Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, May 1, 2015

NANI KAMA MAMA-70





Kwa wanaofuatilia kisa wakumbuke kuwa kisa hiki nasimuliwa na rafiki yangu, na mapaka hapa tulipofikia rafiki yangu huyu anasimulia jinsi alivyosimuliwa na mama yake, kwani hayo matukio ya nyuma yeye alikuwa mdogo na hakujua ni kitu ani kilitokea, yeye hakuwa anamjua mama yake huyo

Sehemu iliyopita tuliishia kwenye swali `Je kuna nini huko…’’ ,

Rafiki yangu anayenisimulia kisa hiki alipofika hapo aliangalia saa yake, na mara akasimama, wakati mimi najiweka sawa kusikia jibu la swali hilo. Cha ajabu  Nikamuona rafiki yangu akisogeza kiti nyuma, na kujikunguta mapajani kuondoa vitu vilivyodondokea kwenye suruali yake, halafu akainuka kama anataka kuondoka, mimi nikayulia nikimuangalia.

 Nikajiuliza anataka kwenda kujisaidia nini, kwani kauli yake ya mwisho alivyoitamka, nilijua kabisa kaitamka ili kunogeshea kisa, kumbe ilikuwa kauli ya kuhitimisha na kuniacha roho juu. Sikukubali…kwani nilikuwa na hamu ya kujua nini kilitokea nikasimama haraka kumzuia.


‘Vipi ndugu yangu mbona unaondoka wakati hujafika mwisho wa kisa hiki, na mkasa wa maisha ya mama yako…’ nikamwambia na yeye akatabasamu halafu akakunja uso kuonyesha ishara ya huzuni. Akasema....

‘Mjumbe, sehemu iliyobakia ….mmh, nashindwa kuendelea nayo kwasasa kwababu ni sehemu inayonitia huzuni sana , na sikupenda kumsimulia mtu yoyote, kwani ni sehemu ambayo nilikuwa nimeshaanza kuelewa.. , ingawaje nilikuwa bado mdogo, lakini kumbukumbu za nini kilitokea, zipo akilini, kwakweli maisha yalivyokuwa yalikuwa ni shida, taabu, unyanyaswaji na…huwezi amini.... naona niishie hapa tu...’akasema

‘Hapana, hujanielezea kulitokea nini baada ya nesi kupokea simu kuwa nyumbani kwa dada yao kuna matatizo aende huko haraka, je wakubwa zake walimruhusu ….je aliondoka na mtoto, na kulionekana kama vile maakitari wanahisi jambo, kuwa mtoto hayupo, ilitokeaje...?’ nikamuuliza, nay eye akakaa kimia kwa muda, na sikumpa nafasi nikaendelea kumuuliza

‘Na huyo mama haonekani, kaenda wapi na je huyo mama ndio huyo mama yako au kulikuwa na mama mwingine kajiigiza kama yeye, maana hospitalini hayupo, na haijulikani alipokwenda, au…?’ nikamuuliza

Jamaa yangu akatulia, akageuka na kuangalia kwa wahuumu wa hiyo hoteli, akaagiza vinywaji na chakula, akasema;

‘Unajua wengi wanahisi kisa hiki ni cha kutunga, lakini ndivyo ilivyotokea kwa mama yangu, mama yangu kapitia maisha magumu, na hayo niliyokuelezea ni baadhi tu, kuna mengine nikikumbuka..hata mimi mwenyewe nalia..mama aliteseka sana, na utaona kuwa aliteseka kwa ajili yangu, ...

‘Mama yangu aliniambia kuna muda alijiwa na kitu kama njozi achague kuishi kwa mateso hayo kwa ajili yangu, mtoto wake,  au achague kufa akastarehe peponi,...lakini  kwa mapenzi aliyo nayo dhidi yangu alimuomba mungu aendelee kuishi, ajifungue kwa shida, hata kama ni kwa kuteseka, ili niweze kuiona dunia, na ikamjia yena wakati nimeshazaliwa kuwa afe, maana nimeshazaliwa, akaomba kuwa hata kama ni kwa mateso anaomba aishi ili aweze kuniona, ili tu aweze kuhakikisha nipo salama.

‘Hebu fikiria kwa hali ya mama, hana aina yoyote ya kipato, hana mahali pa kuishi,hajijui,  lakini bado alinitafuta, bado alinitaka niwe naye..mimi simjui ...yeye hadi hapo alipofikia hanijui, ...anachojua ni kutokana na ndoto...sasa jiuliza akikutana nami atanitambuaje...

‘Hapa uone jinsi gani damu ilivyo na nguvu, jinsi gani mama anavyoweza kutambua damu yake, hata uwe wapi akikuona atakujua...ni kwanini...hata akiwa kapoteza kumbukumbu, lakini kumbukumbu ya mtoto wake haipotei,..ni kwanini, hata awe hana akili sawasawa, lakini akili hiyo bado ina mapenzi ya mtoto wake..hataki mtoto wake achukuliwe, hujawahi kuona akina mama wenye matatizo ya akili, mabarabarani wana watoto wao, hebu jaribu kumchukua mtoto wake uone kasheshe lake...

‘Utakuja kuona kuwa mama yangu alijua hana uwezo, lakini hakutaka kabisa kuniachia niishi na watu wengine,...mimi simjui...nalelewa maisha bora,.. utakuja kuona jinsi gani ilivyokuwa huko mbele kuwa hata kama utapata ukachuma, au unaishi masha bora kamwe usije kutakabari, ukamkana mama yako, utaumia,..’akatulia
Utakuja kuona ujanja ujanja....uliotokea, na kujua kama kweli huyu mama wa huko hospitalini kweli alikuwa ndiye mama yangu...au alikuwa ni mama wa uwongo,.., ..

‘Ndugu yangu usinione leo nipo hivi, ...’akajiangalia huyo rafiki yangu ambaye kipindi cha nyuma nilipokutana naye alikuwa kakonda hai kuonekana kama anaumwa ukimwi, lakini leo ni pandikizi la mbaba, tajiri...

‘Yote haya yasingelikuwepo isipokuwa kwa kujitolea kwa mama kuteseka kunyanyasika, kaanzia kuitwa mgumba,..eti hazai,...haya akapata ujauzito ...na bado akawa haaminiki, eti mimba hiyo ni ya kuzini....akapigwa, na kuponea tundu la sindano, akiwa na mimba yangu...akajifungua kwa shida, na baada ya kujifungua akawa hajijui...akaja kuitwa mchawi, na huk kuitwa mchawi kaanzia kuitwa bado hajanizaa, kanizaa,..nimekuwa mkubwa najijua nina kazi,....anaitwa mchawi, kwasababu ya macho, kwasababu ya kuharibiwa sura,,,inaniuma sana

Alipofika hapo hakuweza kujizuia, akaanza kububujikwa na machozi.

‘Ndugu yangu, ..nani kama mama...mama yangu alitambuliakana amekufa, na kufufuka kwa ajli yangu, na kaburi lake bado lipo,...nimefika hiyo seheme, seheme ambayo, iliambiwa ndipo mama alizikiwa, akaja kufufuka kwa ajili yangu....

Mama alipojifungua kunizaa mimi akapoteza kumbukumbu zote, lakini bado kumbukumbu ya kuwa ana mtoto ikaendelea kuwepo, kumbukumbu ya mtoto wake haikupotea kwanini,...na bado akiwa hajitambui anatembea kama mtu yupo kwenye njozi, akaendelea kunitafuta, hapo hajijui hata yeye mwenyewe hajijui kuwa ni nani....’akatulia

‘Narudia rudia ili upate kuelewa zaidi....’akasema

‘Kwahiyo huyo mama aliyekuwa kachanganyikiwa ndiye mama yako au ilikuwaje?’ nikamuuliza

‘Tutakuja kujua huko mbele, maana dunia hii nayo ina mambo yake, wanadamu wanaweza kufanya mambo ukashindwa kuamini, watu wanaweza kujisingizia kuwa ndio wao kumbe sio wao....muhimu kumbuka kuwa kisa hiki hadi hapo anayenisimulia ni mama yangu, maana mimi nilikuwa bado mchanga, sijijui simjui ,,na niliyekuwa namfahamu kuwa ni mama yangu, ni mama huyo wa kufikia...

‘Sawa endelea na sehemu hiyo pale nesi alipopigiwa simu, ilikuwaje,....?’ nikamwambia ili asije kuondoka kabla hajamaliza kisa hiki

Tuendelee na kisa chetu

*******

‘Nesi alipopata hiyo simu yenye utata, aliomba ruhusa aondoke haraka akawaone ndugu zake, lakini madakitari hasa bosi wake akatoa rai, kuwa ni vyema waondoke pamoja  na yeye, na pia waondoke na yule mtoto, maana huenda huyo mama atakuwa kaelekea huko.

‘Na kwa muda huo vipimo vilikuwa tayari, lakini cha ajabu hakuna aliyekumbuka hilo, ...uone miujuza ya mungu ilivyo, hakutaka hilo liwekwe wazi mapema...’akasema rafiki yangu kutoka kwa maelezo ya mama yake.

Basi ikakubalika hivyo na wakati huo mtoto alishachukuliwa kule alipokuwa akicheza na wenzake, unajua watoto tena, wakikutana na wenzake, wanasahau kila kila kitu...

‘Baby twende kwa mama...’akasema nesi

‘Twende mama...’akasema akionyesha furaha kubwa,

‘Ndio twende kwa mama yako...’akamwambia

‘Sokoni...?’ akauliza maana aishaambiwa kuwa mama yake yupo sokoni hajarudi.

‘Mhhh..nyumbani, ...’akasema na ikabidi apitie kwake, kujiandaa kidogo na alipokuwa tayari, bosi wake akaja na gari lake wakachukuliwa na msafara ukaanza kuelekea huko kijijini...

NB: Le ni siku ya mapumziko tupo nyumbani, nilitaka kuliweka hili wazi kidogo maana watu wamesahau wapi kisa kilipoanzia, kuwa kisa hiki nasimuliwa na rafiki yangu ambaye kwa sehemu sehemu kubwa alisimuliwa na mama yake alikutana na mateso haya.

WAZO LA LEO: Tufanye nini ili kumkidhia haja mama yako angalau aone kuwa wewe una mjali, ...na hata kama katungulia mbele ya haki, una wajibu gani wa kufanya kuwa kweli unamjali mama yako.

Ni mimi: emu-three

No comments :