‘Kiukweli kama nilikuwa sijasikia
sifa za huyu mama kutoka kwa huyo mlinzi mkusanya mizigo nisingeliogopa vitisho
kama hivyo, vitisho kama hivyo kwenye hizo kazi nilishavizoea, ....’
Tuendelee na
kisa chetu...
*********
Mwanzoni
nilipoanza kujiunga na tabia hizo chafu, nilikuja kusimuliwa habari za makundi
hayo haramu,....
‘Kulikuwa na
makundi ya kijambazi, maharamia, wanyang’anyi ,wabakaji, wenye kila kila aina
za hila....’ wenyeji wakawa wanasema
‘Watu hao
hao wabaya waliwatumia vijana, masharubaru, wenye nguvu, wakawaingiza kwenye
magenge, na kuanza kupora watu njiani kwa kutumia pikipiki, na wengine
wakajiingiza kwenye ujambazi wa silaha,
na zaidi wakaanziaha wizi wa mitandao, utekaji nyara , ubakaji, na kula
milungula(blackmail) ....’wakaendelea kusema.
‘Kiukweli
ilikuwa ni zama ya majinamizi,maana
ulikuwa huna amani, huwezi kutembea peke yako,na hata mkiwa kundi,badohuna
amani,kwani hujui wanavyoweza kukuingilia....’ walisema .
‘Mmm,kwahiyo
wengi wao walikuwa vijana?’ nikauliza
‘Si ndio,si
ndio wenye nguvu, na pupa ya maisha,lakini pia walikuwepo watu wazima, ambao
walikubuhi kwenye hizo kazi....wanaume na wanawake....’akasema mtu mzima mmoja
‘Hata
wanawake....?’ nikauliza kwamshangao
‘Haaah,yah,
hata wanawake,...tena wanawake ndio walikuwa hatari zaidi,maana akikujia huwezi
kumdhania vibaya,...’akasema huyo mtu mzima , sikuwa nimewahi kuambiwa kuhusu
huyu mama kabla, ila nilisikia tu kuwa kulikuwa na mama mmoja aliyekua jasiri,
lakini sikutegemea kuwa atakuwa huyo mama...
‘Hata waamke
, walikuwa mstari wa mbele hadi kupewa uongozi wa kuongoza makundi hayo,haiwezekani...!?’
nikasema kwa dharau, na sikutaka kusikiliza zaidi kuhusu huyo mwanamke
aliyekuwa kiongozi wao,mimi nilikuwa na kasumba ya kuzarau wanawake....sasa
kumbe ningelisikia mapema, huenda ingenipa tahadhari fulani...
‘Lakini
mkono waserikali mrefu, wengi wao walikuja kukamatwa...baada ya msako wa nyumba
hadi nyumba...’akasema mama mmoja mtu mzima
‘Lakini sio
wote...’akasema mume wake
‘Ndio kwa
muda ule hawakukamatwa wote, ....walibakia viongozi wao, wakajificha, wakawa
wanafanya mambo yao kwa siri....’akasema huyo mama
‘Walipoona
kuwa kuna bado mabaki,na hayo mabaki ndio hatari zaidi, ndio wakabuni mbinu ya
kuweka mitambo ya mitandao kila kona kuoana mizunguko ya watu, mitandao hiyo
iliwekwa kwa siri, ilichukua muda sana....na ndipo wakaja kuwanasa hao wakubwa
zao, na mmoja wa hao alikuwa ni mwana mama aliyekuwa tishio...’akasema huyo
mama mtu mzima.
‘Mwanamke gani huyo alikuwa jasiri kihivyo...?’ niliuliza
japokuwa sikuwa makini sana, kwani niliona kama hadithi tu...
‘Usiombe
ukutane naye...’jamaa mmoja akasema na mimi nikazarau tu.
‘Cha kutisha
zaidi wengi wao bado wapo jela,...’wakaniambia
hawakuniambia kuwa huyo mama alikuwa kaweza kumaliza kifungo,au kuachiwa
kwa msamaha,...kwani ndivyo ilivyokuwa kwa huyo mama, kumbe baadaye alikuja
kuachiwa kwamsamaha,baada ya kuonyesha mwenendo mzuri huko jela,lakini baada ya
kusota jela miaka mingi, ...
‘Kwa kipindi
kile sikuwa na hamasa ya kumfahamu sana huyo mama, ningelijua ningelijua cha
kufanya, huenda ningemchunguza na kumfahamu kuwa ni mama gani..., ila
waliposema alifungwa na huko jela alikuwa kiongozi wa wafungwa,..na jela ni
kama nyumbani kwake.,...
‘Moja ya sifa kubwa ya huyu mama ni kuwa haogopi,
ana uwezo wa kupigana kwa kutumia mikono yake bila silaha, lakini silaha pia
anaimudu vyema,..yeye akikosana na mtu anapanga pambano, na anakuambia kabisa
ukimshinda basi umfanye utakavyo, ila akikushinda cha moto utakiona, ole
wako....damu yako ni halali yake, na hakuna aliyewahi kumshinda....’
nikakumbuka maneno ya yule mlinzi.
Sasa kumbe
huyo mama ndio aliyekuwa bosi wangu,ndiye huyo nilimuingilia na kuanza kufanya
mambo yale aliyokuwa ameyaacha yeye...nikachokoza nyoka aliyekuwa kajificha
shomoni....
*********
Wazo la
kwanza lilikuwa kutafuta usaidizi, kwani kulikuwa na watu kazi yao ndio hiyo,
kutoa ulinzi, muhimu uwe na pesa za kuwalipa, au wanakwenda kupambana na huyo
mtu, nikaona nifanye hivyo haraka iwezekanavyo....maana nimeshatishiwa
amani...., nikampigia jamaa mmoja mwenye kumiliki kundi la walinzi kama hao;
‘Rafiki
yangu kuna mtu kanitishia amani, nataka msaada wako...si unajua zangu ni za
mdomoni,..... sasa huyu haongei anatenda kwa kipigo....’profesa akamwambia huyo
mkuu wa walinzi
‘Hamna shida
ni pesa yako tu...’akaambiwa
‘Si unanijua
tena mkuu, kwasasa sina kianzio, ila nakuahidi kuwa nitakulipa haraka
iwezekanavyo...na ahadi kwangu kwako ni deni...kwa hivi sasa sijapata pesa
yangu, ....’profesa akasema
‘Hapana wewe
siku hizi umebadilika kabisa, ...sifa zako zimekuwa za maneno tu, siwezi kutoa
watu wangu halafu niwaambie wasubirie, hata mimi nipo katika hali mbaya
kibiashara....’akasema
‘Mkuu je nilishawahi
kukubabaisha kwa ahadi hewa,...?’ akauliza profesa
‘Kwangu
hujawahi, ...najua ukifanya hivyo kwangu hutaishi, huwa sibabaishwagi, ujue
kabisa,...sitaki usumbufu, sasa hivi serikali ipo makini sana na watu kama
sisi...usije nikaja kunyang’anywa leseni yangu....’akasema
‘Kwahiyo...?’
profesa akauliza akijifanya anazo,
‘Nimekupa
angalizo tu, kuwa sitaki kazi ya ubabaishaji, kwanza nataka kianzio,...’akasema
‘Aaaa kianzio
ndio hicho,.... huyu mtu hataki kunilipa nahitaji watu wakunisaidia, ili
nizipate pesa zangu......’akasema
‘Ok,...kama
ni kwenda kuchukua pesa yako tu, nambie
ni nani ili watu wangu waanza kumfanyia kazi,kama kweli kuna malipo sahihi...ni
nani na anaishii wapi?’ akauliza
‘Madame
Africa..yule ni bosi wangu namdai pesa zangu nyingi tu hataki kunilipa nataka niende
na walinzi wawili....najua atanilipa tu, na baada ya hapo wawe wananilinda,
..si unajua tena....’akasema profesa akijua sasa mambo yatakuwa safi,
Akilini
alishaliwazia hilo, kuwa akienda kwa huyo mama, akiwa na hao walinzi,kuwa
anadai pesa zaidi, kwa kumzalilisha,na anamstishia kuwa ukizidi kumfuata fuata
atazitangaza siri zake zote, na
keshaajiri hao walinzi..
Japokuwa historia
zake za nyuma zilitisha, lakini niliona siwezi kuziachia pesa alizokuwa tayari
azipate, na akizipata anahama kabisa..
‘Nilipoongea
hivyo, nikatulia kimia, sasa kusikia jamaa huyo anayemiliki hao walinzi
atasemaje,nilijua ataulizia namdai huyo mama shilingi ngapi, maana huyo mama kwa muda huo ni tajiri, ana
uwezo,...’
Basi profesa
akiwa kashikilia simu kwa madaha,akatulia, akasikilizia majibu kutoka kwa huyo
mkuu wa mabaunsa..., lakini hakupata hayo majibu, kumbe simu ilishakatwa
‘Halooh,
vipi....’simu haikuweo hewani,..akajaribu kupiga tena, kwanza ikaita halafu
ikakatwa, ilionyesha kuwa jamaa hataki kupokea tena simu yake..., na baadaye
ikawa akipiga hiyo namba anaambiwa haipatikani.
‘Mhh,huyu
jamaa vipi....’profesa akabaki
akijiuliza huku nywele zikimsisimuka
kwa woga.
******
Siku hiyo
ikapita profesa akawa kama mgonjwa, ....
‘Hapo sina
pesa, nina madeni lukuki, mimi nitazipatia wapi hizo pesa, na kiukweli nilikuwa
nadaiwa pesa nyingi, kuacha hizo za huyo mama, ...
Unajua kuna
kule kujidanganya kwa kujipa moyo, sikukata tamaa, unajua tabia ya maisha hayo
yalivyo, na mimi yalishanikaa mwilini,unaweza ukasota kweli, huna pesa, maisha
magumu, lakini ukiibuka wewe ni tajiri, japo ni kwa muda...nikajipa moyo kuwa
huo ni muda wa kusota, lakini nitakuja kuibuka tu....
Nikachukua
karatasi na kupiga mahesabu, pesa anazonidai huyo mama peke yake, ooh,
nilijikuta mwenyewe siamini kuwa nilikuwa nimetumia pesa nyingi sana kwa huyo
mama.
‘ Pesa
haramu , pesa za dhuluma za huyo mama zilikuwa nyingi, achilia za hao wengine
na kutokana na huyo mama alivyosema, keshawapanga watu wengine, niliowahi
kuwafanyia hivyo,sijui aliwezaje kuwafahamu....akidai kuwa yeye sasa
keshajiunga na kundi la kusafisha wabaya mitaani....hasa watu kama mimi...’
‘Ujue mimi sasa hivi ni kiongozi wa kufuta
watu wote wabaya wameniamini kwa vile nawafahamu wote, ...sasa wewe kinyamkera
sijui umatokea wapi...nakuhakikishia utazilipa hizo pesa zao..’nikakumbuka
maneno ya huyo mama
Kiukweli siku
hiyo nikaona nisitoke kabisa...nikalala..lakini usingizi ungetoka
wapi,nikajikuta namuota huyo mama akinijia na kisu mkononi,mara akiwa na sura
ya shetani....
Siku ya pili, ikapita, siku ya tatu,..wiki
ikapita nikajua huyo mama keshasahau. Huenda alikuja kunitishia tu, hana
uhakika kuwa ni mimi...Nikaona nitoke niingie kwenye mishe mishe zangu maana
nitakufa njaa, sasa niende wapi, nikajiuliza.
Mara nyingi
mtu ukikwama kuna sehemu tunakwenda kwa mtaalamu wa kupanga dili,...nikaona
ngoja niende kwake nikajaribu bahati yangu..., huenda nikapewa dili ya kuingiza
pesa, japokuwa kwake napo kuna ushuru wa kumlipia, kwanza kwa ajili ya
kukupangia hiyo dili,
‘Hakupangii
mipangilio hiyo bure...unamlipa,ni kama madalali walivyo huku...’akasema
profesa
‘Kwanza
unamlipa pesa ya kukupangia mikakati, halafu ukifanikiwa unamlipa ushuru wake mwingine...ni
wajanja wajanja fulani hivi...’akaongeza kuongea
‘Basi
nikaona nipitie kwake,...’ akasema
‘Kiukweli
bro,huyu jamaa ni kichwa, yeye hafanyi kazi zaidi ya kupanga mikakati, ..mikakati
ya wizi,...., na hakosei...ana mitandao ya aina yake, anaweza akafanya vitu
vyake, akazima mashine ya kuona matukio sehemu fulani unapokwenda kufanyia hujuma,
ikibidi...., lakini hapo unatakiwa umlipe pesa nyingi...’akaendelea kuongea.
Japokuwa
sikuwa na pesa, nikaona nimuone tu, nitamkopa,..pamoja na ubabaishaji wangu,
lakini watu walikuwa wakiniamini kwa kazi za mdomoni, kukiwa na kazi ya kwenda
kuongea, aaah,nimo sana,siunajua wabongo kwa kuongea....’akakuna kuchwa
‘Ila kazi za
kupigana ngumi,kutumia bastola....simo,..naweza kutumia silaha ndio,lakini
ilikuwa sio fani yangu....mimi ni kupepeta mdomo, weee, walikuwa wakinijulia kwa
hilo...hasa hii kazi ya mlingula, kule wanaiita blackmail..hiyo ni kazi nyeti kule...
********
‘Ndugu umekuja,ulikuwa
wapi,sijakuona karibu wiki....’akaniambia huyo jamaa
‘Nipoo nipo
tu....’nikasema
‘Sasa
kulikuwa na kazi moja,...nataka wewe uifanyie....’akaniambia kama vile
alifahamu kuwa nimekuja kwa kwa hilo.
‘Mhh, kwa
hivi sasa nipo mtegoni, siwezi,...’nikasema
‘Sasa
umekuja kufuata nini...?’ akaniuliza akionyesha kutotaka kuongea na mimi tena.
‘Mhh,....kiukweli
nimekuja kwa hilo, ila iwe kazi ya chapu chapu....’nikasema huku moyoni
natamanii anipe dili yenye unafuu, sikutaka shari kwa muda huo.
‘Unajua kazi
yenyewe ni kazi gani....?’ akaniuliza
‘Sijui
nambie wewe....’profesa akasema
‘Hiyo kazi,
nilishaifanyia kazi, ...unajua na mimi nahitajia pesa kidogo, nataka kununua
chombo fulani, ni gharama sana....na nikikipata hicho, dunia nitaiweka hapa....sasa
nikaitafiti hiyo dili,nikaona wewe unafaa....’akasema akionyeshea mkononi kuwa
dunia ataiweka hapa(unakumbuka kisa cha dunia yangu)
‘Mhh, lakini
kwanini mimi..?’ profesa akauliza
‘Aaah, sio
lazima wewe, ila ulivyokuja nikajua una njaa..au..kama hutaki basi...’akasema
akigeukia komputa yake maana masaa yote yupo kwenye komputa.
‘My friend, mtu akija kwako, ujue
hajafika kuongea au sio, ila..sitaki kazi ya kunichukulia muda mrefu..., nataka
kupata na kuachia, na kutoweka, nipo kwenye kamba nyembamba, naweza
kudondoka...’nikamwambia tukitumia lugha zetu
‘Kuna kazi
moja, ikifanikiwa utaingiza ,dola laki moja na elifu hamsini,kama kianzio
unazipata bila ubishi, na hapo ushanilipa ushuru wangu....,’akasema huku
akitabasamu
‘Na kila
mwezi kama kawaida utapata elifu hamsini, kwa miezi kama mitatu,...au hata thelathini,
ukimuhurumia,...na hushuki zaidi ya hapo,...mimi unanipa zangu kumi kumi kila
mwezi kwa miezi hiyo mwili,sitaki zaidi....’akasema akijizungusha kwenye kiti
chake.
‘Unaona
ilivyo,...baada ya mikupuo mitatu, wakati bado anahaha,....unampa unafuu, mimi
naachana na wewe, unabakia wewe na mwenye kisima,maana si umeshamfahamu,
nazimamitamb yangu, unafanya vitu vyako,ukitaka....mpaka utakapohakikisha
kisima kimekauka, ni wewe tu na njaa zako...’akasema huyo mtaalamu.
‘Mhh, dola laki
moja na elifu hamsini, tasilimu!...na bado kila mwezi naingiza hamsini,au
thelathini!...halafu unasema wewe nitakuwa nakulipa kumi kumi kila mwezi, kwa
miezi miwili....mmh hapo bado nitabakia na ...ooh, usinitanie...?’ nikasema
nikitabasamu.
‘Kwanini
niendelee kukulipa kidogo kidogo kidogo,wakati wewe tunakulipa kianzia na
ushuru tu,...?’ nikauliza nikianza kuingiwa na tamaa na ubinafsi hata kazi
sijaifanya.
‘Maana
tukienda kwenye ushuru wangu utaona pesa ni nyingi, ndio nikaona unilipe kwa
mikupuo..uonavyo,vinginevyo tutaingia kwenye asilimia ya pato,..ni wewe tu...’akasema
Kiukweli
moyoni hamasa na tamaa vikajijenga, sikuwa na matarajio kama hayo, na huyu ni
mtaalamu kweli akikuambia kitu ni kweli kinafanyika, na hana ubabaishaji.
‘Hii kazi
nimeshaifanyia utaratibu wote, kinachohitajika ni mtu wa kuongea, mtaalamu wa
kuongea lugha tofauti..maana kuna maeneo saba ya kucheza nayo,...huyu ni kuku
mgeni ,...hana hiana, ni muoga,..ni tajiri bahili,...’akasema
‘Tajiri
bahili dawa yake ni moja tu...hahaha,...huyu jamaa bwana kaibukia toka huko
kwao,..huko naona alikuwa hapati nafasi..., lakini ana upele kila sehemu, japo
anajifunika, tunahtajika tuukune huko upele...natumai unanielewa....hana
ujanja, ila ana pesa anayo,nimeshapata akaunti zake zote....’akasema kwa
kutumia lugha wanazozijua...
Jamaa alipofika hapo akajinyosha kuonyesha
kachoka kuongea na kaka mtu mwenyewe akasimama na kuchukua kopo la maji akampa
ndugu yake anywe, hamasa ya kusikia zaidi ilishamuingia, na ndugu yake
alipomaliza kunywa maji akasema;
‘Bro,hapa
ungenipa kinywaji...mmh, nakumbukia enzi zangu....’akasema
‘Achana na
ulevi,afya yako yenyewe migogoro,..hebu nikuulize swali...’akasema kaka mtu
‘Maswali
utanipotezea mpangilia uliopo kichwani,..kwani unataka kuuliza nini bro,kuhusu
kijana wako...?’ akasema jamaa
‘Ina maana
mlikuwa mkilipwa pesa zote hizo, hizo si dola ukibadilisha kwa pesa ya kwetu ni
shilingi ngapi....mbona pesa nyingi sana...halafu ina maana hata kijana ulimlea
katika mazigira hayo hayo,maana hapo hujamtaja kabisa..?’ akauliza kaka mtu
akiwa na mshangao machoni
‘Hahaha,
bro, tatizo pesa hizo ni chafu, unazipata leo, kesho hakuna kitu...ukizipata
unakimbilia kulipia madeni, kulewa na starehe, ...zinapukutika kama vumbi
hafifu jangwani linavyopeperushwa na upepo...
‘Bro ya
kijana wako utakuja kuyasikia, kwanza uone maisha yangu, na utakuja kuona chanzo
cha kijana wako kuja kupata mke,....ilianzia mbali....’akasema akijiegemeza
kwenye kiti.
‘Haya endelea.....’akasema
kaka mtu
‘Basi huyo
mtaalamu aliponitajia kiwango hicho cha pesa, nikajua nitaweza kupunguza pesa
za huyo mama, na nitamuahidi kuwa nitamrejeshea kila mwezi, elifu kumi kumi
yake, na huku nabakiwa na pesa za kujitanua mitaani, sina shida nikiwa na pesa,....’akasema
akionyesha kwa vidole
‘Bro,unajua maisha ni mafupi tumia pesa ukipata ukikosa unajutia
unabakia kuota ndoto za Alinacha kwenye vitabu vya zamani, kama ninavyoota sasa
hivi...
‘Niliwazia
kuwa huyo mama, pamoja na mengine ana udhaifu mmoja,anapenda sana pesa,
ukamtajia kuwa ataingiza pesa nzuri, mhhh, wewe utakuwa rafiki yake..’
aakatabasamu.
Basi
nikaendelea kuongea na mtaalamu,nikamwambia;
‘Kama una
uhakika,....kuwa nitazipata hizo pesa...nitajaribu..’nikasema huku tamaa ya
kuingiza hizo pesa ikinitawala akilini,akaniangalia kwa jicho la haraka halafu
akakunja sura, akasema;
‘Hakuna
kujaribu hapa, kama huwezi useme si-we-zi....na mimi nitamchukua mtu mwingine
anayefaa....siwezi kupoteza taaluma yangu kwa mtu wa majaribio.....unanifahamu
nilivyo....’akasema huku akikagua kitu kwenye komputa yake.
‘Unasikia
profesa, nataka mtendaji na sio mtu wa kujaribu, na swala la kuwa mimi nina uhakika,
nashangaa kwanini unaniuliza hivyo,na umekuwa mtu wa kwanza kunitilia mashaka
kwenye dili zangu, haijatokea,...mimi sipendi kabisa...’akasema akinitupia
jicho la udadisi.
‘Sijatilia
mashaka dili zako...,najua wewe ni mtalaamu wa dili....nilikuwa nasemea tu...kama
umeshaifanyia kazi, isije nikaingia kichwa kichwa...’akasema profesa
‘Sikiliza
nimechanganua, nikaona wewe unafaa, kuna kazi nyingi tu, lakini hizo nyingine zinahitaji
mtu mwenye nguvu, wewe huna nguvu, nguvu zako zipo mdomoni tu.. .nitakuelekeza
utaratibu..’akasema huku akiendelea kuangalia kwenye komputa yake.
‘Muhimu,ukifanya
nitakavyokuelekeza, haina shaka utafanikiwa, ila ukijifanya una akili zako
nyingine,ukafanya uonavyo wewe,ukivuruga mimi sipo, ninachohitaji kwanza ni
kianzio cha kukupa hii dili na sio mtu mwingine na ushuru wangu ukishafanikisha....’akaniambia
huku akionyesha uso wa kunidadisi.
‘Ok,...ok...lakini
hapo nina shida....’akasema profesa
‘Shida gani
tena, usisema umechacha....kwanza nikuulize ile dili yako binafsi ulishaimaliza...?’
akaniuliza
‘Dili
ipi...?’ nikamuuliza nikionyesha uso wa mshangao,maana dili binafsi ninayoijua
mimi ni hiyo ya huyo mama,...nyingine ni za kuchangia, na hakuna mtu
niliyemuhusisha, sikutaka kumuhusisha mtu yoyote, sasa huyu mtu kafahamu vipi
hiyo dili binafsi...,nilipotaka kumdadisi haraka akasema;
‘Tuyaache
hayo...hayanihusu,...,nakuuliza tena,
upo tayari kwa hiyo kazi,...utaiweza hiyo kazi,asilimia kubwa ya hiyo kazi,
ni mdomo tu, kuongea halafu ikifika kwenye kuchota pesa ni lugha ya vitisho kwa
mdomo tu,lugha ya hadaa kwa mdomo tu...,na wewe ni mkali kwahilo...sasa
usinipotezee muda,nahitajia kumuita mtu mwingine...’akasema
‘Aaa,
sijasema siwezi kuifanya,...nipe hiyo kazi...nitaifanya.....’nikakubali, lakini
moyoni nilikuwa na mashaka, nilishaingiwa na uwoga fulani, ambao nilikuwa sinao
kabla, baada ya kujiunga na mambo haya nilijifunza kutokuwamuoga,kutokuwa na
huruma hasa unapoona jambo hilo ni la pesa...
‘Lakini pamoja
na wasiwasi, mashaka, kiasi hicho cha fedha kilichotajwa kutoka kwa huyu
mtaalamu kilivutia sana...tamaa,...ubinafsi,ukanitawala, na kutokana na njaa , na
shida niliyokuwa nayo, nikajipamoyokuwa nitaiweza hiyokazi,japokuwa
nilikuwasijaambiwa ni kazi gani.
‘Utaifanya hiyo
kazi sio.....?’ akaniuliza akiniangalia kwa macho ya udadisiakitaka uhakika
tena wa kauli yangu,maana mamboyetu unaulizwa mara mbiliya tatu inakuwa
nimkataba...
Nikatabasamu huku akilini nikianza kuzihesabu
pesa kimawazo, nikiwazia kuwa muda huo nipo nimesima mbele ya huyo mama, huku
namuhesibia pesa zake na huyo mama akitabasamu kwa tamaa, lakini cha ajabu alipotabasamuu
niliona meno ya kishetani ya kijitokeza...
NB : Habari
ndio hiyo, na hayo ndiyo mambo ya ulaya
na profesa, je ilikuwaje
WAZO LA LEO: Tamaa ni mbaya, mtu usipotosheka na
pato lako halali ukataka zaidi ya halali yako, ukadumu kwenye dhuluma,
ukajenga, ukajijenga, ukachuma kwa mtindo huo, usitarajie amani katika maisha
yako,dhuluma hiyo itakuandama hadi unaingia kaburini, achana kabisa na tabia
hiyo, rizika na pato lako halali.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment