‘Mimi nina ushahidi
wote,....’akasema huyo mama
‘Kwanza wewe
mdudu, nilikuamini sana, unakumbuka
nilikuchukulia wapi, mitaani, ukihangaika na njaa, unakumbuka siku ile hata
kutembea ulikuwa huwezi, nikajua nasaidia masikini, hohe hahe, omba omba
nilikuonea huruma maana nilikufananisha kama wadog zangu kule nyumbani...unakumbuka,...?’
akawa kama anauliza
‘Yaani, nikaona nikusaidie, unifanyia kazi zangu za
nyumbani, ili usiabike...unakumbuka...’akasema na kuuliza tena
‘Nakumbuka
nashukuru sana,ndio maana mimi siwezi kukufanyia mabaya..haki ya mungu tena,
mimi siwezi kabisa kukufanyia ubaya najua uliponitolea...kwanini nikufanyia
hivyo....’akasema profesa
‘Na kwa
kukuamini kwangu, ukatokea kufanya kazi kwa muda mrefu, sio kwamba nilikuwa
nakuamini mia kwa mia, lakini niliona nikusaidie tu..nikajisahau kuwa mwenye
tabia haachi kuitumia hasa anapopata,...’akasema
‘Kiukweli,
ulinigusa pabaya,. Kuwa utamwambia binti yangu, kuwa sio mtoto wangu utamwambia
kila kitu jinsi alivyotokea, imeniuma sana,....ni kweli ukifanya huo uchafu
wako utaniharibia, ...utafanya binti yangu kipenzi aumie sana..sijui utapata faida
gani, na siwezi kuona binti yangu anaumia, ...’akasema
‘Lakini nina
uhakika kauli ya kumuambia huyo binti hutaweza kuitoa tena...na kama utaweza
labda iwe kauli yako ya mwisho ukikata roho, ..na hata hivyo kwa sasa
hatakuamini,......’akasema kwa kujiamini
‘Aah, siwezi
ila kama ni swala la kuamini, ...hapana, siwezi kukufanyia hivyo, kwako wewe
hapana...’nikataka kumuambia kuwa nikipata mwanya wa kuongea na huyo binti yake
ataamini tu, mimi kwa mdomo, achana name bro...’akasema profesa
‘Nikuambie kitu...,
nyie watu mnataka msaidiweje,...na wewe ndiye uliyetokea kufanya kazi kwangu
kwa muda mrefu, kumbe nilikuwa nafuga nyoka, kweli ngozi hii,
hapana,...’akasema akivuta ngozi ya mkononi mwake.
‘Lakini....’profesa
akawa anataka kulalamika, yule mama akainua mkono wa mkumnyamazisha akasema
‘Mimi nina
ushahidi, usitake kubisha, mimi sio mjinga, mpaka nije kukuambia
hili,..nimechunguza kila kitu, nimegundua, jinsi ulivyochukua kumbukumbu zangu
pale nyumbani, hukuchukua kumbukumbu zangu ukaenda kutoa nakala wewe...’akasema
kama anauliza na profesa alipotaka kusema kitu akashindwa na huyo mama
akaendelea kusema
‘Nimekugundua
jinsi gani ulivyokwenda kuonana na dakitari aliyehusika , ulikwenda kufuata
nini kwake, hivi wewe inakuwashia nini, mimi kuwa na mtoto, unajua jinsi gani
nilivyohangaika....’akatulia kidogo akiwa kashika kiuono
‘Wewe
unakwiba pesa zangu unakwenda kumuhonga dakitari ili akupe nakala za jinsi
nilivyofanya,...ndio alikubali...maana nay eye ni njaa kali kama wewe, nay eye
kitamtokea puani, kazi hana..kakupa stakabadhi ulizotaka na faida yake ni
kupoteza kazi
‘Eti unajifanya
mjanja kupiga simu mitaani, ukaenda mpaka mtaa wa pili ndip unanipigia simu,
nikuambie kitu simu zote za njiani zinanakiliwa, ulivyokwenda ukafanya kote
huko nimekuona, ujue kuwa mimi ni nani,....’akasema akiwa kashika kiuono.
‘Sasa
niambie, nini umepata na hizo pesa, .....’’akasema
‘Unajua...ni
maisha tu...’akasema profesa
‘Mhh ni
maisha tu, haaaa, unanipandisha mori, ingelikuwa enzi zile saa hizi damu
zimetapakaa kila mahali, lakini sasa hivi sitatumia mkono wangu huu, ila
utaumia, nakuahidi utaumia.......’kiukweli nilishangaa kwa jinsi gani
alivyopata hizo taarifa maana ni kweli, ndivyo nilivyofanya na maana hiyo ina
maana kweli keshanigundua.
‘Lakini sio
kweli...ni watu tu hawanipendi wametunga tu hizo habari....’nikajitetea lakini
hakunisiliza, akaendelea kusema
‘Sasa nakuhakikishia,
ama zangu ama zako, kama hukuwahi kunisikia kuwa mimi ni nani kabla, basi
ulizia...ulizia, na mwenye kovu kamwe usizani kapoa....mimi nitakunyesha kuwa
nilikuwa nani..’akasema akjitanua kifua, na alionekama mpana kama mwinua vyuma,
sijawahi kumuona hivyo kabla, akamsogelea profesa na profesa akawa anatetemeka.
‘Lakini ni
nani kakudanganya, si-s-o mimi haki-ki-ki ya mungu tena , kwanini mimi
nikufanyie hivyo, wakati nilishakuona kama ndugu yangu, mkaniamini.....’profesa
alijitetea huku airudi nyuma, na huyo mama akiwa kamuangalia kwa jicho la
kikatili
‘Kukuamini,...kukuamini
wewe,.... mimi sijawahi kumuamini mdudu yoyote, hasa mwenye rangi kama
yangu...’akasema huku akinyosha kidole.
‘Lakini
sijawahi kufanya hivyo unavyosema...’nikasema nikisogea mbali na yeye
‘Nikuambe
kitu, mimi najuana na vikundi vyote vya hapa mitaani na majirani...waulize hata
polisi, wananijua,..sio kwa vile nimekuwa mtu mzima ndio ufikiria nimekwisha,..nilishaamua
kuachana na tabia hizo lakini hujui moyoni mwangu
kupoje....nakusikitia...’akatkisa kichwa
‘Samahani
..ni ni shida..lakini sio mimi...’akasema profesa
‘Yaani
uanifanya nihisi kutapika...’akasema na kutema mate chini
‘Samahani,
enzi zangii kauli kama hiyo ilikuwa ni tikite ya kuihama hii dunia...maana
ukiachiwa zaidi, utazidi kuharibu na kupata dhambi, samaahni maana yake
umeshatubu dhambi zako a upo tayari kwenda ahera au sio...’akasema
‘Mimi
nilishaamua kutulia na mume wangu, kwanini bado watu mnanitafuta, nimechoka
kumwaga damu za watu, ...’akatulia
‘Nitafaya
lolote unalotaka..ila kiukweli sikufanya..sio mimi, watu tu ....’profesa
akasema
‘Nikuambie
kitu, ni huyu mwanaume tu, ...kwa vile aliahidi kunibadilisha, na mimi
nakukabaliana naye, lakini moyoni, ujasiri umedinda kama muhimili wa
nyumba,....mtu akinichokoza, sijali ni nani...wewe umenichokoza, na hustahili
kusamehewa, utajua na utanikumbuka...’akasema akiinua mkono wake juu kuonyesha
nguvu.
‘Ujue kuna
makosa makosa yanafanyika hata mitambo inakosea,watu wanabuni mambo kuwaharibia
wenzao, ...na chuki binafsi,..huyo mpelelezi wako huenda kakosea, hivi mimi
unanionaje kweli mimi naweza kukufanyia hivyo...?’ nikamuuliza
Akatabasamu
, tabasamu la dharau, akasema;
‘Unamfahamu
yule mkusanya mizigo, nilimweka kwenye anga zangu nikamkumbusha wapi alipotoka,
mimi ndiye niliyemfanyia mipango ya ile kazi anayofanya, alitakiwa kutumikia
kifungo cha maisha kwa kosa la mauaji, nikamsaidia, unafikiri mtu kama huyo
anaweza kunisaliti mimi...’akasema na kumfanya profesa kutoa jicho, kumbeee....
‘Ina maana
alikuambia....’profesa akajikuta amesema hayo maneno
‘Hahaha, hata
kabla huyo mlinzi hajafungua bakuli lake nilishakujua wewe ni mtu gani, kawaida
hata nikiweka mpelelezi lazima nihakiki kazi yake,...nilishakujua wewe ni nani,
unajifanya mnajimu,..una unajimu gani, muuaza miti shamba...kwanini unaharibu
uafrika wetu...’akasema
‘Lakini dawa
zangu zinatibu kweli...’akasema professa
‘Kama
zinatibu kweli kwanini hujafanikiwa, kwanini unaishia kuiba, kuwa
tapeli...’akasema kama anauliza
‘Mimi nakujau
kuliko unavyojijua wewe, ....sasa, ..nakuhakikishia, utalia kama mtoto mdogo
huku natoa nyama yako kidogo kidogo kama mchuna ngozi kwenye mnyama ...japokuwa
mimi ni mtu mzima, lakini mikono yangu ni mirefu, inafika huko jela
utakapokwenda kufungwa, utalia na kunikumbuka....’akaniambia
‘Tafadhali, ,...’nikamwambia
sasa nikitamani kumpigia magoti
‘Kwanza
nikuambie, sijawahi kudhulumiwa, na aliyewahi kufanya hivyo keshaliwa na
mafunza,...sasa nataka pesa yangu yote, ..na gharama za kumlipia mpelelezi, na
sijui wewe utazipatia wapi, hiyo sio kazi yangu,...., ukinirejeshea hizo, aaah,
tutakubaliana katika sharti la
pili...’akasema na hapo profesa akapumua, lakii akajiuliza atazipatia wapi hizo
pesa.
‘Sharti gani
la pili,.....?’ akauliza profesa
‘Hilo ni
namba moja, na sharti la pili uhame eneo hili haraka iwezekanavyo, ndio nakuona
ulishafungasha kuondoka,...., lakini huwezi kuondoka bila kunirejeshea pesa zangu, unajia nimezipata wapi, mwanamke
mimi, unajua nimezipata wapi, sasa na wewe utakwenda kugezwa mwanamke, uzipatae,....utakoma
kiumbe wewe...’akasema akikagua begi langu kwa macho.
‘Aaah,...sio
kwamba nakimbia,... hapa nadaiwa sana kodi ndio maana nahama...ila pesa zako
nitakurejeshea nipe muda....’profesa akasema
‘Hahaha,.....unadaiwa
eeh, hahaha, basi nikuambie kitu, wote wanaokudai nimeshawasiliana nao
wanahitaji pesa zao , na mimi nimewaahidi kuwa utazitoa, na nikiwarejeshea
nitalipwa asilimia hamsini yake hiyo nikumbie waziwazi, mimi sifanyi kazi za
uficho, ni lazima watu kama nyie mpotee kaibisa eneo hili, lakini kwa fundisho,
na ni lazima wote waliotoa pesa zako kukupa wewe blackmailer, watazipata, ahadi
hiyo nimeshawapa.......’akasema
‘Lakini mimi
sina pesa...’profesa akasema
‘Hahahaha...na
kabla hujazitoa...utaumia, utalia, utanikumbua..unasema huna pesa...utazipata
tu..huku ukiwa umeteguka kiuno...huku damu zinatoka sehemu za siri..., na
utarejea kwenu ukinikumbuka na kuniota..wenzako wanaota wanawake kwa starehe
walizopata kutoka kwao..,lakini mimi utaniota kwa maumivu...’akasema, halafu
akacheka kicheko cha kiume.
‘Unajua enzi
zangu nikicheka hivyo maana yake nini...’akasema na kabla sijamjibu akaondoka.
NB: Habari
ndio hiyo, msizarau watu
WAZO LA LEO:Kuna watu wana tabia ya kudharau
wenzao, kwa vile tu wao wana uwezo, wana kipato, ni viongozi ni mabosi, basi
wanapandisha mbega, wanajaa kiburi,ukifanya jambo, `unajua mimi nani...’ hata
kama umedhulumu, hata kama mtu anadai haki yake..acheni jamani, ..tendenii haki
na simamieni kwenye haki na kweli, haki na jasho la mtu halipotei bure ni swala
la muda tu..wangapi wangapi na sasa wapo wapi..
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment