Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, June 25, 2015

RADHI YA WAZAZI-10


‘Unamfahamu vyema huyo mama unayefanyia kazi kwake...’ni swali alilokuja kuniuliza yule mgambo mpokea mizigo...aliniuliza hilo swali, nilipofika kumpa taarifa kuwa natarajia kuna mzigo wangu utafika kwake;

Tuendelee na kisa chetu...

********

‘Unatoka kwa nani...?’ nilipomwambia tu akaniuliza huu akiandika kwenye kumbukumbu zake, nikakaa kimia, kidogo, ndipo akanitupia jicho la haraka, halafu akasema

‘Ohoo ni wewe ni kutoka kwa yule mama au...?’ akauliza huku akiandika kitu kwenye kumbukumbu zake

‘Mama yupi,...?’ nikamuuliza maana muda huo nilikuwa sifanyi kazi tena kwa huyo mama, na sikutaka huyo jamaa afahamu vyema kuwa bado nachukua kitu kwake, na siku hiyo nilitaka nimlipe ushuru kidogo, au nimkope tu.

‘Mhh, huyo mtu unayesema ataleta mzigo hapa na wewe utauchukua kwangu unamfahamu vyema,si ni huyo mama, unayefanyia kazi kwake...si bado upo naye?’ swali hilo lilinifanya nishutuke kidogo, maana siku zote namuagiza, au napokea mzigo kwake, na anachouliza ni ushuru wake tu.

‘Mhh,kwani nilikuambia analeta huyo mama, sikumbuki kukuambia kitu kama hicho...’nikasema

My friend, my friend...huwa sisahau....hiki kichwa ni komputa inayotembea,..mwanzoni kabisa uliwahi kuniambia hivyo, unakumbuka, ukasema ni mzigo wa mama mmoja hivi, ukamtaja kwa sifa zake,zikuwa na muda wa kukupa angalizo, anyway, its my job, sitakiwi kukudadisi sana, lakini wewe ni rafiki yangu au sio...’akasema

‘Mhh, sikumbuki, lakini kwani kuna tatizo,...yule mama alikuwa ni bosi wangu...ndio wewe ni rafiki yangu, tupo pamoja...’nikamwambia

‘Kumbe umeachana naye, kama ni huyo mama, sio mama wa mchezo,...nakumbuka enzi zake, alikuwa akiogopewa mpaka na polisi...hakaagi na mfanyakazi kwa muda mrefu, wewe naona umajitahidi...’akasema

‘Kwanini polisi wamuogope...?’ nikauliza nikijua labda, alikuwa na biashara zake, au alikuwa tajiri

‘Huyo mama ni jasiri sana, na vikundi vyote vya kihuni anavijua...’akasema

‘Kwanini, hata hivyo huenda ni kutokana na biashara zake, unafahamu biashara zake...?’ nikauliza kwa udadisi

‘Mhh, biashara zake..! unajua enzi hizo akiwa ndani ya vikundi kama kiongozi alikuwa akiogopewa kama simba dume nkati kati ya nyati kwa ujasiri wake, wewe ni mgeni kidogo, hapa, kipindi cha nyuma kulizuka vikundi hatarishi,...na huyo mama alikuwa miongoni mwao.....’akasema huyo jamaa, na kunifanya sasa nitulia kumsikiliza

‘Unasema! Huyo mama... ! haiwezekani....Sizani kama ni-ni,  huyo mama, naona umekosea, huyu mama niliyekuwa nafanya kazi kwake kaolewa na mzungu...unasikia ni mke wa mzungu, na wana binti mmoja...mnzuri sana...’ nikasema

‘Ehee, huyo mama mwenye mwili mwili, sio....kapanda juu hivi eeh...eeh, si ndio huyo eeh..ya ana binti mnzuri...japokuwa ukiwachunguza binti na wao, hawaendani lakini ndio dunia ilivyo,...ni binti yao..na sijui...huko sijui sana...si ndio huyo?’ akaniuliza akiniangalia kwa makini usoni

‘Mhh, ndio huyo, ..lakini kwa nimjuavyo mimi, hajawahi kuwa mitaani na wahuni, ni mama wa watu mwenye heshima zake....au unazungumzia mama yupi...?’profesa aliuliza hilo swali huku mwili mzima umeshikwa na mshituko, akihisi kuwa huenda,  kaingia choo cha kike, na humo akamkuta mama mkwe.

‘Ndiye huyo huyo...nakumbuka mwanzoni ulisema ni mizigo yake, na baadaye unakuja kuzichukua ukisema kuna sehemu nyingine unatakiwa kupeleka, nashindwa kuelewa, kwanini usipeleke moja kwa moja wewe mwenyewe mpaka ifike kwangu ndio uje uchukue tena kwa akili ya haraka lazima utajiuliza...lakin its not my business, its just a curious’akasema

‘Kwahiyo wewe hutaki kazi, maana kwa kufanya hivyo ndio nakupa ulaji, au nimekosea....’nikasema

‘Aaah, usinielewe vibaya,...kabisa nashukuru sana, ila kibinadamu unakuta unajiuliza uliza tu...na wewe ni rafiki yangu, shauku ikanijia,...nikuulize na kukupa a-nga-li-zo...’akasema akionyeshea mkono wa kusitisha mazungumzo.

‘Ohoo, kumbe unachunguza chunguza watu, nilijua wewe kazi yako ni kuchukua tu mizigo, na huna haja ya kuchunguza chunguza watu...sasa unanipa mashaka...’nikamwambia

‘Ngoja....nakumbuka kuna dume moja alitaka kumfanyia ubaya huyo mama, katika vikundi vyao, walishafanya kazi zao wakapata pesa, si unajua kazi za dili, za haramu haramu, mimi sipo huku, nakudokezea tu.... basi huyo mama, kipindi hicho ni mremb, akamwambia huyo dume wapambane naye wakiwa uchi, atakayeshindwa, aadhiriwe, na pesa hizo zote apewe mshindi...mimi nilishuhudia hilo tukio kwa macho yangu....’akasema bila kujali maelezo yangu

‘Ina maana wewe ulikuwa wapi, au ulikuwa kundi moja na hao wahuni...ikawaje..?’ nikamuuliza

‘Nakupa picha tu...usiseme ooh rafiki yangu hakuniambia,..just imagine...put in your mind,...’akasema akionyesha kidole kichwani.

‘Ikawaje...?’ profesa akawa na hamasa ya kutaka kujua zaidi

‘Hebu fikiria ni mwanamke wa namna gani anaweza kufanya hivyo, wanapigana uchi, na kichupi tu, na kichupi chenyewe...hahaha, usinkumbushe mbali, nilikuwep o nikaona kwa macho yangu dume likiadhiriwa, mwanamke anasimama kidedea watu tunashangilia...’akasema

‘Akamshinda huyo mwanamume, basi huyo mwanamume alikuwa kama mimi tu...’akasema profesa

‘Kama wewe...unamuona huyu mlinzii wangu hapa...huyu ni cha mtoto, ...enzi hizo kuingia kwenye kundi sifa ya kwanza uwe shupavu, ..na ukiwa kiongozi uwe umeshaua, umeshapambana na polisi ukapiga saana...huyo aliyepambana naye alikuwa mmoja wa mashupavu wa kundi, anayeogopewa....’akasema

‘Mhh, ina maana huyo mwanamke ana miguvu ya namna gani, ni mchawi...au walikuwa wakimuhurumia kwa urembo wake...’akauliza profesa

‘Hahaha, ulishawahi kumuona huyo mwanamke maumbile yake.., ana msiuli kama mwanaume,... hutaamini, ila mavazi anayovaa yanamsitiri tu, siku hizi na utu uzima, anajihifadhi, au sio..muda wote na miguo mipana, jiulize kwanini anavaa hivyo, wakati wakazi wengi wa huku, wanajichia tu, wanawake wanatembea nusu uchi, lakini huyo mama muda wote miguo mipana,......’akasema

Kweli hapo, bro..nikaingiwa na mawazo...ni kweli katika kufanya kazi kwangu kwa huyo mama sijawahi kumuona akiwa kavaa nguo za kuonyesha maungo yake, kwahiyo sikuwa na uhakika saana na maneno ya huyo mlinzi.

‘Mara nyingi,huwa enzi hizo alikuwa akiwa kazini anavaa kivazi cha rangi ya chuichui, akivaa hivyo ujue kuna jambo nzito..., na wakati wa mapambanoo hana huruma, anaweza kuua huku anacheka....’akazidi kuongea, ni kama vile alitaka kunifikishia ujumbe bila kukosea, ndio maana hakutaka maswali maswali.

‘Ina maana amewahi hata kuua...?’ nikauliza sasa nikiwa najuta nikijua sasa nimeshapatikana, na huyo mlinzi kwanza akawa kama anakagua watu, akawa katulia, halafu akasema

‘Hahaha,...kuua, vikundi kama hivyo kuua sio jambo la ajabu, ni kama kula wali wenye chuya na mawe useme hutang’ata jiwe,..huyo mama mhhh..., achana naye , kama aliwahi kuwa kiongozi wao, utauliza kuwa hajawahi kuua..., na sio mara moja kushitakiwa kwa kesi ya mauaji, alikuwa akiponea chupu chupu tu, kwa vile..ooh, ngoja nisiseme saana nikaharibu soko langu.....’akasema huku akionyesha ishara ya kukatisha mazungumzo.

‘Sasa kwanini hajafungwa au kunyongwa....kama aliwahi kuua,...?’ nikauliza

‘Hahaha, huyo mama kufungwa, ....ameshawahi kufungwa, mara kadhaa...na huko jela wanamjua utafikiri kazaliwa huko, huko ana marafiki wengi tu, na alifikia kupewa uongozi akiwa jela, kiongozi wa wafungwa....kulikuwa na chumba chake cha amlikia wa jela....’akasema akitabsamu kama anahadithia kitu kizuri sana, au picha yenye mvuto.

‘Ina maana mnajuana na huyo mama..?’ nikamuuliza

‘Mimi ni mlinzi wa siku nyingi,..najuana na watu wengi tu...wengi wa enzi zangu ukiwauliza watakuambia, ila mimi najua zaidi ya hayo kwa huyo mama...’akasema sasa ikiwa kama ananong’ona

‘Ina maana labda uliwahi kufanya kazi na huyo mama,au kwa huyo mama....?’ nikamuuliza

‘Kazi gani,..hapana...siwezi kufanya kazi kwake, hata kama akinilipa mabilioni, hapana, ila elewa hivyo tu, kuwa namfahamu, ...’akasema

‘Sasa kwanini umeniambia hayo yote....?’ nikamuuliza sasa nikimtilia mashaka

You’r y friend..right...?’ akasema akiniangalia moja kwa moja usoni

Yah, of course...’nikasema nikigeuka huku na kule

‘Mimi namuogopa sana huyo mama, na siku ulipoleta ule mzigo ukasema umetoka kwake, nikahisi kuwa ...kuna jambo nyuma yake, si bure, hajawahi kufanya hivyo wangu tangu ..tangu, tangu....ni siku nyingi sija...eeh,...ndio hivyo, sutaki kuongea mengi, ondoka usije ukataka akanijia,...ana masikio yanasikia kama nini....’akasema sasa nahisi akiwa hataki kuendelea kuongea.

‘Mhh, nimekufa...’nikajikuta nikisema huku nikigeuka huku na kule...

‘Kama umeingilia anga zake, sijui labda awe amebadilika kihivyo, lakini nijuavy haat katika uzima wake bado wanamuheshimu, bado anaogopewa,bado I nyoka,....unajua nikuambie kitu, watu kama yeye wanabadilika kinje-nje tu, lakini kindani unyama upo pale pale...’akasema

‘Sasa mbona anaonekana laini laini,hata akitembea, haiji akilini...tofauti na unavyosema wewe....?’ nikauliza

‘Ni laini kama mwanamke , hasa wakati anahitajika kuonyesha ua-nauke wake, unasikia sana, na akiwa kwenye ulingo wa walimbwende ni mrembo kama waridi likiwa linachanua kwenye kikonyo chake, , utasema hakuna mwanamke mrembo kama huyo,...ila my friend, she was a snake....mwenye sumu kali...’akatabasamu kama anavuta taswira.

‘Duuh, nimekufa...’profesa akajikuta akisema.

‘Nikuambie ukweli, ungelikuwepo enzi zake anaitwa binti mrembo kutoka Afrika ungelithibitisha hilo, ila sasa...mhh, akibadilika akiwa kwenye anga za ubabe, huwezi amini, ....akitoa kipigo ni kipigo kweli...’akatulia akigeuka kuangalia upande mwingine, mimi nikahisi nipo tayari kukamatwa, au huyo mama ameshafika.

‘Mhh, siamini maneno yako, ulijuaje... ulimjuaje...?’ nikamuuliza

‘Mama huyo, pamoja na urembo wake, ambao aliutumia kama chui ndani ya ngozi ya kondoo, kiukweli alikuwa mkorofi, muhuni,jambazi, aliyebobea...nahisi huko alipotokea alitokea chuo cha wababe wa kihuni walioshindikana...’akasema akicheza na fimbo yake ya ulinzi kwa sauti sasa ya kutulia kuwa hatanii.

‘Mhh, sijui, ...unachoongea na yeye ni tofauti...’nikasema nikiwa na mawazo mengi kichwani.

‘Hahaha,..ndio hapo, hata polisi wakashindwa kumweka kwenye kundi la majambazi,..lakini tuyaache hayo, kama unahitaji kumjua vyema nenda uliza polisi yoyote wa siku nyingi,. ...watakuambia,...wewe si uniamini, nenda huko kwa watu wa usalama, wana kumbkumbu zake...’akasema

‘Sina haja ya kwenda huk, kwani niende kwanza ananihusu nini mimi....’nikasema nikijifanya sina habari naye

‘Aaa, wewe si uniamini, mimi namfahamu tokea anaingia hapa...mimi ni mtu wa siku nyingi hapa,...namafahmu sana...usimuone alivyo hivyo, mwili kauachi achia,...alikuwa mrembo, ila urembo wake ulikuwa kama ulimbo kwa ndege, polisi wenyewe walijikuta wakihadaika naye....lakini...akafungwa, akatoka, na sasa ndio huyo...anakupa mizigo, mzigo yake ina alama ya shari...naogopa sana...’akasema

‘Polisi hawa hawa, walihadika, inaonekana unamfahamu sana huyo mama, je huko alipotokea ilikuwaje...? Akauliza profesa

‘Mwanaume hata awe vipi, mbele ya mrembo kama huyo anayejua ni nini anachokifanya, mhhh, utashikwa na kigugumizi, kiukweli  mdada huyo alikuwa moto...kwa urembo wake na alikuwa anajua jinsi gani ya kuigiza,..ulimbwende, kudeka pale panapostahiki utafikiri sio yeye..’akawa najionyesha kwa matendo.

‘Kwa mara ya kwanza, Ilikuwa sio rahisi kwake yeye kukamatwa kirahisi, na akikamatwa hakai muda, anatoka...ila baadaye, ndio akafungwa kwa makosa ya mauji ndipo alikaa muda mrefu jela,na huo jela, si unajua tena, akawa ni kama hayupo jela...’akasema

‘Na kweli aliua...akakamatwa?’ nikauliza tena kwa mashaka kama vile siamini, nilikuwa nahisi jamaa anatia chumvi..

‘Hahaha...kuuua, ...nimeshakuambia sio mara moja...achana na huyo mama, .....mimi naogopa sana nikisikia mzigo umetoka kwake, maana ukikosea maagizo yake ujue kama hutaumizwa, utakuwa kilema, na mara nyingi, utaomba ufe tu...huwa anakicheko chake cha shari, akikicheka, ujue damu inatoka......’akaniambia akionyesha uhakika wa anachokiongea

‘Mhh, hili sasa balaa...mimi najiuliza umemjuaje yeye....’akasema profesa akigeuka kuangalia mlangoni, kwani kuna mama mmoja aliingia anafanana sana na huyo mama wanayemuongelea.

‘Ni hayo tu..., nilikuwa nakueleza kile ninachokifahamu zaidi ya hayo nenda kamuulize mwenyewe, au kaulizie polisi, ...kama nakudanganya, na kama nakudanganya uje nikurudishie malipo yote uliyokuwa ukinipia.....kwaheri, nina wateja...’akasema akihangaika na watu waliofika kuingie kwenye hiyo casino.
Sikuweza kupata muda wa kumdadisi tena zaidi, nikaona haina haja, nikajikuta napitia kituo cha polisi, kuna askari mmoja namfahamu, nikamdadisi kuhusu huyo mama

‘Bado unafanya kazi kwake , maana huwa hakai muda mrefu na mfanyakazi mmoja?’ akaniuliza

‘Kwanini....?’ nikamuuliza

‘Kwanini!...huyo mama haamini watu, akikushuku unamchunguza, ni lazima atakufukuza, ...ana historia mbaya, lakini sasa katulia sana, huwezi kuamini ni huyo mama aliyekuwa akisumbuana na polisi,..nahisi huyo mume kambadili kama alivyodai kuwa atafanya hivyo...’akasema

‘Aliwahi kuua, kufungwa,...?’ nikauliza

‘Ndio hivyo,.... lakini binadamu hubadilika,...mimi mwenyewe sikuamini kuwa huyo mama atabadilika, lakini tangu atoke jela, na kukutana na huyo mzungu, sijasikia habari zake tena...’akasema huyo polisi

‘Mbona hafanani na hiyo tabia...?’ nikauliza

‘Hahaha kwa vile ni bosi wako sio,... mchokoze uone, ...hahaha, alikuwa akipigana na midume mitatu, na yote anaitoa makamasi, polisi wenyewe wakitumwa kwake, wanajiuliza mara mbili, tatu...achana na huyo mama , kama unafanyakazi kwake, uwe mwangalifu sana, ....kwani vipi, bado upo naye?’ akaniuliza

‘Hapana nimeona nitafute sehemu nyingine...’nikasema

‘Basi uachane naye kwa wema, kama ni kwa ubaya,..utakuja kujuta, ...atakufuatilia hata kama umejificha pangoni...’akasema huyo askari, na kunifanya moyo uanza kudunda kwa mapigo yasiyo yake.

********

Basi siku hiyo sikulala, nikikumbuka nilishampigia simu ya kutaka mshiko mwingine, nikawa sitoki ndani, na kila simu yangu ilipolia nikajua ni yeye,japokuwa sijawahi kutumia simu yangu ya mkononi, ..

Na kesho yake asubuhi, ndio akanijia nikiwa nipo mlangoni nimeshafungasha mizigo yangu nikitaka kuhama eneo hilo....patamu hapo,, siku hiyo alikuwa kaja kwangu kavalia mavazi ya chui chui, nasikia ndilo lilikuwa vazi lake enzi hizo akiwa na vikundi haramu. 

Ni vazi linalombana na kuonyesha maumbile yake ya mwili wake.

 ‘Tunaushahidi, ...jinsi ulivyochukua kumbukumbu zangu pale nyumbani, jinsi gani ulivyokwenda kuonana na dakitari aliyehusika ....ukamuhonga, akakupa baadhi ya stakabadhi,....na wapi ulikuwa ukipiga simu zako....’akasema na nilishangaa jinsi gani alivyopata hizo taarifa maana ni kweli, ndivyo nilivyofanya na maana hiyo ina maana kweli keshanigundua....

NB:Tuishie hapa kwa leo


WAZO LA LEO: Tabia ya mtu hujengeka toka utotoni, na ujanani ni kwenye vitendo na majaribio, ukubwani ni utekelezaji na hitimisho,..sasa tuweni makini kwa viongozi tunataka kuchagua, wachunguzeni walipotokea, maisha yao walipopitia, ubaya wa mtu huja kuonekana pale tu watakapopata, kwa hivi sasa wengi wao wamejifunika ngozi ya kondoo. Ukitaka kumfahamu mtu ngoja apate..
Ni mimi: emu-three

No comments :