Na
wakati wanaongea nini kifanyike zaidi simu ya nesi ikaita ghafla na namba
iliyoita ni namba ngeni kwenye simu ya huyo nesi, akaiweka hewani ili kusikia
ni nani kampigia.
‘Halloh wewe ni nesi , ndugu yake….’ sauti
ikawa inasema kwa kukatikakatika, mawasiliano yalikuwa sio manzuri, nesi
akasema;
‘Ndio mimi nesi wewe ni nani, na unapiga
simu kutoka wapi?’ akauliza nesi
‘Mimi napiga simu kutoka kijiji kwenu, ni
jirani na ndugu zako, wanasema uende nyumbani kwa dada yako haraka
iwezekanavyo…’ simu ikawa imekatika na hata walivyojaribu kupiga tena ikawa
haipatikani.
Tuendelee na kisa chetu..
***********
Basi msafara ukaondoka, docta nesi mlinzi na mtoto kuelekea
kijijini, ilibidi wamchukue na mlinzi
kwani madocta walihisi huyo mama huenda atakuwa kaelekea huko kijijini, kwahiyo
walihitajia mtu wa kusaidia kama atalet fujo. Njiani waliongea ya kawaida,
hawakutaka kuliongelea jambo linalowakabili, hawakutaka kumtia mtoto kitu cha
kujiuliza, japokuwa walijua kuwa huyo mtoto bado ni mdogo.
Na mara kwa mara nesi alikuwa akijaribu kupiga simu, kuwapigia
ndugu zake huko kijijini, lakini simu hazikuweza kupatikana, hakukuwa na mawasiliano
kabisa. Na docta alipoona nesi anahangaika kupiga simu mara kwa kwa mara
akasema;
‘Mimi nahisi hakuna tatizo kubwa sana huko kijijini kwenu...kama
kungekuwa na tatizo ni lazima wanekupigia simu tena…’akasema docta
‘Sasa kwanini simu zao zote zisifanye kazi, na kwanini mtoa huo ujumbe
kuwa ndugu zangu wana matatizo awe ni
mtu wa jirani, ndio kina nitia mashaka...’akasema nesi
‘Hiyo isikutie shaka nesi,…nahisi simu zao hazina chaji,.. nina
wasiwasi na umeme, ukumbuke siku mbili sasa hakuna umeme hata huku mjini
tunatumia generator..., sasa inategemea kuwa simu ya mtu aliichaji lini…’
akasema docta.
Walifika eneo la kijijini, kwa vile huyo docta, hakuwa mwenyeji
sana, ilibidi nesi awe anamuelekeza
docta njia gani apite hadi wakafika nyumbani kwa dada yake, na walipofika
kwenye hiyo nyumba, nesi kwa haraka akateremka kwenye gari na kukimbilia ndani.
Nesi haakujali kuwa yeye ni mwenyeji na ana wageni kaja nao,
alichojali kwa muda huo ni kutaka kujua kama kuna tatizo lolote hapo nyumbani,…akawaacha
wageni wakiwa ndani ya gari yeye akateremka, na kuelekea mlengoni mwa hiyo
nyumba.
Kulikuwa kimia tofauti na alivyozoea, utafikiri kumehamwa, akahis
ni lazia kuna jambo limetokea, akausogelea mlango,akataka kugonga, akasita,….
Hakugonga mlango tena
akaamua kupiga hodi ;
‘Hodi wenyewe mpo….’akasema na kukawa kimia, akageuka huku na
kule, akitarajia kumuona yule mdada , mfanyakazi wa hapo, hakukuwa na cha
mdada, wala mtu yoyote zaidi ya kuku, waliokuwa wakikimbizana huku na kule.
‘Hodi jamani, dada,…..’akasema
na baada ya muda mlango ukafungulia, na hapo akapumua kidogo,
..aliyefungua mlango alikuwa ni shemeji yake,…dada yupo wapi!?,
Moyo ukamdunda tena, …dada yupo wapi,… wasiwasi ukamrudia tena, aliogopa
hata kuuliza, kwani mara nyingi anapofika hapo nyumbani mtu anayekuja kufungua
mlango ni dada yake au mfanyakazi wa hapo, lakini…leo aliyefungua mlango ni
shemeji, na usoni anaonekana mwenye huzuni…mwenye wasiwasi….
‘Kuna usalama hapa shemu, maana nimepokea simu yenye utata kutoka
kwa jirani, …hebu nitulize moyo wangu kwanza, dada yupo wapi…?’ akauliza huku
anatizama huku na kule.
‘Dada yako…?’ shemeji yake naye akawa kama anauliza swali badala
ya kujibu, na kumzidishia mwenzake shinikizo la moyo.
‘Ndio shemeji, dada yupo wapi, mbona kimya, na…yeye haonekani,
kuna tatizo gani…?’ akauliza mdogo mtu akitaka kupita kuingia ndani lakini
shemeji alikuwa kasimama mlangoni, kama vile anazuia mdogo mtu asiingie,
baadaye akasogea kumpisha apite, na nesi kwa haraka akaingia ndani, na shemeji
yake akamfuata.
‘Kwanza nambie ….huyo..kich---a, huyo..mpo na nani?’ shemeji
kauliza akiangalia lile gari, kwa kupitia mlangoni, hakuweza kumalizia maneno
yake.
‘Shemeji,…dada yupo wapi..?’ nesi akauliza kwa ukali mpaka shemeji
yake akashituka na kumuangalia shemeji yake akajibu;
‘Dada yupo ndani kalala, hajisikii vyema,….nimerudi kazini
kuhakikisha hasumbuliwi,….amelala, tumeche apumzike, najua akisikia sauti yako
ataamuka..’akasema
‘Anaumwa…?’ akauliza.
‘Haumwi,..ila kuliko na vurugu hapa, vurugua ikamletea dada yako
kudondoka akapoteza fahamu, ikawa mshikeshike…’akatulia
‘Mhh dada ana nini, unajua ilitokea kule hospitalini..lakini
alizindukana kwa haraka, akasema hakuna tatizo…hivi mumeshakwenda kupima,…’nesi
akauliza kwa akionyesha mashaka fulani.
‘We acha tu…’akataka kuongea na kuaksikiak mlango wa gari
ukifunguliwa nje, na kufungwa, nesi akakumbuka kuwa ana wageni, akasema;
‘Oh, unaona nimekuja na wageni,…shemeji kuna wageni nimekuja nao,..’akasema
nesi akatoka nje kuwakaribisha na wageni na shemeji yake akamfuatia nyuma, ni
kama vile hakutaka shemeji yake aingie ndani ya kumuamusha ndugu yake.
‘Karibuni wageni..’akasema nesi, na wakati huo walishateremka nje
ya gari, wakiwa wamesimama, na docta alikuwa akinyosha,na upande wa pili wa
gari alikuwa kasimama mlinzi akiwa kambeba mtoto.
Shemeji mtu alipomuona yule
mlinzi kambeba mtoto, akamgeukia shemeji yake ambaye alikuwa kasimama kati kati
yao, yaani shemeji yupo nyuma, na mbele wapo hao wageni, akasema;
‘Yule mtoto wa-na-ni…ni yule mtoto mumemlata tena…?’ akauliza
lakini nesi hakumjibu akawakaribisha hao wageni waingie ndani,na shemeji mtu
akabakia kasimama mlangoni, anashindwa kuwazuia wageni.
Nesi akamchukua mtoto na kuelekea chumba ambacho akiwemo ndicho
anakitumia, akafungua na kwenda kumlaza huyo mtoto, baadaye aakrudi, na
aliporudi tu, shemeji mtu akasema.
‘Mbona-mbo- tena mnaniletea balaa hapa nyumbani kwangu. mngelijua nini kimetokea muda uliopita
msingediriki kumleta huyo mtoto humu kwangu. Shemeji yako kafikia kupoteza
fahamu kwasababu za kizembe..’akatulia
‘Kwani kulitokea nini..?’ akauliza nesi
‘We acha tu, kulizuka ugomvi hapa, ugomvi huo ungeliweza
kumsababishia mke wangu mambo mengina….’ Akasema shemeji mtu na kabla
hajamaliza nesi akamkatisha.
‘Kwani dada ana matatizo gani...?’ akauliza nesi huku akiangalia
mlango wa chumba wanachotumiwa wanandoa hao.
‘Unakumbuka safari yetu ya mwisho kuja kwako, tulikuambia kuwa
tumekuja na jambo la furaha, lakini ukatuletea habari zako za huyo mwanamke
balaa, ukaharibu furaha yote tuliyokuja nayo, na tukasahau hata kukuambia nini
dhumuni la safari yetu…’akasema shemeji yake
‘Mhh ni kweli ...jamani hata sikumbuki maana matatizo ni mengi,
yaani hata kuja hapa bado tumekuja tukiwa hatuelewi, matatio yanaongeeka kila
siku....’akasema nesi akigeuka kuangalia mlango wa chumba kama dada yake
atatokea
‘Kiukweli dada yako hanisikii...siwezi kusema ana matatizo makubwa
sana ni ya kawaida tu,najua keshakuambia…ila anahitajika kupumzika sana kama
alivyoshauriwa…ndio maana namshauri dada yako asijiingize kwenye vurumai au
kwenye matatizo yatakayomletea shinikizo la damu, lakini hanisikii, alivyokuja
huyo kichaa, ndio basi …’akasema huku akionyeshea kwa mikono.
‘Kichaa, kichaa huyo ni nani, ni-ni....yule mama kaja huku....?’
akauliza docta ambaye alikuwa kimia, hakutaak kuingilia maongezi ya wawili hao
kwanza, lakini aliposikia kuwa kuna kichaa, akajikuta akiingilia na
alimuangalai shemeji mtu, na shemeji mtu akawa katulia hakusema neno, na docta
akamgeukia mlinzi na kusema;
‘Nilijua tu...’na mlinzi akawa anatabasamu kuashiria kuwa hata
yeye anasadiki hilo mlinzi
‘Yaani nyie acheni tu...sikutaka kabisa huyu mtu aingie hapa kwangu,
lakini dada yako akamuonea huruma akamkaribisha, hata nyie mlipofika na kugonga
mlango, nikajua ni yeye tena karudi, ...ndio maana nikakimbilia kufungua,
nipambane naye,.....ni kwanini mkamruhusu huyo mtu kuja huku, kaja mangua ya
huko hospitalini…’akauliza shemeji mtu sasa akimuangalai docta.
‘Mhh, aliwezaje kufika huku kwa muda mfupi, alitumia gari gani,
kapatia wapi nauli...?’ nesi akauliza na kumfanya docta abakia kimia.
‘Mhh mimi sijui ...mimi ninachoangalia na kujali ni huyu nduguu yako,
yeye hanielewi,... Jamani mimi nimeshasema simtaki huyu mwanamke hapa nyumbani
kwangu, kwanini mkamuachia kuja huku? ....’akauliza akimgeukia docta na docta
kabla hajajibu nesi akaingilia kati.
‘Alipofika hapa alisema anataka nini..?’ akauliza nesi, na shemeji
akamgeukia nesi na kusema;
‘Anasema eti kaja hapa kumchukua mtoto wake, anadao mtoto wake
yupo hapa kwangu….eti kakumbuka kila kitu, kwahiyo tusimdanganye…’ Akasema .
‘Hebu shemeji tuambie ilitokeaje…mpaka dada apoteze fahamu ,
kwanini, huyo mama alipigana na dada, au ilikuwaje, na huyo mama yupo wapi..?’
akauliza nesi
‘Huyo mwanamke mimi sijui kaenda wapi, na sina haja ya kujua, ila
alipofika hapa alianza kubwata kuwa amejua kabisa kuwa mtoto wake yupo hapa,
akaanza kutafuta huku na kule utafikiri yupo nyumbani kwake... ‘akasema
‘Alipofika alikukuta wewe upo nyumbani?’ akauliza
‘Nilikuja kwa bahati tu, dada yako alikuwa akijisikai vibaya,
nikaja kuangalia anaendeleaje. Na wakati nafika, dada yako alikuwa kwenye
mabanda ya kuku, nikawa nimekaa ndani nikimsubiria mara nikasikia hodi..’akatulia
‘Mtu kapiga hodi na moja kwa moja yupo ndani, …namtaka mtoto
wangu, najua yupo hapa…kaingia huku katoka kaingia huku katoka, nikaona sasa
huyu ananitafuta ubaya, ikabidi mimi nimzuie, akaanza kugombana na mimi,na mara
mke wangu akatokea kutuamulia.
Katika heka heka hizo za kutuamulia, mke wangu akasukumwa na huyo
hayawani, wewe…alinigusa pabaya, nilitembeza mkongoto, mpaka yule mwanamke
akadondoka chini, nilijua nimeua, lakini mwanamke yule ana roho ya paka, alikaa
kidogo akaiunuka na kuanza kuandelea kudai kuwa anamtaka mtoto wake...’
‘Una maana ukampiga mama wa watu , shemeji nawe, mtu mwenyewe bado
mgonjwa, unapiga utafungwa..’akasema nesi
‘Waje wanifunge, mtu ataingiaje
nyumbani kwako na kuanza kutafuta chumbani wapi..kama kwake vile..siwezi
kuvumilia, ..’akasema
‘Alipofika unasema alikuwa na vazi la hospitalini,..alikuwa
kajifunika uso wake?’ akauliza mlinzi
‘Atajifunua,…hahah ili muone hiyo sura yake, hatamaniki …’akasema
na akawa kama anawaza jambo
‘Kwanini, kwani ulishawahi kumuona sura yake..?’ akauliza docta.
‘Huyu mwanamke alipokuja hapa bado alikuwa hajanitambua vyema,sijui
kama mnavyosema alikuwa kapoteza kumbukumbu…lakini tulipoanza vurumai, akawa
kama kaniambua, akabakaia kaduwaa…’akasema
‘Shemeji kukutambua kama baba wa nyumbani au?’ akauliza nesi.
‘Unajua ile kuduwaa, kama vile umeona mzuka au kitu gani, ndivyo
ilivyotokea kwa huyo mama,..nahisi sasa kanikumbuka…’akasema na docta nesi na
mlinzi wakawa kimia .
‘Ghafla, eti… ananisogela na kupiga magoti mbele yangu eti
akiniomba msamaha ya kuwa haikuwa kusudi lake. Nilitamani nimmalize,
kwahasira…nilijikuta nikikivuta kile kitambaa alichojifunga usoni, na kubakia
uso wazi…’akasema
‘Mungu wangu….shemeji, ..’akasema nesi.
‘Hutoamini mke wangu siku zote alikuwa hajawahi kumuona huyo
mwanamke akiwa wazi kiasi hicho, hata hivyo yeye hamjui vyema kuwa ni nani.
Lakini mke wangu alipomuona jinsi mwanamke huyo alivyoiharibika uso akataka
kukimbia,…ulikuwa mshituko mkubwa sana kwake, ndio akadondoka na kupoteza
fahamu.
Nikawa nahangaika na mke wangu, sikuwa na mawazo na huyo mwanamke
tena, ….kabla sijafanya mpango wa kumpeleka hospitalini, ndio akaja jirani,
simu zimezima hazina chaji, nikamwambia anisaidie tumpeleke hospitalini, nahisi
ndiye akkupigia simu kukusumbua bure…’akasema.
‘Hebu kwanza, samahani niingili kati kidogo..’akasema docta
‘Huyo mama yupo wapi?’ akauliza docta
‘Sijui…’akasema shemeji
‘Shemji unasema sura ya uso wake, imeharibiwa, si ni yale mapanga
alikatwa katwa na wale wahuni waliomungilia siku hiyo walipochoma nyumba
moto,au..?’ akauliza nesi.
‘Sijui….’akasema sehmji kama vile hataki kumuongelea huyo mama.
‘Kwani shemeji hukumuuliza vyema kuhusu yaliyomkuta hadi
kuharibika huo uso… ‘akauuliza nesi, na wakati huo docta naye akauliza swali
jingine.
‘Hakuna mtu aliyejua wapi kaenda..?’ akauliza docta.
‘Niwaambia kitu sitakii kuongea kuhusu huyo mama hapa nyumbani
kwangu, simtaki, na nilishamsahau…kwanini anazidi kunitesa..’akasema
‘Ina maana shemeji ulikuwa ukimfahamu huyo mama kabla…na huenda
unajua kwanini aliharibika huo uso, kuacha hilo la kukatwa katwa na mapanga, au…’
akauliza docta.
‘Aliharibikaje huo uso …mimi nitajuaje…?’ akauliza shemeji, sijui
kwanini alirudia hilo swali, lakini nahisi kuna kitu kilikuwa kikimkereketa
moyoni, ingawaje matamshi yake baadaye yalionyesha tofauti.
‘Mimi kuharibika kwake huo uso hakunihusu na kwanini
nimuulize,…ili iweje?’ akawaangalia nesi docta na mlinzi kwa zamu.
‘Lakini ulikuwa ukimfahamu kabla…?’ akauliza docta
‘Ndio namjua sana huyo
mwanamke, namjua sana kipindi akiwa msichana, namjua toka utotoni, namjua
….hadi siku ile aliponisaliti. Huyu mwanamke alikuwa mchumba wangu…’ alapotamka
hapo kila mtu aliguna.
NB: Jamani nipo kwenye mitihani, mitihani ya kimaisha, najaribu
kupambana nayo, lakini akili haijawa sawa , naombeni niishie hapa kwa leo
WAZO LA LEO: Mara nyingi migomo ikitokea wanaoathirika ni raia wa kawaida,
unapoigomea serikali kwa matakwa mbali mbali,…ni nani anaumia? Tuchukulia mfano
halisia mgomo wa madocta, wameigomea serikali, wanaoumia ni nani,…haya leo hii
kuna mgomo wa madereva wanaigomea serikali, ni nani anaumia…Ni yale yale ya
wanapogombana mafahali wawili, zinazoumia ni nyasi, au sio..nyasi ni nani? Sasa
ni wakati wa raia kujua wao ni nani katika nchi, na wanapochagua viongozi wao
wajue kuwa mwisho wa siku matatizo yakitokea wao ndio wahanga. Uchaguzi
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment