‘Pamoja na
hilo kuna mengine nataka akifika wakili wa familia yetu tuyaweke sawa, kuna
mambo muhimu nahitajia yaingie kwenye makubaliano yetu, kiukweli mume wangu sikuamini
tena, kutoka na matendo yako,a zaidi unazidi kunidanganya..’akasemamkewe
‘Kwani mke
wangu nimekudanganya nini hapo, na hayo mengine ni yepi, au kuna kitu gani umesikia mke wangu...majungu
ya watu?’ akauliza mumewe akionyesha wasiwasi na kama kukerwa
‘Kiukweli sio swala la kusikia, ila nimejionea
mwenyewe na kuziona nyendo zako kwa macho yangu, na kwa vile mimi ni mtu
mzima,siwezi kusubiria tatizo liingie ndio nianze kuhangaika, kwa ufupi mume
wangu...sikuamini tena, sikuamii, sikuamini...’akasema
‘Huniamini...mmmh,
ina maana mke wangu umefikia hatua
hiyo...’akasema kwa hamaki,
Tuendelee na
kisa chetu
**************
Mume alirudi
kwenye kiti akakaa ,halafu akasimama, na akilini akawa anasikia sauti kama
inalia kwenye simu ikisema,
‘Kwahiyo unataka tupeleke nakala moja ya hizo
picha chafu kwa mkweo.....unasemaje ili uone kuwa hawa watu hawaogopi...au
tumpe mkeo nakala moja tu, ili ajue jinsi gani mume wake alivyo...’
‘Labda mke
wangu keshatumiwa nakala ya picha, ndio maana kafiki hatua hii, yanaonekana
kama kuna kitu kaambiwa, sio bure....’akawa anawaza akilini
‘Mume wangu nilikupenda sana...nikawa nipo tayari kupata shida kwa ajili yako,nikijua na wewe
mwenzangu upo hivyo hivyo...’akasema mkewe
‘Ulinipenda, ina maana.....’akasita
‘Kutokana na
hayo, nahisi kupenda kisichopendeka,nahisi kuwa mwenzangu una lako jambo,....lakini
tumeshazaa tuna watoto wakubwa, ..hata hivyo, hakijaharibika kitu,...muhimu
nataka wakili akija, tuyaweke haya bayana,na mimi niwe na amani ....’akasema
‘Lakini mke
wangu sizani kuna haja ya hayo yote...mimi nakuamini mke wangu, na wewe
uniamini pia...mbona mimi sikutilii mashaka yoyote....’akasema
‘Nilihisi
huenda nikupe muda, na kama ungeniambia ukweli wote, mimi ningelichukulia kuwa
umekosea kama binadamu,...ningeyasahau hayo yote ...lakini jinsi ulivyonijibu
na jinsi unavyoendelea kunificha ukweli, hukutaka kukiri kuwa umekosea, yaonyesha
wazi, kuwa kweli umedhamiria ...’akasema
‘Lakini
nimeshakuambia kuwa kuanzia sasa sitakwenda huko kwenye bar tena, na nilikuwa
nakwenda kunywa tu, unajua tena mabinti wa pale ni wacheshi tu, na sikuwa na
lolote kwao, nakunywa, wanajipitisha mimi siwajali, nikimaliza kunwya naondoka
zangu....na pia hiyo akaunti ilikuwepo tu , na kuitumia ni kwa dharura tu, na
nimeaidi kuanzia sasa tutaiweka wazi....sihitaji tena kuitumia, hilo
halitoshi...’akasema
‘Mume
wangu....kwa kauli yako hiyo na matendo yako hayo, sasa naanza kuwaamini wazazi
wangu,.....’akasema
‘Kuwaamini
kwa vipi...?’ akauliza
‘Ukumbuke,
nilikubali tuoane, japokuwa wazazi wangu hawakuwa radhi nawe...nikafanya hilo
kwa vile nilikupenda sana, lakini kumbe mwenzangu una lengo lako,...huko kwenu
umeshaanza kujenga, kwa jina la mdogo wako,..utakataa na hilo, badala ya
kujenga kwa jina la wanao, unajenga kwa jina mdogo wako....’akasema
‘Nani
kakuambia uwongo huo...’akasema akitoa macho ya kushangaa
‘Hahaha,
unashituka eeh, hilo ni moja ya mengi niliyoyagundua, kwa muda mfupi
tu.....najua kuna mengi umeyafanya,...mimi sijali, muhimu tu tuingie kwenye
hayo makubaliano...’akasema
‘Mkewangu
sasa huko umefikia kubaya, kama wewe unaamini kila kitu, unachoambiwa,,,huo ni uwongo ukweli ndio huo
niliokuambia, sielewi kwanini ukafikia hatua hiyo, hebu nambie kuna nini
kinaendelea, ...?’ akauliza akimuangalia mkewe kwa macho ya ukali japokuwa
mashaka yalikuwa yememjaa.
‘Mume wangu,
maisha ya ndoa ni makubaliano,na muhimu sana ni uaminifu, ndio maana wanandoa
wanaopendana kiukweli hawana haja ya kufuatiliana, kwanini wafuatiliane wakati
kila mmoja yupo ndani ya mwenzake..kila mmoja anamuamini mwenzake, na kila
mmoja anajichunga ....’akasema
‘Hilo..hi-hilo,
ni kweli kabisa, na mimi nimejitahidi sana kufanya hayo, ..nikuulize mke wangu kwanini
sasa huniamini, kwani kuna kitu gani kimetokea hadi ufikie huko kote,....ni
nani kakuongopea,hadi kufikia kuamini yote hayo..?’ akauliza mume mtu, lakini
mke mtu akaendelea kuongea
‘Tulipofika
hapa Ulaya, nilijua tutaishi maisha ya amani, tuwe na uhuru, ....maana kama
ulivyoona kule nyumbani, wazazi walikuwa wakitufuatilia kila tunalofanya,
nikaona nitakuwa sikutendei haki, kwani ulikuwa kama mfungwa ndani ya family
yangu,...ndio nikaona tuje huku, ili tuwe na uhuru, tuwe tunaweza kufanya mambo
yetu kama mke na mume kwa amani a upendo..., ilimradi yasikiuke masharti ya
ndoa....’akasema mkewe
‘Ni kweli
kabisa mke wangu, hata mimi nashukuru sana kwa maamuzi hayo, na mimi nakuahidi
nitajitahidi kufanya yote kwa matakwa ya ndoa yetu na kama kuna kitu
kimekengeuka, naahidi nitakiacha, si unaoana sasa nimeamua kuacha pombe,...nitakuwa
nakunywa hapa nyumbani tu...’akasema
‘Unajua
wahenga husema kunguru hafugiki, tabia ya mtu kubadilika ni nadra, atajifanya
anaficha makucha yake kwa muda, lakini
muda utafika, atakumbukia ubaya wake...kiukweli waliyosema wazazi wangu sasa naanza
kuyaona moja baada ya jingine....’akasema mkewe
‘U-u-meona
nini...huo uwongo ndio umeona, unajua ni nini kimesababisha yote hayo,
unafikiri mimi nimependa...’ akasema lakini akawa kama kashtuka hakutakiwa
kusema hivyo.
‘Huo sio
uwongo, ...nimethibitisha mwenyewe, na kama ilikuwa ni bahati mbaya kwanini
uendelee kukana, kwanini hukiri makosa, ....ina maana umedhamiria, ina maana
hata hayo niliyoambiwa dhidi yako ni kweli,....unataka ushahidi mwingine
nikutolee....’akaambiwa
Mume mtu
aliposikia hayo maneno, moyo ukaanza kumdunda,...akahisi huenda jamaa
wameshaanza kutoa siri kwa mkewe, na kama wamefanya hivyo, moyoni akaapa kuwa
atawatafuta hao watu mpaka awapate,...maana alishawapa pesa, na akawaahidi kumalizia
pesa nyingine akikabidhi nyaraka za benki, sasa kwanini wamamsaliti.
‘Ushahidi...!?
ushahidi mwingine.....?’akawa kashikwa na kigugumizi
‘Mume wangu kwa
jinsi ninavyoona wewe sasa unahitaji uhuru uliopitiliza, uutumie huo uhuru uutakavyo
si ndio...., inavyoonekana mimi nakubana sana..unahitaji namna nyingine ya
maisha, ..., ‘akatulia
‘Ha-ha..pana,hivi
hivi mke wangu,...naona kama unanitisha,...’akasema
‘Sikutishi,
kwanini nikutishe na wewe ni mtu mzima,
wewe uliwahi kusema kwa vile ni mwanaume unataka kufanya utakavyo,...sawa, nilikubali
hilo, ndio maana sikujali, nikikuona unakunywa, unaongea na wasichana wako,
niliona huenda ni moja ya starehe zako nikawa nakuacha tu..nikijua ni swala la
muda, ndio uanaume uutakao, si ndio ....’akasema
‘Mke wangu
nikuambie kitu, yaani kunywa, na hayo mengine ni kupoteza muda tu,hakuna kitu
kibaya nimefanya, haki mungu, sijawahi kufanya lolote baya, nakuapia...unataka
nifanye nini ili uamini’akasema lakini mkewe hakumpa nafasi akaendelea kusema;
‘Nimekuwa
nikipita pale kwenye bar, nakuona unakushikwa shikwa...mimi kama binadamu naumia,
lakini nikaona nikuache tu, ilimradi isiende mbali...najua huenda, ni kwa vile
nimekuwa na kazi nyingi, sipati muda wa kutimiza yote....basi nikaona nikupe
uhuru huo, si unataka uzungukwe na wanawake, wakushike shike,...basi nikajipa
moyo..nikijua hayo yatakwisha tu...’akaendelea kusema
‘Lakini mke
wagu nimeshakuambia kuanzia sasa ulevi basi sitaenda tena huko kwenye bar...nikitoka
kazini nakuja hapa mimi na wewe tu...’akasema
‘Najua
....yameshakufika shingoni, najua uliyotaka kwa hao wanawake, yamegeuka kuwa
shubiri kwako, nilijua itafika muda utagonga ukuta...najua kabisa hao wanawake
walikuwa wakifanya hivyo kwa malengo yao binafsi..’akasema mkwewe akionyesha
sauti ya kukata tamaa.
‘Lakini mke
wangu sijafanya ubaya wowote...mbona hunielewi, kwanini wanifanya kama mtoto
mdogo, haya sema unayotaka kusema...’akasema sasa kwa hasira
‘Kwangu mimi
sasa nimeona nisikufuatilize zaidi, wewe
sio mtoto mdogo, na kwa vile wewe unachotaka ni mali, uhuru, starehe, ngoja
nikupe hicho unachotaka, lakini ....’akasema sasa kwa sauti ya kuonyesha ukali
‘Unataka
kusema nini...’akauliza
‘Kiukweli
nimegundua kitu, wazazi ni muhimu sana katika maisha yetu,hilo nimeliona,..na
nlitaka tukiishi vyema, tukaaminiana, basi siku twende tukawafurahishe wazazi
wetu waone kuwa kweli tunapendana, kuwa kweli, wewe sivyo kama walivyokuwa
wakikuwazia...’akasema akiangalia saa ya ukutani, akachukua simu na kupiga,
lakini hakuongea kitu, akairudisha mezani
‘Mhh...hilo
ni muhimu sana, tutakwenda tu mkewe wangu mambo si hayo,....’akasema sasa
akihisi mkewe hakuwa na nia mbaya.
‘Lakini,mume
wangu yale wazazi waliyokuwa wakinionya kuhusu wewe na historia ya familia yako,naanza
kuyaona moja baada ya jingine...kweli tabia ya mtu inaonekana pale anapopata...’akasema
sasa akiwa kamkazia macho mume wake
‘Mhh,
sijakuelewa, una maana gani...?’akawa anahisi kukojoa
‘Kweli
nimeamini, wazazi sio watu wa kupuuza, maneno yao unaweza ukayazarau kumbe yale
maonyo yao yakawa kama laana kwako,hata
wasipotamka kitu laana, lakini kauli zao zinafinya....’akatulia
‘Mhh, unafikia
mahali unasema aheri ningewasikiliza
wazazi wangu,na sasa nakiri na najuta,
kumbe ningeliwasikiliza wazazi wangu, haya yote yasingelitokea....’akasema
‘Mke wangu
niambie kuna tatizo gani...?’ akaulizaa kwa hasira
‘Usijali,
wakili anakuja...nimeshayaanisha yote muhimu, ..natakupa nakala yako uipitia,
ili kama kuna tatizo, au kuna kitu nimesahau, ..uniambie, nia ni wewe uwe huru,
ufanye utakavyo, lakini ...’akatulia
‘Mhh...’akaguna mume mtu
‘Nataka
wakati nakupa nakala hiyo, wakili awepo, , yeye alishayapitia, na ameyaona kuwa yote yana
msingi, ..ila kukumbusha yote hayo ni kutaka wewe ukumbuke wapi tulipotoka,
nataka ukumbuke mapenzi yangu, jinsi nilivyojitolea kwako, ...nisigelifikia
hatua hii, ...’akasema
‘Hata laana
ya wazazi isngelituathiri...napata taabu, sifanikiwi,naishi kwa mashaka, hakuna
mafanikio, ni maisha ya shida tu..hii ni kwasababu wazazi hawana furaha nami kwa maamuzi haya, na waliniambia
mtoto akililia wembe muache atajikata tu ataona ubaya wake mwenyewe..’akasema
‘Kiukweli
nafahamu kabisa ndoa yetu haikuwa na baraka za wazazi...na sasa naanza kuipata pata,lakini
sasa...tuyaache hayo...ngoja wakili aje, najua tutayamaliza, ili kila mtu ajue
lake...’akasema
‘Mke wangu
ina maana....kwa-kwa-kwani vipi, ....?’ akawa anauliza na mara mlango
ukagongwa, na aliyeingia na briefcase
alikuwa ni wakili wao wa familia
Mume akanywea,
na aliyeongea kumkaribisha wakili alikuwa mke wa familia, akilini mume alijua
hapo sasa hana chake, ,...huenda huenda.......
NB Je kuna
nini kwenye hayo makubaliano
WAZO LA LEO: Upendo wa mali, upendo wa
kudanganyana, upendo wenye malengo ya ubinafsi, una mipaka yake,kamwe hautaweza
kudumu, lazima itafikia siku ukweli utadhihiri, na upendo huo utageuka kuwa ni
chuki. Tujitahidi kupendana kiukweli, ili kuleta neema kwenye familia.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment