Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, April 28, 2015

NANI KAMA MAMA-67


 Licha ya nesi kujitetea lakini sheria ilitakiwa ifuatwe, kwa kosa la kumchukua mtoto wa mtu mwingine bila maandishi yoyote, ndivyo ilivyoandikwa kwenye kumbukumbu za kiusalama, akaambiwa mengine yanasubiria matakwa ya mlalamikaji, na pia kuna mlango wa majadiliano kati ya walengwa hao yaani nesi kwa upande wake na huyo mama  kama mlalamikaji.

Tuendelee na kisa chetu.

Nesi akafikishwa kituoni, kwanza akatakiwa kujieleza, nini kilitokea hadi akamchukua huyo mtoto, akajieleza kama alivyojieleza kazini kwake, na kabrasha maalumu likafunguliwa kwa ajili ya kesi hiyo.

‘Kwahiyo nimeshitakiwa kwa kosa la kuiba mtoto?’ akauliza nesi alipoona akihojiwa na kuandikwa kila anachokisema.

‘Hapana hujashitakiwa bado..., kwa hivi sasa unaisaidia polisi..kama huyo mama ataamua kukushitaki basi utakuwa mshitakiwa, lakini kwa hivi sasa, kwa vile tuna uhakika unaye huyo mtoto aliyekuwa akitafutwa wewe tunakushikilia kama mshukuwa, kama mtu wa kuisaidia polisi kuhakikisha huyo mtoto anapatikana salama....’akaambiwa

‘Kwanini mna.....eti unasema salama, miaka mwili mlikuwa majua huyo mtoto anaishi wapi, anakula nini...halafu mnataka nilale rumande, hapana hilo sikubali kwa kosa gani…?’ akauliza

‘Taratibu lazima zifuatwe nesi,…..hili tatizo lingeisha mapema kama ungelitoa ushirikiano ulipotakiwa kufanya hivyo,..tunajua huenda huna hatia, lakini kwa vipi, wakati wewe ni makidi wa sheria, ulitaka sisi tufanye nini, tukupigia magoti….’akasema huyo mtu wa usalama.

‘Naomba simu niongee na ndugu zangu…’akasema nesi akiomba vitu vyake ambayo vilishashikiliwa.

‘Hapo umezungumza la msingi, lakini kwanza unatakiwa uingie huko....unakiona chumba kile... ili sisi tumalize kazi zetu..’akaambiwa nesi na nesi akageuka kuangalia kile chumba akakumbuka watu waliwahi kuwekwa hapo wanavosimulia, ni kuchafu...mbu...mwili ukaanza kumsisimuka.

‘Hapana..hapana afande, siwezi kwenda huko,….ina maana mimi nabeba makosa ya wenzangu..’akalalamika, na mara mkuu wa kituoa hicho akafika na akaelezewa kinachoendelea, akachukua simu na kuongea na mtu baadaye akasema;

‘Umeshawasiliana na ndugu zako, kuhusu huyo mtoto?’ akaulizwa

‘Ndio nataka niongee nao..niliwaomba hivyo,......’akasema

‘Basi muachane aongee na hao ndugu zake, halafu tutajua la kufanya…’akasema huyo mkuu na nesi akachukua mkoba wake ambao ulikuwa na simu yake..

‘Hapana usitumie simu yako, tumia simu hii ya hapa kituoni….’akaambiwa na nesi akawatajia namba za ndugu yake , ilikuwa namba ya shemeji yake na simu ikaiita wa muda, na aliyejitambulisha mwanzoni alikuwa mtu wa usalama kuwa hapo ni kituoa cha polisi, akaijielezea kuwa yeye ni nani.

'Kwani kuna nini...?' sauti ya shemeji mtu ikauliza kwa ukali

'Kuna ndugu yako nesi ni shemeji yako, anataka muongee naye....'akasema, nesi akachukua ile simu na kuanza kuongea.

‘Shemeji nimekamatwa nipo kituoni, ..kosa ni kuwa tumemchukua mtoto wa watu bila kibali maalumu…’akawa anaongea kwa sauti ya kulia

'Mtoto yupi..?' shemeji akauliza akijua huenda ni mtego

'Huyo mliye naye hapo...'akasema

‘Subiri uongee na dada yako….’shemeji yake akamwambia na baadaye akawa aanaongea na dada yake akamuelezea hivyo hivyo.

‘Mungu wangu ndio imekuwa hayo, sasa jamani si wao walikukabidhi huyo mtoto kwanini wasifungwe hao waliokukabidhi huyu mtoto, …sasa wanataka sisi tufanye nini, …’dada mtu akawa kachanganyikiwa, na yule mtu wa usalama akachukua simu mkononi mwa nesi akaanza kuongea yeye.

‘Kiutaratibi ndugu yenu atashikiliwa mpaka hapo mtoto huyo atakapofikishwa kunakohusika, tulitaka mumlete huyo mtoto hapa, lakini kwa vile hatujajua kuwa huyo mtoto yupo salama, mtahitajiak mumeleta kule hopsitalini apimwe na taratibu zote zitafanyika huko hospitalini,..., tutakutana huko, tuone cha kufanya….’huyo mtu wa usalama akasema

‘Tafadhali msifunge mdogo wangu, mtoto tunaye hana matatizo yoyote tumemlea kwa uadilifu kabisa kama mtoto wetu..na hatujua kuwa kuna matatizo hayo...ni makosa ya kazini kwako,..mngetakiwa muwakamati hao walimkabidhi mdogo wangu huyu mtoto.....’dada mtu akawa anongea kwa wasiwasi mkubwa...akajikuta anajieleza kupita kiasi, kitu ambacho walikihitajia sana hao watu wa usalama, na kumbukumbu zikawekwa.

‘Hamna shaka, sasa kesho asubuhi tukutane hospitalini mkiwa na huyo mtoto wewe na mume wako...asubuhi na mapema, mnasikia..’akaambiwa

‘Lakini mdogo wangu msifunge….’akasema

‘Usiwe na wasiwasi na mdogo wako , yeye ni mfanyakazi wa serikali, atajidhamini, na pia kazini kwao, wanaweza kumdhamini vile vile..tutaona taratibu zinavyokuwa , muhimu mumuandae huyo mtoto kiasi kwamba hataathirika kisaikolojia...natumai mnanielewa nikisema hivyo...’wakasema

‘Oh,…jamani kwanini hivi….’akawa analalamika huyo mama  na simu ikakatwa.

**********

Ilikuwa ni asubuhi na mapema, wanandoa wakiwa na mtoto walifika hospitali ya mkoa, na walipofika, wakauliza kwa mkuu wa hospitali, wakaonyeshwa, lakini kwa muda huo mkuu alikuwa hajafika, ikabidi wasubirie nje ya hiyo ofisi na walijua kuwa mdogo wao yupo polisi kwahiyo hawakutaka hata kumuulizia.

Haikuchukua muda landrover ya polisi ikafika, na nesi akateremka, na nesi alipowaona ndugu zake akawakimbilia, na kumkumbatia dada yake,...wakaanza kusalimiana na dada mtu aakwa anamkagua ndugu yake kama hakuumia mahali,  na wakati huo huo wale jamaa wawili watu wa usalama na askari wengine wawili, wakatoka kwenye gari na kusimama wakiwaangalia wana familia hao.

‘Oh aheri mumekuja..hata sijui niseme nini..oh jamani mtoto haujambo baby..’akawa anamsalimia mtoto na mtoto alikuwa anaangalia huku na kule hajui kinachoendelea. Mtoto huyo walizoea kumuita hivyo baby, japokuwa ni mtoto wa kiume.

‘Alikuwa amelala,, kaamuka sasa hivi…’akasema mama mlezi

 Mara shemeji mtu, akasimama ghafla ni kama kakumbuka jambo, akamsogela mke wake ambaye alikuwa kambeba huyo mtoto, akamchukua yule mtoto, na kumbeba yeye, akasogea na kukaa mbali kidogo na wao, halafu akawa anamchunguza huyo mtoto usoni, na huku anatingisha kichwa, halafu kama mtu aliyeona kitu cha kutisha, akainua kichwa juu, na akwa anaongea peke yake....,akasema;

‘Mungu wangu, ni sura yake kabisa…hivi kwanini sikujua hili mapema....anafanana sana na baba yake... nilijua tu, mwisho wa siku itakuwaje, sasa iko wapi…malipo ya dhuluma, ni hapa hapa duniani…’ akaendelea kumchungulia tena yule mtoto, sasa hivi akamshika kichwa chake, na huku anamtizama kwa makini.

Akasema, kwa utaratibu kama ananong’oneza :

’Unajua macho yako yanafanana sana na macho ya mama yako, mama yako ana mcho kama haya …na sura yako ya usoni,....mhh ni kama ya baba yako kabisa,… hapana kidogo kwa mama yako, kidogo kwa baba yako. Na huenda hata roho yako itakuwa kama ya baba yako au sio…..’ akasema kama anaongea na mtoto, baadaye akainuka na kuelekea pale walipokaa mkewe na shameji yake, akimkabidhi mkewe mtoto.

Kwa muda huo nesi alikua akiongea na dada yake lakini sikio alikuwa kalitega huko kwa shemeji yake, alisikia baadhi ya maneno maana kulikuwa na upepo, na alichokisikia kilimfanya aweza mara mbili tatu kuhusu shemehji yake na huyo mama. Na jinsi alivyomuona shemeji yake,. alimuona akiwa na mabadiliko makubwa sana, kakonda, hana raha,..na yupo kama ana wasiwasi  kama hayupo sawa, lakini hakutaka kusema kitu kwa muda huo.

Mke mtu naye alikuwa akimuangalia mumewe huku akiongea na mdogo wake, yeye hakuwa makini na hicho mumewe anachokiongea japokuwa alisikia baadhi ya maneno, hata yeye akilini alitambua kabisa kuwa mume wake sio yule mtu anayemfahamu, alikuwa kabadilika kabisa, ile tabia yake ya huruma anayoijua kwa mumewe imetoweka ghafala hasa baada ya kuambiwa kuwa huyo mtoto ni mtoto wa huyo mama wa mitaani

Kwa muda ule hakuna aliyemuuliza swali na kwa muda huo wale watu wa usalama walikuwa wanaongea yao tu….ni kama vile hawana habari na wanafamilia hao.

Mara shemeji akaonekana kutaka kuondoka, akageuka kule waliposimama watu wa usalama, akahisi wakimchuguza kwa mashaka, akatembea hatua kadhaa mbali na walipokaa wanafamilia wenzake, akakaa na kujiegemeza huku akiwa kashika kichwa.

                                                                ***
Baadaye shameji mtu akasimama na kuwaendelea watu wa usalama akaongea nao kwa muda ikaonekana hakuna makubaliano, akarudi akakaa, na haikupita muda, mkuu wa hospitali akafika, na madakitari wengine. Watu wawili wa usalama wakamfuata mkuu huyo wa hospitali ofisini kwake na pape wakabakia askari wawili.

Ilichukua muda, haikujulikana wanaongea nini, na baadaye shemeji akashindwa kavumulia akaeleeka kwenye hiyo ofisi na kuingia , walikaa huko kwa muda, na baadaye shemeji akatoka na kuanza kuondoka.

‘Vipi mume wangu mbona unaondoka na kuniacha…?’ mkewe akauliza

‘Wewe subiri mumalizane nao mimi natangulia kituoni, hakuna tatizo, muhimu kabidhi mtoto wa watu mengine tutaongea nyumbani….’akasema akiendelea kutembea

‘Mume wangu sio vizuri hivyo….’akalalamika mkewe

‘Fanya nilivyo kuambia kwa usalama wako…’akasema na mtoto ndiye aliyekatisha hayo mazungumzo ya wawili hawa ..kwa umri huo alishaanza kuongea ongea maneno, yaonekana pia alikuwa mzito wa kuongea, …., akasema

‘Baba-bye, kazini…zawadi eeh..’akasema na baba mlezi hakugeuka nyuma, mtoto akazidi kuita

‘Baba byeee, zawadi eeh..’alishazoea baba yake akiondoka kama yupo macho babayake huyo humbeba huyo mtoto na kumuambia;`bye nitakueleta zawadi ‘ lakini leo inaonekana tofauti baba anaondoka na hafanyi kama ilivyozoeleka.

‘Baba nanihii..njoo kwanza mtoto anakutaka umuage..’mke mtu akasema lakini mzee mzima ndio kwanza anachanganya miguu

‘Baba bye….zawadi eeh..’mtoto akawa sasa analia anataka kumfuata baba yake, ikabidi mama mlezi aanze kufanya kazi ya ziada, akasema

‘Sikiliza baby…baba kachelewa atakuleta zawadi eeh , haya njoo hapa ulale..’akaanza kazi ya kumbembeleza, na wkati anafanya hivyo hisia za kuwa huyo mtoto sasa sio wao tena na huenda leo ikawa ni mara ya mwisho kuwa naye, hisia hizo zikaanza kumuingia kwa kasi, hakuweza kuvumilia machozi yakaanza kumtoka.

***********
Kwa muda ule nesi alikuwa katoka, akiwa na majukumu mengine ya kikazi,na wakati anarudi ndipo akakutana na shemeji yake akashangaa kumuona shemeji yake akiondoka, na hata alipomfikia hakusema neno, wala kusema natoka au naondoka, ikabidi amuwahi na kumshika mkono.., akauliza

‘Vipi shemeji mbona unaondoka,…?’ akauliza

‘Mimi nimeshamalizana nao, iliyobakia ni wewe na dada yako,…’akasema shemeji mtu akivuta mkono wake kwa nguvu, na nesi akauachia akionyesha mshangao.

‘Lakini shemeji kuna mambo ambayo wanayahitajia,  na wewe yaonekana unayafahmu zaidi, ungesubiri tuyamalize kabisa…’akasema

‘Unanisikia mimi nimeshaongea nao, huyo mwanamke simjui….na huyo mtoto wewe ndiye uliyemleta ukatuomba tumlee, basi iinatosha, sina zaidi..’akasema akitembea kuondoka

‘Shemeji …shemeji..’nesi akawa anaongea lakini shemeji yake utafikiri sio yule mtu aliyemzoea akawa hata hataki kusimama mbio mbio akaelekea njia ya kutoka nje ya hiyo hospitali, hakutaka hata kumsubiria mkewe, sembuse huyo shemeji yake.

Nesi akajaribu kumfuata kwa nyuma shemeji yake lakini ndio kama anamfukuza hadi getini, shemaji akatoka nje,  ya hiyo hospitali. Ikabidi nesi amrudie dada yake ili ajue kuna nini kimetokea, kwani yeye alijua kuwa baadaye wote wataitwa kwa mkuu na kukaa kama kikao, kuyamaliza hayo mambo, na ikibidi huyo mama mzazi aitwe waongee kwa pamoja japokua hilo mama mzazi hakulitaka kabisa..zaidi ya kutaka mtoto wake.

Dada mtu hakuweza kuongea klilichokuwa kinaendelea yeye alikuwa akilia tu, hadi nesi akaona sasa mtoto anaweza kuiona hiyo hali, na kwa vile mtoto alishalala, yeye akamchukua huyo mtoto hadi chumba maalumu na kumlaza, na baadaye akarudi kwa dada yake.

‘Mbona shemeji kaondoka,….?’ Akauliza tena nesi

‘Hivi mume wangu ana nini…ina maana ule upendo  wote wa mtoto umekwisha, ….yaani anaamua kuondoka na kuniacha, …sijui ….’ Akawa aanongea na mdogo wake akafika na kukaa pembeni yake, akawa anamshika shika mgongoni kama kumbembeleza, mtu na ndugu yake hapo.

‘Shemeji inaonekana ana hasira zake sijui ni kutokana na nini, badala ya kusubiri tutafute ufumbuzi , anachukulia hasira  nahisi kuna jambo kati yake na huyo mama, una uhakika kweli walikuwa wakiishi vyema wakati huyo mama yupo hapo nyumbani kwenu?’ akauliza nesi

‘Hakukuwa na tatizo lolote, ila nilihisi namna ya mabadiliko ya tabia ya mume wangu, mara nyingi nilimfuma mume wangu akimuangalia sana huyo mama… nilimuuliza kwanini anamuangalia sana huyo mama, na alisema kuwa anamuonea huruma mama kama huyo..’akasema

‘Hebu niambie kabla hajakuoa, mumeo hakuwa na msichana…au ?’ nesi akajikuta anauliza swali

‘Mhh swali gani hilo tena, wewe unahisi kuwa  huyo mama, alikuwa na ….hapaan, haiwezekani, wewe huoni kuwa huyu mama ni mkubwa kuliko mume wangu..’akasema dada mtu

‘Mhh, ni shida ndio imemfanya huyo mama aonekane mkubwa, lakini, kiumri wala sio mkubwa sana..’akasema nesi

‘Unajua mambo ya shemeji yako ya huko nyuma hapandi kabisa kuyaongelea, nakumbuka wakati tunachumbiana aliwahi kunigusia kuwa aliwahi kuchumbia msichana wakati huo anatafuta mke, hatua ya mwisho huyu mchumba wake akamkimbia eti kwasababu kapata mume tajiri,…akifika hapo anakasirika na hapendi kuendelea kuliongelea hilo..’ akasema dada mtu.

‘Mhhh…’akaguna nesi akikumbuka yale maneno ya shemeji yake alipokuwa akiongea, kuwa huyo mtoto anafanana na mama yake na nusu na baba yake, ..mke mtu alijua anaongea kuhusu wao, kama baba na mama, lakini nsei alijua anaongea kuhusu mama yake mzazi na mume wa huyo mama, kwahiyo shemehi yake anawafahamu, ndio maana alitaka waliongelee hilo mbele ya utawala ijulikane moja.

Dada mtu hakuwa na shaka na mume wake kuhusu huyo mama akilini aliona ni jambo lisilowezekana kwa mume wake kuwa na mahusiano na huyo mama huko nyuma, akabadili maneno na kuuliza;

‘Nilikuona mkiongea naye pale,  kakumbia nini?’ akauliza dada mtu kwani aliwaona kwa mbali wakiongea mdogo wake na shemeji mtu.

‘Kasema tumrudishe huyo mtoto kwa mzazi wake, na hataki kumuona tena huyo mama na mtoto wake wakirudi kwenye nyumba yake…hiyo ni amri..’ akasema mdogo mtu.

‘Lakini sasa nyie mumefikia wapi, maana …hata sijui nifanye nini,….siwezi na sitaweza kukaa mbali na huyo mtoto, ni mtoto wangu jamani..’akasema na machozi yakimlenga lenga.

‘Mhh, dada kwa hatua iliyofikia hatuna la kufanya,…naomba uvumilie ujitahidi, ..na tutaona huko mbele itakuwaje, kama unahitaji mtoto ..nitafanya mipango, unajua wapo watoto, hawana wazazi….na mungu atasaidia ipo siku utapata mtoto wako..’akasema nesi.

 ‘Unajua mimi nawashangaa,  mtoto ana kosa gani…yupo kwenye malezi mazuri tu, kwanini huyo mama yake asisubiri, ..mtoto atakuwa basi huko mbeleni tutakuja kuongea..tutakuja kumfahamisha..’akasema

‘Hilo nililiongelea, lakini wewe hujakutana na huyo mama,..kabadilika, kawa mbogo…hataki kusikia chochote zaidi ya kumpata mtoto wake, hataki mtu kumchukua mtoto wake, kasema yeye mwenyewe atamlea, hata kama nikwa shida ….’ Akasema nesi

*********
Baadaye wakaitwa nesi na dada mtu kwenda kuongea kwa mkuu wa hospitali, na walipofika maelezo yalikuwa mafupi tu, kuwa mtoto keshapata mzazi wake, na kwa vile taartibu za kumchukua huyo mtoto hazikufuatiliwa, basi mtoto arejeshwe kwa mama yake na mengine yote yatategemea mama yake atakavyo penda.

‘Lakinni huyo mama hajiwezi , hana jinsi ya kijikimu..’akasema nesi

‘Kasema anaweza kuishi na mtoto wake kwa hali yoyote..’akaambiwa

‘Hivi kweli nyie mnaubinadamu, huyo mtoto katoka kwenye hali nzuri, analelewa vyema , leo hii umchukue akaishi , sijui wapi, kwani kawaambia anaishi wapi?’ akauliza nesi.

‘Hiyo kwa hivi sasa sio kazi yetu, kazi yetu ilikuwa kuhakikisha kuwa mtoto huyo kapatikana na tunamkabidhi kwa mama yake, sasa kama kuna amtatizo mengine, tutakuja kuyaona,….’akasema mtu wa usalama.
‘Kwahiyo…?’ akauliza mama mlezi

‘Mkabidhi mtoto nesi, yeye atajua ni nini cha kufanya, wewe tunakushukuru kwa wema wako, na ….mngelionana na huyo mama, lakini kwa hasira alizo nazo kuhusu nyie, ..hataki hata kuwaona,..alichosema anataka mtoto wake, ..’akasema

‘Lakini mbona tumeishi naye kwa wema tu, hatukuwahi kumfanyia ubaya wowote, kwanini afikia hatua hiyo..’akasema

‘Ilikuw kumbukumbu hazijamrejea, na kumbukumbu zimemrejea anahis huenda nyie mlifanya mpango ili afe ili mumuchukue mtoto wake,..hizo ni baadhi ya hisia zake, kwahiyo kuna hali ya kutokuwaamini,…’akasema.

‘Jamanio ndio kafikia kusema hivyo…’akasema huyo mama

‘Unajua hapo alipo, anahangaika kupata ukweli, bado hajawa sawa, anatakiwa awe karibu na mtoto wake, na hilo litampa faraja…’wakasema

‘Ina maana akishampata mtoto wake, itakuwaje, ataendelea kukaa hapa hapa..au atakwenda wapi?’ akauliza nesi

‘Hilo tutakuja kufahamu,….kwanza lifanyike hilo la yeye kukabidhiwa mtoto wake, mengine yatafuta …mama wewe unaweza kwenda, nasikia mume wako anakuulizia huko getini hajaondoka, anasema uende haraka…’akasema askari.

Basi angalau nikamuone mtoto kwa mara ya mwisho..’akasema na akaruhusiwa

******

Mama mlezi akafika pale alipolazwa mtoto! Akamwangalia yule mtoto, akajikuta machozi yanaanza kumtoka.

Kiukweli hakuamini kuwa mtoto aliyempenda kwa moyo wake wote, ndio imefikia mwisho wake wa kuwa naye. Akaanza kulia na wakati analia mtoto akafungua macho, mtoto akabakia akimuangalia mama yake huyo, na cha ajabu kabisa yule mtoto akainuka na kusogea pale alipo huyo mama akamfuta machosi akasema;

‘Mama lia….kwanini…?’ akauliza

‘Mhh mwanangu nakwenda sokoni nikirudi nitakueletea zawadi…’akasema

‘Mama- mimi -sokoni..’akasema

‘Huko kuna mbwa, ..huogopi mbwa wewe..’akasema mama mtu.

‘Mama…sini-ache. Mimi-sokoni…..’mtoto akawa kama anahisi kuwa huyo mama anaondoka.

‘Mwanangu ngoja nikavae.., nikja nakuchukua tunakwenda sookoni pamoja..’aliposema hivyo mtoto akafurahi, lakini mama mtu akashidwa kuvumilia, akaanza kutoa machozi, akageuka na akajiukuta analia kwa kwikwi sasa.

Nesi kuona hivyo akamshika dada yake mkono na kumtoa nje, akamuita nesi mwingine aende kukaa na huyo mtoto, ili asije akatoka

‘Hakikisha huyo mtoto hatoki, ngoja nimsindikize dada yangu..’akasema na maensi na madakitari ambao walikuwepo hapo walikuwa hawajui kabisa ni nini kinachoendelea wakabakia kuangalia tu, wakiulizana, kwani swala hilo lilikuwa halijulikani kabisa kwa watu wengine zaidi ya dakitari mkuu na dakitari bingwa, na nesi mmoja ambaye yupo likizo.

Nesi akamfikia dada yake akiwa kasimama, alikuwa kshikiliwa ukuta kainamisha kichwa, akamsogelea na kumshika begani, huku akisema ;

‘Dada sasa ni bora uondoke, shemeji anakusubiria nje…’akasema nesi

‘Hapana mimi sikubali, huyu ni mwanangu, huyo mama anakuja kudai huyo mtoto sasa baada ya miaka miwili…, sikubali kumwachia mwanangu…..’aliposema hivyo ikaonekana dada mtu  akiyumba, na kabla nesi hajamshikilia vyema, dada yake akadondoka chini,….na alionekana kupoteza fahamu

‘Oh nini tena dada….jamani njooni mnisaidie….’

WAZO LA LEO: Mawazo yakizidi sana ni hatari, kama wanadamu tuna matatizo mengi, na wakati mwingine mtu huja kushindwa kujizuia, akatawaliwa na mawazo, na hapo huwa ni ugonjwa.


Mawazo huja kuleta atharai nyingi mwilini. Mtu kama huyu pamoja na kujisaidia yeye mwenyewe, lakini watu wanaishi karibu  naye wanaweza kuwa dakitari wa kwanza, kwa kujaribu kumsaidia kwa ushauri nasaha, kwani madhara ya hayo mawazo yanaweza kuwa makubwa na mkja kuhangaika sana .
Ni mimi: emu-three

No comments :