Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, July 29, 2015

RADHI YA WAZAZI-24

Profesa aligongana na mtu, na kupepesuka, mtu aliyemgonga alikuwa mgumu kama chuma, na athari za kuogangana naye zilimuacha akiwa na maumivu mwili mzima, hajawahi kuhisi hivyo baadaye....


Mtu yule alikuja kuvua mawani, baada ya kusema ‘Oh... am’ sory....’ na ndipo Profesa akamgundua ni nani....

Na kauli yake aliyoitaja mwishoni kabla hajaingia ndani ya kibanda cha simu ilimfanya akumbuke kitu,

Its you again...’

Tuendelee na kisa chetu

*************
Its you again...’

Hii kauli aliisikia wapi vile, akajaribu kukumbuka ....ohoo akakumbuka, ....

Ni siku ile walipokuwa wakisaidiana kumbeba yule jamaa wanayemla pesa za mlungula,...ndio, aliisikia siku ile,

Ni siku ile pale yule jamaa alipozidiwa na ulevi! Alikumbuka kabisa kusikia hiyo kauli siku ile, lakini aliyesema hivyo alikuwa ni mtu mwingine kabisa alikuwa ni ni muhudumu wa ile hoteli, anakumbuka vyema kabisa , sio huyu jamaa aliyekutana naye akiingia kwenye kibanda cha simu....

Sasa iweje, kauli ile ile, sauti ile ile, sasa imetokeaje kauli hizo zifanane, ni bahati tu imetokea hivyo,...

Alikumbuka kabisa kusikia kauli hiyo na kwa sauti hiyo hiyo,  ni baada ya jamaa kuzidiwa  na ulevi, na yeye ndipo alipojitokeza akiwa amevalia sare za humo ndani, alifaya hivyo ,makusudi,...na hapo ndipo akaanza kuongea na mdada wa mle ndani;

‘Mhh, huyu jamaa vipi, mbona yupo hivyo,kalewa kupitiliza nini ...?’ akauliza na yule kwanza akamtupia jicho, halafu akasema;

‘Watu wengine bwana, wanajifaya wanajua kulewa, kumbe ovyo, angalia kanywa kiasi gani mpaka afikie hali hii, mimi hata sijui tumfanyeje....’akasema mdada

‘Hebu nimwangalia vizuri, mmmh huyu si yule jamaa yangu, anayekuja kunywa kunywa hapa, akitaka wasichana warembo wamzunguke kama mfalme,...mmh leo vipi kazidiwa eeh, na imekuwaje, mapaka saa hizi bado hajaondoka,mmh mdada ulitaka kumtoa pesa nini....’akasema

‘Nilimuomba tuje kuywa naye kidogo huku juu, sasa kumbe hakuzoea kunywa zaidi,kajifanya anaweza kunywa ..unaona alivyo, wewe, wewe...unaoa alivyozidwa,.....’akasema akimtikisa tikisa huyo jamaa, na jamaa likuwa kinyosha mkono kama anataka kusema kitu, lakini anaishia kulala kichwa mezani.

‘Niacheni....nataka kwenda nyu-nyumbani....’anasema na kulala

‘S-s-sasa ngoja tufanye hivi  tumsaidie apate nguvu arudi nyumbani kwake isije ikawa tatizo , unamfahamu mke wake alivyo mkali, akija hapa itakuwa hakieleweki.....’akasema

‘Tutamsaidiaje kwa jinsi alivyo, hapa ni kumwagiwa maji labda, .. na huduma ya kwanza,....lakini akiwa hapa tutafanyaje...unasemaje....?’ akauliza

‘Hapana kwanini tusimpeleke chumba hicho hapo cha ya huduma ya kwanza....?’ akawa kama anauliza

‘Oooh, lakini sio mgonjwa, ... lakini sawa, hata hivyo, unamuona jamaa mwenyewe alivyo, bonge la mbaba, ..tutawezaje kumbeba hadi hapo kwenye chumba cha huduma ya kwanza...?’ akauliza mdada

‘Inabidi tutafute msaada, hebu, wewe ....kamuite mfanyakazi mwingine mwaminifu....’akasema huku akiajaribu kumuinua huyo jamaa lakini haikuwezekana.
Na mdada kwa haraka akasogea kuelekea upande mwingine walipokuwa watu wakisherehekea, akaita kwa sauti kubwa

‘Waiter, msaada hapa.....

‘Waiter help...’ na mara akaja jamaa mmoja akiwa kavalia sare za mlemle ndani , na kwa zaidi alikuwa kavalia kofia jeupe, kama alilovalia profesa.....na mawani meusi,...

Kwa muda ule profesa hakuwa na wasiwasi, yeye alijua kuwa ni muhudumu wa humo humo,...na uvwaaji ule wa kuongezea kofia na mawani meusi, kama alivyo vaa yeye, alijua ni mbwembwe tu, maana  walikuwa wakisherehekea siku ya kuzaliwa kwa mmoja wa wafanyakazi wa humo.

Yule jamaa akaja hakuongea kitu, kama alijua, yeye alichofanya ni kuinama, akamuinua huyo mlevi, akawa kama anamsimamisha, na alipoona jamaa hawezi hata kumsimamisha, akaonyesha ishara, kuwa wengine wakae upande ili aweze kumbeba...

‘Mhh,jamaa lina nguvu, alimuinua huyo mlevi, na kumweka begani,na kuanza kuondoka naye...

‘Huku...muingize humo....’akasema mdada, alipoona jamaa anataka kuondoka na huyo mlevi kuelekea sehemu ya chini.

 Basi mlango ukafunguliwa wa hicho chumba cha dharura, na akaingizwa huyo jamaa na kubwagwa kitandani, na jamaa muhudumu, aliyembeba huyo mlezi, akasubiria pembeni.....

Profesa kwa vile alimuamini huyo mdada, wala hakuhangaika kumuangalia yule jamaa zaidi,...yeye alipoona huyo mbebaji kasimama akisubiri, akasema;

‘Inatosha mimi niachieni huyu mtu,mimi ni jamaa yangu najua jinsi gani ya kumsaidia, wewe unaweza kwenda kuendelea na shughuli zako, ..’akasema akimgeukia huyo muhudumu mwanaume aliyembeba huyo mlevi, na kidogo alitaka kumtizama usoni huyo jamaa, japo kavalia mawani,na yule jamaa akageuka kuangalia mlangoni kama anaondoka, na muda ule yule mdada akaondoka kwa haraka...

Mle ndani kulikuwa na kitanda, kuna kilakitu,  kama chumba cha hotelini zaidi kwa juu kuna sanduku la huduma ya kwanza, kulikuwa na kabati jingine la juu kidogo, na profesa alipoingia tu mle cha kwanza kuangalia ni juu ya ile kabati..

‘Mbona sijawahi kukuona humu ndani...?’ akauliza profesa akiongea na huyo muhudumu mbebaji akiwa anatembea sasa kutoka nje, lakini akaona vitu pale mezani, kama muhudumu alitakiwa kuviondoa, na kweli jamaa akafanya hivyo

Yule jamaa hakusema kitu akawa anakusanya vile vyombo kulikuwa na chupa na sinia alilokuwa nalo mdada, naona mdada katika kuondoka kwa haraka alikuwa kavisahau, au vilikuwepo humo kabla, ....

Jamaa alipohakikisha hakuna kitu kingine kistochostahiki humo ndani, akaanza kutembea kutoka na alitembea mwendo wa kuhesabu hatua, hadi mlangoni, halafu akasimama akageuka kidogo, kiasi cha kugeuza kichwa, akasema...,

‘Umesemaje....?’ akauliza

‘Sijawahi kukuona hapa kabla...’akasema

‘Mhh, ....Its you again...hahaha.....see you later..’alisema huyo mtu na kwa haraka akaondoka.

Its you again ...., ni mimi tena, ...ina maana niliwahi kukutaa naye mahali, ni wapi,..ni nani huyu..,mbona sura ngeni kwangu, na karibu wahudumu wote wa humu ndani nawafahamu....’akawa anajiongelesha kichwani, na wakati profesa anatafakari hayo maneno yana maana gani, mara mdada mmoja akaingia akiwa kavaa koti refu, la kujifunika sehemu kubwa ya mwili,  sura tofauti na yule mdada wa kwanza...

Yule mdada alipoingia kwanza akasimama hukua kiwa kashikilia kiuona, akikagua mandhari ya mle ndani, ...Profesa aalibakia kumuangalia huyo mdada mpya aliyeingia kwa mshanga, ...

