‘Huyo mwanamke ni nani..?’ swali likaulizwa
‘Ni yule mama mliyekuwa mkiishi naye, aliyekuwa akiitwa mama wa
mitaani, akaja kuitwa mama wa mkono wa baraka, ambaye aliletwa hapa kutibiwa kutoka
huko kwenu akiwa kaungua…ndiye huyo anayedai kuwa mimi nimemchukua mtoto
wake…sasa mtoto huyo ni nani, kama sio huyo mtoto wenu….’ akasema nesi
Shemeji mtu ambaye alikuwa kakaa sasa akasimama, na kuanza kukuna
kichwa mfufululizo, akainama akiwaza jambo, halafu akainua kichwa na
kumuangalia mkewe, akatembea hatua moja mbele, halafu akasimama…
Nesi alipofika ofisini kwake akawakuta mabosi zake wanamsubiria,
wakiwemo wale watu wa usalama wawili. ambao alishawahi kuonana nao, na safari hii wakaongozana na mwanamke mmoja akiwa kavalia sare za kipolisi....
Tuendelee na kisa chetu.
**********
Wanandoa hawa waili walifika nyumbani wakiwa kimia, utafikiri
wametoka mahakama ya usuluhishi wa ndoa
na kutokuafikiana, na walipofika nyumbani mtoto walikuwa amelala na
aliyewakaribisha alikuwa mfanyakazi wao ndani, akasalamia akaitikiwa na aliona
ajbu furaha ya watu hawa walipoondoka sio kama walivyorudi,
Yule mfanyakazi kwa vile aliwazoea hakusita kuuliza,;
‘Mama kuna nini , mbona naona mumebadilika?’ akauliza
‘Hamna shida na kuchoka , unajua safari yenyewe na usafiri ulikuwa
ni shida…’akasema
‘Oooh poleni, namuana baba kama anaumwa, …’akasema na wakati huo
baba mwenye nyumba alifufuliliza moja kwa moja hadi pale alipolala mtoto,
akainama kumtizama alimtizama kwa muda, halafu akageuka kuondoka akakutana na
mkewe naye akija kumtizama mtoto.
‘Twende huku…’akamshika
mkewe mkono, na mkewe akamfuata wakatoka ndani ya nyumba hadi kwenye mti, ambao
hupenda kukaa wakiwa na mazungumzo yao, hakutaka kuliongelea ndani, asije
akasikia mfanyakazi au kumuamusha mtoto.
‘Nimeamini..?’ akaanza kusema
‘Umeamini nini…?’ akauliza
‘Japokuwa hajaamuka, lakini naiona sura kama yake..’akasema
‘Una maana mtoto wetu?’ akauliza mkewe
‘Unasikia usitake kunichefua,..tunachozungumiza hapa ni nini….ni
hivi huyu mtoto kweli na wa huyo mama..’akasema
‘Haiwezekani umejuaje,..?’ akauliza
‘Sura yake na huyo mama havidanganyi..’akasema
‘Mhh mume wangu umejuaje maana nijuavyo yula mama muda wote
hujifunika, sasa wewe ulimuona wapi…?’ akauliza mkewe,
‘Mbona sikumjua mapema huyu
mwanamke,… au ndio kwasababu kapata adhabu yake, muda wote kajifunika uso, ili
kuficha adhabu ya uovu wake…. Poteleambali, amepata alichokitaka, mimi
ninachoweza kusema sasa hivi ni kuwa sitaki hata kumsikia…si-wamesema mtoto
huyu ni wa kwake,…eeh, sasa waje wamchukue haraka iwezekanavyo..’akasema
‘Mume wangu vibaya hivyo, huyo ni mtoto wetu, ….’akasema
‘Natumai umenisikia,…kesho mguu kwa mguu tunamrudisha huyu mtoto
hospitalini..sitaki blaa hapa, na usitake kujua zaidi,…., vinginevyo, hutaamini
kitakachotokea…..labda mimi sio mwanaume
wa hii nyumba..’akasema na alipomaliza hapo akasimama na kuondoka zake
Mama mwenye nyumba akabakia kauduwaa, akainamisha kichwa hadi
aliposikia mtoto akimuita
‘Mama….mama…’
**********
‘Nesi tumekuja hapa ofisini rasmi…baada ya kufikiwa na hawa watu,
hawa ni watu wa usalama wamekuja kufanya kazi yao baada ya kufanya uchunguzi wa
kina wamegundua mengi tu, na moja wapo ni kuhusu huyo mtoto anayetafutwa na
mama yake..’akatulia.
Nesi akageuka kuwaangalia akaona kuna mwanamke akiwa akshika
pingu, akajua leo kuna mambo, leo ndio siku yake ya mwisho na huenda aakapoteza
kazi.
‘Wao baada ya kujirizisha, wamegundua kuwa huyo mama ana haki na
anayoongea yana ukweli, nay a kuwa yeye ni mama halali wa huyo mtoto uliye
mchukua wewe, na ni kweli kuwa wewe ulimchukua huyo mtoto kutoka hapa
hospitalini kama alivyodai huyo mama..’akaendelea kuongea huyo mkuu wa hiyo
hospitalini na nesi akabakia kimia.
‘Hatujui kwasababu gani ulimchukua, huenda mlikuwa na nia
njema, …lakini hiyo nia njema ni wewe wa
kutuambia, …vinginevyo sisi tutafuata taratibu zote za kisheria za utawala na
watu wa usalama watafuta sheria zao za kiusalama….’akasema
‘Tulikupa muda wa kutosha, ukawa unavuta muda natumai sasa una
jambo la kutuambia,…’akaendelea kusema, alikuwa akiongea hatua kwa hatua, huku
akisubiri kama nesi atasema nini, lakini nesi akawa kimia tu.
Nesi likuwa kazama kwenye mawazo akiwafikiria ndugu zake, ambao
wameondoka bila kumpa jibu lenye muafaka, na hakujua afanye nini kwa muda kama
huo, asemeje…, na hapo anatakiwa kutao jibu lenye kuwarizisha hao wakubwa zake,
akatulia huku akimuomba mungu ampe kauli yenye muafaka.
‘Sasa nesi tuambie ilikuwaje ukamchukua mtoto wa huyo mama, najua
utakuwa ana sababu,..maana hilo ni kosa kubwa sana, ina maana gani kisheria kama
sio kuiba mtoto au utatuambiaje kama huna maelezo yenye kujitosheleza, unawea
kutuambai ilikuwaje, ..?’ akaulizwa
‘Mimi sikumchukua mtoto huyo kwa matakwa yangu,…sikuiba mtoto,
naomba mbadilishe hiyo kauli yenu, naomba
mnielewe hilo, ndio maana nilitaka kuwasiliana na waliohusika, kunibebesha hiyo
dhamana,…hivi kwanini hamjiulizi hilo kwanini mimi nimchukue mtoto wa mtu ....ili
nipate nini….’akasema nesi akionyesha uso wa kukasirika.
‘Ndio maana tulisita kuchukua hatua stahiki, tukawa tunakupa muda,
tulijua ni lazima kuna sababu ya msingi, sasa ili kujikosha kwa hilo tunaomba
utuelezee kisa na mkasa..au sio? ’akaambiwa na huyo mkuu akiwageukia watu wa
usalama.
‘Kisa na mkasa zaidi sina, zaidi ya kuwaambia kuwa mtoto huyo
nilikuja kupewa, baada ya mama yake kuondoka, mama yake huyo ninemjua mimi ,alitoroka
hospitalini, na kwa vile ilionekana mimi ndiye mwenye makosa nikaambiwa
nimchukue huyo mtoto nimlee mimi,….ndivyo ilivyokuwa…’akasema
‘Wewe ndiye mwenye makosa, makosa gani?’ akaulizwa na watu wa
usalama.
‘Mimi nilikuwa nesi kwenye hiyo wodi kipindi hicho, nikapewa
jukumu la kuwa na huyo mama akiwa chumba cha mahututi, wakati hana fahamu,..ikafikia
muda maji na dawa vikawa vimekwisha ikabidi nitoke kwenda kuchukua hizo dawa na
maji ya kumtundikia…., niliporudi nikakuta huyo mama katoroka, nikatoa taarifa…msako
ulifanyika huyo mama hakupatikana, ndio nikabebeshwa hiyo dhamana ya mtoto…’akasema
‘Kwahiyo ulibebeshwa hiyo dhamana kama nini, kama adhabu au…ilikuwaje?’
akaulizwa
‘Ni kama adhabu..ndio…’akasema
‘Kwahiyo huyo mtoto ukampeleka wapi?’ akaulizwa
‘Huyo mtoto …’hapo akatulia akiwaza
‘Tunajua wapi alipo huyo mtoto, ndio maana ndugu zako walifika
hapa, tunajua yote kuwa huyo mama alikuwa akiishi kwa ndugu zako kipindi
kulipotoeka janga hilo la moto,….hayo tumeshayafanyia uchunguzi, na tulitaka
kuongea na ndugu zako ili tulimalize kwa amani, lakini nadugu zako wakawa wakaidi..’akasema
mkuu
‘Hawakukaidi, ila taratibu za kuwataka muongee nao hazikuwa za
kiungwana,….’akasema nesi akimuangalai mkuu wake.
‘Sasa kwanini hukutaka kuwa mkweli muda wote huo, maana kwa
maelezo yako inaonyesha kuwa wewe hukuwa na makosa ulibebeshwa dhamana na
kilichotokea ni bahati mbaya….’akauliza na watu wa usalama.
‘Baadaye ilikuja habari kuwa huyo mama kafariki, ina maana
kutokana na huo uzembe mimi ningelichukuliwa kama msababishi wa kifo cha huyo
mama, ndio maana jambo hili likafanywa liwe siri..’akasema
‘Lilifanywa liwe siri ya nani na nani..?’ akaulizwa
‘Watawala na mimi…’akasema
‘Ok…hata hivyo ungetuambia sisi tungelijua la kufanya, …kuna mambo
mengi yalitokea hapa,kwa hao waliokuwa watawala wako, kuna ..wizi,
ubadhirifu,..na hujuma mbali mbali…na wewe ulikuwepo kipindi hicho,
..tulishindwa kukuingiza moja kwa moja kwenye hilo kosa maana wewe kipindi
hicho ulikuwa nesi mdogo tu…’akasema mkuu.
‘Ni kweli mimi sikuwa na mamlaka yoyote zaidi ya kufuata amri….’akasema
‘Kosa lako kubwa na kutokutoa ushirikiano…’akaambiwa
‘Mimi nilitakiwa kufanya walivyotaka wakubwa zangu, hebu
chukulieni nafasi yangu..hivi kweli mngelifanya hivyo mnavyotaka nyie…?’ akawa
kama anauliza
‘Sasa nesi, sisis tunataka kulimaliza hili kiutaratibu na kisheria
ili kesho na kesho kutwa kusitokee kitu kama hiki tena..sisi ni watendaji na
tumepewa majukumu, na tunatakiwa tuonyeshe mfano mwema,…sasa,sijui wewe
utafanyaje, ..’aaksema mkuu
‘Kufanya nini..?’ akauliza nesi sasa akionyesha wasiwasi.
‘Wewe unasema ulipewa dhamana ya mtoto,..innawezekaan ilikuwa ni
adhabu au kushindwa kuwa na maamuzi yenye hekima…wao wakaona wakwepe jukumu kwa
kukukabidhi huyo mtoto,…sasa kama ulivyokabidhiwa hiyo dhamana, tunakutaka wewe
, uirejeshe hiyo dhamana kwa wenyewe..’akaambiwa
‘Kwa wenyewe akina nani?’ akauliza nesi
‘Ulikabidhiwa hiyo dhamana kibinfsi au kisheria…?’ akaulizwa
‘Mimi sijui..na sikutaka kulifuatilia hilo.., maana nishachanganyikiwa,
..nilikuwa nesi mdogo tu, ….nakumbuaka kuna muda nilishauriwa na mmoja wa
madakitari waliokuwepo hapa kuwa niandikishe kisheria, lakini tuliposikia kuwa
huyo mama kafariki, tukajua huyo mtoto sasa ni wetu..’akasema
‘Sawa nauliza hivi , wakati unapewa huyo mtoto ulipewa kibinafsi
au na utawala wa hospitali?’ akaulziwa
‘Na utawala wa hospitali..’akasema
‘Sasa ni hivi, kwa vile utawala ndio ulikukabidhi hilo jukumu,
basi dhamana hiyo irejeshe kwa utawala ..’akaambiwa
‘Utawala huo haupo…’akasema
‘Utawala muda wote upo, kutokuwepo kwa hao watawala wa muda huo,
hakusababishi utawala usifanye kazi yake, sisi tupo, ..sisi kwa hivi sasa ndio
watawala wa hii hospitalini, tunahitajia huyo mtoto arejeshwe na
tutaandikishana kisheria kumpokea huyo mtoto, na kama ….’akakatisha na
kuwaangalia watu wa usalama.
‘Na kama mama huyo halali wa mtoto, atakubali muendelee kuwa naye,
sasa hapo itakuwa ni jambo jingine..’akasema
‘Lakini mtoto huyo nilishawakabidhi ndugu zangu, na nikawaambia
kuwa huyo sasa ni mtoto wao kwa vile mama yake hayupo tena..inaniwia vigumu
kuwashawishi vinginevyo…’akasema
‘Ndio maana tukatangulia kukuambia kuwa hilo sasa ni jukumu lako,
kama ulivyokabidhiwa na kwenda kuwashawishi kuwa wamkubali huyo mtoto kama
mtoto wao, ..basi fanya hivyo hivyo, tumia busara zako kuwashawishi kuwa mama wa
huyo mtoto sasa kapatikana..’akaambiwa.
‘Lakini mna uhakika gani kuwa huyo ni mama yake?’ akaulizwa
‘Sisi tulishafanya uchunguzi, hatuna shaka na hilo..na kuna siku
tulituma wataalamu kule kijijini, kutoa chanjo kwa watoto, wataalamu hao hao wa
chanjo, ndio waliotuwezesha kupata damu ya huyo mtoto, na tulipolinganisha na
damu ya huyu mama, tukaona ni sawa…siku hizi kuna vipimo vya DNA, si unajua
hilo …’akasema
‘Oh….’nesi akaguna.
‘Sasa baada ya hapo, tutaangalia utaratibu mwingine kisheria, kama
itaonekana wewe hujavunja sheria, na huhusiki kweli basi tutaona la kufanya,
ila ni lazima taratibu zifuatwe, hawa ni watu wa usalama, utaongozana nao, hadi
kituoni, huko mtaandikishana kiutaratibu wao …mengine yatafuata baadaye…’akaambiwa
‘Sasa mnataka kunifunga…?’ akauliza na kabla hawajamjibu akasema
‘Mkinifunga ni nani atakwenda kuwashawishi ndugu zangu…?’ akauliza
‘Hakuna aliyesema unakwenda kufungwa,…hizi ni taratibu tu za
kiusalama,wewe utakwenda kuandikisha na ..wao wanajua ni nini kifanyike,
kitakachofuata hapo ni taratibu tu, sisi tupo na wewe, ukumbuke kuwa wewe ni
mfanyakazi wetu, tutaona ni nini kitakachofuata kiutaratbu, lakini lazima
taratbu zifuatwe..’akasema mkuu
‘Mhh..yaani nyie ndio mnanifanyia hivyo..’akalalamika nesi.
‘Kwani wewe una wasiwasi gani..?’ akauliza mtu wa usalama.
‘Najua mnakwenda kunishikilia, …kuniweka rumande, hamuoni kuwa
mnanizalilisha kwa kosa mbalo sikulifanya mimi..’akalalamika nesi
‘Wewe usijali,…sisi tunajua ni kitu gani tunachokifanya,
muhimu..tuhakikishe kuwa taratbu zote za kisheria zimefuatwa, na waliokuwepo
hapa wote waliohusika kwenye makosa mbali mbali ni lazima wanafikishwa
mahakamani..’akaambiwa
‘Lakini ndugu zangu hawahusiki..’akajitetea nesi
‘Tunajua hilo..na hilo …la wewe kufikishwa huko, …. huenda
likakusaidia, …’akaambiwa
‘Kwa vipi?’ akauliza nesi akionyesha wasiwasi wa dhahiri.
‘Sisi tunachotaka ni mtoto au sio….sasa acha tufanye kazi yetu…na
pili kuna mambp mengi bado tunahitajia kufahamu kutoka kwako…kwa ajili ya huyo
mama, na yaliyowhi kutokea hapa…’akaambiwa na mkuu wake, na kuwapa ishara watu
wa usalama, na watu wa usalama
wakasimama.
‘Lakini mimi sijui zaidi…simjui huyo mama..’akalalamika nsei
‘Twende zetu tusipoteze muda,..utawapigia ndugu zako simu
tukishafika huko kituoni…wao wanajua zaidi unavyojua wewe…’akaambiwa na watu wa usalama wakiwa
wameshikila pingu.
‘Sitaki kufungwa pingu ninakwenda kwa hiari yangu mwenyewe.’akasema
na yule mwanamke wa usalama akatabasamu.
NB: Hii sehemu ina umuhimu wake kwa wenye kujua
WAZO LA LEO: Kunapotokea kosa, sheria hufuatwa, na
kusiwe na ubaguzi wa kuangalia sura au kabila,urafiki au umwenzetu, …ni muhimu
kusiwe na upendeleo wa aina yoyote ili kweli hiyo sheria ifanye kazi yake
ipasavyo, kwani sheria ni msumeno kukata mbele na nyuma.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment