Huyu mume mtu, alifika nyumbani baada ya kutoka benki ,nia mojawapo ni kuangalia jinsi gani ataweza kuongezea kiasi alichotakiwa na wanaodai mlungula,(blackmailer) lakini pia kutafuta muda zaidi kama anaweza kuwakwepa, au kujadiliana nao,hata hivyo,hayo hayakuwezekana.
Na mbaya zaidi alikutana na mtu asiyemtarajia kabisa,...haa,kweli siku ya kufa nyani miti yote huteleza,..kwani alishaharibu mambo, lakini hata hivyo hana ujanja,kwani hao watu wa mlungula wameshamkalia kubaya, hawezi kufurukuta, huku nako ....
Tuendelee na kisa chetu
Mume mtu
alipigwa na bumbuwazi, akabakia mdomo wazi, hakuratajia kabisa kukutana na huyu mtu ,na sio kawaida yake, yeye kuna muda aarudi nyumbani kwa dharura hii na ile kwa vile yeye anafanyia karibu na nyumbani, sasa alipomuona huyo mtu akajua kuna jambo ...akabakia akijiuliza, na kuweka fikira za labda,labda...ni sekunde chache za kuangaliana, hata hivyo,mwenzake, hakuonyesha kushangaa, na ndilo lilimfaya mume mtu kupata ahueni
‘Oh,vipi
mume wangu, mbona upo nyumbani...’akauliza mkewe mtu huku akimpita mumewe kuingia ndani.
‘Nilikuja
mara moja, kuna yaraka nilizifuatilia, jana kuna kazi nilifanyia nyumbani nikasahau
kuchukua hizi kumbukumbu...’akasema huku akionyesha mkoba aliokuwa nao.
‘Mhh, sikukuona ukifanya kazi yoyote jana, Oh,....hata hivyo hata mimi kuna kitu nimesahau.. nina haraka kweli, niwahi kurudi ...’akasema
mkewe mtu akimpita mumewe na kukimbilia ndani, ni kweli kuna kitu alikisahau na
alihitajika kazini kwa haraka na hizi kumbukumbu za kazi aliyokuwa ameifanya
jana usiku.
Mumemtu,akahisi labda mkewe kaja kuzichukua hizo pesa akazitume, hapo akasimama akitaka kurudi, lakini akilini akakumbuka vitisho vya hao watu....akaomba mkewe asije tu kuligundua hilo mapema.
Mumemtu kwanza akavuta subira, lakini moyoni pia, aliona kuwa mkewe ana haraka na uharaka ule, hautamfanya kuhesabu pesa, kama ni kuchukua pesa atazichukua na kuondoka, na akigundua atakuwa keshazirejesha zile pesa alizochukua na muda huo hatakosa uwogo wa kusema
Yeye,kwa haraka
akatoka akapiga tambona kuelekea kwenye gari lake,...akaanzisha gari lake, na kwa haraka akaendesha kutoke eneo la nyumba,
kuelekea sehemu aliyoahidiwa kuupeleka huo mzigo,...ilikuwa ni kule kule kwa
yule mlinzi,yule mlinzi anaaminika kihivyo,na wengi wanamuamini, ...hakipotei
kitu.
Hakusimama
hadi alipofika kwenye hiyo hoteli, ambapo huyo mlinzi yupo na ofisi yake ya
dharura kama hizo, akaingia, na kuelekea sehemu aliyoagizwa,akafika kwa huyo mlinzi,
na kumsogelea huyo mlinzi.
‘Nina mzigo
wangu wa haraka unatakiwa ufike kwa huyu mtu.....’akasema.
‘Atakuja
mwenyewe au unapelekwa kwake,mbona hakuna anuani ya huyo mtu...?’ akauliza.
‘Atakuja
mwenyewe...’akasema.
‘Unavyofanya hivi ni
hatari, je kama mzigo huu usipofika kwa mlengwa mtakuja kunilaumu, ...halafu nikuulize kuna kitu gani ndani..?’
akauliza
‘Kwani
unahitajika kufahamu ni kitu gani kipo ndani...?’ akauliza
‘Poa, haya nipe utambulisho
wake...na gharama zangu?’ akauliza
Bwana
mzee,akatoa kikaratasi na kumpa huyo mlinzi ,kulikuwa na maneno ya siri, ambayo
mlinzi ataambiwa kabla ya kukabidhi huo mzigo na akatoa ushuru aliotajiwa..
‘Sawa,
lakini tusilaumiane,....muhimu kwenye hii bahasha ni lazima kuwe na anuani ya mpokeaji, ili akija na
kitambulisho inakuwa rahisi kumtambua..haya mzigo umefika,...’akasema na mumemtu huyu akabakia kaduwaa,alitaka kuongea na huyo mlinzi, hakuwa na uhakika jinsi gai huo mzigo utafika kwamlengwa, lakini wenyewe wamedai afanye hivyo, na asiwe na wasiwasi kwa hilo
Na wakati bado kaduwaa yule mlinzi akawa anaendelea na kupokea mizigo ya watu wengine, lakini akawa anasita, na
kabla hajatulia vyema simu yake ya mkononi ikaita
Akapokea kwa
haraka, na kabla hajasema neno akasikia sauti ile inaomnyimaraha ikisema;
‘Unaweza
kuondoka, mzigo
umeshafika...’akaambiwa,hapo akageuka huku na kule kama anaweza kumuona huyo
mtu, kwanza akamtilia mashaka huyo mlinzi, mlinzi alikuwa haongei ni simu, alikuwa akiwa anaongea na watu wanaompa mizigo yao
Akageuka huku na kule kama ataona mtu atakayemtilia mashaka, akiwa kashikilia simu,..lakini walikuwa watu wengi, wanaingia na kutoka, na wengine wanafika kwa
huyo mlinzi na mizigo yao.
‘Umesikia
ondoka eneo hilo,...toka kabisa hadi kwenye gari lako..sisi tunakuona, uavyoshangaa hapo...na usizime simu yakohadi tutakapokuambia, ’akaambiwa.
Hapo akawa
hana ujanja, akatoka nje, huku simu ipo sikioni, alipofika kwenye gari lake akaambiwa.
‘Sasa rudi
nyumbani kwako,...’akaambiwa
‘Na-na enda
kazini...’akasema
‘Fuata
tunavyokuambia....’akaambiwa, na hapo akaendesha gari kuelekea nyumbani kwake, a kabla hajafika akaambiwa;
,
‘Simamisha
gari...’akasimamisha gari, na kutulia, ikisubiria amri nyingine, ikapita nusu saa
hasiki kitu, akaitoa simu sikioni, kuoa kama simu ipo hewani, akakuta mpigaji hayupo hewani
Akatulia kwanza,kwani hajaambiwa afanye nini,...na mara simu yake ikaita akijua ni hao watu akaweka sikioni, alikuwamfanyakazi mwenzake akimuarifu kuwa aje kazini,anahitajika.
Kuona hivyo,akageuza gari lake na kuingia barabara ya kurudi kuelekea kazini, huku akisubiria kama hao watu watampigia simu tena kuwa kakiuka maagizo yao kuwa arudi nyumbani.
*********
Huku nyuma mkewe
akaingia ndani,akachukua kitu alichokifuata, hakuwa na wasiwasi,akili yake
ilikuwa kazi aliyokuwa anaihitajia, kwahiyo alipoiona, hakupoteza muda,
akageuka kutoka, akijua atamkuta mumewe nje, ..
Ni wakati
anatoka ndipo ndipo, akaona kitu, macho hayana pazia,akahisi mumewe kadondosha
nyaraka za ofisini, akainama na kuikota,ili amkimbilie mumewe nje labda ni nyaraka
muhimu,..., lakini alipotoka nje hakumkuta mumewe ,kwani alishaondoka.
‘Mhh,sijui
ni kitu gani hiki, labda wala sio kitu muhimu kwake....’akasema akikagua ile
karatasi, ili kuwa karatasi nyepesi tu
‘Kama ni ya
muhimu,nitampitishia kazini kwake...’akasema akiikunjua vyema,akagundua kuwa ni
bank slip, ya kutolea pesa...
‘Mhh,mumewangu
naye, kadondosha hii bank slip,huenda
ni ya kazini,hajui kuwa ataulizwa...’akasema sasa akikagua maandishi yake.
Kwa haraka
akaangalia kiwango cha pesa
‘Mhh, pesa
yote hii,...itakuwa ni ya kazini kwake...’akasema, huku akiendelea kukagua, cha
ajabu anaona jina la mtoaji,ni mumewe, jina la mwenye dhamana,ni mumewe....hapo
akashituka
‘Inakuwaje
kazini kwake,watumie jina la mumewe,...haiwezekani, au ndio kama alivyosema
kuwa akaunti yake ilikuwa inatumika kuweka pesa za kazini, lakini hapana, sio
kwa kiasi hiki, ....akaona sasa kuna kitu, akikumbuka jinsi alivyomuona mume
wake wakati anaingia...Huwa anamfahamu mume wake,akiwa na wasiwasi,akiwa na
huzuni,....ile hali aliyomkuta nayo,ilionyesha waziwazi mume wake alikua na
wasiwasi, kama mtu aliyefumaniwa
‘Hapa kuna
jambo...’akasema akizidi kuikagua ile nyaraka ya bank (bank slip), na kwa vile alikuwa na haraka, akaona akimbilie kazini,hayo
mengine atayashughulikia badaye,akaondoka na ile nyaraka hadi kazini kwake.
Huyu mke mtu
ofisi yake na kazi anazofanya zinafanana na za benki, ni kamuni
inayojishughulisha na kutoa mikopo na dhamana mbali mbali mbali,na kwahiyo mara kwa mara wanakuwa wakiwasiliana na watu
wa benki kupata uhakiki wa watu
wanaotaka kukopa kwao,...,
Kampuni hii pia
wakitaka taarifa fulani kwa waajiri ili kuhakiki baadhi ya mambo, huwa
wanauliza waajiri hasa pale mkopaji anapoaisnisha kuwa muajiri wake ndiye mdhamini wake,....na kwa vile wanaaminiana, huwa
wanapewa taarifa hizo bila kufichwa.
Basi mkemtu
huyu alipofika kazini na kuhakikisha kuwa keshamaliza kazi zake alizohitajiwa
nazo, na kuzikabidhi kwa bosi wake, akarudi mezani kwake,na kuichukua ile
nyaraka ya bank,( bank slip), akatafuta namba ya mtu kwenye ile bank na
ikawa vizuri kuwa huyo aliyemtafuta wameshawahi kuwasiliana naye mara kwa mara,
akampigia;,
‘Tafadhali,kuna
mtu kaleta hundi ya malipo hapa...nataka kuhakiki tu,kama ana pesa za
kutosha...’akauliza akijitambulisha yeye ni nani
‘Mbona
hujafuata utaratibu...kama kawaida yakompendwa...’akasema huyo mtu wa bank.
‘Ni malipo
ya haraka, na kama unavyojua, hundi hii ikipita mnaweza mkapata hasara na ni hundi
ya benki yenu,..’akasema
‘Unaweza
kunitajia ni nani...?’ akauliza na mke mtu akamtajia akaunti namba,na jina la
mwenye akaunti, na hapo akaambiwa asubiri, baadaye akaambiwa
‘Huyu mtu
akaunti yake ina matatizo kuna nyaraka tunasubiria, ila kama ni malipo yanaweza
kuingizwa tu,je hiyo hundi ni kiasi gani?’ akauliza na mkemtu akijua nini
anachokifanya, akataja kiwango kikubwa zaidi
‘Mhh,
haiwezi kupita hiyo hundi, yeye ana salio dogo,ni dola ....’akataja kiasi
‘Lakini kama
maandishi hapa,alikuwa na dola za kutosha....’akasema lakini hakutaja kiasi
‘Ni kweli alikuwa na kiwango, cha kutosha,
kabla hajachukua pesa leo,katoka kutoa pesa kiasi,...na kupunguza salio lake,
inabidi tusubirie mwisho wa mwezi huu,sio mbali, akiweka pesa nyingine, huenda
ikafikia hicho kiasi...’akasema
‘Je akiweka
kiwango hicho anachoweka kitatosha...?’ akauliza huyo mke
‘Ndio kitatosha
maana kila mwezi anaweka dola kama..eeh,...’akataja kiwango
‘Na pia
kilamwezi kuna pesa kutoka kazini kwake, mshahara wake unapitia kwenye hii
akaunti yake, na ukiingia huwa anakuja kuchukua nusu ya mshahara kila mwezi,...pesa
tasilimu...’akasema na maelezo hayo yalimtosha mke mtu kujua ukweli alioutaka,
‘Mhh, huyu
mwanamume ananizunguka, kumbe ana akaunti yake binafsi,na pesa anazodai kila
mwezi kumbe anakuja kuzihifadhi kwenye hii akaunti, na mshahara wake kumbe mkubwa
mara mbili ya huo anaoufahamu yeye,...na zaidi, ..hizi pesa nyingi alizotoa
anapeleka wapi...’akawa anajiuliza, huku akiwa kashikilia ile karatasi ya
kutolea pesa, hakuna maelezo kuwa anamlipa mtu.
‘Kwanza
inabidi niongee naye kabla sijawasiliana na wazazi wangu,najua nikiongea na
wazazi wangu watakimbilia kubaya,...nilishawaambia wazazi wangu mume huyu
waniachie mwenyewe, japo walishasema sio mwaminifu...’akawa anaongea peke
‘Kwanza hizi
simu za usiku zilikuwa za nini...?’ akawa anajiuliza kwani kuna muda usiku alisikia
simu ya mezani na mumewe akatoka na kwenda kuongelea varandani, na akarudi na
baadaye simu ikapigwa tena...akatoka, na alitoka karibu mara nne...
Usiku ule
alipoona simu zimezidi kwa mume akashindwa kuvumilia, akainuka kitandani na kumfuatilia
nyuma.., na ndipo akasikia mume akisema
‘Kwahiyo
mnataka nini..?’ akauliza
‘Nilishawaambia
pesa ni nyingi sana, ni mpaka niende benki....’akasema na akageuka na kuona
mkewe akiwa kasimama mlangoni, akajibaragua na kusema
‘Sawa lakini
sio kosa langu ni tatizo la umeme, nikienda benki nitawalipa....’akasema
Kwa vile
mkewe anafahamu kuwa mumewe ni fundi wa umeme,akajua ni maswala ya kikazi,
huenda kuna tatizo la umeme mahali,na huwa inatokea,..basi akapitiliza, na
kujifanya anakwenda jikoni, baadaye akarudi, na kumkuta mumewe amelala
Sasa leo
akiunganisha haya matukio,...akahisi kuna jambo..huenda linatokana na ile
simu,huenda,kuna jambo mume wake hataki yeye kulifahamu, na kiwango cha pesa
kwenye hiyo akaunti yake kikamtia mashaka,
*********
‘Sasa
nifanyeje..ili niweze kuupata ukweli wote....’akawa anajiuliza,
‘Kwanza ni
kuhakikisha mwenendo mzima wa hiyo akaunti...’akasema na kumigia tena huyo
jamaa aliyempigia mwanzoni, alijua cha kusema, na taarifa aliyoipata ikwamka
uhakika kuwa akaunti hiyo kweli ni ya mume wake,na pesa zilizopo sio kweli kuwa
ni za kazini,ni pesa mume wake, alikwua akiweka.
‘Akaunti hii
imekuwa ya kuweka tu, ...kila mwezi anaeka pesa bila kuhukua kitu, hadi alipotaka
kutoa karibu pesa yote, lakini kutokana na kutokukamilisha baadhi ya nyaraka,
ikabidi apewe pesa kidogo tu....’akaambiwa
‘Pesa
kidogo...! ‘akasema na alipokumbuka kuwa anachohitaji ni kutaka uhakiki, sio
kuelezea, hisia zake, akasema
‘Basi
nashukuru sana, hiyo itanisaidia kuona kama kweli anastahiki kupewa huo mkopo
alioomba.....’akasema na kukata simu, huku akitizama ile nyaraka ya benki ya
kutoa pesa, akijiuliza wapi pesa hiyo mume waka kaipeleka, na mara akakumbuka
kitu, akainua simu na kuongea na mtu anayemfahamu;
‘Habari yako
mhasibu...mimi ni mfanyakazi wa benki binafsi ya kukopesha, nilikuwa nataka
kupata taarifa za mmoja wa wafanyakazi wenu aliyekuja kutaka mkopo hapa kwetu,
naomba msaada wako tafadhali na iwe ni siri....’akasema
‘Hamna shida
, nitakusaidia tu, naweza kujua jina la huyo mfanyakazi....?’ akauliza na
akataja jina la mume wake
‘Mhh, hatuna
barua yoyote ya huyo mfanyakazi ya kutaka uthibitisho, au kudhaminiwa na
kampuni kwa ajili ya kuchukua mkopo kwenye kampuni yenu..labda ni mkopo binafsi
tu.’akasema
‘Nilitaka
kujua kama kampuni inamdai, ..au ana deni lolote ili tuweze kutathimini kiasi
alichotaka kukopa, kwani hapa kaelezea kuwa anahitaji pesa kwa ajili ya kulipia
deni analodaiwa na kampuni...’akasema
‘Deni, .....Mhh,
kwakweli sijui, ..huyu mtu hana deni lolote kwetu, huenda ana maana yake,
unaonaje ukiwapigia simu utawala...’akasema
‘Unauhakika hajaandikiwa deni kwa sababu ya uharibifu wa vifaa vya kazi kutokana na uzembe
alioufanya yeye, na kusababisha uharibifu mkubwa ...kutokana na umeme...?’ akauliza.
‘Kutokana na umeme,....mmh, sijui..lakini hapa kwetu hana deni kabisa ....hajawahi kukopa au kuandikiwa deni, na kampuni
haiwezi kumuandikia mtu deni kwasababu ya uharibifu wa kikazi. Mhh mimi hapo
sielewi...’akasema huyo mhasibu
‘Na huo uharibifu
ulitokea lini, haijawahi kutokea tatizo lolote la umeme,...na sijawahi kuona
kitu kama hicho, hata hivyo huyu mfanyakazi ni mtaalamu sana wa umeme, hawezi
kufanya uzembe wa kusababisha hasara, ndio maana nakushauri uongee na
utawala....’akasema mhasibu
‘Pia kwenye
barua hpa naona kaainisha kuwa alikuwa anapokea pesa za kampuni kwa niaba, na
kuziweka kwa jina lake, na wakati anakuja kuziweka benki akaibiwa pesa nyingi
tu, ina maana nyie mna utaratibu wa wafanyakazi kupokea pesa na kuweka kwenye
akaunti zao binafsi...?’ akauliza
‘Haijawahi
kutokea, hakuna kitu kama hicho, pesa ya kampuni inapitia moja kwa moja kwenye
akaunti za kampuni, na malipo yote yapitia idara ya uhasibu, mtu kama huyu hana
mamlaka ya kupokea pesa ya kampuni...labda kasema hivyo kwa minajili ya kupata
mkopo, lakini kampuni haijawahi kupokea pesa kupitia kwa mtu, hususani yeye....’akasema
‘Basi hamna
shida, ...kama ni lazima nitaongea na utawala, nimekuuliza tu kupata uhakika,
sio kwamba hatutaki kumpa mkopo, nashukuru kwa msaada wako...’akasema na kukata
simu.
Mke mtu huyu
akawa haamini, ina maana mume wake amefiki hatua ya kumdanganya kiasi hicho,
akasimama, ....akakaa...akaangalia muda ,muda wa kutoka kazini bado.
‘Mume wangu
ananidanganya, ...kwa hili, sizani kama nitavumilia, ina maana ni
kweli...walivyosema wazazi wangu kuwa huyu mtu sio mwaminifu, ina maana tabia
za kifamilia zinaweza kurithiwa, kuwa wazazi wake sio waaminifu hata mtoto
atakuwa hivyo hivyo..hapana...sikubali...’akajikuta akiongea peke yake
‘Kwanza
lazima nimbane nijue ukweli....nataka ukweli wote, na ikibidi kama atanificha, nitamtumia mchunguzi....'akasema
'Nahisi kuna kitu.., ni lazima hii akaunti yake idhibitiwe kama zilivyo akaunti
nyingine....'akawa anazidi kuwaza
'Na naona sasa ni wakati muafaka wakupitia makubaliano yetu ya ndoa
na vitega uchumi vyetu, huyu mtu siwezi kumuamini tena kihivyo..., yaani namtetea nambeba,
lakini habebeki, hapana....’akasema na kuinua simu yake
‘Halloh,nataka
kuongea na wakili,..ndio wakili wa familia yangu....’akasema akijitambulisha kuwa
yeye ni nani.....
Siku hiyo
hakuchelewa kuondoka kama ilivyokuwa kawaida yake, akaondoka mapema kabisa
kuwahi nyumbani,.
WAZO LA LEO: Tukumbuke kuwa wanandoa ni kitu kimoja,
ni vyema kama wanandoa mkawa mnaaminiana, mnapanga mambo yenu kwa pamoja hasa
wale mnaofanya kazi, na hata kama mmoja anafanya kazi na mwingine hafanyi,
lakini inapendeza mara kwa mara mkifanya hivyo. Tabia ya kufichanafichana
baadhi ya mambo, inachangia kuyumbisha ndoa yenu, na hilo linaonyesha kuwa kuaminiana
kwenu ni kudogo,,...na kwa hali kama hiyo mnamkaribisha ibilisi kuvuruga ndoa
yenu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment