Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, June 11, 2015

RADHI YA WAZAZI-1



‘Huyu jamaa hutaamini, ni msomi, na alijiweza kwani alifikia kumuoa mke wa kizungu., na alimuolea huyo mwanamke huko huko nje....’akaanza kuongea mzee mmoja.

Mzee huyo tulimkuta akiwa amekaa nje ya  nyumba ambayo inasemakana ni mali ya jamaa ambaye tulimkuta mitaani, mara akihubiri dini, mara anageuka kuwa mkufunzi, mwalimu, dakitari, lakini ghafla akabadilika na kuanza kushusha matusi , matusi mabaya tena ya nguoni.

Mimi na marafiki zangu ambao tulikuwa mitaani katika harakati zetu, za kusaidia wale ambao wana matatizo mbali mbali, tukakutana na huyu jamaa akiwa kazungukwa na watu. Sisi kwa nia njema, tukisaidiwa na wafadhili, tulianzisha kundi maalumu la kuwasaidia wenzetu walioharibikiwa kutokana na madawa ya kulevya, kuumwa, au kuharibikiwa na akili kwa hili au lile.

Kundi hili bado changa, kwani lilihitajia ufadhili, na tulipofika eneo hilo na sisi tukavutika kuona kinachoendelea, tukakaribia, japokuwa tulikuwa tunahitajika kukutana na baadhi ya wafadhili wetu, lakini hisi zikatuvuta tufike hapo tuone kinachoendelea

‘Tutachelewa jamani, huo unawezekana ni ugomvi, au ni hawa watu wanahubiri mabarabarani...’akasema mmoja wetu

‘Tuone kidogo, maana moja ya kazi zetu ni kuangalia shida za watu, huenda hapa tukakutana na mojawapo,...’nikasema

‘Shida hizo zipo nyingi muhimu ni wafadhili, na unakumbuka tuliambiwa tufike saa ngapi....’akasema mwenzetu, na mara tukasikia watu wakipiga makofi, mimi sikuwaangalai wenzanu nikajongea hadi kwenye ilo kundi la watu kuona kuna nini. Kilichotokea hapo baadaye kilitufanya tujikute tunaamulia ugomvi, na tukajikuta tukimbeba jamaa aliyeumizwa hadi kituo cha afya.

‘Huyu mtu wenu hajaumia sana....’akasema docta

‘Sasa ndugu tunaomba utupeleke nyumbani kwake....’tukamuambia jamaa aliyetusaidia kuamua huo ugomvi akisema anamfahamu huyo mtu

‘Nyumbani kwake sio mbali na hapa, twendeni niwapaleke...’akasema huyo mtu na tukaongzana na huyu jamaa aliyemizwa, kwa muda huo alikuwa katulia tu, hangei, na mguu kwa mguu hadi tukafka nyumbani kwa huyo jamaa aliyeumizwa.

**********
‘Ina maana jamaa huyu kachanganyikiwa, na ana matatizo ya akili...?’ nikamuuliza mwenyeji tuliyemkuta baada ya kujitamblisha na kusalimiana naye.

‘Ndivyo  ilivyo, kachanganyikiwa, ... ana matatizo ya akili.....kavurugukiwa...kwani kumetokea nini, maana kanitroka hata sijui katoka saa ngapi,....mmh sasa hata mimi yatanishinda,....’akasema huyo mzee tuliyemkuta hapo nyumbani.

‘Mliwahi kumpeleka hospitalini?’ nikamuuliza

‘Hahaha, ...matatizo hayo hayatibiki hospitalini, hata muende kwa bingwa gani huwezi kuyatibia matatizo kama hayo..’akasema huyo mzee akionyeshea kwa kichwa kumuelekezea huyo jamaa aliyepigwa huko mitaani

‘Kwanini, .....maana kama ni matatizo ya akili yana tiba yake au sio,....mzee labda tukumpe mfano hai,  sisi kuna watu kama huyu ambao tumewasaidia na sasa ni wazima kabisa, tatizo ni kuwa watu hawalichukulii maanani hilo tatizo, na wanachelewa hadi inafikia hatua mbaya,...’akasema mwenzangu

‘Na wengine wakiona ndugu yao anaumwa kama hivyo wanamficha, wanamzarau, badala ya kufuatilia na kuona jinsi gani ya kumsaidia,..wanamuacha tu anazidi kuathiria...’akazidi kuongea huyo mwenztu.

‘Sasa mlitaka mimi nifanye nini...?’ akauliza akionyesha kukerekwa.

‘Ujue mzee, tatizo kama hili ni sawa na magonjwa mengine tu, ukimuwahisha mgonjwa  yoyote kwenye tiba sahihi, ukafika  kwa wataalamu  sahihi, madocta bingwa, mbona wanapona tu, wapo wataalamu bingwa wa magonjwa ya akili, na wengine inabidi kufanyiwa upasuaji ikibidi...kutegemea na chanzo cha hilo tatizo...kuna wengine wanatakiwa kufika hadi India ambapo kuna wataalamu wanafanya upasuaji wa ubongo....lakini, ikibidi.....’akaendelea kuongea mwenzetu.

‘Hivi nyinyi mnanielewa lakini, mnafikiri mimi sina huruma na huyu mtoto, nimekwenda hadi kwa docta bingwa wa pale Muhimbili, kahangaika wee mpaka akanyosha mkono....India, india,...huyo acha ya huko  India, huyu alipelekwa  hadi huko Ulaya, lakini haikusaidia kitu...acheni bwana...huyo, ana matatizo makubwa ya kiasili....’akasema

‘Amelogwa...?’akasema mwenzangu na akatufanya tucheke

‘Aheri angelogwa, ningelijua moja, maana nawafahamu waganga wa kienyeji waaliobobea kwa watu waliofanyiwa hivyo..., mimi mwenyewe ni mganga wa kienyeji, lakini hapo nimenyosha mkono...ila nilichowaambia ni hicho hicho....’akasema akikatiza hayo maneno na kujinyosha kwenye kiti chake cha kunesa.

‘Kama sio kulogwa, kama sio ....basi tatizo nini, au anatumia, madawa ya kulevya...?’ nikauliza

‘Hata sigara hajawahi kuvuta huyo, niwaambie kitu, mkewe alikuwa hapendi harufu ya sigara kabisa, sasa hayo madawa ya kuleya angliwezaje kuyatumia, sana sana ni unywaji wa pombe zao za kizungu.....na hiyo sio sababu ya matatizo yake....’akasema

‘Kwahiyo ni ugonjwa wa akili wa kawaida, au sio..huenda basi hukufika kwa mtaalamu mwenyewe, hebu tuambie pale Muhimbili ulionana na docta gani...?’ tukamuuliza

‘Vijana naona hamunielewi...kwanza hapa nina njaa sijala...nimekuwa nikihangaika kumtafuta huu chizi..mpaka nimeshau kula chips zangu zimepoa,...karibuni....’akasema sasa kwa sauti ya kama kakasirika huku akifungua chips zake kwenye mfuko na kuanza kula.

‘Hapa nataka soda baridiiii...mmmh, alikuja jamaa mmoja ana matatizo yake nimemuagua kanipatia viseneti, ndio nimenunua hiki chakula, na huyo chizi nimemuwekea chake, akijisikia atakwenda kula, anajua kipo wapi,..lakini wageni..si unajua tena nyumba hii tunaishi kizungu....’akasema akiendelea kula.

‘Mzee sikiliza kama tulivyokuambia nia yetu ni kutaka kumsaidia huyu jamaa, maana anaonekana ni mtaalamu, ..mwalimu, msomi, kama tukimsaidia, tutakuwa tumesaidia taifa, nia yetu ni njema kabisa....’nikasema

‘Mhh mumeoana eeh, ni chizi msomi, ...lakini hivi niwaulize, kuna docta bingwa wa maradhi ya radhi ya wazazi ...’akasema huyo mzee  sasa akijifuta mdomoni, nasote tukashituka na tukajikuta tukisema

‘Radhi ya wazazi...??’  tukasema sote kwa pamoja

‘Mhh, hamjui eeh, niwaambie kitu nyie vijana , hasa nyie mnajiona mumekulia kwenye hii zama ya utandawazi, mnaona mambo yapo tu, ...mnasaahu hata asili yenu...hata kijiji mlipozaliwa hamtaki kufika, kisa  nini mumesoma...’akatulia

‘Haya na hata huo utandawazi hamjaufahamu vyema mnaiuingia kichwa kichwa..., hamjui wenzenu wamewatengenezea nini, hamjui lengo lao ni nini, ...mnafahamu wenzenu ni wajanja sana...’akasema

‘Akina nani....?’ nikamuuliza

‘Hao waligundua huo utandawazi,..nia yao kubwa ni kuwaharibu akili zenu,, kuwapotezea maadili yenu mema...mnaiga tu, kila mkiona jambo kafanya mzungu basi ni sahihi, mnafikia hata kutembea uchi, kuangalia mapicha mabaya ya kuwaharibu ubongo, wengine ndio hao wanabwia unga...’akasema na kunyosha mkono mbele,

‘Ina maana huyu anatumia madawa ya kulevya...?’ nikamuuliza

‘Hapana huyu hajawahi kufanya hivyo nina uhakika....’akasema na kumuangalia huyo jamaa akiwa bado kalala pale sakafunii ambapo alijilaza tulipofika naye hapo nyumbani.

‘Tatizo sugu ni kuwa nyie vijana, mumefikia kubaya, mnafikia kuwadharau hata wazazi wenuu waliowazaa eti kwa vile mumesoma, eti kwa vile mna kazi, eti kwa vile...mna cheo, mnawaona wazazi wenu wananuka, hawafai, hawana hadhi, .....nawaambia ukweli, hamna lolote mbele ya wazazi wenu...’akasema

‘Ni kweli mzee, mtu akisoma vyema, hawezi kufanya hivyo, ukiona mtu anafanya hivyo, hakusoma alikwenda kukariri tu shuleni, ili tu apate pesa, elimu humuongoza mtu atende mambo mema.na sahihi...’akasema jamaa yangu.

‘Hahaha, mema na sahihi,...hao wanaiba serikalini, haoo mafisadi..hawajasoma, hayo wanayofanya ni sahihi, ni mema....msitudanganye hapa...’akasema mzee, na tukaona kama anapoteza lengo letu.

‘Mzee tunataka kujua huyu ana tatizo gani....’akasema mwenzangu

‘Sasa mwenzenu huyo alisoma,alisoma kweli...na sio kukariri kama munavyodai nyie...watu wabaya duniani ni wasomi, niwaambie ukweli...hao ndio wanaiharibu dunia...hicha cha kusema kusoma ndio unatenda mema na ukweli sio sahihi...sasa huyo mwenzenu ni msomi kweli kweli..., uliza wasomi wanaomfahamu...hata mkewe alisema huyu alitakiwa kubakia huko majuu, kufundisha....’akasema

‘Kama mumewahi kumsikia huko mitaani, mtajua kuwa kweli alisoma...hajakariri kama mnavyodai..., lakini kisomo chake hakikuwa na maana, ...akashindwa kujua kuwa alizaliwa, ...namsikitikia sana, maana nimehangaika nimeshindwa, imefikia sasa ni kumuangalia tu..’akasema huyo mzee

‘Mhh, mzee, labda ungetusimulia maisha ya huyu jamaa tungejua nini kilimtokea ili kama yawezekana tuweze kumsaidia....’akasema mwenzangu mimi bado nikiwa nimeduwaa

‘Mhh jamani, hilo tatizo alilo nalo, watu wamehangaika, wameshindwa, mimi mweyewe nilihangaika nikamfikisha hadi muhimbili, ikashindikana, akapelekwa sijui wapi ikashindikana, hata mkewe ambaye sasa karudi kwao, alimpeleka kwao uzunguni ikashindikana akamrejesha hapa nyumbani... ndio huyo hapo....nimekwenda zaidi ya hapo, waganga wote wa kienyeji nimemaliza, nikaenda kwenye maombi, wakaomba mpaka wakaukwa na koo, hakuna kilichosaidia.......’akatulia huyo mzee

‘Samani kwanza, nikuulize, ina maana huyu jamaa mkewe alikuwa ni mzungu...?’ nikauliza

‘Ndio mkewe alikuwa ni mzungu, na walizaa naye watoto wawili, watoto wamechukuliwa na mkewe, maana angekaa nao angeliwaua, si mnaona kawa chizi...’akasema huyo mzee

‘Kwanini nyie ndugu zake msingeliwachukua hao watoto, hasa wewe baba yake mdogo...mnaacha watoto wanachukuliwa na wazungu?’ akauliza rafiki yangu

‘Baba zake wadogo...! hahaha, huyu hana baba wadogo, huyu hana mama, huyu hana baba,, na hakuwahi kuwa na ndugu..’akasema mzee, na kuzidi kutufanya tuingiwe na hamasa ya kukisikia kisa cha ‘kichaa msomi...’

‘Wamekufa au....?’ nikauliza

‘Huyu ni kichaa msomi, docta wa miondoka, msomi aliyekubuhu, anayejua kucheza mitindo yote ya muziki, hujasikia wakimuita,  ‘kichaa midundo,..’ au ‘kichaa style..’  kichaa miondoko....ana majina mengi kutegemeana na mazingiza.

‘Hahaha , msione nacheka, moyoni naumia sana, huyu ukikutana naye akiwa katulia hutaweza kuamini kuwa humu hazimo,...ni msomi kweli....lakini akishavurugikiwa masikini mwanangu....’akasema sasa akishika shavu..

‘Huyu, ukikutana naye akitembea, ukamwambia  kichaa style,...kichaa miondoko...basi anabadili mwendo, ana miondoka ya kila aina, anajua kucheza mziki mtindo wa kila aina, anajua kiingereza kuliko waingereza wenyewe....anajua mambo mengi, lakini...kikimcharukia, ni matusi, matusi makubwa makubwa tena ya nguoni.

‘Wasio mfahamu wanakimbilia kumpiga..nimekuwa nikitembea naye, nikimfuatilia kila anapokwenda, ili kumsaidia, watu wasimuumize., inafikia muda na mimi nachoka,.....tatizo hataki kukaa, hataki kutulia hapa nyumbani...unajua, anakwenda hata vyuoni kutaka kufundisha.....lakini kisimcharukie....’akatuliza huyo mzee

 Ni kweli aliyosema huyo mzee, maana siku tulipomkuta mitaani akiwa kavalia vizuri tu, alianza kuongea kiingereza safi kabisa, na akawa anatoa darasa kwa kiingereza na kutafsiri kwa Kiswahili akawa anaongelea mambo mengi, mambo ya uchumi, mara akamaliza, akaingia mambo ya vita baridi, jinsi Warusi na Marekani walivyokuwa wakipambana, akamaliza, akaanza kuongelea mambo ya sayansi ugunduzi mbali mbali jinsi ndege ilivyoguduliwa, au meli, au uguduzi wa madawa...mmh, wengi hasa wasomi wakamsogelea wakijua kuwa huyu ana PHD, na wengine waakaanza kunukuu

Haikupita muda, akapita mama mmoja,..mara yule jamaa akamgeukia yule mama, na kuanza kumporomoshea matusi, matusi mabaya mabaya ya nguoni, ....akiyaelekeza kwa akina mama, yule mama alikuwa hamjui, akaanza kujibishana naye, akimtukana pia,..oooh, akawa kajichongea, maana ilibidi mume wa yule mama kuingilia kati...akaaza kusaidiwa na wenzake na kuanza kumpiga huyo jamaa, wakati huo yule mama akiwa analia..., na sisi tukabakia tumeduwaa

‘Mhh, huyu jamaa vipi,....’mmoja akauliza

‘Hata sielewi, uliona jinsi alivyokuwa akishusha shule ya historia, shule ambayo, sijawahi kuisikia,...’akasema jamaa aliyekuwa karibu yangu

‘Acha hiyo historia, huenda kaogeza chumvi, lakii hiyo sayansi  aliyoiogelea hapo, utafikiri alikuwepo kwenye huo ugunduzi wa mitambo, madawa....hizo fomula zake...ooh, nimezimia, hajakosea kabisa...’akasema jamaa mwingine

‘Lakini mengine huenda anabuni tu, mimi sijwahi kusikia hayo aliyoyaongelea, ...ila mambp ya uchumi nayakubali, hapo aliifikisha kweyewe.....’akasema mwingine

‘Hiyo historia aliyoogolea hapo sio uwongo, hayo aliyoongea ni ukweli mtupu....yalitokea, na ukienda kwenye vitabu vya kumbukumbu kama eclospidia, utayakuta, ndivyo, ilivyo, mimi nafundisha masomo hayo chuo kikuu, nilipomsikia nilijua ni mmoja wa walimu wangu walionifundisha,...’akasema jamaa mmoja aliyevalia suti alikuwa ni mwalimu wa chuo kikuu.

‘Mhh, sasa mbona kabadilika ghafla tena, mumegudua kitu kabadilika ghafla pale alipomuona huyo mama, ...ulimuona alivyofanya, kwanza kaaza kuita , mama....mama, halafu yule mama alipokaa kimia,jamaa sijui kaoaa kazarauliwa, akaanza kutukana....hivi kweli mtu kama huyu hawezi kusaidiwa?’ nikauliza

‘Hapo ndio hata mimi nimeshangaa...huyu kweli aahitajia msaada....’akasema huyo mwalimu wa chuo kikikuu

‘Kuna tatizo....ni lazima tulichunguze hili tatizo, hili ni jembe jamani...’nikasema

‘Ni kweli hebu tufuatilie tulijue ni tatizo gani tuone kama tunaweza kumsaidia...’akasema mwenzangu ambaye tuliamua kuanzisha kampuni binafsi ya kujitolea kuwasaidia vijana na watu wazima waliotindikiwa au kuwa na matatizo ya akili, na kujaribu kuona kama wanaweza kusaidiwa.

Basi safari yetu ikatupeleka hadi sehemu ambapo tulikuja kuambiwa huyu jamaa ndipo anapoishi na hiyo nyumba tuliyoiona hapo ni nyumba yake mwenyewe.

Ilikuwa nyumba nzuri tu, nyumba ya kisasa yenye kila kitu, ni kwa uwani kulikuwa na bwawa la kuogelea la kisasa kabisa, wenyewe wanasema nyumba hiyo  ilijengwa kizungu.

Tulipofika hapo tukatafuta mtu wa karibu ndipo tukakutana na huyo mzee, akajitambulisha kuwa  yeye ni baba yake mdogo, baba ambaye aliamua kumsaidia, zaidi  ya huyo baba hakukuwa na mtu mwingine.

‘Kwahiyo wewe ni nani kwake..?’ nikamuuliza

‘Mimi ni baba yake mdogo,...’akasema

‘Ehe, hebu tuambie, ilikuwaje, je huyu jamaa hana wazazi kweli, kama ulivyodai, kuwa hana baba, hana mama ,...na hana ndugu kweli, sasa wewe imekujaje kuitwa baba yake mdogo wake....’tukamuuliza na mzee huyo akatulia kama anawaza jambo, huku akimuangalia jamaa yetu aliyekuwa kalala, baada ya kupokea kipigo cha watu, watu ambao walikuwa hawamfahamu, .

NB:Kisa ndio kimeanza hivyo,..baada ya ule utangulizi, kama hukuwahi kuupitia utangulizi bofya hapa http://miram3.blogspot.com/2015/06/radhi-ya-wazazi-utangulizi_5.html

Bado hatujafanikiwa kupata wafadhili,na sehemu ya kujishikiza ili tuweze kumudu gharama... lakini nimeona nisikae tu, nitajitahidi hivi hivi kutoa visa vyetu, na mungu yupo pamoja nasi tutakuja kufanikiwa .


WAZO LA LEO: Watiini wazazi wenu, waheshimuni wazazi wenu, na wasaidieni wanapofikia utu uzima, na hata kama hawajiwezi kwasababu hii na ile, msiwanyanyapae, mkawatenga, mkawakataa, maana hamjui jinsi gani walivyoteseka kwa ajili yenu, ogopeni radhi ya wazazi, kwani akifikia hatua ya kuitoa, ujue radhi hiyo haina dawa, na si lazima atamke, .....hala hala, vijana, halahala wapendwa, ogopeni radhi ya wazazi.

Ni mimi: emu-three

No comments :