Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, June 30, 2015

RADHI YA WAZAZI-13


‘Kuna kazi moja, ikifanikiwa utaingiza ,dola laki moja na elifu hamsini,kama kianzio unazipata bila ubishi, na hapo ushanilipa ushuru wangu....
‘Na kila mwezi kama kawaida utapata elifu hamsini, kwa miezi kama mitatu,...au hata thelathini, ukimuhurumia,...na hushuki zaidi ya hapo,...mimi unanipa zangu kumi kumi kila mwezi kwa miezi hiyo mwili,zaidi ya hapo sitaki, kwangu zinatosha ....’akasema akijizungusha kwenye kiti chake.
‘Unaona ilivyo,...baada ya mikupuo mitatu, wakati bado anahaha,....unampa unafuu, mimi naachana na wewe, unabakia wewe na mwenye kisima,maana si umeshamfahamu, nazimamitamb yangu, unafanya vitu vyako,ukitaka....mpaka utakapohakikisha kisima kimekauka, ni wewe tu na njaa zako...’akawa anasikia mtaalamu akiongea kichwani mwake.
‘Dola lakini na hamsini, kianzio tu,na badoo kila mwezi nakinga mkono..ohooo,mungu anipe nini...’profesa akawa anawaza akielekea sehemu alipoelekezwa...
Tuendelee na kisa chetu
***********
Ni kweli sikutarajia kuwa kazi hiyo itakuwa rahisi hivyo,mtu niliyeelekezwa kwake kweli alionekana kuwa ni mgeni, na alionekana kuipenda familia yake..., ila pamoja na hayo alionekana kutamani mabinti, kwa jinsi alivyoonekana hakutulia, ilikuwa ni swala la kumtega tu...
Tabia hiyo ya kuoenakana kupenda mabinti, ilioenakana wazi,na mabinti wakawa wanamchangamkia wakitaka kumpukutisha alicho nacho mfukoni, lakini walisema jamaani bakhili kutoa kilicho mfukoni ni mgumu sana,...
Lakini kwa watalaamu wa kusoma watu kama hao, wakaona kuna njia nyingine ya kumtoa hizo pesa alizo nazo,...,na kwa vile anaonekana mwingi wa mabinti, na kupenda kunywa, wajanja wakaona watumie udhaifu wake huo.
Ndipo mtaalamu akamchunguza na kugundua kuwa huyo jamaa anaingilika, na kwa uzoefu wake wa watu kama hao, ni rahisi sana kuingizwa kwenye mtego, na akajikuta anatoa pesa nyingi tu bila kupenda...
Mtaalamu alinielekeza jinsi gani ya kufanya, na yeye alishakwenda mbali zaidi hadi kujua jamaa ana kiasi gani benki, na matumizi yake kwa siku, na jinsi gani alivyo mbele ya familia yake, na tabia yake na familia yake...
‘Hii familia ina pesa,benk wana akiba kubwa tu, ya pamoja, na kila mmoja pia ana amana yake binafsi kuacha hiyo ya pamoja, ya mke ipo wazi inajulikana kwa mume,...
‘Na huko kwao, wanapotoka, wana miradi, na mingi inatokana na familia ya mke,...mke yeye alisomea huku ulaya, na akarudi kwao kufanya kazi,baadaye akakutana na huyo mwanaume, wakapendana wakaoana,lakini familia ya mume ni ya kimasikini tu...
‘Kwahiyo utaona jinsi gani mke alivyo na nguvu, sio tu kwasababu ya taratibu zao, lakini pia kipesa..na kuoana kwao ni kutokana na mapenzi yao wawili, familia ya mke hakupendezewa binti yao kuolewa na familia ya kimasikini, lakini binti alishapenda,....unaona ilivyo....’akasema  mtaalamu
‘Basi mume akawezeshwa, akasomeshwa zaidi, wakawekezewa, wakajijenga,..hata hivyo kwa vile binti kasomea ulaya, akaona aje huku ili wawe mbali na familia, na kufanyia kazi huku...kalowea ulaya
‘Basi binti, akaomba kazi huku akapata kazi,..na kwa mgongo wa binti,na mume naye akapata kazi...sasa mdondo wetu ni mume...huyu ndiye mlango wa kuipata hiyo hazina,hazina waliyoihifadhi, ..’akasema mtaalamu akijilamba lamba na ulimi.
‘Ipo wapi amana yao,....?’ profesa akauliza
‘Amana zao zote ni za kimataifa kokote wanaweza kuchukua,na mume ana uwezo wa kutoa pesa hata bila kumshirikisha mkewe,...ila kwa upendo na ushirikiano,kila akitoa pesa nyingi, wanafanya hivyo baada ya makubaliano...’akasema
‘Sasa atawezeje kutoa laki na hamsini, kwa mkupuoa...?’ akauliza profesa akionyesha hamasa
‘Mume ana akaunti yake binafsi, ambayo hata mke hajui,...humo ana dola nyingi tu, humo anaweza kutoa hata dola laki moja kwa mkupuoa, na akiongezea kwa mkewe, itafika na lakini na hamsini,...sijui kwanini hiyo amana yake  hajamuhusisha mkewe, japokuwa ya mkewe anaifahamu...tunahisi anamuibia mkewe na kuwekeza huko ili kukitokea lolote aweze kuwa na kianzio...’akasema mtalaamu.
‘Unahisi hajiamini,hampendi mkewe..wanaishi kwasababu ya mali tu.....?’ akaulizwa
‘Unajua kuna kitu nikuambie,mapenzi yapo ya namna nyingi, kuna ya pesa na kuna ya kiasili, kuna yanakuja tu, ...hawa kwa kiasi kikubwa ni pesa, na mke,....’akasema profesa
‘Na kosa kwa mke, yeye, ...karizika, na kajiweka tu, kajaziana...unaona alivyo nenepa, sasa bwana,mmmh,kaona vimwana wa huku ulaya, virika njia,..., si unajua vimwana wa huku wanavyojua kuweka miili yao,....kavutika, hana jinsi,...anatamani,...japo anajifanya hamnazo...siri kubwa,  awali ni awali,tusimchelewe,akijanjaruka atakuwa makini sana,siomjinga kihivyo...’akasema
‘Kama ni hivyo eeh, haina shida...’akasema profesa
‘Sasa kwanza la muhimu ujenge ukaribu na hiyo familia, ili mitego ukikamilika ujue jinsi gai ya kumtisha,...si unajua....kama ulivyo cheza na mama, hahaha, japokuwa hujaniambia,....’akasema
‘Mama yupi...mbona sikuelewi,....’profesa akasema
‘Ulicheza vizuri sana, nimeipenda hiyo,ila umechezea kubaya..tuyaache hayo,mimi hayanihusu...kabisa, muhimu ni hii kazi,...hii itakufanya upate ...’akasema mtalaamu.
‘Mhh, hii kazi nitaifanya, na huna haja ya kunifundisha zaidi, nishajua ni nini cha kufanya...’akasema profesa
‘Najau utaiweza, ndio maana nikakutafuta wew,...’ akasema huyo mtaalamu
‘Jinsi alivyo huyu mwanaume, hana ubavu wa kuhimili vitisho,hasa ukivilenga kwenye ndoa....fanya mbinu uwazoee,na ili jamaa akianza kuhaha, wewe uwe sambamba na yeye,ujifanye mshauri wake mkuu,...’akaambiwa
‘Mbinu ni hiyo hiyo, unauma huku unapulizia ...na kwa vile hawajazoeana na watu, wewe watakuona mtu muhimu kwao, jifaye jirani mwema, au utafute kazi kwao, hilo nakuachia wewe....muhimu, wasijue lengo lako....’akaambiwa profesa
‘Hiyo kazi ndogo kwangu, ...kama pesa ipo , utaona vumbi langu,...’akasema profesa
‘Ndio maana nikupa kazi hiyo, ila uwe makini,...maana huyo mtu anamiliki bastola,na anajua kuitumia vyema..na akikasirika anaweza kuivuta kiwashio na risasi ikatoka bila kutarajia....’akasema na hapo moyo ukanilipuka, bastola....!
*********
Kwa vila ni mgeni nikajua kabisa hatapenda wageni, hasa wa kufanya kazi nyumbani, lakini cha ajabu nikaweza kupata kazi..na hata kuvipata vyote nilivyohitajia, maana ugeni na ushamba uliwaponza.
‘Kwa vipi?’ akauliza kaka mtu akiwa na hamasa ya kutakakujua zaidi
‘Bro,..japo uwa ni dhambi,najua hilo,lakini...mungu anisamehe, ujanja ujanja wa kuwaingia watu, ninao.....’akasema mdogo mtu
‘Mhh,ulifanyaje ukawaingia watu kama hao...?’ kaka mtu akazidi kuuliza.
‘Mtu kama huyo unamwendea kinamna, nliona ili niweze kupata ninachokitaka ni muhimu niwepo karibu nao, kwahiyo kwanza kabisa nilifika nikijionyesha kuwa nina shida, nahitaji kazi za ndani,
‘Sisi hatujui wenyeji, na kweli tulikuwa tunahitajia mtu wa kazi....’akasema.
‘Basi msiwe na wasiwasi, ulizia watu wote, wananifahamu nimewahi kufanya akzi sehemu nyingi, tu, msiwe na shaka kabisa na kama mnahitajia uhakika mnaweza kuulizia mtu wa seriali za mitaa.....’profesa akasema.
‘Hamna shaka,tutakupa kazi,lakini...usije kutudanganya...’wakasema
Na kweli nikapewa kazi ya kulimia bustani,na kufanya usafi wa maeneoya nje,kwasiku mbili tu nikaweza kuifahamu familia yote,na jinsi gani wanavyotoka
Walikuwa na mlinzi,lakini mlinzi mwenyewe ni wale wa kufunga na kufungua mlango hakuwa na utaalamu hasa wa kuwasoma watu,na mimi nikaweza kuingia ndani wakati  wenyewe hawapo na kutafuta kila ninachokihitajia,..hiyo haikuwa kazi ngumu kwangu,nikajua maisha yao,kiundani zaidi
Nilikuwa mcheshi sana kwa mama mwenye nyumba, na akanizoea mapema kuliko baba mwenye nyumba....na kwa vila nilikuwa naifahamu fahamu lugha yao,..hahaha, bro usinione naitwa profesa, mimi kwa lugha ni mkali,nikikaa na mtu akawa anaongea lugha yao,haichukui muda kujifunza
Nikawa nimeshakusanya kila kitu muhimu, sasa ikabakia kumjua huyo mama jinsi gani anavyompenda mume wake, mapenzi yao ya ndani,wanaaminiana vipi,haikuchukua muda,nikajua....
Mume kwa nje alionekana mtu wa heshima zake, lakini cha ajabu akifika kwa mke wake hana usemi,...kuna mila na desturi za watu, msione hapa bongo waume ni wakali kwa wake zao,  kuna sehemu inakuwa kinyume, ....huyu jamaa na ujanja wote wa nje, lakini akifika kwa mkewe ni goigoi, anaogopa sana kumuuzi mke wake...hapo nikanyosha dole kwani hilo lilikuwa muhimu sana
Ama kwa mke,mke hakuonekana kujali sana,alionekana kumuamini mumewe kwa kiasi kikubwa,kwahiyo hakuwa na muda wa kumfuatilia nyuma, yeye akirudi kazini,anakuwa na kazi yake ya kufuma vitambaa, ni mtaalamu kweli wa kufuma vitambaa.
‘Mme wako ni mwaminifu sana, ...’siku hiyo nikamchokoza
‘Ndio.....!  Kwanini unasema hivyo?’ akaniuliza,na alishanizoea kwa uchesi wangu
‘Namuona tu,na nyie ndoa yenu inaonyesha ina raha sana watu wanawaonea wivu sana hapa mitaani...’nikaanza kumchimba
‘Ni kawaida tu,mimi sioni tofauti,muhimu kila mmoja anajali maisha yake na kujali umihimu wa ndoa, na kwanini wanionee wivu, sio kweli...’akasema
‘Mhh,najiuliza mfano..nasemea tu,mfano umkute mume wako na mwanamke mwingine utamfanyaje...?’ nikamuuliza, akaacha kufuma kitambaa na kuniangalia akatikisa kichwa.
‘Aaah,kwanini unasema hivyo...mimi siwezi kumfikiria vibaya mume wangu maana tunaaminiana...’akasema na mimi nikawa nakata kata maua ambayo niliyachuma kwa ajili ya kupambia ndani
‘Ni mfano tu,si tunaongea tu...usinifikiria vibaya, unajua ukikutana na watu unajifunza mila na desturi zao,huenda nikaja kuoa huko kwenu...’nikasema
‘Kuoa kwetu,...ina maana hujaoa...?’ akaniuliza akionyesha mshangao
‘Naweza kuoa tena kwani ubaya....’nikasema
‘Uliuliza swali gani vile...?’ akasema akishika kitambaa chake
‘Niliuliza hivi,mfano ukagundua kuwa mume wako ana mke mwengine wa nje, sio lazima awe wa moja kwa moja, ukamfuma ....utafanyaje...?’ nikamuuliza na hapo akaweka chini kitambaa, akainama kama anawaza jambo,halafu akasema;
‘Weeeh,kama ni kweli...hahaha,...sijui kama nitamsamehe...atajuta kunioa, lakini mume wangu namuamini, tunaaminiana...kwahiyo siwezi kufikiria kitu kama hicho...’akasema
‘Mhh,ni kweli,lakini yeye si kakuoa,huwezi kusema nimpe talaka au tuachane,au sio....maana mwisho wa siku wewe mwanamke utakosa, utakwenda kwenu...sijui kwenu ipoje....’nikasema
‘Ndoa yetu ni ya kimila zaidi,sisi wanawake ndio tunatoa mahari,kwahiyo naweza kumuacha mume....,na ni kimuacha anakuwa hapati kitu....anarudi kuwa masikini ...’akasema huku akionyesha kutukupendelea kuliongelea hilo.
‘Mhh,...mila zenu ni tofauti kidogo na za kwetu,naona zinampa nguvu sana mwanamke...’nikamwambia
‘Ndio ni mila na desturi zetu,ndio maana sisi wanawake hatuna mashaka dhidi ya wanaume wetu,....mwanaume anatakiwa kujichunga kweli..ni kweli pamoja na hayo mwanaume ni mwanaume,yeye ni kiongozi wa familia,kwahiyo anatakiwa kulijua hilo....’akasema
‘Nimeipenda hiyo,...maana huna haja ya kuhangaika na mume wako, ...weweukirudi ni nyumbani tu,lakini mume yeye anapitia kupata kinywaji,huoni kuwa hiyo inaweza kuwa kishawishi, atakutana na wanawake, na hujui tabia za wanawake wa huku, wanaweza kumshawishi...huliogopi hilo,...wivu kidogo eeh?’nikamuuliza
‘Kunywa ni jadi ya wanaume wa kwetu,na wakinywa ni lazima kuwa na watu wa kuongea naye,wanaweza hata kuwa ni wanawake,muhimu ni kuchunga masharti ya ndoa,..kuongea ni swala jingine,lakini asije akavuka mipaka...’akasema huyo mke wake
‘Utakuwa na uhakika gani, kuwa unalinda mipaka ya ndoa...?’ nikamuuliza na hapo akanitupia jicho la udadisi
‘Kwanza hebu nikuulize wewe mke wako yupoje,maana wewe ni mdadisi sana....?’ akaniuliza
‘Yupo nyumbani, huko kwetu afrika...mimi huku nimekuja kutafuta maisha ...’profesa akasema
‘Sasa wewe unamwamini vipi mke wako huko alipo, maana swali kama hilo unatakiwa ujiulize na mwenyewe kabla ya kuuliza wenzako....?’ akaniuliza
‘Huko anaishi na ndugu zangu,wanahakikisha havunji miiko ya ndoa,hakuna shida kabisa...’profesa akasema
‘Na wewe huku atakuaminiaje maana na huko kuongea kwako yaonekana hujatulia..’akasema
‘Sisi wanaume huwa hawafuatiliwi sana, naweza nikawa na nyumba ndogo nyingi tu,siulizwi,muhimu mke wangu apate mahitajia yote muhimu....’profesa akasema
‘Nyie mnawanyanyasa sana wanawake wenu,hamna haki sawa kama ni hivyo, sisi hilo halipo,mume ni lazima atii ndoa yake, akikosea cha moto atakiona....’akasema na hapo moyoni nikasema mambo si hayo
 Sikuwahi sana kuongea na mume wake, lakini siku moja nilipata muda wa kuongea naye, na aliniambia jambo
‘Mimi naipenda sana familia yangu,sipendi kabisa kumuuzi mke wangu,nahakikisha nipo safi mbele yake...na sipendi mtu kuja kuiharibu ndoa yangu...’akasema
‘Lakini wewe nakuona mmmh,kama vile unapenda nyumba ndogo...?’ nikamuuliza kwa utani
‘Nyumba ndogo,! ..una maana gani, hahaha hapana bhana...ni kuongea tu,..ulishawahi kunioana nikiongea na wale akina dada, nawatania tu,...yah, kuna muda unatamani...lakini wee, namuogopa sana mkewangu,najua akifahamu nitakuwa na hali ngumu,...sipendi kabisa kumuuzi mke wangu na familia yangu...’akasema
‘Pale kwenye bar unapokunywa kuna wasichana warembo sana mke wako akifahamu,  au akija kukuona unavyotaniana nao, mhh, atajisikia vibaya,  hatafurahia kwakweli...’nikasema akageuka kuangalia kule alipokuwa mkewe halafu akasema;
‘Mke wangu anajua nakunywa pale, lakini ananiamini sana, naongea tu,sifanyia mabaya,ananifahamu nilivyo, nikinywa naongea sana, utani kidogo, lakini wee, hapana chezea ndoa yangu...’akajitetea
‘Mhh,mimi kwa ushauri wangu, pale sio mahali pazuri kwa mtu kama wewe unayependa familia yako,ipo siku utapitiwa, na itakuwa ni hatari, si unajua tena, mke wako anavyokupenda....’nikamwambia kama kumshauri
‘Pale pazuri sana,napoteza mawazo ya kazi,mabinti wanajua kuwafurahisha wateja,...hata hivyo nakuwa makini,.hata nikilewa,sivunji masharti ya ndoa yangu...wakati mhh, unahisi ...unajua eeh, ...,lakini nafikiria mara mbili tatu,faida na hasara yake,basi naondoka mapema, ...’akasema
Moyoni nilimuambia sasa wewe umekwisha nilichokitaka nimekipata,ni swala lakuingia kwenye anga zangu tu...lakini bro, sikio kila mkaa kimia hajui kusema...
‘Kweli wewe ni shetani...’akasema kaka mtu akiwa kama anaangalia sinema kichwani mwake,kumhusu mdogo wake.

‘Hahaha bro....bado hujasikia mambo yenyewe...., subiri nikuonyeshe maisha ya mlungula, wenyewe huko wanaita blackmail 


WAZO LA LEO: Heshima ni kitu cha bure,kama muungwana unahitajika kujiweka jinsi jamii inavyotaka, huwezi kujiweka tofauti eti kwa vile wewe umatokea nje, ukaiga watu wa nje wanavyofanya, jamii nyingine wanavofanya, ukatembea nusu uchi, au ukafanya vitu kinyume na jamii ililivyo, eti kwa vile...utaonekana ni kioja,ndio maana wanasema ukifika kwa wenye chongo, na wewe fumba lako jicho.
Ni mimi: emu-three

No comments :