Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, April 29, 2015

NANI KAMA MAMA-68



Haikuchukua muda dada mtu aliamuka hata kabla hajafanyiwa huduma ya kwanza, akasema alihisi kizunguzungu tu, na sasa yuopo salama, akasema anataka kuondoka kwani mume wake atakasirika kama akichelewa zaidi.

‘Dada lakini unaonekana haupo sawa, kwanini tusikupime kwanza, ..?’ nesi akamuuliza

‘Hapana wewe mwenyewe unamfahamu shemeji yako, mimi sina tatizo, mtoto…’akajisahau kuwa hatakiw kuondoka na mtoto.

‘Kalala…’akaambiwa

‘Oh mungu wangu unajua nilihisi ninaota kumbe ni kweli…mungu wangu, ..haya mimi nitafanyaje..’akasema akianza kuondoka

‘Dada lakini nakuona haupo sawa…’akasema nesi

‘Nipo sawa, ….usijali, nimekuachia huyo mtoto lakini moyoni sijarizika,….’akasema sasa akitembea kwa mwendo wa haraka kuondoka…

Tuendelee na kisa chetu.


‘Yaani mdogo wangu, ndio umeamua hivyo, yaani wewe na shemeji yako mumeamua kuninyang’anya mtoto wangu, kipenzi changu…’ akaanza kulia kwa sauti, huku akimpa mdogo wake mkoba waliokuwa wamebebea juice ya mtoto na maziwa.

Nesi huku naye machozi yakimlenga lenga akachukua ule mkoba na akageuka kuondoka hakutaka kuangaliana na ndugu yake tena, kwani nay eye angeendelea kulia,

Nesi aliondoka moja kwa moja hadi ofisi ya mkuu wa madakitari kwa bosi wake, alipofika akakuta huyo bosi wake katoka. Akageuka na kwenda ofisi ya dakitari bingwa, akamkuta naye hayupo, ikabidi asubirie hapo..aliona labda , aende moja kwa moja wodini akaongee na huyo mama anayedai mtoto wake, kuwa mtoto huyo keshamleta.  Akaona sio vyema, lazima kwanza akutane na wakubwa zake ili ajue utaratibu upoje.

Ni wakati huo akiwaza hatua gani ifuate ndipo simu yake ya mkononi ikaita, na alipoitizama akaona ni simu kutoka nje,akaihisi atakuwa ni dakitari kijana, japokuwa namba ilikuwa tofauti na ile anayoifahamu yeye.

‘Vipi sister, mambo yanaendaje huko, ulipata kumbukumbu zozote za yule mama…?’ akauliza, ilikuwa sauti ya docta kijana. Na nesi alipoikisikia hiyo sauti akashukuru mungu, akijua sasa angalau kapata mtu wa kubeba naye hilo jukumu. Akatafuta sehemu ya kukaa, ili aweze kuongea vyema.

‘Docta, yaani hapa nilipo nimechanganyikiwa maana mambo yamekwenda haraka na hata sijui nifanyeje…’akasema

‘Kwani kumetokea nini..?’ akaulizwa, na mara akamuona nesi akija kwake akiwa na yule mtoto, akamuashiria huyo nesi kuwa anaongea na simu.

‘Hutaamini kuwa hapa nilipo nipo na yule mtoto, …’akasema

‘Oh, kwanini, utafanyaje kazi na huyo mtoto , si mtoto huyo alikuwa kwenye mamlaka ya ndugu zako kwani imetokea nini,….?’ Akauliza

‘Kumetokea mambo makubwa..ikabidi huyo mtoto aletwe hapa hospitalini, kwani yule mama anadai kuwa ni mtoto wake,…’akasema

‘Kwa ushahidi gani mna uhakika huyo mama ndiye mwenyewe, muwe makini na hilo…’akasema

‘Utawala na watu wa usalama wamesema wamethibitisha kuwa ni kweli huyo mama ndiye mwenye mtoto..’akasema

‘Watu wa usalama ina maana polisi wameingilia kati?’ akauliza

‘Ndio na nilishikiliwa kituoni kwa kosa la kumchukua mtoto bila maandishi, kilichoniokoa ni ukweli tu…..’akasema.

‘Mhh na ndugu zake wamesemaje maana nijuavyo watakuwa walishamzoea huyo mtoto kama mtoto wao?’ akauliza

‘Hutaamini hapa nilikuwa nalia na dada yangu…, dada yangu hakupenda kabisa, kuachana naye…lakinii hakukuwa na lakufanya  kwani huyo mama amedai kuwa hataki ushauri na yoyote yule anachotaka ni mtoto wake. Yaani hapa nilipo bado nina wasiwasi kwani huyo mama ananitafuta kila wodi, na ameapa kuwa akininipa atafanyia kitu ambacho sitakisahau…yaani hapa hospitalini, hakukaliki, ….’akasema

‘Sister, naomba muwe makini na maamuzi yenu, maana mtu yoyote mwenye nia mbaya anaweza kutunga uwongo wa namna hiyo, mimi sijawa na uhakika, maana kama mama huyo alikufa..umesema wamathibitisha kwa vipimo…mmh, lakini je kama ndiye huyo mama yake, kweli anaweza uishi na huyo mtoto…je  akili za huyo mama zipo sawasawa…maana kama ulivyosema analeta fujo, huenda bado akili yake haijakaa sawa….?’ akauliza huyu docta.

‘Sina uhakika na hilo bado maana mambo yote sasa hivi yanashughulikiwa na dakitari bingwa wa mambo ya akili..na ulisema bado na wewe unatafuta zile kumbukumbu umeshazipata…?’ akauliza nesi.

‘Yah….ila bado sijapata muda wa kuzipitia unajua tulikuwa na mitihani na mambo mengi ya kufanya, nitazipitia na nitaona jinsi gani ya kusaidia…’akasema

‘Lakini kwa hivi sasa sioni kwamba itasaidia kitu..’akasema nesi

‘Kwanini….?’ Akauliza

‘Mtoto ni lazima akabidhiwe kwa huyo mama, na mtoto ninaye, …huoni kama itachelewa, sijui ufanyeje..’akasema

‘Nitaongea na huyo docta, ili tujue nini cha kufanya kitaalamu, naomba umwambia nitampigia simu baada ya nusu saa hivi, kwani nipo kazini kwa vitendo, unajua masomo yetu yalivyo, kuna vitendo na darasani….’akasema

‘Kwahiyo unataka kusema nini kuhusu huyu mtoto?’ akauliza nesi.

‘Hakikisha kuwa huyo mtoto hafiki mikononi kwa huyo mama kwanza, mpaak nionge na huyo docta…’ simu ikakatika!

‘Mhh, mbona huyu naye ananichanganya kwani kagundua nini….mbona hawa wamesema kuwa wamehakikisha kuwa huyu mtoto ni halali ya huyo mama, ….mmh,..’akawa anaongea peke yake na nesi aliyekuwa na huyo mtoto akamsogelea na kumwambia

‘Mtoto anamtaka mama yake….’akasema, na nesi akamchukua huyo mtoto na kuanza kumuongelesha

‘Mama kaenda sokoni, atakuja na zawadi…’akasema

‘Nataka-mama angu….’akasema

‘Atakuja sasa hivi, …’akasema na kuchukua ule mkoba alioachiwa na dada yake, akatoa ile chupa yenye maziwa akampa mtoto na mtoto kwanza alikataa akisema anamtaka mama yake.

‘Nataka mama..angu….’akawa anaanza kulia, nesi akahisi machungu moyoni akatamani amchukue na kuwakimbilia ndugu zake kama hawajaondoka, lakini hilo haliwezekani tena, ikabidi afanye kazi ya ziada ya kumbembeleza yule mtoto hadi mtoto akakubali kunywa yale maziwa na alipomaliza akashikwa na usingizi ikawa ndio nafuu yake.

Huyo mtoto alikuwa ana afya njema, miaka miwili, ila alionekana hajaweza kuunganisha maneno vyema, akawa kakaa naye akiwa kamlaza mapajani, na kwa mbali fikira zikamjia kuwa huyo angekuwa ni mtoto wake, na  na docta kijana, mbona angejisikia raha.

Akachukua mkono wa yule mtoto kumwangalia vidole vyake, halafu akawa anamshika kichwani huku akiwaza, mengi, hasa jinsi gani angepata nafasi ya kumwambia docta kijana anampenda na hatamani mwanaume mwingine yoyote, kwani muda mwingi amekuwa akimuwaza yeye.

‘Umegeuza ofisi yangu, chumba cha kulelea watoto…huyu mtoto ana matatizo ya akili..?’ akagutuka kusikia sauti ya bosi wake..alikuwa dakitari bingwa wa mambo ya akili, na kwa haraka akainuka pale kwenye kiti huku akiwa kambeba huyo mtoto mkononi

‘Kwani huyo mtoto ana matatizo gani, kwanini usimpeleke kwa dakitari wa watoto unanileta huko ofisini kwangu, na leo nina mambo mengi ya kufanya…’akasema akionyesha kuchoka.

‘Docta, huyu ndiye yule mtoto anayetafutwa na yule mama…’ akasema nesi na yule dakitari aliposikia hivyo akainua kichwa na kumtizama huyo mtoto, halafu akasema.

‘Oh, lakini haya maswala unatakiwa kwenda kwa dakitari mkuu, hayapo mikononi mwangu si unajua tena utaratibu au nenda kwa msaidizi wake..’akasema huyo mkuu wake.

‘Sawa najua wewe ndiye unyeshughulika na huyo mama, nikaona na wewe ni mhusika mkuu, au nimekosea….’akasema.

‘Ok ni hivi…sasa hivi tumetoka kujadili hili swala na ilishaamuliwa kuwa huyo mama apewe mtoto wake, akishapewa tutaangalia maabdiliko ..ni lazima kutakuwa na mabdiliko kwa huyo mama, na inaweza kumsaidia akapona kwa haraka, na kukumbuka kila kitu…’akasema

‘Sasa mimi nauliza huyo mtoto si ndio anatakiwa kukabidhiwa kwa huyo mama, sasa si wewe docta wake, ndiye unatakiwa kumpeleka huyu mtoto na kumkabidhi au…’akasema

‘Mhh, hapana kwanza mtoto huyo tunatakiwa tumkabidhi kwa utawala,…kulikuwa na ajenda nyingi sana leo,…na nyingie zimeshatekelezwa,a ilibakia hili la huyo mtoto tumetoka mapumziko kidogo, …nimetoka nikajikuta Napata kazi nyingine, wagnjwa ni wengi…..sasa mimi naona uende kwa msaidizi wa docta mkuu atakuambia kila kitu,..natumai umenielewa…niache nifanye kazi moja kwanza’akasema

‘Sawa bosi..’akasema

‘Na kuna swala jingine, …tunataka kujua zaidi kuhusu huyo mama, na hili tunataka ushirikiano na ndugu zako, nahisi yule mwanaume, ni nani kwako..?’ akauliza

‘Shemeji yangu..’akasema

‘Kuna kitu anakificha kwa huyo mama..atakuwa anamfahamu huyo mama unajua lolote kuhusu hilo? ,…hatutaki kulichukulia uzito wake, lakini tunaomba huyo shemeji yako, ajaribu kutoa ushirikiano tu…ni kwa manufaaa ya huyo mama,…..’akasema

‘Mimi kwakweli sijui….nitajaribu kuongea naye nisikie atasemaje…’akasema na kabla hajasema zaidi, simu ya huyo nesi ikaita akagundua ni simu ya docta kijana, akamgeukia bosi wake na kusema;

‘Kuna docta aliyekuwepo kipindi hicho cha huyo mama, yeye ndiye aliyemfanyia huyo mama upasuaji anataka kuongea na wewe..’akasema nesi

‘Kwanini siku zote hukusema hilo, kumbe ulikuwa na mawasiliano naye…oh’akasema huyo docta na kuipokea hiyo simu

Akageukia upande mwingine na kuanza kujitambusha, na wakaanza kuongea na huyo docta kijana….alisikiliza kwa muda halafu akasema

‘No..no…mimi sina maamuzi, …mwenye maamuzi ni docta mkuu,…unasema una uhakika...?'’akasema na kuendelea kusikiliza.

Alisikiliza maelezo, na akawa anaandika andika kitu kwenye karatasi, na hadi mwenzake alipomaliza kuongea, akainua uso na kumuangalia huyo nesi, na bado akawa anasikiliza, akageuza kichwa na kumuangalia huyo mtoto, alikuwa bado amelala. Halafu tena akamwangalia yule nesi kwa makini,…akatabasamu.

‘Ok nimekuelewa…nitalifanyia kazi,..’akasema na kumaliza maongezi halafu akamwangalia nesi na kusema;

‘Samahani sana nesi, mimi nilishakuweka kwenye kundi la watu wasiotimiza wajibu wao, sipendi kabisa watu wanaochezea kazi, hasa ikimuhusu mgonjwa…unajua nesi watu wengi wanatulalamikia kuwa hospitali zetu zina utendai mbaya, na kiukweli wanaosababisha ni watu wa ngazi zenu. 

'Unajua nesi, sisi madakitari kazi yetu ni kutoa maagizo kwenu, sasa utekelezaji unakuwa mgumu sana katika ngazi zenu…’akasema huku akionyesha kutabsamu ile sura ya kukasirika ikawa haipo tena hadi esi akashikwa na mshangao, hakujua wameongea nini na dakitari kijana.

‘Mimi nikiwa kazini nataka uwajibikaji, na msipotoa ushirikiano, unafikiri sisi tutafanya nini …kwakweli kama nisingeyasikia haya maelezo,nisingeliweza kukutetea maana swaal lako lilishafikishwa mbele ya utawala, na sijui maamuzi yao yangelikuwaje…ok, sasa hebu twende huko kwa huyo mkuu naona kuna mambo muhimu tunahitajika kuyafanya kabla hatujamkabidhi huyo mama mtoto wake…’ akasema akiwa na hamasa ya jambo hilo.

Wakaondoka hapo ofisini ya docta mkuu, ilikuwa ofisi ya pili yake, wakaingia na docta mkuu alikuwa akiongea na simu,  alipowaona, akawaashiria wamsubiria kwani anaongea na simu muhimu, na alipomaliza akawakaribisha.

‘Vipi naona mna mtoto…kuna nini tena..?’ akauliza

‘Yule mtoto wa yule mama, ndiye huyo hapo, ….’akasema

‘Aah, si muda wa kuliongelea bado au kuna haraka sana..?’ akauliza

‘Nimepokea simu kwa mmoja wa madocta waliowahi kumuhudimia huyo mama..’akasema

‘Oh , ni nani huyo..?’ akauliza huyo mkuu kwa hamasa

‘Ni docta mmoja sasa hivi yupo nje anasoma….kanielezea hilo tukio kwa kirefu na nimemuelewa…unajua sasa hivi tunahitajika kuchukua vipimo kwa huyo mama na mtoto tuthibitishe, kuna kuwalakini, na huenda kuna mchzo mchafu unachezwa.…kaniambia na mimi nimeona ni muhumu kuchukua vipimo, na maelezo yake yana uhakika, na huko alipo ana vipimo kwahiyo tukishavipata hivi vipimo, tutajirizisha na yeye pia yupo tayari kututumia vipimo vyake…na hata picha ya huyo mama…’akasema

‘Ina maana mlikuwa hamjalifanya hilo..la vipimo!, mbona mliniambia kuwa mumeshamfanyia huyo mama vipimo na mtoto..?’ akauliza nesi.

‘Tulifanya hivyo ili huyo mtoto apatikane,….na kwasababu kaptikana sasa cha muhimu ni kufanya hivyo vipimo vyote, na kama huyo mama sio mama wa huyo mtoto tutajua nini cha kufanya…kwani kama tusingelifanya hivi kunamengi yangelitokea,...kuna ushahidi wa wizi wa watoto....hayo ni mambo ya kiusalama zaidi....’akasema huyo docta na kumuacha nesi akiwa kaduwaa, kumbe yote ilikuwa ni mbinu za kuhakikisha kuwa huyo mtoto anapatikana.

‘Sasa nesi wakati utaratibu wote huo ukifanyika, vipimo na kila kitu huyo mtoto atakuwa kwenye mamlaka yako, utakwenda kukaa naye huko kwako..’akaambiwa

‘Oh,…jamani mbona mnipa majukumu makubwa namna hii, mtoto mwenyewe anamtaka mama yake..’akasema

‘Mama yake yupi ..?’ akauliza

‘Mama yake aliyemlea…’akasema.

‘Ni lazima hili lifanyike,…na wao walielewe hivyo, vinginevyo tungelijikuta kwenye matatizo,…kwani kuna shida yoyote, hivi vipimo vitachukuliwa leo, na kesho kila kitu kitakuwa tayari….hatuna haja na vipimo vya huyo docta anayesoma huko nje, tutachukua vipimo vyetu kwa kujirizisha tu…..na kama unaogopa usalama, useme tu, ...’akasema huyo docta bosi

‘Mhh..kazi kweli..’akasema nesi akimtizama yule mtoto ambaye alishafungua macho, na yule docta akamsogelea, akamwangalia huyo mtoto akasema;

‘Baby…’akasema na kumchunguza yule mtoto machoni, akageuka kumuangalia mwenzake, akasema;

‘Haina shaka…ndio yeye, ni swala la uhakiki tu…’akasema


WAZO LA LEO: Kila jambo lina uhakiki wake, hatuwezi kuthibitisha jambo mpaka tuwe na uhakiki wa kitaalamu, kama ni ugonjwa kuna vipimo, kama ni kosa kuna ushahidi wa kitaalamu wa kuthibisha kosa, na ni muhimu kukawepo na vidhibiti ili kuhakiki huo uthibitisho au kosa lenyewe. Kuongea tu hakusaidii, maana kuna watu wanajua kuongea na hata kugeuza ukweli ukawa vinginevyo. Tuwe makini katika kuhukumu mambo.
Ni mimi: emu-three

No comments :