‘Wewe nani unafuata nini huku...’akauliza profesa akionyesha mshangao, na yule mdada mpya kwanza kaonyesha ishara ya kidole, kama kumnyamazisha profesa, halafu akageuka kuangalia kule kitandani.

‘Na wewe nambie unafanya nini na huyu mtu, unajua huyu mtu na nani kwangu....?’ akauliza mdada,na kumfanya profesa abakia na mshangao, na akauliza

‘Ni nani kwako huyu mtu....?’ akauliza

‘Mmmh, nimemfuata my baby is  he ok,.......’akasema huyo mdada sasa akitembea kwa madaha, na alipofika pale kitandani, akageuza uso kimadaha, ....taratibu akaondoka lile koti la juu, na kubakia na kivwazi cha aina yake, kilikuwa ni  kivwazi cha kulalia,ni sawa na nusu uchi tu...

Who are you...?’ akauliza profesa kwa ukali

‘Nimeshakuambia huyu ni mpenzi wangu aliniacha chini sikujua yupo huku,mmmh, niache na mpenzi wangu, nimfanyie masaji,najua sasa hivi atazindukana, unaweza kuondoka, ....’akasema huyo mdada akiwa sasa anamuinamia huyo jamaa pale itandani alipolazwa huyo jamaa, na jamaa alikuwa kama anaanza kujitambua, ...

Jamaa alijitikisa, akajiinua, akapangusa uso, akapiga miayo, halafu akatikisa kichwa, akashika kichwa,halafu akasema

‘Ni...ni..nipo wapi....’akasema kwa sauti ya kilevi

‘Umenisahau baby..ulinikimbia kumbe umekuja huku juu,...’akasema huyo mdada

‘Nataka kwe-kwe ndani nyumbani.....’jamaa akasema akijaribu kusimama,  lakini akawa anapepesuka, akataka kuanguka, na mdada akamdaka, wakawa kama wameshikama kusaidiana, na wote wakaangukia kitandani.

What are you doing...?’ akauliza profesa alipoona hiyo hali

‘Hiyo sio kazi yako, unasubiri nini, huyu ni mpenzi wangu...nataka nimsaidie tuondoke,....’akasema mdada

Ok,....but be careful, kalewa ...’akasema profesa

Mara jamaa akawa sasa kidogo kama anajielewa, akajikuta yupo mikononi mwa huyo mdada,akawa sasa kama anataka kujitoa kwa huyo mdada,na huyo mdada akawa kama anamsaidia ...profesa akatupa jicho juu ya lile kabati kwa kujiiba, na kutikisa kichwa, akasema;.

Ok, let me go but be careful,... lakini uwe makini na huyo mlevi,kalewa, anaweza kukufanyia ubaya, ....’akasema profesa akitoka mle ndani, akaondoka na kuja kukaa nje akisubiria, kama atahitajika...

Alipofika nje hakumuona yule jamaa, akatembea kidogo na kuangalia huku a kule, akakuta hakuna mtu, na upande mwingine kulikuwa na sherehe za kumpongeza mfanyakazi mwenzao siku ya kuzaliwa, hakuwa na shughuli nao, mawazoyake ni huyu mtu, aliyemuambia kuwa 'its you again...

Ni wewe tena...ni mimi tena,nilionana naye wapi, labda ni humu humu ndani, lakini kauli hiyo ni kama kunikoga...’akawa anawaza profesa, ....

Haikupita muda mara ukelele wa ‘help... help ....ananibaka..saidia huku....’ukasikika...
Na muda ule kulikuwa na wahudumu wawili wa kike , walikuwa wakipita, wakasikia hivyo, wakaanza kukimbilia kuelekea kwenye hicho chumba, na profesa akawa wahi na kutangulia yeye, yeye aliingia kwanza na wale wadada wawili wakafuatia

‘Ni nini kinaendelea huku mbona kelele za kuomba msaada....?’ wakauliza

Mle ndani kilichokutwa,mjamaa alikutwa uchi,akiwa kweli kwenye harakati za kulazimisha, na wale wadada kuona vile wakaanza kumsaidia yule mdada, 

Profesa hakuhangaika nao,...., akanyosha mkono juu ya lile kabati,na kuchukua chombo chake , na taratibu akaondoka zake....

