemnyeshea.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment