‘Pole sana profesa hayo ndiyo malipo ya mtu
kama wewe,
‘Lakini vipi maisha ya kijana wako, uliyemtengeneza wewe mwenyewe maana
kaharibikia mikononi mwako, hebu
tuambie,unasema ameshaoa mwanamke, tena mwanamke wa kizungu..., je maisha yake yapoje...na
vipi anatarajia kurudi huku kwao tena..?’ akaulizwa
Maisha ya kijana hadi kuoa kwake, au
jinsi alivyokutana na huyo bibiye chanzo ilikuwa ni mimi..undani wake
alivyokubaliana naye yeye mwenyewe akiwa hapa mtakuja kumuuliza....’akasema
‘Kwahiyo atarudi nchini, ...?’
akaulizwa
‘Ndio ni lazima arudi maana huko sio
kwake, japokuwa keshapata kazi,...’akasema
‘Haya hebu tuambie ilikuwaje, maana
unasema wewe ndiye uliyemfanyia mpango wa kumpata huyo binti wa
kizungu....’akaambiwa
Tuendelee na
kisa chetu
**********
‘Tuliandoka
hapa kwa shinikizo kama mnakumbuka, ilikuwa sina jinsi, na ...ilibidi ili niwahi
kupata mafao kutoka kwa wafadhili, kwani kama ningelimuachie aende peke yake,
ile dhamana ya kuwa mimi ni mlezi wake ingeliondoka...’akaanza kusimuliza
profesa
‘Tulipofika huko kijana aliendelea na masomo yake kama
kawaida, kidarasani alikuwa akijitahidi kwa kweli...na ilikuwa kila mwisho wa
wiki anakuja hapo ninapokaa, na sikuacha kmshauri sana kuwa analofanya la
kuwakataa wazazi sio jambo jema, ...’
‘Unajua hata
mimi sikupenda hilo, ndio maana ilifika muda nikajaribu hata kumuelewesha jisi
gani nilivyompata akiwa katikati ya msitu akitaka kuliwa na wanyama wakali,
lakini sikupenda kumuonyesha huo ushahidi nilijua unaweza kumfanya akawachukua
wazazi wake kabisa.
‘This is not true I will nevet believe this
...’ akasema na kweli hakuamini hayo, yeye alishikilia hivyo, kuwa yeye ni
yatima na hana wazazi...
‘Basi
nikasema ngoja nione mwisho wake huenda akabadilika, lakini kiukweli kila siku
ilivyokwenda ndio alizidi kujiona kuwa yeye ni mtoto asiye wahi kuwa na
wazazi..,na hata mimi ni kama mpita njia tu niliyejitolea kwake, ...
‘Nilipoona
ananikasirikia na mimi, ikabidi sasa niachane naye katika ushauri maana niliona
anaweza hata kukataa kuja kwangu, na hapo nitaonekana kuwa mimi sio mlezi wake
kama nilivyoahidi, na tulikwenda hivyo hivyo mpaka akafikia muda wa yeye kuanza
kazi na alipewa kipaumbele na wale wale wafadhili katika kutafutiwa kazi
‘Tutamchukua
huyu kijana afanye kazi kwenye moja ya kampuni zetu....’siku hiyo nikaambiwa na
mmoja wa wafadhili nilipoona hakuna kinachoingia kwenye akaunti yangu ya benki
‘Kwahiyo
hakuna fedha yoyote ya kusaidia, maana nilikuwa na mambo yake mengi
nafuatilia..’nikajaribu kujitetea
‘Mambo kama
yapi, maana matibabu, na jinsi ya kuishi atakuwa sasa analipwa kutokana na
mshahara wake, ...sisi tunaona hahitaji mtu wa kumsaidia tena, tumeshaongea
naye na amesema anajimudu..na zaidi alisema hakuwa anapata hivyo unavyodai kuwa
wewe ulikuwa ukimfanyia...’wakasema
‘Sio kweli,
unajua huyo ni mtoto, na watoto wanataka kila kitu uwape, nilijitahidi kama
mzazi kuhakikisha anapata kile kinachostahiki....’nikajitetea hivyo
‘Sisi kama
wafadhili wake tutalifanyia uchunguzi,
na tukiona kuwa kweli wewe ulikuwa ukimtendea kinyume na makubaliano,
tutahakikisha sheria inachukua mondo wake...’wakasema na hapo nikaanza
kushituka, maana kiukweli nilikuwa nikitumia pesa zake kwa kiasi kikubwa kwa mambo
yangu, na sikuwa namfahamisha huyo kijana kuwa kuna pesa nazipata kwa ajili
yake.
Siku hiyo
nikamtafuta kijana wetu ili nimuweke sawa, akubali kuwa nilikuwa nikimsaidia,
lakini pia nilitumia muda huo kumshauri, kuwa sasa hivi sipati pesa zake kwa
ajili ya mahitajio yake, kwahiyo akipata kazi asinisahau maana biashara zangu
hazilipi tena....
‘Dad, siamini kuwa ulikuwa ukipata pesa
kwa ajili yangu, mbona nimekuwa nikiishia maisha ya shida, kila nikikuambia
nahitajia hiki au kile unasema huna pesa, ...na kumbe ulikuwa ukipewa pesa kwa
ajili yangu...’akasema akionyesha kunikasirikia
‘Unasikia
mimi kama mzazi nilitakiwa nihakikishe sikupi pesa ovyo , nilijua kwa tabia
yako itaharibika nilikulea kama mtoto wa nyumbani, ili ujue maisha jinsi
yalivyo...’nikamwambia hivyo
‘Kwa vile
mimi ni yatima au sio , ...sina baba , na sina mama, hata walezi ndio nyie
mnapewa pesa zangu mnazitumia wenyewe, sitakuamini kamwe, na sasa nitajitegemea
mwenyewe, sihitaji msaada wako, nimeongea nao nimewaambia nitaweza kujimudu,
haina haja ya wao kukutumia pesa tena kwa ajili yangu, labda wakupe tu kama
kukusaidia wewe....’akaniambia
‘Sikiliza
kijana wewe bado ni mdogo sana...., usijione kuwa umepata kazi ndio ujione kuwa
unaweza kujimudu, unahitaji mtu mzima kama mimi wa kukuongoza, ..unajua wewe ni
muafrika, hata kama unaishi huku, unatakiwa ujue maisha ya kikwenu, huko nyumbani
maisha ni magumu, unatakiwa uwakumbuke wazazi wako,..ndio maana nilitaka
nikujenge kihivyo....’nikamwambia
‘Sina
uhakika na hilo... sizani kama ulikuwa ukiwatumia ndigu zako pesa yangu...ila
kwa mahesabu niliyopewa na hao waliokuwa wakinifadhili, ningeliweza kuishi
maisha mazuri tu....lakini hakuna shida, ulichotumia kinatosha, na sihitaji
chochote kutoka kwako zaidi, na kwahiyo hatudaiani, nitawaambia ulikuwa
ukinisaidia haina shida, ila kuanzia sasa mimi na wewe basi...kwaheri...’akasema
na kutaka kuondoka
‘Mimi na
wewe basi kivipi, ....Kwaheri kivipi, huoni nahitajika kulipia pesa ya kodi ya
nyumba, nitapatia wapi pesa,
usiponisadia..umesikia nimekuambia hao wafadhili hawaingizi pesa tena kwenye akaunti
yako, sina pesa, nitaishije...na mimi nimefanya haya yote kwa ajili yako...’nikamwambia
na yeye akaniangalia kwa dharau.
‘Kijana ana
dharau...hata sijui kama utaweza kuishi naye bila kukwaruzana, anajiona na
uafrika kwake ni kama bahati mbaya...’akasema
‘Lakini yote
si umeyafanya wewe kumuharibu...’akasema kaka mtu
‘Mhh,
hapana...nilifanaya kile nilichoona ni sahihi kwa muda huo,sikujua kuwa atakuja
kubadilika hivyo...’akasema
‘Mhh, sasa
mkamalizana na yeye vipi, alikubalia kukusaidia, kulipia kodi ya nyumba?’
akaulizwa
‘Hakunisaidia,a
lichosema kilikatisha tamaa, akasema;
‘Wewe rudi
nyumbani kwenu..kama ulikuwa unaishi kwa mgongo wangu, ujue sasa mimi naishi
kwa kujitegemea,ninaweza kujimudu mwenyewe, sihitaji msaada wako, nina mshahara
wangu na maisha yangu, nimeshapata sehemu ya kuishi, nzuri tu....’akaniambia
‘Basi
nitakuja tuishi sote maana hapa napo wananizingua, ni wapi nije ..nitamwambia
huyu mwenye nyumba siishi tea hapa natoa notice ya kuondoka..kwanza alishanipa
notice ...’nikasema na yeye akaniangalia kwa madharau akasema
‘Ninaishi
kwenye sehemu yangu mwenyewe, sihitajii kuishia na mtu, labda nikioa nitaweza
kuishi na mke wangu, na nikioa siwezi kuishi hapo nipoishi sasa hivi nitatafuta
sehemu yenye nafasi, nina mahesau yangu, ya kunitosha mwenyewe....’akasema
‘Mhh, kijana
usisahau kuwa mimi ndiye niliyekufikisha hapa, hutakiwi kunitupa
hivyo...’nikamwambia
‘But,
...umeshatumia pesa yangu nyingi, ...na ukumbuke hatukuwa na mkataba wowote kuwa nikipata kazi
nikusaidie..au kuna mkataba kama huo, nikawaulize hao wafadhil...?’ akaniuliza
akijua kuwa hakuna kitu kama hicho, na kabla sijajbu akasema
‘Kiukweli
hakuna mkataba kama huo,.. wewe ulitumia ujanja ujanja tu...dad, whoever you are...nakushauri
utafute njia nyingine ya kuishi, usitegemee tena kupitia mgongo wangu, maana hao watu wamesema hawatakuingizia pesa
tena, na ...mimi siwezi kukusaidia, nitakachokukusaidia ni kuwaambia kuwa kweli
ulikuwa ukinisaidia, basi yaishe mengine, ..samahani sana....’akasema na
hakupotea muza akaondoka.
‘You...son...a....’nikataka kumtukana
lakini alishaondoka.
‘Ulitaka
kumtukanaje wakati kosa ni lako, cha mjanja huliwa na mwerevu zaidi
yake,...umeonaeeh, na maisha hayo ya ujanja ujanja matokeo ndio hayo...’akasema
kaka mtu
‘Sawa kaka,
...kuna mengi yalitokea hapo....ila katika kuhangaika nikafanikiwa kufanya kazi
kwa majumba ya watu kama niivyosema kazi za ovyo weli, na siku moja nikapata
kazi kwa mama mmoja wa kiafrika aliyeolewa na mzungu, mama huyo tukaivana,
akaniamini kupitiliza...
Wao
walibahatika kumpata binti mkubwa tu, lakini ukimuangalia huyo binti , sura
yake na wao haviendani kabisa,...nikajua hapa kuna namna..kawaida kila nikipata
sehemu kazi yangu kubwa nikuchunguza maisha yao,...nilitafiti familia hiyo
nikagundua kuna kitu kisicho sahihi....
‘Sasa maisha
ya watu yanakuhusu nini...?’ kaka yake akauliza
‘Hahaha,
bro....maisha hayo, niliishi nayo sana, hasa nilipokuwa sina kazi, nilikuja
kufundishwa na washikaji fulani, ambao huishi kwa maisha hayo....’akasema
‘Mhh,....tabia
mbaya sana hiyo...’akasema kaka mtu
‘Kwa vile
hiyo familai waliniamini sana, niliweza hadi kuingia ndani, na kama hawapo
natafuta kila kona, kuona kama kuna kitu kitanisaidia, hawakujua kuwa
wameingiza nyoka ndani...’akasema
‘Maisha hayo
nilifundishwa bro, ukiwa ulaya usipokuwa mjanja unaweza kufa njaa huku watu
wanakuangalia tu, kial mtu na bajeti yake...watu wanakula wanasaza lakini
hawawezi kumkumbuka mwenye njaa,....
‘Nilishakutana
na kundi la mitaani,ambao huishi kwa utapeli, nilishapanga mipango nao mingi
mmojawapo ni huo ..kuwa kila nipofanya kazi kwa watu nachunguza zile tabia
ambazo zinaweza kuwaumbua, ...kama wanandoa kusalitiana, mambo ya siri ambayo
hawataki yagundulikane....
Nilikuja
kugundua kuwa binti yao huyo hawakuwa wamezaa pamoja, huyo mwanamke hakuwa na
kizazi, wakapandikiza mbegu , na kumpata huyo binti, niligundua hilo kwenye
kumbukumbu zao...nikaona sasa hapa ninaweza kufanya jambo
‘Jambo gani,
kwani hayo yanakuhusu nini...?’ akasema kaka yake
‘Bro, wewe
sikiliza, ...nikuonyeshe maisha niliyopitia, usinione ivi bro, nimeteseka sana,
hadi kufikia kufanya hivyo, niliwahi kukaa siku mbili, sina kitu cha
kula....hebu fikiria njaa inavyouma, nikafika kwa kijana akanifukuza kama
mwizi....’
‘Ndio
nikaanza kuhangaika, ...nilipoligundua hilo, kuwa familia hiyo ina mtoto wa
bandia, na wakati wao walishaniambia walimzaa kihalali, nikajua kuna jambo..
‘Hilo
nilologundua sikuwaambia kundi langu, nilichofanya ni kutafuta simu za mitaani ,
siku hiyo nikiwa nimejipanga nikabadili sauti, ..najua kubadili sauti za kila
namna,....nikawapigia hawa watu wenye mtoto wa kupandikiza,
‘Haloh,,....mimi
ni mchunguzi huru wa magaeziti ya udaku,
katika kufuatilia kumbukumbu zangu nimegundua kuwa nyie hamna mtoto halali
...’nikawaambia
‘Nani
kakuambia hatuna mtoto halali na una maana gai kusema mtoto halali..?’ akaniuliza
huyo mama, nilifurahia kuwa aliyepokea hiyo simu ni huyo mama mwenyewe, maana
nilipiga simu ya ndani
‘Nyie huyo
mtoto mumempata kwa kupandikiza uzazi....,’nikamwambia
‘Eti
nini,....ok, sasa hata kama ni kweli, japokuwa sio kweli inakuhusu nini....?’ akaniuliza
‘Kwasababu
kwenye kumbukumbu zenu inanyesha mumezaa kihalali, na kunamambo ambayo
mumeficha ukweli....’nikasema
‘Hata kama
ni hivyo inakuhusu nini..kuna kosa gani tumefanya?’ wakauliza
‘Je binti
yenu analifahamu hilo...?’ nikauliza nilishapanga kuwa huo uwe ndio mtego
wangu, na niliposema hivyo, nikasikia mama akihema kwa mshituko.
‘Hata kama
hafahamu inakuhusu nini wewe,...?’ akauliza...mwanzoni mama huyo
alijifanya
hajali, lakini kwa uzoefu wangu nikagundua hilo la kumuambia binti ya limemusa
kwani niliwahi kuongea naye alisema kama kuna kitu ambachoo hataki kukifanya
..ni kumuuzi binti yake anampenda sana..kwahiyo aliposikia kauli hiyo, alihisi
vibaya sana.
‘Basi mimi
nitamwambia binti yenu tuone kama hatawachukia nyie kwa kitendo hicho...unakumbuka
watoto kama hao wanavyokuwa wengine huweza hata kujiua...na wengine wanaachana
na wazazi wao kabisa...’nikawaambia
‘Kwahiyo
unahitajia nini kwetu...ni nini lengo lako?’ akaniuliza
‘Ili
nihakikishe kuwa siri hiyo haivuji, na binti haipati hiyo taarifa, inabidi
mlipe gharama fulani...kama dola elifu kumi tu...sitaki pesa nyingi....’nikasema
‘Wewe unaota
hizo pesa sisi tutazipatia wapi, wakati kipato chetu ni shida....’akasema
‘Nataka hizo
elifu kumi haraka...zingine nitajua jinsi gani ya kuwapunguzia...vinginevyo
nitamwambia huyo binti yenu kila kitu kuwa nyie mlimpataje huyo binti.....’nikawaambia,
na kukata simu
Watu kama
hao hutakiwi kuwapa muda, mengine yanakuja yenyewe, nikakaa siku mbili,
ukumbuke kuwa mimi nafanya kazi humo,na nilishaweka mitego yangu, kila
kinachoendelea humo ndani nakifahamu, mama alionekana hana raha kabisa, na
niliona kuwa hakuwahi kumuambia mume wake,
‘Mbona huna
raha...?’ nikamuuliza
‘Nani,mimi...aah,
ni mamb yangu tu..ni mambo ya kimaisha, ni..maisha magumu tu..’akaniambia
‘Kama kuna
tatizo niambie, mimi kuishi mitaani ninajuana na watu wengi tu, ....najua mambo
mengi tu....’nikamwambia
‘Hakuna
tatizo, na kama lipo nitalimaliza mwenyewe sihitaji msaada wako...’akaniambia,
na niliposikia hivyo nikajua kuwa kunahitajika shinikizo, ndio siku hiyo
nikatafuta sehemu nyingine nikampigia simu
‘Nataka hizo
pesa umpelekee yule jamaa wa kasino jirani yako, mlinzi wewe umkabidhi na
bahasha, mimi nitajua jinsi gani ya kuzipata, vinginevyo, leo nitakutana na
binti yako, ni siani kama utafurahia nikimwambia yote nina kumbkumbu zako sote....’nikamwambia
‘Sina hizo
pesa...sijazipata bado nazitafuta....’akasema, nilishajua kuwa ana pesa
alishakusanya, japokuwa hazikufikia hivyo, hakujua anayempigia simu ni nani,..
‘Wewe una
kiasi gani?’ nikamuuliza
‘Nusu
yake...’akasema
‘Nataka
kumi, fanya haraka usinitanie...kwanza kuna mashindani ya watoto kuwaonyesha wazazi wao vipaji vyao,
hapo hapo nikimwambia najua atawachukia sana nyie wazazi wake...,sizani kama
atafurahia kuwaona nyie kama sio wazazi wake...’nikamwambia na mama huyoo
alioekana hana raha, hata nilipofika kazini, nilimuona kanyong’onyea
‘Kuna mzigo
nataka umpelekee yule mtu wa kasino, yule mlinzi wao anayefanya kazi ya kupokea
mizigo ya watu na kuifikisha anapoelekezwa..., lakini nataka iwe siri, nataka
uchunguze baadaye ni nani atakuja kuzichukua kwa huyo mlinzi...’akaniambia
‘Mhh, mama
naona kumbe kuna tatizo kwanini usiniambie ni tatizo gani ili niweze kukusaidia,...’nikasema
‘Sikiliza
hakuna tatizo, nataka hiyo bahasha usije kuifungua, nitakufuatilia kwa nyuma,
hakikisha inafika kwa huyo mtu...’akaniambia, basi mimi nikaongea na huyo
mlinzi, namfahamu sana, kazi yake mojawapo ni hiyo kupokea mizigo ya watuu kwa
ajili ya kuwapa watu wengine...anatambulikana na huwezi kumshitakia,,...
‘Basi mimi
nikafanya kama nilivyoambiwa, nikamkabidhi huo mzigo, na nikarudi kwa huyo
mama, nilikuta hayupo, nikajua anachunguza ni nanii atakuja kwa huyo mlinzi, na
huyo mlinzi nilishapanga naye wapi nikachukue huo mzigo,...haikuwa shida kwake
kwani ni kazi yake..., nikaupokea,..hahaha nikajua sasa huyu mama kaingia
kwenye anga zangu....
Kesho yake
nikafika kwa huyo mama, nilimkuta hana raha kama kawaida yake, nikamuuliza
majibu yakawa ni yale yale, mwisho akaniuliza
‘Hivi yule
mlinzi nikiongea naye hawezi kuniambia ni nani aliyempelekea huo mzigo, hata nikimpa kitu kidogo...?’
akaniuliza
‘Mhh, mimi
sijui,...lakini kama kazi yake ni hiyo ya kupokea mizigo kwa mtu fulani na
kupeleka kwa mtu mwingine sijui kama atakuwa na kumbukumbu ya watu wote,...’nikasema
‘Nilikuambia
ufuatilie ujue wapi kaupeleka huo mzigo...’akaniambia
‘Mimi
nilijaribu kumfuatilia, nikakuta ana watu wengi wamempa mizigo na akizitoa
inakuwa kwa siri kubwa,...sasa ungeniambia ni nani unamshuku au kuna tatizo
gani ingelikuwa ni rahisi kwangu kuweza kusaidia...’nikamwambia
‘Mimi ni
mtoto wa mjini, ....nimetokea huko huko, hanijui huyo mtu, utakuja kuona jinsi
gani nitakavyo mnasa, si amekula pesa yangu hiyo, lakini atakuja
kuirejesha...tena kwa malipo makubwa sana, ya maumivu...’akasema
Mimi
sikujali maana ukiwa katika shughuli kama hizo, moyo unaota sugu, na kwa vile
nilikuwa naye sambamba, sikuwa na wasiwasi, basi tukakaa hadi mwezi ukaisha ,
kulikuwa na tukio fulani shuleni kwa mtoto wake, la wazazi kukutana shuleni, na
hapo tena nikaona kuna haja ya kupata pesa, nikampigia simu
‘Ni wewe
tena, unajua unanitafuta ubaya, nitakuja kukuumiza ...’akasema
‘Kwani kuna
tatizo, nilisema ili niweze kulimaliza hilo nahitajia kumi kumi kila mwezi,kwa
miezi mitatu, ulitoa nane badala ya kumi, unadaiwa mbili, na kumi za mwezi huu,
mimi nitajua jinsi gani ya kulifuta hilo, maana sipo peke yangu
nitawanyamazishaje wenzangu...’akasema
‘Sikiliza
hupati pesa yangu yoyote safari hii, nenda kokote,...’akasema
‘Leo ni siku
ya wazazi, muulize binti yako aliongea na nani, na alihidiwa kupewa siri
gani....?’ nikamwambia, nilishampigia huyo binti kwa siri, na kumwambia nina
siri kubwa kutoka kwa wazazi, sikutaka kumuambia zaidi, nikasema
‘Ni nani
wewe mbona sikujui....?’ akasema huyo binti kwenye simu
‘Wazazi wako
wananifahamu sana,...’nikasema
‘Siri gani
wataka kuniambia?’ akaniuliza
‘Nitakupa
siri hiyo siku ya sherehe ya wazazi...’nikasema na kukata simu, nilijua ni
lazima huyo binti atamwambia mama yake kwani walikuwa karibu sana..na kweli
nilipoongea na huyo mama akaonyesha kuogopa zaidi akajua kumbe kweli niliongea
na binti yake, akasema
‘I will kill you....ipo siku nitakunasa,
utalia machozi ya damu...utanijua mimi nilitokea wapi...’akasema na kweli siku
ile akapeleka elifu tisa, nikaona sio haba...
‘Unajua maisha
yangu yalikuwa hivyo, kwangu mimi sikuwa nataka mapesa mengi,..hizo hizo elifu
tisa, nane, kuna siku alitoa hadi elifu kumi na tano, nilimtega kubaya, nilijua
ana pesa, nikampigia na hapo hapo nilishaongea na binti kwa siri..siku hiyo
alijua kabisa siri itajulikaa akatoa kumi tano..
‘Kuna namna
nyingi nilitumia kumtoa pesa huyo mama, hakujua kuwa ,mimi nilikuwa nafuatilia,
nyendo zake, lini ana pesa, na lini naweza kumtoa, na inakuwa vigumu kwake
kushindwa kunikatalia,..akawa ni mteja wangu, pamoja na wengine, na maisha
yakawa yanakwenda.....
Baadaye huyo
mama akamshirikisha mume wake, mume wake alikuwa mjanja sana,...wakaanza
uchunguzi wakatafuta mpelelezi wa kujitegemea kunisaka mimi, lakini hawakujua
kuwa nyoka wao yumo humo humo ndani...
Mwanzoni
walishindwa,, lakni walipotafuta mpelelezi, mpelelezi akaja kuwashitua kuwa
inawezakana mbaya wao atakuwa humo humo ndani kwani kwanini kila wanachopanga
kinajulikana,....ghafla wakaamua kunisimamisha kazi
‘Ndugu sisi
tuna matatizo makubwa,...hatutaweza kukulipa tena, kwahiyo tunakuomba utafute
kazi sehemu nyingine...’siku hiyo wakaniambia, nikajua huenda wameshanihisi
..lakini sikuwa na njia ya kujitetea nikaachana nao,....
Nikawa nina
shida ya pesa, na hapo ilikuwa ni sehemu yangu ya kunikoa, nikashindwa nifanye
nini,...nikaona nitafute njia nyingine, nikaona labda nipitie kwa binti yao, ili kupata
taarifa za hapo nyumbani, kwahiyo kila mara nikajitahidi kukutana na binti yao,
na weli alinizoea sana kwa vile nilikuwa karibu naye nikiwa hapo nyumbani,
hakuweza kugundua lengo langu....
‘Kwahiyo
huyo binti yao, ukataka akupe siri za hapo nyumbani kwao, wewe weli ni
shetani...’akauliza kaka mtu
‘Bro wewe
tulia, nikuonyeshe nilivyoishi ulaya kipindi hichoo cha shida...maisha yana
fundisha mengi,...hapo ndipo nikagundua kuwa kijana wako alikuwa akimtamani
huyo binti, kumbe alishaniona nikiwa sambamba na huyo binti, na kuna siku alikutana
nami nikiwa na huyo binti baadaye akaja kunipigia simu
‘Dad, nimekuona na binti mmoja
unamafahamu anapotokea?’ akaniuliza
‘Leo
unaniita dad, si ulisema hunitambui tena
mimi kama baba yako...’nikasema
‘Ninakuuliza
tu...hamna shida, akakata simu, na nikajua sasa hapa naweza kufanya jambo,
nikamtafuta kijana na kumueleza kuwa kama anamtaka huyo binti mimi nitamfanyia
mipango, muhimu tu anijali..haikuwa shida, kijana alishazimia kwa huyo binti,
akakiri kuwa kweli angelifurahi kuwa na urafiki na huyo binti
‘So how much...utanilipa mimi...?’
nikamuuliza
‘Kukulipa
nini dad, hiyo inahitajia mimi nikulipe,...wewe unatakiwa kunielekeza wapi
nionane naye, na ....’akasema
‘Oooh, hujui
kuwa mimi nipo karibu sana na huyo binti, na naweza kukurahisishia hiyo
kazi.....’nikasema
‘Nitakupa
kiasi,....sina pesa kwa sasa...’akasema
‘Wewe ni kijana
wangu, hata kama hunitaki, nipe kiasi tu,...lakini ujue kuwa nahitajia kumhonga
huyo binti ili aweze kuachana na wazazi
wake,wazazi wake ni wakali sana, wanamlinda sana binti yao...’nikamwambia,
kwahiyo nikapata mwanya wa kupata vijisenti, kutoka kwa kijana, akawa ananipa
pesa, na zawadi, ili nimpelekee huyo binti
Yule binti
yao nilishazoeana naye, nikawa nimefanya mipango ya kuwakutanisha na kijana
wetu,na kweli wakaja kukutana na wakaivana, na kuwa wapenzi wa kweli, nikaona
hapo hapo pia naweza kutumia mbinu zangu na kuzidi kupata chochote kutoka kwa wazazi wake...,
Nikawa
namdadisi huyo binti kuhusu familia yao sasa wapoje, wazazi wana matatizo gani
, naongea naye kama mtu wa karibu, na binti akawa ananielezea yale
yanayoendelea ndani ya familia kama mtu aliyekuwa anawajali...
Nilipojaribu
kupiga simu na kuwataka wanilipe kama ilivyokuwa awali, nikakuta wananijibu kwa
dhihaka;
‘You again, ...sasa tukumekufahamu kuwa
wewe ni nani, utajuta kuzaliwa...’akasema huyo mama
‘Hata
mkinijua haisaidii kitu, muhimu ni kunipa hiyo pesa haraka iwezekanavyo...kwani
binti yenu nipo naye kila siku naongea naye na nimeshamuahidi kumuelezea kila
kitu kuhusu wazazi wake...’nikawaambia, lakini pesa haikuletwa na kesho yake,
nikajikuta nipo uso kwa uso na huyo mama, akaniambia;
‘Nina
maongezi na wewe....’akasema
‘Kuhusu
kazi, kama ni kazi msubiri hadi wiki ijayo...sasa hivi sina nafasi...’
nikajifanya kuringa, kumbe moyoni nilikuwa na wasiwasi kweli
‘Ni kuhusu
malipo yako ya kila mwezi ya elifu kumi....’akasema huku akiniangalia usoni, na
aliposema hivyo nikajua sasa nimeshapatikana, lakini nikajifanya sielewi
anachoongea nikasema
‘Malipo gani
ya elifu kumi....?’ nikamuuliza kwa wasiwasi
‘Unafikiri
wewe ni mjanja sana, ..unajiona wewe una akili sana, umekuwa ukiishi nasi huku
ukituchunguza,...na kuanza kutuibia, hizo elifu kumi kumi, utazilipa kwa
maumivu makali sana, utajua kuwa mimi ni nani....’akasema akiniangalia kwa
macho ambayo sijawahi kuyaona, yalionyesha ukatili ndani yake.
Nilikuja
kugundua kuwa mama huyu alikuwa mmoja wa watu wakatili sana, katika usichana
wake, alipitia uhuni wote, na ndipo alipoharibikiwa na kizazi, aliwahi kuwa
mitaani na kujiunga na vikundi vya kijambazi, na katika kundi lake alikuwa
mmoja wa watesaji, alikuwa na nguvu zaidi ya midume,...kwahiyo alikuwa
akijulikana na wahuni wahuni, baadaye akatulia na kuingia kwenye ndoa...
‘Mbona sijui
unaongea nini...’nikasema nikifanya nashangaa kwa maneno yake
‘Nimeshagundua
kuwa wewe ndiye uliyekuwa ukitu-blackmail....’akaniambia
akiniangalia kwa uso wa chuki.
‘What...! Mimi..hapana, siwezi kuwafanyia
kitu kama hicho..’nikajitetea
NB:Naishia hapa
kwa leo....tuzidi kuombeana heri
WAZO LA LEO: Wakati mwingine wenye makosa
wanahitajia muda, na namna ya kuwarekebisha, wakati mwingine makosa hayo
yanatokana na uelewi na malezi waliyoyapitia, au kutokana tu na ushawishi wa makundi rika,
ulevi, nk...na sababu nyingine za kijamii a wakipata mongozo wanaweza kubadilika na kuwa
watu wema kabisa.
Sasa ni,
muhimu kwa mzazi, mlezi na yule mwenye dhamana ni kuchukua muda, na kutafuta
mbinu za kuwaelimisha hawa watu na sio tu kukikimbilia kuwaadhibu kwa kifungo,
au kufukuza kazi, au kuwalaani kuwa hawafai katika jamii,...au wengine
hukimbilia kuwatesa, au hata kuwaua, tutakuwa hatujatenda haki, ni muhimu kuwe
na hatua za kurekebisha hawa watu, kwani tunaweza kuharibu kabisa badala ya
kutengeneza.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment