Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, April 30, 2015

NANI KAMA MAMA-69


‘Tulifanya hivyo ili huyo mtoto apatikane,….na kwasababu mtoto keshapatikana bila madhara, maana watekaji wa watoto wanakuwa na ajenda ya siri, kuna hao wa ushirikina wanawakata watoto viungo, wengine wanawafanyia mambo machafu, …sisi tuliyaona hayo tukaona tutumia njia hii ya busara…’akatulia

‘Sasa kilichobakia, ambacho kilikuwa katika mpangilio wetu, ni kufanya vipimo vyote muhimu..kuangalia afya yake, na jingine kuhakiki kitaalamu kuwa huyu mtoto ni mtoto kweli wa huyo mama, …, na kama huyo mama sio mama wa huyo mtoto tutajua nini cha kufanya…’akasema.

Na wakati taratibu hizo zikifanyika, nesi wewe utabeba dhamana ya huyo mtoto, utakaa na huyo mtoto, utakwenda kukaa naye huko nyumbani kwako..’akaambiwa

‘Docta…’ akaanza kulalamika

Tuendelee na kisa chetu

*************
Amri ikatolewa kuwa vipimo muhimu  kwa mtotop vifabyike ili kujua hali ya mtoto na pia vipimo vingine vifanyika kwa huyo mama, ili kuweza kumtambua kama kweli mama huyo ndiye mama mwenye mtoto kihalali na hili lifanyike kwa haraka.

 Kazi hiyo ikapewa kipaumbele, huku dakitari wa akili akipewa jukumu la kumhudumia huyo mama na kuhakikisha anagundua nini kinachomsumbua. Na kuwa muda huo huyo mama alikuwa katulia, na alikuwa hajaambiwa kuwa mtoto anayemtaak yupo tayari kwenye mamlaka ya hospitalini.


Nesi naye akaendelea na jukumu la malezi ya huyo mtoto, kwani kama itaonekana kuwa siyoo huyo mama mhusika, inabidi mtoto huyo arudishwe kwa wazazi walezi, ambao walishakubali kubebe hiyo dhamana.

Ilikuwa asubuhi, kazi zimeanza kila mtu akiwajibika kwenye kazi yake, docta bingwa wa magonjwa ya akili akafika chumba maalumu ambapo wamemuweka huyo mama, alitakiwa kupelekwa wodini, lakini kiusalama akawa kwenye chumba hicho.

 Docta aliingia pale kwenye chumba, hakumkuta nesi, moja kwa moja akelekea kwenye kitanda anapolala yule mama, alijua kuna mtu kalala, akafika na kuinua shuka taratibu, huku kichwani akiwaza, nini kimemsibu huyu mama, au kazidiwa na kupoteza fahamu, au…

‘Huu ulalaji sio wa kawaida…’akawa anaongea kimoyo moyo,

‘Na huyu mama hana kawaida kujifunika kiasi kile, lakini hata hivyo, aliona ajabu mtu gani angekuwa kalala vile kitandani, ajifunike kutoka vidolenihadi kichwa chote na joto lote hili, akahisi kuna kitu kimefanyika na kama ndivyo anavyohisi basi huyo mama ana ajenda ya siri.

Akalifunua lile shuka, sehemu ndogo ya eneo analojua ni la kichwani, docta akaliachia huku akiguna, halafu akageuka na kumuona nesi anaingia mlangoni, akalirudishia lile shuka kama lilivyokuwa, na kugeuka kuondoka pale kitandani


Nesi akaja hadi pale kitandani na kuiona ile hali, akasema

‘Mungu wangu, huyu mama ananini tena…’ akasema nesi huku akilifunua lile shuka lote kitandani , na alipohakikisha kuwa anachokiona ni sawa, akamgeukia docta, ambaye alikuwa kaduwaa kwa muda…Docta akatizama huku na kule halafu akamtizama nesi kutaka kupata maelezo, na nesi kwa muda huo alikuwa akilirudishia lile shuka na kusogea kitanda cha pili yake! Akamtizama mgonjwa aliyelala kwenye kile itanda, yule mgonjwa alikuwa kalala fofofo.

Aliogopa kumwamsha, lakini akaona kwa dharura kama ile hana jinsi, akamtikisa kidogo yule mgonjwa , na yule mgonjwa akafunua macho kwa shida, kwani usingizi bado umemjaa, lakini alipomuona kuwa aliyesimama mbele yake ni nesi, akainuka haraka na kuanza kulalamika.

‘Mwambie Docta mbavu zinanibana sana, halafu,. …’ akawa anaonyeshea sehemu za mbavu, na dakitari aliyekuwa aksimama karibu akasogea pale kumuona huyo mgonjwa, akajifanya anamchunguza, lakini mawazo yake yalikuwa yakiwaza mbali.

‘Usijali utapata dawa …’akasema na kurudi kwenye kile kitanda cha kwanza alichokuwa kalala yule mama,  na kabla hajamwambia kitu yule mgonjwa anayelalamika, akamgeukia nesi, nesi alikuwa bado kuduwaa hakujua aseme nini nesi mawazoni anahisi huenda huyo dakitari anajua wapi alipoelekea huyo mama

Baadaye akamsogelea yule mgonjwa na kumuuliza;

‘Mto wako wa kulalia upo wapi?’

Dakitari akawa anaendelea kukagua kile kitanda alichokuwa kalala huyo mgonjwa, na yule mgonjwa akashangaa alipoona kalala bila mto wake, akajitetea kuwa yeye haoni tofauti ya kulalia na mto au kutokuulalia, kwani hana mazoea ya kutumia mto. Docta akasogea kitanda kingine, ambacho kilikuwa hakina mtu akaona kuwa na mto wake haupo pia.

‘Nesi huyu mgonjwa atakuwa kaenda mbali sana, na sidhanii hata kama tukimtafuta tutamkuta maeneo ya humu hospitalini, lakini kwa usalama ngoja tuwaarifu walinzi wamtafute,,’ akasema docta huku akikagua sehemu za vyoo na bafuni.

Alitaka kumwambia nesi afanye hiyo kazi lakini kwa haraka aliyo nayo akaamua kufanya ukaguzi huo mwenyewe, na alipohakikisha kuwa huyupo popote humo ndani,akachukua simu yake na kumwita mlinzi.

Yule mlinzi alipokuja akatizama moja kwa moja kitanda cha yule mgonjwa akijua kuwa kaitiwa kuhusiana na vurugu za yule mama na alitakiwa kumdhibiti au kuchukua hatua fulani , lakini hakuona dalili ya yule mama, na akamwangalia Docta asikie nini anachoambiwa.

‘Nakumbuka tuliwaambia muwe makini na yule mama aliyekuwa analeta fujo, …na muhakikishe akitoka nje, kuna mtu yupo naye, ….sasa huyu mama yaonekana katoka, na dalili za humu ndani zaonyesha kuwa alidhamiria kufanya hivyo…je mlimuona huyo mama akitoka…?’ akauliza docta

‘Sawa kabisa, lakini tangu muda ule hajaleta vurugu yoyote, na kuna muda tuliamua kuja kumchunguza, na tulimkuta kalala,  tena kalala fofofo, tukaona tupumzike tu hapo nje…’ akasema yule mlinzi

‘Sasa yupo wapi huyo mama?’ akauliza docta

‘Si huyo hapo kalala, na anaonekana amelala kama gogo…’ akasema yule mlinzi akisogelea kile kitanda, lakini alipokikaribia akashikwa na butwaa, akamwangalia Docta, halafu akainua shuka kwa mashaka, kwani alijua kama huyo mama yupo, itakuwa kosa…lakini kwa jinsi ilivyo, ilionekana hakuna mtu au kama yupo mtu ni mfu… kabla halijafunuka lote akalirudisha lile shuka haraka. Akamwangalia Docta tena

‘Ina maana gani Docta…?’ akauliza yule mlinzi

‘Nikuulize wewe, kuwa hii ndio kazi mliyopewa kuifanya,, hamuoni sasa mtawajibika mbele ya sheria, na kama kuna lolote baya itabidi …nyie muwajibike…’ akasema Docta, na kabla hajamaliza yule mlinzi akaanza kukagua vyema , akamtizama nesi na kabla hajapata alichotaka kusema akaelekea sehemu ya vyoo na huko alikaa kwa muda liporudi akasema kwa wasiwasi.

‘Huku hayupo, ina maana aliweka hiyo mito hivyo hapo kitandani kuonyesha kuwa kalala, halafu akatoroka…lakini akili ya kufanya hivyo imetokea wapi…..haiwezekani, na katorokea wapi…alipitia wapi….?’ akasema yule mlinzi kama anauliza

‘Wewe wasema hivyo, na unajua wewe kuwa kafanya hivyo na kutoroka…sisi hatujui, tunataka mkaandikishe hayo maelezo yenu haraka kwa Dakitari mkuu..’ akasema Docta huku akitoka mle wodini, na nesi akamfuata docta wake nyuma, huku wote wakiwaza kuhusiana na tukio hilo la aina yake.

Walipofika kwa Dakitari mkuu na kuelezea nini kimetokea, ikabidi walinzi waitwe kujieleza, na wao hawakuwa na jipya la kuelezea, zaidi ya kusema wao walijua kuwa yule mgonjwa kalala, na waliogopa kwenda kumwamsha. Na kama katoroka, hawana uhakika katorokaje, kwani yeye ni rahisi kugundulika kwa uvaaji wake wa kujifunika usoni, …

‘Tumejaribu kutafuta sehemu zote za hospitalini na kuulizia kama kuna mtu yoyote kamuona huyo mama,lakini hakuna mtu yoyote aliyemuona mwanamke kama yeye, kwahiyo ina maana kuwa alipotoka, labda alijifunua uso au alijifunika kinamna nyingine ambayo mtu mwingine asingeweza kumtilia mashaka..’akasema mlinzi.

‘Sasa atakuwa kaenda wapi na kwanini aamue kutoroka hospitalini..?’ akauliza Dakitari mkuu

‘Au kagundua kuwa alichokuwa akidai ni uongo na kwa vile kaona atagundulika uongo wake akaona atoroke..jana tulipotaka kumtoa damu aligoma, hadi tukambembeleza ndio akakubali….sasa hiyo inaonyesha kuwa huyu mama, ana ajenda ya siri…au?’ akasema nesi kwa mashaka, huku akimtizama docta.

‘Mimi sidhani kuwa ametoroka kwasababu hiyo ya kuogopa kuwa kasema uongo, mimi nadhani kuwa , kwa vile kumbukumbu zimeanza kumrejea, huenda ana kitu anakifuatilia na anataka kuhakikisha kuwa jambo fulani alilolifanya kipindi fulani ni kweli…’ akasema docta bingwa. Alipomuona nesi wake hajamuelewa vyema, akafafanua nini alichokuwa akimaanisha;

‘Kwa uzoefu wangu wa hawa wagonjwa, pindi fahamu na kumbukumbu zinapoanza kuwarejea, huwa wadadisi sana, na kujaribu kufuatilia mambo ambayo waliyayafanya au kuhakikisha kuwa kweli walifanya hivyo…’akatulia

‘Sasa anafuatilia nini..?’ akauliza nesi.

‘Kwasasa huwezi kusema anafuatilia nini…na wakati mwingine inaweza kuwa hatari, kwani katika kufuatilai hivyo wanaweza wakagundua kuwa walifanya jambo baya na wanataka kuficha siri, kwahiyo wanaweza hata kudhuru au kuua, ili kuficha siri…au wakaona wamefanya jambo la aibu, na wengine huishia kujiua, sasa cha muhimu ni kujaribu kufikiria nyendo zake siku mbili tatu…’ akasema docta

‘Na huko kijijini alipokuwa akiishi,…alikuwa na tabia za ajabu ajabu kutoroka…au …?’ aakuliza docta

‘Mimi nijuavyo huyu mama kwa mara ya mwisho alikuwa akiishi na ndugu zangu, na sikuwahi kusikia kufanya jambo baya. Watu kwa imani zao haba wao ndio walimzushia kuwa eti ni mchawi, na hata kufikia kumuunguza na moto..’ akasema nesi

‘Isije kawakumbuka hawo wabaya wake na labda kaamua kwenda kuliipiza kisasi, maana mama mwenyewe anaonekana kaka kishari shari, na alivyo, anaweza kupambana na midume, na hata kuitoa jasho..’ akasema mlinzi.

‘Cha muhimu watu wajaribu kufuatilia wapi alipopitia hasa huko kwa ndugu zako …na naona ni vyema uwasiliane na ndugu zako haraka iwezekanavyo, kama hajafika huko, wajiandae na kama kafika huko tujue kuwa kuna usalama…. hebu wapigie simu nesi sasa hivi tusikie watasema nini, na kuwatahadharisha…,’akasema

Nesi akachukua simu na kuanza kupiga namba ya shekemji yake, ikawa inaita bila kupokelewa, akapiga simu ya dada yake. Na wakati nesi anajaribu kupiga simu. Docta bingwa na mkuu wao, wakawa wanaulizana hili na liel kuhusu huyo mama, kama kuna lolote wanaloweza kulifanya kwa muda huo.

‘Ina haja ya kuwajulisha watu wa usalama…polisi’akauliza mlinzi

‘Bado..sio muda muafaka, yawezekana huyo mama yupo maeneo ya hapa karibu tu…’akasema docta mkuu, na docta bingwa akatikisa kichwa kukubali.

‘Hawezi akawa kaenda mbali, lakini kwa tahadhari ni bora kufanya kila liwezekanavyo ili kuona hakuna madhara yanayoweza kutokea kwake na kwa watu wengine.

********

Docta bingwa alikuwa akimuwazia sana huyo mama, tangu amuone huyu mama amekuwa akihisi kuna jambo zaidi linalimsumbua huyu mama, na mwanzo alihisi huenda ni sababu ya kumtaka mtoto wake. Lakini kadri siku zilivyokwenda akahisi kuna zaidi ya hilo.

Yeye alishahisi kuwa huyu mama hana ugonjwa wa akili kama watu wengi wanavyomfikiria, kwasababu zile dalili za ugonjwa wa kili hazipo kwenye matendo yakea. Alichogundua ni kuwa mama huyu alipoteza kumbukumbu, na hii kitaalamu inaitwa `amnesia’ na lazima ipo sababu kubwa iliyofikia hadi mama huyu akapoteza kumbukumbu.

Kitu ambacho kinamshangaza ni kuwa kila anapojaribu kupata habari moja, anajikuta anakabiliwa na tatizo jingine ambalo anashindwa kuliunganisha moja kwa moja na tatizo lilopita. Alikuwa na hamu sana ya kupata kumbukumbu za mama huyu, lakini wamejaribu kuzitafuta bila mafanikio, inaonekana kumbukumbu zote zilishaharibika kabisa, na huyu mama hajaweza kukumbuka kabisa asili yake,..alichoweza kukumbuka zaidi ni mtoto na jinsi alivyompata…

Na alipojaribu kumuulizia huyo dakitari aliyemfanyia upasuaji , na yeye alisema hana taarifa zazote za wapi huyo mama anatokea, na hakupata nafasi ya kujua ni kitu gani kilimsibu huyo mama kama ni kweli huyo mama ndiye huyo aliyewahi kumfanyia upasuaji.

 Kwa uhakika alishindwa kukubali moja kwa moja kuwa huyo mama aliyefanyiwa upasuaji na huyo docta ndio huyo mama waliye naye hapo mpaka vipimo vitoke, na hata kama docta huyu ataweza kumtumia picha, ni jinsi gani ya kumshawishi huyo mama ajifunue, maana kagoma kabisa kufanya hivyo.

 Kwa uchunguzi wa harakaharaka na dalili inaonekana akawa ndiye huyo mama, ..na docta mkuu ambaye aliwahi kumuona huyo mama usoni, anasema mtoto anafanana na huyo mama, lakini kufanana yaweza ikawa sio sababu, anaweza akazuka ndugu wa huyo mama kwa malengo yake akaja kumdai huyo mtoto …!

‘Je huyo mama tunawezaje kumpata?’ lilikuwa swali muhimu kwao.

‘Ni kwanini atoroke…?’ akauliza docta mwenzake.

‘Huyu mtu hajatoroka, nina uhakika kuna jambo analifuatilia,…’akasema docta mwenzake.

‘Lakini umesema kapanga mito kaam vile mtu kalala,..hivi unalionaje hilo si kuonyesha kuwa huyo mama kadhamiria, ni kama shushu fulani hivi….’akasema docta mkuu.

‘Unahisi ana akzi anaifanya humu..hahahaha, sio kweli….’akasema mwenzake

‘Simu za ndugu zangu zote ..mwanzoni nilipiga zikaita lakini sasa kila nikipiga hazipatikani tena,  sijui kuna tatizo gani, sio kawaida yao kuzima simu zao wote wawili..’ akasema nesi huku akiwa kachanganyikwa.

‘Labda zimeisha chaji, siunajua tena tatizo hili la umeme na mgawo..’ akasema docta mkuu. Na wakati wanaongea nini kifanyike zaidi simu ya nesi ikaita ghafla na namba iliyoita ni namba ngeni kwenye simu yake.

‘Halloh wewe ni nesi .?.’ sauti ikawa inauliza na simu hakiuwa na mawasiliano mazuri.

‘Ndio wewe ni nani,..?’ akauliza

‘Mimi ni jirani na ndugu zako,….hapa kijijini’ sauti ikasema

‘Kuna tatizo gani huko kijijini….?’nesi akauliza kwa mashaka

‘Nimepewa ujumbe nikupigia, dada yako anasema kaam inawezekana uje huku kwani ana matatizo makubwa…’ simu ikawa imekatika na hata walivyojaribu kupiga tena ikawa haipatikani.

‘Kuna tatizo ..ndugu zangu wamepatwa na nini tena, na kwanini simu zao zisipatikane…’nesi akawa anajiuliza na madocta wakawa kimia wakilitafakari hilo.

‘Au huyo mama keshafika huko…sasa utamuuliza nani, hakuna jamaa yoyote wa huko unayeweza kumuulizia kama una namba yake..?’ akauliza docta

‘Mhh, sina nilikuwa nayo ya jirani wa hapo, lakini akabadili namba, simu yake ilipoibiwa, na sijawahi kupata namba yake hiiyo mpya…’akasema

‘Jaribu kuwapigia tena na tena…’akaambiwa na nesi akafanya hivyo bila mafanikio…

‘Mhh….sasa tufanyeje, maana wewe huwezi kuondoka kwa vile kuna hili tatizo, kwanza mtoto yupo wapi..?’ akaulizwa nesi

‘Yupo chumba cha watoto anacheza na wenzake, nesi anamlinda hakuna tatizo naye…’akasema

‘Una uhakika..?’ akauliza docta mkuu

‘Kwanini unasema hivyo…’akauliza nesi,

‘Nenda kahakikishe….’akasema docta akionyesha wasi wasi fulani...

NB:Je kuna nini ,usicheze mbali!

WAZO LA LEO: Tumshukuru mola kwa kila jambo likiwa jema au baya...japokuwa mengine yanaweza kua magumu kiasi kwamba mtu ukajiona kama wewe umeonewa huo ugumu unaweza kuwa ndio ngazi ya kwenda kwenye mafanikio. Muhimu, kujibidisha kwenye mambo ya heri , na kuwa na subra kwenye matatizo, tutafanikiwa tu


Ni mimi: emu-three

No comments :