Basi mtoto akaambiwa aitwe ili picha ya pamoja ipigwe, lakini aliyetumwa akarudi na taarifa ya kushitua, akasema
‘Mtoto haonekani…’
‘Umemwangalia huko alikokuwa akicheza na wenzake..’ akauliza nesi
‘Kote nimeangalia na nimewauliza wenzake wanasema hawajui wapi mtoto ameenda..’akasema
‘Atakuwa kaenda wapi naye hana tabia ya kutembea mbali na hapa
nyumbani..’akasema mama wa kufikia alipopewa hiyo taarifa.
Mtoto kaenda wapi...
Tuendelee na kisa chetu
*************
Wakati wanahangaika huku na kule kumtafuta mtoto mara simu ya nesi ikaita, nesi kwa haraka akaichukua akijua huenda ni watu wamempata huyo mtoto, lakini alipotizama akakuta ni simu ya bosi , moyo ukamlipuka akijua sasa tatizo limefika kubaya, atasema nini kwa mabosi wake,..akajipa moyo na kuanza kuongea;
‘Halloh bosi, mambo huku sio shwari, maana
mtoto haonekani, na tumejaribu kumtafuta kila mahali lakini haonekani
kabisaa,…yeye alikuwa akicheza na wenzake nje, wakati sisi tupo na wageni…’
nesi akawa anaelezea huku akiwa na wasiwasi sana
‘Mimi sikuelewi nesi, maana
unakumbuka tulivyoondoka hapa niliambiwa kwa msisitizo na wewe mwenyewe uliomba
iwe hivyo na hapa utawala umekuamini kwa hilo kuwa takuwa salama, na mimi nilipofika
huku nimewahakikishia kuwa mtoto yupo salama, sasa unaniambia habari kama hiyo, unafikiri
mimi nitawaelezeje utawala…’ akasema docta akionekana kukasirika.
‘Bosi haikuwa nia yetu,
kwakweli tulijua hakuna matatizo kabisa…sasa sijui tufanyeje, naona tukatoe
taaarifa polisi ,…; akasema nesi. Kwa vile usiku ulishaingia ikabidi wasubri
kesho huku kila mmoja akiomba mtoto awe kwenye mikono salama, na waliomba huyo
mama mwenye mtoto asitokee.
‘Oh hata sijui nikuambie nini….maana
nilipofika hapa tu cha kwanza kuulizwa ni hicho na wakanipa angalizo kuwa mtoto
huyo anatakiwa kulindwa sana….oh, nimechoka…’akasema docta
‘Unajua nimechoka…maana yule
mama naye hajapatikana hajarudi , hatujui kapotelea wapi , sisi tulijua yupo
huko, …hawa watu niliwaambia akirudi hapa wasimruhusu kuondoka, lakini
hawakufanya hivyo….yaani, hata sijui,….’akasema docta
‘Ndio imeshatokea hivyo docta,
tufanyeje maana hata mimi sijui la kufanya..nikatoe taarifa polisi..natakakibali
chenu, nisije kutoa taarifa kumbe sio sahihi…nifanye hivyo?’ akauliza nesi
lakini akahsi simu ipo kimia, kumbe mawasiliano yyalishakatika, bosi wake
hakuwepo hewani, labda aliamua kukata simu au ni mawasiliano mabovu.
‘Docta, bosi….oooh’akajiukuta
anaongea peke yake…simu haikuwa hewani.
Nesi baba mwenye nyumba na mama
mwenye nyumba na baadhi ya wanafamilia wakakutana kikao cha dharura kujadili la
kufanya huku wengine wakiendelea kutafuta.
‘Tuendelee kutafuta, kwani hata
sasa hivi ukienda polisi, watakuambia msubiria masaa 24, ….’akasema mjumbe
Baba mwenye nyumba pamoja na
kutokupendelea hilo, lakini akajitahidi na wakazi wote majirani wakawa
wanahangaika huku na kule kutafuta wapi huyo mtoto yupo , lakini hadi usiku wa
saa sita hakuna kilichopatikana, ikabidi walale, wakiomba mungu..
Asubuhi kazi ikawa kwenda
polisi na wengine wakitafuta huku na kule wakijaribu kuulizia watu
wengine hadi vijiji vya jirani, lakini hakuna aliyekuwa na taarifa yoyote
kuhusiana na huyo mtoto, na hata polisi walipokuja na kuulizia waliishia
kusambaza taarifa kuwa kuna mtoto kapotea kama kuna mtu kamuona mtoto
mwenye sifa hizo wawataarifu polisi na picha yake ikasambazwa, lakini
haikusaidia kitu mtoto akawa hapatikani.
Siku tatu, ya nne, ikaingia siku ya tano,
hakuna cha mtoto wala taarifa ya huyo mtoto…
‘Lakini hata hivyo leo ni siku
ya tano, hakuna taarifa ya huyo mtoto, na hata huyo mama hajulikani wapi alipo,
ina maana yule mama naye kapotea au kaenda wapi…?’ akauliza mkuu dakitari mkuu.
‘Yaani hapo ndio inashangaza ,
maana haiwezekani yule mama akae siku zote hizo bila kurudi kumtafuta mtoto
wake..’akasema docta mwingine.
‘Kwa hali hiyo tunaweza kuhisi
kuwa huenda huyo mama yupo na huyo mtoto…’ akauliza docta mkuu, wakiwa kwenye
kikao maalumu cha kutafakari kupotea kwa mtoto, aliyekuwa kwenye mamlaka yao na
mgonjwa, yaani huyo mama.
‘Tunaweza kuhisi hivyo lakini
haina uhakika, kitu cha kujiuliza huyo mama alifika muda gani huko kijijini, na
kusitokee hata mtu mmoja kumuona…’akasema docta mkuu
‘Hapo ndio tunashangaa, maana
polisi wamehoji watu mbalimbali, watoto waliokuwa wakicheza naye,…na kutangaza,
kutoa picha, lakini hakuna aliyewahi kumuona huyo mtoto au huyo mama
‘Mhh, hili ni tukio la aina
yake, maana ni siri, siri…mambo ya huyo mama ni ya kiajabu ajabu, na ..hili
tena linabakia kwenye historia ya kazi kwenye hospitali hii…’akasema docta mkuu
‘Huyo mama, sitamsahau….naombea
siku nikutane naye tena..’akasema docta aliyekuwa akimtibia huyo mama
‘Mimi wala sitaki, …kama ni heri
basi yaishe kwa heri tu….imenipa wakati mgumu sana..’akasema docta mkuu
‘Pole sana mkuu, ndio kazi,…’akasema
mwenzake
‘Hata hivyo, tunahitajika kukaa
na nesi na familia yao, ikibidi baba mwenye nyumba, atusaidia tufike huko kwa
huyo baba wa huyo mtoto…’akasema
‘Mhh, polisi wamefika huko,
hakuna mtu kaam huyo…wanasema huyo mtu alipotea zamani sana..’akasema mtu wa
usalama wa hapo hospitalini
‘Hana hata ndugu wengine?’
akauliza
‘Wapo, ndio wamesema hivyo,
wanasema wao walishahitimisha kuwa ni marehemu,kwahiyo hawana la kufanya..’akasema
huyo mtu wao wa usalama
‘Unaona eeh, huyo mama ni kama
katokea hewani…na familia za huyo mama?’ akauliza
‘Hata zenyewe zilihama eneo
hilo, na haijulikani walihamia wapi, walihama wakimuogopa huyo jamaa kwani
wanasema aliapaapa kuwa atawafanyia kitu kibaya hiyo familia, …’akasema
‘Kwanini..?’ akauliza
‘Wanavyosema familia hiyo
ilikuwa inadaiwa sana na huyo mtu, yaani baba wa huyo mama, na ikatokea
mtafaruku, kutokuelewana, na haijulikani wapi huyo mama alipotoelea, huyo jamaa
akadai familia hiyo ndio imefanya hivyo, kukawa na vita vya familia hizo mbili,
…sasa ikatokea ghafla huyo jamaa akapotea, kutokana na mke wake mdogo..’akasema
‘Ina maana alikuwa na mke
mwingine?’ wakauliza
‘Ndio wanadai mke mdogo ndiye
aliyefanya mke mkubwa kupotea kiajabu…japokuwa haikuwa wazi…ila sasa ndugu wa
mke huyo mdogo, na wao si o mchezo, wakajenga kisasi na huyo baba wa huyo
mtoto, …ikawa ni vita, jamaa akapotea, na kipindi hicho huyo jamaa sio tajiri
tena..’akasema mlinzi
‘Ilikuwaje alifirisika..?’
ikaulizwa
‘Ndio alifirisika akawa na hali
mbaya, hata matatizo hayo yanatokea hakuwa na kitu, kwahiyo alikimbia akijua
hana kitu nyuma..’akasema
‘Na huyo mke mdogo anasemaje
kuhusu kupotea kwa mke mkubwa
‘Huyo mke mdogo aliolewa tena,
na hajulikani wapi alipoolewa, kwani walipoona na mume wake wakahama hapo…’akasema
‘Hakuna cha kutusaidia hapo…’akasema
docta mkuu
Hutaamini mwezi ulikatika na
hakukuwa na taarifa yoyote ya mtoto aliyepatikana au kusikia mtoto anayetafuta
wazazi wake au kuonekana mtoto akitangatanga. Mwishowe watu wakakata tamaa na
kusubiria kama huyo mama atarudi kuulizia tena huyo mtoto wake.
NB: Nimetoa sehemu hii fupi, sehemu
hii inaendelea lakini wenye kampuni wameshafika wanataka makabidhiano ya ya
vitu vyao nk…si mnajua tena mwisho wa mwezi huu sitakiwa kuwa hapa tena, …Yote
maisha..tutaonana nikiweza kutulia, hata kesho naweza kuendelea na sehemu hii
WAZO LA LEO: Ubaya
mfanyie mwenzako, na wakati unafanya unaweza kuona ni jambo la kawaida tu, kwa
vile unaona ni sahihi, unawajibika, …hata kama unafanya sivyo ndivyo, ilimradi
unatimiza hicho unachoona ni sahihi. Uongozi, dhamana za utawala una uadilifu
wake, na jambo kubwa ni kuhakikisha unatenda yaliyohaki, kwa uadilifu na sheria
lakini pia kwa hekima. Tujue kuwa dhamana ni deni, na uadilifu katikautendaji ni
ngao ya maisha yako ya baadaye, ukitenda vibaya utajiwekea maisha yako katika
mashaka na uadui..ukumbuke uliyowatendea wenzako na wewe yatakukuta hivyo
hivyo.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment