Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, June 15, 2015

RADHI YA WAZAZI-4



Ilikuwa ni kijiji kingine profesa akiwa na kijana wake walifika kwenye kiunga cha makazi ya familia mojawapo kwenye hicho kijiji, na wakapiga hodi, lakini kulikuwa kimia kama vile hakuna watu, yawezekana wakazi wa hapo walikuwa mashambani kama alivyofikiria huyu profesa

Dad, lets go back, ...there is no life here....wewe huoni wamehama, hakuna mtu hapa, ...you see dad,.... mtu anawezaje kuishi mahali kama hapa....’akasema kijana akikagua kwa macho mazingira ya eneo hilo.

‘Mhh, kijana, kua uone...hapa ndipo ulipozaliwa, nikuambie kitu hapa ndipo unatakiwa uonyeshe adabu zako...humu,  ndipo mama yako anapoishi ndiye aliyekubeba miezi tisa tumboni, sasa ukitaka uharibikiwe, cheza na mama yako....’akaambiwa.

I don’t know, whoever ...mom, or dad, mimi sioni tofauti,...mimi najua kuwa mimi ni yatima, ulisema wakati nasoma, mimi ni yatima, sasa unanielezea haya, mimi sikuelewi...halafu hao wazazi, mbona hawaelekei kuwa ni wazazi wangu, hatufanani kabisa na wao...hapana, unataka kunitia majaribuni...am very sory, I  I don’t like them...’akaongea yule kijana, ni mwepesi wa lugha tu.

‘Unaona Kiswahili chako sasa kinaanza kuwa safi...thats how I want you to be, like me, nafahamu lugha nyingi tu...na hatimaye utakuwa mswahili, utakuwa mtanzania halisi, unasikia wewe sasa ni msomi, maana unajua kiingereza, nchi msomi ni yule anayejua lugha, hasa kiingereza, unaona, ukimaliza shule huko nje unakuja hapa nchini kwako, unakuwa mkurugenzi,....but you have to promise me one thing....’akaambiwa lakini alionyesha kama kupotezewa muda wake, akasema;

‘Sitaki kabisa ....i don’t like to be mswahili.....my language is English, na there....,  is where I belong...nitarudi huko nilipokuwa nasoma na sitarudi huku tena....’akasema. Na profesa akamuangalia kwa makini halafu akasema;

This is your country boy, whether you like it or not, unasikia huku ndio kwenu, huko ulaya ulikwenda kusoma tu....sasa sikiliza....’akasema yule profesa na yule kijana akawa katulia tu.

‘Sikiliza nataka uniahidi kitu kimoja, kuwa utafanya ninavyokuelekeza,...kama nilivyokuelekeza,...wewe hutaki pikipiki....sasa sikiliza ukiwa huko nje,  huko wewe ni yatima, tulifanya hivyo ili upate elimu, ni ujanja, ndio maisha yetu, ujanja ujanja....’akasema na kijana akanyosha mkono wa kuyapuuza hayo.

‘Ndio hivyo, kama nisingelifanya hivyo ungesoma wewe, ona hapa ndipo ulipozaliwa, ungewezaje kufika ulaya..hebu tumia akili yako,....sasa muhimu,  ukirudi hapa hasa eneo hili, unahitajika uwatambue wazazi wako, japo .....’kabla hajamaliza akasikia mtu akikohoa nyuma yao, wote kwa pamoja wakageuka kuangalia.

Alkuwa ni mama mmoja akiwa kashika fimbo, kwa jinsi anavyotembea, ilionyesha dhahiri haoni, ila anatumia fimbo kama kiongozi wake, na kwa muda ule alikuwa akija muelekeo wao,...na kwa mbali kulikuwa na watu wengine wanakuja, yule mama alipokaribia pale waliposimama, ghafla akatulia, akasimama, na wale watu walikuwa mbalia wakawa wamemkaribia,

‘Kuna wageni, .....au wamepotea njia...’sauti ya wale watu wengine ikasikika ikisema

‘Mhh, wanatoka wapi hawa watu..yule kama mzungu-koko.....’sauti ya mwanamke ikasema, ni kweli huyo profesa, alifuga nywele akazitegeneza ki namna, akazifunga kwa nyuma, huwa ana nywele ndefu na kwa vile alikuwa mweupe, wengi walimuona kama ana damu ya mchanganyiko.

Wale watu wengine wakawa wamafikia huyo mama, na sasa wanawaangalia hawa wageni waliosimama kwenye njia ya kuingilia kwao, wakajua  hao watu yawezekana ni wageni wao, na kabla hawajatoa kauli ya kukaribisha au salamu, yule mama aliyekuwa kashika fimbo akatamka maneno yaliyowafanya wote kuduwaa.

‘Nahisi ishara ya mwanangu...nahisi.....mwanangu amekuja....mwanangu,umekuja mwanagu....’huyo mama akasema na sasa akawa anakuja muelekeo wa pale aliposimama huyo kijana, na huyo kijana kwanza alishikwa na butwaa, lakini alipoona yule mama anamkaribia akamkwepa.

Kwa muda ule wale watu wengine walikuwa wameshafika karibu na hao wageni, wamesimama, walkuwa akina mama wawili na mzee mmoja mwanaume, na wao wakawa wameduwaa kuona kile kitendo kinavyoendelea pale

Who is this dad....is she ok, ....she is blind...whats she wants from m......’akasema yule kijana akionyesha wasiwasi.

‘Mhh, she might be  your mother....’akaambiwa

What.....i can’t believe this....’akasema huyu kijana sasa akiwa kasimama mbali na yule mama, akawa anamuangalia kwa uso uliojaa mshangao.

Do what I told you....’akaambiwa na ile sauti ya profesa ilimfanya yule kijana sasa asimama, huku akionyesha hali ya wasiwasi akimuangalia huyo mama kwa tahadhari, na yule mama akamsogolea, na kunyosha mkono wake had ikashika kichwani mwa huyo kijana.

Yule kijana akamuagalia profesa akitaka kufanya jambo , hakupeda kabisa hicho kitendo anachofanya huyo mama, aliona kama anachafuliwa nywele zake, lakinii akaona ishara kutoka kwa profesa kuwa atulia, na yule mama akaanza kumpapasa ule kijana kichwani na mkono ulianzia kichwani, na ukawa unashuka hadi usoni,na kijana yule alionekana kama anasikia vibaya, lakini akawa anafuata alivyoelekezwa na profesa.

‘Oh mwanangu, umekuja,..nilijua tu kuwa upo hai...umekuwa mkubwa kiasi hiki, masikini....nisamehe mama yako, yaliyotokea siku ile sio matakwa yangu, sikupenda kukuacha uchukuliwa....’akasema huyo mama.

Yule kijana hakuvumilia tena, taratibu akaushika mkono wa huyo mama na kuondoa mwilini mwake,....akasogea mbali na huyo mama, akionyesha hali ya kutahayari, na huyo mama akasema;

‘Mwanangu, umerudi mwanangu.....nisogelee mwanangu, leo nilikuwa nahisi utakuja,.....ila leo sijisikii vizuri...naogopa hali mbaya yaweza kunitokea, lile balaa liloanya nikupoteze, oh, oh,....’akasema huyo mama, na haikuchukua muda kweli huyo mama akaanza kutetemeshwa na kabla ndugu zake hawajamfikia kumshika akadodoka chini, na kuanza kutikisika a kama kujinyonga nyonga.. na haikupita muda akawa anatoa mapofu mdomoni

Yule kijana kuona vile, hakusibiri cha profesa wala cha nani, akatimua mbio, na kupotelea msituni, na profesa, ambaye alikuwa akimuangalia yule mama, hakujali kumuangalia yule kijana alivyokuwa akikimbia...yeye kwa haraka akamsogelea huyo mama, pale alipolala, akatoa dawa zake alizokuja nazo;

‘Mnaweza kunipatia maji ya uvugu vugu, kama yapo, kama hakuna nipeni maji tu ya kawaida...’akasema na mama mmojawapo akafanya hivyo, akamletea huyo profesa maji, na yule profesa akatoa dawa ya unga unga, achanganya na maji, halafu akasema;

‘Nisaidieni tumpe dawa hii itamsaidia, atapona...’akasema  huyo ptrofesa na wale watu wakamsaidia kumuiua huyo mama, na kupanua mdomo wake na huyo mama akapewa hiyo dawa, akanywa, na haikupita muda, huyo mama, akainuka , kwanza akawa anashangaa, na kuuliza;

‘Kumetokea nini...? ‘ akauliza na alipoona watu wamemzingira, akaiamisha kichwa a baadaye akasema

‘Ooh, ni huu mtihani tena, ooh, mungu wangu lini nitaachana na hii adhabu,....eeh muu wangu, naomba uichukue tu roho yangu nisizidi kuadhirika hivi, maana nikidondka sijijui, sijui.....kinachoendelea, mungu wangu nakuomba...nakuomba... nimechoka kutaabika na kuadhirika, ...’akawa kainamisha kichwa chini akilia na mama yake akamsogelea na kumshika mgongoni akasema

‘Mwanangu usiseme hivyo, utapona tu,...mbona sisi tupo pamoja na wewe, huu ni ugonjwa utapita, na utasahau...’akasema mama yake akiwa kama na yeye anataka kulia

‘Mama lini nitapona,....wewe mwenyewe unaona miaka mingapi sasa nateseka....mume kaniacha kwasababu hii hii, mtoto naye.....ooh mungu wangu nina nini tena katika hii dunia, nimeshaadhirika, nimeshadhalilika, na walimwengu wameshanidharau, na kunipuuza....nimekuwa mgumba, kipofu, na hili gonjwa lisilo na dawa.....jamani....na....’ghafla akatulia akageuza kichwa kuangalia huku na kule, japo kuwa haoni, lakini alikuwa kama anatafuta kitu.

‘Mwanangu yupo wapi...?’ akauliza akigeuka huku na kule

‘Mwanangu yupo wapi huyo ndiye burudiko la moyo wangu kabla sijakata tamaa ya mwisho, kabla sijafariki, nataka mwanangu awe karibu yangu, mwanangu yupo wapi, nimemuhisi, nimemgusa kwa mikono yangu mwenyewe....’akasema, na profesa akawa anaweka dawa zake kwenye mkoba, akauliza

‘Ina maana huyu mama haoni....?’ akauliza profesa

‘Ndio ...alipoteza uwezo wa kuona kutokana na kukaa ndani akiomboleza kupotelewa na mtoto wake....’akasema mama mmojawapo

‘Haiwezekani....ina maana upofu huo umetokana na kupotea kwa mtoto wake, kwani hamna uhakika kuwa mtoto wake yupo hai, kwanini aomboleze wakati huenda, au ana uhakika gani kuwa mtoto wake keshafariki...’akasema profesa

‘Mtoto wangu hajafariki,.....nina uhakika....alikuwa hapa muda mfupi uliopita...’akasema yule mama mgonjwa kwa hasira, na wote wakatulia, na aliyevunja huo ukimia alikuwa mama wa huyo mama mgonjwa,akasema;

‘Mtoto wako yupo wapi, tumeshakuambia sahau hilo usimkufuru mungu... miaka mingapi imeshapita, karibu kumi na sita au kumi na saba sasa, kwa muda wote huo kama yupo hai, yupo wapi,...’akasema huyo mama

‘Mhh, na nahisi ...’profesa akawa anaonyesha kwa vitendo kuwa huenda huyo mama kachanganyikiwa

‘Kiukweli imekuwa kama hivyo, ....kaomboleza kupita kiasi, yeye anadai kuwa ana uhakika mtoto wake yupo hai....sisi tumeshakata tamaa, na tunajua kuwa hueda keshafariki....’akasema na kabla hajaendelea kuongea kuongea, yule baba mzee, akasema

‘Hebu tuambie, unafahamu lolote kuhusu mtoto wa huyu mama?’ akauliza huyo baba mzee

‘Yaonekana kama una jambo lakutuambia...tuambie wewe, kama unafahamu lolote, maana kiukweli kupotea kwa mjukuu wangu imekuwa pigo kubwa kwetu, ni miaka mingi, lakini hata mimi naendelea kumuota, mara namuona, lakini nikimuita ananikimbia, anasema hanijui, hebu tuambie una lolote la kutuambia, ....?’ akauliza mzee aliekuwa kaongozana na hao akina mama, kumbe huyo ndiye baba wa huyo mama mwenye matatizo

Profesa akageuka kuangalia kule alipokimbilia yule kijana alijua yupo sehemu kajificha, lakini hakutaka kumfuata akasema;

‘Mhh, kwakweli sina la kuwaambia, na sijui lolote kuhusu huyo mjukuu wako..., lakini ngoja ipo siku nitakuja  mtanielezea vizuri, nitaona jinsi gani ya kusaidia....leo sina muda wa mangezi, leo nilikuja kuleta dawa za huyo mgonjwa....., tutaongea siku hiyo...,’akasema

‘Tunashukuru, ....’akasema mama wa huyo mama mgonjwa

‘Matumizi yake, ..ni dawa ya unga, kijiko kimoja kwenye maji ya moto..uvuguvugu, kumpa huyu mama mgonjwa,  kila siku asubuhi kabla hajala kitu na akilala kwa siku saba mfululizo bila kukosa..zitamsaidia, ni dawa nzuri za matatizo kama hayo...’akasema

‘Na yule kijana aliyekimbia ni nani?’ akauliza mmojawapo wa hao akina mama.

‘Mhh, ni kijana wangu tu.....’akasema profesa akikwepa kuangalia na hao watu

‘Na wewe ni nani mbona sikukumbuki....ni mgeni kabisa machoni mwangu....?’ akauliza huyo mzee mwanaume

‘Mhh, ...labda, .....ila mimi naitwa ...eeh, wananiita profesa...’akasema

‘Profesa, ndio jina lako hasa...mimi namfahamu mtu mmoja kwa jina hilo, alipewa hili jina kutokana na kufanya mazingaumbwe, ...mmh anatokea kule alipokuwa kaolewa huyu binti yangu, na tulisikia huyo mtu alikamatwa na madawa ya kulevya huko uchina akanyongwa...’akasema, na profesa akatikisa kichwa na kusema

‘Mhh, mimi sijui...haya jamani kwaherini, mimi nilikuja niliposikia huyu mama anaumwa,...na kwa vile ni mtu ninayemfahamu, nikaona nimsaidie...sihitaji malipo yoyote kwasasa, kama atapoa, mtafikiria cha kunipa, najua atapona...niwaulize tu kitu kimoja...’akatulia

‘Wewe umetokea wapi....?’ akaulizwa na yule mama mwingine

‘Je kwenye historia zenu, kuna mtu alikuwa anaumwa, yaani, baba zenu, babu..mliwahi kusikia ugonjwa kama huo kwenye familia zenu...?’ akauliza profesa

‘Hakua hata mmoja, ugonjwa huu umetokea huko huko kwa mume wake...’akasema mama mtu

‘Basi atapona.....kwa hivi sasa naomba niondoke, si mnaona kijana wangu kakimbia,..anaogopa, ...tutaongea nikija tena...na kuangalia hali ya monjwa...’akasema akigeuka kuondoka, akamtupia yule mama mgonjwa jicho, na yule mama kwa muda huo alikuwa kasimama akiwa kaelekeza uso wake kule alipokimbilia huyo kijana na huyo mama akasema;

‘Wewe mtu, nashukuru kwa dawa zako, lakini umlete mtoto wangu, najua ni wewe uliyemchukua...’akasema huyo mama kwa sauti nzito yenye msisitizo na ukali, na profesa akashituka kidogo, akataka kusimama, .... lakini akasita na kuendelea na safari yake, akaondoka akielekea kule alipoelekea yule kijana wake.


WAZO LA LEO: Kuna watu wanahisi maisha ya ujanja ujanja, kudanganya na kupata hata kisicho halali yao kiujanja ujanja , na wengine hufikia kusema ni mungu kapanga iwe hivyo,..au ni elimu, au ni ujasiri, ...na wengine wanafikia hata kujenga kutajirika kwa hali hiyo. Huo sio ujanja, hiyo si elimu, huo ni wizi...hiyo ni dhuluma, na utakuja kuulizwa kwa hao wote uliowatendea hivyo ukapata kwa kupitia migongo yao, hilo deni mbele ya mungu.
Ni mimi: emu-three

No comments :