Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, April 21, 2015

NANI KAMA MAMA-62


 Nesi akiwa kapewa nafasi ya mwisho, vinginevyo utawala unamchukulia hatua za kinidhamu, na haitaishia hapo, hatua itakayofuata ni yeye kufikishw mhakamani kwa kosa la kumchukua mtoto wa mama wa mitaani…

‘Mama keshasema akitoka hapa anakwenda mahakamani, japokuwa alisema mwanzoni yeye hahitaji kwenda mahakamani anaweza kuomba kwa mungu jambobaya likampata kila aliyeshiriki, lakini kaona kuwa walimchukua mtoto wake hawakuwa na nia nje..’aliambiwa

‘Unaona kwa vile anajua hana haki..ni mwongo huyo mama, anatumia viini macho kuwahadaa watu,mimi bado sijamuamini na pia sina lolote kuhusiana na hizo shutuma..’akasema

‘Kama wewe umejiaminia hivyo, acha sisi tuone la kufanya..ila tunakumpa nafasi ya mwisho ya kulifikiria hili usije kutuona wabaya..’akambiwa

Basi nei alipotoka hapo akiwa hajui hata afanye nini, akaona akajaribu kumigia simu tena dakitari kijana kama anaweza kupatikana, na akimaliza hilo inabidi akaongee na ndugu zake ili wajua ni nini kinachoendelea hakupenda kabiasa kuwahusisha na kinachoendelea mpaka awe na uhakika, lakini kwa hali ilivyo, anajua kuwa ndugu zake hao wanaweza kuingiliwa na polisi, ..

‘Hapana, kwanini…kwanini hawa ambosi zangu hawanielewi….’akawa anaongea peke yake.

‘Ni wakati nesi anatoka,…akiwa akili imevurugika mara macho yake yakaona jambo…

Kwenye wodi ya wazazi, alimuona mama  akiingia , akahisi huyo mama hastahiki kuingia huko..na alikuwa na uhakika sio mfanyaakzi wa hapo, na kulishapigwa marufuku mtu ambaye sio mfanyaakzi wa hapo kuingia eneo hilo tena kwa kupitia mlangowa dharura…kuna mpango bango limewekwa hapo mlangoni,…akaona aende kuongea na nesi aliyekuwepo hapo kwa muda huo,.

Kitu kilichomtia mashaka nesi huyu mkuu ni uvaaji wa yule mama , mama huyo alijifunika kama yule mama wa mitaani, nesi  akaamua kumfuatilia huyo mama kwa nyuma, na kwa kumbukumbu zake yule mama wa mitaani likuwa wodini kwake kalala, sasa huyu mama ni mama gani. Alikimbia hadi kwenye wodi hiyo ya wazazi, na kukuta mhusika pale naye katoka, akaaanza kuhisi wasiwasi.

‘Na huyu nesi naye kaenda wapi kwanini kaacha mlango huu wa dharura wazi..’akaanza kusema ukali, lakini kabala hajafanya lolote mara akasikia sauti nyuma yake.

‘Vipi mbona upo mbiombio…ni maswala ya huyo mama nini…’ akagutuka na kugeuka nyuma, na nesi aliyekuwa zamu kwenye wodi hiyo ya wazazi alikuwa kabeba sinia la dawa na vifaa vingine.

‘Mbona umeacha mlango wazi..?’ akauliza

‘Mlango wazi, hapana mimi nilihakikisha nimefunga huo mlango kabla ya kutoka, labda kaja mtu mwingine akaufungua, ..’akasema huku akionyesha ufunguo wake.

‘Nahisi kuna mama kaingia humu kwa kupitia mlango huu.., ambaye hastahili kuingia humu, na…’ aliposema hilo akasikia sauti ikiita kutokea ndani

‘Wewe nesi upo wapi, nataka mtoto wangu…’ ilikuwa ni sauti ya mama wa mitaani, nesi mkuu akashituka, akageuka nyuma kama vile anaweza kuona kule kwenye wodi maalumu, maana ana uhakika huyo mama alikuwa kalala, na kama katoka basi atakuwa aktumia mlango wa dharura kutoka kwenye wodi hiyo, na mlango wa dharura aliufunga yeye..

‘Mhh haiwezekani….’akasema

Tuendelee na kisa chetu

***

Yule mwenzake kusikia sauti huko ndani kwa haraka akikimbilia huko wodini huku akikumbuka matukio yaliyowahi kutokea kwa mama mmoja kupita mahospitalini na kuiba watoto, akitumia visngizio mbali mbali…alimuacha nesi mkuu akiwa kashikwa na mshangao.

Nesi huyo wa zamu kwenye hiyo wodi, alipofika akamkuta mama aliyejifunika uso akikagua vitanda vya wazazi na kila aliyempita alikuwa akimuulizia kuwa anajua lolote kuhusiana na mtoto ambaye hana mama…na akina mama waliolazwa hapo ambao wengi ni wajawazito wakawa wanashangaa tu.

Yule nesi naye alipomuona huyo mama akabaki kaduwaa, akishindwa kuelewa maana huyo mama alitakiwa kuwa wodi ya wagonjwa maalumu na alijua yupo huko,..sasa hapa kaja kufuata nini,…akashindwa hata afanyaje,…

‘Mhhh ni huyu mama mbona leo limenikuta….hata sijui nifenye…’ alijikuta akisema kwani  alishasikia visa vya huyo mama, na vingi vya ajabu ajabu, akaogopa kumsogelea akijua dhahama lake,… lakini kwa vile yupo kazini akaamua kuchukua hatua akamsogelea yule mama na kutaka kumuuliza, na alipomkaribia tu yule mama kwa haraka akageuza kichwa kumuelekea huyo nesi na kwa sauti ya ukali, akasema;

‘Sio wewe ninayekutafuta…namataka yule mwezenu , yule mnayemuita nesi mkuu…’sauti nzito ikamtoka huyo mama wa mitaani, ikamfanya nesi huyo wa zamani kurudi nyuma na kusimama.

‘Samahani mama,  humu hakuruhusiwi kuingia mtu baki, unaona hao akina mama wote humu wanasubiri kujifungua,wewe unakuja huku kufuata nini… na huyo nesi ana ofis yake mfuate huko ofisini kwake…’akasema

Yule mama akamgeukia huyo nesi, na wakawa wamesimama karibu karibu wakiwa wameangaliana nesi akahisi mkojo kumtoka…alikuja kusema kuwa aliona kwenye matundu ya macho ya huyo mama, kwenye kile kitu alichovaa, macho ya ajabu..lakini akajitahidi akajipa moyo, akasimama vile vile.

Cha ajabu huyo mama,  kwa haraka akapiga magoti na kuanza kuongea;

‘Sio wewe ninayekutafuta,namtaka yule nesi mwingine, anajua wapi mtoto wangu alipo, au na wewe sijui kama unajua lolote kuhusiana na mtoto aliyekosa mzazi wake…ulishawahikusiki kitu kama hicho hapa hospitalini kwenu….?’akasema huyo mama,  nesi huyo akiwa kaduwaa tu, hakusema kituna baadaye huyo mama akarudia yale maneno na kusema zaidi.

‘……mimi ndiye mzazi wa mtoto huyo….tafadhali kama umesikia niambie haraka…’akasema

‘Mtoto aliyekosa wazazi , mbona hakuna mtoto kama huyo..’akasema nesi.

‘Unajua ni muda,..nafahamu mtoto wangu kwa sasa atakuwa mkubwa…huenda keshaanza kutembea, jamani….’akasema kwa sauti ya huruma.

‘Nesi…tafadhali….’akasema akiinua uso kumuangalia nesi..

‘Mtoto wangu yupo wapi..’akasema sasa akiwa kainua uso kumuangali nesi.

‘Sikiliza mama sisi hapa tupo kazini, nakuomba utoke humu ndani..’akasema nesi

‘Tafadhali nesi naomba msaada wako, nipo chini ya miguu yako, kama unajua lolote kuhusu mtoto aliyeachwa na mama yake,….naomba unionyeshe wapi alipo…nesi hebu fikiria wewe umejifungua mtoto halafu unapatwa na ..kuchanganyikiwa unaondoka…..’akatulia.

‘Haoa hatuhifadhi watoto, akina mama wakishajinfungua wanakwenda wodini hapa hakuna mtoto ..’akasema nesi

‘Nesi tafadhali….mimi  sikupenda kabisa kumuacha mwanangu, naomba tafadhali unisaidie, wewe kama mzazi , wewe kama mke, wewe kama nesi, naomba tafadhali ..’ akiwa bado kapiga magoti na kumshika huyo nesi miguu, na yule nesi akawa anashangaa tu, hakujua kabisa nini kinachoendelea, hakujua amfanyeje yule mama…

‘Wewe mama…’mara mlango ukafunguliwa

**********

Wakati haya yakiendelea huku kwa dada yake nesi, kulikuwa na fuaraha kubwa sana, baada ya sherehe fupi ya kujipongeza, waliamua kufunga safari kuja huku mjini, kumutembelea ndugu yao, na walipofika walisubiri mapokezi, huku ndugu yao akitafutwa, kwani simu yake ilikuwa haipatikani na wapi alipokwenda ikawa ni kitendawili.
‘Nyie subirini , huyo yupo kwenue mihangaiko, yeye hapa ni nesi mkuu, kwahiyo kila sehemu anapitia kuona mambo yapo kama yanavyotakiwa kuwa…nilijua atakuwa huko kwenye wodi maalumu, lakini huko tumeambiwa katoka….’akasema mtu wa mapokezi.

‘Tatizo tumekuja bila kumuarifu…’akasem dada mtu.

‘Msijali, mtaonana naye tu…’akasema huyo mtu wa mapokezi.

Nesi aliyekuwa akitafutwa kumbe alikuwa kashikwa na kichwa cha ghafla, akasikia kitu kama kizunguzungu akadondoka na kupoteza fahamu, aliyekuja kumuona ni mlinzi,akatoa taarifa na huyo nesi akabebwa hadi chumba cha dakitari, na alipofikishwa huko akazindukana.

‘Vipi nesi ..kazi zimekuwa nyingi nini, …?’ akaulizwa

‘Kwani yule mama yupo wapi?’ akauliza

‘Mama yupi, ..?’ akaulizwa

‘Mimi nina uhakika nilimuacha wodini, akiwa kalala..sasa huku kafuata nini…waiteni walinzi wamrudishe wodini kwake..’akasema

‘Nesi tulia kwanza, kwa hali kama hii utachanganyikiwa, unajua umeokotwa nje ukiwa umedondoka, umepoteza fahamu…’akaambiwa

‘Hapana,..sija……oh, lakini hilo ninalokuambia ni muhimu yule mama wa mitaani kaingi wodi ya wazazi anaweza kuleta madhara, waiteni walinzi wamarudishe wodini kwake….’akawa anasema na yule dakitari akawa kama anamshngaa nesi, akaona kama huyu nes kachanganyikiwa nini,….alichoweza kusema ni..

‘Kwani nesi unajisikiaje kwa sasa..?’ akaulizwa

‘Umenielewa lakini docta, ..ngoja niende mwenyewe.’nesi akasema akitaka kuondoka

‘Nesi tulia kwanza, upo kwenye kuchunguza hali yako,huwezi kuondoka kwanza, hebu nisikilize..’akasema docta

‘Sikilizadocta hili ninalokuambia ni muhimu sana, mimi hapa sijambo,,,unanielewa, yule mama wa mitaani katoroka wodini kwake, na kwenda wosi ya wazazi, wakati namfuatilia ndio nikadondoka….’akasema nesi.

‘Lakini yule mama yupo wodini kwake, mimi nimetokea huko ..nilipoitwa kuwa wewe umeokotwa nje ukiwa umedondoka..’akasema huyo docta.

‘Mhh,…una uhakika, umemuacha huyo mama wodini kwake..?’ akaulizwa

‘Mimi nimetokea huko sasa hivi huyo mama kama ndiye unayemsema nimemuona kwa macho yangu yupo kalala…’akasema

‘Haihawezekani…basi kuna jambo, kuna …hapana, hili sasa sitaweza kulivumilia tena,..huyo mama sio wa kawaida, kumbe anaweza kujigeuza hivyo …..hapana mimi nemshindwa…’nesi akawa anaongea mwenyewe kama kapagawa.

‘Wewe una uhakika ulimuona huyo mama…?’ akauliza docta akipiga simu kwenye hiyo wodi maalumu.

‘Eti huyo mama ….eeh, yupo kitandani kwake, mna uhakika…?’ akauliza na kukapita muda, baadaye akarudisha simu mahali pake akasema

‘Yupo kalala….’akasema docta.

‘Mhh hiyo mpya, kama mnbisha hebu muulizeni nesi wa waodi ya akina mama, atawambia hayo yote..’akasema

‘Lakini cha muhimu ni kuwa huyo mama yupo kalala wodini kwake, kwanini tuhangaike kuulizia hayo, kwani kuna tatizo..’akasema huyo dakitari.

‘Docta mimi sasa nimechoka, unajua kuchoka…mimi  nilikuwa na nia njema, lakini sasa ..hapana huyu mama ataniua, hata mansema huyo mama huko kwenye wodi ya wazazi sio yeye, basi kuna tatizo…. sitaweza kuvumilia tena…’akawa anaongea huku akishuke kwenye kile kitanda alichokuwa kalala na dakitari akawa anamuangalia tu.

‘Docta mimi nipo safi naweza kuondoka..?’ akauliza nesi akiwa kasimama na akamuona huyo dakitari akimuangalia tu, na nesi alipoona hivyo akaanza kuondoka, na huyo dakitari akasema;

‘Unaweza kwenda lakini ningekushauri uende nyumbani ukapumzike…’akasema

‘Haaah, unafikiri, mimi nipo safi mbona docta, sina tatizo…’akasema

‘Kama huna tatizo kwanini ukapoteza fahamu?’ akamuuliza

‘Hata sijui, kuna kitu kilinijia tu…nikahisi kizunguzungu, na sikumbuko kilichotokea, na nilipozindukana najikuta nipo hapa…lakini sina matatizo  akinyosha nyosha nguo yake, na kutoka pale kwa dakitari..na alipofika nje ndio akakutana na mtu wa kupeleka ujumbe na kusambaza barua.

‘Nesi kuna wageni wako wamefika muda tu..’akaambiwa

‘Wageni wangu kutoka wapi?’ akauliza

‘Kutoka kijijini…’akaambiwa

‘Mhh kuna nini tena..mhh afadhali wamefika, sasa nitaongea nao kila kitu..’akasema na kuelekea sehemu ya wageni.

Yule nesi alipita wodi ile ya wazazi, wakati anaelekea sehemu ya wageni, akaona apitie hapo wodini kuhakikisha alipofika akamkuta nesi mwingine.

‘Nesi uliyemkuta keshaondoka..?’ akauliza

‘Kaondoka, na..siunajua anaanza likizo, ..’akasema

‘Oh kweli..hakukuambia lolote kuwa kuna mama kaingia humu, wodini..?’ akauliza

‘Hapana…na sikuwa na muda wa kuongea naye maana alikuwa akiwahi usafiri anasafiri leo kwenda kwako mkoani kwake…kwahiyo sasa hivi atakuwa kwenye basi la kwenda kwao..’akaambiwa

‘Mhh….’akasema an kulipitia daftari la kumbukumbu ambalo kama kuna tukio muhusika anatakiwa kuandika, akaona hakuna kilichoandikwa, akataka kwenda wodi maalumu alipolazwa huyo mama lakini akakumbuka kuwa hana simu yake hakukumbuka wapi walipoiacha…baadaye akakumbuka kuwa kaicha ofisini kwake.

Akapitia ofisini kwake kwanza,ili kuichukua simu yake akakuta imezima.., na ilipowaka akakuta kuna simu zilikuwa zikimtafuta na mojawapo ni simu ya dada yake, akaipiga hiyo simu ya dada yake..

‘Vipi sisi tunataka kuondoka tumekuja muda mrefu, wanasema hauonekani wapi ulipo, upo nje ya hospitalini nini..na mbona umezima simu yako…?’ akauliza dada yake.

‘Hapana…, nipo humu humu hospitalini, subirini nakuja….’akasema na kukata simu. Alikimbilia haraka mapokezi na kuwakuta dada yake na shemeji yake.

‘Vipi jamani, mbona mwaja bila taarifa kuna jema huko..’ akauliza akimuangalia shemeji yake ambaye siku nyingi hawajaonana hata kupigiana simu, kila akimpigia simu anajikuta anaongea na dada yake.

‘Kuna jema sana, ..yaani ni furaha kwa kwenda mbele…na ndio maana tumekuja , kwani tumekusubiri tukaona huji labda kuna matatizo huku kazini…’akasema dada mtu akijitikisa tikisa kuonyesha furaha.

‘Haukuna matatizo, ni mambo ya kawaida tu…ila kiukweli nilitaka kuja huko..’akasema nesi akisita sita kuongea alicho nacho moyoni

‘Kuja , ungekuja tu, …nyumbani kwako huko…’akasema dada mtu, shemeji mtu ambaye mara nyingi wakikutana anakuwa muongeaji lakini kwa leo hakuonekana hivyo na nesi akamtupia jicho na akashindwa kuvumilia akauliza;

‘Shemji vipi, upo sawa kweli...nakuona kama haupo hapa, umekuja kwa mkeo halafu unamfikiria mwingine unanitisha bwana…’akasema akimuangalia shemeji yake na shemeji yake akatabsamu na kusema;

‘Mhh, mambo mengi, kichwa kina mambo mengi…najikuta kuchoka, hata sijijui..sijui ndio uzee, hata sijielewi…watu wengi wananiambia nimebadilika ghafla, lakini mimi najiona kawaida tu…ni kuchoka tu..’akasema.

‘Kiukweli bila kuficha umebadilika shemji yangu, nahisi una tatizo, ni bora uongee, useme kuna tatizo gani ili tuweze kukusaidia, … au mumeshaliongea ndio maana mna furaha…..’akasema nesi.

‘Sina tatizo, kama ningekuwa nalo ningelisema…usijali shemeji ….’akasema shemeji mtu.

‘Sasa jamani mimi huku kuna tatizo nilikuwa nataka kuja huko tuongea nanyi faragha, naona hata hapa hapafai kuliongelea hilo tatizo...mimi naona twendeni kule kwenye ofisi za madakitari. Kule kuna ofisi yangu huko tunaweza kuongea bila wasiwasi....’akasema akiwaangalia mmoja mmoja

‘Mhh ni kuhusu nini..?’ akauliza shemeji mtu akisita

‘Nitaambiwa tu tukifika huko,. Kwanza mtoto anaendeleaje?’ akauliza nesi kuwaondoa mashaka.

‘Mtoto hajambo kabisa..kuna muda alikuwa analia lia sana,..lakini ikaja ikapotea, sasa hivi anaendelea vyema, tulitaka kuja naye, lakini baba yake akasema huku hakustahiki kuleta watoto labda awe anaumwa..’akasema

‘Ni kweli, hamna shida….kiukweli nina hamu ya kumuona mtoto….najua sasa kawazoea sana hana mashaka yoyote,..’akasema akionyesha uso wa huzuni.

‘Kwanini asituzoee na sisi ndio wazazi wake..mtoto wetu hana shaka kabisa, yaani ukimuona…keshakuwa mkubwa, hutoamini…yaani tunavyompenda, mmh, sijui nikuambie nini, mtoto yule hivi sasa hamtako yoyote zaidi ya wazazi wake…, hataki kuachana na mimi na baba yake akirudi mbio mbio kumpokea, yaani tunampenda mtoto wetu siwezi kukuelezea..’akasema dada yake, na nesi akamuangalia dada yake na alipoona chozi linataka kumtoka akageuka kuangalia nje.

Akatoa leso ya kwa haraka akajifanya ana mafua akapikicha macho na kujiweka sawa, halafu akasema

‘Mhh, nakumbuka siku moja tuliongea ukasema mtoto ana macho mazuri , kwani macho yake yapoje, unajua mimi sikuwahi kumchunguza vyema kwenye macho yake kwani yapoje….?’ akauliza


‘Wewe utamchunguzaje mtoto sio wako, sisi wenye mtoto ndio tunaweza kumchunguza, …mmh, macho yake mmh, unajua siku ile nakupigia simu nilikuwa namuangalia, macho yake ni mazuri sana, na macho kama hayo mara nyingi wanakuwa nayo wazungu..’akasema

‘Hahaha..dada naye, yaani mumempenda mtoto mpaka mnafikiri hivyo, sasa kama yanafanana na mzungu, nyie nani anafanana na mzungu,..kwani hayo macho yanafanana na macho ya nani, baba au mama..?’ akauliza nesi na dada mtu akamtupia jicho mume wake, akasema;

‘Mhh, kiukweli macho…mmh, hakuna anayefanana naye kati yetu wawili,..lakini kwa sura ,…kwa mbali anafanana na baba yake….’akasema na shemeji mtu akawa kaangalia pembeni akatikisa kichwa kaam kukubaliana na mkewe.

Wakati huo walikuwa wameshafika ofisini kwa huyo nesi, nesi akawa anafungua mlango na wakati anafungua mlango, mkuu wa hospitalia akaonekana kwa mbali akija kuelekea hapo , lakini alipoona kuna wageni akageuka kurudi.

‘Yule ndio bosi wangu,mkuu wa hii hospitali, naona alikuwa na jambo, lakini nitaonana naye baadaye..’akasema huyo nesi

‘Kama ni maswala ya kikazi endelea tu, sisi tulikuja kukuona tu,na ilimradi upo salama, sisi tunaondoka..’akasema shemeji mtu.

‘Hapana mumefunga safari kote kuja kuniona, ingieni ndani tuongee, na kama nitaona nina nafasi tutakwenda nyumbani kwangu..’akasema mdogo mtu.

‘Nyumbani kwako hatuwezi kwenda kwa leo….’akasema shemeji mtu.

‘Tatizo lako mume wangu una wivu unafikiri labda kuna mwenzako huko , hakuna yoyote zaidi yako..’akasema akimtania shemeji yake.

‘Mhh,..nitajuaje nawe hutaki kuja nyumbani, huenda yupo..na kama yupo nikimuona nitaishia jela, ndio maana naogopa kwenda huko….haya tuambie , maana ulisema kuna tatizo, …’akasema shemeji mtu.

‘Kwanza kaeni kwenye viti maana hili jambo tunatakiwa tuliongee na mnielewe, …lakini kwanza kabla hatujaliongelea hilo,..hebu niambieni furaha yenu, maana furaha ni muhimu kuliko tatizo, na tatizo hilo ni la kawaida tu…’akasema nesi

‘Aaah, wewe tuambie kwanza, umesema kuna tatizo…, kwani jambo letu ni jema tu, lakini wewe lako umesema ni tatizo, kwahiyo umeshatutia mashaka, hebu tuambie kwanza kuhusu hilo tatizo lako, …’ akasema shemeji mtu.

‘Kweli hili ninalotaka kuwaambia, ni jambo zito, na nilipanga nilisubirishe kwanza ili nipate uhakika, lakini baadaye naona mambo yanazidi kuwa magumu. Yaani hamtaamini leo hii  nilidondoka na kupoteza fahamu….hata sijui kilichonitokea, nimejikuta nipo chumba cha dakitari wananiambia nilidondoka nje….mmh, sijui….’akasema akitikisa kichwa

‘Oh, imekuwa hivyo, kwani kuna nini….usije ukawa una mimba…’akasema dada mtu akimkagua mdogo wake kwa macho…na akaona kaongea jambo ambalo huenda hakutakiwa kuliongea mbele ya mume wake, ingefaa waongee kwanza na mdogo wake ndipo kama ni lazima amuambie mume wake. Akatabasamu kuonyesha ni utani tu.

Shemji mtu akawa makini sasa, akawa anamuangalia shemeji kwa jicho la haraka haalfu akatizama pembeni, sasa naye akionyesha wasiwasi.

‘Hahaha..mimba itoke wapi…mimi dada naitunza ahadi yangu mpaka ndoa,…hilo niamini..ni-ni mambo ya kikazi tu,  na kama mlivyomuona bosi wangu, alikuwa anakuja kutaka kuongea na mimi kuhusu hilo tatizo na nisingeliweza kuongea naye kabla sijakutana na nyie..kwahiyo namshukuru mungu mumefika wakati muafaka…’akasema

‘Mhh ni kuhusu nini maana unaanza kututisha hebu ongea moja kwa moja linahusu nini hilo tatizo….?’ Wakamuuliza sasa wakiwa wote wamenuangalia nesi, ambaye ni mdogo mtu na shemeji mtu.

‘Ni kuhusu huyo  mtoto wenu…’akasema kwa suati ya chini, halafu kwa haraka  akasimama na kugeukia dirishani machozi yakaanza kumtoka.

‘Mtoto wetu ana nini….?’ Akauliza dada mtu, na shemji mtu kwa pamoja utafikiri walipanga kuuliza hivyo kwa pamoja….


NB: Mmmm jamani muda umekwisha salio linakata..

WAZO LA LEO: Ubinadamu na utu wema ni; ujirani, upendo , kuhurumiana na kuaidiana, katika kutimiza haya, ni muhimu sana kutembeleana na kujuliana hali, hii ni desturi yetu waafrika sanasana, lakini inaonyesha jinsi gani tulivyo na mashirikiano mema.  Mkitembeleana mkajuana hali, bila kujali hali za vipato, bila kujali tofauti za kiitikadi, kimila au vyovyote vile…tunajenga upendo, na amani.


 Kuna watu wao wanajiona ni tofauti na wengine, majirani zao…, hawataki kujuliana hali, na kama ni kufanya hivyo wanajaribu kuchagua wale wanaoendana na wao kihali, ..tukumbuke kuwaa sote ni wamoja, mali, ukubwa, ni vya kupita tu… sote ni watoto wa Adamu na Hawa, tukianza kujibagua, tujue tunajenga matabaka, na matabaka ni chanzo cha chuki, husuda, na uhasma,  na ikitokea siku hali ikibadilika  basi huruma itakuwa ni adimu.
Ni mimi: emu-three

No comments :