********

 Profesa alipokumbuka hiyo kauli aliyosikia siku ile kwenye hilo tukio akajikuta akisema

‘Haiwezekani, haiwezekani...ina maana huyu jamaa alikuwepo kwenye lile tukio, lakini mbona sikuwahi kumuona, nakumbuka yule aliyekuwemo siku ile alikuwa ni muhudumu wa pale ndani, nina uhakika alikuwa muhudumu, japokuwa sikuwahi kumuoa kabla...’akawa anaongea peke yake

Akajaribu kukumbuka maumbile ya huyu mtu na yule muhudumu, lakini hakuweza kuoanisha vyema, maana tukio lile lilikuwa la haraka,hakutarajia hivi,maumbile kama yanafanana....nguvu, mhh...

‘Haiwezekani ni lazima niongee na mdada aniambie ukweli. ...haiwezekani....’akawa anajilaumu

Kwa muda ule alikuwa kasimama kwenye barabara, akigeuka kutafuta sehemu nyingine ili apige simu kwa mdada kuhakikisha hicho anachokifikiria, alijua kwenye kile kibanda alichokuwa akitumia mwanzo jamaa atakuwa yupo hapo akipiga simu.

Kwanza akajaribu kumtupia jicho yule jamaa kwenye kibanda cha simu, ili kumuona vyema, lakini......hakukuwa na mtu

Kwa mshangao hakumuona mtu yoyote kwenye kile kibanda cha simu,.... ni sekunde chache tu za kutembea kuelekea barabarani na alipogeuka kuangalia kwenye hicho kibanda, alikuta kipo cheupe hakuna mtu.

‘Huyu mtu kaenda wapi,...uwepesi gani huo, nina uhakika alikuwa ameshaanza kupiga simu, na kuanza kuongea, sasa iweje, atuweke kwa haraka hivi kama  upepo,....’akawa anajiongelesha mwenyewe

Profesa akageuka kuangalia huku na kule lakini hakuweza kuona dalili ya mtu kama yule hapo karibu, na hapo akajua kweli sasa yupo matatani.

‘Huyu mtu ni kupe akikudanga keshakuganda, ni lazima ainyonye damu 
yako....’akamkumbuka maneno ya mtaalamu alivyokuwa akimwambia.

*********

 Profesa akawa anatembea kuelekea ofisini kwa mtaalamu, alikuwa anataka kupata pesa, pesa ndio suluhisho ya haya anayokumbana nayo sasa, bila pesa hataweza kuwashinda maadui zake,....pesa ataipataje !

Na pia alikuwa na maswali mengi ya kumuuliza huyo jamaa anayejiita mtaalamu, alijua bila msaada wa huyo jamaa sasa yupo mtatani, jamaa anaonekana kujua mengi,na anaweza kuwa msaada mkubwa kwake, lakini jamaa anaonekana pia kuwa anataka kumgeuka, tamaa ya pesa imeshamtawala...na yeye anahitajia pesa tena pesa nyingi, sasa afanyeje

‘Dawa nikamuone uso kwa uso,.....nitapambana  naye uso kwa uso,kabla usiku sijaanza kuwasiliana na mtu wangu,kabla usiku sitajaingia kazini lazima kieleweke..’

Alifika mtaa unaoingia kuelekea maeneo hayo  ya ofisi ya mtaalamu,...na mara gari likaja kwa nyuma yake, likampita, yaonekena gari hilo lilikuwa likielekea kwenye hizo ofisi, na cha ajabu gari hilo lilifika mbele likasimama,....

Kwa hali ile profesa akahisi hatari akageuka kutaka kurudi alipotokea, hakutaka kuongea na mtu mwingine zaidi ya mtaalamu, hakutaka kujulikana anaelekea kwenye hizo ofisi, lakini lile gari likarudi kinyume nyume kwa haraka, hadi pale alipo

Mara viyoo vikashushwa, kwenye hilo gari, na jamaa akatokeza kichwa na kuanza kuongea

‘Profesa , profesa, long time never see you,...unaelekea wapi....?’ ilikuwa sauti nyingine iliyompa mshituko, akageuka kwa haraka kumtizama huyo mtu kwenye gari, hakutegemea kuonana naye kariuni hivyo,....

‘Nipo tu,...sielekei mahali...’akasema profesa akitaka kuondoka lakii mguu ukawa mnzito

‘Ni vyema nimekuona nina mazungumzo na wewe muhimu sana....’akasema huyo mtu kwenye gari, na hapo akajua ni yale yale huenda tayari ameshaanza kazi.

‘Kuhusu nini,sina mazungumzo na wewe kwa hivi sasa....tulishamalizana...’akasema profesa

‘Najua, ...lakini si unajua kazi zangu, leo nina kazi hii kesho kazi hii...’akasema

‘Hayo I majukumu yako hayaihusu...’akasema profesa

‘Najua mlishakubaliana na mama mtemi, japokuwa sivyo sahihi..kwani sheria ilitakiwa ichuke mkondo wake,lakini nikaona mnajuana, na kazi yangu sio kushinikiza bali I kufichua ukweli na uamuzi unakuwa kwa mwenyewe...kazi yangu ni kutafuta ukweli na kuuweka wazi, au sio.....’akasema

‘Ukweli,au uzushi tu,....kupekenyua yasiyokuhusu...mnafiki mkubwa wewe...’akasema bila kujali

‘Mhh, ....wabaya wananisema hivyo, lakini wakweli wananiamini,...yule mama alitaka kujua ukweli, na mimi nikamtafutia ukweli, au sio..., japokuwa analalamika kuwa wewe hujazigatia makubaliano, umekuwa sio mkweli,..’akasema

‘Kwahiyo ndio kakutuma kuongea na mimi...?’ akauliza

‘Mhh...hapana, kwa hivi sasa hilo halinihusu, kasema yeye mwenyewe atakushughulikia...’akasema huyo mtu...hiyo kauli ikazidi kumtia hofu profesa, yeye mwenyewe atamshughulikia..

‘Sasa unataka nini kwangu....?’ akauliza profesa kwa hasira

‘Kuna kitu nataka tuongee,...si unajua kazi zangu, naruhusiwa kuwahoji watu, lakini sio kwa nia mbaya, ili niupate ukweli, na leo nimeona niongee na wewe,  kabla sijaingia zaidi kwenye undani wake, ...’akasema

‘Kwanini mimi...unataka kuongea na mimi kuhusu nini....ya mama mtemi si umeshamaliza umeshalipwa pesa yako au..?’ akauliza profesa

‘Hapa ni barabarani,sizani kama upo tayari tumwage mtaka kwenye kuku wengi,....au sio,ingia ndani ya  gari tuongee kiuungwana...’akaambiwa

‘Nina kazi nafuatilia, sina muda wa maongezi, hususani na wewe...’akasema

‘Hata hii ni kazi na huenda ikakusaidia zaidi na hata ukaghairi kwenda huko unapotaka kwenda, ni muhimu sana mtu wangu...vipi kule unapofanya kazi kwa sasa...?’akasema na hapo profesa akajua ni yale yale aliyokuwa hayataki.

‘Wapi ninapofanya kazi....na inakuhusu nini kufanya kazi kwangu, toka lini ukajali maisha yangu?’ akauliza profesa

‘Najua wewe kawaida yako, hufanyi kazi mahali bila kuacha majeraha,....sasa unaingia tuongee au unataka nipayuke hapa hapa,unaona watu wanapita wakisikia nakuulizia haya ninayotaka kukuulizia, inakuwa sio vizuri, hata wewe mwenyewe hulioni hilo, tuongee kiuungwana au sio...’akasema

Japokuwa Profesa alikuwa na uharaka wa kwenda kwa mtaalamu ili akapate pesa za kwenda kumpooza mama mtemi, lakini kwa hali ile hakuwa na jinsi, ikabidi aingie kwenye lile gari, na kusubiria kitakachofuata...na alipoingia jamaa aliyekuwemo mle ndani hakuwa na haraka ya kuongea...alikuwa kashikilia usukani akiwa kaangalia mbele...

‘Haya nambie maana nina haraka zangu....nakupa nusu saa,tena hizo nyingi, dakika kumi na ....sekende kadhaa....’akasema kwa hasira huku akiangalia saa.

‘Usiwe na haraka saana...unajua mambo haya mambo msiyapeleke kwaharaa kihivyo...na,kiujumla nimeshaanza kukuelewa, sasa sijui, yote inategemea wewe, maana inabidi ifanye kazi yangu ,....na bila kufanya hivyo, unafikiri nitakula wapi.....sasa yote inategemea wewe....sijui, labda safari hii tukaelewana,....’akasema huyo mtu

‘Kuelewana kuhusu nini, wewe umeniharibia maisha yangu...’akataka kulalamika

‘Mimi nikuharibie maisha yako....! Kwa vipi profesa, ...nimekufanya nini...hebu nambie...? ‘akawa kama anauliza.

‘Mhh, hebu nambie unachotaka kuniambia, unajifanya hujui eeh, ni nini umekifanya kwa mama mtemi,umenitia doa, sasa nasakwa kama muhalifu, halafu unasema tuelewane na wewe,....siwezi kuelewana na mtu kama wewe, kwanza kwa lipi, wakati ulishamaliza...’akasema

‘Tutaelewana tu, mbona hakuna shida kabisa,...nikuambie ukweli profesa mimi sio mbaya, mimi huwa nafanya kazi yangu tu,...siunajua kazi yangu ilivyo, sasa mimi nimekosea nini....’akawa kama anauliza

‘Niambie ulichonitaka...nachelewa kwenye shughuli zangu...’akasema

‘Unakwenda kwa mtaalamu au sio...’akasema

‘Hayakuhusu....’akasema

‘Unajua profesa sasa hivi,tutaelewana sana, huna ujanja...ni uamuzi na tena uwe uamuzi wa busara, na...sikutakii mabaya, ila upo kubaya sana, sasa ni uamuzi wako, ama uelewane na mimi, au ukapambane na mama mtemi, na safari hii ujue hayupo peke yake,...’akaambiwa

‘Sijakuelewa....’akasema profesa

‘Umeshanielewa sana, usitake mpaka nimwage sera, wakati wewe umeshazitekeleza kwa matendo....ni uamuzi tu, tuelewane..funuka tushirikiane mbona mimi sina matatizo....’akasema

‘Ongea unachotaka.....vinginevyo mimi natoka kwenye gari lako, unasikia wewe mpekuzi wa mambo yasiyo kuhusu, mimi sikuogopi,.....nenda kwa hao waliokutuma waambie .....’akatulia

‘Unajua profesa, kila mtu ni mkali kwenye sehemu yake,...na sitaki tufike huko,...wewe sasa hivi si unafanya-fanya kazi kwa yule jamaa kutoka India au sio...?’ akawa kama anauliza.

‘Nafanya sehemu nyingi tu,....kwanini useme kwa huyo mtu...?’ akauliza

‘Unaona sasa..., mimi nimeshakufahamu vyema tu, ...nakudokezea hilo ili ujue kuwa nimeshafahamu mengi,sio kwamba nakupotezea muda wako, hili huenda likawa na manufaa kwako, tukielewana lakini, unielewe hapo, mimi ndivyo nilivyo, sitaki kumuumiza mtu, sitaki ubaya na mtu, najua wewe unatafuta maisha, au sio, na kila mtu ana njia zake,japo nyingine mhh,...’akatulia kidogo

‘Sasa mimi nilikuwa a ombi kwako, ....na ombi hilo ni la kuamua tu,...ama uwe na mimi au nikuache ufanye upendavyo, na najua kwa vyovyote kuna watu wapo nyuma yako, wanakutafuta kwa kila hila, ....siwezi kusema ni maadui zako, ...hapana,...ila ni wahasimu wako, natumai unanielewa hadi hapo...’akasema huyo mtu

‘Mimi sijakuelewa.....’akasema profesa akijifanya haelewi kitu,  na simu yake ikawa inaita alipoangalia mpigaji akaona ni namba ya mama mtemi...

‘Pokea simu yako.....’akaambiwa  na huyo jamaa
NB: Naishia hapa naona muda umetaradadi, na mambo yanazidi kubadilika, hata sijui la kuamini, ...labda ndio kidunia.


WAZO LA LEO: Uongozi wa ujanja ujanja wa kuwahadaa watu kwa lugha tamu lakini zenye sumu ndani yake,ni utapeli...ni dhuluma,....wewe kama kiongozi ndani ya shirika, wewe kama mtawala, mwanasiana au yoyote mwenye dhamana, kaa ukijua kabisa , kudanganya, kuhadaa, kwa visigizio vyovyote,  ili upate kisicho halali yako, ili ufaulu malengo yako, huo sio uongozi, huo ni ujambazi wakujificha, huna tofauti na jambazi anayekwiba usiku,...na ukumbuke ipo siku utanaswa tu, maana unadhulumu, kudhulumu ni wizi, na za mwizi ni arubaini.
Ni mimi: emu-three

No comments :